Yaliyomo - cjpc.kccb.or.ke
Transcript of Yaliyomo - cjpc.kccb.or.ke
1
YaliyomoSala ya Kumtakia Mtumishi wa Mungu Kutangazwa kuwa Mtakatifu .................. 2
Dibaji Kuunganisha, Kuponya na Kujenga Upya Taifa Letu…Zawadi ya Mungu .......... 3
Utangulizi Kwaresima katika Kanisa Katoliki .............................................................................. 5
Wiki ya Kwanza Kuhifadhi na Kutunza Mazingira ................................................................................6
Wiki ya Pili Maadili ya Familia ....................................................................................................... 10
Wiki ya Tatu Ufisadi ........................................................................................................................... 14
Wiki ya Nne Kushiriki Wote katika Masuala ya Kijamii na Kisiasa ............................................ 18
Wiki ya Tano Kuheshimu Utawala wa Sheria .................................................................................. 22
Kiambatisho Michango ya Kampeni ya Kwaresima ya 2018 ......................................................... 25
2
E Mungu, ulimpa mtumishi wako, Maurice Michael Kadinali Otunga, neema ya kuwa mchungaji wa kipekee katika utumishi wa Kanisa; ukamfanya kuwa ishara ya unyenyekevu na mapenzi kwa maskini,
wanyonge na wasiobahatika katika jamii, huku akijinyima na kujitenga na anasa za dunia hii. Twakusihi utupe nasi uwezo wa kuzingatia imani kamili katika kutekeleza matakwa yote ya utumishi wa Kikristo, huku ukizibadili kila nyakati na hali za maisha yetu kuwa nafasi za kukupenda wewe na majirani zetu kwa furaha na ukarimu, na kuutumikia ufalme wa Mungu kwa
unyenyekevu.
Tunakuomba kwa unyenyekevu umpe mtumishi wako, Kadinali Otunga, nafasi kwenye makao yako takatifu mbinguni, nafasi ambayo imeahidiwa waliokutumikia vyema duniani. Kwa maombi yake, libariki Kanisa lako, nchi yetu, familia zetu na pia watoto, na ututimizie yote tunayokuomba ... (ongeza
maombi na nia zenu).Kupitia kwa Yesu, mwokozi wetu.
Amina
Sala ya Kumtakia Mtumishi wa MunguKutangazwa kuwa Mtakatifu
3
Mafunzo ya jamii ya Kanisa ni mojawapo ya hati zinazotuelimisha kuhusu tupasavyo kuishi katika imani yetu na pamoja na wengine. Ukweli ni kwamba iwapo tunataka kuungana na kuliponya taifa, tunahitaji kuzingatia
mafunzo hayo ya jamii. Yanatufunza kuhusu utakatifu wa maisha ya mwanadamu na kwamba hadhi ya kila mtu ndiyo msingi wa nidhamu na mwelekeo thabiti wa jamii.
Mafunzo ya jamii ya Kanisa Katoliki huzingatia kanuni 10, nazo ni: Hadhi ya utu; Jamii na manufaa ya wote; Haki na wajibu; Haki ya kutenda na kuamua ya maskini na wasio salama au wanyonge; Kushiriki kwa wote na kusaidia; Hadhi ya kazi na haki za wafanya kazi; Utumishi na usimamizi wa vitu vyote vilivyoumbwa; na Umoja/mshikamano.
Ni dhahiri kwamba mafunzo ya jamii ya Kanisa yakifahamika kikamilifu na kutekelezwa ipasavyo, yanaweza kuwa msingi muafaka wa kujenga taifa thabiti, taifa ambamo hadhi ya binadamu inaheshimiwa na kuimarishwa. Tunaombwa kuleta umoja na mshikamano kwa binadamu wenzetu. Mafunzo ya umoja na mshikamano ni muhimu katika kutufahamisha kuhusu majukumu ya kijamii ya kila mtu binafsi, jamii, asasi na mataifa. Binadamu hawana budi kujifunza kuishi na wengine na hawafai kumtenga yeyote.
Tunahitaji kuimarisha maadili yetu ya kitamaduni na kuwafundisha watoto wetu thamani ya tamaduni zetu. Ina maana kwamba Waafrika tusipokomboa utamaduni wetu, tutaendelea kugawanywa.
Mojawapo ya matarajio ya Katiba ya Kenya (2010) ni kuleta umoja wa kitaifa katika jamii ya watu wenye asili mbali mbali za kikabila. Yasikitisha kukuta kwamba ukabila umeendelea kutumiwa kama chombo cha kuwatenganisha watu binafsi, jamii na kuchochea fujo. Kabila la mtu limekuwa kigezo cha kufikia rasilmali za umma na pia mahusiano na majirani na raia wengine.
Mwaka huu tumeazimia kujadili mambo yanayoathiri mshikamano miongoni mwetu. Kwa kuangazia masuala hayo, huenda tukafanikiwa kuleta uponyaji, umoja na kulijenga upya taifa letu.
Mnamo wiki ya kwanza, tutaangazia suala muhimu la Uhifadhi na Utunzaji wa Mazingira. Kanisa linaamini kwamba sote hatuna budi kulinda na kuhifadhi mazingira. Siku hizi, watu wengine wanaugua maradhi yanayotokana na mitindo ya maisha ya kisasa, na hasa vyakula tunavyotumia na jinsi tunavyoyatendea mazingira. Matokeo yake yamekuwa ni watu wengi kutumia pesa nyingi kugharamia matibabu, huku boma nyingi zikiachwa maskini na uchumi wa familia nyingi kuathiriwa. Kuhusu utunzaji
Kuunganisha, Kuponya na Kujenga Upya Taifa Letu … Zawadi ya Mungu
Dibaji
4
wa makao yetu sote, Baba Mtakatifu Fransisko anatukumbusha kwamba “tunapaswa kuutunza ulimwenguu huu ambao ni makao yetu sisi binadamu pamoja na viumbe wengine wote. Mazingira sio kitu kilicho mbali nasi: sisi tu sehemu muhimu ya dunia hii. Ndiposa tunapaswa kuitunza dunia kwa manufaa ya kila mwanadamu na kwa vizazi vijavyo.’’
Maadili ya Familia ndiyo mada ya wiki ya pili. Familia nyingi zimeumia kutokana na kuenea kwa maadili ya kigeni ambayo yamesababisha kuvunjika kwa familia nyingi. Tukiwa Wakristo, hatuna budi kukomboa maadili ya familia zetu iwapo tunanuia kujenga jamii yetu kwa misingi ifaayo.
Ufisadi utajadiliwa katika wiki ya tatu. Ufisadi ni utumiaji mbaya wa mamlaka kwa manufaa ya binafsi. Ufisadi ni tisho kwa ustawi endelevu wa kiuchumi, maadili na haki. Ni ovu linaloyumbisha jamii na kuhatarisha utawala wa sheria. Huchelewesha utekelezaji wa miradi muhimu kama ujenzi wa barabara na nyumba. Ufisadi umeathiri nyanja zote za maisha ya jamii, uchumi na siasa bila kujali sheria zilizopo ambazo zikitekelezwa kikamilifu, zitapunguza ovu hilo.
Kushiriki Wote katika Masuala ya Jamii na Siasa ndiyo mada yetu ya wiki ya nne. Changamoto ambazo taifa linakabili ni pamoja na migawanyiko ambayo imechochewa na ushindani mkali wa kisiasa kati ya miungano ya vyama vya kisiasa na wanasiasa binafsi. Migawanyiko hiyo inaongezwa nguvu na tofauti zilizopo kati ya matajiri na maskini kwa sababu ya kuendelea kuongezeka kwa gharama ya maisha, ukosefu wa nafasi za kazi miongoni mwa vijana na mengineyo. Hatufai kukubali kumtenga yeyote katika jamii. Kufanya hivyo ni dhuluma isiyo na msingi iliyo kinyume na wito wa Kikristo na moyo wa Katiba ya Kenya.
Tangu Kenya ijinyakulie uhuru, kuvunja sheria bila kujali kuadhibiwa ni ovu ambalo limeendelea kuathiri nchi. Tunaangazia suala la Kuheshimu Utawala wa Sheria katika wiki ya tano. Lengo la kuweka sheria ni kuhakikisha tunaishi kwa amani na upatanifu ili kupunguza mizozo kwenye jamii, tukizingatia sheria kikamilifu. Wakristo hawana budi kutii sheria, isipokuwa tu zilizo kinyume na amri za Mungu. Hatuwezi kuwa na umoja na mshikamano ikiwa baadhi ya watu wataruhusiwa kuvunja sheria makusudi wakijua hawataadhibiwa.
Huku tukilenga kuangazia suala la umoja na uponyaji, tufanye hivyo kwa moyo wa Kwaresima. Kwaresima ni msimu wa kuomba, kufunga na kutoa zaka. Masuala yatakayojadiliwa katika msimu huo yatapata mizizi miongoni mwetu tukisali kwa dhati na kufunga. Tuipatie nchi yetu nafasi nyingine ya kunawiri mnamo siku zijazo kwa kutoa nafasi kwa roho wa msamaha na upatanisho kuota mizizi katika nyoyo zetu.Nawatakieni nyote msimu wa Kwaresima uliojazwa Roho wa Mungu na wenye mafao.
____________________________________Mhashamu Askofu John Oballa Owaa wa Jimbo la Ngong’Mwenyekiti, Tume ya Kikatoliki ya Haki na Amani
5
Kwaresima katika Kanisa Katoliki
Kwaresima ni kipindi cha siku 40 cha kufunga na kujinyima, kusali na kutubu kabla ya Pasaka. Kulingana na utamaduni wa Kikristo, msimu huu katika mwaka wa kiliturjia huanza Jumatano ya Majivu na kumalizika Jumapili ya Matawi. Ni adhimisho la kila mwaka ambalo
huwatayarisha waumini — kupitia sala, toba, kutoa zaka na kujinyima — kwa matukio yanayohusiana na mateso ya Yesu msalabani, na maadhimisho ya ufufuko wake. Wakatukumeni hubatizwa Jumapili ya Pasaka.
Kwa nini siku 40?
Nambari 40 ni muhimu katika maisha ya Wakristo. Musa na wana wa Israeli, kwa mfano, walitanga jangwani kwa miaka 40 wakijiandaa kwenda katika nchi waliyoahidiwa na Mungu. Musa alikaa juu ya Mlima Sinai kwa siku
40 bila kula wala kunywa alipokuwa ameenda kupokea vibao vya mkataba ambao Mungu aliwawekea Waisraeli. Nyakati za Nuhu, gharika iliendelea kwa siku 40 mchana na usiku. Eliya alikaa siku 40 mchana na usiku juu ya Mlima Horebu bila chakula. Yesu naye alienda jangwani na kufunga kula na kunywa kwa siku 40 mchana na usiku.
Asili ya Kampeni ya Kwaresima Kenya
Kuzingatia wito wa kiroho wa msimu wa Kwaresima, Kanisa Katoliki katika Kenya liliazimia kuwapasha wananchi habari kuhusu matatizo yanayokumba jamii na kushirikiana nao kutetea mabadiliko. Kupitia kwa
Kampeni ya Kwaresima, Maaskofu wa Kanisa Katoliki huwaita Wakristo wote na watu wa mapenzi mema kuungana na kukabiliana na matatizo hayo, huku wakitetea mabadiliko. Kwa kuungana na maaskofu katika utetezi huo wa mageuzi, juhudi za kila mtu binafsi pamoja na sauti ndogo ya kila mmoja ikiunganishwa na ya wengine husikika mbali, nayo matendo ya kila mmoja huongezeka yakijumuishwa na ya wengine.
Utangulizi
7
Kuhifadhi na Kutunza Mazingira
Tazama: Simulizi
Sikujua, mojawapo ya vijiji vya Kaunti ya Kwetu, kilitunukiwa milima na misitu ya kiasili. Milima ilikuwa chanzo muhimu cha mito ya maji safi na makao ya aina tofauti za ndege na wanyama. Kijiji kilibarikiwa pia kuwa na
udongo wenye rutuba uliofaa kwa kilimo na kuwapatia wanakijiji mavuno mazuri. Wanakijiji walikuwa na chakula cha kutosha.
Idadi ya wanakijiji ilizidi kuongezeka kila kukicha. Shughuli za kilimo zikawa nyingi, viwanda vingi vipya vikaanzishwa na mahitaji ya ardhi yakaongezeka. Watu wakaingia misituni na kuharibu vyanzo vya mito na makao asili ya wanyama. Miti karibu yote ilikatwa na mito ikakauka.
Hali ilizoroteshwa na viwanda ambavyo vilitupa takataka za sumu mitoni na katika maziwa, jambo lililoathiri mimea na wanyama wa majini. Mazingira yaliathirika na kusababisha kuzorota kwa mashamba yaliyoishia kutoa mavuno duni. Njaa kubwa ilikumba kijiji cha Sikujua na ikasababisha utapia mlo, magonjwa yasiyoeleweka, misimu mirefu ya ukame, mafuriko na maporomoko ya ardhi.
Jamii ilisikitishwa na kusumbuliwa na ongezeko la matatizo na majanga yaliyotokana na kuzorota kwa mazingira. Wanakijiji walikusanyika kujadili yaliyowakumba. Viongozi wa kidini na kisiasa katika kaunti, mashirika ya serikali ya masuala ya mazingira na washika dau wengine wa mambo ya uhifadhi na utunzaji wa mazingira walialikwa kutoa mashauri na kusaidia kutetea kutunza na kurejeshea mazingira hali ya awali. Waliazimia kushirikisha jamii katika upandaji wa miti, mbinu bora za kilimo ikiwa ni pamoja na utumiaji wa mbolea, upandaji wa mimea ya chakula kwa misimu, upandaji wa miti katika mashamba ya mimea ya chakula au ufugaji, na utunzaji wa maeneo ya maji. Walipendekeza pia mbinu za kusimamia ukusanyaji wa takataka na kuwasihi wenye viwanda kutumia mbinu zinazojali hali ya mazingira wanapotupa takataka. Matokeo yakawa ni jamii kufurahia mazingira safi na yaliyoimarisha afya ya wote.
Amua: Uchunguzi wa hali halisiBaba Mtakatifu Fransisko (Laudato Si, 2016) anatutaka tuchukue hatua za
dharura kulinda na kutunza makao yetu sote … kuikusanya pamoja familia yote ya wanadamu ili kutafuta maendeleo endelevu na kamili yanayofungamana na mafunzo ya jamii ya Kikatoliki. Tunadhuru uhusiano wetu na makao yetu sote kila tunapoharibu mazingira. Tunaharibu uhusiano wetu na binadamu wengine, hasa wasio salama au wanyonge, maskini na vizazi vijavyo. Tunasahau maingiliano yaliyopo kati ya dunia na ubinadamu, uhusiano unaotegemea usimamizi bora wa vitu vyote vilivyoumbwa. (No.13)
8
Hali ya makao yetu sote inatia hofu. Kubadilika kwa hali ya anga ndilo tisho kubwa zaidi ambalo ardhi yetu imewahi kushuhudia. Hali hiyo imesababishwa na wanadamu na matokeo yake yamekuwa ni kumalizwa kwa hifadhi za maji safi na kupotea kabisa kwa baadhi ya mimea na wanyama, kuongezeka kwa kiwango cha joto duniani, madhara ya kutegemea shughuli za kiuchumi zinazotoa gesi ya kaboni inayochafua dunia asili na kudhuru maisha ya wanadamu, na athari za uchimbaji migodi kwa jamii na mazingira. Mazingira yetu yanatishiwa pakubwa na shughuli mbali mbali zinazoendeshwa na wanadamu, kuongezeka kwa kiwango cha joto na kubadilika kwa hali ya hewa. Mambo hayo yamefikia kiwango ambapo usalama wa wanadamu na mfumo wote wa uhusiano wa viumbe na mazingira umo hatarini. Tumeshuhudia kuharibiwa kwa misitu, mbinu mbaya za kilimo, utupaji ovyo na usimamizi mbaya wa takataka, mambo ambayo yamechangia kuharibiwa kwa mali asili kama vile hewa, maji na udongo; kuharibiwa kwa mifumo ifaayo kwa maisha ya viumbe na mazingira, makao ya viumbe, kumalizwa kwa wanyama wa pori na uchafuzi. Tumeshuhudia misimu mirefu ya ukame, mafuriko na hali za hewa zisizotabirika. Majira hayo yanaweza kuhusishwa na maamuzi yasiyofaa ya uhusiano wa viumbe na mazingira, kawi, mali asili, upanuzi wa miji, muundo msingi, uzalishaji, utumiaji na jinsi tunavyoshughulikia takataka.
Baba Mtakatifu Fransisko anatualika kuzingatia ‘Injili ya Maumbile’ inayoiangalia dunia kulingana na jinsi Mungu alinuia iwe alipoiumba. Anatuonya kuhusu mifumo ya ulaji, utumiaji ovyo na inayolenga tu faida ya uchumi kandamizi, na isiyojali hali ya mazingira na maisha ya binadamu. Anatushauri tupunguze kasi na kuiangazia hali halisi iliyopo kwa njia tofauti. Tunahimizwa kushikamana kama familia moja ya binadamu iliyo na jukumu la pamoja kwa wengine na vyote vilivyoumbwa. Pana haja ya hatua za pamoja katika ngazi ya kimataifa, na mikataba ya kimataifa na sheria kuhusiana na mabadiliko ya hali ya hewa, viumbe na bahari. Tuchukua hatua na kubadilisha jinsi tunavyoishi na kutumia tulivyo navyo. Wamwaminio na wasiomwani Mungu, familia na jamii, wanahimizwa kuchukua hatua zitakazoleta manufaa, hata kama ni kwa kiwango kidogo.
Profesa Wangari Maathai (2004) alitukumbusha kwamba: “Kulinda na kutunza mazingira huchangia katika kuleta amani; ni kazi ya kuleta amani … nilivyoona mimi, kazi yetu haikuwa tu ni kupanda miti. Ilikuwa ni kuwatia watu moyo wa kuyatunza mazingira yao ipasavyo, mifumo yao ya uongozi, maisha yao na hali yao ya baadaye.”
Baba Mtakatifu Fransisko anasisitiza kwamba udhalimu si jambo lisiloonekana (Laudato Si no.74) na anatatutaka kutafuta kuishi kama alivyokusudia Mungu kwa kuanzisha upya uhusiano kati yetu naye, sisi wenyewe, kila mmoja na mwingine na vyote vilivyoumbwa.
9
MasomoKumbukumbu la Sheria 26:1-11Waroma 10:8-13Luka 4:1-13
Tafakari ya kirohoMaudhui ya Jumapili hii ni alivyojaribiwa Yesu na ibilisi. Mungu alitupatia
mamlaka ya kusimamia vyote alivyoviumba. Matarajio yake ni kwamba tutakuwa wasimamizi wema wa alivyoviumba. Lakini mara kwa mara, huwa tunajaribiwa kuharibu uumbaji wa Mungu kwa sababu ya ubinafsi na ulafi. Tunakabiliwa na changamoto sawa na Yesu alipokuwa jangwani akijaribiwa na ibilisi lakini akabaki kuwa mwaminifu kwa Baba. Mungu anatutaka tukiri kwamba madaraka yote ni yake na hatufai kamwe kuwa na shaka na anavyotupenda. Somo la pili linatukumbusha kwamba lazima tuikiri maishani mwetu na kuihubiri imani yetu kwa Mungu.
Tenda: Maswali ya kuwazia1. Ni matatizo gani ya kimazingira tunayokumbana nayo tukiwa jamii?2. Yataje baadhi ya madhara yanayosababishwa na kubadilika kwa hali ya
hewa. Wewe, mimi au jumuia tunaweza kuchukua hatua gani kukabiliana na madhara hayo?
3. Ni mambo gani niwezayo kutekeleza mimi, wewe au jumuia kushughulikia yanayotuhangaisha?
4. Je, mimi nawe tukiwa wanajumuia, tunawezaje kutunza maeneo yetu?
KujichunguzaJe, nimewahi kutupa ovyo takataka? Nimechafua mazingira?
Mpango wa vitendo1. Kupanda miti, kuzoa takataka na kusafisha makao. 2. Utumiaji ufaao wa maji na karatasi, hasa katika maeneo ya kazi.3. Kushirikisha wataalamu wa masuala ya mazingira katika kutoa ushauri
kuhusu uhifadhi na utunzaji wa mazingira.
