NYIMBO ZA MUNGUNi dawa kwa wenye makosa kuponyesha roho. 4 Watumwa wa makosa Yesu anawafungua; Na...
Transcript of NYIMBO ZA MUNGUNi dawa kwa wenye makosa kuponyesha roho. 4 Watumwa wa makosa Yesu anawafungua; Na...
NYIMBO ZA MUNGU
et
NYIMBO ZA WOKOVU
Pour vos commentaires et suggestions :
Email : [email protected]
SMS : +243 84 095 00 00
NYIMBO ZA MUNGU
ORDRE NUMERIQUE
ORDRE ALPHABETIQUE
PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
1. MUSIFU MUNGU KWA BARAKA
1 Musifu Mungu kwa baraka,
Musifu Mungu, watu wote,
Musifu Mungu, malaika,
Musifu Baba, Mwana, roho.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
2. HESHIMA NA SIFA
1 Heshima na sifa kwake Baba mbinguni,
Aliyetupenda zamani na sasa.
Haleluya, usifiwe! Haleluya, Amina!
Haleluya, usifiwe! Haleluya, Amina!
2 Heshima na sifa kwake Yesu Mwokozi,
Alitukufia kwa ’jili ya zambi.
3 Heshima na sifa kwake Roho ya nuru,
Anashuhudia Mwokozi na damu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
3. SIFU! SIFU!
1 Sifu! Sifu! Yesu Mwokozi wa watu!
Imba kutangaza mapendo yake!
Malaika vile, mulete heshima;
Jina lake kweli ni takatifu!
Bwana Yesu anatulinda sana,
Kama Muchungaji anatubeba.
Sifu! Sifu! Yesu Mwokozi wa watu!
Sifu! Sifu! Imba ukubwa wake.
2 Sifu! Sifu! Yesu Mwokozi wa watu!
Kwa makosa alitukufilia;
Kristo, Mwamba, matumaini ya roho
Alitukomboa na damu yake.
Imba sifa kwake aliyeteswa
Kwa kutuonyesha mapendo yake.
3 Sifu! Sifu! Yesu Mwokozi wa watu!
Kule mbingu wanamwimbia sifa;
Yesu Kristo, mwenye kushinda daima,
Ni Mufalme, Nabii, Kuhani wetu.
Atakuja kwa kutawala hapa,
Yesu mwenye enzi na utukufu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
4. TUNAIMBA SASA NYIMBO KWAKE YESU
1 Tunaimba sasa nyimbo kwake Yesu,
Nyimbo za furaha, nyimbo za wokovu;
Yesu Mukombozi, Mwana wake Mungu,
Ni Mwokozi wetu, na tunamwabudu.
Kazi zake zote zinatengenea;
Kule kwake mbingu atatupokea.
2 Watu wa zamani walimuchukia,
Walimushitaki, na walimupiga;
Ju-u ya Kalvari walimutundika,
Yesu alikufa kwa kutuokoa.
3 Ndani ya kaburi alilala kimya,
Hakubaki pale, alifufuliwa;
Alikwenda ju-u kwake, Mungu Baba,
Atarudi tena kwa kutukamata.
4 Kwa maisha yetu hapa kwa dunia,
Yesu anachunga, anatuombea,
Kwa wakati wote anatusaidia,
Tumusifu sana, tumufurahie!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
5. MUNGU MUTAKATIFU
1 Mungu Mutakatifu, Mungu Mwenyezi,
Tunakuimbia nyimbo, tutakuabudu;
Baba, Mwana, Roho, wote ni mumoja,
Mutakatifu, ndiye wewe tu.
2 Mungu Mutakatifu, tunakusifu,
Jeshi la mbinguni wanatoa taji zao;
Malaika wote wanakwabudu,
Mwanzo na mwisho, ndiwe wewe tu.
3 Mungu Mutakatifu, unafunikwa,
Macho ya wenye makosa yasikutazame;
Wewe peke yako ni Mutakatifu,
Mukamilifu, ndiwe wewe tu.
4 Mungu Mutakatifu, Mungu Mwenyezi,
Kazi ya mikono yako inakutukuza;
Wewe mwenye nguvu, Mungu wa Mapendo,
Mwenye rehema, ndiwe wewe tu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
6. KUJA, MUFALME WETU
1 Kuja, Mufalme wetu, tunakusifu sana, tuna-abudu;
Ee, utukufu kwako, wewe ni Mushindaji,
Ututawale sisi, Mungu Mwenyezi!
2 Kuja, Mwokozi Yesu, ili utubariki, tunakuomba;
Utusaidie sisi, utushindishe vile,
Tuwe watakatifu, tukupendeze.
3 Roho Mutakatifu, jaza mioyo yetu, utuongoze;
Ututawale wote tusikuasi kamwe,
Una uwezo mwingi, Roho wa Mungu.
4 Mungu Muju-u wa wote, tatu katika moja,
tunakusifu;
Tuta-abudu kule kukutukuza vile,
Tutakapokuona kwako mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
7. TUSIFU JINA LAKE YESU
1 Tusifu jina lake Yesu, sisi watu wake;
:: Na taji tumuvike yeye Bwana na Mufalme ::
2 Wachaguliwa wake sisi, tuliokolewa
:: Kwa njia ya ne-ema yake, Bwana na Mufalme::
3 Kwa kila lugha na kabila katika dunia,
:: Wazidi kutukuza Yesu Bwana na Mufalme ::
4 Na mbele yake sisi sote tuanguke chini,
:: Tuimbe sifa kwake Yesu Bwana na Mufalme ::
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
8. MUTAZAME UTUKUFU WA MWOKOZI
1 Mutazame utukufu wa Mwokozi wetu Yesu;
Alibeba taabu kubwa, naye alishinda kufa.
Tia taji, tia taji!
Yeye Mushindaji kweli! Yeye Mushindaji kweli!
2 Mumuvike Kristo taji, nyara zake ndizo nyingi;
Mwenye nguvu na mamlaka, sifa kwake kule mbingu.
Tia taji, tia taji!
Kwa Mwokozi na Mufalme! Kwa Mwokozi na Mufalme!
3 Wenye zambi kwa zihaka walimuvalisha taji;
Watu wake kwa mapendo wanamutukuza sana.
Tia taji, tia taji!
Sifa yake mutangaze! Sifa yake mutangaze!
4 Shangwe kubwa kumwimbia nyimbo za kumutukuza;
Yesu kwa pahali pake, utukufu uwe wake.
Tia taji, tia taji!
Kristo, Bwana na Mufalme! Kristo, Bwana na Mufalme!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
9. FURAHA KUBWA KUTANGAZA SIFA
1 Furaha kubwa kutangaza sifa ya Mwokozi,
Na utukufu wa Mufalme, ndiye Mungu wangu.
2 Ee Bwana wangu na Mufalme, usaidie sasa
Pahali pote nitangaze sifa yako kubwa.
3 Ee Yesu, jina tamu sana kupunguza woga,
Ni dawa kwa wenye makosa kuponyesha roho.
4 Watumwa wa makosa Yesu anawafungua;
Na damu yake inafaa kwa kuniosha mimi.
5 Wanaokombolewa wote, muheshimu Bwana,
Na mutangaze pa’li pote Yesu ni Mwokozi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
10. NITAIMBA NA KUSIFU
1 Nitaimba na kusifu Yesu Kristo Mukombozi;
Aliacha utukufu, alikufa kwa Kalvari.
Nitaimba na kusifu Yesu Kristo Mukombozi;
Imba na watakatifu wenye kukutana kwake.
2 Nilikuwa mupotevu, Yesu alinitafuta;
Ali-ita na mapendo, alinirudisha kwake.
3 Hata mimi ni zaifu, Yesu aliniokoa;
Yeye Kiongozi wangu anachunga kila siku.
4 Atachunga hata mwisho, atanipeleka kwake;
Pale nitamutukuza kwa uzuri wake wote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
11. NINAFIKILI, MUNGU BABA WANGU
1 Ninafikili, Mungu Baba wangu,
Viumbe vyote ulivyoviumba
Vinaonyesha nguvu yako nyingi
Pahali pote pa dunia hi-i.
:: Ninakusifu, Mungu na Mwokozi,
Wewe mukubwa, wewe mukubwa::
2 Ninatazama miti na maua,
Ninasikia ndege za peponi,
Vilima na bahari kubwa vile
Zinaonyesha nguvu yako, Mungu.
3 Ninafikili, Mungu, ulituma
Mutoto wako kufa kwa Kalvari,
Na damu yake inatoa zambi;
Ninashangaa kuona pendo lile!
4 Yesu Mwokozi atarudi tena
Kunipeleka kwako, Mungu wangu;
Nitafurahi, nitakushukuru,
Kukutukuza kwa ukubwa wako.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
12. TUNATAKA KUPA KWAKO SIFA
1 Tunataka kupa kwako sifa na heshima zetu,
Yesu ndiwe Kimbilio wetu sisi wenye zambi.
Tunakusifu wewe sasa na kwa milele,
Tunaheshimu jina lako zuri;
Tunakusifu wewe sasa na kwa milele,
Kwa pendo lako kubwa kwetu.
2 Ulilipa ukombozi, na uzima unatupa;
Ndani yako ni wokovu na taraja na salama.
3 Tutaimba na furaha na watakatifu wote,
“Wewe tu unastahili kupokea sifa yetu.”
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
13. MUSINGI WA KANISA
1 Musingi wa kanisa ni Kristo, Bwana yake,
Aliliumba vile kwa utukufu wake;
Na alilitafuta kutoka kwake mbingu,
Na alilinunua na damu yake safi.
2 Kutoka makabila kanisa liko moja,
Na Bwana ni mumoja, ni Bwana wa Kanisa.
Wokovu ni mumoja kwa watu wa dunia,
Taraja vile moja, taraja ya mbinguni.
3 Katika taabu nyingi, mateso duniani,
Kanisa linangoja salama ya milele;
Litakapowashinda adui na Shetani,
Litapumzika mbingu pamoja na Mwokozi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
14. SIFA KWA BWANA, MWENYEZI
1 Sifa kwa Bwana, Mwenyezi, Mufalme, Na Mwumba;
Ee nafsi yangu, usifu Mwokozi daima.
Wasikiaji, mukaribie Mwokozi,
Muje, tusifu pamoja.
2 Sifa kwa Bwana anayetawala na haki,
Mwenye kulinda na mwenye upole na pendo;
Amekujibu mara kwa mara maombi,
Kukubariki zaidi.
3 Sifa kwa Bwana aliyeku-umba na ’kili;
Na ananyosha mukono kwa kukuongoza;
Saa ya huzuni yeye anakufariji,
Ukifichama kwa Bwana.
4 Sifa kwa Bwana, nisifu na moyo wa shangwe;
Mbele ya Mungu tufike kuleta asante;
Acha sauti za watu wake wapenzi
Kumutukuza milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
15. NINASHANGA-A KABISA
1 Ninashanga-a kabisa kwa pendo la Bwana Yesu,
Sababu alinipenda, na mimi mwenye uchafu.
Ajabu tu, ajabu tu, wimbo wangu kwa milele ;
Ajabu tu, ajabu tu, pendo la Mwokozi kwami.
2 Kwami Mwokozi shambani alinyenyekea Mungu;
Na jasho kama matone ya damu ilianguka.
3 Na malaika wa Mungu walikaribia Yesu
Kumufariji kwa taabu aliyoipata kwami.
4 Aliyabeba makosa niliyoyafanya yote,
Na alikufa kwa muti kwa kunilipia deni.
5 Nitakapofika kwake, milele nitamusifu
Kwa pendo lake Mwokozi aliyenikufilia.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
16. NILIPOSIKIA YESU AKI-ITA
1 Niliposikia Yesu aki-ita nimwamini,
Nilijibu, “Bwana Yesu, ninataka kuwa wako.”
Nitasifu Bwana Yesu, alikufa kwa makosa;
Tutukuze jina lake, damu yake inatusafisha.
2 Njia ya Mungu ni diki, majaribu yanazidi;
Nita-acha zambi zote, nitafuata Yesu pekee.
3 Heri jina lake Yesu, alinipokea mimi,
Alinisamehe zambi na kuosha moyo wangu.
4 Utukufu kwake Baba, utukufu kwake Mwana,
Utukufu kwake Roho, wao watatu ni mumoja.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
17. VIKA MWOKOZI TAJI
1 Vika Mwokozi taji, Kondo-o na Mufalme,
Majeshi yote ya mbinguni wanasifu sana!
Ee nafsi yangu, sifu aliyekukufia,
Mufalme wako, Bwana kwa milele na milele.
2 Vika Mwokozi taji, ni Bwana wa mapendo,
Vidonda vyake utazame kwa mikono yake.
Ni neema kubwa sana kwa watu wa makosa,
Ee tunashangilia sana, tunamutukuza.
3 Vika Mwokozi taji, ni Bwana wa uzima,
Aliyetoka kaburini, aliyefufuka.
Tunamwimbia sifa kwake aliyekufa
Kutuletea ukombozi, yuko hai milele.
4 Vika Mwokozi taji, ni Bwana wa mbinguni,
Aliyetuma Roho kwetu toka Baba Mungu.
Tutoe sifa kwako uliyetukufia;
Ee Bwana wetu, utukuzwe sasa na milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
18. TUSIFU MUNGU WA MBINGUNI
1 Tusifu Mungu wa mbinguni, mwenye utukufu,
Aliyetuma Mwana wake kwa kutuokoa.
:: Heri jina lake, heri jina lake,
Heri jina la Yesu Bwana::
2 Ni ju-u ya majina yote, linakuzwa sana;
Na malaika wanaabudu mwenye nguvu yote.
3 Mwokozi na Rafiki wetu alitukomboa;
Shauri la wokovu wetu Mungu alitoa.
4 Ni Mwana wa Mufalme na Mukubwa wa salama;
Atatawala kwa milele, Bwana na Mushinda.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
19. NAPENDA KUIMBIA BWANA SIFA
1 Napenda kuimbia Bwana sifa, Nimekombolewa!
Ni wimbo ju-u ya Mwokozi wangu, Nimekombolewa!
Tangu nilikombolewa,
Tangu nilikombolewa ninasifu jina lake!
Tangu nilikombolewa ninasifu jina la Mwokozi !
2 Ninafurahi sana kwa Mwokozi, Nimekombolewa !
Nataka sana kumutumikia, Nimekombolewa !
3 Najua kweli mimi mwana Wake, Nimekombolewa !
Nitamutegemea sikuzote, Nimekombolea !
4 Na nitaka-a kwa milele kwake, Nimekombolewa!
Kumutukuza, kumusifu yeye, Nimekombolewa !
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
20. EE SIKU YA PUMZIKO
1 Ee siku ya pumziko na siku ya furaha,
Na siku kusahau mateso ya dunia;
Ni siku yake Bwana, Mwenyezi wa mbinguni,
Ni siku takatifu kusifu Mungu wetu.
2 Kwa siku hii zamani ilitokea nuru,
Na siku hii Mwokozi alifufuka vile;
Hii siku vile Roho wa Mungu alifika,
Na hivi mara tatu ni siku kubwa sana.
3 Na leo duniani katika inchi zote
Waamini wanaitwa kusifu Mungu wao;
Tunakusanywa vile kwa jina lake Bwana,
Na kuabudu Mungu na kusikia Neno.
4 Chakula tunapata kwa roho zetu leo,
Na vile raha tamu kutoka Mungu Baba.
Heshima iwe sana kwa Baba na kwa Mwana,
Na Roho ’takatifu; watatu ni mumoja.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
21. HATA JUMA HILI, BWANA
1 Hata juma hili, Bwana, umechunga watu wako;
Hivi leo tuko hapa kuingia nyumba yako.
:: Kuja,Bwana ,kubariki, kwani tunakungojea::
2 Sasa tunaomba, Mungu, usamehe zambi zetu,
Na uoshe roho zetu tuwe safi mbele yako.
::Tupumzike ndani yako toka mambo ya dunia::
3 Tunakuja kukusifu, kweli wewe ni karibu;
Tunataka kutazama utukufu wako, Bwana.
::Hivi tuna hamu sana kuingia kwako mbingu::
4 Tuma Neno lako, Mungu, kufundisha watu leo,
Wapotevu wa-amini na kuacha zambi zao.
::Hivi tukutane, Bwana, hata utakaporudi ::
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
22. EE BWANA, TUNASIFU MAPENDO YAKO
1 Ee Bwana, tunasifu mapendo yako sana,
Tunashanga-a kweli, tunapokutazama;
Kwa sisi ulikuja kwa kutukufilia,
Tupate usamehe, tufike kwako mbingu.
2 Taraja yetu iko kufika kwako, Bwana,
Na kutazama uso waliou-umiza;
Faraja ya mioyo na sifa ya midomo
Katika majaribu, furaha na salama.
3 Mwokozi wetu Yesu, pokea shukurani.
Uliyevumilia makosa, haya vile;
Na sasa unangoja kutufikisha kwako;
Unastahili kweli kupata utukufu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
23. DAMU YA KRISTO IMENIOKOA
1 Damu ya Kristo imeniokoa,
Na nimezaliwa mwenye roho mypa;
Ee sifa kwa Baba na sifa kwa Mwana,
Damu ya Kristo imeniokoa.
Sifa! Sifa! Mwokozi amenisamehe makosa!
Sifa! Sifa! Kwani damu ya Kristo imeniokoa!
2 Damu ya Kristo imeniokoa,
Furaha mbinguni kwa kazi ya Bwana!
Mutoto wa Baba, na vile muriti,
Damu ya Kristo imeniokoa!
3 Damu ya Kristo imeniokoa,
Na Baba alinisamehe makosa;
Ee bei ya damani ni kufa kwa Bwana;
Damu ya Kristo imeniokoa!
4 Damu ya Kristo imeniokoa,
Utatu wa Mungu wapate heshima;
Ee sifa kwa Baba na Mwana na Roho,
Damu ya Kristo imeniokoa!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
24. MWOKOZI ALITUKUFIA
1 Mwokozi alitukufia, Mwokozi mukubwa!
Kwa damu tumeokolewa, Mwokozi mukubwa!
Ee Mwokozi mukubwa ni Yesu, ni Yesu ;
Ee Mwokozi Mukubwa ni Yesu Mupendwa.
2 Nasifu Yesu kwa wokovu, Mwokozi mukubwa !
Na upatano naye Mungu, Mwokozi mukubwa !
3 Amesafisha moyo wangu, Mwokozi mukubwa!
Na sasa ananitawala, Mwokozi Mukubwa!
4 Anatembea nami sasa, Mwokozi mukubwa!
Ananichunga na salama, Mwokozi mukubwa!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
25. TUNASIFU BWANA YESU
1 Tunasifu Bwana Yesu kwa furaha na kwa nguvu;
Tukijua deni yetu, tujitoe kwake.
2 Tunavikwa na silaha kupigana na Shetani;
Kwa imani tunaweza kumushinda kweli.
3 Tumutegeme-e sana, yeye tu ni mwaminifu;
Kweli kitu hakiwezi kututenga naye.
4 Bwana, utuchunge kwako kwa imani na mapendo
Hata siku ya kuona utukufu wako.
5 Tutakuwa pale kwako, tutapata sura yako,
Vitu tusivyoona bado tutavipokea.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
26. YESU, MWANZO WA UZIMA
1 Yesu, Mwanzo wa uzima, tunaishi kwako, Bwana;
Ulishinda Diabolo, haya, woga, vile kufa.
Ulipita kwa mateso kwa kuturudisha kwako;
:: Mashukuru elfu elfu yawe kwako kwa milele::
2 Bwana Yesu, ulipata fimbo na kuzarauliwa;
Wewe Bwana wa wabwana, walikuvalisha miiba;
Wewe ulituokowa kwa vifungo vya makosa;
::Mashukuru elfu elfu kwako, Bwana na Mwokozi::
3 Walitia haya nyingi ju-u yako, Ee Mwokozi;
Ulitubebea yote kwa kuleta ukombozi.
Kwa uchungu wako, Bwana, tunaweza kuokoka;
::Mashukuru elfu elfu kwako, Bwana na Mwokozi::
4 Sifa ya mioyo yetu tunakupa, Bwana Yesu,
Kwa mateso na mauti uliyopokea yote.
Ulidumu kwa huzuni kwa kutupatia raha;
::Kwa milele tutaimba mashukuru kwako, Bwana::
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
27. NINAHESHIMU YESU KRISTO
1 Ninaheshimu Yesu Kristo kwa uzuri wake;
Mwenye kuva-a taji njema kwa kiti cha ufalme,
Kwa kiti cha ufalme.
2 Na hatuwezi kumufananisha na mwingine;
Anawapita na uzuri watakatifu wote,
Watakatifu wote.
3 Aliniona nikizama ndani ya makosa,
Na alinikomboa mimi kwa musalaba wake,
Kwa musalaba wake.
4 Uzima na furaha yote ananipa bule,
Na ananishindisha sana kwa zambi na kaburi,
Kwa zambi na kaburi.
5 Sababu ananionyesha hivi pendo lake;
Maisha yangu yote pia nitayatoa kwake,
Nitayatoa kwake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
28. TUNAKUSHUKURU, MUNGU
1 Tunakushukuru, Mungu, kwa Mwokozi wetu Yesu,
Na kwa kila neno jema tunalopokea kwako,
Kwa mashamba na mavuno, jua, mvua, na chakula;
Tunakushukuru sana kwa salama toka mbingu.
2 Tunakushukuru vile kwa ruhusa ya kuomba,
Na asante kwa uwezo wa kushinda majaribu,
Kwa ubaya, kwa uzuri, kwa faraja yako tamu,
Na kwa neema bora kwetu, kwa mapendo yako, Mungu.
3 Tunakushukuru sana kwa baraka zako zote,
Na kwa nyumba zetu vile, na jama-a, na rafiki,
Kwa huzuni, kwa furaha, kwa salama nawe, Mungu;
Tunakushukuru sasa kwa taraja ya milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
29. EE MUNGU BABA, NINAKUTUKUZA
1 Ee Mungu Baba, ninakutukuza,
Uaminifu wako ni mukubwa,
Huruma zako hazitapugunka,
Hutageuka hata kwa milele.
Ee wewe Mungu wangu, ni mwaminifu kweli,
Siku kwa siku unanibariki:
Vyote ninavyo uliniletea.
Uaminifu mukubwa wa Mungu.
2 Jua na mvua na mwezi na nyota,
Bonde, milima, mashamba na mito,
Yote inashuhudia pamoja
Uaminifu wa Mungu Mwenyezi.
3 Ulisamehe uovu na zambi,
Na ulinipa salama rohoni;
Wewe mwenyewe unaniongoza,
Shangwe ya kweli unaniletea.
