Fasihi Andishi . Kf 202 Notes Zote 2
-
Upload
okatchlosh -
Category
Documents
-
view
560 -
download
32
description
Transcript of Fasihi Andishi . Kf 202 Notes Zote 2
-
1
FASIHI ANDISHI
ONYO KALI: HIZI NOTISI ZIMECHUKULIWA KATIKA MIHADHALA YA MWALIMU WA KF 202 NA SIYO NAKALA YAKE. NIMEZIANDIKA KATIKA MIHADHALA. KOSA LOLOTE LA NOTISI
HIZI LISIELEKEZWE KWA MWALIMU WA SOMO BALI KWANGU LABDA KAMA NILIKOSEA
KUANDIKA. KAMA UMEZIKUBALI USIWE MCHOYO NIPIGIE KWA 0786684062
__________________________________________________________________
I. USHAIRI
Kuna mitazamo ya aina mbili katika kuelezea dhana ya
ushairi. kuna wanamapokeo na mamboleo. Hata hivyo kabla ya
kuendelea zaidi kuwachambua tuangalie wataalam mbalimbali
wanavyofasili dhana hii . Dhana ya ushairi imejadiliwa na
wataalamu mbalimbali huku kila mmoja akitoa fasili yake.
Baadhi ya wataalam hao ni kama ifuatavyo:
MAPOKEO
Mssamba, (2003) akimnukuu Shaban Robert, anasema;
ushairi ni sanaa ya vina inayopambanuliwa kama nyimbo, mashairi na tenzi zaidi ya kuwa na sanaa ya vina ushairi
unaufasaha wa maneno machache au muhtasari.
Mnyampala (1970) anasema kuwa ushairi ni msingi wa maneno ya hekima tangu kale ndicho kitu kilichobora sana
maongozo ya Dunia kwa kutumia maneno ya mkato na lugha
nzito yenye kunata iliyopangwa kwa urari wa mizani na vina
maalum.
Amri Abeid (1954:1) anasema kuwa ushairi au utenzi ni wimbo, hivyo kama shairi haliimbiki halina maana.
-
2
Abdulatifu anasema kwamba ushairi ni ule ulio na sifa ya
ulinganifu wa vina na mizani, lugha laini (lugha tamu) na lugha
hii iweze kugusa moja kama ilivyokusudiwa.
Encyclopedia American (EA) inaeleza kuwa ushairi ni kauli
zenye hisia na ubunifu, mpangilio fulani wenye urari,
uwasilishaji wa tajiriba au mawazo ya mtunzi kwa maana
ambayo huibua tajiriba kama hiyo katika nyayo za wasomaji au
wasikilizaji na kutumia lugha ya picha yenye wizani wa sauti.
MAMBOLEO
Kezilahabi ( )anasema kuwa ushairi ni tukio hai au wazo ambalo limeonywa kwetu kutokana na upangaji uzuri wa
maneno fasaha yenye mizani Fulani ili kuonyesha ukweli
Topan (1996) anasema kuwa shairi ni unaoeleza hisia za ndani za binadamu kwa mpangilio Fulani wa maneno hivyo kwa mujibu wa Topan ushairi lazima uguse hisia za ndani ya moyo
wa binadamu.
Njogu na Chimerah (1999) wanasema ushairi ni sanaa ya lugha inayoeleza jambo kwa njia ya mkato na kwa namna
inavyoteka hisia za msomaji au msikilizaji
Mulokozi na Kahigi (1982:25) wanasema ushairi ni sanaa inayopambanuliwa kwa mpangilio maalum na fasaha na wenye
muwala, kwa lugha ya picha, sitiari au ishara katika usemi,
maandishi au mahadhi ya wimbo ili kuleta wazo au mawazo,
kufunza au kueleza tukio au hisia fulani kuhusu maisha au
mazingira ya binadamu kwa njia inayogusa moyo.
Hivyo basi tunaweza kusema kuwa ushairi ni kazi ya sanaa
yenye kuandikwa au kuimbwa kwa kufuata kanuni za ushairi au
-
3
kutofuata kanuni za ushairi ikiwa na maana kuwa ushairi
waweza kuwa wa kimapokeo au wa kisasa ilimradi ushairi huo
uwe na ujumbe.
Katika ushairi FANI na MAUDHUI ni muhimu sana, mawazo
fikra au sihi za ndani ni vitu muhimu sana katika ushairi
CHANZO/CHIMBUKO LA USHAIRI
Dhana ya chimbuko inafasiliwa na TUKI (2004) kuwa ni
mwazo au asili ya kitu.
Baadhi ya wataalamu wameweza kuelezea chimbuko la
ushairi wa Kiswahili kwa kuzingatia mitazamo au nadharia
mbili ambazo ni kama ifuatavyo:
1. Nadharia ya kwanza inadai kuwa; Chimbuko la ushairi wa Kiswahili ulitokana na ujio wa Waarabu.
2. Na nadharia ya pili inasema kuwa; Chimbuko la ushairi wa Kiswahili ni zao la jamii ya waswahili
wenyewe.
Hapa tunaenda kuzielezea nadharia hizi kila moja na kujaribu
kuona ubora wake na udhaifu wake katika kuelezea chimbuko la
ushairi
1.Na nadharia ya pili inasema kuwa; Chimbuko la ushairi wa
Kiswahili ni zao la jamii ya waswahili wenyewe.
Kwa kuanza na Lyndon (1962) Swahili Poetry anatoa hoja tatu ambazo ni:
ushairi wa Kiswahili umetokana na Uislamu,
ushairi ulianzia kwenye upwa wa kaskazini mwa Kenya hususani Lamu.
-
4
Na maudhui ya ushairi wa Kiswahili yalitokana na ushairi wa Kiarabu. Utungo wa kwanza wa ushairi
andishi wa Kiswahili ni Tambuka, Mwengo bin
Athmani (1728)
Ubora wa Nadharia hii
Ubora wa nadharia hii au mtazamo wa Harries kuhusu chimbuko la ushairi wa Kiswahili ni kwamba umesaidia
wengine kuendelea kuchunguza zaidi kuhusu chimbuko la
ushairi wa Kiswahili.
Udhaifu wa nadharia hii
Udhaifu wa nadharia hii ni kuwa si kweli kwamba ushairi wa Kiswahili uliletwa na Uislamu bali ulikuwepo hata kabla
ya ujio wa Uislamu, kwani ushairi hautenganishwi na
jamii husika. Hivyo jamii za waswahili walitumia Nyanja
mbalimbali za ushairi katika shughuli zao mbalimbali au
shughuli zao za kila siku, kama vile; shughuli za kilimo na
ufugaji.