11
Maadili ya Familia
Tazama: Simulizi
Kijiji cha Bora Sisi kilikuwa maarufu kwa kulinda na kutunza maadili ya familia na uadilifu maishani. Umoja wa wanakijiji ulikuwa nguzo muhimu, jambo lililowawezesha kujiendeleza na kuwa na mifumo thabiti
iliyoheshimika ya uongozi, ndoa na familia. Kufanikisha yote hayo, kila mmoja alikuwa na jukumu la kutekeleza. Akina mama waliwashughulikia wasichana nao wanaume wakawashauri wavulana kuhusu maadili na kutenda haki kwa wote.
Siku zilivyozidi kupita, ndivyo mambo yaliendelea kubadilika kijijini. Maisha ya kidunia yasiyojali dini yakamea mizizi na kijiji kikaathiriwa na mila za kigeni, kikawa tofauti na watu wakaanza kuishi kiholela na bila kuwajali wengine. Heshima kwa wazee na kati ya wanaume na wanawake ikapotea. Utakatifu wa ndoa haukuwa na maana tena na hakuna aliyejali maadili ya familia. Matokeo yakawa ni kuvunjika na kuvurugika kwa ndoa na mifumo mingine muhimu ya jamii.
Mfumo wa kutoijali dini uliandamana na maendeleo ya kiteknolojia. Malezi hafifu ya wazazi na kuvunjika kwa mshikamano wa wanakijiji ziliwaelekeza vijana kwa mitandao ya kijamii isiyokaguliwa wakitafuta kitulizo, uongozi na ushauri. Matokeo yake yakawa ni ongezeko la maovu katika jamii kama vile uhalifu, ukahaba, utumiaji mbaya wa dawa za kulevya na itikadi kali.
Makanisa ambayo yalifunza kuhusu umuhimu wa uadilifu maishani na kujaa wafuasi, yakaanza kuonekana kuwa maeneo yaliyopitwa na nyakati. Watu wakajiunga na makundi yaliyowaahidi mambo mazuri kuliko maadili. Pole pole, uabudu wa mitindo ya kisasa na miungu, pamoja na tamaa ya vitu na anasa zikamea mizizi. Viwango vya umaskini vikaongezeka na vijana waliokosa nafasi za kazi wakageukia kamari wakitumaini kutajirika haraka. Hadhi na bidii ya kazi zikapoteza maana. Uhalifu ukaongezeka kwani wengi walitumia pesa zao kucheza kamari na ikawa ni lazima watafute njia za kugharamia uraibu huo. Vijana wangefanya lolote lile wapate senti za kucheza kamari.
Baadhi ya wanakijiji hawakufurahishwa na jinsi mambo yalibadilika na wakaamua kurejeshea kijiji maisha ya uadilifu yaliyosahaulika. Walikusanyika kutafuta jinsi ya kukabili maovu yaliyokumba jamii, kuikarabati na kuirejeshea sifa ya zamani. Waliapa kufanya juhudi za kurejesha maisha ya uadilifu na kuhakikisha yanazingatiwa na wote, kufufua utukufu wa ndoa na jukumu la familia kulea watoto wenye nidhamu. Jamii ilijikomboa, ikarejesha maisha ya uadilifu na maadili ya familia. Kanuni na taratibu za jamii zilirejeshwa na kila mmoja alitekeleza jukumu lake.
12
Amua: Uchunguzi wa hali halisiFamilia ndiyo msingi wa jamii. Ufanisi wa jamii yoyote hutegemea familia. Siku
hizi, familia inakabiliwa na changamoto nyingi, ikiwa ni pamoja na utumiaji mbaya wa dawa za kulevya, uhalifu, magenge ya wahuni miongoni mwa vijana, wanaume kuvutiwa kimapenzi na wanaume na mahusiano ya kimapenzi ya wanawake kwa wanawake, kudhulumu watoto, athari za vyombo vya habari na mitandao ya mawasiliano, utovu wa nidhamu, kupuuzwa kwa familia kwa sababu ya shughuli za kutafuta riziki, tamaa ya mali na anasa, umaskini, talaka na mengineyo. Zote hizo ni ishara za kuzorota kwa imani na maadili katika familia na jamii. Watu hawajali tena kukiri na kutangaza imani kwa Mungu. Uadilifu maishani si muhimu tena. Tamaduni zisizojali kamwe maadili zimeibuka. Mambo yanayothaminiwa na familia kama vile busara, upendo, kuwajali wengine, kutojivuna, nidhamu, uaminifu, uwajibikaji, heshima, haki na usahihi yamesahaulika katika jamii.
Baadhi ya maovu tunayoshuhudia leo kama vile ufisadi, kutoaminika, utovu wa nidhamu, migomo shuleni na wazazi wasiowajibika yanatokana na ukosefu wa maadili ya familia. Wazazi waliopewa jukumu la kulea watoto wamepuuza wajibu wao. Picha na habari nyingi za vijana wakijihusisha na uasherati na maovu mengine mijini zimekuwa zikisambazwa kwa mitandao ya jamii, hasa #Ifikie wazazi. Maovu yote hayo yanatokana na ukosefu wa malezi yenye msingi wa maadili katika familia. Isitoshe, maadili ya familia huathiriwa pia na sera za kijamii na kiuchumi
Kanisa, nguzo muhimu katika malezi, linatuhimiza kutafakari jinsi familia inahusika katika mpango wa Mungu wa wokovu. Kauli hii inatokana na ufahamu kuwa familia ndiyo msingi wa jamii ya wanadamu. Kanisa linakariri wito huu katika katekisimu inayotuhimiza kuthamini uadilifu maishani, nguzo yake kuu. Mafunzo ya Yesu kuhusu amri mbili kuu za upendo — kumpenda Mungu kuliko mengine yote na kumpenda jirani yako ujipendavyo — ni muhtasari wa Amri 10; amri tatu za kwanza zinahusu kumpenda Mungu na nyingine saba zinahusu kumpenda jirani.
Kanisa linatufundisha pia kwamba watu wana haki na jukumu la kushirika katika masuala ya jamii, kushirikiana kwa manufaa na hali njema ya wote, hasa maskini na wanyonge. Hata hivyo, yote hayo yanapaswa kutilia maanani ndoa na familia, asasi muhimu za jamii zinazopaswa kuungwa mkono na kuimarishwa, wala si kudunishwa.
Ndiposa uwajibikaji ni muhimu mtu akikubali jukumu la kuwa baba au mama. Anayejitwika mzigo huo wa ubaba au umama anafaa kutilia maanani mpangilio ufaao wa maadili katika jamii. Hiyo ina maana kuwa wanandoa lazima wawe tayari kukabiliana na changamato za maisha. Kila wanapochukua uamuzi wowote, wanandoa wana haki ya kutilia maanani hali zao za kimwili, kiuchumi, kimawazo na kijamii, mambo yanayobaini kiwango cha uwajibikaji cha wazazi.
13
Baba Mtakatifu anamhimiza kila mmoja wetu kukabili maisha ya baadaye kwa matumaini. Anapendekeza maneno yanayotunza na kuendeleza upendo katika familia, nayo ni ‘Naomba, Tafadhali, Ahsante, Samahani’. Kadhalika, anashauri kwamba pasiwe na yeyote atakayekubali jua litue kabla ugomvi au sintofahamu hazijatatuliwa. Tunapokosa, tuwe wanyenyekevu na kuomba msamaha.
MasomoMwanzo 15:5-12.17-18Wafilipi 3:17-4:1Luka 9:28-36
Tafakari ya kirohoFamilia yoyote hufanikiwa ikitembea na Mungu. Abrahamu alitembea na Mungu.
Ukiwa na Mungu, hakuna lolote liwezalo kuharibika. Tunaombwa kuachana na maisha ya anasa za dunia na kumfuata Mungu. Familia zinazomwamini Mungu hufanikiwa, hata kama zitakumbana na pingamizi maishani. Mungu huangaza njia za wafuasi wake.
Tenda: Maswali ya kuwazia1. Kanisa lina jukumu gani katika kudumisha maadili ya familia?2. Yataje maadili muhimu ya familia unayoyafahamu.3. Tukiwa jumuia, mchango wetu ni gani katika kujenga maadili ya familia? 4. Tukiwa jumuia, tunasisitizaje utumiaji ufaao wa teknolojia za kisasa za
habari na mawasiliano kwenye familia?
Kujichunguza1. Ninahusikaje katika kuimarisha maadili ya familia?2. Ninahusikaje katika utumiaji ufaao wa teknolojia za kisasa za habari na
mawasiliano?3. Nimetunza haki za wazee na wanyonge katika jamii?4. Ninawezaje kutunza na kuimarisha haki hizo?
15
UfisadiTazama: Simulizi
Wakazi wa Logando waliishi kwa upatanifu na amani kwa miaka mingi. Walifanya bidii katika kila juhudi ili kujikimu na kulipa kodi kwa uongozi wao. Walikuwa na miradi muafaka na ya manufaa kwa jamii
kama vile uzoaji wa takataka, usafishaji wa soko na upandaji wa miti. Viongozi wote walitambua majukumu yao kwa jamii na pia kuwafunza vijana maadili kama vile kuwaheshimu wengine, uaminifu, kutegemewa, utiifu, uadilifu, unyoofu, haki, na la muhimu zaidi, kumcha Mungu. Maadili hayo yaliisaidia jamii ya Logando kustawi.
Jamii ya Logando ilidhamini kilimo. Wakazi wote walishirikiana kuhakikisha wanapata chakula cha kutosha kwa kila familia na cha ziada kikauziwa majirani wao wa eneo la Macho Magumu ambao hawakujali na daima hawakujitosheleza kwa chakula. Afya ya jamii yote iliimarika. Walianzisha pia miradi ya kuweka akiba ya pesa kwa makundi tofauti ya vijana, wanawake na wanaume. Walibeba kwa pamoja majukumu kama vile kulipa karo kwa watoto wao. Kadhalika, walitoa michango ya juu makanisani na kushiriki katika kuamua kuhusu miradi yote ya kanisa.
Jamii ya Logando ilistawi na kupatia eneo lao utajiri kutokana na bidii ya kazi, uadilifu na utiifu. Wakazi walikuwa na ari ya kuzidi kuimarisha maisha yao na kuinua maendeleo ya kijiji. Walimteua mzee mmoja wa kijiji kusimamia miradi. Mipango mingi ya maendeleo ilianzishwa na kumalizika kwa muda na kiwango kilichowekwa. Viongozi walidumisha uaminifu, uwazi na uwajibikaji.
Mambo yalianza kubadilika na mzee aliyeteuliwa na jamii akaanza kushirikiana na wakazi aliokubaliana kimawazo pekee. Akachagua miradi ya kutekelezwa badala ya kuwapatia wakazi nafasi ya kujiamulia wenyewe. Matokeo yakawa miradi yenye dosari nyingi na usimamizi mbaya wa rasilmali. Jamii ikaanza kulalamika na ikawasilisha mateta yao kwa wazee. Ajabu ni kwamba ujumbe uliwageuka na kuungana na waliokuwa wakitekeleza miradi kiholela. Jamii ikageukia viongozi wa kidini lakini baadhi yao wakawanyamazia na karibu watu wote wa Logando wakazidi kuteseka. Baadhi ya wakazi wakasusia kulipa kodi na kuanza kutoa hongo kila walipohitaji huduma muhimu za jamii. Upendeleo ukaathiri utekelezaji ya miradi ya jamii kama vile shule, barabara na masoko. Vibaraka wa watawala ndio walifaidika zaidi. Taratibu za kukusanya kodi zilibadilika. Wakazi wakawa na hiari ya kulipa kodi iliyofaa kwa uongozi wao ama kuhonga viongozi kwa kiasi kidogo cha pesa. Ubinafsi na ulafi zikasababisha kuporomoka kwa taasisi mbali mbali na pia taratibu.
16
Amua: Uchunguzi wa hali halisiUfisadi ni utumiaji mbaya wa mamlaka kwa manufaa ya kibinafsi miongoni mwa
maafisa wa serikali na wasio wa serikali kwa kufuja mali na kuendeleza upendeleo, hasa wa ukoo. Maovu mengine ya kifisadi ni ulaji na utoaji wa hongo, upokonyaji na unyakuzi kwa kutumia nguvu, vitisho na ulaghai. Ni ovu linaloathiri afisi mbali mbali za umma na kisiasa. Ufisadi waweza kuwa wa kiwango kdogo au kikubwa, wenye utaratibu au unaofanyika kiholela. Baadhi ya mazao ya ufisadi ni ulanguzi wa dawa za kulevya, kujipatia pesa kiharamu na utoaji wa vyeti bandia vya kumiliki ardhi.
Ufisadi unatokana na kuzorota kwa maadili. Ni nduli anayeathiri sio tu ngazi zote za siasa lakini pia uchumi na jamii. Wizi wa mali za umma huwanyima maskini chakula na dawa katika dispensari za umma. Watumishi wa umma hukosa mishahara. Umesababisha pia mabadiliko ya hali ya hewa kwani tumeharibu mama yetu ardhi kusudi tujitajirishe binafsi bila kujali vizazi vijavyo.
Nchini Kenya, ufisadi unaongezeka kwa kasi isiyomakinika na hali inazidi kuzorota. Ni kama kwamba Wakenya wamekubali kuwa ufisadi ni sehemu yao ya maisha. Kiini cha ufisadi ni kutojali kuadhibiwa, hasa miongoni mwa vizito wenye mahusiano na wakuu wa vyombo vya dola na wanaamini hawawezi kuguswa. Matokeo yamekuwa ni wizi wa mali za umma na za binafsi, ovu linaloendelezwa na wenye jukumu la kuchunga mali hizo. Ufisadi umewanyima wengi haki ya uraia.
Baadhi ya wataalamu wa uchumi na bajeti wanaamini kuwa kashfa kubwa za ufisadi huanza katika ngazi ya kutayarisha bajeti katika mashirika ya umma na ya binafsi. Baadhi ya watu wana tamaa ya kutajirika haraka kwa kufanya hila za kujitengea pesa za umma wao wenyewe, mawakala, walanguzi na wafanya biashara katika bajeti. Hutenga pesa pia kwa miradi isiyo na faida kwa umma. Njama hizo hutekelezwa katika hatua za kuunda kwa utaratibu, kupanga, kutekeleza na kudhibiti.
Mara nyingi huwa tunapuuza jukumu ambalo sisi binafsi hutekeleza katika kudumisha njama na taratibu zinazotuza kutoaminika na kashfa. Ni wangapi wetu hutoa hongo ili kuajiriwa kazi iwe tumehitimu au hatujahitimu? Ni miradi mingapi ya vyuo vya elimu, afya na dini imekwama hata baada ya raia kujinyima ili kukusanya pesa za kuikamilisha? Watu wamechanga pesa mara ngapi, kisha zinatumika kwa miradi ambayo haikupangiwa? Ni wangapi tumetumia afisi zetu kuwanufaisha watu wasiostahili? Tukiwa wazazi, ni mara ngapi tumewatuza watoto wetu kwa majukumu ya kimsingi nyumbani? Baadaye maishani, tunaweza kubaini uhusiano wa ‘hongo’ hizo za familia na yanayofanyika katika shughuli za umma? Ni mara ngapi tunasikia kuhusu mikutano ya familia ya kusuluhisha kesi za unajisi nje ya mahakama na kuwaacha waathiriwa wakiteseka? Serikali za kaunti zikishindwa
17
kukusanya pesa za kutosha kugharamia ujenzi wa barabara kwa sababu hatulipi kodi, tuna haki ya kulalamikia rekodi yake ya maendeleo? Pana haja ya dharura ya kujichunguza. Ili kutambua kuwa matendo yetu ndiyo hutuumiza, hatufai kukubali maslahi ya kibinafsi kulegeza juhudi za kuumaliza kabisa ufisadi katika jamii zetu. Tunapaswa kubaki imara na kupigana na ufisadi katika ngazi zote. Kwa bahati nzuri, tumeanza kushuhudia washukiwa wakitiwa nguvuni na kushtakiwa.
MasomoKutoka 3:1-8.13-151 Wakorintho 10:1-6.10-12Luka 13:1-9
Tafakari ya kirohoKwaresima ni msimu wa kutubu. Tumeshuhudia kwamba uhalifu na ufisadi
hututenganisha na Mungu. Mungu anatuhimiza kubadili nyendo zetu na kuamua kumfuata. Musa alipoitwa na Mungu, aliacha shughuli zake na kukubali wito wa Mungu kurudi Misri kukomboa watu wake. Wewe na mimi tunahimizwa kukomboa nchi yetu, Kenya, kutokana na minyororo ya ufisadi. Safari hii ya ukombozi ni ndefu na ngumu. Kama wana wa Israeli walivyoshawishiwa mara nyingi kurejelea maisha ya zamani, nasi pia tunashawishiwa kuupiga vita ufisadi. Somo la pili linatukumbusha kwamba tukiwa Wakristo, ni lazima tukumbane na majaribu, tuteleza na kuanguka.
Tenda: Maswali ya kuwazia1. Ni aina gani za ufisadi tumekumbana nazo kazini, kwenye familia zetu,
jumuia na ngazi ya kitaifa?2. Ufisadi una madhara gani?3. Taja baadhi ya matendo ya kifisadi unayoyajua. Tunawezaje kuyazuia?4. Ninawezaje mimi, sisi na hata jumuia kuumaliza ufisadi katika jamii na
maeneo ya kazi?
Kujichunguza1. Tumewahi kuhusika na tendo lolote la kifisadi?2. Nimepigana na ufisadi katika jamii?3. Nimewahi kuathiriwa na visa vya ufisadi?
19
Kushiriki Wote katika Masuala ya Kijamii na Kisiasa
Tazama: Simulizi
Mabadiliko lilikuwa jimbo lenye watu wa makabila tofauti lililozawadiwa mila na tamaduni nyingi. Wengi wa wakazi wake walikuwa wakulima, wafugaji na wafanya biashara. Jimbo jirani la Twende halikuwa linapata
mvua za kutosha lakini lilikuwa na mali asili nyingi na utamaduni wa kuvutia. Kiuchumi, Twende ilikuwa hatua nyingi mbele ya Mabadiliko na ilikuwa na sera muafaka za ugavi wa faida kutokana na mali zake asili. Palikuwa na mgawano sawa wa mali asili miongoni mwa wakazi kulingana na mahitaji yaliyotambuliwa. Mfumo huo wa uongozi ulifanikishwa na uangalizi wa wazee wa jamii, kushirikishwa kwa wote na kushiriki kwa kila mkazi.
Baada ya muda, jamii ya Twende ilianza kufuata mila na tamaduni za kigeni na bila kutambua, wakaanza kuzingatia mifumo iliyoathiri uongozi wao na shughuli zao za kila siku. Jamii ambayo kwa vizazi ilijivunia umoja na mgawano sawa wa rasilmali, ilianza kusambaratika. Mfumo wa kugawana rasilmali hukulingana tena na mahitaji ila kutegemea ushawishi katika jamii. Hatimaye, watu wakaanza kupigania nyadhifa za uongozi kwa manufaa ya kibinafsi wala sio kwa manufaa ya jamii ya Twende. Baadhi ya makundi yakaachwa nje ya masuala na taratibu muhimu.
Ikafikia wakati ambapo wakazi wa Twende walihimiza mfumo wa uongozi ufanyiwe mabadiliko. Hamu yao kuu ilikuwa ni kupata mfumo wa demokrasia ambao ungewezesha uchaguzi kufanyika kila baada ya miaka mitatu na kuwashirikisha wote katika masuala ya kijamii na kisiasa.
Wagombeaji wengi walijitokeza kushindania nyadhifa za uongozi katika uchaguzi. Mmoja wao, Bw Tumbo, alikuwa amerejea kutoka ng’ambo. Wakazi walikuwa na matumaini makubwa sana naye kwa sababu ya mali yake, ujuzi kutoka nje na masomo ya juu. Aliwasilisha manifesto ya kuvutia na kuahidi kuinua kiwango cha maisha ya wakazi. Alishinda uchaguzi kwa kura nyingi na kwa wafuasi wake, mabadiliko hayangeepukika.