4 Mimi zaifu, unanipa nguvu;
Moyoni mwangu taraja ni tamu;
Siku kwa siku baraka ni nyingi.
Elfu na elfu unanimwangia.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
30. ABUDU MUFALME
1 Abudu Mufalme, mwenye utukufu,
Kwa nyimbo tangaza mapendo wa Mungu;
Ni Mwumba, Mwokozi, Rafiki, Mulinzi;
Tusifu uzuri wa Mungu Mwenyezi.
2 Mwenye nguvu nyingi, mwenye neema vile,
Mwenye kufunikwa kwa macho ya watu.
Ni Mungu muju-u, ni Mungu wa nuru;
Inama kusifu na kumushukuru.
3 Mapendo ya Mungu makubwa kabisa!
Hatuna maneno kwa kuyaeleza;
Pahali po pote tunayatambua,
Na yanazijaza dunia na mbingu.
4 Na vile viumbe tunavyoviona
Vinashuhudia ukubwa wa Bwana;
Musingi wa inchi ni tangu zamani,
Unasimamishwa imara milele
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
31. MUMUKARIBIE MUNGU
1 Mumukaribie Mungu kumusifu na asante ;
Amebarikia shamba, na chakula tumepata;
Mungu wetu anajua mahitaji yetu yote;
Hivi tumwimbie Bwana wimbo wetu wa mavuno.
2 Ulimwengu wetu huu ndio shamba lake Mungu;
Mbegu njema na magugu yanamea kandokando;
Kwanza jani, kisha suke, na nafaka inaota;
Utuchunge, Mungu Baba, sisi ni nafaka yako.
3 Bwana Yesu atakuja, atavuna shamba lake;
Siku ya mavuno yake ataiokota ngano;
Naye atateketeza kila kitu cha uovu;
Ngano njema ataweka na kuchunga kwa milele.
4 Hata hivi kuja, Bwana, kwa kuvuna shamba lako;
Ukusanye watu wako, huru toka zambi zao;
Kule mbingu watu safi wataona uso wako;
Kuja tu na malaika kwa mavuno ndiyo mwisho.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
32. KWA MUNGU MUJU-U
1 Kwa Mungu Muju-u uwe utukufu,
Sababu ya yote aliyoyafanya;
Alitutumia Mwokozi muzuri,
Ndiye Mwana wake kwa ’jili ya zambi
Tutukuze, tutukuze jina la Mungu wetu!
Tutukuze, tutukuze na tumufurahie!
Ee kuja kwa Baba, kwa Yesu Mwokozi,
Na umutukuze, Mukubwa zaidi!
2 Ametukomboa, ametununua
Kwa njia ya damu iliyo damani ;
Mwenye zambi nyingi anayeamini,
Anasamehewa kwa siku yenyewe.
3 Kwa Mungu Muju-u uwe utukufu ;
Tumufurahie kwa jina la Yesu ;
Furaha kuliko tutakuwa nayo
Wakati tutakapomwona na macho.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
33. YESU UNITAZAMISHE
1 Yesu unitazamishe musalaba wako,
Nisikusahau wewe na mauti yako.
Musabala wako, Bwana, ni taraja yangu
Hata nitakapokwenda kupumzika kwako.
2 Nilitetemeka pale, mimi mwenye zambi ;
Kwa mapendo na rehema ulinipokea.
3 Yesu, unilinde huko, unifahamishe
Jinsi ulivyochukua zambi zangu zote.
4 Nitangoja na taraja na imani vile
Hata nitakapokwenda kwako kwa milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
34. TAZAMA YESU NI KONDO-O
1 Tazama Yesu ni Kondo-o kwa musalaba wa Kalvari;
Kwa sisi alimwanga damu kwa musalaba wa Kalvari.
Sauti yake usikie, “Eloi, lama sabaktani!”
Tazama Yesu akikufa kwa musalaba wa Kalvari.
2 Tazama damu inavuja kwa musalaba wa Kalvari;
Kutoka mbavu na mikono kwa musalaba wa Kalvari.
Halafu giza kubwa sana lilitokea kwa dunia,
Mwokozi alikufa pale kwa musalaba wa Kalvari.
3 Na sasa kazi imekwisha kwa musalaba wa Kalvari;
Alizishinda zambi zote kwa musalaba wa Kalvari.
Na sasa njia kwake Mungu ni wazi kwa wenye imani,
Kwa maana Yesu alikufa kwa musalaba wa Kalvari.
4 Alifufuka, alikwenda kwa Baba yake kule mbingu;
Na anaketi kwa kuume ya Baba yake kule mbingu.
Tunainama kumwabudu, Heshima kwako, Ee Kondo-o!
Yesu, pokea sifa zetu, wewe Mwokozi kule mbingu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
35. BWANA, MUFALME WA UZIMA
1 Bwana, Mufalme wa uzima, walikuvika taji;
Nisisahau miiba ile uliyova-a kwami.
Nisisahau Get’semane, nisisahau musalaba,
Nisisahau pendo lako na taabu kwa Kalvari.
2 Uniongoze kwa kaburi lililo wazi sasa,
Pahali ulipofufuka na ulishinda kufa.
3 Kama Maria na zawadi ninainama kwako,
Kukuonyesha pendo langu; uipoke-e, Bwana.
4 Niwe tayari kukufuata na musalaba wangu,
Ili nijue ushirika wa taabu ya Kalvari.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
36. YESU MWOKOZI WETU MWEMA
1 Yesu Mwokozi wetu mwema, yeye muzuri wa kupita;
Mungu mukamilifu ndiye Yesu Mwokozi wa Kalvari.
Mwokozi wa Kalvari, namupa roho yangu;
Alinikufilia, mwenye kubarikiwa!
2 Ali-ikunywa kopo tele ya matukano, taabu vile;
Alilipia zambi zote, Yesu Mwokozi wa Kalvari.
3 Mwenye makosa anaweza sasa kupata usamehe;
Alimimia damu yake, Yesu Mwokozi wa Kalvari.
4 Anafariji roho yangu, siku nyingine nitamwona;
Nitatukuza na shuk’rani Yesu Mwokozi wa Kalvari.
5 Tutakutana kule mbingu kwa kulisifu pendo lako;
Tutafanana nawe pale, Yesu Mwokozi wa Kalvari.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
37. PENDO LILIKUSUKUMA
1 Pendo lilikusukuma, Yesu, kutukufilia;
Ulitubebea taabu, haya kwa makosa yetu.
Kisha ulifufuliwa, ulishinda kufa kweli;
Na watakatifu wote watashinda kwa milele.
2 Sasa umekwenda mbingu, taabu zako zimekwisha;
Makusudi yake Baba uliyatimiza pia.
Sisi ni Kanisa lako, unatuombea sana,
Na kututengenezea pa’li petu kule kwako.
3 Sasa sisi wana wako, kwa sababu yake Roho,
Tunalia, Aba, Baba, bila haya, bila woga.
Deni yetu ya mapendo kwako iko kubwa sana,
Tumekutambua wazi, wewe Bwana wa salama.
4 Ni furaha kukusifu, unayetukuzwa ju-u,
Unatuonyesha wazi roho yako ya mapendo.
Ee pokea kuabudu kwa mioyo yetu yote,
Kwani ulimwanga damu ili sisi tuokoke.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
38. EE SALAMA YA MILELE
1 Ee salama ya milele inatoka Baba Mungu;
Ni salama ya kujua Yesu ni Mwokozi wangu.
2 Kwangu ni salama sasa kwa sababu yake Yesu,
Alimwanga damu yake kuondoa zambi zangu.
3 Alikufa kuonyesha ana haki na mapendo,
Na kuleta wenye zambi njia kuingia mbingu.
4 Tunakuabudu, Kristo, wewe Mwana wake Mungu.
Na tunakusifu, Bwana, umeshinda zambi zote!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
39. EE NINI, MUNGU WETU
1 Ee nini, Mungu wetu, ilikuvuta wewe
Kwa ’jili ya makosa kutoa Mwana wako?
Mapendo tu yalikuvuta kwa kutoa Mwana wako,
Kwa kutuo Mwana wako.
2 Ee nini, Bwana Yesu, ilikuleta hapa
Kumwanga damu yako, kupata maumivu?
Mapendo tu yalikuleta kwa kumwanga damu yako,
Kwa kumwanga damu yako.
3 Kwa nini, Mungu wetu, ulimutuma Roho
Ajaze roho zetu na pendo na salama?
Mapendo tu yalitumia watu wako Roho yako,
Watu wako Roho yako.
4 O tutakupa nini kwa neema yako kubwa?
Tuzidi kwa milele kusifu jina lako!
Na sasa tunakuabudu kwa mapendo yako, Mungu,
Kwa mapendo yako, Mungu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
40. NI TAMU SANA JINA LA MWOKOZI
1 Ni tamu sana jina la Mwokozi Yesu Bwana,
Linafariji kwa huzuni, na kutoa woga.
2 Linaponyesha roho inayoumia sana,
Ni mana kwa kulisha roho, na kuleta raha.
3 Ni Mwamba wetu tunaosimama ju-u yake,
Na ngabo na pahali pa maficho vilevile.
4 Mwokozi, Muchungaji, na Rafiki na Kuhani,
Uzima wetu, Njia, Kweli, sifa nyingi kwako.
5 Zaifu sisi na baridi mioyoni mwetu,
Lakini sifa za kufa-a utazipata mbingu.
6 Kutoka sasa tutapasha pendo lako kubwa ;
Kwa jina lako kufa na kaburi tutashinda.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
41. YESU, YESU, YESU, JINA TAMU SANA
1 Yesu, Yesu, Yesu, jina tamu sana,
Linawasha roho na kuleta raha.
2 Yesu, Yesu, Yesu, anatoa zambi;
Yesu, jina zuri linatufariji.
3 Yesu, Yesu, Yesu, nguvu analeta,
Vile uhodari kwa kushinda vita.
4 Yesu, Yesu, Yesu, jina la kushinda
Majaribu yote hapa kwa dunia.
5 Yesu, Yesu, Yesu, ni furaha kwetu
Kwa maisha yote, vile kule mbingu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
42. MWOKOZI WETU NA MUPENZI
1 Mwokozi wetu na Mupenzi, uliyetupenda,
Ulijitoa kwa ajili yetu wenye zambi.
2 Tunakupenda sana kwani ulipenda kwanza ;
Mbinguni uliacha yote kwa kufika hapa.
3 Na ulika-a pale ju-u sawa na Mungu Baba ;
Ulijinyenyekeza sana kututumikia.
4 Ulikubali kukamata sura yetu, Yesu ;
Nawe ulifanyika mwili, wewe ndiwe Mungu.
5 Kwa hivi tutaonekana kama wewe, Yesu;
Na tutakuwa wenye haki mbele yako ju-u.
6 Hakose kwa rafiki yetu sisi tutakufa,
Lakini ulikufa kwa wenye kukuchukia.
7 Tunakumbuka pendo lako kubwa sana kwetu,
Linalopita na zaidi pendo letu, Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
43. KWA KILIMA CHA KALVARI
1 Kwa kilima cha Kalvari, akiteswa– yeye nami?
Kichwa chake na migu-u na mikono ni michungu.
Mbele alikuwa ju-u na furaha kule mbingu,
Mwana wake Mungu, ndiye kule kwa Kalvari– pekee.
2 Kwa kilima cha Kalvari, akifungwa– yeye nani?
Watu wakimuzihaki, wakisema: “Shuka chini!”
Yeye alifika hapa na mapendo na baraka,
Mwana wake mutu, ndiye kule kwa Kalvari – pekee.
3 Kwa kilima cha Kalvari, akikufa– yeye nani?
Kwa ajili ya makosa yetu-si makosa yake.
Alilipa bei ya zambi, ni sadaka ya ahadi,
Ni kondo-o wetu, ndiye kule kwa Kalvari – pekee.
4 Kule mbingu ni Mufalme, Mushindaji – yeye nani?
Alikufa kwa dunia, bali juu anatukuzwa .
Ee tunainama kwake, anayestahili kweli,
Bwana wa wabwana ndiye, na Mufalme wa wafalme!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
44. “MUTU WA MASIKITIKO”
1 “Mutu wa masikitiko”, jina gani kwa Mwokozi,
Aliyetukufilia! Haleluya, Bwana Yesu!
2 Sisi watu wa uchafu, yeye Mungu mwenye haki,
Alitutafuta sisi; Haleluya, Bwana Yesu!
3 Aliacha Baba yake, akakuja duniani,
Akapata taabu nyingi; Haleluya, Bwana Yesu!
4 Watu walimuzihaki, wakamupatisha haya,
Wakamuhukumu bule; Haleluya, Bwana Yesu!
5 Yesu alisulibishwa, akalia: “Imekwisha,”
Alilipa zambi zote; Haleluya, Bwana Yesu!
6 Atarudi kama Bwana na Mufalme wa wafalme,
Tutaimba kwa furaha, Haleluya, Bwana Yesu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
45. KUKUFIKILI WEWE, YESU
1 Kukufikili wewe, Yesu, iko kutamu kwangu;
Zaidi kukuona wewe, na kupumzika kwako.
2 Hakuna jina tamu sana kuliko lako, Yesu;
Inatushinda kufahamu uziri wako wote.
3 Taraja kwa wenye kutubu na wenye kuanguka,
Unawahurumia wote wanaokutafuta.
4 Inatushinda kueleza mapendo yako, Bwana;
Na ni wapenzi wako tu wanaoyafahamu.
5 Wewe furaha yetu pekee na taji yetu vile,
Na utukufu wetu, Bwana, sasa na kwa milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
46. PENDO LAKO, BWANA YESU
1 Pendo lako, Bwana Yesu, linapita kila pendo;
Ni furaha ya mbinguni, ni furaha yetu huko.
Yesu, wewe mwenye neema, vile mwenye pendo kubwa,
Utukaribie sasa, uingie roho zetu.
2 Yesu, sasa utujaze roho zetu na mapendo;
Tunapata ndani yako yote tunayohitaji.
Uondoshe zambi zote tusizitamani tena;
Tukikuamini kweli, tunapata kuwa huru.
3 Tunaomba utujaze na uzima wako, Bwana;
Sisi ni hekalu lako, na huwezi kutuacha.
Tuna hamu ya kupata kukutumikia hapa,
Kukusifu sikuzote kama jeshi la mbinguni.
4 Umalize kazi yako, utukamilishe sisi;
Tukikutazama sana, tufanane nawe, Bwana,
Toka utukufu hata utukufu wake Mungu,
Hata tunafika mbingu mbele yako kuabudu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
47. NAJUA JINA MOJA ZURI
1 Najua jina moja zuri kuliko kila jina huko,
Kuniletea raha tamu, ni jina hili, Yesu.
Yesu, jina zuri sana! Yesu, sikuzote sawa!
Yesu, tumwabudu sasa na kumwimbia sifa.
2 Napenda jina hili jema, linanivuta kwake Mungu,
Kwa saa ya taabu na huzuni linafariji sana.
3 Siwezi mimi kueleza uzuri wake jina hili,
Lakini nitaimba sifa kwa jina lake Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
48. INATUSHINDA KUFAHAMU
1 Inatushinda kufahamu mapendo yake Mungu kwetu,
Mapendo haya yanapita mapendo yetu sisi watu.
Alimutuma Bwana Yesu kutoka kwake mbinguni
Kututafuta, wenye zambi, tupate kusamehewa.
Inatushinda kufahamu mapendo haya makubwa,
Lakini tunajua kweli yatabakia daima.
2 Hata miaka inapita, vizazi vinakombolana,
Na hata watu wa dunia wanakata-a kuamini,
Mapendo ya Mungu ni sawa, makubwa sana na nguvu,
Tayari kuokoa wote wanaotubu makosa.
3 Ee Mungu mwenye pendo kubwa, unifundishe kukupenda,
Nipende vile watu wote na pendo unaonipenda.
Nataka sana, Bwana Yesu, mapendo yako makubwa
Yanisukume kukufuata, kukupendeza daima.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
49. EE BABA, NITAKUWA KAMA YESU
1 Ee Baba, nitakuwa kama Yesu,
Baraka ile alinipatia!
Ni mushangao na ajabu pia,
Kwa sura yake atanigueza.
2 Ee Bwana Yesu, nani kama wewe
Alinipenda hata nitazame
Milele utukufu wako, Kristo,
Mimi zawabu ya mateso yako?
3 Mapendo yako hayakustarehe
Mbele ya kubariki wana wako;
Yanashiriki vitu vyote nasi,
Hata uriti wako, Bwana Yesu.
4 Wapenzi wako wote kwa milele
Kwa utukufu watakusanyika,
Na kwa furaha watakuzunguka,
Kukuabudu na kukutukuza.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
50. NAPENDA KUSIKIA JINA LA BWANA
1 Napenda kusikia jina la Bwana Yesu Kristo,
Ni kama wimbo tamu sana kuliko kila jina.
2 Linaonyesha pendo lake aliyenikufia,
Na damu yake ya damani iliyonikomboa.
3 Linanifurahisha roho, machozi yanakwisha,
Na linaniambia kwamba: “Usiogope kamwe.”
4 Pamoja na waamini wote, wenye kuokolewa,
Nitamwimbia Yesu sifa mbinguni kwa milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
51. JINA LA PENDO KUBWA
1 Jina la pendo kubwa, Yesu Mwokozi,
Linalopita yote, Yesu Mwokozi;
Sisi hatuna kitu kukupendeza, Mungu.
Sharti utupe yote, Yesu Mwokozi.
2 Ulifanyika mwili, Yesu Mwokozi,
Na ulitoa damu, Yesu Mwokozi;
Ulilishuhudia pendo lililo kubwa
Kuliko pendo lote, Yesu Mwokozi.
3 Na kwako tuna haki, Yesu Mwokozi,
Makimbilio yetu, Yesu Mwokozi;
Hatuna woga mwingi wa taabu na huzuni,
Kwako tunafichama, Yesu Mwokozi.
4 Utarudia tena, Yesu Mwokozi,
Kwa kutimiza raha, Yesu Mwokozi;
Bwana, tutakuona, halafu tutakuwa
Sawa nawe milele, Yesu Mwokozi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
52. EE BWANA, ULIVUMILIA
1 Ee Bwana, ulivumilia hukumu, mauti kwa mimi,
Kwami ulipata huzuni, mateso na miiba Kalvari;
Na uli-ibeba azabu niweze kupata uhuru;
Milele nitakushukuru, Mwokozi na Bwana Mupendwa.
2 Ulivumilia laumu, zarau na vile zihaka,
Mapigo na haya, mateso, na mate ya wenye makosa;
Kulipa makosa kwa mimi, ulisulibishwa, Ee Bwana;
Milele nitakushukuru, Mwokozi na Bwana Mupendwa.
3 Ee Bwana, ninakushukuru kwa yote uliyoyabeba,
Mauti na giza na taabu, niweze kupata uzima,
Na vile nishinde milele nawe kule kwa utukufu;
Milele nitakushukuru, Mwokozi na Bwana Mupendwa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
53. TUNAPENDA SAA HII TAMU
1 Tunapenda saa hii tamu kukumbuka musalaba
Wa Mwokozi wetu Yesu, sisi watu wa makosa.
2 Ustarehe tunapata kwa zabihu yetu Yesu,
Alitukomboa sisi, alilipa deni zetu.
3 Hapa mbingu ni karibu tunapotazama Yesu,
Kwani alitusamehe, yeye ndiye mwaminifu.
4 Na imani tunafika mbele ya Mwokozi Yesu;
Bwana nasi ni mumoja na hatutatengwa naye.
5 Twende kwake kwa akili, tufahamu nia yake,
Tujifunze sikuzote neema na rehema zake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
54. KWAKO PEKEE, BWANA, NI SALAMA TAMU
1 Kwako pekee, Bwana, ni salama tamu.
Unajua taabu ya mioyo yetu;
Ulitoka mbingu kwa kutuokoa,
Uliteswa sana kwa wenye makosa.
Si rafiki hapa, Bwana, kama wewe,
Kwa wenye huzuni hatuna mwingine.
2 Watu wa huzuni waje kwake Kristo,
Atatoa taabu, zambi, na mizigo;
Yesu anaita: ‘‘Muje kwangu sasa,’’
Kuna ustarehe tamu kwa mioyo.
Si rafiki hapa, Bwana, kama wewe,
Kwa mwenye mizigo hatuna mwingine.
3 Hata mali yote ya dunia huko
Haileti raha kwa mioyo yetu;
Wewe, Bwana Yesu, unatuletea
Kufurahi sana, raha na salama.
Si rafiki hapa, Bwana, kama wewe,
Kwa roho ya kiu hatuna mwingine.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
55. NINAPO-ONA MWOKOZI WA WATU
1 Ninapo-ona Mwokozi wa watu
Kwa musalaba wa haya na taabu,
Ninahesabu faida yo yote
Kuwa hasara kwa ’jili yake.
2 Nisijisifu kwa kitu kingine,
Ila kwa kufa kwa Kristo Mwokozi;
Vyote nilivyovipenda zamani,
Ninavitoa kwa damu yake.
3 Ona machapa kwa mbavu ya Kristo,
Na kwa mikono na vile migu-u ;
Yanaonyesha mapendo ya Mungu
Aliyokuwa nayo kwa watu.
4 Na kama ningalipata dunia,
Ndogo kabisa–zawadi kwa Bwana;
Kwa pendo hili nitamutolea
Roho, maisha, na vitu vyote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
56. MUFALME WA UTUKUFU
1 Mufalme wa utukufu, tunakuabudu sasa,
Na tunainama kwako, unapita wote pia!
Tunakutukuza wewe, njia zako nzuri zote!
2 Mufalme wa utukufu, Bwana ya viumbe vyote,
Ulikataliwa hapa hata na taifa lako;
Sasa tunakuheshimu wewe, mwenye utukufu.
3 Bwana wa uzima wetu, ulibeba taabu zetu,
Mupenzi wa Baba yako, Ee uliumia sana;
Tunakukumbuka wewe, na kusifu jina lako.
4 Kristo, utavikwa taji na mavazi ya kifalme,
Na tunakushuhudia kwamba wewe ni Mufalme;
Ee tunakunyenyekea, Kristo, Bwana kwa milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
57. NINATIMIA NDANI YAKO
1 Ninatimia ndani yako na ninapata haki kwako;
Mauti yako, Bwana Yesu, ililipia deni yangu.
Ninatakaswa nawe, Bwana, na ninahesabiwa haki;
Kwa damu ulinisamehe, na utanitukuza vile.
2 Ninatimia ndani yako, makosa hayatatawala
Katika moyo wangu tena, uwezo wako umeshinda.
3 Umetimiza mahitaji ya roho yangu, Bwana Yesu;
Ee wewe unafaa kabisa, sitahitaji kitu tena.