Pia ushairi wa Kiswahili ulianza karne ya 10BK na ushairi wa Kiswahili ulikuwa ukitungwa na kughanwa kwa ghibu
bila kuandikwa. Wataalam wengi wanakubaliana kuwa
asili ya ushairi wa Kiswahili ni tungo simulizi hasa ngoma
na nyimbo.
Udhaifu mwingine katika mtazamo wake wa kusema kuwa ushairi ulianzia pwani ya kaskazini ya Kenya si kweli kwa
kuwa waswahili walikuwepo hata sehemu nyingine kama
vile Kilwa na Bagamoyo ambapo ushairi wa Kiswahili
ulitumika.
-
5
Hoja ya kusema ushairi wa Kiswahili ulitokana na Kiarabu haina mashiko kwa kuwa waswahili walikuwepo hata
kabla ya waarabu na walikuwa na ushairi wao isipokuwa
ujio wao ulileta athari kubwa kwa kuwa ulichanganya na
mambo ya dini ya kiislamu na hati.
Knappert (1979) Four centuries of Swahili verse anasema; Ushairi wa Kiswahili ulichipuka kwenye upwa wa Kenya kutokana na nyimbo na ngoma za waswahili na ulianza katika
karne ya 17 na pia ni ushairi wa Kiislamu wenye kuchanganya
sifa za tungo za kiafrika na za kiajemi.
Ubora wa hoja hii ni kwamba, ni kweli Knappert amekubali
kuwa,ushairi wa Kiswahili ulitokana na waswahili wenyewe.
Hata hivyo hoja yake ina udhaifu kwa kuwa ushairi wa
Kiswahili ulianza kabla ya karne ya 10 BK na pia amejikita
katika maudhui ya mambo mengine kama vile siasa, uchumi na
kijamii. Vilevile amechanganya chimbuko la ushairi wa
Kiswahili na Uarabu.
2. Nadharia ya pili inasema kuwa ushairi ni zao la waswahili
wenyewe.
Nadharia hii imejadiliwa na wataalam mbalimbali akiwemo
Shaban Robert, Jumanne Mayoka (1993) na Senkoro, Mulokozi
na Sengo.
Jumanne, M. Mayoka (1993) anasema ushairi umetokana na
jamii ya wanadamu wenyewe na umesheheneza ukwasi mkubwa
wa lugha ambayo imekuwa ikitumika katika hatua zote za
kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni katika historia ambayo
mwanadamu amepitia, Kwa mfano kuwa msamiati uliotumika
tangu enzi za kuishi mapangoni, enzi za uwindaji, ujima,
-
6
utumwa, vita vya makabila, uvamizi wa wageni, ukoloni na
harakati za kupambana na ukoloni hadi kupata uhuru na
maendeleo yake.
Ubora wa hoja
Ubora wa hoja hii ni kwamba ina mashiko ndani yake kwa
sababu, kila jamii ina sanaa yake na ushairi ni moja kati ya
sanaa hizo ingawa inaweza ikaathiriwa na sanaa ya jamii
nyingine. Pia ushairi umekuwa ukikua na kuendelea kadri jamii
inavyokuwa na kuendelea.
Udhaifu wa hoja.
Udhaifu wa hoja hii ni kwamba si kweli kuwa katika kipindi
hicho ushairi ulikuwa tayari umesheheni ukwasi mkubwa wa
lugha, na kama ulikuwa kweli umesheheni huu ukwasi wa lugha
alipaswa kutuonesha huo utajiri wa lugha anaouzungumzia
katika ushairi.
Senkoro (1988) anasema kuwa ushairi uliibuka pale lugha
ilipoanza katika kipindi cha uhayawani (kipindi ambacho
mwanadamu alipoanza kupambana na mazingira yake) kwenda
katika kipindi cha urazini (maana) ili kumwezesha binadamu na
mazingira yake kwa mfano, zana za kazi zilizotumika
ziliwafanya waimbe kwa kufuata mdundo wa zana hizo.
Masamba anasema kwamba kimsingi chimbuko la ushairi wa
Kiswahili ni waswahili wenyewe katika nyimbo, ngoma nk
ambazo ziliimbwa katika masuala ya kilimo, jando na unyago
n.k. Massamba anaendelea kusema kwamba nyimbo hizi
zilikuwa zikiimbwa bila kufuata vina na mizani lakini kwa kadri
muda ulivyoenda walizidi kuziendeleza na kuziboresha. Hivyo
-
7
suala la vina na mizani lililetwa na wageni sio kiini cha ushairi
wa kiswahili
Mulokozi fasili ya fasihi haiwezi kutenganishwa na utamaduni
wa maisha ya watu. Anaelezea kuwa ushairi wa Kiswahili
hutumia lugha ya Kiswahili, hivyo ili kujua chimbuko la ushairi
wa Kiswahili ni lazima ujue juu ya waswahili wenyewe
Pamoja na kuwa nadharia hii imeonesha kukubalika na
wataalamu mbalimbali kama vile Senkoro, Mayoka na Shekhe
Amri Abeid, lakini bado ina mapungufu. Hii ni kwa sababu
imeshindwa kuonesha muda maalumu ambapo ushairi wa
Kiswahili ulianza na ni wapi ulianza kutumika. Hili ni suala
ambalo linaumiza vichwa vya wataalamu mbalimbali hadi hivi
sasa, kwani hakuna mtaalamu yoyote aliyefanikiwa kuonesha ni
wapi na ni lini ushairi wa Kiswahili ulianza.
Hivyo basi, kutokana na nadharia hizo mbili tunaungana na
nadharia inayosema kuwa, chimbuko la ushairi wa Kiswahili ni
zao la waswahili wenyewe, kwa sababu waswahili wana
utamaduni wao ambao ulikuwepo kabla ya ujio wa Waarabu. Na
waliutumia ushairi huo katika shughuli mbalimbali za kijamii,
kwa mfano katika harusi, jando na unyago.