Miezi mitatu ya kwanza haikumalizika kabla tabia yake kamili kujitokeza: ujeuri, kupuuzilia mbali ushauri wa wazee, viongozi wa kidini na washika dau wengine. Aliwapa kazi za ngazi za juu marafiki zake wa kisiasa, kijamii na kibiashara. Kwa kufanya hivyo, alitupilia mbali kanuni za sheria kuhusu kuwashirikisha waliotengwa, walio wachache, usawa wa jinsia, vijana na watu wenye mahitaji maalumu. Kadhalika, hakuwashirikisha wakazi katika kuchukua maamuzi muhimu kwao. Hali ya kisiasa, kiuchumi na kijamii ya wakazi wa Twende ilizorota. Alisimamia vibaya rasilmali, akazima sauti za wakazi na kuvuruga maslahi yao.
20
Ndiposa wakazi wakagundua kwamba manifesto yake na ahadi za kampeni zilikuwa ni njama tu za kuwashawishi kumpigia kura. Wakazi wakaanza kuungana na kutetea mabadiliko na kuimarishwa kwa huduma. Kwa mara kadha, waliandamana nje ya afisi ya Bw Tumbo na kuhakikisha hakuna yeyote angeweza kuingia wala kutoka afisini. Polisi hawangevunja maandamano hayo kwani yalikuwa ya amani na yalifuata sheria. Ikawa ni lazima Bw Tumbo ashauriane na wakazi, akashughulikia masuala ya kutenga baadhi ya wakazi, usimamizi wa matumizi ya pesa za umma, kuzingatia haki kutoa tenda kwa vijana, wanawake na watu wenye mahitaji maalumu. Matunda ya juhudi za wakazi yakaanza kuonekana. Ushiriki wa wakazi katika masuala ya kijamii na kiuchumi uliimarishwa. Hatimaye, harakati za wakazi zilirejesha sifa ya zamani ya Kaunti ya Twende.
Amua: Uchunguzi wa hali halisiImethibitishwa kwamba katika nchi yoyote inayozingatia demokrasia, taratibu
thabiti na endelevu za kisiasa huhitaji mchango wa kila mmoja katika jamii, bila kujali iwapo mchango huo ni wa walio wengi ama makundi ya walio wachache. Ushiriki huo ni muhimu sio tu kwa taratibu za kisiasa lakini pia kwa umoja wa kijamii na kisiasa na hivyo basi kuwezesha kila mmoja kujitambulisha na taifa na serikali zake.
Kenya imeteseka kutokana na sera mbaya za kijamii na kisiasa zilizowatenga wengi. Wanasiasa wamenufaika kutokana na unyonge wa wengi nchini, hali ambayo imetumiwa kueneza tofauti za kikabila badala ya kujenga umoja wa taifa. Matukio ambayo yamekuwa ni kawaida wakati wa uchaguzi tangu 1992 yanabaini pana uhusiano mkubwa kati ya ubaguzi wa kijamii na visa vya fujo na pia kuzorota kwa usalama. Matukio hayo ni pamoja na misukosuko ya jamii, mizozo ya kivita na matendo ya kigaidi. Ni rahisi kwa baadhi ya makundi yasiyobahatika ambayo yana sifa zinazofanana kama vile asili ya kikabila au dini kuchukua silaha kutafuta haki na kusawazisha mambo tena. Tofauti baina ya makundi si sababu tosha ya kuzusha mzozo lakini kunyimwa haki na usawa ni sababu ya kutosha kuchochea fujo. Ndiposa dhana ya kushirikisha jamii inasaidia kukabiliana na mizozo kwani hutambulisha baadhi ya sababu za mizozo hiyo. Kwa kuchunguza ni kwa nini baadhi ya jamii zenye tofauti kubwa hukumbwa na mizozo, ni wazi sababu kubwa ni kutokuwa na usawa wa kijamii, kiuchumi na kisiasa.
Ingawa tuna Katiba, sheria na sera mbali mbali zinazolingana na nyakati, Kenya bado haijafikia kiwango cha kuridhisha katika kudumisha sheria na utengamano. Tofauti kubwa iliyopo kati ya matajiri na maskini haifai kukubalika katika jamii inayotarajia kuzingatia haki na amani.
21
Ili kutafuta suluhu ya maswala hayo na kukuza uchumi wa Kenya kwa asilimia 10 kila mwaka chini ya Ruwaza ya 2030 (Vision 2030), lazima kiwango cha usawa wa jamii kiinuke na pawe na mgawano sawa wa miradi ya maendeleo na rasilmali. Wakenya wanafaa kuzika ubinafsi na kuzingatia uzalendo. Kadhalika, pana haja ya kuwa na taratibu za kuhakikisha wote nchini wanashiriki katika shughuli za uraia na serikali. Inafaa pia kufufua taratibu za kisheria za kushirikisha raia katika maamuzi ya kuunda sera, kuandaa mikakati na hatua zote za kuhakikisha hakuna makundi ama watu binafsi wanaotengwa. Hatua hizo zitahakikisha wote wananufaika na ustawi na maendeleo, uwajibikaji wa kijamii na kuelimisha raia juu ya masuala ya umma yanayohusu uongozi, utoaji huduma na kuheshimu utawala wa sheria.
MasomoYoshua 5:9-12Zaburi 322 Wakorintho 5:17-21Luka 15:1-3, 11-32
Tafakari ya kirohoWana wa Israeli walifika nchi waliyoahidiwa si kwa bidii yao ila ni kwa uongozi
wake Mungu. Tunahitaji kupatanishwa na Mungu na wengine katika jamii. Tunapojitenga na wengine, tunavunja uhusiano wetu na Mungu. Yule mwana mpotevu alipoiacha familia yake, aliteseka sana. Kaka yake pia alitaka atengwe lakini baba yao akasisitiza kuwa wote wawili walikuwa wanawe.
Tenda: Maswali ya kuwazia1. Utaratibu wa uongozi nchini ukoje na una mapendekezo gani ya
kuuimarisha?2. Nina wajibu gani katika kuimarisha ushiriki wa wote katika masuala ya
kijamii na kisiasa?3. Tunaimarishaje kushiriki kwa wote katika masuala ya kijamii na kisiasa
tukiwa watu binafsi na katika jumuia?
Kujichunguza 1. Je, nimewahi kumwajiri mtu kwa misingi ya kikabila?2. Je, nimezingatia mtazamo wa mambo yasiyo na uasili na ya chuki katika
kuwataja wengine?3. Je, ninawabagua watu kijinsia?
23
Kuheshimu Utawala wa Sheria
Tazama: Simuluzi
Malimali, makao makuu ya Kaunti ya Mjini, ilikua haraka kwa sababu ya pesa za ugatuzi na mgao wa fedha nyingine za serikali ya kitaifa za kugharamia ustawi wa miji. Watu wengi walihama kutoka mashambani
na kwenda kutafuta kazi Malimali. Idadi ya watu katika Malimali iliongezeka kupindukia, hasa vibarua na wafanya
kazi wenye mapato ya chini. Wengi wao waliishi katika mitaa ya mabanda nje ya mji. Wengi walijigawia ardhi ya umma kiharamu, ikiwa ni pamoja na maeneo yaliyotengewa upanuzi wa barabara, na wakaliita eneo hilo Kijiji Chetu. Walijenga shule, makanisa, misikiti na hospitali kwenye maeneo yaliyotengewa miradi ya jamii. Baada ya miaka mingi kupita, pakawa na haja ya kupanua barabara kutoka Kijiji Chetu hadi Malimali kulingana na mipango ya maendeleo ya serikali ya kitaifa.
Mzee Msafi, mfanya biashara mjanja aliyefahamika kwa maisha yake ya kifahari na uhusiano mkubwa na wanasiasa katika kaunti, alikuwa na habari kuhusu upanuzi huo wa barabara. Alifanya njama na maafisa wafisadi na akapata hati za kumiliki ardhi yote ya Kijiji Chetu. Baadaye alifanya mpango kuwafukuza wakazi wa Kijiji Chetu akitarajia kulipwa fidia na serikali upanuzi wa barabara ukianza. Wakazi walipata habari kuhusu kunyakuliwa kwa ardhi yao na kuamua kumshtaki Mzee Msafi. Kesi yao ilitupwa kwani hawakuwa na hati miliki na mahakama ikathibitisha kuwa ardhi ilikuwa ya Mzee Msafi. Hawakuridhishwa na uamuzi huo wa mahakama. Walifanya maandamano na kuubomoa ua uliozungushiwa ardhi hiyo. Mzee Msafi alitumia ushawishi wake mkubwa kuhakikisha polisi wamewatimua wanakijiji, tukio lililozusha fujo na kusababisha vifo vya wanakijiji wawili na polisi mmoja.
Mkazi aliyefuzu masomo ya sheria za mashamba aliitisha mkutano wa viongozi na wazee wa kijiji kujadiliana kuhusu hatua walizofaa kuchukua. Waliwaalika maafisa wa idara husika na pia Mzee Msafi. Ikathibitishwa kwamba ardhi ambayo Mzee Msafi alidai kuwa ni mali yake ilikuwa ya jamii na sehemu nyingine ilitengwa kwa upanuzi wa barabara muda mrefu kabla wanakijiji hawajaanza kuishi humo.
Ukweli ulipobainika, wanakijiji waliazimia kuhama katika muda wa miezi sita ili kutoa nafasi ya miradi ya maendeleo, ikiwa ni pamoja na upanuzi wa barabara. Kadhalika, walikubaliana kuwa hawangedai fidia. Uongozi wa Kijiji Chetu ukapewa kibarua cha kuwachukulia hatua Mzee Msafi na washirika wake waliomwezesha kupata hati miliki za ardhi hiyo kiharamu wakinuia kuilaghai sio tu jamii lakini pia serikali ya kitaifa.Amua: Uchunguzi wa hali halisiSheria ni muhimu kwa jamii, shughuli za raia na hufanikisha utekelezaji wa mabadiliko katika jamii. Sheria hulinda haki za kimsingi na kuzuia mizozo baina ya makundi ya kijamii na jamii yote kwa jumla.
24
Katiba yetu, katika utangulizi, inatambua sheria takatifu kwa kuutambua utukufu wa Mungu Muumba wa vyote. Ndiposa sheria takatifu inatuhimiza sote kufanya yaliyo mema na adilifu kama tulivyoagizwa na Mungu ambaye ni lazima awe kiongozi wetu maishani. Ingawa Katiba inatambua utukufu wa Mungu, utawala wa sheria hauzingatiwi ipasavyo nchini. Kwa nini iwe hivyo? Mageuzi ya asasi na mipaka ya mamlaka kama ilivyokusudiwa na Katiba haijatekelezwa kikamilifu. Kenya inakumbwa na kiwango kikubwa cha uvunjaji sheria bila kujali adhabu, huku watu wengi wakikosa kuwajibikia matendo yao. Tatizo kubwa ni wanasiasa ambao hawajali kamwe uwazi, uwajibikaji wa kibinafsi na uadilifu.
Je, Kanisa linatufunza nini kuhusu utawala wa sheria? Mafunzo ya Kanisa husisitiza umuhimu wa utawala wa sheria katika kulinda thamani ifaayo ya hadhi ya mwanadamu. Lakini utawala wa sheria hautoshi kila mara kulinda hadhi ya binadamu. Sheria ni chombo cha kijamii cha kuendeleza maadili ya kimsingi katika jamii na utamaduni. Kanuni za kisheria zikihitilafiana na maadili ya kimsingi, sheria haiwezi kulinda kikamilifui hadhi ya binadamu. Ndiposa Kanisa husisitiza kuwa utawala wa sheria ni lazima ufungamane na hadhi ya binadamu. MasomoIsaiya 43:16-21Wafilipi 3:8-14Yohana 8:1-11
Tafakari ya kirohoWaraka wa Mtakatifu Paulo kwa Wafilipi unahusu sheria na wokovu. Utekelezaji maradufu wa sheria ni pigo kwa hadhi ya binadamu. Katika Injili, mwanamke aliyefumaniwa na uzinzi alibaguliwa, jambo ambalo Yesu alilikataa.
Tenda: Maswali ya kuwazia 1. Je, unaufahamu vipi utawala wa sheria?2. Je, unaifahamu vipi sheria takatifu?3. Ni madhara gani yanayotokana na kutoheshimu utawala wa sheria?4. Nikiwa mwanajumuia, nina wajibu gani katika kudumisha na kuheshimu
utawala wa sheria?
Kujichunguza 1. Je, kuna chochote nimejipatia kiharamu?2. Je, ninaamini kuzingatia kikamilifu Katiba na utawala wa sheria?3. Nina wajibu gani nikishuhudia tukio la kuvunja na kutotii utawala wa sheria?4. Nimewahi kushiriki matenda ya kifisadi? Iwapo nimehusika, ninaweza kufanya nini?5. Umeendelezaje kushiriki kwa wote kijamii na kisiasa wewe binafsi na katika
jumuia?
25
MICHANGO YA KAMPENI YA KWARESIMA YA 2018 (KSHS)Kiambatisho
JIMBO KIASI
Jimbo Kuu la Nairobi 3,228,280.00
Jimbo la Meru 3,010,521.00
Jimbo la Bungoma 2,800,000.00
Jimbo Kuu la Nyeri 2,713,955.00
Jimbo la Kakamega 2,000,000.00
Jimbo la Eldoret 1,835,391.00
Jimbo Kuu la Kisumu 1,401,040.00
Jimbo la Machakos 1,368,428.00
Jimbo la Nyahururu 1,175,063.00
Jimbo la Embu 1,105,785.00
Jimbo la Muranga 780,000.00
Jimbo la Ngong’ 606,831.00
Jimbo la Homa Bay 598,217.00
Jimbo Kuu la Mombasa 518,566.30
Jimbo la Nakuru 477,189.00
Jimbo la Kericho 463,042.00
Jimbo la Kitui 443,979.00
Jimbo la Marsabit 399,051.00
Jimbo la Kisii 350,000.00
Jimbo la Kitale 307,520.00
Jimbo la Malindi 300,000.00
Jimbo la Lodwar 223,934.00
Jimbo la Maralal 212,357.00
Jimbo la Isiolo 70,300.00
Jimbo la Garissa 63,280.00
Jumla 26,452,729.30
TAASISI KIASI
Millitary Ordinariate 975,012.00
Religious Superiors Con-ference of Kenya (RSCK)
50,000.00
Association of Sisterhood in Kenya (AOSK)
47,620.00
Administration Police Service
42,200.00
St. Thomas Aquinas Seminary
25,000.00
Franciscan Sisters -St. Joseph
17,500.00
St. Mary’s Propaedeutic Seminary
15,880.00
Kenya Wildlife Service (KWS)
13,500.00
St. Matthias Mulumba Tindinyo
13,420.00
Chuo Kikuu cha Kisii 12,500.00
Jumla 1,212,632.00
Jumla 27,665,361.30
26
JIMBO KUU LA NAIROBIParokia Kiasi
Makadara Deanery
Blessed Sacarament Buruburu 52,717.00
Holy Trinity Buruburu 31,240.00
Mary Magdalena Kariokor 71,800.00
Our Lady of Visitation Makadara 78,000.00
St. Joseph and Mary Shauri Moyo 34,300.00
St. Joseph Jericho 42,000.00
St. Mary Mukuru 40,126.00
St. Teresa’s Eastleigh 92,332.00
Sub-Total 442,515.00
Central Deanery
Consolata Shrine West Land 290,066.00
Holy Familiy Basilica 516,738.00
Holy Trinity Kileleshwa 80,000.00
Our Lady Queen of Peace, South B 208,941.00
St. Catherine of Alexandria, South C 27,165.00
St. Austin Muthangari 51,678.00
St. Catherine of Sienna, Kitusuru 100,000.00
St. Francis Xavier, Parklands 200,000.00
St. Paul’s Chapel UoN 100,000.00
St. Peter Claver’s 48,500.00
Don Bosco, Upper Hill 314,765.00
Sub-Total 1,937,853.00
Eastern Deanery
Christ The King, Embakasi 60,000.00
Divine Word, Kayole 306,098.00
Holy Family, Utawala 153,250.00
Mary Immaculate, Mihang’o 136,058.00
St. Annie and Joachim, soweto 300,575.00
St. Joseph Freinademetz, Ruai 174,500.00
st. Monica, Njiru 86,018.00
St. Peter, Ruai 60,000.00
St.Vincent, Kamulu 80,405.00
Sub-Total 1,356,904.00
Outering Deanery
Assumption of Mary, Umoja 894,979.00
Divine Mercy, Kariobangi South 39,120.00
Holy Cross, Dandora 20,000.00
Holy Innocent, Tassia 153,634.00
Holy Trinity, Kariobangi North 136,414.00
St. Jude Doonholm 281,870.00
Sub-Total 1,526,017.00
Western Deanery
Christ the King, Kibra 68,035.00
Mary Queen of Apostles, Dagoretti Mkt
56,200.00
Our Lady of Guadalupe, Adams Arcade
67,454.00
Regina Caeli, Karen 119,284.00
Sacred Heart, Dagoretti Corner 212,966.00
St. John the Evagelist, Lang’ata 50,300.00
St. Joseph the Worker, Kangemi 89,652.00
St. Michael, Otiende
Sub-Total 663,891.00
Ruaraka Deanery
Christ the King, Githurai Kimbo 75,300.00
Holy Mary Mother of God, Githurai 147,754.00
Madre Teresa, Zimmermann 42,300.00
Queens of Apostles, Ruaraka 160,000.00
Sacred Heart, BabaDogo 41,000.00
St. Benedict, Thika Road 47,000.00
St. Clare, Kasarani 70,000.00
St. Dominic, Mwiki 26,500.00
St. Joseph, Kahawa Sukari 127,500.00
St. Joseph Mukasa, Kahawa West 204,567.00
Sub-Total 941,921.00
Thika Deanery
Immaculate Conception, Kilimambogo
8,218.00
St. Benedetta, Ngoingwa 70,000.00
St. Partick’s Thika 106,944.00
St. Matia Mulumba Thika 58,000.00
St. Maria Magdalena, Munyu 18,350.00
Sub-Total 253,294.00
27
Ruiru Deanery
St. James , Juja Farm 20,000.00
St. Augustine, Juja 60,000.00
St. Christopher, Kembo 51,592.00
St. Francis of Assisi, Ruiru Town 342,208.00
St. Lucia Membley
St. Peter, Kwihota 80,000.00
St. Teresa, Kalimoni 21,550.00
Sub-Total 575,350.00
Gatundu Deanery
Archangle Gabriel, Mutomo
Christ the King Karinga 15,209.00
Ituuru 14,250.00
Mary Help of Christian Ndundu 27,150.00
Our Lady of Annunciation, Gatitu 4,500.00
St. John the Baptist, Munyu-ini 17,700.00
St. Joseph, Kiganjo 45,000.00
St. Joseph Mutunguru
Uganda Martyrs, Gatundu 13,500.00
Sub-Total 123,809.00
Githunguri Deanery
All Saints, Komothai 15,380.00
Holy Family, Githunguri 7,000.00
Holy Spirit, Miguta 11,050.00
Nativity of Our Lady, Kagwe 20,164.00
Our Lady of Assumption, Kambaa 5,000