4 Wachaguliwa siku moja watakutana kwako, Bwana,
Na nitakuwa pale vile, nikitimia ndani yako.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
58. EE KRISTO, KWAKO ROHO YANGU
1 Ee Kristo, kwako roho yangu inakuta raha;
Salama niliyotafuta nimepata sasa.
Ee Kristo, wewe unafa-a kupumzisha roho;
Salama, shangwe, na mapendo ninapata kwako.
2 Nilitafuta raha pekee, sikukutafuta;
Nilipopita, pendo lako lilinikamata.
3 Nilijaribu upendezi wote wa dunia,
Lakini sikupata ustarehe na furaha.
4 Kipofu mimi, sikuona macho yako, Bwana,
Lakini sasa wema wako wazi ninaona.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
59. NAFSI YANGU, ANGALIA YESU
1 Nafsi yangu, angalia Yesu Mukombozi wako;
Yeye ni kwa utukufu, mbali na makosa yote.
2 Anaketi kule mbingu, haki yake inanga-a;
Anaionyesha damu, bei ya ukombozi wetu.
3 Alibeba zambi zote kwa kilima cha Kalvari,
Na hukumu imepita, Ee furaha kubwa sana!
4 Sasa Mungu anataka sisi tuwe kwake mbingu;
Anatutengenezea vitu vyote taratibu.
5 Neno hili, “kwa milele”, ni baraka ya kuzidi,
Wala kitu hakiwezi kututenga na Mwokozi.
6 Tumusifu Bwana wetu, sisi ni watoto wake;
Tutaimba kwa milele, na tutafurahi kwake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
60. REHEMA YA KUHANI WETU
1 Rehema ya Kuhani wetu tunaikumbuka,
Na moyo wako unajaa na pendo kubwa sana.
2 Anafahamu majaribu, uzaifu wetu,
Sababu alijaribiwa kama sisi watu.
3 Makosa hayakuchafua Mukombozi wetu;
Kondoo mutakatifu, yeye ni sadaka yetu.
4 Wakati alipotembea hapa kwa dunia,
Machozi mengi alitoa – anajua yetu.
5 Tukaribie kiti cha ne-ema bila woga,
Tupate neema kusaidia saa ya mahitaji.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
61. KWA KONDO-O TUNAPUMZIKA
1 Kwa Kondo-o tunapumzika, kwa mapendo ya mushangao;
Zambi zetu alisamehe, damu yake ilizitoa.
2 Sasa roho zetu za woga zinajazwa na raha tamu;
Mungu Baba alipendezwa na sadaka ya Yesu Mwana.
3 Sasa woga hauko tena kwani damu ya Bwana Yesu
Mara moja iliondoa zambi zote kwa roho yangu.
4 Ninajazwa na raha tamu na ningali kwa ulimwengu;
Kisha ngambo kwa utukufu nitakuta raha yenyewe.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
62. EE MUNGU NDIYE NGUVU YETU
1 Ee Mungu ndiye nguvu yetu, raha, na taraja,
Anachungaga watu wake sasa na milele.
2 Na hata mbele ya milima Mungu alikuwa;
Uwezo wake uliumba vyote duniani.
3 Miaka elfu ni kwa Mungu kama siku moja;
Milele Mungu yuko sawa, jana, leo, kesho.
4 Ee Mungu, Musaidizi wetu, tumaini vile,
Utuongoze hata mwisho wa safari yetu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
63. EE BWANA YESU, MWUMBA WA DUNIA
1 Ee Bwana Yesu, Mwumba wa dunia,
Mwana wa Mungu na mutu vile,
Ninakupenda, ninakusifu,
Wewe furaha yangu pia.
2 Shamba na mwitu, yote ni mizuri,
Lakini unaipita mbali;
Wewe ni mwema, mutakatifu,
Unayenipa shangwe kubwa.
3 Jua na mwezi inanga-a sana,
Pamoja na nyota za mbinguni;
Uzuri wako na utukufu
Unatushinda kufahamu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
64. KAMA ULIVYOAGIZA, BWANA
1 Kama ulivyoagiza, Bwana, ninafika meza yako
Kwa kukumbuka kufa kwako kwa mimi mwenye zambi.
2 Mwili wako uliovunjika ni mukate wa uzima,
Na damu iliyomwangika, agano jipya kwami.
3 Nikiona musalaba wako kwa kilima cha Kalvari,
Nakukumbuka na sadaka uliyonitolea.
4 Ninakukumbuka na mateso uliyoyabeba kwami;
Ningali na maisha yangu nitakusifu wewe.
5 Hata saa midomo yangu hii itakapofungwa kimya,
Nitatangaza kufa kwako, na utanikumbuka.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
65. KWA MUKATE NA KWA MVINYO
1 Kwa mukate na kwa mvinyo, arabuni yake Roho,
Kwa maneno ya mapendo, tunakusifu, Bwana.
2 Mvinyo na mukate vile ni mufano wa mauti
Ya Mwokozi wetu mwema ; tunakusifu, Bwana.
3 Kwa maneno ya Kitabu ya kutuonyesha Yesu,
Na kutukokota kwake, tunakusifu, Bwana.
4 Kwa habari za mbinguni na kwa ufufuko wetu,
Na kukaa karibu nawe, tunakusifu, Bwana.
5 Huu mukate ni mufano wa Mwokozi akikufa,
Hakushindwa na mauti; tunakusifu, Bwana.
6 Na kikombe ni mufano wa kutukumbusha damu
Uliyoimwanga yote, tunakusifu, Bwana.
7 Na kwa siku ya furaha utakaporudi kwetu
Kwa kupata utukufu, tunakusifu, Bwana.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
66. TUNAZUNGUKA MEZA
1 Tunazunguka meza na Yesu katikati,
Kwa Kristo wote ni mumoja, hata sisi wengi.
2 Kwa zambi zetu Yesu alitukufilia,
Na tulikufa ndani Yake na tulifufuka.
3 Mukate na kikombe tunakamata sasa;
Tunapumzika kwa kifua cha Mwokozi Bwana.
4 Tutatawala naye Mufalme Yesu Kristo;
Tutafurahi kwa karamu, ndoa ya Kondoo.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
67. TUNAZIKWA KWA KABURI LA MWOKOZI
1 Tunazikwa kwa kaburi la Mwokozi Yesu Bwana;
Mungu anatuhesabu kuwa wafu kwa makosa.
2 Kufa na hukumu vile haziwezi kutugusa;
Bwana alibeba yote, nguvu yao amemaliza.
3 Yesu alifufuliwa toka wafu, yeye kwanza;
Nasi tumeumbwa tena, sisi ni wahuru sasa.
4 Ubatizo tunapa, sura ya mauti yake ;
Na tunafufuka naye, ndani yake tunakaa.
5 Tunangoja ukombozi wa mi-ili yetu vile ;
Atatugeuza pia kufanana naye Yesu.
6 Bwana, sasa tunataka kushiriki haya yako;
Mungu atatupokea, kwani tuko ndani yako.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
68. ULIAGIZA, YESU BWANA
1 Uliagiza, Yesu Bwana, na ninazikwa kwa mufano,
Hivi ninatangaza wazi mimi ni mutu wako sasa.
2 Ninakutii kwa neno hili, ninakunyenyekea hivi,
Kwani nataka kukufuata hata katika ubatizo.
3 Huu ni mufano wa kaburi ulipozikwa ndani yake;
Niki-ingia, natambua bei kubwa ya wokovu wangu.
4 Ninapotoka, ni mufano wa ufufuko wako, Bwana,
Na nitaishi mutu mupya, mimi si tena wa dunia.
5 Nijihesabu kuwa mufu kwa zambi zilizoku-ua,
Mufu kwa mambo ya dunia yasiyokupendeza, Bwana.
6 Ninapokutazama, Bwana, na utukufu wako wote,
Ninahesabu haya bule ninayobeba kwawe hapa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
69. TANGAZA NENO HILI
1 Tangaza neno hili dunia isikie
Mwokozi ametuma Musa-idizi kwetu;
Wakristo pa’li pote wafarijiwe naye.
Musa-idizi yuko!
Musa-idizi yuko, Musa-idizi yuko,
Ni Roho yake Mungu aliyetumwa kwetu;
Ahadi yake nzuri inatimia kweli,
Musa-idizi yuko!
2 Kumbuka Roho huyu aliyetumwa kwetu
Anatukuza Yesu katika roho zetu;
Na anawaongoza wenye kupenda Bwana,
Musa-idizi yuko!
3 Anatufunulia habari za maneno
Yatakayotokea kwa mwisho wa dunia;
Anayasema yote anayoyasikia,
Musa-idizi yuko!
4 Na nina Roho huyu katika moyo wangu,
Ananifahamisha maneno yake Yesu;
Ninashanga-a sana kwa neema yake Bwana ,
Musa-idizi yuko!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
70. MWOKOZI ALIAHIDIA
1 Mwokozi aliahidia wanafunzi wake
Kutuma Musaidizi kwao toka mbingu.
2 Kwa hivi Roho alikuja, naye anapanga
Katika roho ya mwenye unyenyekevu.
3 Katika kweli yote ana’ngoza wa-amini,
Maneno yale anayosikia kwake.
4 Anatukuza Yesu, naye anatutagaza
Habari za maneno yatakayokuja.
5 Matunda yake Roho ni mapendo na furaha,
Salama, neema, wema, na uaminifu.
6 Ee utujaze Roho yako, Mungu, tunaomba,
Apange kwetu kubakia sikuzote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
71. MANENO YA MUNGU NI TA-A
1 Maneno ya Mungu ni ta-a na nuru kwa njia yangu,
Kwa kunisafisha kwa zambi na kuniongoza kwake.
Nimeficha Maneno ya Mungu
moyoni nisimukose-e,
Nisimukose-e, nisimukose-e,
Maneno ya Mungu moyoni.
2 Milele Maneno ya Mungu yanasimamishwa juu;
Yanatufundisha kujua Mwokozi ni mwaminifu.
3 Mapema, saa sita, usiku, nisifu Mwokozi wangu,
Sababu maneno matamu yananipatisha nguvu.
4 Biblia inatuambia Mwokozi ni Yesu Kristo;
Anawaletea wokovu wanaopotea mbali.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
72. BIBLIA INASIMAMA SANA
1 Biblia inasimama sana kama mwamba wa imara;
Katika Biblia tunapata Neno la Mungu wa milele.
Biblia inasimama sana, haitapunguka hata milele,
Na nitasimama kwa mambo yote ju-u ya Biblia.
2 Biblia inasimama sawa na mulima ju-u sana,
Na watu hawataweza kweli kuishinda na nguvu yao.
3 Biblia inasimama sana, kwa milele itashinda;
Sababu Mungu aliandika ndani yake sheria zake.
4 Biblia inasimama kwani ni Kitabu chake Mungu;
Nita-amini na nitadumu kuitii kwa maisha yangu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
73. NENO TAKATIFU SANA NI BIBLIA
1 Neno takatifu sana ni Biblia yake Mungu,
Nikisoma ndani yake inanifundisha sana.
2 Inanikemea vile ninapotembea mbali;
Inanionyesha njia, na mapendo ya Mwokozi.
3 Inanifariji mimi ninaposumbuka sana;
Niki-iamini kweli nitashinda hata kufa.
4 Inaniambia wingi wa furaha ya mbinguni;
Ninapenda Neno hili, ni hazina ya damani.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
74. NI NEEMA YA KUNISHANGAZA
1 Ni neema ya kunishangaza iliyoniokoa ;
Nilipotea, lakini Yesu alinivuta kwake.
2 Hukumu ya Mwamuzi Mungu niliogopa sana,
Lakini sasa, kwa neema yake, sitaogopa tena.
3 Katika majaribu mengi nimesimama nguvu ;
Kwa neema yake alinichunga, hataniacha kamwe.
4 Tutashukuru Mungu wetu milele na milele
Kwa neema kubwa tuliyo-ona katika Mwana wake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
75. MUNGU ALIPOSIFIWA MBINGUNI
1 Mungu aliposifiwa mbinguni,
Zambi ilipoijaza dunia,
Yesu alitoka muji wa Baba
Awe Mwokozi kwa wenye makosa.
Alinipenda, kunikufia,
Na alizikwa katika kaburi;
Alifufuka na kuniokoa;
Atarudia – Ee siku ya shangwe!
2 Watu walimupeleka Kalvari,
Kwa misumari walimutoboa;
Walizihaki na walizarau
Mwenye kubeba makosa ya watu.
3 Kufa hakuweza kumuzuiza
Mwana wa Mungu katika kaburi;
Alifufuka kwa siku ya tatu,
Yeye Mushinda na Bwana ya yote!
4 Atarudia katika mawingu
Kwa kukamata wenye kumwamini;
Tutafurahi kuona Mwokozi
Na tutaishi naye kwa milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
76. NINA NENO TOKA BWANA
1 Nina neno toka Bwana, Haleluya!
Na neno hili nitakupa;
Ma-andiko ya Kitabu, Haleluya!
Yanasema: “Utazame Yesu.”
Utazame Yesu, ndugu, utazame Yesu sasa;
Ma-andiko ya Kitabu, Haleluya!
Yanasema: “Utazame Yesu.”
2 Nina neno la mapendo, Haleluya!
Ni neno, Ee rafiki, kwawe;
Na ni neno toka ju-u, Haleluya!
Yesu Kristo alisema kweli.
3 Na uzima utapata, Haleluya!
Uzima wa milele, ndugu;
Utazame Yesu sasa, Haleluya!
Yesu pekee atakuokoa.
4 Ninaweza kuhubiri, Haleluya!
Habari ya wokovu wangu,
Kuamini jina lake, Haleluya!
Nimepata kwake tu uzima.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
77. DUNIA ’NALALA
1 Dunia ’nalala kwa giza la zambi,
Nuru ni Yesu pekee;
Mwenye utukufu anatuangaza,
Nuru ni Yesu pekee.
Kuja kwa Nuru, anakuita,
Nimeipata kwa roho yangu;
Mimi kipofu, sasa naona
Nuru ni Yesu pekee.
2 Hatutatembea kwa giza kabisa,
Nuru ni Yesu pekee;
Sababu tunafuata Yesu Mwokozi,
Nuru ni Yesu pekee.
3 Kwa wenye makosa, wenye kupotea,
Nuru ni Yesu pekee;
Kwendeni kuoshwa na damu ya Yesu,
Nuru ni Yesu pekee.
4 Hawana hitaji la jua mbinguni,
Nuru ya mbingu Yesu;
Kondo-o wa Mungu ni nuru ya muji,
Nuru ya mbingu Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
78. MWOKOZI WANGU ALINIMWANGIA DAMU
1 Mwokozi wangu alinimwangia damu yake;
Kwa mwenye zambi, mwenye haki alitoa mwili.
Kule kwa musalaba wa Yesu Mwokozi
Niliacha zambi zangu kabisa;
Nilimupokea na nimeokoka,
Na sasa furaha inazidi.
2 Makosa yangu yalifunga Yesu kwa Kalvari;
Huruma na mapendo yake ni makubwa kweli.
3 Na giza lilificha Yesu pale kwa Kalvari :
Ajabu kubwa, Mwumba wangu alikufa kwami!
4 Siwezi kulipia deni kwa huzuni yangu,
Lakini nitatoa vyote kwa Mwokozi wangu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
79. MOYO ULIGEUZWA NA VILE MAISHA
1 Moyo uligeuzwa na vile maisha, saa Yesu alipoingia;
Nikapata uwezo na nuru moyoni, saa Yesu alipoingia.
Saa Yesu alipoingia, saa Yesu alipoingia,
Haleluya kwa Yesu Mwokozi pekee,
Aliniokoa kabisa!
2 Niliacha makosa na njia ya zambi, saa Yesu alipoingia;
Naye alisamehe na alisafisha, saa Yesu alipoingia.
3 Nilipata salama iliyo ya mbingu, saa Yesu alipoingia;
Woga uliniacha na shaka njiani, saa Yesu alipoingia.
4 Nilipata taraja ya kwenda mbinguni, saa Yesu alipoingia;
Na furaha ilijaza roho kabisa, saa Yesu alipoingia.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
80. EE SIKU YA KUOKOLEWA
1 Ee siku ya kuokolewa ni kweli siku ya furaha ;
Kwa neema na mapendo kwangu, aliondoa zambi zangu.
Siku kubwa ya furaha, mimi ni mutu wake sasa,
Ndiye anayeniongoza
kumwangalia na kumwomba.
Siku kubwa ya furaha, mimi ni mutu wake sasa.
2 Sitapotea tena kamwe, ananiita mwana wake.
Alinivuta kwa mapendo, nifuate mwito wake pekee.
3 Na tumekwisha kupatana; mimi ni wake, yeye wangu.
Ninamushuhudia Yesu; nitamutii, nitamufuata.
4 Furaha yake ninapata, ananijaza raha sasa.
Hakuna kitu wala mutu anayeweza kunitenga.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
81. NILIPOFIKA KWA MUSALABA
1 Nilipofika kwa musalaba,
nikanyanyua sauti yangu:
“Yesu Mwokozi, unirehemu!” Akaniokoa.
Yesu asifiwe, Yesu asifiwe!
Alisikia kilio changu, Yesu asifiwe!
2 Nilipofika kwa Bwana Yesu,
nikamusihi Mwokozi wangu:
“Unitakase, unisafishe!” Akanisikia.
Yesu asifiwe, Yesu asifiwe!
Alisikia maombi yangu, Yesu asifiwe!
3 Ona kisima cha musalaba,
leo kingali cha nguvu sawa
Kukuokoa na kusafisha, Yesu asifiwe!
Yesu asifiwe, Yesu asifiwe!
Kukuokoa na kusafisha, Yesu asifiwe!
4 Kuja kuoshwa katika maji
yaliyo damu ya Yesu Kristo;
Umusadiki, utatimizwa, Yesu asifiwe!
Yesu asifiwe, Yesu asifiwe!
Umusadiki, utatimizwa, Yesu asifiwe!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
82. YESU KWA MUJI WA BETELEHEMU
1 Yesu kwa muji wa Betelehemu
Alizaliwa katika ta-abu;
Ninashangaa sababu Mwokozi alitafuta mimi.
Alitafuta mimi, alitafuta mimi,
Ninashangaa sababu Mwokozi alitafuta mimi.
2 Yesu Mwokozi, zamani Kalvari
Deni ya zambi alinilipia;
Kuniletea uhuru wa kweli alinikufilia.
Alinikufilia, alinikufilia,
Kuniletea uhuru wa kweli alinikufilia.
3 Yesu Mwokozi alinikumbuka
Nami ningali tu mbali na Baba,
Na sikuzote alinitafuta, akini-ita mimi.
Akini-ita mimi, akini-ita mimi,
Na sikuzote alinitafuta, akini-ita mimi.
4 Yesu Mwokozi aliniahidi
Atarudia kutoka mbinguni,
Na nitamwona katika mawingu, atanitwa-a kwake.
Atanitwa-a kwake, atanitwa-a kwake,
Na nitamwona katika mawingu, atanitwa-a kwake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
83. NILIZAMA KWA MAKOSA
1 Nilizama kwa makosa, katika maji ya zambi;
Roho yangu iliona kufa na giza tele;
Mungu alinisikia nilipomulilia,
Akanipandisha na kuniokoa.
::Nimeokoka, nimeokoka,
Kwa Yesu Mukombozi nimeokoka::
2 Sasa Yesu amekuwa Makimbilio yangu;
Pendo lake kubwa sana liko moyoni mwangu;
Neema yake ya kuzidi inanijaza roho;
Niwe mwaminifu kwake siku zote.
3 Nawe mwenye sikitiko, kuna matumaini;
Yesu anakufahamu na atakusaidia;
Atakupandisha toka tope la kuteleza;
Upoke-e neema yake kwa wokovu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
84. BWANA YESU AMESEMA
1 Bwana Yesu amesema: “Ee wewe ni zaifu;
Angalia na kuomba kwa kupata nguvu kwangu.”
Yesu alikufa kwa ajili yangu,
Aliziondosha zambi, furaha kubwa kwangu!
2 Pendo la Mwokozi wangu limeyeyusha moyo;
Ametoa zambi zangu na kiburi na uchoyo.
3 Sina kitu mukononi cha kunifaidia;
Ni zaifu, muhitaji, Yesu, ninakulilia.
4 Mungu akinisaidia, nitamaliza mwendo;
“Yesu alikufa kwami”, nitaimba pale ngambo.
5 Siku moja nitafika mbinguni kwako, Bwana;
Tutaimba sisi sote, tutakushukuru sana.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
85. WAISRAELI KULE KWA MISRI
1 Waisraeli kule kwa Misri walipaka-a miimo na damu,
Na malaika hakuingia kwa kuharibu mwana wa kwanza.
Mungu akiona damu, damu yake Yesu Kristo,
Kweli kufa kutapita, kutapita kabisa kwa sisi.
2 Kule Farao hakukubali kuwafungua watu wa Munga;
Hakuamini na hakuti-i, na alipata taabu kuzidi.
3 Mwenye makosa , kuja kwa Yesu, aliahidi kukuokoa;
Atafunika zambi na damu, tena hukumu hutaipata.
4 Neema, rehema, pendo la Bwana,
ni aminifu, kweli na kubwa;
Makimbilio utayapata, damu inapitisha hukumu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
86. NEEMA YA BWANA NI KUBWA SANA
1 Neema ya Bwana ni kubwa sana,
Kubwa kuliko zambi za watu,
Kule Kalvari tunaiona,
Pa’li pa kufa kwa Bwana Yesu.
Neema yake inasamehe makosa yetu,
Neema yake kubwa kuliko uovu wetu.
2 Tuko katika hatari kubwa,
Tutapotea tusipotubu;
Neema ya Bwana inaonyesha
Yesu Mwokozi ni Kimbilio.
3 Ndugu, huwezi kuficha zambi,
Mungu mbinguni anaziona!
Ee unataka kusukuliwa?
Damu ya Yesu itakuosha.
4 Neema ya Bwana ni kubwa sana,
Iko tayari kwawe, mupenzi;
Kiri makosa, amini Yesu.
Atasamehe kwa neema yake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
87. YOTE NINAYO NILIYAPOKEA
1 Yote ninayo niliyapokea
kwa wema wake unaoenea;
Mimi si kitu, namutegemea ;
nimeokolewa ka ne-ema.
Niliyekuwa nimetoroka,
kwa pendo lake nimeokoka!
Yesu ni mwema na mwenye rehema.
Nimeokolewa kwa ne-ema !
2 Nilitembea zamani kwa zambi
katika njia ya kufa, lakini
Yesu alinitafuta polini ;
nimeokolewa kwa ne-ema.