AINA ZA USHAIRI/BAHARI ZA USHAIRI
Kwa ujumla ushairi upo katika makundi mbalimbali. Uainishaji
wa ushairi unategemea wataalam. Mlokozi (1996) anadai kuna
bahari 13 za ushairi ambazo kwa mujibu wa tapo la wataalamu
wa Mombassa
1. Wimbo/Tathilitha
-
8
Shairi la aina ya wimbo lina mishororo 3 inayoweza kuwa na mikondo tofauti, unaweza kuwa na kina kimoja
mwishoni
Mara nyingi wimbo huwa na vipande viwili 2. Shairi/Tarbia
Utungo ambao una mishororo 4 katika kila beti na kila mshororo una vipande 2
Shairi huweza kuwa na maudhui ya namna yoyote ile 3. Utenzi/utendi
Ni ushairi wenye mizani michache kuliko 12
Una vina vinavyobadilikabadilika isipokuwa cha mwisho
Kwa kawaida husimulia visa virefu vya kihistoria.mfn vita nk
4. Zivindo
Ni shairi linalofafanua maana ya maneno
Lengo kuu ni kufunza lugha. Mfn shairi la Kihindi. 5. Tumbuizo
Hauna idadi kamili ya mizani na mishororo
Nia yake ni kutoa hisia ambazo zimembana mtu. Mfn Mbolezi-nyimbo za misibani, nyimbo za kubembelezea
watoto
6. Hamziyya
Una mishororo miwili miwili na vina vyake viko mwisho tu wa beti
Ulitungwa na Sharif Aidarus bin Uthman
Ulikuwa ni wa kumsifu mtume Mohamadi S.W.A 7. Dura Mandhuma au Inkishafi
Unatokana na utenzi wa mtu aliyeitwa Inkishafi
Una mambo ya kuonya, kufuata mambo ya kidini na kuelekeza
-
9
8. Ukawafi
Una mstari mmoja wenye vipande vitatu
Ukwapi-silabi 6
Utao-silabi 4
Mwandamizi 5
Zinahusu maudhui ya kidini 9. Wajiwaji
Ni utungo ambao una mishororo 5 kila ubeti wenye mizani 5
Zinahusiana na mambo ya kidini, kumsifu mtu shujaa na bingwa
10. Wawe au Vave
Asili yake ni kaskazini ya mwambao wa Pwani hasa sehemu za Amu na Pate
Unahusu kilimo, ziliimbwa wakati wa kufyeka mistu, kuchoma pori nk
11. Kimai
Ni utungo unaohusu mambo ya baharini au wakati wavuvi wanapomtafuta mwenzao ambaye amepotea
Ni utungo unaohusu ubaharia
Idadi ya mizani hubadilika badilika na vina si vya lazima 12. Ngonjera
ni mazungumzo au mabishano ya kishairi kuhusu mada Fulani
huundwa kwa kulumbana pande mbili
suluhisho la kile kinachojadiliwa hupatikana mwishoni 13. Kikwamba
Ni utungo ambao neno moja hutumiwa kila mwanzo wa ubeti na neno hilo hufululizwa na mabadiliko
mbalimbali.
-
10
MABADILIKO NA MAENDELEO YA USHAIRI
WA KISWAHILI
MAENDELEO YA KIHISTORIA:
Wataalamu ambao wanajaribu kutupa taarifa kuhusu maendeleo ya ushairi wa Kiswahili ni pamoja na M.M.
Mulokozi (1996) ambaye anatuambia kwamba ulianza
karne ya 10BK
Katika kipindi hiki hakukuwa na ushairi ambao ulikuwa umeandikwa kwa utamaduni wa Waswahili bali kulikuwa
na ushairi simulizi uliganwa kwa ghibu
Kuanzia miaka ya 1000BK wakati wa ukoloni kulitokea athari kubwa katika ushairi wa Kiswahili k.v hati ya
maandishi na dini ya kiislamu
Ushari uliwaunganisha Waswahili na duni pana ya umma na taaluma ya uandishi kwa hati ya Kiarabu uliwapa
wenyeji ujuzi wa kusoma na tabia ya kuandika
1000-1500BK
Katika kipindi hiki kulikuwa na ustawi na ustaarabu wa kimji wa waswahili katika miji yote ya Pwani na
biashara ilistawi kati ya wageni na wenyeji
Katika kipindi hiki fasihi pia ilistawi Mashujaa wanaosimuliwa katika tendi k.v Fumo Lyongo
waliishi kipindi hiki
Ushairi uliendelea kuwa simulizi Ushairi wa mwanzo uliitwa SWIFA
1500-1750BK
-
11
Hiki ni kipindi cha tatu na kilikuwa kipindi cha misukosuko ya wenyeji na Wareno
Kulikuwa na tungo zilizohidhiwa zilizowahusu Wareno, Migeni, Poatugei afila
Tungo nyingine zilikuwa ni utendi wa Hamziyya, Siri Lasinari, Utendi wa Tambuka 1723 nyingi zilikuwa
zikiwapa moyo Waswahili
Waswahili walifanikiwa kuwaondoa wareno.
1750-1900
Hiki kilikuwa ni kipindi cha nne, na kilikuwa ni kipindi cha utawala wa Waarabu
Kulikuwa na migogoro mingi ya kivita katika utawala wa Waarabu
Tabia za Mamwinyi, wafanya biashara, matajiri na wamisionari vilistawi
Kipindi hiki kilitawaliwa na fasihi ya kidini ambayo ilitafakari theologia na falsafa ya maisha
Kulikuwa na tendi nyingi zilizoibuka kuko Arabuni wakati wa mtume Muhamed. Mfn Shutaki, Angamia, Nakaa,
Masahibu nk
Pia kulikuwa na tungo za kitamaduni, mawaidha na tumbuizo. Mfn utendi wa Mwanakupona
Washairi walijitokeza kuhusu mashairi ya kisiasa ambao ni Myaka bin Haji (1776-1840), huyu aliishi Mombassa.
KARNE YA ISHIRINI (20)
-
12
Katika kipindi hiki uchapishaji wa magazeti na vitabu ulijitokeza. Kulikuwa na Asasi za kudai uhuru. Waandishi
waliandika sana kuhusu kudai uhuru. Mfn Saada Kandoro
Baada ya uhuru ushairi wa kisiasa ulienea zaidi kama vile Ngonjera na makue.
MAJARIBIO NA MABADILIKO KATIKA USHAIRI
WA KISWAHILI
Senko ( ) anasema baada ya fahamu zake kufunguliwa alianza
kuangalia mabadiliko katika ushairi.alidai kuwa kuwa kuwa
dunia inabadilika hivyo na ushairi hauna budi kubadilika.
Wangai Mwai (2008:73) fasihi hubadilika badilika katika kumbo na maudhui kwa hiyo ushairi wa Kiswahili sharti
uruhusu mabadiliko yanapotokea.