St. John the Evagelist, Githiga 14,000.00
St. Teresa of Child Jesus, Ngenya 6,000.00
Sub-Total 73,594.00
Kiambu Deanery
All Saints, Riara 80,000.00
Holy Rosary, Ikinu 25,248.00
Our Lady of Holy Rosary, Tinga’ng’a 42,000.00
Our Lady of Victories, Lioki 39,000.00
St. Joseph Gathanga 17,400.00
St. Martin De Porres, Karuri 80,000.00
St. Peter and Paul Kiambu Town 74,008.00
St. Stephen, Gachie 29,000.00
Sub-Total 386,656.00
Kikuyu Deanery
Holy Cross, Thigio 25,000.00
Holy Eucharist, Kinge’ero 27,890.00
Immacualate Conception, Gicharani 17,000.00
Our Lady of Holy Rosary, Ruku 15,279.00
St. Peter the Apostole, Kikuyu 37,995.00
St. Charles Lwanga, Waithaka 22,500.00
St. John the Baptist, Riruta 30,000.00
St. Joseph, Kerwa 34,200.00
St. Joseph, Muguga 6,600.00
St. Peter the Rock, Kinoo 12,290.00
Sub-Total 228,754.00
Limuru Deanery
Kamirithu 11,104.00
Our Lady of Mt. Carmel, Ngarariga 20,500.00
St. Joseph, Limuru 25,400.00
St. Andrew, Rironi 0.00
St. Charles Lwanga, Githirioni 12,100.00
St. Francis, Limuru Town 40,000.00
St. Joseph, Kereita 24,000.00
Sub-Total 133,104.00
Mang’u Deanery
Our Lady of Fatima, Kiriko 20,000.00
Our Lady of Holy Rosary, Kamwangi 8,000.00
St. Annie Mataara 12,000.00
St. John the Baptist, Mang’u 20,000.00
St. Peter, Nyamangara 15,000.00
St. Peter Kairi 29,845.00
St. Teresa Kiangunu 15,650.00
St. Teresa of Avila Gachege 7,000.00
Sub-Total 127,495.00
Chaplaincies
CIC Msongari 0.00
Kamiti Prison 4,000.00
Kenyatta National Hospital 20,020.00
Kenyatta University 52,394.00
National Youth Service 4,740.00
St. Raphael Kabete 0.00
Sub-Total 81,154.00
28
Institutions
Franciscian Sisters of St. Anna 6,000.00
Resurrection Garden 0.00
SMI- St. Teresa of Avila Region 30,000.00
Mary Hill Girls High School 19,000.00
Sub-Total 55,000.00
Jumla 8,934,029.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
3,228,280.00
JIMBO KUU LA KISUMUTAASISI PAROKIA FUNGU LILILOPEWA AFISI YA KITAIFA YA CJPC
Uzima University College St Paul’s Parish 67,500.00
St Mary’s Lwak Girls High Lwak Parish 30,000.00
St Francis Rangala Girl’s Secondary Rangala Parish 26,000.00
Holy Trinity Rangala Boys High Rangala Parish 12,030.00
KUAP-PandPieri Staffs Milimani Parish 12,000.00
St Barnabas Girls Secondary Barkorwa Parish 10,250.00
Koru Holy Family Mission Hospital Koru Parish 9,516.50
St Thereza’s Girls Secondary Kibuye Parish 7,652.50
St Anne’s Ahero Primary Ahero Parish 7,600.00
Nyabondo Boys High School Nyabondo Parish 6,000.00
St Augustine Kandege Secondary School
Koru Parish 5,067.50
St Mary’s School Yala Yala Parish 5,000.00
St Joseph Milimani Priest’s House Milimani Parish 5,000.00
Koru Girl’s High School Koru Parish 5,000.00
St Vincent Raliew Secondary School Raliew Parish 5,000.00
Ukweli Pstoral and Development centre
St Paul’s Parish 5,000.00
Xaverian Secondary School Milimani Parish 5,000.00
Ragumo Primary School Nyamasaria Parish 4,285.00
St Aloys Ojola Primary chool Ojola Parish 3,785.00
Archbishop Okoth Ojola Girls Secondary school
Ojola Parish 3,550.00
TAASISI PAROKIA FUNGU LILILOPEWA AFISI YA KITAIFA YA CJPC
St Gabriel’s Minor Seminary Ojola Parish 3,500.00
Dominicans Frairs Community OP -Kisumu
St Paul’s parish 3,250.00
St Steven’s Aluor Mixed Secondary School
Nyamonye Parish 3,000.00
St Paul’s Mwei High School Uradi Parish 2,640.00
St Ignatious of Loyola Secondary Magadi Parish 2,500.00
Awasi Dispensary Awsasi Parish 2,500.00
29
School Sisters of Notre Dame St Paul’s Parish 2,500.00
JOOST -St John Henry Newman-Bondo Chaplaincy
Bondo Parish 2,300.00
Franciscan Sisters of St Joseph-Kibuye Convent
Kibuye Parish 2,150.00
Kogola Father’s House Kogola Parish 2,000.00
Dala Boarding Primqary School Uradi Parish 2,000.00
St Mary Magdalene Oasis of Peace Children Home
Chiga Parish 2,000.00
Fr Gulik Girl’s Uradi School Uradi Parish 1,982.50
St Patrick’s Secondar School-Oduwo Muhoroni Parish 1,590.00
Aluor Girls Primary School Aluor Parish 1,500.00
Brothers of our Lady of Perpetual Help-Milimani
Milimani Parish 1,500.00
Ukwala Priest’s House Ukwala Parish 1,500.00
St Aloyce Secondry School Katito Parish 1,500.00
Father’s House Bolo Parish Bolo Parish 1,500.00
Usenge High School Nyamonye Parish 1,310.00
TAASISI PAROKIA FUNGU LILILOPEWA AFISI YA KITAIFA YA CJPC
St Augustine Nyamonye Girls Secondary School
Nyamonye Parish 1,260.00
Dr Robert Ouko Primary School Ojola Parish 1,255.00
St Sylveter’s Girls Secondary School Madiany Parish 1,250.00
St Agnes’s Primary School Muhoroni Parish 1,250.00
Aluor Convent-FSSA Aluor Parish 1,000.00
Mill Hill Sisters-FMSJ Milimani Parish 1,000.00
Our Lady of Grace Primary School-Dominicans Frairs
St Paul’s Parish 1,000.00
Joakim Owang Secondary School Nyamonye Parish 1,000.00
Padre Pio Masogo Girl’s Secondary Masogo Parish 1,000.00
Our Lady Queen of Peace Mix Secondary School
Muhoroni Parish 1,000.00
Sisters of Mary-Ojola Covent Ojola Parish 1,000.00
Kanyateng Primary School Katito Parish 715.00
Lisana Primary School Katito Parish 625.00
Lisana Secondary School Katito Parish 600.00
T.T.T -Barkanyango Bondo Parish 600.00
St Aloyce Primary School Katito Parish 500.00
Nyawara Primary School Ojola Parish 500.00
Wenwa Primary School Katito Parish 325.00
St John Mixed Koru Primary School Koru Parish 250.00
30
St Elizabeth Grail School Ojola Parish 150.00
Ngomo Primary School Katito Parish 25.00
Disi Primary School- Ahero 500.00
294,764.00
PAROKIA FUNGU LA PAROKIA FUNGU LILILOPEWA AFISI YA KITAIFA YA CJPC
St Thereza’s Kibuye 66,666.67 100,000.00
St Joseph’s Milimani 58,606.67 87,910.00
St Paul’s 53,886.67 80,830.00
Magadi 37,666.67 56,500.00
Nyamasaria 26,666.67 40,000.00
Holy Cross 26,666.67 40,000.00
Barkorwa 26,666.67 40,000.00
Riwo 25,000.00 37,500.00
Nyabondo 22,000.00 33,000.00
Bolo 20,416.67 30,625.00
Ahero 20,166.67 30,250.00
Ukwala 20,000.00 30,000.00
Nanga 17,776.67 26,665.00
St John XXIII-Rabuor 16,666.67 25,000.00
Ojola 15,700.00 23,550.00
Raliew 15,000.00 22,500.00
PAROKIA FUNGU LA PAROKIA FUNGU LILILOPEWA AFISI YA KITAIFA YA CJPC
Tamu 14,283.33 21,425.00
Madiany 13,500.00 20,250.00
St Pantaleon 13,465.00 20,197.50
Muhoroni 13,366.67 20,050.00
Uradi 12,500.00 18,750.00
Reru 12,000.00 18,000.00
Bondo 11,000.00 16,500.00
Katito 10,783.33 16,175.00
Withur 10,733.33 16,100.00
Nyangoma 10,666.67 16,000.00
Yala 10,000.00 15,000.00
Sigomere 10,000.00 15,000.00
Rangala 10,000.00 15,000.00
Ugunja 9,333.33 14,000.00
Nyagondo 9,333.33 14,000.00
Nyamonye 8,666.67 13,000.00
31
Kogola 8,666.67 13,000.00
Sega 8,333.33 12,500.00
Uwai 8,333.33 12,500.00
Kajimbo 7,666.67 11,800.00
Obambo 7,816.67 11,725.00
Yogo 6,666.67 10,000.00
Awasi 6,666.67 10,000.00
Kianja 6,540.00 9,810.00
Mutumbu 6,058.67 9,088.00
Nduru 4,500.00 6,750.00
Aluor 3,700.00 5,550.00
Koru 3,500.00 5,250.00
Masogo 3,350.00 5,025.00
Chiga 3,333.33 5,000.00
Mbaga 3,333.33 5,000.00
Jumla 737,650.33 1,106,775.50
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
1,401,040.00
JIMBO LA LODWAR Parokia/Taasisi Kiasi
St. Augustine Cathedral Parish 150,726
Holy Family Kanamkemer Parish 65,000
Risen Christ Nakwamekwi 20,600
St. Dominic Kerio 10,000
St. Gabriel Kangatosa 3,000
St. Kizito Turkwel 5,050
St. Peter Lorugum 34,000
All Saints Kainuk 30,027
Immaculate Conception Katilu 9,150
St. Daniel Comboni, Lokori 20,225
St. Lawrence Nakwamoru 6,800
St. John Lokichogio 18,000
St. Benedict Kalobeyei 10,020
Good Shephered Kakuma 40,000
Holy-Cross Kakuma Refugee Camp 30,000
St.Mark Lokitaung 18,025
10,000
St. Titus & Timothy Kaeris 8,950
St. James Kaikor 7,000
St. Dennis Kataboi 4,000
Mary Mother of God Kalokol 20,000
St. Stephen Losajait 7,310
Christ the King Lokichar 42,000
Our Lady Queen of Peace Todonyang 10,000
Nariokotomoe Mission 12,000
St. Michael Napetet 30,000
Our Lady of Sorrows Oropoi 4,800
St. Joachim & Anne Kibish 12,000
Sub Total 638,683
Taasisi
St. James Minor Seminary 10,600
Lodwar High School 3,000
St. Kevin Secondary School 1,350
32
St. Daniel Comboni Girls’ High School 12,100
Our Ladies of Mercy Secondary school 10,000
Lodwar Girls Secondary School 2,000
P.A.G. Secondary School 1,000
Salvation Army Secondary School 900
Kakuma Girls Primary School 1,500
Vicky Wendy Wairimu’s family 1,000
St. Monica Girls Primary School 7,200
Lodwar Vocational Training Centre 2,000
Sisters of Mary of Kakamega, Lodwar 4,000
Sisters of Mary of Kakamega, Lorugum
3,000
Sisters of Mary of Kakamega, Kalobeyei
1,000
Lodwar Prison 2,150
Sub Total 62,800
Our Lady Queen of Peace Todonyang Intergrated
3,170
Centre
Kainuk Mixed Secondary School
4,540
Kaeris Girls High School 7,100
St. Marys Primary School 5,000
Bishop Mahon Primary 2,000
St.Augustine Boys Primary School 15,000
Kerio Boys High School 1,000
St. Michael Kawalase Primary School 1,000
Alfred Powery Primary School 1,600
Queen of Peace Girls Primary School 15,000
Nadapal Primary School 2,000
Kaitese Primary School 1,000
Kalomegur Primary 1,000
Kaeris Primary School 550
Kadongolo Primary School 550
Lochwa ECD 1,000
Kalapata Primary School 250
Karoge Primary School 800
Kangakipur Primary School 500
Lokichar Girls’ Primary School 4,000
Kapese Nursery School 350
RCEA Lokori Boys’ 1,000
White Angels Academy 1,300
Lotubae Girls’ High School 1,000
Kadam Primary School 1,100
Sisters of Mercy Lokori 2,000
Fathers House Lokori 2,000
Jumla 671,803
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC 223,934
JIMBO LA MACHAKOSParokia Kiasi
Syokimau 287,500.00
Tala Central 271,508.00
Kyale 261,455.00
Tawa 200,000.00
Matiliku 170,000.00
Kanzalu 135,540.00
Kithimani 132,050.00
Mbumbuni 120,000.00
Kinyui 110,205.00
Komarock 104,000.00
Mlolongo 101,400.00
Cathedral 100,000.00
Kitwii 96,216.00
Ikalaasa 95,250.00
Nguluni Tala
86,295.00
St. Jude Catholic
81,400.00
St. Mary’s Tala 78,237.00
Kola 75,000.00
Mwala 71,445.00
Masinga 65,200.00
Utangwa 59,150.00
Kangundo 57,640.00
Kalawa 52,150.00
Kaewa 51,250.00
Mbuvo 51,000.00
Makueni Pr 51,000.00
Kilungu 50,875.00
Joska 50,400.00
Mbooni 45,330.00
Kaumoni 43,400.00
Mitaboni 41,882.00
Kambu 40,700.00
Mbiuni 39,410.00
Makindu 36,000.00
Miseleni 35,150.00
Kithangaini 35,000.00
Mtito Andei
34,000.00
St Jude Kivaa
33,850.00
Emali 31,250.00
Tulimani 30,000.00
Muthetheni 30,000.00
Kwa Kathule
30,000.00
Mutituni 28,603.00
St. Joseph Makaveti
27,510.00
Mavoloni 27,000.00
33
Kithangaini 35,000.00
Mtito Andei
34,000.00
St Jude Kivaa
33,850.00
Emali 31,250.00
Tulimani 30,000.00
Muthetheni 30,000.00
Kwa Kathule
30,000.00
Mutituni 28,603.00
St. Joseph Makaveti
27,510.00
Mavoloni 27,000.00
Kawethei 26,230.00
Mbitini 24,800.00
Kiongwani Parish
24,800.00
Kasikeu Parish
24,400.00
Kabaa 23,890.00
Precious Blood Kilungu High l
22,770.00
Matuu 21,500.00
Nguluni - kilungu
20,330.00
Donyo Sabuk
20,000.00
Mbuani 20,000.00
CDM Ekalakala Parish
20,000.00
Katoloni 19,175.00
Kinyambu 15,000.00
St. Augustine Machakos University
12,500.00
Katheka 10,055.00
Yathui 10,000.00
St. Camilus 10,000.00
Masii 9,365.00
St. Thomas Aquinas Thomeandu Secondary
8,050.00
Mukuyuni 7,500.00
Sultan Hamud
7,000.00
St. Joseph’s Catholic Church Prison
5,000.00
St. Teresia Kilungu Academy
3,050.00
St Luke, Makutano
5,000
St Chris-topher, Kyumbi
20,000
4,045,666.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
1,368,428.00
JIMBO LA MERU
Parokia Kiasi
Cathedral 655,910.00
Nkubu 412,000.00
Laare 304,525.00
Mikinduri 251,845.00
Kangeta 213,000.00
Chuka 202,960.00
Kionyo 200,000.00
Kibirichia 162,325.00
Muthambi 160,090.00
Tuuru 152,350.00
St. Massimo 146,720.00
Gatimbi 140,000.00
Igoji 136,000.00
Kajuki 130,650.00
Timau 130,000.00
Runogone 129,189.00
Riiji 128,740.00
Kariene 127,965.00
Mutuati 127,000.00
Kinoro 123,500.00
Magundu 112,895.00
Mbaranga 110,150.00
Miruriiri 105,500.00
Limbine 105,100.00
Nkabune 104,965.00
Iruma 101,750.00
Chogoria 100,000.00
Mujwa 96,160.00
Athi 95,965.00
Amung’enti 93,500.00
Maua 93,175.00
Magumoni 93,070.00
Tigania 91,200.00
Ruiri 90,525.00
Gatunga 90,000.00
Mpukoni 90,000.00
Kiirua 88,260.00
Mitunguu 81,090.00
Giaki 80,000.00
Mukothima 78,000.00
Mikumbune 77,250.00
Kirogine Pro 75,970.00
Chaaria 75,850.00
Michaka 75,050.00
Munithu 70,700.00
34
Ndagani (Prop) 70,365.00
Nkondi (Pro) 68,300.00
Buuri 66,301.00
Nthare 65,855.00
Kanyakine 61,400.00
Antubetwe 61,300.00
Kariakomo 61,000.00
Munga 61,000.00
Katheri 59,705.00
Kagaene 55,200.00
Marimanti 51,000.00
Tunyai 50,200.00
Chera 50,000.00
Nthambiro 50,000.00
Athiru 47,900.00
Igandene 42,400.00
Mukululu 42,000.00
Kianjai 40,900.00
Kaongo 39,000.00
Nciru 38,960.00
Matiri 38,235.00
Kiamuri 28,605.00
Nchaure 27,555.00
Charanga 27,000.00
Maraa 27,000.00
Mbwiru 24,850.00
Thanantu 6,000.00
Institutions
Christ the Saviour Meru Prison Chapel
182,410.00
Consolata Hospital Nkubu 77,950.00
Consolata Hospital Chaplaincy Nkubu
35,000.00
Consolata Hospital School of Nurs-ing Nkubu
25,000.00
Marimba Chapel 22,470.00
Chuka Girls’ 80,000.00
Our Lady of Mercy Girls’ Sec Sch 78,930.00
Muthambi Girls’ Sec 60,132.00
St. Pius X Seminary 60,000.00
Allamano School Kangeta 52,800.00
Chuka Boys’ 45,000.00
St. Angela Nguthiru Girls’ Sec 33,250.00
Magumoni Day Sec 25,435.00
Kibirichia Boys’ Sec 25,000.00
Consolata Primary 25,000.00
St. Rita Amwamba Girls 20,000.00
St. Massimo Sec Sch 18,000.00
Mfariji Primary Sch 17,100.00
Akaiga Sec Sch 16,000.00
St. Theresa’s Hospital Kiirua Staff 15,050.00
St. Daniel’s Boys High 15,000.00
Blessed Virgin Sisters Kangeta 10,000.00
Don Orione Srs Laare 10,000.00
Bishop Bessone Primary Sch 10,000.00
Kithitu Prayer House 10,000.00
Fr. Soldati Memorial Primary 9,210.00
St. Dorothy School Massimo 8,556.00
St. Theresa’s Primary Sch Riiji 8,200.00
Poor Handmaids of Jesus Christ Sisters St. Ann Igoji
8,000.00
St. Lawrence Igoji Teachers College Chapel
8,000.00
Joseph Allamano Boys 8,000.00
Muthara Day Mixes Sec 7,700.00
Kinoro Girls Sec 7,650.00
Kanyuru Sec Sch 7,000.00
Brothers of St. John of God 7,000.00
St. Augustine Kirindine Sec Sch 7,000.00
St. Francis of Assissi 5,600.00
Kimiri Primary Sch 5,500.00
Muthambi Boys Sec 5,300.00
NSA Divine Mercy Printers 5,000.00
NSA St. Ann Community 5,000.00
Igandene Boys Sec 5,000.00
Mpukoni Sec Sch 5,000.00
St. Anselmin Mururi 5,000.00
Matei Dei Primary 5,000.00
Akithi Sec Sch 5,000.00
35
Kaongo Girls Sec Sch 4,800.00
Kirindara Primary 4,585.00
Poor Handmaids of Jesus Christ 4,000.00
Consolata Primary Sch Community Srs.