3 Nimetakaswa na Yesu Mwokozi,
si kwa matendo na si kwa machozi,
Ila kwa damu nina ukombozi ;
nimeokolewa kwa ne-ema.
4 Raha ya mbingu imeni-ingia,
kwa shangwe kubwa namufurahia.
Kwa kuwa Yesu ’nanirehemia ;
nimeokolewa kwa ne-ema.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
88. NE-EMA, NENO TAMU
1 Ne-ema, neno tamu kwa masikio yangu,
Ni wimbo wa mbinguni ju-u, dunia isikie.
Nimeokolewa na ne-ema pekee;
Yesu Kristo alikufa kwami na watu wote.
2 Kwa neema jina langu lina-andikwa mbingu,
Na neema ilinipeleka karibu naye Yesu.
3 Kwa neema njia yako ni wazi mbele yangu;
Ninapokea kwa ne-ema ninayoyahitaji.
4 Kwa neema ninaweza kuomba Mungu Baba;
Ni neema inayonichunga mupaka saa ya kufa.
5 Uache neema yako kuniendesha mbele,
Unipe neema kujitoa kwawe, Mwokozi wangu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
89. PENDO LA MUNGU NI KUBWA
1 Pendo la Mungu ni kubwa, pasha habari hizi;
Pendo la Mungu ni kubwa, mwanzo wa nyimbo zote;
Na malaika mbinguni walihubiri dunia ;
Mutu wa zambi ,sikia, pendo la Mungu ni kubwa!
Pendo kubwa, pendo kubwa,
Pendo kubwa, pendo la Mungu ni kubwa!
2 Pendo la Mungu ni kubwa kwako uliye mbali;
Pendo la Mungu ni kubwa, yeye anakuita.
Toka kilima Kalvari, tangu ku-umba dunia,
Limeonyeshwa hakika, pendo la Mungu ni kubwa!
3 Pendo la Mungu ni kubwa, kutuletea raha;
Pendo la Mungu ni kubwa, tutafurahi sana.
Tutakutana mbinguni na waliotangulia,
Na tutaimba pamoja : ‘‘Pendo la Mungu ni kubwa.’’
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
90. IMBA NENO LA MUNGU
1 Imba Neno la Mungu tena, Neno lenye uzima ;
’Nionyeshe uzuri wake, Neno lenye uzima.
Linaleta uzima, linaleta imani.
Neno la kweli, Neno la ’jabu,
Neno la Mungu na uzima ;
Neno la kweli, Neno la ’jabu,
Neno lenye uzima.
2 Kristo mwenye mapendo yote anakuita sasa;
Mwenye zambi, sikia Yesu, anakuita sasa.
Analeta uzima kwa kufika mbinguni.
3 Uhubiri Habari Njema, Neno lenye uzima.
Linaleta salama kubwa, Neno lenye uzima.
Yesu ni Mukombozi kuokoa milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
91. YESU ALINIOKOA TOKA ZAMBI
1 Yesu aliniokoa toka zambi,
Ni Mwokozi muzuri kwa mimi;
Yesu alinifungua toka woga,
Ni Mwokozi muzuri kwa mimi.
Yesu Mwokozi muzuri kwa mimi,
Ni Mwokozi muzuri kwa mimi ;
Toka zambi zangu aliniokoa,
Ni Mwokozi muzuri kwa mimi.
2 Ni Rafiki mwenye neema na mapendo,
Ni Mwokozi muzuri kwa mimi;
Mahitaji yote ninapata kwake,
Ni Mwokozi muzuri kwa mimi.
3 Yeye ni karibu kwa kunifariji,
Ni Mwokozi muzuri kwa mimi;
Ananisamehe zambi zangu zote,
Ni Mwokozi muzuri kwa mimi.
4 Pendo langu kwaye linaongezeka,
Ni Mwokozi muzuri kwa mimi;
Neema yake tamu inaniongoza,
Ni Mwokozi muzuri kwa mimi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
92. DUNIA YA ZAMBI HAILETI FURAHA
1 Dunia ya zambi haileti furaha
Kama Neno la Mungu kwa mimi,
Sawa Yesu Mwokozi alivyobeba zambi,
Na damu inazifunika.
Damu inazifunika ubaya na zambi zangu,
Hukumu na taabu Yesu alizibeba,
Na damu inazifunika.
2 Mapigo ya Yesu na mi-iba mikali
Yote yanaonyesha mapendo;
Nikiona Kalvari nina haya kwa zambi,
Na damu inazifunika.
3 Nilimutazama kule kwa musalaba
Na ajabu kwa neema ya Mungu;
Nilipiga magoti zambi zangu kukiri,
Na damu inazifunika.
4 Ninamushukuru kwani alinunua
Roho yangu na bei ya damani;
Na furaha na nyimbo ninamusifu sana
Kwa damu inayonika.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
93. RAFIKI, MUYASIKILIZE
1 Rafiki, muyasikilize sasa mafundisho yetu
Yanayoweza kusaidia na kuwaokoa watu.
Nani anaokoa watu?
(Mwana wa Mungu kwa Kalvari)
Kwa njia gani? ( Kutukufia )
Na yuko wapi? (Amini )
Mbinguni anatuombea.
2 Hakuna malaika ju-u aliyeliweza hili;
Mwenye kuteswa kwa Kalvari alikuwa Mwana Mungu.
3 Ni neno la kutushangaza na kuwasha roho zetu;
Yesu, Kuhani letu, sasa anatuombea juu.
4 Utapokea Yesu sasa, utamunyenyekea?
Ataijaza roho yako na uwezo na furaha.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
94. MWOKOZI YESU ALIKWENDA
1 Mwokozi Yesu alikwenda kule kwa Kalvari,
Alitukufilia pale kwa kutuokoa.
Mapendo gani ya Mwokozi! Tumupende sana,
Na tuamini damu yake, tumutumikie.
2 Inatushinda kufahamu aliyoyabeba,
Lakini tunajua alitukufia sisi.
3 Kwa kusamehe zambi zetu Yesu alikufa,
Kwa damu tuokoke na tufike kwake mbingu.
4 Mwingine hakufaa kutulipia deni yetu;
Mwokozi pekee aliweza kufungua mbingu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
95. KWA PENDO LAKE KUBWA
1 Kwa pendo lake kubwa Mwokozi alikuja,
Na alinitafuta katika poli mbali;
Na malaika wali-imba na furaha ju-u yangu.
Alinitafuta, akaniokoa,
Akaniondosha kwa mabaya.
Akanirudisha kwake Mungu.
2 Kwa zizi lake zuri alinibeba tena,
Na aliniambia, “Wewe ni wangu sasa.”
Sauti yake ya mapendo ilinifariji sana.
3 Ninakumbuka jinsi alivyotoa damu,
Ninakumbuka vile mi-iba na mateso,
Mwokozi alibeba yote kwa sababu ya mapendo.
4 Ninakufuata, Yesu, katika nuru yako;
Ninakumbuka sana baraka yako nyingi;
Milele nitaendelea kukusifu kwa furaha.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
96. UMESOMA HABARI ZA MUSALABA
1 Umesoma habari za musalaba wa Mwokozi Yesu?
Damu yake ilimwangika pale kukulipia deni.
Alikukufia musalabani, hivi umekombolewa;
Mapendo yake ya mushangao,
mapendo makubwa gani!
2 Umesoma ya kwamba walimuvika taji ya mi-iba?
Aliwaombea: “Uwasamehe, kwani hawafahamu.”
3 Umesoma ya kama aliokoa mwizi mwenye toba,
Aliyemusihi musalabani: “Bwana, unikumbuke”?
4 Umesoma ya kwamba Mwokozi alilia, “Imekwisha”?
Umesema: “Bwana, asante kwako uliyenikufia”?
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
97. BWANA YESU ALIKUJA
1 Bwana Yesu alikuja kutafuta wapotevu;
Kwa rehema yake Mungu tunapata kuokoka.
Tunaimba kwa furaha, kwani tumekombolewa,
Sifa kubwa kwake Yesu, kwani alituokoa.
2 Bwana Yesu alikufa kwa ajili yetu yote;
Tunapata kuponyeshwa kwa mapigo yake kule.
3 Tulifungwa na Shetani, tulikuwa wafu kweli;
Mukombozi alikuja, sasa tunafunguliwa.
4 Wala mali, wala kazi, haziwezi kuokoa;
Yesu pekee anaweza kusamehe zambi zetu.
5 Wewe ndugu, usingoje, kuja sasa kwake Yesu;
Atakuokoa leo, utaimba na furaha.
6 Siku moja Bwana Yesu atarudi duniani;
Atatupeleka kwake kwa mungini wa mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
98. NIMEKOMBOLEWA KABISA
1 Nimekombolewa kabisa, nitaitangaza daima;
Nimekombolewa na Yesu, na mimi ni wake milele.
Nimekombolewa na damu ya Yesu Mwokozi;
Nimekombolewa, na mimi ni wake milele.
2 Kwa Yesu furaha ni nyingi, kuliko furaha nyingine;
Najua yeye ni karibu na tunabakia pamoja.
3 Ninamufikili saa zote, Mwokozi muzuri wa watu;
Mapendo makubwa ni yake, kwa hivi naimba na nguvu.
4 Najua nitamutazama Mufalme Mupenzi mbinguni,
Anayenichunga na pendo, kunipa furaha moyoni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
99. SIKU NYINGI NILIFANYA ZAMBI
1 Siku nyingi nilifanya zambi,
Sikujua neno la Mwokozi,
Sikujua taabu yake kwami kwa Kalvari.
Bwana Yesu alinirehemu,
zambi zangu alizisamehe,
Nilipata kuwa huru kweli kwa Kalvari.
2 Niliposikia Neno lake,
Moyo wangu ukalia sana,
Nikakiri zambi zangu zote kwa Kalvari.
3 Sasa Yesu ni Mufalme wangu,
Atanitawala kwa milele;
Roho yangu inaimba sifa kwa Kalvari.
4 Ee mapendo gani ya Mwokozi!
Na rehema yake kubwa kwetu!
Tulipatanishwa naye Mungu kwa Kalvari.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
100. PASHA HABARI ZA YESU
1 Pasha habari za Yesu, uziandike moyoni ;
Uni-imbie zaburi za kumusifu Mwokozi,
Sifa iliyotangazwa na malaika zamani :
“Mungu akuzwe mbinguni, iwe amani duniani.”
Pasha habari za Yesu, uziandike moyoni
Uni-imbie zaburi za kumusifu Mwokozi.
2 Pasha habari za Yesu, jinsi alivyoyashinda
Taabu, jaribu, na teso, umasikini na bezo ;
Zambi, hukumu ya Mungu akachukuwa mwenyewe ;
Kila wakati tayari kwa kusaidia wahitaji.
3 Pasha habari za Yesu za musalaba na kufa
Ona kaburi mwambani alipotoka Mwokozi.
Pendo la Yesu ni kubwa aliyekufa Golgota,
Akafufuka hakika, namushukuru siku zote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
101. NI AHADI YA MUNGU
1 Ni ahadi ya Mungu kuleta wokovu
Na wenye kuamini Mwokozi ni Yesu.
::Haleluya! imekwisha, ninaamini kabisa
Na nimeokoka kwa damu ya Yesu::
2 Hata njia ni yenye hatari na mbaya
Ninajua Yesu Kristo atanichunga.
3 Ndugu zangu wapenzi ni wengi mbinguni,
Wanachungwa na Yesu na wanamwimbia.
4 Hata sasa tuimbe pamoja nao vile,
Na kusifu Mwokozi, Mupenzi milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
102. MUGANGA AMEKUJA
1 Muganga amekuja hapa, ndiye Bwana Yesu;
Anaponyesha roho zetu kwa ugonjwa wote.
Jina lake linapita kila jina duniani;
Jina kubwa, jina jema, Yesu, Bwana Yesu.
2 Anasamehe zambi zetu kama tukitubu;
Anatukaribisha kwake kwa rehema kubwa.
3 Wakati wa masikitiko, anatufariji;
Akitukaribia sana, woga unatoka.
4 Watoto wanapenda sana jina lake Yesu;
Linawalinda kwa ubaya wakijaribiwa.
5 Katika vita na mabaya linatupa nguvu;
Shetani analikimbia jina lake Yesu.
6 Mbinguni kwa furaha kubwa tutaona Yesu,
Tutasahau taabu yote, tutamushukuru.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
103. SIWEZI MIMI KUFAHAMU SANA
1 Siwezi mimi kufahamu sana
neema yake Mungu kwangu;
Zamani nilikuwa mukosaji, sasa amenisamehe.
Ninajua Mwokozi wangu anayeweza kulinda sana
Uriti kwami mbinguni hata siku yake Bwana.
2 Siwezi mimi kufahamu sana namna alivyonivuta;
Niliamini Neno lake kweli, ninaona raha tele.
3 Siwezi mimi kufahamu kazi Roho anayoifanya,
Anayeweza kufundisha mutu kuamini Yesu Kristo.
4 Sijui mimi siku zangu tena kutembea duniani;
Na labda nitaona taabu na mateso na huzuni nyingi.
5 Sijui mimi kama siku moja nitaona kufa huko;
Ao kwa haraka nitabadilika Bwana atakapokuja.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
104. ZAMANI MUKE MWENYE UGONJWA
1 Zamani muke mwenye ugonjwa katika makutano
Ali-igusa nguo ya Yesu naye aliponyeshwa.
Na wewe vile amini, na utaokolewa ;
Uzima mupya utapata kwa Yesu Mukombozi.
2 Ee alikuja na woga mwingi karibu naye Bwana ;
Alifahamu aliponyeshwa na nguvu yake kubwa.
3 Yesu alisamehe makosa ya mwanamuke yule,
Salama tamu ili-ingia rohoni mwake pale.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
105. PENDO LA MUSHANGAO
1 Pendo la mushangao hili kuniokoa,
Mutu mubaya, mwenye zambi, bila taraja;
Giza lilinifunga vile. Ee siku kubwa,
Nilipopata kuokoka. Pendo la Mungu !
Pendo la Mungu liliniokoa,
Pendo la Mungu lilinisafisha;
Pendo la Mungu lilitoa Yesu,
Pendo la Mungu, sifu jina lake!
2 Pendo liliongoza Yesu kwa musalaba
Hata kwa watu wa makosa, Ee pendo kubwa!
Vile kwa pendo ninaweza kuomba Mungu,
Nimeokoka, Haleluya! Pendo la Mungu!
3 Pendo lilifungua mbingu kwa wenye zambi;
Kule milele Mukombozi atatawala.
Toka kwa giza niliingia pa’li pa nuru;
Yesu pekee alisaidia. Pendo la Mungu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
106. SISI NI HURU
1 Sisi ni huru toka torati,
Damu ya Kristo ni ukombozi ;
Tulipofungwa chini ya laana,
Kristo alitufanya huru.
Huru kabisa, ndugu, sikia!
Huru kabisa, ndugu, amini!
Kwa neema Kristo musalabani
Alitufanya huru kweli.
2 Sasa azabu haitakuwa
Kwa wenye kumwamini Mwokozi;
Tuna wokovu mutimilifu,
Kwani tuna-amini Yesu.
3 Sisi ni sasa wana wa Mungu,
Kwa neema yake anatuchunga,
Tumepokea kwake uzima
Na tumepita toka kufa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
107. SINA AKILI NYINGI KUFAHAMU
1 Sina akili nyingi kufahamu Neno lake Mungu,
Najua hili moja tu : Yesu ni Mwokozi wangu.
2 Najua alikufa kwa Kalvari kwa makosa yangu ;
Ninahitaji Yesu tu kuwa Mukombozi wangu.
3 Siwezi mimi vile kufahamu pendo lake kubwa.
Na linanishangaza tu, pendo la Mwokozi wangu.
4 Na sasa anaishi kwa pahali pa Mbinguni juu ;
Yeye Mufalme wangu tu, ndiye Mukombozi wangu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
108. ZAHABU NA FEZA
1 Zahabu na feza haziniokoi,
Na mali haiwezi kutoa makosa;
Lakini kwa damu ya Yesu Mwokozi
Nimenunuliwa nipate uhuru.
Nakombolewa pasipo mali,
na kwa neema nimeokoka:
Ni bei gali, kwa damu yake
alilipa deni yangu.
2 Zahabu na feza hazina uwezo
Kwa kunipatia usafi rohoni;
Mwokozi alinikomboa kwa damu,
Nipate wokovu, nitoke kwa zambi.
3 Zahabu na feza haziufungui
Mulango wa kukaribia Mwenyezi,
Lakini kwa damu nimeifikia
Ne-ema ya Mungu aliye Mukuu.
4 Zahabu na feza hazinifikishi
Nyumbani mwa Mungu niliyemubisha;
Lakini nimekombolewa kwa damu,
Kwa hivi nitachukuliwa mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
109. WATU WA MAKOSA
1 Watu wa makosa wana zambi nyingi,
Zambi zinaleta kufa kwa milele;
Watahukumiwa na Mwamuzi Mungu,
Kisha watapata taabu na mateso.
Mwana wake Mungu anaita leo:
Kiri zambi zako zote mbele yake ;
Uamini sasa na kufuata Bwana.
Atakusamehe zambi zako zote.
2 Mwenye kukata-a Bwana Yesu Kristo
Anamukata-a Mungu vilevile;
Kwa milele moto utamutaabisha
Kwani anabisha ma-agizo yake.
3 Pa’li pa Shetani ni pabaya sana.
Moto unawaka pale kwa milele;
Mungu atatupa Diabolo kule
Na wenye kubisha Neno lake Mungu.
4 Tutaona Yesu kule kwake mbingu,
Ni pahali pa furaha kubwa sana;
Yesu Mukombozi, Bwana wa wabwana,
Anashinda kule akituombea.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
110. DAMU YAKO YENYE BARAKA
1 Damu yako yenye baraka inayotuosha makosa,
Ilitoka musalabani, Bwana Yesu, ulipokufa.
Ee ninastahili hukumu, na siwezi mimi kujiosha;
Unioshe katika damu, nipate usafi kabisa.
Safi, safi kweli! Safi, safi kweli!
Unioshe katika damu, nipate usafi kabisa.
2 Yesu ulivikwa mi-iba, kutundikwa ju-u ya muti,
Ulivumilia mateso, maumivu na majeraha;
Damu yako ilimwangika, ni kisima nisafishwe nacho;
Unioshe katika damu, nipate usafi kabisa.
3 Baba, kweli nina makosa, moyo wangu wa uzaifu,
Mimi mwenye zambi rohoni nitaona wapi Mwokozi?
Yesu, kwako musalabani ninakuja kuamini sasa ;
Unioshe katika damu, nipate usafi kabisa.
4 Bwana, nimefika karibu, unilinde kwako milele,
Ufunguwe kamba ya zambi, na ujaze moyo wenyewe !
Na karibu na musalaba nibakie hata kufa kwangu;
Unioshe katika damu, nipate usafi kabisa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
111. NAONA SASA DAMU YA KONDO-O
1 Naona sasa damu ya Kondo-o yake Mungu,
Ilimwangika kwa Kalvari kwa ajili yangu.
Naona damu ya Mwokozi, nasafishwa ndani yake;
Kwa damu ninasifu Mungu, damu ya damani
kweli.
2 Kwa nia na zamiri safi ninakwenda mbingu,
Sababu ninavikwa sasa haki yake Yesu.
3 Ajabu kubwa, nimeonja heri ya mbinguni !
Kwa damu yake Yesu aliosha moyo wangu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
112. UNAKUBALI KUACHA MAKOSA?
1 Unakubali kuacha makosa?
Kwa damu ya Yesu kuna uwezo;
Na unataka kushinda Shetani
Kwa damu ya Yesu Mwokozi?
:: Kuna nguvu ya ajabu kubwa,
Ndiyo damu ya Mwokozi::
2 Unakubali kuvunja tamaa?
Kwa damu ya Yesu kuna uwezo;
Kuja upate usafi wa moyo
Kwa damu ya Yesu Mwokozi.
3 Unakubali kuoshwa moyoni?
Kwa damu ya Yesu kuna uwezo;
Vitaondoshwa vipaku vya zambi
Kwa damu ya Yesu Mwokozi.
4 Unakubali kutenda vizuri?
Kwa damu ya Yesu kuna uwezo;
Na unataka kufika mbinguni
Kwa damu ya Yesu Mwokozi?
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
113. NINI ITANISAFISHA?
1 Nini itanisafisha? Damu ya Mwokozi Yesu;
Kuondosha zambi zangu? Damu ya Mwokozi Yesu.
Ee damu ya Mwokozi ina uwezo wote
Kutusafisha sisi tunaoamini Yesu.
2 Nini itaniokoa? Damu ya Mwokozi Yesu;
Nini itanisamehe? Damu ya Mwokozi Yesu.
3 Nini itanikomboa? Damu ya Mwokozi Yesu;
Na kulipa deni yangu? Damu ya Mwokozi Yesu.
4 Kuna njia moja pekee, damu ya Mwokozi Yesu,
Ninaweza kuamini damu ya Mwokozi Yesu.
5 Ile ni taraja yangu, damu ya Mwokozi Yesu;
Na salama yangu yote, damu ya Mwokozi Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
114. KWELI MAJI HAYAWEZI
1 Kweli maji hayawezi kusafisha roho,
Hayawezi kuondosha zambi, hata moja.
Damu ya Mwokozi Yesu ina nguvu nyingi
Kusafisha roho zetu toka zambi zote.
2 Yesu alikuja kufa kwa ajili yetu,
Akamwanga damu yake kwa kutuokoa.
3 Damu yake ni tayari kutuchunga safi,
Tupendeze Bwana yetu aliyetupenda.
4 Kila mara tunaanguka Yesu ni karibu
Kutusimamisha tena kwa uwezo wake.
5 Tuamini damu yake kutupa uwezo
Kwa kushinda majaribu ya mudanganyifu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
115. KISIMA CHENYA DAMU SAFI
1 Kisima chenye damu safi kutoka musalaba
Kina uwezo kuondosha vipaku vya makosa,
Vipaku vya makosa, vipaku vya makosa,
Kina uwezo kuondosha vipaku vya makosa.
2 Musalabani munyanganyi alimwamini Yesu,
Na alipata usamehe, nitaupata vile;
Nitaupata vile, nitaupata vile,
Na alipata usamehe, nitaupata vile.
3 Mwokozi wangu, damu yako daima ina nguvu
Ya kuokoa wenye zambi wa makabila yote;
Wa makabila yote, wa makabila yote,
Ya kuokoa wenye zambi wa makabila yote.
4 Kisima kile cha ajabu ni tumaini langu;
Ninakusifu wewe sasa na hata kufa kwangu;
Na hata kufa kwangu, na hata kufa kwangu,
Nitakusifu wewe sasa na hata kufa kwangu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
116. HATA NINALIA
1 Hata ninalia na machozi kama muto,
Haitaondosha woga, haitasafisha zambi,
Ninalia bule.