MGOGORO WA USHAIRI WA KISWAHILI
Baadhi ya washairi kama vile E.Kezilahabi, M.M Mulokozi, K.K Kahigi na wengineo walinza kuandika kazi
za ushairi zisizo na urari wa vina na mizani
Wengi walichukulia na kurudi nyuma kwa ushairi lakini waandishi hao waliona ni hatua ya maendeleo
Hivyo mashairi yaliyotungwa kwa mfumo huo yalipata majina mbalimbali kama vile Makue, Mtiririko, Mapingiti.
Nk
Na hivyo watungaji wa mashairi haya waliwaita wanamapinduzi na wengine wakawaita wachochezi
Ibrahim Noor Shariff (1988:183) amedai kuwa mzozo uliibuka pale wanamabadiliko walipodai mambo matatu:
1) Mbinu za kutunga mashairi zilikuwa chache mno
-
13
2) Sharia za kutunga mashairi ziliwanyima uhuru wa kutunga
3) Muundo wa tungo za kishairi uliokuwa wa Kiswahili hapo awali haukuwa na vina wala mizani, hivyo sharia
si za lazima.
Kauli hizi za wanamabadiliko zilipingwa sana na wanamapokeo ambao waliamini kwamba urari wa vina na
mizani ndiyo roho ya ushairi, ruwaza ya vina na mizani
ndizo zinazoufanya ushairi wa Kiswahili ujitambulishe.
Njogu na Chimerah (1999:113) wanadai kwamba mgogoro
huu ulikuwa baina ya vijana na wazee waliokuwa
wamekulia katika mazingira ya tungo za vina na mizani
Mawazo yao kwa ujumla yalipingana kwa kiasi kikubwa na
mawazo ya wanamapokeo japo kuna mazingira Fulani
walifanana. Wanamabadiliko waliamini kuwa
Hakuna sheria za kutunga mashairi (Kezilahabi 1977:60), kila shairi lina njia yake ya kutunga na njia yake ya kutoa
mawazo.
Dhamira/maudhui, mawazo, maadili na falsafa zitawale fani ya ushairi
Walidai kuwa mabadiliko ya umbo la ushairi yamefungamana na maendeleo ya historia ya jamii zetu, ni
sehemu ya jamii yetu,hivyo kubadilika kwa ushairi wa
Kiswahili si kitu cha kigeni
Vina na mizani ni kunga za utungaji zilizozuia ushairi wa Kiswahili kukua na kusambaa kwa mapana yake na marefu
yake.
Soma Njogu na Chimerah (1999) ufundishaji wa fasihi.
-
14
II. RIWAYA
Riwaya sio utanzu wa muda mrefu sana bali ni utanzu ambao
umeanza kushika mashiko hivi karibuni kuanzia karne ya 19
huko Ulaya
Encloypedia hudai kuwa riwaya ni ubunilizi ya kinathari1
inayotosha kuwa kitabu (kitabu kwa mujibu wa UNESCO ni
chapisho lolote lenye kuanzia kurasa 48 na kuendelea.) bunilizi
ya kifasihi ni ambapo matukio mengi yamebuniwa
Enclopedia Bratanica wanasema riwaya ni masimulizi marefu ya kubuni ya kinathari yaliyochangamana kiasi na yenye
kuzungumzia tajiriba2 ya binadamu. Wanaendelea kusema
kwamba kwa kawaida riwaya huwa na mfululizo wa matukio
yanahusiana na yenye kulihusu kundi Fulani la watu kaka
manthari mahususi
Mphahlele (1976) anasema kwamba riwaya fupi huwa na
kati ya maneno thelathini na tano elfu (35,000) na hamsini elfu
(50,000) na riwaya ndefu zaidi inaweza kuwa na maneno zaidi
ya sabini na tano elfu (75,000)
Mhando na Balsidya wanadai kwamba katika riwaya
lazima kuwe na mchanganyiko wa matukio na ujenzi wa
wahusika naye Foaster (1949) anachangia kwa kusema kwamba
riwaya lazima iwe na wakati.
SIFA ZA RIWAYA
Ni masimulizi ya kubuni Ni hadithi ya nathari katika masimulizi
1 nadhari-ni maelezo ya kina yanayoelezea jambo kwa mapana (hii inafanya itofautiane na ushairi na tamthiliya
2 Tajiriba ni uzoefu alio nao mtu. Uwe mbaya au mzuri
-
15
Ni ya mpangilio au hakuna mpangilio Inafungamana na wakati (yaani yale yanayotendeka katika
jamii hiyo)
Ina sifa ya urefu kama tulivyoona hapo juu Ina mawanda mapana (yaani inaweza kuzungumzia mambo
kwa upana sana)
Lazima kuwe na mchangamano wa visa mfano; katika riwaya ya Janga Sugu la Wazawa ina visa kama, ushirikina,
vifo, mapenzi ya kweli na ya uongo,ndoa, mila nk
Ina wahusika wengi
CHIMBUKO LA RIWAYA
Riwaya imejazwa na mambo makubwa mawili:
1) Fani za kijadi za fasihi 2) Mazingira ya kijamii
a) Ngano-hadithi za kubuni zinazohusu wanyama, watunzi wengi wameathiriwa na ngano kw wasababu wanachota
visa, mbinu za kifani , dhamira katika ngano (zinaonekana
kwamba ni za kingano zaidi)
b) Visasili-masimulizi ya kubuni ambayo yanaeleza juu ya maisha, asili, ya vitu na hatima yake. Kwa kawaida visasili
huaminiwa kuwa ni hadithi za kweli
c) Visakale-ni hadithi za kale zinazohusu kabila la kale, udini nk. M.M.Mulokozi anasema kuwa kila kabila lina visakale
vyake. Katika riwaya visakale vinajitokeza katika riwaya
ya Kisima cha Giningi
-
16
d) Hekaya-ni hadithi za kusisimua kuhusu masaibu na matukio ya ajabu yasiyo ya kawaida, mara nyingi masaibu
yanasababishwa na mapenzi, huwa ni ndefu kuliko hadithi
nyingine lakini si ndefu kuliko riwaya. Katika taaluma ya
Kiswahili ni riwaya ya Adili na Nduguze-Shaaban Robert,
Riwaya ya Ubeberu Umeshindwa ya KIIMBILA( 1971) e) Tendi-ni hadithi ya kishairi kuhusu mashujaa wa kihistoria
na wakubuni wa jamii au taifa.mfano Utendi wa Fumo
Lyongo, kuna baadhi ya riwaya zimeiga mbinu za kiutendi.