4,000.00
Mukuuni Sec Sch YCS 4,000.00
San panpuri Primary 3,850.00
Matakiri Sec Sch 3,300.00
St. Elizabeth Primary Iruma 3,270.00
Igandene Day Sec 3,000.00
St. Francis F. C. Convent 3,000.00
St. Jude Kangeta Prison 3,000.00
Consolata Sisters Gitoro 3,000.00
St. Mary Primary Antubetwe 3,000.00
Mfariji Girls Secondary 3,000.00
Holy Family Primary Sch Kiamuri 3,000.00
Evangelising Sisters Mikinduri 3,000.00
Kiriani Boys 3,000.00
Aithu Primary Mutuati 2,900.00
Holy Family Athiru Primary 2,790.00
Thuuria Primary Sch 2,500.00
K. K. Etara Primary 2,500.00
Mbayo Sec Sch 2,250.00
Sacred Heart Primary Sch Kinoro 2,150.00
Ntiruti Primary Sch Mbaranga 2,150.00
Kamwimbi Sec Sch 2,150.00
Lubuathirua Day Sec Sch YCS 2,120.00
Sisters of Holy Angels Allamano 2,000.00
Kaare Primary 2,000.00
Mukululu Day Sec 2,000.00
St. Bonventure Mumbuni YCS 2,000.00
St. Peter & Paul Primary Laare 2,000.00
Thitha Sec Sch 1,570.00
Muthambi Primary 1,550.00
Giantune CCM Primary Sch 1,535.00
Thuuria Sec Sch YCS 1,500.00
Antuonduru Sec Sch YCS 1,500.00
St. Mary’s Sec Sch Ntaki Antubetwe
1,500.00
Kirindara Sec Sch 1,500.00
Mukuthuku Day 1,500.00
Sisters of St. Joseph of Tarbes 1,200.00
Ntiruti Sec Sch Mbaranga YCS 1,200.00
CCM Meru Township Primary 1,005.00
Nkamathi Primary Mutuati 1,000.00
CCM Meru Township Sec Sch 1,000.00
Kagongo Primary 1,000.00
St. Charles Lwanga Day and Board-ing
1,000.00
Kiamuri Day & Boarding Primary Sch
1,000.00
Rex Mukona 935.00
Marima Primary 750.00
Irinda Day Sec Sch 700.00
Ikindu Primary Sch 700.00
Thege Primary Sch 500.00
Mikinduri Primary Sch 470.00
Maatha Primary 300.00
Mutiguru Day Sec 200.00
Ramesh - MD Silverspread Hardwares Ltd
50,000.00
Jumla 8,845,598.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
3,010,521.00
JIMBO KUU LA NYERIParokia Kiasi
Doldol 67,025.00
Kigumo 51,544.00
Wamagana 72,974.00
Our Lady of Consolata Nyeri Cathedral
376,924.00
St. Vincet Depaul Catholic Giathugu
35,050.00
St. Charles Lwanga Narumoru Town 51,320.00
Our Lady of Consolata Thegu 56,000.00
Kiamuiru 67,043.00
Mugunda 41,957.00
36
Sirima 105,886.00
Gathugu 51,145.00
Kigogoini 9,460.00
Mweiga 136,640.00
St. Joseph Giakanja 133,332.00
St. Martin’s Wiyumiririe Mission 18,475.00
King’ong’o 123,640.00
Mukurweini 118,700.00
Karangia 42,000.00
Kangaita 110,350.00
Kaheti 66,625.00
St. Jude 171,940.00
Kariko 51,180.00
St. Cyprian Kagicha 63,800.00
St.Teresa Equator 343,900.00
Kahiraini 22,893.00
Our Lady of Consolata Birithia 100,200.00
Kimondo 39,600.00
Karemeno 46,190.00
Karatina 160,000.00
Karima 167,000.00
Gikondi 40,250.00
Gikumbo 83,800
St Joseph Kamariki 45,000.00
Endarasha 80,000.00
St.Charles Lwanga Ngangarithi
70,000.00
Irigithathi Project 82,560.00
Munyu 25,000.00
Mwenji 80,873.00
Ngandu 150,000.00
Tetu 130,012.00
Kalalu 140,000.00
Nanyuki 154,383.00
Gititu 71,250.00
Kabiruini 97,140.00
Othaya 153,330.00
Miiri 96,000.00
Matanya 149,200.00
Ithenguri 80,000.00
St. Michael Kiganjo/Chaka 42,000.00
St Joseph Karuthi 21,800.00
Giakaibei 80,000.00
Gatarakwa -
Sub-Total 4,775,391
Institutions/Offices
Nyeri High School 14,000
Franciscan Sisters of The Immacu-late Heart of Mary
2,000
A.D.N Catholic Action 40,000
St.Augustine’s Catechist Training institute
26,360
Christ the King MC Recurrent Expenditure
93,525
Mary Immaculate Convent 31,500
Othaya Girls Secondary School 4,600
ADN Caritas Nyeri 98,300
Archbishop Emiritus Retirement Home
27,700
Fenician Sisters 3,000
Consolata Fathers Mathari 10,000
Consolata Cathedral Institute 12,000
Cash ADN Finance 8,000
Mathari Chaplainacy Catholic 8,000.00
Friends of Caritas 273,535.00
Sub-Total 652,520
Jumla 5,427,911
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
2,713,955.00
JIMBO LA EMBU Parokia Kiasi
St. Joseph Mukasa Mbiruri 349,907.00
St. Francis of Asissi Nthagaiya 329,460.00
Our Lady of Assumption Embu 288,724.00
Sacred Heart Kyeni 269,815.00
St. Paul’s Kevote 248,191.00
37
St. Joseph Kianjokoma 247,905.00
Holy Family Nguviu 220,058.00
St. Thomas Moore Kairuri 179,645.00
Ss. Peter & Paul Cathedral 163,672.00
St. Francis Xavier Siakago 156,650.00
Our Lady Of Consolata Iriamurai 129,540.00
St. Benedict Karau 105,180.00
Mary Mother of God Karurumo 74,470.00
St. Teresa Kithimu 145,980.00
St. Anthony of Padua Mutuobare 68,300.00
Christ the King Kathunguri 59,550.00
Good Shepherd Ishiara 49,915.00
Sacred Heart Karaba Wango 33,825.00
St. Lawrence Munyori 32,290.00
St. John the Baptist Kirie 26,220.00
St. Paul’s Makima 22,000.00
Holy Trinity Gwakaithe 15,000.00
Sub-Total 3,216,297.00
Taasisi
St. Paul’s Kevote Parish
ACK St. Marks Karue Primary 400.00
Mt. Kenya Academy pupils 2,040.00
Mt. Kenya Academy staff 500.00
St. Joseph of Tarbes Secondary 10,400.00
St. Joseph of Tarbes Primary 6,270.00
Consolata Primary staff 950.00
Primary pupils 2,780.00
St. Michael Secondary staff 250.00
St. Michael Secondary students 3,045.00
St. Michael Kevote Primary staff 1,700.00
St. Michael Kevote Primary pupils 7,470.00
St. Philip’s Makengi Primary 4,080.00
ACK St. Catherine Keruri Primary 1,915.00
Consolata Secondary 9,151.00
St. Paul’s High School students 143,408.00
St. Paul Parochial Primary pupils 4,401.00
St. Joseph Kiandari Primary pupils 4,927.00
St. Joseph Kiandari Primary staff 950.00
St. Francis Ngoire Secondary staff 420.00
St. Francis Ngoire Secondary students 2,870.00
Deputy St. Paul’s High 1,000.00
Principal St. Paul’s High 5,000.00
St. Francis Ngoire Primary staff 600.00
St. Francis Ngoire Primary pupils 3,555.00
ACK Kianjuki Primary staff 550.00
ACK Kianjuki Primary pupils 1,115.00
ACK Kianjuki Secondary students 1,400.00
Priests of Kevote Parish 15,000.00
Sub-Total s 236,147.00
Saints Peter & Paul Cathedral Parish
PMC Gachoka 1,015.00
Carlo Liviero Home 6,000.00
Rianjeru Primary 560.00
Saints Peter & Paul Primary 680.00
Itabua Secondary 10,601.00
Itabua Primary 775.00
Kihumbu Primary 861.00
Embu Shepherd Academy 5,166.00
Gatondo Primary 355.00
Gatondo Secondary 500.00
Embu Kawa Academy Cathedral 2,000.00
Felician Sisters Embu 9,000.00
Don Bosco Technical-Embu 2,040.00
Embu High 550.00
Sub-Total s 40,103.00
St. John the Baptist Kirie Parish
Kirie Primary 3,250.00
St. John Kirie Secondary 2,255.00
St. Elizabeth Primary 2,060.00
Feather’s Education Centre 1,200.00
St. Peter’s Mbarwari Secondary 1,120.00
Mbarwari Primary 1,150.00
Nguthii Primary 850.00
Kavui Primary 825.00
Kathigagaceru Secondary
750.00
Itururi Primary 490.00
38
Usambara Primary 310.00
Sub-Total 14,260.00
St. Paul’s Makima Parish
Blessed Irene Mbondoni Secondary
2,000.00
St. Joseph Kitoloni Secondary 1,500.00
St. Mary’s Mashamba Secondary 1,000.00
St. Augustine’s Kanyonga Secondary
1,500.00
Sub-Total 6,000.00
St. Francis Xavier Siakago Parish
St. Michael Gacuriri Primary 975.00
Mathai Primary 2,670.00
Rwanjeru Primary 380.00
Ngunyumu Primary 400.00
Don Marino Primary 650.00
Gitiburi Primary 2,000.00
Siakago Primary 2,580.00
St. Rita Ngunyumu Secondary
270.00
St. Albert Siakago Boys’ 2,025.00
Sub-Total 11,950.00
Good Shepherd Ishiara Parish
St. Teresa Fasce Primary 7,450.00
St. Peter’s Boarding Primary
5,700.00
St. Kizito Primary 4,175.00
St. Thomas Kigwambiti Primary 600.00
Mang’ote Primary 1,105.00
Kamukanya Primary 1,975.00
Mbaci Primary 200.00
Ciaikungugu Primary 1,050.00
Mbaraga Seondary 1,245.00
Kambugu Primary 870.00
St. Mary’s Ntambari Primary 3,205.00
St. Ann Kigwambiti Primary 955.00
Mbaraga Primary 1,090.00
Kianjeru Primary 465.00
St. Augustine’s T.T College 20,000.00
St. Monica Girls 27,000.00
Sub-Total 77,085.00
St. Francis of Assissi Nthagaiy
Elizabethian Sisters 2,000.00
Nthagaiya Catholic Dispensary 1,150.00
Kavuru Primary 75.00
St. Mary’s Kigaa Secondary 2,070.00
Nthagaiya Catholic Priests 5,700.00
St. Jerome Ugweri Secondary
1,685.00
St. Catherine Nthagaiya Girls’ 2,905.00
Kigaa Primary 1,740.00
Kathamba Primary 970.00
Sub-Total 18,295.00
Our Lady of Assumption Embu Parish
University of Embu 2,100.00
Our Lady of Assumption Embu Priests 5,000.00
St. Emilio Kithungururu 4,875.00
Our Lady of Assumption Embu Primary
3,894.00
St. Angelas Embu Children Home 3,250.00
Kirimari Boys’ Secondary 1,691.00
KMTC Embu Level 5 Hospital 750.00
St. Joseph Gituri Secondary 800.00
Gituri Primary 865.00
St. Martha Gatoori Secondary 2,060.00
Kangaru Girls Secondary 6,800.00
St. Michael Primary 3,281.00
Kangaru High 2,370.00
Gatoori Primary 575.00
Sub-Total 38,311.00
St. Teresa’s Kithimu Parish
St. Teresa’s Girls’ 86,640.00
St. Benedict Secondary 335.00
St. Andrew’s Primary 5,600.00
Joseph Allamano Primary 760.00
39
St. Mary’s Ithangawe Primary 4,000.00
Mother Angelina Primary 1,420.00
Kiandundu Primary 200.00
Kithegi Day Secondary 240.00
Kamuthatha Boarding Primary 5,600.00
Rukira Primary 790.00
Nembure Primary 1,990.00
Nembure Junior Academy 620.00
Nembure Polytechnic 1,005.00
Rukira Day Secondary 1,300.00
Bethany Junior Academy 250.00
Mbukori Primary School 365.00
Sub-Total 111,115.00
St. Joseph Kianjokoma Parish
St. Boniface Mugui Secondary
2,305.00
St. Joseph Kianjokoma Parish Priests
350.00
St. Joseph Kianjokoma Primary 10,970.00
St. John Fisher Primary 2,295.00
St. John Fisher Secondary 1,010.00
Irangi Primary 175.00
St. John Gaikama Boarding Primary 1,000.00
Mugui Primary 3,755.00
Kavutiri Secondary 640.00
Sub-Total 22,500.00
Our Lady of Consolata Iriamurai
Igumori Primary 355.00
Consolata Girls Secondary 5,200.00
St. Thomas Aquinas Igumori Secondary
1,180.00
Sub-Total 6,735.00
Mary Mother of God Karurumo Parish
St. Jude Secondary 2,260.00
Karurumo Primary 2,460.00
Kandete Primary 530.00
St. Barnabas Rarurumo School 150.00
Mary Mother God Karurumo Priests
1,880.00
Sub-Total 7,280.00
St. Joseph Mukasa Mbiruri Parish
St. Joseph Mukasa Mbiruri Priests 7,730.00
St. Petroc Academy 500.00
YCS Kagaari Secondary 1,210.00
DEB Kubukubu Memorial Primary 14,200.00
Maragari Secondary 150.00
Gichiche Primary 205.00
Mwenendega Primary 2,010.00
Subrina Academy 970.00
DEB Gitare Secondary 2,005.00
DEB Gitare Primary 3,300.00
SA Nduuri Secondary 225.00
SA Nduuri Primary 2,690.00
Munyutu Primary 570.00
Millenium Annex 306.00
Moi High Mbiruri Secondary 1,400.00
Our Lady of Annunciation Primary 1,280.00
Sub-Total 38,751.00
St. Lawrence Munyori Parish
Kangungi Primary School 2,555.00
St. Mary’s Kangeta Primary 1,960.00
St. Clare’s Girls’ Kangeta 1,360.00
CCM Kangeta Primary 1,280.00
St. Francis Kamunyange Primary 1,190.00
St. Monica Munyori Primary 1,000.00
Rugakori Primary 1,000.00
St. Mary’s Gataka Primary 985.00
Yoder Karwigi Secondary 930.00
St. Mary’s Munyori Primary 800.00
DEB Muraru Primary 745.00
St. Joseph Gachuriri Primary 640.00
Rianguu Primary 640.00
St. Mary’s Gataka Secondary
200.00
St. Francis Kamunyage Secondary 200.00
40
Sub-Total 15,485.00
Sacred Heart Kyeni Parish
Sacred Heart Kyeni Girls’ 48,170.00
Sacred Heart Kyeni Boarding Primary
16,895.00
St. Luke Rukuriri Primary 3,035.00
Rukuriri Primary 4,160.00
St. Mary’s Parochial Primary 3,490.00
St. Michael Primary-Kiangungi
2,050.00
SA Secondary 1,235.00
Fidenza School of Nursing 1,915.00
Kiangungi Secondary 2,085.00
St. Mary Goretti Rukuriri Secondary
5,710.00
Gakwegori Primary 545.00
Gakwegori Secondary 8,000.00
Kathari Secondary 1,980.00
St. Agnes Kiagaanari Secondary 820.00
Rukuriri Tea Factory staff 1,750.00
Njeruri Primary 1,350.00
ACK Kathanjuri Secondary 130.00
Felician Sisters Kyeni Community 2,500.00
Clergy of Sacred Heart 5,800.00
Sub-Total 111,620.00
Sacred Heart Karaba Wango Parish
Karaba Wango Boys’ Secondary 1,700.00
Wachoro Boys Secondary 2,050.00
Unyuani Primary 7,750.00
Consolata Girls’ Gitaraka 2,100.00
Wachoro Security Team 1,000.00
Wakalia Primary 2,700.00
Makawani Primary 240.00
Iria Itune Primary 3,500.00
FA Masaku Family 2,170.00
Whiterose Medical Centre Gategi 2,000.00
St. Joseph Gategi Girls’ 1,755.00
Karaba Primary 1,080.00
St. Mary’s Gategi Primary 3,410.00
Wachoro AP Camp 1,250.00
Wango Boarding Primary 3,350.00
Gitaraka Primary 550.00
Sub-Total 36,605.00
Jumla 4,008,539.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
1,105,785.00
JIMBO LA NYAHURURUParokia Kiasi
Cathedral 246,925.00
Ol Kalou 198,879.00
Ng’arua 180,000.00
Ndunyu Njeru
130,000.00
North Kinangop
117,683.00
Marmanet 100,000.00
Ngano 98,000.00
Mairo Inya 88,000.00
Manunga 84,870.00
Ndaragwa 80,000.00
Equator 70,000.00
Mutanga 65,550.00
Ol Joro Orok
75,000.00
Murungaru 61,000.00
Shamata 61,000.00
Njabini 59,643.00
Kasuku 48,200.00
Muhotetu 47,100.00
Pondo 45,000.00
Rumuruti 40,560.00
Dundori 40,000.00
Geta 40,000.00
Weru 38,500.00
Mukeu 37,000.00
Ngorika 32,000.00
Shamanei 31,400.00
Tumaini 29,950.00
Kanyagia 27,000.00
Magumu 25,600.00
Igwamiti 23,673.00
Ol Moran 21,500.00
Mochongoi 20,113.00
Sipili 18,750.00
Maina 12,000.00
Rironi 0
Taasisi
Njonjo Girls High School
13,000.00
Mary Mother of Grace Boys High School
5,625.00
Sisters of Mary Im-maculate
5,000.00
North Kinangop Hospital
5,000.00
41
Nyakiambi Girls High School
5,000.00
St. Anne Institute
4,880.00
Ndururi Secondary School
4,140.00
Ngumo Secondary School
3,000.00
Kangui Secondary School
3,000.00
Leshau Boys High School
2,685.00
Manunga Girls Sec-ondary
2,100.00
Gatimu Secondary School
1,200.00
Muhotetu Girls Sec-ondary
6,00.00
Jumla 2,350,126.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
1,175,063.00
JIMBO LA GARISSAInstitution Kiasi
Garissa Cathedral 14,600.00
Wajir Parish 28,100.00
Bura Parish 22,600.00
Mandera Parish 6,500.00
St. Kizito SCC Dadaab
13,000.00
Hagadera SCC Dadaab
20,000.00
St.Peter’s Church Garissa
13,500.00
Wenje Parish 3,260.00
Hola Parish 5,000.00
Jumla 126,560.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
63,280
JIMBO KUU LA MOMBASAParokia Kiasi
Holy Ghost Cathedral
202,820.00
Chan-gamwe
168,775.00
Customs/Nyali
140,014.00
Mtopanga 114,831.00
Kilifi 93,110.00
Tudor 61,750.00
Miritini 60,000.00
Chaani 54,658.00
Kongowea 45,150.00
Ukunda 40,000.00
Shimba Hills
38,250.00
Shanzu 32,550.00
Taveta Mjini
30,300.00
Timbwani 30,000.00
Kiembeni 30,000.00
Mikindani 25,102.00
Mbungoni 25,000.00
Bangla-desh
22,850.00
Voi 22,000.00
Timbila 20,900.00
Mtwapa 20,100.00
Mariakani 20,000.00
Bamba 19,824.00
Ramisi 19,100.00
Bomu 17,000.00
St George Chaplain-cy- Shimo la Tewa
13,800.00
Kitumbi 12,400.00
Kinango 12,300.00
Wundanyi 11,500.00
Mgange Dawida
11,450.00
Pope Francis–Mikindani Outstation
11,190.00
Mivumoni 10,400.00
Giriama 10,400.00
Taru 10,000.00
Lushan-gonyi
10,000.00
Migom-bani
8,500.00
Kikambala 8,450.00
Kwale 7,500.00
Sagalla 7,500.00
Kikoneni 6,800.00
Bura Parish
6,050.00
Chala 5,000.00
Kichaka Simba
5,000.00
Maungu 4,000.00
Ndavaya 1,500.00
Mwanda 3,700.00
Makupa -
Mtongwe -
Kaloleni -
Lunga Lunga
-
Eldoro -
Chumvini -
Taasisi 4,000.00
Sisters of St. Joseph - St. Elizabeth Commu-nity
1,500.00
Secular Franciscan Order-Mombasa
St Joseph Catholic Primary School-Ukunda
13,000.00
St Angelo Prmary School-Ukunda
11,500.00
St. Joseph Herman Maxx Nursery & Primary School-Mtopanga
42
JIMBO LA KITUIParokia Kiasi
Migwani 30,500
Kabati 10,000
Kavisuni 38,430
Kyuso 12,275
Ikanga 25,000
Mutune 36,000
Kamuwongo 11,050
Nuu 10,825
Kiio 2,400
Nguni 7,000