Yesu alinikufia, aliteswa kwa Kalvari,
Yesu ananingojea, ataniokoa.
2 Hata ninafanya kazi nyingi njema sana,
Sitapata roho mpya, vile sitasamehewa,
Kazi yangu bule.
3 Kama nikingoja bila kuamini Yesu,
Bila kumukaribia; nitakufa kwa milele,
Ninangoja bule.
4 Sasa ninaamini Yesu alinikufia,
Alifanya kazi yote, Bwana Yesu peke yake
Ataniokoa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
117. MIMI MWENYE MAKOSA
1 Mimi mwenye makosa nilikombolewa,
Mwokozi alipojitoa;
Zambi zangu na zako alizichukua,
Kwa damu aliniokoa.
Zambi zangu zilimutundika Mwokozi
Alipojitoa Kalvari;
Alizauliwa na kukataliwa
Atupatanishe na Mungu.
2 Yesu mwenye upole na mwenye mapendo
Ananitakasa rohoni;
Nimepata uhuru kwa Yesu Mwokozi,
Alikufa musalabani.
3 Namwambata Mwokozi, sitaki kumwacha,
Kwa kuwa alinikufia;
Nakusifu, Ee Yesu, unayenipenda,
Daima nakushangilia.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
118. MWAMBA ULIOPASUKA
1 Mwamba uliopasuka, ndani yako nijifiche;
Damu iliyomwangika toka mbavu zako, Bwana.
Iwe dawa kuponyesha roho yangu toka zambi
2 Kazi za mikono yangu haziwezi kukomboa;
Hata ningelia sana na kutenda kazi nyingi,
Singeweza kuokoka, wewe pekee ni Mwokozi.
3 Ndani yangu sina kitu, ninashika musalaba;
Mimi bule, univike; sina nguvu, usaidie;
Ni muchafu, unioshe; nisipate kupotea.
4 Kwa maisha yangu yote hata nitakata roho,
Hata siku ya kuitwa mbele ya Mufalme wangu.
Mwamba uliopasuka, nijifiche ndani yako.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
119. TUMEPATA NENO ZURI
1 Tumepata neno zuri : Yesu alituokoa !
Tulipashe kwa dunia : Yesu alituokoa !
Linapaswa kusikiwa na wakubwa na watoto,
Ni habari za furaha : Yesu alituokoa !
2 Tuna hamu ya kuimba : Yesu alituokoa !
Ni uzima kwa waovu : Yesu alituokoa !
Kweli alitufungua, alivunja munyororo,
Sisi mali yake sasa : Yesu alituokoa !
3 Neno kubwa la makubwa : Yesu alituokoa !
Linashinda na zaidi : Yesu alituokoa !
Sema niki-ishi hai, hata nitakapokufa,
Ninataka kusikia : Yesu alituokoa !
4 Tutangaze neno hili : Yesu alituokoa !
Kila mutu asikie : Yesu alituokoa !
Inchi zote zifurahi, watu wote wa-amini,
Na waimbe na kusifu : Yesu alituokoa !
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
120. MUNGU NI PAHALI POTE
1 Mungu ni pahali pote, hutamukimbia yeye;
Anakutazama sana, naye hatalala kamwe.
Giza, nuru, sikuzote Mungu anakutazama;
Hata unafanya nini, Mungu anona yote.
2 Neno gani unasema, Mungu analisikia;
Hata mafikili yote anayatambua wazi.
3 Yesu atakapokuja, atawahukumu wote
Kwa kadiri ya matendo yanayoandikwa kwake.
4 Unajua deni yako? Utalipa kitu gani?
Uamini Bwana Yesu, naye atakusamehe.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
121. PIGA MAKENGELE
1 Piga makengele ya furaha leo
Kwa sababu mutu ametubu!
Mwana mupotevu amerudi sasa,
Baba amemusamehe yote.
Nyimbo za furaha za mbinguni,
Nyimbo za furaha za waamini!
Tunasifu Mungu kwa sababu sasa
Mutu huyu anaamini Yesu.
2 Piga makengele, ni furaha nyingi,
Mukosaji amefunguliwa!
Yesu alivunja minyororo yake,
Alimupa roho ya kimwana.
3 Piga makengele, hizi ni habari
Za kupasha mbali na karibu!
Mutu amepata kuwa mutu mupya,
Zambi zake zimeondolewa!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
122. UMEKUJA KWAKE YESU
1 Umekuja kwake Yesu kusafishwa?
Umeoshwa kwa damu ya Kristo?
Unategemea neema yake sasa?
Umeoshwa kwa damu ya Kristo?
Umeoshwa, umeoshwa,
Umeoshwa kwa damu ya Kristo?
Roho yako imepata kuwa safi?
Umeoshwa kwa damu ya Kristo?
2 Sikuzote unafuata njia yake?
Umeoshwa kwa damu ya Kristo?
Umepata raha na salama kwake?
Umeoshwa kwa damu ya Kristo?
3 Wewe ni tayari kwa kuona Yesu?
Umeoshwa kwa damu ya Kristo?
Naye atakupeleka kwake mbingu?
Umeoshwa kwa damu ya Kristo?
4 Ndugu yangu, ninaku-uliza sasa:
Umeoshwa kwa damu ya Kristo?
Usikawe tena, kuja kuamini,
Utaoshwa kwa damu ya Kristo.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
123. UTAZAME MWOKOZI
1 Utazame Mwokozi aliyekufa kwawe
Ili wewe upate uzima;
Utazame kwa pendo atakusa-idia,
Usidumu zambini daima.
Ona, ona Yesu!
Utazame Mwokozi aliyekufa kwawe
Ili wewe upate uzima.
2 Bwana Yesu alisulibishwa kwa Kalvari
Ili sisi tupate wokovu;
Na alitukomboa kwa damu yake safi,
Kwake yeye tupate uzima.
3 Ee rafiki, Mwokozi anakuita leo,
Anataka ufike upesi;
Unakawa kwa nini, ufike bila woga,
Uondoke katika hatari.
4 Fika sasa, pokea uzima wa milele,
Bwana Yesu alituletea;
Na kuishi mbinguni ni tumaini letu,
Umwamini na hutapotea.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
124. KUJA KWA YESU
1 Kuja kwa Yesu na usikawe, anonyesha njia ya mbingu;
Umusikie, anakusihi : ‘‘Mutu wa zambi, kuja !’’
Kuja sasa kwake Bwana Yesu,
atakuokoa toka zambi;
Amini Yesu moyoni mwako, upate usamehe.
2 Kuja, mutoto, anakuita, anakupenda, atakuchunga;
Umuchague kwa Bwana yako, wewe mutoto, kuja.
3 Atapokea watu wo wote, sasa anakungojea wewe;
Tubu upate kusamehewa, kuja na zambi zako.
4 Sasa ni siku kuokolewa, kuja upesi kwa musalaba;
Mwenye masikitiko na zambi, kuja kwa Yesu sasa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
125. YESU MWOKOZI ANAITA WATU
1 Yesu Mwokozi anaita watu, mimi na wewe na wote;
Anakungoja kukukaribisha, wewe uliye zambini.
Urudi, urudi, sasa urudi kwa Yesu!
Anakuita na anakungoja; leo urudi kwa Yesu!
2 Unakata-a Mwokozi kwa nini? anakungoja ufike;
Kuna nafasi karibu na Yesu, njia ni wazi kwa wote.
3 Kumbuka saa zinapita upesi, hazitarudi kabisa!
Kuja kwa Yesu upate amani, leo ungali muzima.
4 Ona mapendo makubwa ya Yesu, yanaenea kwa wote;
Na kwa ne-ema anatukumbuka, wewe na mimi na wote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
126. NA HALI YANGU NINAKUJA
1 Na hali yangu ninakuja pasipo neno ila moja:
Ulimimia damu yako, ninakuja kwako, Bwana.
2 Na hali yangu sitangoja kujisafisha kosa moja ;
Kwa damu utaniokoa, ninakuja kwako, Bwana
3 Na hali yangu kwa matata, mashaka, woga wa azabu,
Nipate raha kwako, Mungu, ninakuja kwako, Bwana.
4 Na hali yangu masikini, kipofu, bule, na zaifu,
Nipate mali ya milele, ninakuja kwako, Bwana.
5 Na hali yangu ninaamini ahadi zako zote kweli;
Nipate usamehe wako, ninakuja kwako, Bwana
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
127. USIKIE BWANA YESU
1 Usikie Bwana Yesu anayekuita leo;
Aliteswa, alikufa kwa ajili yako wewe.
Usikie Bwana Yesu, anapiga hodi kwako;
Umufungulie moyo, umukaribishe sasa.
2 Sikuzote ulicheza, kupendeza mwili wako;
Ulimusahu Yesu aliyekukufilia.
3 Unasema: “Nitakuja kusikia Neno lake”;
Ee rafiki, ukumbuke unaweza kufa leo.
4 Yesu anaita sasa kwa ne-ema na mapendo;
Leo siku ya wokovu, umufungulie moyo.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
128. MWENYE KUSIKIA
1 Mwenye kusikia, kuja kwake Yesu,
Yeye ni Mwokozi wa wenye makosa;
Acha zambi zako, umwamini yeye.
Kila mwenye zambi aje.
Kila mwenye zambi aje kwa Mwokozi,
Mutangaze neno ili kila pa’li ;
Baba ya mapendo anaita leo:
Kila mwenye zambi aje.
2 Mwenye kusikia, kuja, usikawe,
Leo lango la wokovu liko wazi;
Yesu ndiye Njia, Kweli, na Uzima,
Kila mwenye zambi aje.
3 Mwenye kusikia na kufika kwake,
Atamupokea, ni ahadi yake;
Atachunga vile, hata kwa milele,
Kila mwenye zambi aje.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
129. “HAKOSE KESHO NITA-AMINI
1 “Hakose kesho nita-amini,
Nitapokea Yesu Mwokozi.”
Mungu anakuita, usikawie tena,
Leo ni siku nzuri kuokolewa.
2 Hakose kesho saa itapita;
Kwa nini unazarau Bwana?
Kwa neema yake kubwa Mungu atapokea;
Saa haijapita bado, kuja kwa Yesu.
3 Hakose kesho saa ya hukumu
Itakupata mbele ya Mungu;
Umusikie sasa, anakupenda sana,
Fikili neno hili, usipote-e!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
130. USIKIE YESU KRISTO
1 Usikie Yesu Kristo, yeye anakuita,
Sikia na kujibu, sasa kuja kwa Bwana.
2 Anaweza kuokoa mwenye kumusadiki,
Na atakuokoa kama ukimwamini.
3 Anapenda kusamehe watu wanaotubu,
Na atakusamehe – kuja sasa kwa Yesu.
4 Ukimbie sasa kwake, na atakupokea,
Kimbia kwa Mwokozi na atakupokea.
5 Omba Yesu, omba Yesu, na atakusikia,
Uombe Yesu sasa, na atakusikia.
6 Anapenda watu wote, Yesu anakupenda,
Milele na milele Yesu atakupenda.
7 Haleluya, Haleluya, Haleluya, Amina!
Tuimbe Haleluya, Haleluya, Amina!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
131. EE KUJA, MUTU WA MAKOSA
1 Ee kuja, mutu wa makosa, kuja kwa rehema;
Mwokozi atakupokea kama ukikuja.
Umwamini, umwamini, umwamini Yesu,
Naye atakuokoa, umwamini Yesu.
2 Mwokozi alimwanga damu yake kwa Kalvari,
Na damu ile inaweza kusafisha safi.
3 Ee Yesu tu ni njia kuingia kule mbingu ;
Amini sasa kwa kupata usamehe kwake.
4 Ungana nasi watu wake, njia iko wazi;
Na tutakuwa kwa milele na furaha nyingi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
132. HATUA MOJA INAKUTENGA NA MWOKOZI
1 Hatua moja inakutenga na Mwokozi;
Unangoja nini? Ufike kwake leo!
Hatua moja, hatua moja; kuja, anangoja;
Kuja kutubu zambi, atasamehe zote!
Usikatae tena wokovu wake Mungu!
2 Hatua moja mbele, anakungoja sasa;
Amini Neno lake, na utasamehewa.
3 Hatua moja mbele, uzima utaona ;
Siku si nyingi huko, unangojea nini?
4 Hatua moja mbele, kwa nini unakawa?
Omba: Ee Bwana Yesu, unipoke-e sasa!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
133. UTAFURAHI KUWA NA UHURU?
1 Utafurahi kuwa na uhuru? Umutazame Yesu;
Kukuokoa alikukufia, Umutazame Yesu.
Umutazame Yesu, umutazame Yesu,
Yesu pekee atakuokoa, kuja na kumwamini.
2 Kama Shetani akikujaribu, umutazame Yesu;
Nguvu kushinda atakupatia; umutazame Yesu.
3 Njia ni ndefu, unachoka sana ? Umutazame Yesu;
Atafariji na mapendo yake; umutazame Yesu.
4 Usiogope siku za huzuni; umutazame Yesu;
Hata kwa siku za furaha nyingi; umutazame Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
134. KAMA UKITAKA
1 Kama ukitaka kuwa mutu wake Yesu,
Kama ukitaka kumufuata yeye,
Kama ukitaka asaidie sikuzote,
Umufungulie moyo.
Ataondoa zambi zako zote,
Na utaipokea nguvu yake;
Ukiokoka utaona kwamba
Ni vema kumufuata Yesu kweli.
2 Kama ukitaka kuwa mutu mwenye heri,
Na kushinda zambi kwa uwezo wake,
Kama ukitaka utulivu na faraja,
Umufungulie moyo.
3 Kama ukitaka kumutumikia Yesu
Na kufuata njia yake duniani,
Kama ukitaka kuingia kule mbingu,
Umufungulie moyo.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
135. MATESO YANAKUSUMBUSHA
1 Mateso yanakusumbusha, na unatembea kwa giza?
Geuka, tazama Mwokozi, uzima na nuru pokea.
Utazame Mwokozi, fikili uzuri wa Bwana;
Mambo ya dunia yatapunguka
Mbele ya utukufu wa Yesu.
2 Mwokozi alitukufilia, tuishi pamoja na yeye;
Na tusijitoe kwa zambi, kwa Yesu tushinde kabisa.
3 Ahadi za Mungu ni kweli; amini na utaokoka;
Halafu uende po pote, hubiri habari za Bwana.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
136. NINA MWOKOZI ANAYENIOMBEA
1 Nina Mwokozi anayeniombea,
Rafiki kuliko wengine wo wote;
Na sasa mbinguni ananitunza sana,
Laiti upate Mwokozi mwenyewe!
Ninakuombea, ninakuombea.
Ninakuombea, upate kuamini!
2 Nina taraja kutoka Baba wangu,
Ya kama atanipokea mbinguni;
Na sasa ninamungojea kuni-ita,
Laiti upate taraja yenyewe !
3 Nina mavazi yanayoningojea,
Mavazi meupe ndiyo utukufu ;
Na nitayapata mbinguni kwake Mungu,
Laiti upate mavazi yenyewe !
4 Nina salama inayopita yote,
Si kama dunia inayoitoa ;
Inatoka Yesu kwa pendo lake kubwa,
Laiti upate salama yenyewe!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
137. TAMU SANA NI MANENO YA HABARI NJEMA
1 Tamu sana ni maneno ya habari njema,
Jana, leo, na milele Yesu yuko sawa;
Hata sasa anapenda watu wa makosa,
Kufariji wenye taabu. Sifu jina lake!
Jana, leo, na milele, Yesu yuko sawa,
Vyote vinapogeuka, Yesu yuko sawa.
Sifu jina lake! Sifu jina lake!
Vyote vinapogeuka, Yesu yuko sawa.
2 Mwenye kusamehe Petro atatusamehe;
Atatoa shaka zote kama kwa Tomasi;
Mwanafunzi alilala kifuani mwake;
Anaita watu sasa kupumzika kwake.
3 Alinyamazisha maji kule kwa bahari,
Hivyo anaweza kuondoa woga vile;
Akaomba na huzuni kwa Getesemane;
Anaweza kufahamu taabu zetu zote.
4 Kama alivyotembea na wafuasi wake,
Na kuwafariji kwa safari ya Emau,
Vivyo hivyo anapenda kutembea nasi,
Yeye mufariji mwema leo na milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
138. HERI KABISA
1 Heri kabisa, Yesu ni wangu!
Ni Muchungaji, na mimi ni wake;
Nimezaliwa mara ya pili,
Ninasafishwa kwa damu yake.
:: Yesu ni wimbo wa roho yangu,
Nitamusifu hata milele ::
2 Kule mbinguni kuna furaha
Ju-u ya mwenye kutubu makosa;
Nilisikia Neno la Mungu,
Nilijitoa kwa Bwana Yesu.
3 Ninashukuru Yesu Mwokozi,
Na roho yangu inashangilia;
Mimi si kitu mbele ya Mungu,
Kwa neema yake ananipenda.
4 Ninastarehe sasa kwa Yesu,
Nina salama kutoka kwa Mungu;
Ninangojea Yesu afike
Kunipeleka kwake mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
139. MOYO WANGU UNA WIMBO LEO
1 Moyo wangu una wimbo leo, Yesu ananiambia:
“Siku zote nitakuongoza, Ee usiogope tena.”
Yesu, Yesu, Yesu, jina tamu sana;
Linajaza roho na furaha na salama.
2 Mbele nilitaka kuharibu roho yangu na makosa ;
Yesu aliingia kuokoa, sasa nimesamehewa.
3 Hata ana’ngoza kwa mateso, taabu ya kuzidi sana,
Yesu ni Mushinda sikuzote, naye anajua njia.
4 Yesu ni karibu kurudia kutukaribisha kwake,
Kutawala naye kwa milele kwa mungini wake mbingu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
140. EE NITAKIMBIA KWA MWAMBA
1 Ee nitakimbia kwa Mwamba wa nguvu
Kutoka huzuni, mateso, na taabu;
Nachoka na zambi, nataka tu Mungu;
Ee nitafichama kwa Mwamba wa nguvu.
Nitafichama kwako, Mwokozi;
Ee Mwamba wa nguvu, unifiche kwako.
2 Kwa saa ya salama na vile kwa taabu,
Na saa majaribu yanaponitesa,
Nina Kimbilio katika zoruba,
Ee nitafichama kwa Mwamba wa nguvu.
3 Adui ya roho anapozunguka,
Naweza kusema habari kwa Yesu,
Atanisikia na kunifariji,
Ee nitafichama kwa Mwamba wa nguvu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
141. USIMAME KWA AHADI ZAKE
1 Usimame kwa ahadi zake Kristo,
Sasa na milele umusifu sana;
Leta utukufu wote kwake Mungu,
Usimame kwa ahadi zake.
Usimame, leo usimame kwa ahadi zake;
Usimame, simama kwa ahadi zake Mungu.
2 Usimame kwa ahadi za milele,
Hata majaribu yanatesa sana;
Utapata nguvu kwa Maneno yake,
Usimame kwa ahadi zake.
3 Usimame kwa ahadi zake Bwana,
Kwani unafungwa kwa milele kwake;
Roho atakushindisha sikuzote,
Usimame kwa ahadi zake.
4 Usimab me kwa ahadi, hutaanguka,
Ukisikiliza Roho aki-ita;
Upumzike ndani ya Mwokozi wako,
Usimame kwa ahadi zake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
142. USIOGOPE MATESO YAKO
1 Usiogope mateso yako, Mungu anakulinda;
Bali tazama mapenzi yake, Mungu anakulinda.
Mungu anakulinda siku kwa siku njiani mwake;
Anakulinda daima, Mungu anakulinda.
2 Una muzigo muzito sana? Mungu anakulinda;
Na kwa hatari ya njia yako, Mungu anakulinda.
3 Anakumbuka hitaji lako, Mungu anakulinda;
Utashiriki uzuri wake, Mungu anakulinda.
4 Katika njia ya taabu nyingi, Mungu anakulinda;
Hata ukifazaika sana, Mungu anakulinda.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
143. EE YEHOVA, MUNGU WANGU
1 Ee Yehova, Mungu wangu, uni’ngoze duniani;
Mimi ni zaifu sana, una nguvu ya kutosha.
Kweli wewe ni Mukate wa uzima,
Nitashiba, Yesu, kwako tu daima.
2 Kama ulivyo-ongoza watu wako wa zamani,
Acha nguzo ndiyo moto kuniangazia njia.
Mushindaji, uwe ngabo yangu nguvu;
Nisishindwe na adui zangu, Mungu.
3 Nikifika kwa kivuko cha kupita kule kwako,
Uondoshe woga wote, nifikishwe kwa salama.
Nitatoa sifa nyingi kwako, Mungu;
Nitaimba nyimbo za kukushukuru.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
144. HUZUNI YANGU NI KITU KWELI
1 Huzuni yangu ni kitu kweli machoni mwa Bwana Yesu?
Saa ya masumbuko na majaribu yeye ananihurumia?
Kabisa! Anaona yote na ananihurumia;
Taabu yangu yote nilete kwake, hataniacha
kamwe.
2 Mwokozi yuko karibu kweli ninapo-ogopa sana?
Na nikitembea katika giza, Bwana ni karibu kuchunga?
3 Wakati ninapopima sana nishinde saa ya jaribu,
Na nina-anguka, huzuni kubwa! Atapenda kunisamehe?
4 Wakati wa kufa kwa wapenzi, kuachwa na ndugu zangu,
Na upekee ukinishika nguvu, Bwana atakuwa karibu?
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
145. JINA LAKE YESU KRISTO
1 Jina lake Yesu Kristo tunapenda kusikia;
Ni furaha na faraja saa tunapolikumbuka.
Jina kubwa, jina zuri, ni taraja ya dunia;
Jina kubwa, jina zuri, ni furaha ya mbinguni.
2 Jina lake Yesu Kristo ni mulinzi kama ngabo,
Vile kimbilio letu, tukijaribiwa sana.
3 Jina lake Yesu Kristo ni furaha yetu kubwa,
Saa tunapoimba sifa kwa Mupenzi wetu Yesu.
4 Tutaona Yesu Kristo, tutaanguka mbele yake,
Kwa sababu yeye Bwana na Mufalme wa wafalme.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
146. YESU NI RAFIKI YANGU
1 Yesu ni Rafiki yangu, anayenipenda sana;
Sawasawa sikuzote, jana, leo, na milele.
Haleluya, Yesu, Kristo ni Mwokozi na Rafiki,
Muchungaji na Mufariji, Mwaminifu kwa milele.
2 Yesu ni Mushinda wangu, anayenificha kwake,
Nikijaribiwa sana, yeye ni uwezo wangu.