Mfano huko Ulaya Illiad Odyssey, Don Tuliv 1928, Toistoi
(1828-1910). Mfano katika Afrika ni riwaya ya Ngugi wa
Thiongo ya Matigali. f) Masimulizi ya wasafiri-ilihusu masaibu waliyopata wasafiri
mbalimbali. Mfano Riwaya ya kiingereza ya kwanza ni
Robinson Kruso ilihusu habari ya mhusika mkuu ambaye
alikuwamo katika merikebu iliyozama na akaokoka na
kuamua kuiishi katika kisiwa peke yake. Katika Kiswahili
kuna riwaya kama vile utumwa Kwa Heri Iselamagazi hizi zote ziko katika muundo huu.
Katika karne ya 16 fani nyingi ziliendelea. Na mojawapo ya
sababu ya kuendelea kwa riwaya ilikuwa ni:
1) Ukuaji mkubwa wa shughuli za kiuchumi huko Ulaya baada mapinduzi ya kiviwanda
2) Mageuzi ya kijamii na kisiasa yaliyofungamana na mabadiliko ya kiuchumi
3) Ugunduzi wa teknolojia ya upigaji chapa
-
17
Mpaka sasa hakuna vigezo maalumu vya uainishaji wa
riwaya, kila mtaalamu huangalia kwa jinsi anavyoona yeye.
Wengine wanaangalia muundo, mtindo, umbo,
lengo/shabaha/historia. Madumula (2009:61 anasema
riwaya inaweza kuainishwa kifani, kidhamira, kihistoria na kiitikadi
Naye Mulokozi M.M (1996) anaonyesha michepuo miwili ya
riwaya:
1) Riwaya ya dhati 2) Riwaya pendwa
Katika mhadhara huu tutaangalia riwaya kama alivyoainisha
Madumula
Inahusu maisha ya mtu binafsi, yaani mwandishi mwenyewe, tatizo hapa ni uaminifu wa mwandishi, si rahisi
kuandika kweli yote.
Mfano katika Kiswahili ni Riwaya Maisha yangu baada ya miaka 50 ya Shaaban Robert
Inahusu mtu mwingine na siyo mwandishi mwenyewe Pia inahusu maisha ya mtu binafsi lakini ni maisha ya mtu
mwingine na siyo ya mwandishi mwenyewe
Ni matukio ya kusisimua ambayo hayajawatokea watu wengine
Lengo kuu ni kueleza ugumu wa maisha ya maisha ya mhusika mkuu jinsi anavyopambana na maisha. Mfano
Wasifu wa Siti Binti Saadi ya Shaaban Robert
-
18
Ina lengo la kufundisha maadili mema ambayo ndiyo msingi katika maisha
Inahusu: mateso na uvumilivu, majuto baada ya kutambua kosa. Mfano katia Kiswahili ni Adili na Nduguze,
Kusadikika, Kufikirika-zote za Shaaban Robert
Huchanganya historia halisi na sanaa ili kuleta maudhui Fulani
Hazielezi matukio yote ya kihistoria bali yale ya muhimu tu, yaliyoathiri mwelekeo na mwenendo wa jamii Fulani
Maudhui yake ni kumbukumbu ya mambo yaliyopita na dhamira zake huwagusa watu wengi. Mfano katika
Kiswahili ni Riwaya ya Uhuru wa Watumwa ya J. Botela,
Kwa Heri Iselamagazi ya J Mapalala, Zawadi ya Ushindi
ya Beni Mtobwa, na Njozi iliyopotea ya Mungongo
Inahusu maisha ya watu na msisitizo wake ni katika mila, desturi na mabadiliko ya kijamii
Dhamira huanzia ngazi ya familia hadi kitaifa na hata kiulimwengu
Husawiri matatizo yaliyo katika jamii kwa kuonyesha chanzo chake. Mfano katika Kiswahili ni Dunia Uwanja
wa Fujo ya Kezilahabi, Siku ya Watenzi Wote ya
Shaaban Robert na Harusi ya J.Safari
Aina hii inaweka mkazo juu ya mikinzano ya ndani ya binadamu, kiakili, kinafsi na kijinsia
Huonyesha uwezo na udhaifu wa binadamu katika kuzikabili hali ngumu za maisha
-
19
Mhusika mkuu husukumwa katika ukingo wa aidha kufa ili ayaepuke matatizo au aishi na hayo matatizo. Mfano katika
Kiswahili ni riwaya ya KIU ya Muhamedi S.Abdalah,
Nyota ya Rehema ya huyu huyu Muhamed, Rosa Misitika
ya Kezilahabi na Kichwa Maji ya Kezilahabi
Ni riwaya ambayo inajadili matatizo ya kisiasa Inalenga kuleta mabadiliko ya kisiasa na kijamii Mara nyingi riwaya za kimapinduzi zina mwelekeo wa
kisosholisti ambapo mlengwa mkuu ni umma kushika
hatamu
Mkazo upo katika ITIKADI kama msingi na dira ya kuongoza jamii
Wahusika wake wanatoka katika matabaka mbalimbali Mfano katika Kiswahili ni riwaya ya KULI ya Adamu
Shafi, Utengano ya Saidi A Mohamed, Dunia Mti Mkavu
ya S.A.Muhamedina KASRI MWINYIFUAD ya Shafi A
Shafi
Inajadili migogoro na maisha ya binadamu kwa kutafakari kwa mantiki na kwa kina kuhusu mambo yanayohusu
maisha
Inajadili maswali kama vile: maana ya maisha nini? Hatima ya binadamu nini? Uhusiano wa binadamu na malaika
ukoje?
Mifano ya riwaya ya kifalsafa ni: Mzingire, dunia uwanja wa fujo, Nagona, babu alivyokumbuka ya S.A Muhamedi,
Riwaya ya Binadamu-ya K.w Wamitila. Riwaya hizi ni
ngumu sana kuelewa zinaelezea, hata wahusika wake ni wa
kufikirika zaidi, mfn wanyama nk
-
20
Ni riwaya ambazo hujishughulisha na masuala ya upelelezi, mapenzi na ujasusi, mara nyingine zinahusisha
mapigano ya kimwili na ya kiakili kati ya mtu mmoja na
watu wengi. Na mara nyingi huyu mtu mmoja
huwashinda watu wengi
Riwaya hii inakuwa na mhusika mkuu mkweli (ambaye anapewa sifa ambazo zinazidi uwezo wa mwanadamu
wa kawaida-yaani huwezi kumshinda kuanzia mwanzo
hadi mwisho). Riwaya za namna hii zina chumvi nyingi.
