Taafifa kwa vyombo vya habari (kisahili) Ipsos Tanzania september 2015

4
Dar es Salaam, Tanzania September 24, 2015 Utafiti juu ya Maswala ya Uchumi, Siasa, tamaduni na mambo ya kijamii Utafiti wa robo ya tatu 2015 Utangulizi Huu ni utafiti unaofanywa na kampuni ya Ipsos Tanzania kila baada ya miezi mitatu. Utafiti huu unadhaminiwa na lpsos. Utafiti huu unatumila kutoa taarifa kwa umma kuhusu masuala tofauti ya nchi. Utafiti huu ulifanyika kupitia njia ya mahojiano ya ana kwa ana na ulianza tarehe 5 – 22 Septemba 2015 katika kiwango cha kaya katika mikoa yote ya Tanzania Bara. Sampuli imewakilishwa katika kiwango cha kitaifa (margin of error 2.3% at 95% confidence interval) Alama za muhtasari za utafiti nchini Tanzania: 1) Changamoto nyingi za kimaendeleo ambazo hazijafikiwa zinasubiria awamu ya serikali ifuatayo ya Tanzania, kwa yeyote atakaye shinda katika uchaguzi huu. 2) Kwa kigezo cha kwamba hakuna hata eneo moja kati ya maeneo ya sera lililokuwa na watu waliyozidi nusu waliyoonyesha imani katika chama tawala, hii inaashiria kwamba uchaguzi huu utakuwa na ushindani mkubwa kuliko chaguzi zote tangu nchi ilipoanzisha mfumo wa vyama vingi. 3) Kwa ujumla, zaidi ya mara mbili ya watanzania wanaunga mkono CCM ukilinganisha na CHADEMA; Hata hivyo kuna baadhi ambao wanaonekana kutojihusisha na chama chochote cha siasa . 4) Katika kipindi cha utafiti, J. Magufuli wa CCM anaongoza kwa 2-1 (62% vs 31%) dhidi ya mpinzani wake mkuu E. Lowassa wa (Chadema/Ukawa).Ingawa tofauti kati yao ilikuwa ni ndogo kwa wahojiwa ambao hawakuwa na maamuzi au ambao hawakuweka wazi chaguo lao. Hii inamaanisha kuwa shughuli za kampeni zinazoendelea katika kipindi kilichobaki zinaweza kuleta mabadiliko makubwa katika matokeo ya uchaguzi

Transcript of Taafifa kwa vyombo vya habari (kisahili) Ipsos Tanzania september 2015

Page 1: Taafifa kwa vyombo vya habari  (kisahili)  Ipsos Tanzania september 2015

Dar es Salaam, Tanzania

September 24, 2015

Utafiti juu ya Maswala ya Uchumi, Siasa, tamaduni na mambo ya kijamii Utafiti wa

robo ya tatu 2015

Utangulizi

Huu ni utafiti unaofanywa na kampuni ya Ipsos Tanzania kila baada ya miezi mitatu. Utafiti

huu unadhaminiwa na lpsos. Utafiti huu unatumila kutoa taarifa kwa umma kuhusu masuala

tofauti ya nchi. Utafiti huu ulifanyika kupitia njia ya mahojiano ya ana kwa ana na ulianza

tarehe 5 – 22 Septemba 2015 katika kiwango cha kaya katika mikoa yote ya Tanzania Bara.

Sampuli imewakilishwa katika kiwango cha kitaifa (margin of error 2.3% at 95% confidence

interval)

Alama za muhtasari za utafiti nchini Tanzania:

1) Changamoto nyingi za kimaendeleo ambazo hazijafikiwa zinasubiria awamu ya

serikali ifuatayo ya Tanzania, kwa yeyote atakaye shinda katika uchaguzi huu.

2) Kwa kigezo cha kwamba hakuna hata eneo moja kati ya maeneo ya sera lililokuwa

na watu waliyozidi nusu waliyoonyesha imani katika chama tawala, hii inaashiria

kwamba uchaguzi huu utakuwa na ushindani mkubwa kuliko chaguzi zote tangu

nchi ilipoanzisha mfumo wa vyama vingi.

3) Kwa ujumla, zaidi ya mara mbili ya watanzania wanaunga mkono CCM ukilinganisha

na CHADEMA; Hata hivyo kuna baadhi ambao wanaonekana kutojihusisha na

chama chochote cha siasa .

4) Katika kipindi cha utafiti, J. Magufuli wa CCM anaongoza kwa 2-1 (62% vs 31%)

dhidi ya mpinzani wake mkuu E. Lowassa wa (Chadema/Ukawa).Ingawa tofauti kati

yao ilikuwa ni ndogo kwa wahojiwa ambao hawakuwa na maamuzi au ambao

hawakuweka wazi chaguo lao. Hii inamaanisha kuwa shughuli za kampeni

zinazoendelea katika kipindi kilichobaki zinaweza kuleta mabadiliko makubwa katika

matokeo ya uchaguzi

Page 2: Taafifa kwa vyombo vya habari  (kisahili)  Ipsos Tanzania september 2015

5) Akiwa anaongoza kwa kiasi kikubwa dhidi ya mpinzani wake katika makundi tofauti

ya idadi ya watu, mgombea wa CCM ana mvuto mkubwa miongoni mwa wanawake

na watu wanaoishi vijijini kuliko miongoni mwa wanaume na watu wanaoishi mijini.

Vivyo hivyo kwa upande wa umri ,ambapo wazee wameridhika zaidi na CCM.

Matokeo ya kina

A. Ajenda ya maendeleo

1. Watanzania wanakubaliana vikubwa kuhusiana na matatizo yanayoikabili nchi,

yakiwemo yale yanayothibitisha umaskini ambayo yametajwa mara kwa mara:

gharama za maisha, njaa, usambazaji wa maji, uzalishaji katika kilimo, n.k.