3 Yesu Mufariji wangu katikati ya huzuni,
Saa ninapolia kwake, ananisikia mbio.
4 Yesu ni Mwongozi wangu, Muchungaji wangu mwema;
Ananionyesha njia, na sitapotea kamwe.
5 Yesu, ninapata kwako yote ninayohitaji;
Kwani ulininunua, mimi wako, wewe wangu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
147. BABA WANGU MUFALME
1 Baba wangu Mufalme, ndiye Mungu Mwenyezi,
Kweli ananipenda kabisa;
Ana nyumba tayari kwami kule mbinguni,
Mali yake nitaishiriki.
Baba wangu Mufalme ananipenda sana,
Naye ananilinda daima;
Kwa wakati mwingine Yesu atani-ita
Kwa kuka-a nyumbani na yeye.
2 Baba wangu Mufalme ni mwenye neema nyingi,
Ananihurumia hakika;
Kwa maneno yo yote na pahali po pote
Ninaweza kumutegemea.
3 Baba wangu Mufalme ananiahidia
Kwamba atani-ita mbinguni;
Pale nitatazama uso wake milele,
Nami nitasahau huzuni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
148. PAHALI POTE NINAPOKWENDA
1 Pahali pote ninapokwenda, ama kwa jua, ama kwa giza,
Yesu Mwokosi aliahidi hatanipungukia daima.
Nuru ya mbingu, nuru ya mbingu,
Ninatembea sasa kwa nuru;
Haleluya! Ninamusifu na shangwe kubwa,
Yesu ni wangu.
2 Wakati taabu inapokuja; Yesu hawezi kunisahau;
Aliahidi neno la kweli, atanichunga hata milele.
3 Ninamusifu kwa nuru yake inayoniongoza kwa njia;
Nikitembea kando ya Yesu, sitapotea hata kidogo.
4 Katika njia kwenda mbinguni niendele-e ndani ya nuru,
Ninamwimbia nyimbo za sifa kumushukuru kwa pendo
lake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
149. HAKUNA RAFIKI KAMA YESU
1 Hakuna rafiki kama Yesu, Yesu tu, Yesu tu!
Wapi mwingine kutuokoa? Yesu tu, Yesu tu!
Anajua mateso yetu, anapenda kutusaidia;
Hakuna rafiki kama Yesu, Yesu tu, Yesu tu!
2 Yeye pekee ni mutakatifu, Yesu tu, Yesu tu!
Na vile yeye munyenyekevu, Yesu tu, Yesu tu!
3 Nani karibu pahali pote? Yesu tu, Yesu tu!
Nani anayetupenda wote? Yesu tu, Yesu tu!
4 Alijitoa kwa zambi zetu, Yesu tu, Yesu tu!
Na tutakuwa naye mbinguni, Yesu tu, Yesu tu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
150. MUCHUNGAJI YESU
1 Muchungaji Yesu, mwenye pendo kubwa,
Sisi wa-amini ni kondo-o zake;
Tukihuzunika, Yesu anajua,
Anakaribia kwa kutusaidia.
2 Na Shetani hapa anatutafuta,
Sawasawa simba anatungojea;
Tukumbuke Yesu ndiye Musaidia,
Kama aki-ita tutamusikia.
3 Tutabarikiwa mioyoni mwetu,
Kama tukifuata nyuma yake Bwana;
Hatutaogopa tukimutazama
Akikwenda mbele ya kondo-o zake.
4 Muchungaji mwema, Yesu Mukombozi,
Alituokoa sisi watu bule;
Damu yake safi alitumwangia,
Kutupatanisha naye Mungu Baba.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
151. KWAMI MUCHUNGAJI NI BWANA YESU
1 Kwami Muchungaji ni Bwana Yesu, sitapungukiwa kitu;
Kwa maana ananitembeza katika lisho bichi.
Ee, nira yake laini kabisa, ananifunga na
mapendo,
Kuniongoza katika njia, muchana na usuiku.
2 Na anarudisha nafsi hakika, ananiogoza vile
Katika njia yenye haki kwa jina lake safi.
3 Hata nikipita kati ya bonde la kufa na giza lake,
Sitaogopa neno baya kwa maana wewe yuko.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
152. NIWE KARIBU NAWE
1 Niwa karibu nawe, Ee Mungu wangu,
Hata katika taabu niwe karibu;
Huu wimbo wangu, Bwana: Niwe karibu nawe,
Niwe karibu nawe, Ee Mungu wangu!
2 Ninasafiri hapa, sitakawia;
Giza ni duniani, raha haiko;
Hata ni hivi, Bwana, niwe karibu nawe,
Niwe karibu nawe, Ee Mungu wangu!
3 Hata mateso mengi yananipata,
Nitakumbuka hili, una rehema,
Na yatanikokota niwe karibu nawe;
Niwe karibu nawe, Ee Mungu wangu!
4 Saa nitakapokwenda kwako mbinguni,
Nitasahau taabu ya duniani;
Ungali wimbo wangu: Niwe karibu nawe,
Niwe karibu nawe, Ee Mungu wangu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
153. NINAJUA RAFIKI MWEMA
1 Ninajua Rafiki mwema, anatunza sana kila siku,
Anaweza kuponyesha ku-umia kwa mutima;
Jina lake ni Yesu Kristo.
Najua Rafiki mwema, naye anaja-a neema,
Nikiomba na kulia yeye ananisikia,
Ndiye Yesu, na si mwingine.
2 Nimepata Rafiki mwema kufariji na kunipa raha;
Namutegemea yeye, sina woga wa adui;
Na Rafiki ni Yesu Kristo.
3 Nikifika mutoni pale, unaitwa ‘‘kufa’’ na ‘‘kaburi’’,
Sitafazaika kamwe, Yesu atakuwa nami ;
Ni Rafiki mukubwa sana.
4 Pwani nzuri ya kule ju-u, nitafika kwa ne-ema kubwa ;
Nitaimba na kinubi, nitasifu Yesu sana
Kwa mapendo na urafiki.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
154. NINATAKA BWANA YESU
1 Ninataka Bwana Yesu awe nami sikuzote;
Pendo lake litakuwa sawa kwa miaka yote.
Ee ukubwa wa mapendo yake Yesu, Bwana wangu;
Ameniokoa kweli, atanipeleka kwake.
2 Ninataka Bwana Yesu kwa wakati wa mateso;
Anajua kufariji na kufurahisha moyo.
3 Ninataka Bwana Yesu kumutegemea sana,
Kuongozwa naye vile kwa safari yangu hapa.
4 Ninataka Bwana Yesu, kumupenda, kumufuata,
Hata nitakapo-ona uso wake kule mbingu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
155. NANI ANAYENINYANYUA?
1 Nani anayeninyanyua? Ni Yesu Kristo;
Na anayenipigania ? Ni Yesu Kristo.
O Yesu, ninakuamini, wewe tu utanishindisha,
Kwani silaha ya kushinda ni Yesu Kristo.
2 Mwenye kunifikisha mbingu ni Yesu Kristo;
Mwenye kunipa shangwe kubwa ni Yesu Kristo.
Na hata katika mateso na masumbuko, majaribu,
Kwami taraja na furaha ni Yesu Kristo.
3 Nani aliyeniokoa ? Ni Yesu Kristo ;
Nani anayefa-a kwangu ? Ni Yesu Kristo.
Bado kidogo nitakwenda kule kwa nyumba yake Baba.
Na nitaishi kwa milele na Yesu Kristo.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
156. MUSINGI WA NGUVU NI YESU
1 Musingi wa nguvu ni Yesu Mwokozi,
Tuweke imani kwa Neno la Mungu;
Alituahidi kutupa wokovu,
:: Tuliokimbia karibu na Bwana::
2 “Usiwe na woga, usifazaike,
Nitakusaidia kwa saa ya mateso,
Kukusimamisha na kukupa nguvu;
:: Mukono wa neema utakushindisha::
3 “Katika mateso na saa ya jaribu,
Ne-ema ya Mungu inafa-a kwawe;
Ukali wa moto hautaku-uma,
:: Nataka kutoa uchafu wa roho ::
4 “Mwenye kupumzika na kuniamini,
Siwezi, siwezi kumwacha daima,
Na hata Shetani atamujaribu,
:: Siwezi,siwezi kumwacha daima”::
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
157. NINA USHIRIKI NA FURAHA KUBWA
1 Nina ushiriki na furaha kubwa,
Nikitegemea Yesu Bwana;
Ninapata heri na salama vile,
Nikitegemea Yesu Bwana.
Raha, raha, raha kwa Yesu na salama;
Raha, raha, nikitegemea Yesu Bwana.
2 Raha ya ajabu ni rohoni mwangu,
Nikitegemea Yesu Bwana;
Nuru inangaza njia ya maisha,
Nikitegemea Yesu Bwana.
3 Woga na huzuni zinatoka kwangu,
Nikitegemea Yesu Bwana;
Ninafarijiwa sikuzote naye,
Nikitegemea Yesu Bwana.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
158. USIACHE ZAMBI
1 Usiache zambi kushinda rohoni,
Yesu anataka kukupa uwezo
Kushinda Shetani na hila ya zambi;
Imani kwa Yesu itakushindisha.
Omba Yesu kwa nguvu ya kushinda Shetani;
Anapenda kuchunga na atakushindisha.
2 Acha urafiki na watu wabaya,
Na usitukane jina lake Mungu;
Uwe na imani, na neema na kweli;
Imani kwa Yesu itakushindisha.
3 Mungu ataleta taji ya uzima
Kwa mwenye kushinda adui Shetani;
Tazama Mwokozi, ndiye mwenye nguvu;
Imani kwa Yesu itakushindisha.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
159. YESU UNAYENIPENDA
1 Yesu unayenipenda, leo nijifiche kwako;
Zambi kama mvua zimetaka kunishinda.
Ee Mwokozi, unifiche, unitwae niwe kwako,
Niokoke kwa mabaya na nisiwe mbali nawe.
2 Wewe tu ni kimbilio, hapa ni matata mengi,
Ninakuhitaji sana, Ee usiniache pekee.
Mimi ninakuamini, wewe Musaidizi wangu;
Chini ya mabawa yako ninachungwa na salama.
3 Yote ninayohitaji ninapata kwako, Bwana;
Roho inapolegea, unisimamishe tena.
Wewe mwenye haki pia, mimi mwenye zambi kubwa;
Wewe pekee unaweza kusafisha moyo kweli.
4 Neema nyingi iko kwako kufunika zambi zangu;
Unitwae, unichunge, unilinde hata mwisho.
Hivi nikukaribie, unishike kwa mikono:
Nikujue wewe pekee, hapa chini, kule ju-u.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
160. EE MARA NGAPI TUNASUMBUKA
1 Ee mara ngapi tunasumbuka na roho inalegea,
Tunazungushwa na giza kubwa, tunaogopa sana?
Sauti tamu ya Bwana Yesu tunasikia kusema:
“Mutoto wangu ninakupenda, sitakuacha daima.”
:: Kwa kila wakati, kwa kila pahali,
Aliahidi kuchunga, hataniacha daima::
2 Mupenzi, umesahau mbio sauti hii ya mapendo
Ya Bwana Yesu aliyetoa uzima wake kwawe?
“Mutoto unayechoka sana, kumbuka sitakuacha;
Niliahidi nitakuchunga na kuwa nawe daima.”
3 Halafu, ndugu, ufarijiwe katika kila matata,
Mwokozi wako anakupenda, hatakuacha kamwe;
Unyoshe kwake mukono wako, utamukuta karibu,
Faraja tamu kumusikia : “Sitakuacha daima.”
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
161. KATI’ MIKONO YAKE YESU
1 Kati’ mikono yake Yesu ananilinda,
Katika pendo kubwa ninapumzika sana.
Ninasikia sasa sauti yake Bwana,
Na inanikumbusha mbingu na raha yake.
Kati’mikono yake Yesu ananilinda,
Katika pendo kubwa ninapumzika sana.
2 Kati’mikono yake nitapumzika kimya,
Yesu atanilinda,yeye uwezo wangu.
Sasa hakuna shaka, wala sioni woga ;
Saa ya kupata taabu,Yesu anafariji.
3 Yesu Mwokozi wangu aliyenikomboa
Atanificha kwake, katika Mwamba nguvu.
Kwa siku ya matata na majaribu tele,
Ninangojea Yesu, atarudia kwami.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
162. TUKIKWENDA PAMOJA
1 Tukikwenda pamoja kushikana na Mungu,
Tunapata amani na raha;
Tukifanya daima yanayomupendeza,
Ni karibu kwa kutusaidia.
Raha, furaha, tunapata kwa Bwana,
Tukidumu katika kuamini, kutii.
2 Kama pepo, tufani zikivuma kabisa,
Zinakoma kwa neno la Yesu;
Tukiona jaribu na ku’gopa adui,
Tutashinda kwa nguvu ya Yesu.
3 Hatuwezi kujua pendo tamu la Mungu
Na furaha ya kweli moyoni,
Kama hatujatoa vitu vyote kwa Bwana
Na kutii ma-agizo ya Mungu.
4 Tuna raha ya Mungu kwa shindano lo lote,
Tukitii na tukimusadiki;
Jua lake la pendo linawa-angazia
Wa-amini na wenye kutii.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
163. YESU, MUCHUNGAJI WETU MWEMA
1 Yesu, Muchungaji wetu mwema, utuchunge siku zote,
Utulishe sisi kundi lako na chakula cha milele.
:: Bwana Yesu, Bwana Yesu, sisi wako, utuchunge::
2 Tuna taabu na mateso mengi, sisi ni zaifu sana;
Tunajaribiwa na Shetani, utulinde kwa mapendo.
:: Bwana Yesu, Bwana Yesu, usikie tukiomba::
3 Ulisema utatupokea hata sisi wenye zambi;
Una neema na rehema nyingi, utuhurumie sisi.
:: Bwana Yesu, Bwana Yesu, tunakutafuta sana::
4 Yesu, uwe nasi hata mwisho, tusiache njia yako;
Tukufuate kwa mapenzi yako, hivi tutakupendeza.
:: Bwana Yesu, Bwana Yesu, utukaribishe kwako::
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
164. NJIA YOTE NAONGOZWA
1 Njia yote naongozwa kwa mukono wa Mwokozi;
Ninaona wema wake, sina shaka wala woga,
Nina raha ya mbinguni, na salama tamu sana,
:: Na katika mambo yote ananitendea mema ::
2 Njia yote naongozwa, ninategemea Yesu;
Analinda jaribuni, ananipatisha nguvu.
Nikiona kiu hapa, nikichoka kwa safari,
:: Ninapata maji mengi toka Mwamba wa milele ::
3 Njia yote naongozwa kwa mapendo yake bora;
Ananituliza sana na ahadi yake nzuri.
Nitafika kwake mbingu kufurahi kwa milele,
:: Nitaimba neno hili, Yesu aliniongoza ::
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
165. UNACHOKA KWA MATATA
1 Unachoka kwa matata na masikitiko?
Yesu anaita: “Kuja kupumzika.”
2 Nitamutambua wazi kwa alama gani?
Ona mbavu na mikono na miguu.
3 Taji nzuri ya mufalme inapamba kichwa?
Ndiyo, utaona taji ya mi-iba.
4 Kama nikifuata Yesu, atanipa nini?
Utulivu na salama na furaha.
5 Nikiomba anitwae, atanifukuza?
Sivyo, atalinda sana kwa milele.
6 Nikifuata, nikishinda, nitapata mema?
Wengi wanashuhudia: “Ndiyo, ndiyo.”
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
166. JUA LA ROHO
1 Jua la roho ni wewe, Mwokozi,
Giza haliko pahali ulipo;
Wingu la zambi lisifiche
Uso wa Bwana machoni mwangu.
2 Hata kwa saa ya kulala usiku
Sitaogopa, wewe ni karibu.
Nitapumzika kwa salama
Kwani unanitunza daima.
3 Saa ya muchana unanishindisha,
Nita-anguka usiponichunga,
Uache nuru ya mbinguni
Kunionyesha njia ya haki.
4 Uwe karibu nami saa ya kufa,
Uniongoze kwa bonde la giza
Unifikishe kwako juu,
Nione uso wako mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
167. WATU WANAKUZARAU
1 Watu wanakuzarau, woga ni moyoni ?
Huta-achwa peke yako-Yesu hageuki.
Yesu hageuki, Yesu hageuki,
Vitu vyote vinapita, Yesu yuko sawa.
2 Hata taabu inakuja, majaribu mengi,
Ukumbuke Yesu yuko, yeye ni karibu.
3 Kwa mateso na huzuni, anapenda sawa;
Umutegeme-e yeye, ndiye mwaminifu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
168. NIKIPATA ULIMWENGU WOTE
1 Nikipata ulimwengu wote, na kukosa Yesu Mukombozi,
Sitakuwa na furaha kamwe, vitu vya dunia hii ni bule!
Nikipata ulimwengu wote, na kukosa Yesu Mukombozi,
Nitakuwa na huzuni sana, Yesu pekee anafurahisha.
2 Kama mimi mutajiri kweli, na kuheshimiwa na wengine,
Na kukosa kuwa na taraja ya kufika muji wa mbinguni;
Nikipata ulimwengu wote, na kukosa Yesu Mukombozi,
Yeye aliyenikufilia, nitakwenda wapi saa ya kufa?
3 Ee maisha yangu bila Yesu ni faida gani kwami hapa?
Tena kwa milele bila yeye, taabu na machozi bila mwisho ;
Hata niki-ishi bila Yesu, nina’gopa sana saa ya kufa,
Kukutana na Mwamuzi Mungu, kwa milele bila Mukombozi!
4 Ee furaha iko kwake Yesu, anajua kufariji moyo,
Hata nina zambi nyingi sana, yeye atazisamehe zote;
Nikiishi na Yesu pamoja, na kukosa mali ya dunia,
Nina vitu vyote kwake Yesu, yeye Muchungaji wangu
mwema!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
169. NINA RAFIKI MWEMA
1 Nina Rafiki mwema naye alinikufia;
Alinivuta kwake na amenifanya mupya.
Ni mali yake Yesu tu, ninaongozwa naye;
Na alinikomboa kwa agano la mapendo.
2 Nina Rafiki mwema aliyeondoa zambi;
Aliniweka huru na kunipa Roho yake.
Na vitu vyote ninavyo ninavitoa kwake,
Maisha yangu yake tu, kuimba sifa kwake.
3 Nina Rafiki mwema na ana uwezo wote;
Pamoja naye Yesu ninashinda majaribu.
Atanitwa-a kwake kwa mungini wa furaha,
Nitastarehe kwake kwa milele na milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
170. MAPENDO YAKE MUNGU
1 Mapendo yake Mungu yanatu-unganisha,
’Shirika wa watakatifu, heri ya mbinguni.
2 Kwa kiti cha ne-ema tukaribie Baba
Kwa tumaini, ujasiri, kwa imani moja.
3 Tunashirikiana uchungu na mateso .
Mizigo tunabebeana kwa mapendo mengi.
4 Tuna-achana huko kwa sikitiko sana,
Tutaonana tena kwake na furaha kubwa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
171. NIKUTAMU SANA KWANGU
1 Ni kutamu sana kwangu kumutegemea Yesu,
Kuamini Neno lake na ahadi zake bora.
Yesu, Yesu, ninaamini, ninajua wema wake;
Yesu, Yesu, ninapenda, ni Rafiki ya damani.
2 Ni kutamu sana kwangu kumutegemea Yesu,
Kuamini damu yake kusafisha zambi zangu.
3 Ndiyo, ni kutamu sana kumutegemea Yesu ;
Kwake ninapata raha, na furaha, na salama.
4 Kumutegemea Yesu ni furaha yangu yote ;
Yeye ni Rafiki bora anayetembea nami.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
172. SINA WOGA KWENDA NA MWOKOZI
1 Sina woga kwenda na Mwokozi Yesu,
Ataniongoza na kunibariki;
Bila Yesu sitakuwa na furaha.
Yesu tu anafukuza woga wote.
Kila pa’li na Mwokozi sitajua woga,
Kila pa’li na Mwokozi nitakwenda.
2 Na Mwokozi sitakuwa peke yangu,
Hata nikiachwa na rafiki zangu;
Hata akiniongoza kwa mateso,
Nitasifu kwani Yesu ni karibu.
3 Kila pa’li Yesu anaponituma
Kutangaza Neno lake la wokovu,
Nitapenda kwenda kama aki-ita,
Ao kubaki hapa kama akitaka.
4 Yesu ni pamoja nami, nitalala
Saa ya giza la usiku bila woga,
Nikijua kwake mbingu nitafika
Na safari hapa itamalizika.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
173. BWANA YESU UNIONGOZE
1 Bwana Yesu, uniongoze kwa bahari ya maisha,
Hata kwa mawimbi mengi, kwa zoruba ya hatari;
Bwana Yesu, uniongoze, nakutegemea wewe.
2 Bwana Yesu, uniongoze, utulize moyo wangu;
Neno moja toka kwako lilinyamazisha pepo ;
Bwana Yesu, uniongoze, leta utulivu wako.
3 Bwana yesu, uniongoze, niyashinde majaribu;
Mengi yananidanganya, mengi yanafunga macho;
Bwana Yesu, uniongoze, niwe mushindaji kweli.
4 Bwana Yesu, uniongoze, nitakapo vuka ngambo;
Nikiona woga, giza, leta nuru na amani;
Bwana Yesu, uniongoze, uwe nami hata mwisho.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
174. HAKIKA YESU MWAMBA NGUVU
1 Hakika Yesu Mwamba nguvu, nitafichama kwake Yesu.
Kwa saa ya taabu na mateso, nitafichama kwake Yesu.
Ee Yesu yeye pekee ni Mwamba nguvu,
Kwa kunificha, kuniokoa;
Ee Yesu yeye pekee ni Mwamba nguvu,
Kwa siku ya hukumu kubwa.
2 Shetani hataniumiza, nitafichama kwake Yesu;
Siwezi kuogopa tena, nitafichama kwake Yesu.
3 Hatari ikinifikia, nitafichama kwake Yesu;
Sitaki kutembea mbali, nitafichama kwake Yesu.
4 Usiku na muchana vile, nitafichama kwake Yesu;
Atasaidia sikuzote, nitafichama kwake Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
175. MAPENDEZI YA DUNIA
1 Mapendezi ya dunia sitamani tena ;
Nina-acha yote, Yesu, nifanane nawe.
Nifanane nawe, Yesu, ao nyumbani ao po pote;
Kila siku ya maisha, nifanane nawe.
2 Ulivunja kila pingu la makosa yangu,
Hata ni kutumikie, nifanane nawe.
3 Toka hapa kwenda mbingu kwa safari nzima.
Nitapasha Neno lako, nifanane nawe.