Nguutani 32,351
Mutomo 91,000
Mwingi 44,258
Kimangao 5940
Muthale 32,340
Mulutu 25,825
Boma 50,000
Mbitini 20,000
Ikutha
Miambani 33,500
Zombe 15,220
Mutito 30,000
Museve 34,200
Endau
Mbondoni 15,130
Kanyangi 93,440
Kasyala 34,010
Jumla 740,694
Taasisi
Assumption Sisters of Nairobi - Boma
2,000
St. Augustine Secretariat 18,800
Jesus the Good Shepherd Academy
6,112
Mwingi Boys’ Secondary School
29,100
Maliku Girls’ Secondary School
1,555
Mwingi Teachers Train-ing College
267
Kanginga Primary School
667
Kyethani Secondary School
207
AIC Nzeluni Girls’ School
3,534
Mwingi Universal College
1,534
Ikanga Girls’ School 5,000
Mlamba High School - Mgange Dawida
1,000.00 St James Primary School- Mgange Dawida
800 St Susan Nursery & Primary School - Mgange Dawida
600
Jumla 1,563,924.00
Kiasi remitted to the National CJPC
518,566.00
Ikanga Boys’ Secondary School
2,700
St. Josephine Bakhita Zombe
16,200
Musengo Secondary School
300
Tulia Vocational Centre 400
Mutongoni Polytechnic 140
Ithiiani Secondary School
2,000
St. Charles Lwanga Secondary
60,753
Thitani Girls’ Secondary School
5,005
Matinyani Boys’ Second-ary School
7,000
Kathonzweni School 2,381
St. Angelas Girls’ Sec-ondary
67,080
St. Gabriel B. Primary School
33,000
St. Michael’s Primary School
94,032
Sub-Total 359,767
Jumla 1,100,461
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
443,979
JIMBO LA MURANG’AParokia/ Taasisi
Kiasi
Baricho 103,280.00
Cathedral 98,000.00
Difathas 50,000
Donga 19,650.00
Gaichanjiru 40,000.00
Gatanga 235,380.00
Gatura 61,911.00
Gaturi 9,000.00
Gitui 49,189.00
Ichagaki 13,320.00
Ithanga 53,720.00
Kaburugi 21,000.00
Kagumo 110,000.00
Kahatia 12,000.00
Kangaita 73,800.00
Kangari 100,000.00
Karaba 66,903.00
Karumandi 75,000.00
Kenol 100,000.00
43
Ikanga Boys’ Secondary School
2,700
St. Josephine Bakhita Zombe
16,200
Musengo Secondary School
300
Tulia Vocational Centre 400
Mutongoni Polytechnic 140
Ithiiani Secondary School
2,000
St. Charles Lwanga Secondary
60,753
Thitani Girls’ Secondary School
5,005
Matinyani Boys’ Second-ary School
7,000
Kathonzweni School 2,381
St. Angelas Girls’ Sec-ondary
67,080
St. Gabriel B. Primary School
33,000
St. Michael’s Primary School
94,032
Sub-Total 359,767
Jumla 1,100,461
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
443,979
Kerugoya 117,570.00
Kiamutugu 40,000.00
Kiangai 142,970.00
Kiangunyi 100,100.00
Kianyaga 55,457.00
Kiriaini 50,000.00
Kitito 20,000.00
Kutus 189,355.00
Makuyu 56,460.00
Maragua 60,000.00
Mariira 90,000.00
Mugoiri 35,000.00
Mukurwe 31,613.00
Mumbi 58,681.00
Muthangari 21,000.00
Mwea 221,000.00
Nguthuru 20,000.00
Piai 46,300.00
Ruchu 100,000.00
Sabasaba 18,350.00
Sagana 45,000.00
Tuthu 25,000.00
Kanyenyeini 56,106.00
Kibingoti 19,250.00
Kagio 128,988.00
Makomboki 26,140.00
SMI 20,550.00
Jumla 3,087,043.00
Fungu lili-lopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
780,000.00
JIMBO LA MARALALInstitutions Kiasi
Suguta Parish 49,999.50
Prison Chaplaincy 10,000
CDM Secretariat/Cartas Maralal 7,750
Good Shepherd Minor Seminary 0
Wamba Parish 136,050
South Horr Parish 61,000
Archers Post Parish 15,250
Maralal CathedralParish
135,075
Tuum Parish 60,000
Lorroki Parish 33,690
Baragoi Parish 60,000
Barsaloi Parish 10,000
Morijo Parish 31,500
Lodokejek Parish 100,000.50
Lodungokwe Mission 14,703
Bishop Philip Perlo Girls’ Secondary 0
Sisters of Mary Immaculate 0
Suguta Girls Rescue Centre 0
Sereolipi Parish 44600
KCB Maralal 50,000
Sererit Parish 29,200
Equity Bank Maralal 5,000
Jumla 853,817
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
212,357
JIMBO LA NAKURUNakuru Deanery
Parokia Kiasi
St Joseph the Worker 143,996
St Francis Kiti 115,243
St Monica Section 58
100,000
Cathedral 97,077
Holy Trinity Milimani 80,000
St Augustine Kiamunyi 79,000
Holy Cross 68,587
Hekima 32,418
Prisons Chaplaincy 10,105
Jumla 726,422
Lanet Deanery
St John’s Muguga 183,057
St Peter Lanet 78,616
St Paul’s Wanyororo 51,060
St Peter and Paul Kip-tangwanyi
48,000
Jumla 360,733
Molo Deanery
St Mary’s Molo 175,000
St Timothy Jumla 40,000
Kamwaura Parish 30,000
St Simon Peter-Turi 17,000
St Kizito Olenguruone 10,000
St Veronica Keringet 10,000
Mwaragania Parish 7,100
Jumla 289,100
Njoro Deanery
St Lwanga Njoro 120,000
Mangu Parish 80,000
St Peters Elburgon 41,700
Larmudiac Parish 30,000
Rongai Parish 30,000
44
TUME YA HAKI NA AMANI YA AOSKShirika/Taasisi Kiasi
Sisters of Mary of Kakamega - Nairobi 5,000.00
LSOSF, EORV REGION 17,410.00
Kitale District Unit 6,750.00
Nakuru District Unit 13,000.00
Mombasa District Unit 22,000.00
Machakos District Unit 26,550.00
Sisters of Our Lady of Mission 17,300.00
AOSK Justice and Peace Commission 10,000.00
Jumla 121,010.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC 47,620.00
JIMBO LA KERICHOParokia Kiasi (received in diocese)
Bomet 30,000.00
Cathedral 15,000.00
Chebangang -
Chebole 20,000.00
Chemelet 26,000.00
Chepseon 12,000.00
Embomos 3,000.00
Fort Ternan 25,000.00
Kabianga 20,000.00
Kaboloin 5,850.00
Kapkatet 10,000.00
Kapkilaibei 8,000.00
Kaplomboi 15,000.00
Kaplong 70,000.00
Kapsigiryo -
Kebeneti 8,000.00
Keongo 15,000.00
Egerton Chaplaincy 20,000
St Francis Lare 15,000
Jumla 336,700
Bahati Deanery
Bahati Parish 142,000
St Michael Kiamaina 90,000
St John’s Upper Subukia 70,000
St Francis Lower Subukia
35,000
All Saints Kabazi 20,000
Jumla 357,000
Koibatek Deanery
Marigat Parish 59,840
St Patricks Eldama Ravine
20,000
Mogotio Parish 15,000
Jumla 84,840
Kabarnet Deanery
St Joseph Kituro 35,000
St Mary’s Kabarnet 35,000
Kipsaraman Parish 17,000
St Peter’s Kaptere 11,350
St Mary’s Tenges 2,200
Kerio Valley Parish- Salawa
Jumla 100,550
Naivasha Deanery
St Xavier Naivasha 83,980
Holy Spirit Gilgil 109,000
St Anthony DCK Parish 68,000
St Stephen Karati Parish 28,500
Kinungi Parish 25,540
Longonot Parish 15,000
Jumla 330,020
East Pokot Deanery
Kositei 2,500
Barpello C Mission
Tangulbei
Rotu
Jumla
Institutions
Christ the King Academy
37,450
St. Clare Girls Sec Elburgon
12,400
Bishop’s House 10,000
Franciscan Missionary Sisters for Africa
2,500
Franciscan Missionary Sisters for Africa- Novi-ciate
2,500
Jumla 64,850
Jumla 2,662,719
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
477,189.00
45
Kimatisio 10,000.00
Kimugul 15,000.00
Kipchimchim 60,000.00
Kipkelion 18,000.00
Kiptere 20,000.00
Koiyet 24,000.00
Litein 40,000.00
Londiani 39,234.00
Longisa 8,000.00
Makimeny -
Marinyin 37,500.00
Matobo 100,000.00
Magogosiek 10,000.00
Mombwo -
Mugango 12,000.00
Ndanai 34,000.00
Nyagacho 10,000.00
Roret 10,100.00
Segemik -
Segutiet 27,000.00
Sigor 5,000.00
Siongiroi 11,000.00
Sironet 16,000.00
Sotik 58,000.00
Tegat 10,000.00
Telanet 16,540.00
Kapcholyo High 540.00
Kaplong Girls’ Primary
340.00
Queen of Angels Primary
590.00
Kaplong Boys’ Primary
220.00
Kaplong Girls’ High 10,450.00
Queen of Angels High 2,660.00
Kaplong Boys’ High 6,660.00
St. Clare Kaplong School of Nursing
400.00
St. Mary’s Primary Day & Boarding Mixed School
30,000.00
Fr Kaiser 10,000.00
Jumla 926,084.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
473,042.00
JIMBO LA ISIOLO
Parish/Institution Kiasi
Kinna Catholic Mission 3,000.00
Merti Catholic Mission 3,410.00
Our Lady of Assumption Catholic Mission
6,100.00
Garbatulla Catholic Mission 12,340.00
Kiwanjani Catholic Mission 8,000.00
Camp Garba Catholic Mission 7,000.00
Oldonyiro Catholic Mission 15,000.00
St.Francis Xavier Catholic Mission -
St.Eusebius Cathedral Parish 30,550.00
Kipsing Catholic Mission 17,050.00
Ngaremara Catholic Mission 3,000.00
Jumla 105,450.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
70,300.00
Kositei 2,500
Barpello C Mission
Tangulbei
Rotu
Jumla
Institutions
Christ the King Academy
37,450
St. Clare Girls Sec Elburgon
12,400
Bishop’s House 10,000
Franciscan Missionary Sisters for Africa
2,500
Franciscan Missionary Sisters for Africa- Novi-ciate
2,500
Jumla 64,850
Jumla 2,662,719
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
477,189.00
46
JIMBO LA ELDORETParokia Kiasi
Arror 13,150.00
Burnt Forest 30,000.00
Chemnoet 33,000.00
Cheptarit 15,000.00
Chepterit 50,000.00
Chepterwai 15,000.00
Cheptiret 23,500.00
Chesoi 30,000.00
Chesongoch 20,000.00
Embobut 22,720.00
Endo 11,150.00
Huruma 185,562.00
Iten 40,000.00
Kaiboi 11,500.00
Kabechei 12,150.00
Kabuliot 14,720.00
Kamwosor 6,000.00
Kapcherop 25,560.00
Kapkemich 5,040.00
Kapkeno 15,000.00
Kapsabet 197,727.00
Kapsoya 126,850.00
Kapsowar 50,000.00
Kaptagat
Kapyemit 53,000.00
Kapkenduiywo 24,070.00
Kapkatet 7,100.00
Koptega 14,326.00
Kimumu 202,965.00
Kipsebwa 15,000.00
Kipngeru 10,000.00
Kobujoi 15,200.00
Langas 95,490.00
Lelwak 64,050.00
Majengo 223,350.00
Matunda 60,000.00
Moi University Chaplaincy 70,200.00
Moiben 21,600.00
Moi’s Bridge 71,100.00
Mokwo 23,700.00
Mosop 100,000.00
Nandi Hills 100,000.00
Ndalat 16,420.00
Nerkwo 30,085.00
Ol’Lessos 51,000.00
Ossorongai 80,030.00
Sacred Heart Cathedral 263,221.00
Sangalo 20,100.00
Soy 49,213.00
St.Augustine-Emsea
St John XXIII 102,890.00
St. Gabriel Chaplaincy 10,145.00
Singore Chaplaincy 10,000.00
Tambach 15,000.00
Tachasis 20,000.00
Tembeleo 32,200.00
Timboroa 14,620.00
Tindinyo 35,000.00
Tiryo 30,000.00
Turbo 40,000.00
Yamumbi 75,000.00
Ziwa 39,620.00
C.E.E.A Gaba Campus 15,510.00
School of Law Annex 4,285.00
Eldoret Prison’s Chaplaincy
6,500.00
Sub-Total 3,085,619.00
Shule
Our Lady of Assumption Academy Eldoret
15,485.00
St. Thomas Secondary - Kaiboi 10,000.00
Ancilla Catholic Academy 13,580.00
Jubilee Catholic Primary 8,365.00
lelwak High 1,450.00
47
Kemeliet Secondary 5,000.00
St. Peter’s High 40,000.00
Immaculate Heart Juniorate 2,141.00
St.Charles Lwanga-Chepkoiyo 2,500.00
St. Agatha Girls Secondary-Mokwo
44,000.00
St. Anthony Kaptumek Secondary 3,000.00
Maraba Secondary 1,100.00
Kapkoros Girls’ Secondary 5,010.00
St. Ann Girls Kapkemich 13,000.00
Christ the King Sambut 2,000.00
Kapkagaon Secondary 5,210.00
St. Josephs Kipsaina 14,400.00
Our Lady of Peace Nandi Hills 6,051.00
Apostolic Carmel Primary/Pre-Primary 50,250.00
Kimaren Secondary 5,000.00
St. Monica Secondary-Kapkoros 10,500.00
Christ the King- Tindinyo Academy 2,300.00
St. Raphael Chepyemit Secondary 20,000.00
Kaptagat Girls Secondary 18,000.00
Kondabilet Secondary 5,000.00
Kiborom Secondary 3,000.00
Kamoi Secondary- Kapcherop 6,000.00
St. Francis Secondary-Kimuron 21,776.00
Holy Cross Education Centre 4,000.00
Chirchir Secondary -Matharu 2,000.00
St. Ansalm Secondary-Matharu 2,100.00
Loreto Convent Girls’ Secondary-Matunda
5,000.00
St. Theresa Primary-Moi’s Bridge 1,005.00
Mogoiywo Primary 130.00
Samoget Primary 600.00
Kapkenduiywo Primary 500.00
Cheptoyoi Primary 1,300.00
St. Michael Kapkenduiywo Secondary 1,100.00
Christ the Kin High- Chepterit 10,000.00
Sambirir Girls High 24,200.00
Holy Trinity Girls’- Kaiboi 20,000.00
Patrician Primary- Kabongo 2,000.00
St. Mary’s Tachasis Girls Secondary
15,700.00
St. Placido Academy 3,000.00
St. Jude Academy-Huruma 10,100.00
St. Peter’s Secondary- Ngoisa 4,311.00
St. Peter-Kapkata 5,000.00
Limnyomoi Primary 800.00
St. Canisius High-Mateget 4,550.00
St. Benedict Seconary- Teber 1,000.00
St. Paul Primary- Kabechei 275.00
St. Patrick Kabirirsus Primary 1,120.00
Kapsergong Primary 550.00
St. Lawrence Academy- Ketigoi 2,000.00
St. John Academy- Setano 450.00
St.James Academy-Enego 250.00
Benedictine Academy-Kabichei 635.00
St. Vincent Academy-Kabirokwo 3,600.00
Ann John Kavuta 1,000.00
Chorwa Primary 1,280.00
St. Teresa Koibarak 5,000.00
Kobujoi Institute 2,300.00
St. Andrew’s Koibarak Secondary 2,010.00
St. Teresa of Avila-Ndalat 38,400.00
St. Augustine Secondary-Emsea 27,730.00
Kipsoen Boys Secondary 15,000.00
Sub-Total 554,114.00
Congregations
Cornelian Carmelite Sisters of Adorable Jesus
4,550.00
A.S.E-Novitiate Community 7,000.00
Carmelite Nuns-Tindinyo 4,000.00
Social Missionary Sisters of Church 2,000.00
Daughters of the Holy Rosary-Langas
1,000.00
Franciscan Sisters of Divine Mercy 3,000.00
Divine Mercy (FCDM) Sisters 500.00
Brothers of St. Joseph Nyeri-Soy Parish 2,000.00
Mary Immaculate Sisters of Nyeri 3,000.00
Sisters of Charity of the Immaculate Conception of IVREA
1,000.00
48
Apostolic Carmel-Moiben 2,000.00
Little Sisters of St. Francis-Eldoret 1,000.00
Sub-Total 31,050.00
Grand Total 3,670,783.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
1,835,391.00
MILITARY ORDINARIATEParish Kiasi
St. Charles Lwanga - Kahawa Garrison 139,330.00
St. Michael - 21 KR AMISOM 130,000.00
Holy Rosary - Embakasi 93,727.00
Our Lady of Star of the Sea -KN Mtongwe 68,300.00
Mother of Mercy 62,625.00
Saints Peter and Paul - DHQ CAU 61,300.00
St. Ignatius - 7KR AMISOM ( Busar) 56,600.00
St. Michael - AMISOM ( Dhobley) 50,000.00
7KR - AMISOM (Fafadun)
50,000.00
St. Joseph the Worker - Thika 45,650.00
Our Lady of Assumption - MAB 40,500.00
St. Augustine - DSC 37,700.00
St. Ignatius of Loyola - LAB 21,640.00
St. Monica - Moi Bks 21,410.00
Our Lady Queen of Victory - 3KR 13,990.00
St. Raphael - DFMH 13,450.00
St. Michael - 5KR 10,070.00
St. Benedict’s - Garissa Camp 10,000.00
St. Luke - Kenyatta Barracks 9,050.00
St. Peter - 4 Bde 8,150.00
St. Paul - KMA 7,200.00
St. Thomas Aquinas - Kabete 7,000.00
Our Lady of Mt. Carmel - Manda 5,500.00
Our Lady of Consolata - SOI 5,000.00
St. Francis of Assisi - 78 Tank Battalion 3,820.00
Sacred Heart of Jesus - 77 Arty 3,000.00
Jumla 975,012.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC 975,012.00
49
JIMBO LA HOMA BAYParokia Kiasi
Sacred Heart-Ang’iya 12,000
St. Theresa’s-Asumbi 123,000
St. Paul of theCross-Awendo 25,000
St. Paul’s Cathedral- Homa Bay 101,000
St. Thomas More- Isibania 83,830
St. Michael-Kadem 23,500
St. Theresa’s-Kakrigu 5,000
St. Gabriel Our Lady of Sorrows-Karungu
13,000
St. Charles Lwanga- Kebaroti 20,015
St. Mathias Mulumba-Kegonga 20,045
Our Lady Queen of Martyrs-Kehancha
40,000
Our Lady of Immaculate Conception-Kendu Bay
12,150
St. Mary’s-Mabera 28,900
Martyrs of Uganda-Macalder 30,000
St. Francis of Assisi-Mawego 25,000
Star of the Sea-Mbita 20,000
St. Linus-Mfangano 7,610
St. Joseph-Migori 63,000
St. John Mary Vianney- Mirogi 10,000
St. Peter and Paul-Ntimaru 12,300
St. Francis of Assisi-Nyagwethe 6,200
St. Arnold-Nyalienga 13,225
St. Mary’s-Nyarongi 2,500
Blessed Sacrament-Oriang 8,000
St. Celestino-Oruba 40,000
Holy Spirit-Osogo 20,000
St.Peter’s-Oyugis 84,000
Our Lady of Fatima-Rakwaro 11,800
St. Monica-Rapogi 39,150
St. Bernadette-Raruowa 11,000
St. Mary’s-Ringa 10,000
St. John-Rodi 20,000
Emmaus-Rongo 36,000
Christ the Good Shepherd-Sindo 13,500
St. Joseph-Tonga 10,000
St. Martin De Porres-Ulanda 23,500
St. Mary’s-Uriri 16,550
St. Andrew’s Wandiji 6,000
Institutions
Asumbi Girls’ National High School 33,000
St. Mary’s Girls School Mabera 10,180
St. John’s Minor Seminary-Rakwaro 2,100
St. Mary Gorrety Dede HighSchool-Rakwaro
8,000
St. Vincent Rongo Univerity Chaplaincy
7,250
St. Benedict Parochial Primary-Migori
10,250
St. Joseph Mukasa Mirogi Girls High School
10,000
St. Augustine Mirogi Boys’ High 10,000
St. Josephine Bakhita Girls’ School-Nyalienga
10,010