Mfano Riwaya ya Kifo ni haki yangu mhusika wake mkuu Camila anayekata nyeti za wanaume. Mfano
mwingine ni Simu ya kifa ya Faraji Katambula, Kikosi
cha Kisasi ya E.Musiba. Mzimu wa watu wa kale, Kosa
la Bwana Msa-vya Muhamedi S.Abdula-mhusika wake
mkuu ni Msa
Utanzu wa riwaya umekuja baada ya utanzu wa ushairi na tamthiliya lakini ukuaji wake umekuwa kwa kasi
kubwa. Inasemekana kwamba riwaya ya Kiswahili
ilianza kujitokeza katika mwisho mwa karne ya kumi na
tisa. Kwa nini ilichelewa sana hapa Afrika? Sababu yake
ni kwamba
1. Hadhira kubwa ya watu haikujua kusoma na kuandika
2. Hadhira kubwa ya watu haikuweza kununua vitabu
3. Jamii ya waswahili haikuwa na mitambo ya kupigia chapa
na pia haikuwa na mfumo mzuri wa usambazaji
vitabu(hapakuwa na printers nk)
-
21
Hivyo tunaona kwamba wakati wa ujio wa wakoloni
ulisababisha kuanzishwa kwa baadhi ya vituo vya kupigia
chapa, kwa mujibu wa Mulokozi ( ) anasema ukoloni uliweka
mazingira ambayo yameweza kuilea riwaya. Mfano: hati ya
maandishi ya Kirumi, mfumo wa usambaji wa vitabu
Mwanzo riwaya ya Kiswahili ilianza kujitokeza kwanza kama
tafsiri ya kazi za nje, hivyo tafsiri nayo ilisaidia sana
kuchipuka kwa riwaya. Kwa kadri tafsiri zilivyokuwa
zikifanywa, waswahili walianza kuiga vitabu hivyo.
Kamati hii ilihimiza uandishi katika lugha ya Kiswahili kwa
njia ya kushindana. Hivyo ilianzisha mashindano ya uandishi
wa Kiswahili. Riwaya ya kwanza ya Kiswahili ilikuwa Uhuru
wa Watumwa ya MBOTELA Ilichapwa mwaka 1934, riwaya
nyingine ni riwaya ya Mzimu wa watu wa kalena Simu ya Kifo
Kulijitokeza riwaya ambazo zilikuwa zikifuata mkondo wa
kingano.Njogu na Chimerah (2008) wanaeleza
kuwakimaudhui riwaya nyingi zilikuwa na mambo ya kimila na tabia kama njia ya kutunza maadili. Miongoni mwa riwaya
hizo ni Utu bora mkulima, Kufikirika, Kusaidikika, Adili na
Nduguze na Siku za watenzi wote zote za Shaaban Roberti.
Kulikuwa na mambo yafuatayo:
Ukombozi wa bara la Afrika na ujenzi wa jamii mpya, hivyo
maudhui yake yalikuwa ni ujenzi wa jamii mpya na:
-
22
Kusuta ubinafsi na ukandamizaji
Zilikuwa zikihakiki unyama wa maisha ya kimiji
Zilikuwa zikiielekeza jamii katika mkondo wa kibinadamu katika usawa na ustawi. Mfano riwaya hizo ni LILA NA FILA,
KABURI BILA MSALABA-iliandikwa na KAREITHI
Katika kipindi hiki pia kulijitokeza kundi la Riwaya Pendwa
zilizohusu upelelezi na uharifu mfano Mzimu wa watu wa
kale, Kisima cha Giningi, Simu ya Kifo
Zile za uharifu ni MTAKA YOTE HUKOSA YOTE ya Leo
Odera Omera, Tatizo Kisauni ya CHADHORO
Ni kipindi cha kupevuka na kushamiri kwa riwaya ya Kiswahili, katika kipindi hiki riwaya nyingi zilianza
kujishughulisha na uongozi na usaliti wa kisiasa.
Njogu na Chimerah (2008) wanadai wasanii walianza kutafakari jinsi ukoloni ulivyoanza kufungua milango
kwa watu wachache na kutumia mali kwa manufaa yao
wenyewe
Katika kipindi hiki kuliibuka riwaya za kihistoria kwa mfano KWA HERI ISELAMAGAZI iliyoandikwa na
Mapalala. Miradi Babu ya wazalendo.
Katika kipindi hiki kulizuka riwaya ya kifalsafa na ya majaribio. Mfano Nagona 1987, Mzingile(1991)-
Kezilahabi. Riwaya ya Zilahiri na Zirani ya William
Katika kipindi hiki kulikuwa na ongezeko la riwaya ya vijana na watoto. Mfano wa riwaya hizo ni Mashujaa wa
Kaza kamba-ya Shija (1980) wimbo wa Sokomoko
(1990), Ngome ya Mianzi (1990), Ngoma ya
-
23
Mianzi(1991) Moto wa Mianzi (1995) zote hizi ni za
Mulokozi.
Fasihi huithamini jamii kihistoria, kiitikadi, kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni na kijamii, na kwa kuwa jamii
imekuwa ikibadilika badilika kimtazamo, fasihi nayo
imekuwa ikibadilika kwa sababu jamii inabadilia. Na hivyo
fasihi nayo inahitaji kupokea mabadiliko hayo ili kwendana
na jamii husika.
Mabadiliko katika riwaya (fasihi) yanatokea kwa sababu ya wasanii kutumia vionjo vipya katika kuziumba kazi
zao. Kama anavyosema Khamisi (2007) anasema,mara moja
tunaona neno kionjo linajisemea lenyewe kimya kimya juu ya
mabadiliko ya utanzu wa fasihi. Lengo la mabadiliko hayo ni
kwamba chenye mwanzo hakikosi kuwa na mwisho
Utanzu wa riwaya ya Kiswahili haukuepuka mabadiliko. Sababu zilizobadilisha mabadiliko haya ni makali
ya wembe wa kisiasa, mfano nchini Kenya makali ya kisiasa
yalikuwa dhidi ya Masosholisti. Mfano wa riwaya ni Gamba
la Nyoka,
Majaribio na mabadiliko ya riwaya ya Kiswahili yalianza pale ambapo waandishi wengi wa Kenya na
Tanzania walipoanza kukataa kukubali kila kitu
walichokisikia. Walipoanzaa kukataa kanuni za jamii za
ughunaji, hivyo wakaanza kuandika riwaya tofauti na za
mwanzo.