4 Nikukute kule mbingu, Mukombozi wangu.
Nisikie neno “Vema”, nifanane nawe.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
176. EE, TARAJA YAKO NI WAPI
1 Ee, taraja yako ni wapi, ndugu,
Kwa kukusaidia saa ya taabu?
Una kimbilio katika Kristo,
Ao unategemea nani?
Tuna taraja ya kweli, ndugu,
Saa ya mateso na saa ya taabu,
Mwamba wenye nguvu Bwana Yesu
Anayetuchunga kwa mambo yote.
2 Kamba ya mapendo inakufunga,
Wewe na Mwokozi ni pamoja ?
Saa Shetani anapokujaribu,
Yesu anakupatisha nguvu?
3 Tutafika mbingu kuona Yesu
Na pamoja tutamushukuru
Kwa kuchunga kwake kwa sikuzote
Na kulipa deni yetu yote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
177. NINAKUTA BWANA YESU
1 Ninakuta Bwana Yesu Rafiki yangu kweli,
Kwa mapendo anapita sisi sote,
Kwa matata Musaidizi, kwa zambi ni Mwokozi,
Mufariji kwa huzuni yeye pekee.
Na anataka sana nilete taabu kwake,
Mateso, masumbuko, ayabebe.
Anapenda watu wote, alinikufilia,
Mwana wake Mungu na Rafiki yangu!
2 Kwa dunia alibeba huzuni na mateso,
Alikufilia wenye zambi wote,
Walipiga walitesa Mupenzi wake Mungu,
Alibeba taabu ya makosa yetu.
Anastahili kweli kupata sifa nyingi,
Nitamukuza Yesu Kristo pekee.
3 Ailiniahidi hivi, hataniacha kamwe,
Atachunga watu wake kwa huzuni;
Hata kitu gani hapa kinaningoja mimi,
Sitakiogopa kwani Yesu yuko.
Halafu kule mbingu karibu na Mwokozi
Furaha itakuwa kwa milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
178. NAVUTWA KWAKE YESU
1 Navutwa kwake Yesu na ninamufurahia,
Uzuri wake unapita vyote vya dunia;
Siwezi ku-upima kweli kwa mawazo yangu,
Uzuri wake unazidi kuwa bora kwangu!
Siwezi kueleza uzuri wake huko,
Lakini nitaufahamu wote kule mbingu.
2 Mapendo ya ajabu kubwa nayasifu sana,
Yakanivuta kwa upole, nije kwake Bwana;
Yakanitoa mimi katika unyonge wangu,
Mapendo yake yanazidi kuwa bora kwangu!
Siwezi kueleza mapendo yake huko,
Lakini nitayafahamu yote kule mbingu.
3 Wokovu wake wa ajabu usifiwe sana,
Uliondoa woga, ukanipa utulivu;
Napenda Yesu aliyechukua zambi zangu,
Wokovu wake unazidi kuwa bora kwangu.
Siwezi kueleza wokovu wake huko,
Lakini nitaufahamu wote kule mbingu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
179. NINATAKA KUMUFUATA YESU
1 Ninataka kumufuata Yesu Mukombozi
Ama kwa rafiki ama kwa wageni vile;
Kwa pahali pa furaha ama sikitiko,
Nimukaribie Yesu sikuzote.
Nimufuate, nimukaribie,
Sikuzote na po pote nitembe-e naye;
Nimufuate, nimukaribie,
Yesu mbele, mimi nyuma hata mwisho.
2 Ju-u ya milima nitasikiliza Yesu,
Hata mabondeni nitashikamana naye;
Jua, giza; afya, ’gonjwa; utulivu, vita;
Kwa maneno yote Yesu ni karibu.
3 Nikiteka maji ao nikilima shamba,
Nikibaki kwa mungini, ama kwa safari;
Neno hili moja pekee ninataka sana,
Nimukaribie Yesu sikuzote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
180. EE NINATAKA KUSIKIA
1 Ee ninataka kusikia ju-u ya neema yake Bwana,
Yeye aliyekufa kwami, maana ananipenda sana.
Habari za Yesu, habari za Yesu,
Na za mapendo yake kwami, ninafurahi kusikia.
2 Ee ninataka kutambua vile mapenzi yake Bwana,
Ili nijue kumufuata, kumutukuza sikuzote.
3 Ee ninataka kufahamu vile Kitabu chake Mungu,
Hata niweze kuongozwa na Yesu kwa maneno yote.
4 Ee ninataka kusikia ju-u ya Yesu kule mbingu;
Yeye mwenyewe atarudi kutupeleka wote kwake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
181. UCHUNGE WAKATI
1 Uchunge wakati kusema na sema Bwana;
Na vile kusoma Neno takatifu;
Fanya urafiki na wenye imani;
Na omba baraka kwa neno lo lote.
2 Uchunge wakati, saa inakimbia;
Ushinde saa zote pamoja na Bwana;
Ukimutazama, utabadilishwa
Kupata mufano wa Yesu hakika.
3 Uchunge wakati, atakuongoza;
Umutegeme-e kwa mambo yo yote;
Katika furaha, katika huzuni,
Umutumaini, atakushindisha.
4 Uchunge wakati, salama moyoni;
Yesu atawale hata mafikili;
Atakufundisha na Roho ya kweli;
Utatayarishwa kufika mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
182. UNITEMBEZE, BWANA WANGU
1 Unitembeza, Bwana wangu, katika njia ya kwenda mbingu;
Unipatishe vile nguvu niende mbele nawe, Yesu.
Niende mbele nawe, Yesu,
katika Neno lake Mungu;
Uniwezeshe kila siku niende mbele nawe, Yesu.
2 Shetani ananijaribu, lakini utanipa nguvu;
Unisaidie, ninaomba, niende mbele nawe, Yesu.
3 Maneno ya dunia hapa siyatamani tena, Bwana;
Kuliko vyote ninataka niende mbele nawe, Yesu.
4 Ninakata-a zambi zote, nataka tu nikupendeze;
Hata kufika kule mbingu niende mbele nawe, Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
183. ROHO YANGU INAJA-A NA FURAHA
1 Roho yangu inja-a na furaha na salama,
Maana ninajua Yesu ananifanyia mema.
Yesu, Yesu, nitafuata Mukombozi wa pekee;
Roho yangu inaja-a na mapendo kwa Mwokozi.
2 Yesu alinitafuta mwenye kusahau Mungu;
Alimwanga damu yake kuokoa roho yangu.
3 Sitamani zambi tena, haziwezi kunifunga ;
Munyororo wa Shetani Yesu aliufungua.
4 Ninawaombea ndugu katika dunia pia,
Hata Neno la uzima wataweza kusikia.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
184. NINAPENDA KUMUSIFU BWANA YESU
1 Ninapenda kumusifu Bwana Yesu,
Ni Rafiki wangu mwaminifu kweli ;
Alinipa moyo mupya na uzima,
Nani ataweza neno kama hili.
Ee mapendo yake ni makubwa!
Sina Musaidizi kama Yesu;
Yeye tu aliondosha zambi zangu,
Ee, ananipenda sana.
2 Nilikuwa na makosa mengi sana,
Moyo wangu ulikuwa na huzuni;
Yesu alinizungusha na mapendo,
Alinionyesha njia ya wokovu.
3 Ee furaha kujuana naye Bwana,
Na maneno yake yote ya mapendo;
Kisha siku nitakapofika kwake
Macho yangu yataona uso wake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
185. KIONGOZI, MWANA WA MUNGU
1 Kiongozi, Mwana wa Mungu, ni karibu na mwaminifu;
Anatuongoza saa zote, sisi wasafiri jangwani.
Tukichoka, tunafurahi tukimusikia Yesu
Akisema: “Kuja, mupenzi, nitakuongoza mbinguni.”
2 Sikuzote yeye Rafiki ni tayari kutusaidia ;
Na hatutabaki na shaka, na hatutakuwa na woga.
Saa zoruba inapovuma, nafsi inapolegea,
Anasema: “Kuja, mupenzi, nitakuongoza mbinguni.”
3 Kazi yetu inapokwisha, tutatazamia pumziko;
Damu yake Mwana wa Mungu ni taraja yetu ya mbingu.
Hatutaogopa mauti, tutachungwa na Mwokozi,
Akisema: “Kuja, mupenzi, nitakuongoza mbinguni.”
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
186. NISADIKI YESU KRISTO SIKUZOTE
1 Nisadiki Yesu Kristo sikuzote duniani,
Hata na imani ndogo, nisadiki Yesu pekee.
Nisadiki Yesu pekee, nisadiki sikuzote,
Kati ya bahati gani, nisadiki Yesu pekee.
2 Roho yake anaangaza roho yangu njia zote,
Nikifuata, sitaanguka, nisadiki Yesu pekee.
3 Ninaimba kwa furaha, ninaomba saa ya taabu,
Kati ya hatari vile, nisadiki Yesu pekee.
4 Nisadiki hata mwisho wa uzima wangu hapa,
Hata kwenda kwangu mbingu, nisadiki Yesu pekee.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
187. KAMA UNA MAHITAJI
1 Kama una mahitaji, huna mali nyingi tena,
Nja-a vile ikifika kwako nyingi,
Ukumbuke Mungu Baba analinda kila saa,
Leta taabu yako yote kwake Yesu.
Uiache yote kwake,
Acha taabu yako yote kwake Yesu;
Ukimusadiki Mungu, atakupatisha nguvu,
Acha taabu yako yote kwake Yesu.
2 Wewe ni mugonjwa vile, mwili unauma sana,
Taabu inaleta woga mwingi kwako?
Yesu anajua yote naye atakusaidia,
Leta taabu yako yote kwake Yesu.
3 Kama wewe ni muzee, unachoka sikuzote,
Ee, usisahau Mungu yuko nawe;
Yesu ni karibu sasa, na atakuchunga sana,
Leta taabu yako yote kwake Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
188. YESU MWOKOZI ALINIKUFIA
1 Yesu Mwokozi alinikufia,
Naye amenipa uzima mupya;
Nikitazama Mwokozi daima,
Kila dakika naishi kwa Bwana.
Kila dakika nachungwa na Yesu,
Kila dakika napata uzima;
Nikitazama Mwokozi daima,
Kila dakika naishi kwa Bwana.
2 Kwa majaribu, mateso na taabu,
Yesu Mwokozi ananishindisha,
Na anabeba mizigo ya roho;
Kila dakika ananisaidia.
3 Saa ya huzuni, machozi, uchungu,
Saa ya hatari, saa ya uzaifu,
Hata Mwokozi ni kule mbinguni,
Kila dakika ananifikili.
4 Hata ugonjwa unanikamata,
Yesu anaweza kuniponyesha;
Hata katika maneno yo yote,
Kila dakika ananichungaga.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
189. UKICHUKULIWA NA MASHAKA YAKO
1 Ukichukuliwa na mashaka yako,
Na kuona woga kwamba utashindwa,
Uhesabu tu baraka yake Mungu,
Na utashanga-a kwa rehema yake.
Uhesabu tu baraka zote,
Mungu alikubariki nazo!
Ukumbuke mambo yote pia,
Na utashanga-a kwa rehema yake.
2 Na ukisumbushwa na huzuni nyingi,
Ukiona musalaba ni muzito,
Uhesabu tu baraka kila siku,
Na kwa moyo wote utasifu Mungu.
3 Usi-itamani mali ya dunia,
Utajiri wako ni Mwenyezi Mungu;
Uhesabu tu baraka na kumbuka
Mali haiwezi kufungua mbingu.
4 Na katika mambo yote huko chini
Ukumbuke pendo kubwa la Mwokozi;
Vile ujumlishe tu baraka zote,
Tena mwisho atakupeleka kwake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
190. WAKATI SALAMA INAPOJAZA ROHO
1 Wakati salama inapojaza roho,
Na vile wakati wa taabu,
Umenifundisha kusema kwa kweli:
“Najua Mwokozi ni wangu.”
Ninajua Yesu Bwana,
Ninapata salama moyoni.
2 Wakati Shetani anaponijaribu,
Salama inachunga roho,
Kwa maana Mwokozi ananikumbuka
Na kunipa nguvu kushinda.
3 Hukumu ya zambi sitaogopa tena,
Mwokozi ali-imaliza
Saa alipobeba makosa Kalvari
Na kuyaondosha kabisa.
4 Ninatazamia kurudi kwake Yesu
Afike katika mawingu,
Nione kwa macho ninayemupenda,
Ni-ishi milele na yeye.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
191. MUFALME WA MAPENDO
1 Mufalme wa mapendo ndiye Muchungaji wangu;
Sipungukiwi kitu kwani mimi ni wa Yesu.
2 Anaongoza kando ya vijito vitulivu;
Ninakulishwa sikuzote kwa malisho yake.
3 Nawe karibu siogopi sasa hata kufa;
Na gongo lako, fimbo yako zinafariji.
4 Kwa sikuzote za maisha nitapata wema;
Nyumbani mwake nitasifu Muchungaji wangu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
192. EE KUNDI LA MUNGU, MUSIYAOGOPE
1 Ee kundi la Mungu, musiyaogope
Maneno yo yote katika dunia;
Uwezo wa Mungu anawapa ninyi,
Na anawalinda anaowapenda.
Mumusadiki, mumusadiki,
Vyote vinawezekana kwa Yesu.
Mumusadiki, mumusadiki,
Vyote vinawezekana kwa Yesu.
2 Ee kundi la Mungu, musiyaogope
Maneno mabaya, huzuni, na taabu;
Mwokozi mwenyewe atawaongoza,
Yeye alikunywa uchungu wo wote.
3 Ee kundi la Mungu, musiyaogope
Maneno ya kesho musiyoyajua;
Hawezi kuacha mwenye kumwamini
Na atabakia karibu saa zote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
193. MWOKOZI ANANIONGOZA
1 Mwokozi ananiongoza, ni neno la kunifariji!
Pahali pote, sikuzote, mukono wake unaniongoza.
Mwokozi ananiongoza pahali
pote na mukono wake;
Niwe mufuata wake kweli
na kumutumikia sikuzote.
2 Pahali pa matata kubwa, pahali pa furaha nyingi,
Si neno kama nikijua mukono wake unaniongoza.
3 Ee Bwana, ninataka sana karibu nawe kubakia;
Ninafurahi kutambua mukono wako unaniongoza.
4 Na siku kazi yangu hapa nitakapomaliza yote,
Mauti sitaiogopa ; Mwokozi atanifikisha kwake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
194. MWOKOZI ALINIAMBIA
1 Mwokozi aliniambia : “Nitasamehe zambi zako;”
Furaha inazidi sasa, furaha kama ya mbinguni.
Ee haleluya, nimusifu! Alisamehe zambi zangu!
Pahali pote na saa zote nina furaha ya mbinguni.
2 Zamani sikujua njia kunifikisha kule mbingu;
Lakini sasa ninajua Mwokozi alinikufia.
3 Katika utajiri mwingi na hata kwa umasikini,
Pahali pote na saa zote nina furaha ya mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
195. NINASIMAMA KWAKE KRISTO
1 Ninasimama kwake Kristo, yeye Mwamba wa imara;
Sina mwingine kuamini, yeye tu taraja yangu.
Ninasimama kwake Kristo
Mwamba wa imara, sana,
Pengine pote ni muchanga.
2 Saa giza linapomuficha, ninaamini neema yake;
Na katikati ya zoruba, ninashika Yesu sana.
3 Ananisimamisha sana ju-u ya ahadi zake;
Na hata nyota vinaanguka, nimutegemee pekee.
4 Wakati atakaporudi, atanipeleka kwake;
Atanivika haki yake, sitamukosea tena.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
196. ZAMANI NILI-ISHI KWA ZAMBI
1 Zamani nili-ishi kwa zambi, nilikosa nuru,
Lakini sasa nimepokea Kristo ndani yangu.
Kristo ndani yangu, Kristo ndani yangu,
Wokovu mukubwa sana, Kristo ndani yangu.
2 Kwa moyo wangu nimegeuzwa, nimejazwa tele
Na Roho, nuru, uzima, pendo, Kristo ndani yangu.
3 Nataka kufanana na Yesu, kuwa sawa naye;
Nataka wote wajue kweli Kristo ndani yangu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
197. NIKIONA UZAIFU NA IMANI NDOGO
1 Nikiona uzaifu na imani ndogo,
Nikijaribiwa sana, Yesu, unilinde.
Unilinde vema, unilinde vema,
Kwa sababu ya mapendo, unilinde vema.
2 Peke yangu sitaweza kukushikilia ;
Pendo langu ni zaifu, Yesu, unilinde.
3 Mimi mali yako sasa ulinikomboa,
Ulitoa damu yako, Yesu, unilinde.
4 Huta-acha nipote-e, unalinda sana ;
Kwani ninakuamini, Yesu unilinde.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
198. EE MWOKOZI, UNILINDE
1 Ee Mwokozi, unilinde na uniongoze kweli,
Njia ni matata sana, bila wewe nitaanguka.
Bwana Yesu, uni’ngoze kwa upole,
Nikufuate duniani kila siku, kila saa.
2 Wewe ndiwe Kimbilio kwa wakati wa zoruba,
Nawe siogopi kitu, kwako tumaini langu.
3 Kisha siku ya mauti utanifikisha kwako,
Nitazame uso wako, na machozi yatakwisha.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
199. NAPENDA KUTANGAZA
1 Napenda kutangaza habari za Mwokozi,
Habari za mapendo na utukufu wake;
Napenda kuzipasha habari hizi tamu,
Inanifurahisha kuliko kila neno.
Napenda kutangaza habari za Mwokozi,
Habari za mapendo ya Yesu Bwana yangu.
2 Napenda kutangaza habari za Mwokozi,
Ni mushangao kwangu, ajabu kubwa kweli ;
Napenda kuzipasha sababu zilikuwa
Baraka kubwa kwami na ziliniokoa.
3 Napenda kutangaza habari za Mwokozi,
Ni kila mara tamu kuliko kwa mutima;
Napenda kuzipasha ; wengine hata leo
Hawajazisikia, hawajaokolewa.
4 Napenda kutangaza habari za Mwokozi
Kwa watu wenye nja-a, kwa watu wenye kiu;
Na nitakapofika mbinguni, nitaimba
Habari hizi tena, habari za mapendo.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
200. WATU WA MUNGU, MUMALIZE KAZI
1 Watu wa Mungu, mumalize kazi
ya kuhubiri Neno la Mwokozi ;
Yeye aliyeumba watu wote hataki mutu kupotea kwake.
Hubiri watu Neno la Yesu,
La ukombozi, salama na wokovu.
2 Tazama watu wanafungwa sana katika giza la makosa
mengi ;
Na wanagonja kusikia neno la Yesu mwenye kuwakufilia.
3 Pasha habari watu wasikie Mungu alionyesha pendo lake
Siku alipotuma Bwana Yesu awe Mwokozi kwa wenye
makosa.
4 Tuma vijana wako kutumika kazi ya Mungu kwa pahali
pote;
Na toa mali kwa kuwasaidia, Yesu atakurudishia yote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
201. NATAKA SANA KUSIKIA
1 Nataka sana kusikia Neno yako waziwazi,
Na nitakwenda kutafuta wenye kupotea mbali.
2 Uniongoze ili mimi nitafute wapotevu
Na kuwaleta kwako, Bwana, waokoke, wakufuate.
3 Unipatishe nguvu, Bwana, nisimame kwa imara;
Unifundishe, kisha mimi nitawafundisha wana wako.
4 Ufanye kazi yako nami, pa’li gani, kila siku;
Nataka kusaidia wenye mahitaji na huzuni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
202. KUTUMIKA KAZI KWA MWOKOZI
1 Kutumika kazi kwa Mwokozi Yesu kunaniletea shangwe;
Roho yangu inapata kufurahi kutumika kazi yake.
Kutumika kazi yake ninaleta vitu vyote;
Ninapata shangwe nyingi kutumika kazi yake.
2 Kutumika kazi kwa Mwokozi Yesu kunaniletea shangwe;
Nitaimba hata kati ya huzuni, kutumika kazi yake
3 Kutumika kazi kwa Mwokozi Yesu kunaniletea shangwe;
Kila siku Yesu ananiongoza kutumika kazi yake.
4 Kutumika kazi kwa Mwokozi Yesu kunaniletea shangwe;
Ninaleta vitu vyangu vyote kwake kutumika kazi yake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
203. SIMAMA KWA MUFALME
1 Simama kwa Mufalme, askari yake Yesu!
Nyanyua na furaha bendera yake safi;
Tufuate nyuma yake kushinda Diabolo,
Mwenye kutudanganya, mwenye kutuonea.
2 Sikia baragumu inatuita sasa!
Tuendele-e mbele, kusudi ni kushinda;
Tusiogope kamwe hatari ya shindano,
Lakini tupigane kwa nguvu yake Mungu.
3 Simama, fanya vita kwa jina lake Yesu!
Tuvikwe na silaha ya haki kwa kifua;
Hakika tutashinda na ngabo ya imani,
Kofia ya wokovu, upanga ndio Neno.
4 Shindano letu hapa ’takwisha siku moja,
Tupige vita leo, pumziko ni mbinguni;
Na kila mushindaji atapokea taji
Na utukufu tele karibu na Mufalme.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
204. EE BENDERA INATWEKA
1 Ee bendera inatwekwa kututangulia,
Tusione woga tena, twende kwa kushinda.
Bwana Yesu anakuja, tumutazamie,
Kwa uwezo wake Yesu atatushindisha.
2 Ee Shetani ni karibu, anatutafuta,
Anataka tuanguke, tufe, tupote-e.
3 Tunajua Bwana Yesu ni pamoja nasi ;
Tusimame sawasawa na askari wema.
4 Vita kubwa, vita kali iko mbele yetu;
Tuwe watu wahodari, twende, tutashinda.
5 Basi, kwa bendera yake tunashikamana;
Atutie nguvu yake hata kuja kwake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
205. CHINI YA BENDERA YAKE YESU
1 Chini ya bendera yake Yesu Kristo tunakwenda mbele sasa;
Tunainyanyua watu waione, tuki-imba sifa kwake.
Twende mbele, twende mbele,
kwa Kristo tuna-acha yote;
Tumuvike taji, tumwimbie chini ya bendera
yake.
2 Musalaba wake ni bendera yetu, tutashinda chini yake;
Sisi ni askari za Mufalme Yesu, hatutaogopa kamwe.
3 Kwa pahali pote pa dunia hii tutangaze Neno lake;
Wenye kuamini wataokolewa, watakuwa wana wake.
4 Basi asubui ni karibu sana Yesu atakapokuja
Mushindaji wa adui zake zote, duniani kutawala.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
206. UWATAFUTE WANAOPOTEA
1 Uwatafute wanaopotea, kwa pendo uwaondoe kwa zambi;
Lia na wenye huzuni rohoni, uwapeleke kwa Yesu Mwokozi!