St. Stephen Angiro Mixed Secondary-Nyalienga
800
St. Augustine Achego Mixed School-Nyalienga
2,270
St. Paul’s Ligisa Boys’ Secondary-Nyalienga
1,600
St. Pauls Catholic Educational Centre-Homa Bay
2,000
Nyabera Girls’ School-Sindo 2,000
Moi Girls’ Secondary- Sindo 8,000
St. Mary’s Academy-Sindo 700
Ragwe Secondary-Sindo 1,000
Nyakia Secondary-Sindo 600
St. Paul Ageng’a Secondary-Macalder
3,000
50
St. Gemma Girls Sec. School - Macalder
3,300
YCS Moi Nyatike Boys-Macalder 1,800
St. Francis Kibuon Secondary-Macalder
1,000
St. Gabriel’s Godkwach-Macalder 1,050
St. Gabriel’s Primary-Macalder 2,650
St. Gorrety Mikei High School-Macalder
3,000
St. Jacob Kolanya Secondary-Macalder
1,100
St. Puis Got Orango Secondary-Macalder
500
St. Thomas Diruma Secondary-Macalder
1,000
St. Sabianus Owich Secondary-Macalder
500
St. Claudio Okenge Secondary-Macalder
1,500
Nyakweri Primary-Macalder 350
St. Peter’s Ofwanga Secondary-Rongo 4,000
Minyenga Secondary-Rongo 300
St. Joseph Tuk Jowi Girls’ Secondary-Rongo
3,000
Kangeso Secondary-Rongo 500
Nyagwethe Secondary 1,000
Obanga Secondary-Nyagwethe 2,000
Pini Franco Polytechnic-Nyagwethe 1,000
Mr. Pius O. Sakwenda’s family-Nyagwethe
350
YCS Obanga Secondary-Nyagwethe 300
St. Monica Devotional Group Nyagwethe
2,150
Catechist-Nyagwethe 820
St. Ann Devotinal Group-Nyagwethe 3,000
St. John’s Koyombe Secondary-Nyagwethe
500
Mr. Maurice Opinde’s family-Nyagwethe
500
Mr. Sabiano Otiwa’s family-Nyagwethe
400
CWA-Nyagwethe 1,000
Nyagwethe Primary School 1,200
Youth Group-Nyagwethe 700
Sikri TTI for the Blind andDeaf-Oyugis
10,000
Daughters of Our Lady of Holy Rosary Sisters-Oyugis
1,000
Brothers of OLM-Sikri community 1,000
Brothers of OLM-Oyugis community 1,000
Felician Sisters-Oyugis 2,000
St. Joseph Ombo Hospital 34,500
St. Joseph Rapogi Boys’ 17,615
Mawego TTI 1,720
St. Charles Lwanga Kebaroti Primary 2,000
St. Charles Lwanga Kebaroti Secondary
4,695
St. Cecilia Kebaroti Primary 3,185
Santa Lucia Kebaroti Academy 1,000
Nyabosongo Bena Academy-Kebaroti 3,015
St. Monica Remanyanki Primary 2,555
Fr. Scheffer Boy’s Primary Boarding School, Asumbi
10,000
St Joseph’s Boys 5,000
St Gabrielle Gwasi Girls 5,000
Jumla 1,319,235
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
598,217
51
JIMBO LA KAKAMEGAParokia Kiasi
St. Joseph’s Cathedral Kakamega 206,015
St. Peter’s Mumias 185,925
St. Joseph the Worker Shibuye 183,160
Christ the King Amalemba 162,470
All Holy Angels Lutonyi 155,915
St. Pius X Musoli 122,060
St. Augustine Eregi 120,000
St. Paul’s Ejinja 115,000
The Sacred Heart Mukumu
108,000
Our Lady of the Holy Rosary Shiseso
97,563
St. Agnes Mukulusu 95,445
St. Kizito Lusumu 82,574
St. Charles Lwanga Hambale 80,000
St. Marks Nzoia 75,000
Our Lady of Assumption Mau-tuma
71,550
St. Joseph’s Kongoni 70,400
Our Lady of the Assumption Shitoli
69,990
St. Paul’s Erusui 68,650
St. Joseph’s Luanda 67,333
Our Lady of the Immaculate Conception Chimoi
65,550
St. Anne Eshisiru 65,530
St. Theresa’s Malava 59,670
St. Caroli Lwanga Lutaso 56,260
St. Ursula Chamakanga 53,220
Our Lady of the Nativity Mutoma 50,000
St.Luke’s Bumini 47,325
St. Philip’s Mukomari 46,810
St. Mathias Mulumba Matunda 45,000
Holy Family Lubao 43,000
St. John the Baptist Likuyani
42,830
St. Xavier Shikoti 40,060
Holy Trinity Soy 35,307
Holy Spirit Bulimbo 35,190
St. Charles Lwanga Chekalini
33,500
Our Lady of Assumption Indan-galasia
21,800
Our Lady of Fatima Buyangu 15,440
Corpus Christi Irenji 15,240
St. Joseph’s Shirotsa 15,000
Holy Cross Emalindi 10,200
Our Lady of Consolata Bukaya 9,400
St. Patrick Lufumbo 8,640
Sub-Total 2,953,022
Taasisi Nyingine
Eregi TTC 3,000
MMUST Chaplaincy 71,757
Mukumu Hospital 8,200
Mumias CTC 10,200
Bishop’s House Mukumu 4,570
Sub-Total 97,727
Secondary schools
St. Gerald Injira 4,000
St. Elizabeth Bumia 5,000
St. Joseph Ortner Girls’ 10,000
St. Mary Goretti Shikoti Girls’ 59,265
St. John’s Shinoyi 6,300
St. Bonventure Shimanyiro 5,000
St. Francis Xavier Shikoti 10,800
St. Ursula Chamakanga 15,000
Our Lady of Nativity Mutoma 5,000
St. Teresa Bumini 3,850
St. Mary’s Mumias Girls 49,855
52
St. Peter’s Seminary 9,590
St. Angela Mumias School for the Deaf
24,700
St. Vincent Butende 7,100
St. John’s Museno 6,200
St. Dennis Munjiti 4,000
Eregi Girls’ 80,000
St. Peter’s Mumias Boys’ 28,500
St. Teresa Eshisenye Girls’ 1,500
St. Gerald Shianjero 7,000
St. Gabriel Isongo 8,400
St. Charles Lwanga Koromaiti 8,000
St. Beda’s Bukaya 12,300
St. Teresa’s Emukhuwa Girls’ 1,500
St. Clare’s Maragoli Girls’ 16,000
St. Francis Imalaba 6,700
St. Teresa Itete 23,400
St. Luke’s Lumakanda 23,500
Kaptik 8,000
Eshibinga 5,000
St. Monica Lubao 20,000
St. Anne’s Buyangu Girls’ 5,000
St. Augustine Roasterman 12,785
Malinya Girls’ 4,800
Holy Cross Injira 10,000
St. Joseph’s Shichinji 6,165
Kivaywa Boys’ 830
St. Francis Shipalo 4,000
St. Joseph’s Shirotsa 4,000
St. Anne’s Ikuywa 3,000
Holy Cross Emalindi 10,100
St. Joseph’s Malimili 3,000
St. Anne’s Musoli Girls’ 50,000
Musingu Boys 1,200
St. Mathias Kholera Boys 11,000
St. Monica Soy 2,300
St. Michael Kilimani 1,500
St. Charles Lwanga Mukumu 10,000
St. Bakhita Ebusiratsi 35,000
St. Clare’s Luanda 2,150
Holy Family Musembe 15,000
St. Joseph’s Kogo 7,300
St. Patrick’s Ikonyero 4,000
Eshisiru 6,330
Bulimbo Girls’ 25,000
St. Elizabeth Lureko 4,000
St. Ignatius Mukumu Boys’ 40,000
St. Agnes Shibuye Girls’ 60,000
St. Joseph’s Girls Kakamega 21,000
St. Anthony Kagoi 12,850
St. Francis Majengo 2,000
Bishop Sulumeti Lugari 32,920
St. Cecilia Lufumbo 5,000
St. Henry Saisi Girls’ 7,000
Saisi Girls’ 6,150
Bishop Njenga Girls’ 70,000
ACK Shinamwenyuli 650
St. Philip’s Mukomari grls 15,000
The Sacred Heart Mukumu Girls 154,000
St. Augustine Milimani 8,000
St. Mukasa Boys’ Chimoi 6,000
St. Mukasa Girls’ Chimoi 6,120
Immaculate Heart Lugari 9,000
St. Joseph’s Shirotsa 4,000
St. Benedict Lugulu 5,000
Holy Cross Sango Girls’ 5,400
St. Joseph’s Lukongo 3,755
St. Paul’s Emulakha 3,000
St. Joseph’s Lumino 3,000
St. Michael Kilimani 3,000
St. Teresa Mukunga 2,000
St. Joseph’s Nyorolis 6,000
St, Anne’s Nzoia Girls’ 25,000
St. Peter’s Moi’s Bridge 3,500
53
St. Benedict Mukoye 3,100
Sub-Total 1,236,365
Primary schools
Mirembe 2,000
St. Albert Shibuye 6,000
St.Angela Bulimbo 3,700
St. Michael Irenji 1,550
St. Gerald Injira 4,000
Lwanda 10,875
Trinity Academy 1,555
St. Peter’s Mautuma 2,300
Maraba 5,000
Kilagiru 2,365
Shikulu 2,000
St. Mary’s Shibuye 3,000
St. Mary’s Mukumu Girls 12,000
Moi’s Bridge Matunda 3,000
Sacred Heart Itenyi 2,600
Ebushibo 3,000
St. Christopher Malimili 4,850
St.Anne’s Mundulu 3,675
St. Michael Chemulele 1,210
Mary Immaculate 3,230
St. Mathew’s Bukhulunya 5,000
St. Christopher Enyapora 11,000
St. Emmanuel Masasuli 2,120
Chirobani Primary 1,330
St. Ursula Museno 4,000
Shikoti Mixed 1,700
Albartos 5,725
St. Angela Eregi 4,500
St. Kizito Shihingo 2,000
Shisenya 1,450
St. Mary Immaculate 400
St. Paul’s Shivakala 2,300
St. Paul’s Shibuye 2,000
St. Louis Mautuma 1,300
St. Mary’s Mautuma 4,000
Itubini 2,000
Shivakala 2,300
St. Kizito Bukusi 3,000
Baharini Pri. Chekalini 1,070
St. Patrick’s Sisokhe 4,335
Simboyi 1,160
Omunoywa 1,450
Adolph Ludiga 500
St. Francis Hambale 24,500
Munasio 1,200
St. Lawrence Ichina 1,400
St. Joseph’s Lusumu 3,000
St. Thomas Musoli Mixed 2,000
St. Peter’s Boys Mumias 25,150
Namelenge 4,520
Kholera 3,200
St. Clare’s Musoli 5,300
Imani Springs Academy 5,000
St. Augustine Lubao 3,000
Eregi Mixed 1,700
St. Gerald Sasala 5,000
St. Peter’s Matundu 2,850
Ebukuluti 1,000
St. Bernard Chamakanga 1,350
St. Patrick’s Mwilitsa 3,310
Sabane 1,775
St. Philip’s Mukomari 1,500
Shirotsa 2,200
Ivono 1,200
Notre Dame 3,000
Ikonyero 1,800
54
St. Anne’s Mumias 61,450
Chamakanga Special School 1,350
St. Peter’s Ebunayi 3,400
Sub-Total 313,705
Other institutions 97,727
Jumla 4,599,819
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
2,000,000.00
JIMBO LA KITALEParokia Kiasi
Christ the King 177,480.00
Immaculate 68,766.00
Kipsaina 68,300.00
Kibomet 48,000.00
Chepchina 43,400.00
Kwanza 43,000.00
Kachibora 42,055.00
Kiminini 40,400.00
Kaplamai 38,000.00
Sirende 35,290.00
Kapenguria 35,000.00
Endebess 34,000.00
Kolongolo 30,000.00
St. Joseph’s 30,000.00
Ortum 24,250.00
Mbara 18,000.00
Saboti 17,000.00
Chepnyal 15,450.00
St. Kizito Matisi 15,320.00
Tartar 15,000.00
Amakuriat 13,000.00
Makutano 12,800.00
Kacheliba 12,155.00
Chepareria 12,000.00
Kaptabuk 11,100.00
Suwerwa 11,000.00
Sina 7,185.00
Kabichbich 1,000.00
P’Sigor 600.00
Lomut -
Jumla 919,551.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
307,520.00
JIMBO LA BUNGOMAParokia Kiasi
Amukura 74,115.00
Buhuyi 67,000.00
Bukembe 80,000.00
Bungoma 862,000.00
Busia 127,370.00
Butula 46,250.00
Butunyi 170,000.00
Chakol 105,000.00
Chebukaka 32,500.00
Chelelemuk 40,000.00
55
Dahiro 71,950.00
Kabula 102,000.00
Kaptalelio 70,000.00
Kibabii 661,520.00
Kibuk 50,750.00
Kimatuni 220,000.00
Kimwanga 50,008.00
Kimilili 97,150.00
Kisoko 188,685.00
Kochoilia 80,000.00
Magombe 50,000.00
Misikhu 332,100.00
Mundika 93,505.00
Myanga 45,825.00
Naitiri 61,000.00
Nangina 150,000.00
Ndalu 65,000.00
Port Victoria 50,000.00
Samoya 72,460.00
Sikusi 46,000.00
Sirimba 51,405.00
Sirisia 55,000.00
Tongaren 160,020.00
Webuye 204,679.00
Institution
Sacred Heart-Wamalwa Kijana High School
12,000.00
St. Anne’s Kisoko Girls High School
51,545.00
Kisoko Girls Primary School 3,000.00
Little Sisters of St Francis-Kisoko Convent
3,600.00
St. Anne’s- Mukwa Secondary 5,000.00
Mukwa Primary School 1,400.00
Nalondo RC Primary School 1,800.00
St. Mary’s Kibabii High School 56,250.00
St. Mary’s Mundika Boys High 3,000.00
St. Mathias Secondary-Busia 2,000.00
St. Monica-Bukokholo Girls’ High 10,000.00
St. Anthony-Sirisia Secondary 3,000.00
St. Mary Immaculate Mayekwe Secondary
2,000.00
St. Paul-Lwandanyi Primary 2,000.00
St. Charles Kaptoboyi Secondary 500.00
St. Charles Kaptoboyi Primary 500.00
St. Joseph’s Kakala Primary 1,500.00
St. Joseph’s Chemses Primary 500.00
St. Cecelia -Nangina Girls Sec 85,000.00
St. Bennadete-Samoya Primary 2,500.00
St. Mary-Magadeline Siloba RC Secondary
3,000.00
St. Francis of Assisi-Wekelekha Primary
4,120.00
St. Mary-Magadeline Siloba RC Primary
2,150.00
St. Jude-Muanda RC Primary 1,000.00
St. Thomas-Samoya Secondary 6,070.00
St. Jude-Muanda RC Secondary 4,000.00
St. Agnes-Biliso Primary School 1,500.00
St. Elizabeth-Tulumba Primary 1,000.00
St. Antony-Walala Primary 2,000.00
Lwanya Girls Secondary School 10,000.00
Bwake RC Primary School 950.00
Bwake RC Secondary 2,700.00
Sirare RC Primary School 1,000.00
Sirare RC Secondary School 3,000.00
Luuya RC Primary School 1,400.00
Luuya Girls Secondary School 5,000.00
Lurende Secondary School 1,000.00
Lurende RC Primary School 1,000.00
Mabanga RC Primary School 3,755.00
St. Joseph’s-Nalondo Boys Second-ary
7,000.00
Nangili RC Primary School 2,000.00
St. Joseph’s-Nalondo Girls Sec 5,000.00
56
St. Christopher-Mabanga Girls Secondary
50,000.00
Bishop Phillip Anyolo- Kakamwe Secondary
6,300.00
Chebukwa Primary School 2,500.00
Bukusu Primary School 1,500.00
Khalaba Primary School 710.00
Kibabii Boys’ Primary School 3,000.00
Cardinal Otunga Girls’ Secondary 8,885.00
Chemwa Primary School 3,940.00
St. Jude-Lumasa Primary School 500.00
Namilkelo Primary School 2,000.00
Sango Primary School 2,200.00
Netima Primary School 1,200.00
Kabubero Primary School 2,400.00
Sikata Primary School 2,600.00
Namuninge Primary School 1,000.00
Bosio Primary School 5,000.00
Miluki Primary School 1,200.00
St. Paul’s-Miluki Girls’ Secondary 4,300.00
Chema Academy 18,125.00
Assumption Sisters-KibukConvent
1,500.00
St. Mary’s-Kibuk Girls’ Secondary 10,000.00
St. Agnes-Lapkei Primary School 4,000.00
St. Peter’s-Cheptoon Primary 500.00
St. Jude’s-Kaimugul Primary 1,000.00
St. John’s-Chepyuk Secondar 2,000.00
St. Teresa’s -Cheptoror Secondary 1,200.00
St. Martin’s-Chepyuk Primary 1,000.00
St. Peter’s-Cheptonon Secondary 2,000.00
St. Jude’s-Kaimugul Secondary 500.00
Tendet Primary School 500.00
Sacho Primary School 500.00
Nomorio Primary School 1,000.00
Kapkuseng Primary School 1,000.00
Kashock Primary School 1,000.00
St. Augustine Sec-Nomorio 1,000.00
Chebich Primary School 1,000.00
St. Peter’s-Cheromis Primary 1,000.00
Bumala RC Primary School 2,200.00
Makwara Primary School 200.00
St. Mary’s-Siribo Mixed Sec 5,000.00
St. Romano-Tingolo Mixed Sec 5,000.00
St. Romano-Primary School 1,500.00
Buhuyi Secondary School 3,360.00
Isongo Primary School 500.00
St. Mary’s-Okatekok Secondary School
3,200.00
St. Augustine-Nasira Secondary School
7,330.00
St. Joseph’s-Segero Secondary School
7,000.00
St. Mary Immaculate -Urban Secondary
7,000.00
St. Paul’s-Elwanikha Girls Sec 2,000.00
St. Mary-Assumpter Mabunge Secondary
1,000.00
St. Peter Khwirare Secondary 1,005.00
St. Charles Lwanga-Emukhuyu Secondary
1,500.00
St. Mary Buyofu Secondary School 2,175.00
St. Agather-Kajoro Primary-Kisoko
500.00
St. Martin-Special Sch-Kisoko 1,650.00
St. Charles Lwanga Emukhuyu Primary-Kisoko
1,700.00
St. Joseph’s Primary-Kisoko 9,000.00
St. John-Sibembe Primary-Kisoko 3,200.00
St. Francis-SegeroPrimary-Kisoko 5,400.00
St. Agnes Manyole-Primary 1,350.00
St. Mary Madibo Pri-Kisoko 2,000.00
St. Peter’s-Khulwanda Pri-Kisoko 250.00
St. Veronica- Indoli Pri -Kisoko 1,000.00
St. Peter’s-Nasira Primary-Kisoko 1,000.00
St. Francis-Makongeni Pri-Kisoko 1,570.00
57
St. Mary Assumpter Mabunge Primary-Kisoko
1,000.00
St. Joseph’s Buyofu Pri-Kisoko 760.00
St. Peter-Khwirale Primary-Kisoko 2,400.00
St. Paul-Elwanikha Pri-Kisoko 1,500.00
St. Alex-Sidende Primary-Kisoko 1,500.00
St. Teresa-Busidibu Primary-Kisoko
1,500.00
St. Peter’s-Sunshine Academy Okatekok
2,000.00
St. Philomena Academy Okatekok 1,100.00
St. Teresa Academy- Okatekok 500.00
St. Clare Academy- Madibo 500.00
St. Benedict Academy-Mungatsi
3,000.00
St. Monica-Chakol Girls Sec 11,620.00
St. Teresa-Chakol Girls Primary 10,000.00
St-Thomas-Chakol Boys Primary 8,110.00
St. John’s Alupe Secondary School 7,500.00
St. Joseph Chakol Secondary 5,255.00
St. Paul-Okokor Primary School 4,165.00
St. Lawrence-Ojaamong Primary 4,000.00
St. Paul-Olepito Primary School 3,800.00
St.Francis of Asis-Asing’e Sec 3,500.00
St. Mary-Otimong Primary 3,370.00
St. Saverio-Ong’aroi Primary 3,000.00
St. Marm-Among’ura Secondary School
3,000.00
Alupe University College 2,100.00
St. John Bosco Alomodoi Primary 2,000.00
St. Magadeline-Apegei Primary 1,730.00
St. Peter-Ojaamong Secondary 1,630.00
St. James-Omoloi Primary School 1,110.00
St. Francis of Assisi-Okame Sec 1,000.00
St. Festus-Ong’ariama Primary 1,000.00
St. John-Bosco-Alupe Primary 1,000.00
St. Magadeline-Ongorom Primary 1,000.00
Keriamata Primary School 850.00
St. Jude-Okerebwa Primary School 600.00
St. Karoli Goria Primary School 500.00
St. Anne-Okiporo Primary School 415.00
Akites Primary School 200.00
Ikonzo Secondary School 10,000.00
St. Austine Kingandole Secondary 5,500.00
St. Augustine Boys Butunyi 3,250.00
St. Kizito-Busire Primary 2,640.00
Immaculate Heart Bumala 2,000.00
St. Siomn Elunyiko Primary 2,000.00
St. John Bosco-Butunyi Mixed Pri 1,500.00
