Somo la 1 Kwa akili ya Aprili 6, 2019 kamili wa kiroho. (Waebrania 5:12-14). Hebu tujifunze badiliko...

Post on 04-Feb-2020

3 views 0 download

Transcript of Somo la 1 Kwa akili ya Aprili 6, 2019 kamili wa kiroho. (Waebrania 5:12-14). Hebu tujifunze badiliko...

Somo la 1 Kwa akili ya Aprili 6, 2019

MABADILIKO YANAYOJIRUDIA

• Mpangilio na Mahadhi

• Mahadhi ya maisha

MABADILIKO YASIYOJIRUDIA

Mabadiliko ya siyotarajiwa

Mpito

Mwingiliano

“Kwa kila jambo kuna majira yake…” (Muhubiri 3:1). Mungu aliuumba muda na mahadhi ambavyo vinaongoza Maisha duniani (mimea, wanyama, na binadamu). Mahadhi hayo ni sawa Kwa kila mmoja, lakini siyo kila mmoja anayaishi kwa namna iliyo sawa. Kuna mabadiliko yanayowadhuru watu tofauti. Mabadiliko hayo yanaumba Maisha yetu.

“Muda nchi idumupo, majira ya kupanda, na mavuno, wakati wa baridi na wakati wa hari, wakati wa kaskazi na wakati wa kusi, mchana na usiku, havitakoma.(Mwanzo 8:22)

Kulingana na Mwanzo 1, Mungu aliiumba dunia na akaibadilisha kutoka kutokuwa na mpangilio hadi ukamilifu

Kwa utaratibu alitenganisha nuru na giza, akayagawanya maji, akafanya nchi kavu ionekane, akafanya mimea iote, na akaumba mianga katika anga ili ianzishe mahadhi ya dunia (siku, miezi, miaka). Kwa mpangilio mzuri, aliijaza dunia Kwa viumbe hai, na akaweka mpangilio katika Maisha yao (kuzaa na kuongezeka) “Mpangilio ni sheria ya kwanza ya mbinguni.” (ST, June 8, 1908).

Ingawa dhambi ilileta machafuko katika ulimwengu wetu, mahadhi ambayo Mungu aliyaanzisha mwanzo bado yanaongoza.

Utoto(Judges13:24; Luke 2:40).

Ujana(Psalm71:5; 1 Timothy 4:12).

Utu uzima(Genesis 41:46; Acts7:23).

Uzee(Psalm 90:10; Philemon1:9).

“Fahari ya vijana ni nguvu zao, Na uzuri wa wazee ni kichwa chenye mvi." (Mithali

20:29)

Kama Sulemani alivyosema, kuna "wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa." (Muhubiri 3:2). Kuna baadhi ya mahadhi au mizunguko kati ya nyakati hizo mbili za Maisha yetu:

Mahadhi hayo ni sawa Kwa kila mmoja, lakini siyo kila mmoja anayaishi Kwa namna iliyo sawa. Tuko tofauti na tunaishi katika hatua tofauti. Japokuwa, kila mmoja ni wa thamani na ana kitu cha kutoa.

“Akasema, Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nili uchi, nami nitarudi tena huko uchi vilevile; BWANA alitoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA na libarikiwe." (Ayubu 1:21)

Wote tuna mahadhi na taratibu zetu. wakati mwingine, mabadiliko yasiyotegemewa yanaweza kuvuruga. Kesi ya Ayubu Ilikuwa iliyokithiri Sana (alipoteza mali, watumwa, watoto, Afya yake, na msaada wa mke na rafiki zake). Japokuwa, kila mmoja ni mhusika wa mabadiliko makubwa, ambayo yanaweza kubadilisha mazingira ya maisha yetu, Kwa mema au mabaya.

Habili alikufa mapema sana, Yusufu aliuzwa kama mtumwa na ndugu zake mwenyewe.

Kama tutajishikamanisha na Mungu na kumwamini, tutaweza kuyakabili mabadiliko yasiyotegemewa na kupata vitu vilivyo bora kutoka kwenye hayo mazingira mapya (Mwanzo 50:20).

“Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu;" (Wafilipi 1:6)

Mapito huweka badiliko kati ya hatua za maisha: utoto, ujana, utu uzima, uzee.

Kuna mapito katika Maisha yetu ya kiroho pia. Mungu hutuchukua toka tunapoongoka hadi ukuaji kamili wa kiroho. (Waebrania 5:12-14).

Hebu tujifunze badiliko mtume Paulo alilolipitia (AA, pp. 119, 120):

Mawazo na hisia za ndani ya moyo wake zilibadilishwa na Neema ya Mungu

Akili zake nzuri sana zikaletwa katika upatanifu na makusudi ya milele ya Mungu.

Kristo na haki yake akawa Kwa Sauli zaidi ya ulimwengu wote.

Maisha yetu yanaathiriwa sana na namna watu wengine wanavyoingiliana nasi. Tunawaathiri wengine pia tunavyoingiliana nao

Miingiliano hiyo inaweza kuleta mabadiliko, pengine Kwa mema, au mabaya. Kama.Wakristo, daima lazima tuwe washawishi wazuri Kwa wengine. (Warumi 12:18).

Miingiliano yetu chanya inaweza kuwa nguvu ya ushawishi. inaweza kuathiri Maisha ya wengine Kwa namna ambayo watamshukru Kristo Kwa kazi yake kupatia sisi.

Mahusiano yetu ni lazima daima yaongozwe na Upendo na upole.