-
24
Madumula anawanukuu SCHOLES na APLLOE riwaya huweza kubadiliko kutokana na utanzu wenyewe
kuwa hauna mashiko legelege na tepetepe, hubadilika badilika
Hivyo kutokana na majaribio na mabadiliko katika riwaya ya Kiswahili tunaona upywa katika kazi za riwaya
katika fani na maudhui yake. Kisanaa riwaya hizi
zinachanganya uhalisia na falsafia. Mfano wa riwaya ya
Kufikirika. Mfano mwingine ni UKIUSHI-Mtiririko
haueleweki, na riwaya hizi zinakuwa na mwingiliano matini
yaani kuchanganya kazi nyingi katika kazi moja.kisanaa pia
zina wahusika wa kidhani
Pia riwaya hizi zina mazingaombwe sana, kwa mfano katika Nagona lugha yake ni ya mafumbo, visasili, pia ni
lugha inayoelekeza, haifafanui sana.kimaudhui riwaya hizi za
majaribio inatazama matatizo kwa mtazamo wa ndani.
Inashughulikia masuala ya ulimwengu wote, riwaya hizi pia
kimaudhui zinaitetea dunia dhidi ya maangamizi ya uovu
mkubwa.
3. TAMTHILIYA NA DRAMA
Kumekuwa na mkanganyiko kati ya dhana hizi mbili, watu
wamekuwa wakizichanganya sana.
Tamthiliya ni drama na kinyume chake
Tamthiliya ni drama lakini si drama zote ni tamthiliya
A. TAMTHILIYA
Mulokozi (1999:88) tamthiliya ni kazi iliyokusudiwa kutendwa jukwaani kwa ajili ya hadhira fulani
-
25
Tamthiliya huitwa mchezo wa kuigiza. Istilahi hii tamthiliya imetokana na neno methali lenye maana ya
mfano/ishara ya kitu
Wamitila (2003)tamthiliya ni kazi ya kidrama na ya kimaongezi ambayo huigizwa mbele ya hadhira/kazi
iliyoandikwa ili kusomwa
Kimuundo tamthiliya hudhihilika katika:
matendo na maonyesho, mazungumzo huchukua sehemu kubwa katika uwasilishwaji wake wa maudhui (huwa
katika diolojia)
haiweki msisitizo mkubwa katika uwasilishwaji wake jukwaani wakati drama inaweka msisitizo mkubwa katika
uwasilishwaji wake
Penina Mhando anadai kuwa Tamthiliya ni ule utungo unaoweza kuwa umeandikwa au haukuandikwa ambao
ambao unaliweka wazo linalotaka kuwasilishwa katika
umbo la tukio la kiliwezesha kutendeka mbele ya hadhira
Kutokana na sifa hii ya kutendeka jukwaani tamthiliya inawekwa kwenye kundi la sanaa za maonyesho(Mulokozi)
SANAA ZA MAONYESHO
Mohamedi na Balysidya wanasema kuwa sanaa za maonyesho
ni kitendo chochote chenye sifa 4
a) Mchezo b) Mchezaji c) Uwanja wa kutendea d) Watazamaji
tamthiliya ni andiko la kiuigizaji linalotoa simulio kwa
kuonyesha maneno na matendo
-
26
B. DRAMA
Wamitila (2003) anasema ni aina ya utanzu wa fasihi ambao kimsingi hudhamiriwa kuigizwa mbele ya hadhira inaweza kuwa imeandikwa au haikuandikwa lakini msisitizo wake ni
kuigizwa
Msingi mkuu wa drama ni utendaji na utanzu huu umebuniwa kwa ajili ya thieta
Wahusika hupewa majina ya kuigiza mbele ya hadhira
Iwochukuu (2000) anasema drama ni mabadiliko, ubunifu na usawiri wa uhalisi jukwaani. Msingi mkuu wa drama ni
matendo. Hoja hii imeungwa mkono na Aristotle anayeifafanua
drama kama uigaji wa matendo
Bretcht anasisitiza kuwa drama si uigaji wa matendo pekee pia ni chombo cha ufafanuzi wa hali za kijamii, chombo
cha mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi
Kitendo huitwa drama endapo kitendo hicho ni mwigo wa kitendo cha kilichokwishatangulia.
DRAMA ZA KIJADI
Jamii ya waafrika ikiwemo ambayo utamaduni wake ulikuwa
haujaingiliwa na wakoloni ilikuwa na sanaa ya maonyesho
zilizogawanyika katika makundi mbalimbali. Balisdya na
Mhando walianisha aina mbalimbali za drama hizo
1. SHEREHE
Zilihusishwa na kundi moja kwenda kundi jingine mfano. Jando na unyago, jina kwa mtoto, kuota meno nk
Ziliambatana na madaraka kwa mwanajamaii ya mwanajamii aliyeingia katika kundi jipya. sherehe
-
27
ziliwekwa katika katika umbo la vitendo na vikapewa uzuri
wa kisanaa
2. NGOMA
Mhando na Balisdya wanasema ni chombo, sherehe au uchezeshaji wa viungo vya mwili. Malengo yake ni
kuburudisha
3. MASIMULIZI YA HADITHI
Katika usimuliaji wa hadithi kuna vipengele vya kidrama vinavyojitokeza. Yaani:
Usimuliaji Uigizaji Uimbaji Muziki
4. KUSALIA MIUNGU
Jamii fulani inapopata mafanikio au matatizo fulani ndipo huenda kutambikia miungu yao kwa kushukuru au
kuomba kutatuliwa matatizo yao
5. MAJIGAMBO
Masimulizi ya kujigamba ya mtu kuhusu mambo ya kishujaa aliyopata kuyatenda maishani mwake
Kwa kawaida hutumia lugha ya kishairi na masimulizi huambatana na vitendo vya majigambo yenyewe.
Pia yaliambatana na matumizi ya maleba
AINA ZA TAMTHILIYA
1. TANZIA
Ni tamthiliya yenye huzuni inayogusa hisia za wasomaji kiasi cha kuogopesha na kumuonea huruma mhusika mkuu ambaye
hupatwa na masahibu/matatizo/majanga hayo
-
28
Msingi mkuu inalenga msomaji kupata hisia
Mhusika mkuu huwa ni maarufu
Aristotle anasema kuwa mhusika mkuu lazima atoke katika familia yenye nasaba bora/tabaka la juu
Si tanzia zote mhusika anatoka tabaka la juu. Mfano KIFO KISIMANI-mhusika mkuu hapa anatokea katika tabaka la
chini kabisa
Misingi ya utokeaji wa tanzia
Iamushe hisia za woga na huruma miongoni mwa hadhira
Shujaa lazima awe mtu mwema, sura nzuri,umbo zuri, ili yanayomtokea yasitarajiwe
Mhusika huonyesha kuumia kadri mtu anavyoonekana kuwa ni mwema na ana umbo zuri.