St. Jude-Khunyangu Primary 1,300.00
St. Joseph-Bumutiru Secondary 1,050.00
Namwitsula Primary School 1,020.00
St. Melitus Saka Primary School 1,000.00
Butunyi Vocational Training 1,000.00
St. Timothy Bumutiru Primary 1,000.00
Buriya Primary School 1,000.00
St. Teresa Neela Primary School 1,000.00
Kingandole Primary School 1,000.00
St. Lazaru -Ikonzo Primary 1,000.00
St. Christopher Emagombe Pri 1,000.00
St. Francis Masebula Secondary 1,000.00
Bishop Stam Secondary School 1,000.00
St. Michael Musoma Primary Sch 900.00
Burinda Primary School 500.00
St. Andrew Sikoma 500.00
Bukhwaku Primary School 500.00
Bumala Township 200.00
Our Lady of Assumption-Khacho-nge Girls
6,400.00
St. Emmanuel Miruri Secondary 1,500.00
Chebukaka Girls Primary School 2,250.00
Chebukaka Boys Primary School 2,800.00
Matibo RC Primary School 3,620.00
St. Thomas Aquinas Kitayi Pri 2,700.00
58
Maloho RC Primary School 2,150.00
Nabeki RC Primary School 800.00
Misiri Primary School 1,050.00
Our Lady of Peace-Chebukaka Primary School
5,000.00
St. Joseph Khachonge Primary 3,500.00
Sikimbio RC Primary School 1,500.00
KMTC Sichei 200.00
Sichei Primary School 600.00
St. Elizabeth-Lunao Secondary 18,000.00
Bishop Atundo-Kimaeti Secondary School
4,000.00
St. Peter’s Namaika Secondary l 2,210.00
St. Anthony-Tulukuyi Secondary 1,960.00
St. Stephen Secondary - Kimaeti 1,500.00
St. Joseph’s-Bukirimo Secondary 1,135.00
St. Jude-Napara Girls Secondary 98,600.00
Mt. Carmel Girls Secondary 10,000.00
Kibabii Diploma Teachers College 1,400.00
St. Peter’s-Namaika Primary 650.00
St. Denis-Libolina Special School 2,000.00
St. Stephen Primary-Brothers 1,650.00
St. Anthony- Tulukuyi Primary 1,200.00
Siloba Shine RC Primary School 1,000.00
Myanga RC Primary School 1,250.00
Kimaeti RC Primary School 2,420.00
St. Monica, Kamurumba Primary 2,000.00
Lunao Primary School 2,600.00
St. Stephen, Chiliba Secondary 2,700.00
St. Teresa, Girls High-Kimilili 3,000.00
St. Jan High School-Kimilili 1,200.00
St. Joseph Kamusinde High School-Kimilili
500.00
St. John High Buko-Kimilili
3,500.00
St. Luke Kimilili High School 20,000.00
St. John Buko Primary School 1,500.00
St. Joseph-Kimilili Primary 5,000.00
St. Benedict Primary-Kimilili 1,000.00
Our Lady of Lourdes Primary-Kimilili
1,000.00
St. Joseph’s-Kamusinde Primary 3,000.00
St. Antony-Matili Primary School 1,500.00
Farcon Academy-Kimilili 2,000.00
St. Anne, Royal Academy-Kimilili 1,000.00
Immaculate Academy-Kimilili 1,500.00
Ng’oli Primary-Kimilili 500.00
Ekisegere Primary School 1,700.00
St. Mary’s-Osajai Primary School 300.00
Koruruma Primary School 1,700.00
Kajei Primary School 500.00
Opeduru Primary School 1,000.00
Kapina Primary School 500.00
Akudiet Primary School 1,600.00
Malaba Township Primary School 2,750.00
Okuleu Primary School 700.00
Kasogol Kapel Primary School 1,750.00
Mother Kevin Primary School 22,000.00
Bungoma Prisons 1,200.00
St. Bridgid Nangwe Girls Secondary School
2,300.00
Buhuyi Primary School 4,000.00
Musibiriri Primary School 600.00
St. Ignatius-Esirisia 4,000.00
Bishop Sulumeti Girls Secondary 7,675.00
St. Martin SecondarySchool-Chelelemuk
1,300.00
St. Elizabeth, Kabukuri 2,000.00
St. Antony-Akabuit Girls Secondary School
1,500.00
St. Benard, Kakurikit 5,000.00
Kaejo Primary School 500.00
St. Anne, Kakapel Primary School 1,675.00
Kabukui Primary School 1,000.00
Kakurikiti Primary School 500.00
Kakameri Primary School 1,000.00
59
St. Luke Special School-Kakameri
1,400.00
Machakha Primary School 1,000.00
Mwari Primary School 2,000.00
Chelelemuk Girls Primary School 1,300.00
Chelelemuk Boys Primary School 1,250.00
St. Mathew Primary School 900.00
St. Charles-Okanya Samoya 1,200.00
Asiriam Primary School 1,000.00
St. Jude-Syoya Primary School 1,400.00
St. Paul-Wamunyiri Primary 1,700.00
St. Peter’s Mwiruti Primary l 2,000.00
St. Charles Lwanga Talitia Primary 950.00
St. Mary’s Mukhuma Primary 2,850.00
St. Peter’s Mwiruti Secondary 4,650.00
St. Joseph Secondary Sch-Bulondo 2,400.00
St. Ann Polytechnic-Bulondo 340.00
St. Mary Kamba Primary School 1,200.00
St. Jude Luyekhe Secondary School 580.00
St. Jude Luyekhe Primary School 1,305.00
ERSF Namwacha Secondary 1,000.00
St. Anne Wamumali Primary 1,500.00
St. Elizabeth Malinda Secondary 3,270.00
St. Elizabeth Malinda Primary 1,400.00
St. Mary Magadeline Secondary 2,000.00
St. Patrick Lukusi Primary School 800.00
St. Antony Naburereya Primary 500.00
St. Teresa Sang’alo Primary School 2,405.00
St. Paul Shiangwe Primary School 550.00
St. Paul Shiangwe Girls Secondary 1,190.00
St. Patrick Naitiri Secondary 2,000.00
St. Monica, Kamurumba 2,000.00
Tulukuyi RC Primary School 1,300.00
Napara RC Primary School 1,120.00
St. Stephen Chiliba Primary 1,000.00
Namaika RC Primary School 1,000.00
Sihilila RC Primary School 800.00
Siloba RC Primary School 1,000.00
St. Elizabeth BitoboSecondary 2,000.00
St. Anthony Tulukuyi Secondary 600.00
St. Elizabeth Lunao Secondary 16,620.00
St. Marys Mukhuma Secondary 10,000.00
St. Peters Sang’alo Secondary 5,000.00
St. Mary’s Kamba Secondary 2,000.00
St. Anne Sang’alo Institute 2,000.00
Apokor Primary School 1,000.00
Kochek Primary School 2,000.00
Katanyu Primary School 200.00
St. Peters Katanyu Secondary 800.00
Kamolo Primary School 1,600.00
St. Pius Secondary School 1,000.00
Kidera Primary School 500.00
Kamarinyang’ Primary School 770.00
Sidelewa Primary School 2,000.00
St. Jude Onyunyuri Secondary 600.00
St. James Kwang’amor Secondary 5,545.00
St. Patrick Kwang’amor Primary 1,500.00
Alexanda Papa Primary School 2,000.00
St. Michael Apatit 2,000.00
Lupida Primary School 1,000.00
Lupida Secondary School 3,200.00
St. Peter Tulienge 1,000.00
Akoret Primary School 1,450.00
Kamunuoit Primary School 700.00
St. Patrick Busibwabu 2,000.00
St. Teresa Busibwabu 1,500.00
St. Mary’s High School-Webuye 20,000.00
St. Mary’s Kibabii Girls Primary 5,500.00
St. Mary Magadeline Kimatuni Secondary
11,500.00
St. Anthony Mateka Secondary 4,800.00
St. Paul Lubunda Primary School 3,100.00
St. Mary Magadeline Kimatuni Primary
3,010.00
60
St. Mary Namatotoa Primary 3,000.00
St. Teresa Tabuti/Sudi Primary 2,700.00
St. Stephen Buloosi Primary 2,450.00
St. Mary Namatotoa Secondary 2,300.00
St. Joseph’s Lumboka Seconadry 2,000.00
St.Peter’s Syekumulo Secondary 2,000.00
St. Veronica-Masuno Primary School-Kisoko
1,300.00
Mungore Girls Secondary School 1,210.00
St. Joseph’s Lumboka Primary 1,100.00
St. Jude Namanze Primary School 1,100.00
St. Bartholomayo, Burangasi Primary School
1,000.00
St. Wilfrida Mulukoba Primary 1,000.00
St. John Nakholo Primary School 600.00
St. Aquinas Mateka Preparatory 500.00
St. Peter’s Syekumulo Primary 500.00
Our Lady of Mercy, Chebukaka Girls
20,000.00
St. Joseph’s Primary School-Busia 22,655.00
St. Andrew Bulanda Primary 10,120.00
St. Teresa Primary School-Busia 9,100.00
Our Lady of Mercy Secondary School-Busia
8,000.00
St. Mary ECD/Hostel-Busia 8,000.00
St. John the Baptist Mabale Secondary School
5,300.00
St. Benardette Ojamii 2,455.00
St. Rose Mabale Busia Primary 3,100.00
St. Paul Amerikwai Primary 2,000.00
St. Luke Amoni Primary School 1,550.00
St. Peter’s Bwamani Primary 350.00
St. Anne’s Institute of Science & Technology
2,000.00
St. Mary’s Kamba Secondary 800.00
St. Peter’s Secondary School 5,000.00
St. Martin Primary -Mwibale 1,000.00
St. Martin Secondary -Mwibale 17,000.00
St. Sarah Namisi Secondary School 1,450.00
Chesito Primary School 285.00
Kaptalelio Secondary School 1,000.00
Kaptalelio Primary School 1,300.00
Kongit Secondary School 2,050.00
Kongit Primary School 2,700.00
Chesito Secondary School 515.00
St. Peter’s Nakalira Secondary 10,000.00
St. Thomas Boys Secondary School-Misikhu
14,450.00
Holy Family Misikhu Primary 10,000.00
Holy Family Misikhu ECDE 2,060.00
Sacred Heart Misikhu Primary 7,500.00
Makemo Primary School 1,000.00
St. Francis Makemo Secondary 7,000.00
St. Stephen Bugwanga Primary 2,400.00
St. Michael Namable Secondary 500.00
St. Agnes Bunyala Girls Secondary 26,000.00
St. Peter’s Makunda Secondary 3,000.00
St. Henry Rugunga Primary 2,000.00
St.Joseph’s Busagwa Primary 3,185.00
St. Nicholas Mundika “B” Primary 2,000.00
St. Margaret Mubwaya Primary 1,000.00
St. John Machakha Secondary 2,000.00
St. Peter’s Buyosi 4,600.00
Lung’a Primary School 1,620.00
St. Jude Mundika Boys Primary 1,600.00
Mundika Girls’ Primary School 1,685.00
Grace & Compassion Primary 800.00
Igero Primary School 700.00
Igero Secondary School 3,000.00
Buyende Primary School 900.00
Buyende Secondary School 800.00
Mujuru Primary School 1,000.00
Mujuru Secondary School 1,050.00
Bukalama Primary School 3,000.00
Murende Secondary School 2,000.00
61
Murende Primary School 5,500.00
St. John Montessori 1,000.00
Maina PAG Primary School 1,430.00
St. Mary’s Mabusi RC Primary 370.00
St. Paul’s Mbirira Primary School 2,200.00
St. Anne Siangalamwe Primary 1,700.00
St. Elizabeth Binyenya Primary 500.00
St. Mary’s Narati RC Primary 450.00
St. Mary’s Mwikhupo Secondary 1,500.00
Bishop Atundo Girls Mabusi 9,030.00
St. Joseph’s Binyenya Secondary 1,500.00
Tongaren Mixed DEB Secondary 2,800.00
St. Augustine Lukhuna Girls’ Sec 13,000.00
St. Anne’s Siangalamwe Secondary 3,000.00
Tongaren Vocational Training Centre
740.00
St. Teresa Kabula Secondary 20,000.00
St. Monica Mungeti \Primary 3,000.00
Buema Primary School 1,500.00
St. Louis Butula Boys High School 10,000.00
St. Clare Butula Girls Secondary 5,000.00
St. Mary Butula Girls Primary 5,050.00
St. Joseph Butula Boys Primary 1,000.00
St. Catherine Special School 3,650.00
St. Paul Bukhuma Mixed Secondary
5,000.00
Madola Primary School 2,200.00
Bwaliro Primary School 500.00
Masendebale Primary School 1,500.00
Elukhari Primary School 500.00
Bwaliro Girls Secondary School 500.00
Bukati Primary School 1,000.00
Mung’abo Primary School 500.00
Enakaywa Primary School 500.00
St. Mary’s Butula Hostel 1,000.00
St. Peter’s Bumala ‘B’ Mixed Secondary
7,500.00
St. Joseph Bunambobi RC Primary 10,521.00
St. Monica Mukuyuni RC Primary 4,600.00
Lwanja RC Primary School 3,140.00
St. Kizito Mayanja RC Primary 1,850.00
Kimwanga RC Primary School 3,365.00
St. Jude Nabuyeywe RC Primary 3,000.00
St. Veronica Tunya Primary School 1,000.00
Khasolo RC Primary School 1,480.00
Nangata RC Primary School 900.00
Nakalira RC Primary School 800.00
St. Peter Siboti RC Primary School 500.00
Tabala RC Primary School 600.00
Kimwanga School for the Deaf 500.00
Nakhwana RC Primary School 500.00
Carmel View Pre-Primary & Primary School
10,000.00
St. Kizito Mayanja Secondary 15,000.00
St. Peter Siboti Secondary School 5,300.00
St. Paul Bunambobi Sec 1,400.00
St. Michael Nakhwana Secondary 1,000.00
Musakasa Technical Training Institute
3,100.00
Apostolic Carmel Sisters-Kimwanga
10,000.00
Our Lady of Mercy-Busia 10,000.00
St. Maurice Namboko Secondary 1,120.00
Eluuya Friends 2,000.00
St. Angela Academy Primary School Webuye
7,131.00
St. John Primary Lutungu Webuye 320.00
St. John Sec. Lutungu Webuye 1,180.00
St. Monica Primary School Murumba, Webuye
500.00
St. John the Baptist Convent Webuye
2,000.00
St. Jude Syoya Secondary Kabula 2,000.00
St. Antony Naburereya Sec, Kabula 25,000.00
Jumla 6,306,574.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
2,800,000.00
62
JIMBO LA NGONG’Parokia Kiasi
Abosi 10,000
Embulbul 126,870
Enoosupukia 5,650
Entasekera
Ewuaso Kedong 16,015
Fatima 184,150
Kajiado 28,874
Kandisi 10,000
Kibiko
Kilgoris 7,500
Kiserian 93,738
Kisaju 16,310
Lemek 31,200
Lenkisem 7,067
Lolgorien
Loitokitok 49,650
Magadi 11,200
Mashuru
Matasia 53,863
Mulot 40,680
Nairegia Enkare 23,000
Namanga 15,204
Narosura 15,000
St Joseph Cathedral 90,000
Nkoroi 172,800
Noonkopir 80,000
Ololkirikirai 30,000
Ongata Rongai 144,423
Ololulunga 19,000
Rombo
Sultan Hamud 15,000
St Joseph HBVM Narok
St Peter Narok 82,977
Kimana-Christ the King 36,686
Olokurto-St James
Bishop’s office
Jumla 1,455,400
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
606,831.00
JIMBO LA MARSABITParokia Kiasi
Dirib Gombo 15,000.00
Illeret 1,411.00
Karare 26,060.00
Kargi 8,050.00
Korr 45,590.00
Laisamis 18,650.00
Loiyangallani 66,150.00
Maikona 25,000.00
Marsabit Cathedral 70,215.00
Moyale 64,000.00
North Horr 14,850.00
Dukana 14,200.00
Kalacha 18,000.00
Logologo 11,875.00
Jumla 399,051.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
399,051.00
Kiasi remitted to the CJPC
63
JIMBO LA MALINDIParish/ Institution/ Office Kiasi (Kshs.)
Christ the Sower Parish, Mpeketoni
164,820
St. Francis Xavier’s Parish, Kisumu Ndogo
160,800
St. John the Evangelist, Hindi 135,390
St. John’s Parish, Watamu 134,170
St. Mary’s Assumption Parish, Hongwe
75,770
St. Anthony’s Cathedral Parish, Malindi
74,387
St. Paul’s Parish, Gongoni 70,405
St. Charles Lwanga’s Parish, Muyeye
55,580
St. Joseph Freinademetz Parish, Witu/ Kipini
36,200
St. Francis of Assisi Parish, Baharini
34,500
Mary Mother of Jesus Parish, Lamu
28,290
St. Joseph the Worker Parish, Wema
24,050
St. Catherine’s Parish, Tarasaa 21,290
St. Joseph the Worker Parish, Marafa
20,730
St. Mary Helper of Christians Parish, Lango Baya
20,240
Sacred Heart of Jesus Parish, Garsen
18,150
St. Mary’s Parish, Msabaha 17,370
St. Michael’s Catholic Mission, Mida
7,310
Catholic Mission, Mere 6,135
Our Lady of the Holy Rosary Mission, \Chakama
5,000
Blessed Joseph Allamano Mis-sion, Adu
2,800
Bishop’s House, Emmaus
6,000
Pope Francis Rescue Home Staff
3,550
CJPC Malindi Staff and Friends 2,350
Jumla 1,125,287
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
300,000
RELIGIOUS SUPERIORS CONFERENCE OF KENYACongregations Kiasi (Kshs)
Holy Cross Congregation 25,000.00
St. Bridget (Capuchin) 21,210.00
Order of St. Augustine Friars 20,000.00
Consolata Missionaries 20,000.00
Foreign Mission Society of Quebec
18,000.00
Xaverian Brothers 10,000.00
Kiltegan Fathers 10,000.00
Mont Fort Fathers 10,000.00
Camilians/Servants of the Sick 8,000.00
The Marianist 7,500.00
Hospitalar Order of St. John Brothers
5,000.00
Missionaries of The Poor 5,000.00
Society of Africa Missions (SMA)
5,000.00
Redemptorist Fathers 5,000.00
Sacred Heart Brothers 5,000.00
Canosian Fathers 2,000.00
CMM Brothers 2,000.00
Missionaries of Charity Brothers
2,000.00
Jumla 180,710.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC
50,000.00
64
ST.MATTHIAS MULUMBA SENIOR SEMINARY
ST.MARY’S SENIOR SEMINARY, MOLO
ADMINISTRATION POLICE SERVICE
KENYA WILDLIFE POLICE SERVICE
ST. THOMAS AQUINAS SENIOR SEMINARY
KISII UNIVERSITY
St.Matthias Mulumba Senior Seminary 13,420.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC 13,420.00
St.Mary's Senior Seminary, Molo 15,880.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC 15,880.00
Administration Police Service 42,000.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC 42,000.00
Kenya Wildlife Police Service 13,500.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC 13,500.00
St. Thomas Aquinas Senior Seminary 25,000.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC 25,000.00
Kisii University 12,500.00
Fungu lililopewa afisi ya kitaifa ya CJPC 12,500.00