2. Hii inathibitishwa na uwepo wa hali ya umaskini katika maeneo ya wahojiwa (89%),

ikiwemo kiwango kidogo cha uboreshaji wa maeneo ya mjini tofauti na maeneo ya

kijijini. (89% vs. 95%).

3. Vivyo hivyo, vitu hivyo vya msingi katika maendeleo kama vile miundombinu na

huduma za afya ni kipaumbele kikubwa kwa watanzania cha kukabili umaskini.

B. Maswala kabla ya uchaguzi : Vyama vya siasa na Wagombea.

1. Katika kipindi cha utafiti, karibia robo tatu ya watanzania walikuwa wana muelekeo

wa chama fulani cha siasa (78%), na karibia wote hao, walikuwa wameshafanya

maamuzi juu ya nani watakaomchagua (70%). Hali kadhalika kiasi fulani cha

wahojiwa walisema kwamba kuna uwezekano mkubwa (11%) au kuna uwezekano

wa kiasi fulani (7%) kwamba watampigia kura mgombea tofauti wa urais tarehe 25

Oktoba.

2. Katika suala la maeneo makuu 7 ya sera za maendeleo (mf. Miundombinu, elimu,

afya, nk) karibia mara mbili ya idadi hiyo ya watanzania wameonyesha kuwa na

imani na CCM katika kuwasimamia tofauti na Chadema, pasipokuwa na takwimu za

kitofauti katika uwiano wa majibu yao.

3. Mgawanyiko huu unaashiria jinsi mashabiki wa vyama vikuu vya siasa walivyojigawa,

ambapo mashabiki wa CCM ni mara mbili ya wale wa chama pinzani, Chadema

(60% vs. 29%)

Page 3: Taafifa kwa vyombo vya habari  (kisahili)  Ipsos Tanzania september 2015

4. Vile vile katika kipindi cha utafiti, mgombea wa CCM J. Magufuli ana washabiki

karibia mara mbili Zaidi ya mpinzani wake E. Lowassa miongoni mwa wale

waliokwishafanya maamuzi (62% vs 31%)

5. Mgombea wa CCM anaushabiki mkuwa kwenye vigezo viwili (jinsia na Makazi); Kwa

kuangalia jinsia ushabiki kwa mgombea wa CCM na Chadema, kuna tofauti ya 17%,

wakati kwa upande wa wanawake tofauti inaongezeka kwa 30% Hali kadhalika

miongoni mwa wakazi wa vijjijini tofauti inaongezeka kwa 20%. Lakini inapungua kwa

5% kwa kuangalia wakazi wa mjini.

6. Vile vile watu wazima wanaonekana kushabikia CCM, kukiwa na tofauti ndogo ya

ushabiki inayopokea toka kwa kundi la vijana na wazee

7. Ikiwa umebakia mwezi mmoja kamili kufikia tarehe ya uchaguzi; ni theluthi mbili tu ya

wale walionyesha msimamo wa nani watamchagua ambao hawatobabadilisha

maamuzi yao (70%) ikiacha theuthi moja ya wale ambao wanaweza kubadilisha

mawazo yao kuanzia sasa na October 25.

Survey Methodology /Njia ya kufanya utafiti

Walengwa katika utafiti huu walikuwa ni watanzania wenye umri wa miaka 18 na

zaidi, kati ya hao 1,836 wanaoishi maeneo ya mjini na kijijini Tanzania bara

walihojiwa. The margin-of-error attributed to sampling and other random effects is +/-

2.3 with a 95% confidence level. Kwa maelezo ya kidemografia angalia nakala ya Power

Point iliyoambatanishwa.

Utafiti ulifanyika kati ya tarehe 5-22 Septemba 2015. Taarifa zilikusanywa kwa njia

ya mahojiano ya ana kwa ana kwa kutumia simu za kisasa za mkononi.

Page 4: Taafifa kwa vyombo vya habari  (kisahili)  Ipsos Tanzania september 2015

ALAMA MUHIMU KWA AJILI YA VYOMBO VYA HABARI/ WASOMAJI.

1. UTAFITI HUU HAUKUWEZA KUWEKA DHAHIRI NI WAHOJIWA WAPI KATI YA

HAWA WOTE WATAENDA KUPIGA KURA TAREHE 25 OKTOBA KATIKA VITUO

VYAO VYA KUPIGA KURA. KUTOKANA NA HISTORIA YA KIPINDI CHA NYUMA

AMBAPO KIASI CHA UHUDHURIAJI WA WAPIGA KURA KINATOFAUTIANA

SEHEMU ZOTE NCHINI. MATOKEO YA SAMPULI HII HAYAWEZI KUTUMIKA

KUTABIRI MATOKEO HALISI HATA KAMA UCHAGUZI UNGEFANYIKA KESHO.

2. UKIZINGATIA MUDA ULIOBAKI KUAZIA SASA MPAKA TAREHE 25 OKTOBA

PAMOJA NA KAMPENI ZINAZOENDELEA, HAKUNA UHAKIKA KUWA MATOKEO

YA UTAFITI HUU HAYATABADILIKA KATI YA SASA MPAKA SIKU YA UCHAGUZI.

For further clarification or comments, please contact:/ Kwa maelezo zaidi

au maoni wasiliana na ;

Charles Makau Dr. Tom Wolf

Country Head: Ipsos Tanzania Research Analyst

[email protected] [email protected]

+ 255 22 277 5851 / 277 5628

David Luhinda

Project Manager

[email protected]

+ 255 22 277 5851 / 277 5628

twitter.com/ipsostanzania

facebook.com/ipsostanzania

http://www.ipsos.co.tz/

http://www.ipsos.com