Anguko la shujaa huja kutokana na uamuzi wake ama kosa lake mwenyewe
Katika tanzia ya kirasimi shujaa hutoka katika nasaba bora 2. RAMSA/KOMEDI
Ni tamthiliya ambayo inachangamsha na huishia kwa kufurahisha/ni tamthiliya ya vichekesho, hii haina maana
kwamba haina maudhui mazito ndani yake.
Inashughulikia mambo yale yale yanayoweza kushughulikiwa na tanzia. Mfano masuala ya unafiki,uzembe, wivu nk, hata
hivyo inayashughulikia kwa namna tofauti na tanzia
Kwa kawaida wahusika wa Ramsa huumbwa vibaya kuliko walivyo
Udhati wa ramsa si kwamba usanii humalizika katika kicheko/furaha zaidi ni kuishia mhusika mkuu kufanikiwa
shujaa wa kiramsa
-
29
Si lazima awe mtu maalum/mbabe au shujaa, anaweza kuwa mtu wa kawaida
Kwa mujibu wa Aristotle anasema mhusika wa ramsa lazima awe mtu wa wastani chini ya wastani, awe ni mtu ambaye
hatarajiwi kujitokeza na mtu wa nasaba duni na matendo yake
yawe ya ucheshi
Ni lazima awe mtu ambaye akifanikiwa wasomaji au watazamaji watafurahi
uhusika wa wahusika wa ramsa
Ramsa inawahusu watu wa kawaida kuliko ilivyo tanzia
Inawahusu watu wa kipato cha kati na cha chini
Na dhamira zote huelekezwa kwa watu wa kipato cha chini na duni. Mfano walalahoi
AINA ZA RAMSA
a) UTANI
Ni aina ya ramsa ambayo mambo inayozungumzia yanaokana kuwa ya kipuuzi
Mambo hugeuzwa kuwa kinyume kabisa na jinsi yalivyo
Kwa kawaida sura za wahusika hubadilishwa kuwa kama vinyago
Lengo kuu ni kuchekesha-ambalo ndilo haswaa, lengo la tamthiliya ya ramsa
b) RAMSA ZA MAPENZI/MAHABA
-
30
Hizi zinahusu mapenzi ambapo wapendanao huwekewa vikwazo kama vile fedha, elimu, din,
kabila nk
Wahusika hawa hushinda vikwazo hivyo c) TASHTITI/DHIHAKA
Zinalenga kwa viongozi wa kisiasa au dini
Zinawahusu matapeli, wanafiki, wala rushwa, ni
Mhusika mkuu anakuwa na sifa za utapeli nk
Lengo kuu ni kumdhihaki huyu kiongozi ili aachane na tabia hizo
ni njia ya walalahoi kupeleka malalamiko yao kwa viongozi
SIFA ZA RAMSA
Sharti ivutie akili na siyo hisia
Ni lazima kuwa na matendo bila kufikiria hii itapelekea msomaji au mtazamaji kujua kwamba
wahusika hawa hawana akili
lazima iwe na hali ya utu (ikitukumbusha ubinadamu wetu)
sharti iwe na mila na desturi ambazo hadhira inazifahamu toka katika jamii yake
Hadhira isiogope au kupata uchungu kwa sababu hii sio lengo lengo la ramsa
Wahusika wa ramsa hujaribu kuepuka vikwazo ambavyo vimewekwa
Inaonyesha haja ya kuikomboa nafsi Mfano wa ramsa ni kama vile MFALME JUHA
d) TANZIA-RAMSA
-
31
Hii ni tamthiliya ambayo inaonyesha mabaliko ya aina fulani yanayogeuza matukio ya tanzia kuwa ya ramsa
Ni tamthiliya inayochanganya vipengele vya tanzia na ramsa
Hutumiwa sawa na tamthiliya ya kibwege-hii ni
tamthiliya ambayo inaonyesha kwamba kicheko au
furaha ndiyo jibu pekee la maisha kwa watu ambao
hawana imani na maisha ambao kwao misingi
dhabiti ya maisha imeondoleo. Mfano tamthiliya ya
AMEZIDI ya S.A Mohamedi
e) MELO-DRAMA
CHIMBUKO , MABADILIKO NA MAENDELEO YA
TAMTHILIYA YA KISWAHILI
CHIMBUKO: Tamthiliya chimbuko lake duniani kote
linashahibiana/zinapatikana duniani kote na kuonekana
katika maumbo tofauti tofauti. Tamthiliya inahusishwa
sana na visakale na matendo ya kidini. Katika bara la Ulaya
tamthiliya inahusishwa na miviga ya kidini katika jamii ya
Wayunani/Wagiriki wa zamani/ancient Greek. Miviga hii
katika jamii ya wayunani iliambatana na dua ya
kuzaliwa..mpaka kufa na kuoza na kuwa binadamu tena
Huko India tamthiliya zilitokana na tenzi zilizoitwa
Mahabharata na pia zilitokana na miviga zilizoendana na utendi wa tendi hizo kutika mahekalu ya
kidini
Kule Japani na China-drama inatokana na dansi na
miviga ya kidini baadaye miviga hii ilijitenga na dini na
kuanza kujishughulisha na sanaa
Katika Afrika-maigizo ya tamthiliya yalikuwa
yanapatikana huko Misiri na maigizo haya yalikuwa
-
32
yanahusu kufa na kufufuka kwa mungu wa wamisiri
aliyeitwa osiais. Miviga hii ilikuwa inaigizwa kila mwaka
kwa miaka kama elfu mbili. Pia katika Afrika kulikuwa na
maigizo ambayo hayakuwa yameandikwa lakini yalikuwa
ni sehemu ya matendo ya kijamii yaani miviga na ngoma.
Kulikuwa na tamthiliya bubu, maigizo ya watoto na
maigizo ya watani. Drama hizi zilikuwa
zikifungamanishwa na fasihi simulizi
Hivyo tamthiliya inatokana na mambo makuu matatu
a. Miviga na viviga vya kijamii, na dini pamoja na tendi b. Usawilishaji wa maisha ya kawaida kwa ajili ya burudani,
elimu nk
c. Sanaa za maonyesho za kijadi; ngoma na dansi
BWANA YESU ASIFIWE SANA
0786 684062 0715684062
PASTOR: SENI DANIEL JOHN
B.A KISWAHILI