Uwatafute wanaopotea!
Yesu Mwokozi atawaokoa.
2 Anatafuta waliokimbia, anawangoja warudi upesi;
Uwafundishe kwa pendo na kweli ju-u ya neema na haki ya
Yesu.
3 Ndani ya roho na katika siri hakose wanatafuta wokovu.
Uwaongoze kwa Yesu Mwokozi, uwaonyeshe mapendo ya
Mungu.
4 Uwatafute wanaopotea. Mungu atatupa pendo na nguvu;
Uwapeleke kwa Yesu Mwokozi, ataokoa wanaoamini.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
207. FANYIA MUNGU KAZI
1 Fanyia Mungu kazi, usiku unakuja,
Utumikie Mungu siku zako zote.
Anza mapema sana, dumu muchana kutwa,
Usiku unakuja, kazi itakwisha.
2 Fanyia Mungu kazi kama ingali jua,
Usipoteze bule siku zako hapa!
Uyatimize yote bila kukosa neno;
Usiku unakuja, kazi itakwisha.
3 Fanyia Mungu kazi, saa inapita mbio,
Fanya bidi-i sana kutafuta ndugu!
Utumikie Mungu kwa nguvu yako yote;
Usiku unakuja, kazi itakwisha.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
208. PANDA MBENGU NJEMA
1 Panda mbegu njema, anza asubui,
Omba Mungu sana kubariki kazi.
Kwa wakati wake utakwenda vile
Na kuvuna mbegu na furaha tele.
:: Twende kwa mavuno, twende kwa mavuno,
Kwa furaha kubwa twende kwa mavuno ::
2 Panda mbegu njema ju-u ya milima,
Na tuendele-e hata mabondeni!
Neno lake Mungu litawafungua
Watu wa makosa kwa furaha kubwa.
3 Panda mbegu njema hata kwa machozi,
Ukumbuke Yesu, leo uhubiri!
Bwana wetu Yesu atakuja tena
Na zawabu yetu kwa furaha kubwa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
209. EE ASKARI, TWENDE
1 Ee askari, twende, vita tuipige,
Macho yetu yawe ju-u ya Mufalme,
Anatuongoza kwa kupiga vita,
Twende mbele na kufuata nyuma yake Bwana.
Twende mbele, sisi askari, vita tuipige;
Musalaba wake unatangulia.
2 Kweli tutashinda jeshi la Shetani,
Ee askari, twende mbele na Mufalme;
Watatetemeka wanaposikia,
Nyimbo zetu za kusifu Yesu Kristo Bwana.
3 Kama jeshi kubwa twende naye mbele,
Tunafuata ndugu zetu za zamani;
Katika Mwokozi tuna roho moja,
Mafundisho na mapendo na taraja sawa.
4 Basi ninyi ndugu, tu-ungane sasa,
Tushirikiane kumusifu Yesu;
Sifa, utukufu kwake Kristo Bwana,
Wimbo huu tutauimba kwake kwa milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
210. ASKARI WAHODARI
1 Askari wahodari, tusimame kwa kushinda;
Tupige vita kali kwa wakati wa muchana.
Adui wanangoja, ndugu, tusiwaogope;
Imani ni uwezo wetu kwa kushinda wote.
Imani kwa Yesu Kristo, imani kwa Yesu Kristo,
Imani kwa Yesu Kristo ni uwezo wetu.
2 Bendera ni mapendo, na upanga Neno lake;
Tufuate na furaha wa-amini wa zamani;
Kwa nguvu ya imani yao Shetani alishindwa,
Na ngabo ya imani yao ni ngambo yetu vile.
3 Shetani ni tayari, ana hila nyingi sana;
Tutupe uzaifu wetu, twende kumushinda;
Tujifungie kweli na kofia ya wokovu;
Adui za Mwokozi ni zaifu mbele yetu.
4 Mushinda wa adui atapata vazi zuri,
Na jina lake Yesu atakiri kule mbingu.
Mapendo yakitusukuma twende kupigana;
Kwa jina la Mwokozi tutashinda Diabolo.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
211. TOKA GIZA
1 Toka giza watu wengi wanalia:
“Tuma nuru, tuma nuru!”
Kuna wapotevu, kuna wenye zambi,
Tuma nuru, tuma nuru!
Tuma nuru ya Habari Njema, iangaze pa’li pote;
Tuma nuru ya Habari Njema, iangaze kwa milele.
2 Leo Mungu anaita, akisema:
“Tuma nuru, tuma nuru!”
Tujitoe kwake, tutafute watu,
Tuma nuru, tuma nuru!
3 Na tumwombe Mungu neema itangazwe,
Tuma nuru, tuma nuru!
Hata watu wengi wapoke-e Kristo,
Tuma nuru, tuma nuru!
4 Tusichoke sasa kumutumikia,
Tuma nuru, tuma nuru!
Mungu atatupa taji ya uzima,
Tuma nuru, tuma nuru!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
212. ASKARI WA MWOKOZI
1 Askari wa Mwokozi mimi na mufuata wake,
Sitaogopa kutangaza jina la Mwokozi.
2 Sitaogopa majaribu na kupata taabu
Katika vita na makosa kwa ajili yake.
3 Nitapigana na adui na uwezo wake;
Dunia inamuchukia Yesu Bwana wangu.
4 Ee Bwana, niwe muhodari, niwe mwaminifu,
Nibebe taabu na uchungu kwa ne-ema yako.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
213. NANI NI WA YESU?
1 Nani ni wa Yesu? Amutumikie!
Atafute watu na kuwahubiri!
Nani anataka kujitoa leo
Kumufuata Yesu katika mateso?
Mimi ni wa Yesu, nimutumikie!
Nitafute watu, kwake warudie!
2 Kwa mapendo yake tunalazimishwa
Kutafuta wenye zambi na makosa ;
Tunaendelea kuhubiri Neno,
Na kuvuta watu ili waokoke.
3 Yesu alitununua sisi sote
Akimwanga damu yake kwa Kalvari;
Kwake tumepata raha na uhuru,
Tunataka sasa kuwa waaminifu.
4 Hata vita ikiongezeka huko,
Tuko na bendera ya kushinda kwetu;
Siku ya pumziko inakaribia,
Itabadilisha vita kuwa shangwe!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
214. NITAFIKA KWAKE BWANA
1 Nitafika kwake Bwana, yeye Mukombozi wangu,
Na sikumutumikia hata siku moja hapa?
Nitakuenda kukutana naye na mikono bule,
Bila tunda hata moja? Itakuwa haya kubwa!
2 Hata siogopi kufa, kitu ninacho-ogopa
Ni kufika kwake Bwana bila nafsi hata moja.
3 Siku nyingi nimeishi bila kumutumikia;
Zimepita zote bule, zimepita kwa milele!
4 Ee wapenzi, musimame, mutumike kila siku,
Mutafute wapotevu, muwalete kwake Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
215. PENDO LA BABA WA MBINGU
1 Pendo la Baba wa mbingu linanga-a sikuzote ;
Anataka tusambaze nuru yake duniani.
Nuru yetu iangaze mbele ya wenzetu huko ;
Ionyeshe kila mutu njia wazi ya mbinguni.
2 Zambi zimetia giza huko chini duniani ;
Macho ya watu wengine wanatazamia nuru.
3 Ndugu wangu, angalia ta-a yako iwe safi,
Ili mutu asikose kuiona, aokoke!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
216. NINASIKIA MUCHUNGAJI
1 Ninasikia Muchungaji anayeita toka jangwa,
Akiwaita wapotevu kama kondo-o bila zizi.
Uwalete, uwalete, uwalete toka zambi zao;
Uwalete, uwalete, uwalete kwake Yesu.
2 Nani ’takwenda kusaidia kuwatafuta wapotevu,
Kuwaletea Muchungaji, awaokoe toka zambi?
3 Katika jangwa wanalia na kwa vilima na mabonde;
Bwana anakuita wewe: “Kwenda kuwafikisha kwangu.”
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
217. SHAMBA LA MUNGU NI TAYARI
1 Shamba la Mungu ni tayari kuvuna mbegu za kukomea;
Wavunaji, mufike mbio kwa kuyavuna mavuno yake.
Bwana Yesu, tunaomba, uwatume watenda kazi,
Waokote miganda yote, na watapata mavuno
mengi.
2 Uwatume mapema sana, na uwatume saa ya muchana;
Hata sa-a ya mangaribi wengine waje kutenda kazi.
3 Ee Mukristo, usichelewe, lakini kwenda mbio kwa kazi!
Macho yako nyanyua kwani Mwokozi Yesu yuko karibu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
218. SAFARI YANGU HUKO
1 Safari yangu huko ina hatari nyingi,
Na inapita katika giza na jaribu;
Najua kwa hakika, Mwokozi ni karibu,
Na ninamufuata pahali po pote.
Pamoja na Yesu njiani sina woga;
Ni kweli furaha na heri rohoni pahali pote;
Nitayashiriki mateso pamoja naye,
Na nitamufuata Mwokozi hata mwisho
2 Nikitangaza Neno la Mungu duniani
Katika mataifa walio wakaidi,
Nina furaha kubwa moyoni mwangu kwani
Mwokozi ni nami pahali po pote.
3 Na Bwana akitaka nibaki hapa kwangu,
Wengine wakitumwa kwa inchi mbalimbali,
Kusudi langu moja, nidumu kumufuata,
Mungini na vile pahali po pote.
4 Si sharti nifahamu kusudi la Mwokozi,
Ni kazi yangu huko kufuata Kiongozi;
Na hata nikibaki ao hata nikikwenda,
Nitafuata Yesu pahali po pote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
219. EE BWANA, NIWE MUFUATA WA KWELI
1 Ee Bwana, niwe mufuata wa kweli,
Nikupendeze kwa kila wakati,
Nikikutii na furaha daima,
Hii tu ni njia kupata baraka.
Ee Yesu Bwana wangu, ninajitoa kwako,
Sababu ulimwanga kwa mimi damu yako;
Mufalme wangu ndiwe, unitawale sasa,
Maisha yangu yote yawe kwa heshima yako.
2 Ee Bwana, ulijitoa kwa mimi,
Na ulilipa bei ya zambi zangu;
Mapendo haya yananisukuma
Maisha yangu kutoa kwa wewe.
3 Ee Bwana, nikupendeze daima,
Kila wakati nikutumikie;
Mimi tayari kubeba mateso,
Haya, hasara kwa ajili yako.
4 Kuliko mambo mengine yo yote
Ninakusudi kukufurahisha,
Nikiwaleta waliopotea
Karibu nawe wapate uzima.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
220. YESU, NINAUCHUKUA MUSALABA
1 Yesu, ninauchukua musalaba wangu kwawe,
Nina-acha vitu vyote nilivyovipenda mbele,
Baba, mama, na watoto, ndugu, nyumba, mali yote;
Hata hivi ninapata utajiri ndani yako.
2 Watu wengi wanacheka, wananizarau sana,
Wananidanganya vile, wewe tu ni mwaminifu.
Mimi ni mufuata wako, nitakuwa kama wewe.
Walitesa Bwana wangu, na watanitesa vile.
3 Taabu zote za dunia zinanikokota kwako,
Huko unanipa neema, kwako nitapata raha;
Kweli siogopi kwani ninajua unachunga,
Ni furaha sikuzote kukutegemea, Bwana.
4 Nyuma ya maisha yangu nitafika kwako mbingu,
Unaniongoza pale, ninafuata na imani.
Ee furaha kuonana nawe, Bwana na Mupenzi,
Kwa milele nitaimba Haleluya kwako, Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
221. YESU, UNAPITA NDUGU
1 Yesu, unapita ndugu na rafiki za dunia ;
Kwa maisha yangu yote nikufuate tu karibu.
Nikufuate wewe, Yesu, nikufuate wewe, Yesu,
Kwa maisha yangu yote nikufuate tu karibu.
2 Sitamani mali tena wala sifa na heshima.
Kitu hiki ninataka, nikufuate tu karibu.
3 Hata unaniongoza kwa mateso na huzuni,
Nitafika siku moja kupumzika kwako, Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
222. FANYA MAPENZI
1 Fanya mapenzi yako, Ee Bwana,
mwenye akili nyingi kabisa;
Kama udongo unifinyange, ninapongoja kimya kwa wewe.
2 Fanya mapenzi yako, Ee Bwana, unitafute kwa roho yangu;
Unitakase, ninakuomba, niweze kuwa kwawe faida.
3 Fanya mapenzi yako, Ee Bwana, mimi zaifu na ninachoka;
Wewe ni Mwenye nguvu ya kweli, Ee uniguse, uniponyeshe.
4 Fwanya mapenzi yako, Ee Bwana, unitawale, ninakuomba;
Na unijaze na Roho yako watu waone Yesu tu kwangu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
223. KITU KISI-INGIE
1 Kitu kisi-ingie kutenga mimi na Yesu, Bwana mupendwa;
Nimeokoka, sasa sipendi kutenda zambi, Yesu ni wangu.
Kitu kisi-ingie kutenga mimi na Yesu, Bwana
Mupendwa;
Sitaki neno kuhuzunisha Yesu Mwokozi na Bwana
yangu.
2 Kitu kisi-ingie kutenga mimi na Yesu, Bwana Mupendwa;
Vyote Mungu asivyovipenda, ninaviacha kwa Yesu Bwana.
3 Kitu kisi-ingie kutenga mimi na Yesu, nisijisifu;
Hata rafiki wasitutenge, ninakusudi kumupendeza.
4 Kitu kisi-ingie kutenga mimi na Yesu, hata mateso;
Nitamupenda na kumufuata, nitashindishwa kwa nguvu
yake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
224. YOTE KWA MWOKOZI WANGU
1 Yote kwa Mwokozi wangu, kwaye nguvu yangu yote,
Mafikili na matendo, vile siku zangu zote.
Yote kwa Mwokozi wangu, yote kwaye tu daima;
Yote kwa Mwokozi wangu, utukufu na heshima.
2 Hii mikono na migu-u ni kwa kazi yake Yesu;
Macho yatazame ju-u, na midomo imusifu.
3 Tangu nilipotazama Yesu kule kwa Kalvari,
Vitu vyote vya dunia vilikuwa bule kwami.
4 Ee ajabu kubwa, Yesu, yeye Bwana wa wabwana,
Ananipokea kwake na mapendo ya kuzidi!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
225. BWANA, UPOKEE MAISHA YANGU
1 Bwana, upokee maisha yangu yawe yako tu kwa sikuzote;
Na mikono ninakupa itumike kazi ya mapendo
Kwa kukutukuza, Bwana.
2 Hii migu-u yangu upoke-e ikimbie kukutumikia;
Na sauti ukamate kwa kuimba sifa yako, Yesu,
Wewe ni Mufalme wangu.
3 Na midomo vile itangaze Neno lako kwa wenye makosa;
Mali yangu yote iwe mali yako, Yesu Bwana wangu,
Kwa kufanya kazi yako.
4 Kwa migu-u yako, Bwana Yesu, ninatoa mwili wangu wote;
Ee ninakupenda, Bwana, sikuzote ninataka sana
Wewe pekee utukuzwe.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
226. NILIKUBALI KUTOA UZIMA WANGU
1 Nilikubali kutoa uzima wangu kwawe,
Na damu ilimwangika upate kuokolewa;
:: Kwa wewe niliutoa mwili, kwami utatoa nini?::
2 Na niliacha mungini wa Baba wangu ju-u,
Kufika huko dunia na giza lake na taabu;
:: Kwa wewe niliziacha mbingu, kwami uta-acha nini? ::
3 Ee nilibeba uchungu kushinda mafikili,
Usi-ingie kwa moto kuteswa pale milele;
:: Kwa wewe nilizibeba zote, kwami utabeba nini? ::
4 Kutoka kule mbinguni niliyaleta kwako
Mapendo, vile wokovu, na usamehe wa zambi;
:: Kwa wewe niliyaleta yote, kwami utaleta nini? ::
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
227. MIMI WAKO, BWANA
1 Mimi wako, Bwana, nimesikia sauti ya mapendo;
Nina hamu sana kuvutwa tena karibu nawe, Bwana.
Univute, univute kwa musalaba wako, Bwana;
Univute, Bwana, univute kwako nibakie pale tu.
2 Ee, unitakase kwa kazi yako kwa neema, Bwana Yesu;
Roho yangu ikutazame hata ninakupenda pekee.
3 Ni kutamu sana kushinda saa ya maombi mbele yako,
Ninapoinama kusemezana nawe, Mwokozi wangu.
4 Sijajua bado mapendo yako kwa mimi duniani,
Shangwe itazidi saa ya kufika mbinguni kwako, Bwana.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
228. UNATAKA SALAMA
1 Unataka salama na imami zaidi,
Umeomba saa nyingi kushinda ?
Hutapata pumziko ao baraka ya Bwana
Hata unajitoa kwa Mungu.
Umetoa maisha mazima kwa Mungu,
Na Roho anakutawala ?
Utapata baraka na salama moyoni,
Ukimupa mutima na mwili.
2 Unapenda kufanya ma-agizo ya Bwana,
Na kupata salama na nuru?
Sharti umupendeze, kumufuata kabisa,
Ujitoe mwenyewe kwa Mungu.
3 Tutaweza kujua pendo toka mbinguni
Na furaha kuja-a moyoni,
Upatano mutamu kwa migu-u ya Yesu
Kama tukijitoa kwa Mungu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
229. NINAKUSHUKURU, BWANA
1 Ninakushukuru, Bwana, kwani uliniokoa;
Vile ulinisafisha niwe chombo chako safi.
Chombo chako, Bwana Yesu, niko mikononi
mwako,
Unijaze, utumie, kila siku, kila saa.
2 Mimi chombo ’tupu, Bwana, unijaze na baraka;
Hivi maji ya uzima yatatoka ndani yangu.
3 Sina nguvu ila yako, ndiyo Roho yako, Mungu;
Unijaze na uwezo niwe mushuhuda wako.
4 Mimi chombo cha udongo, utukuzwe ndani yangu;
Ulininunua Bwana, niwe kweli mali yako.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
230. YESU, NINAKUTOLEA
1 Yesu, ninakutolea vitu vyangu vyote leo,
Nikupende, nikufuate sikuzote duniani.
Ninakupa vyote, ninakupa vyote;
Vyote kwako, Bwana Yesu, ninakupa vyote.
2 Kwa migu-u yako, Yesu nikunyenyeke-e sasa;
Ninakutolea vyote, roho, mwili, na kutaka.
3 Ninakupa mali yangu, sitaitamani tena ;
Ulikuwa masikini ili niwe mutajiri.
4 Kwa baraka ninakuja, unijaze Roho yako;
Uni’ngoze, nipa nguvu, niwe mushindaji kweli.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
231. NIMEAHIDI, YESU
1 Nimeahidi, Yesu, nitakutumikia;
Usiniache kamwe, Rafiki yangu mwema;
Sitaogopa taabu pamoja nawe, Yesu,
Na sitahangaika, nikiongozwa nawe.
2 Ee Bwana, unichunge katika majaribu
Yanayonizunguka kwa kunitamanisha,
Adui ni karibu, ni hata ndani yangu;
Ee Bwana, karibia na chunga nafsi yangu.
3 Umeahidi, Yesu, kwa watumishi wako
Kukaa pamoja nawe katika utukufu;
Nimeahidi, Yesu, nitakutumikia
Unipatishe nguvu nifuate nyuma yako.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
232. YESU, NIVUTE KARIBU NAWE
1 Yesu, nivutwe karibu nawe,
ninakupenda, Mwokozi muzuri;
Uliyekufa musalabani,
unizungushe na pendo na neema,
Unizungushe na pendo na neema.
2 Yesu, nivutwe, mimi ni bule,
sina zawadi kwa kukutolea;
Mimi muchafu katika moyo,
unipokee, unioshe kwa damu,
Unipokee, unioshe kwa damu.
3 Yesu, nivutwe, nikupe yote
niliyo nayo, Ee Bwana Mupendwa;
Ninakuomba, uyaondoe
yote yanayonitenga na wewe,
Yote yanayonitenga na wewe.
4 Yesu, nivutwe karibu nawe,
hata kwa mwisho wa vita na taabu;
Tena mbinguni nitabakia
karibu nawe, Ee Yesu Mwokozi,
Karibu nawe, Ee Yesu Mwokozi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
233. NASIKIA BWANA YESU
1 Nasikia Bwana Yesu, anaita nimufuate;
Anaponitangulia, nitafuata Yesu njia yote.
Nitafuata nyayo zake, nitafuata nyayo zake,
nitafuata nyayo zake, nitafuata Yesu njia yote.
2 Nitafuata Bwana Yesu hata kwa mateso, kufa,
Nitafufuliwa naye, nitafuata Yesu njia yote.
3 Atanipa neema yake kwa kudumu hata mwisho,
Hata nitakapomwona Yesu Bwana wangu kule mbingu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
234. PAHALI PA SALAMA TAMU
1 Pahali pa salama tamu ni mbele yake Bwana ;
Makosa si pahali pale kwa kututesa tena.
Ee Yesu Mukombozi uliyetumwa kwetu,
Uchunge watu wako wote karibu nawe.
2 Pahali pa faraja nzuri ni mbele yake Bwana;
Tunapoweza kukutana naye Mwokozi wetu.
3 Pahali pa uhuru vile ni mbele yake Bwana ;
Pahali pa furaha tele na ustarehe kweli.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
235. YESU NI RAFIKI YETU
1 Yesu ni Rafiki yetu anayetupenda kweli,
Tunaweza kumwambia mahitaji yetu yote.
Siku nyingi tunabeba taabu na huzuni kubwa,
Kwa sababu tuna-acha kumwambia kila neno.
2 Tunapata majaribu na masikitiko sana;
Tusishinde na huzuni, twende kumwambia Bwana.
Kweli hatuna rafiki kama Yesu Musaidia,
Anayefahamu kwamba sisi ni zaifu sana.
3 Tunachoka na uzito wa makosa sikuzote?
Bwana Yesu ni Mwokozi, atatupokea wote.
Watu wanatuchukia? Twende kumwambia Bwana;
Yeye atatufariji, atachunga na mapendo.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
236. MUKATE WA UZIMA, BWANA
1 Mukate wa uzima, Bwana, uvunje,
Kama zamani kando ya bahari ;
Gawa maneno yako kwa roho yangu ;
Ee nina hamu kubwa kwawe, Yesu.
2 Bariki Neno lako kwa roho yangu;
Kama mukate kule Galilaya,
Nipate kuwa huru toka makosa,
Salama yako itanitawala.
3 Mukate wa uzima ni wewe, Bwana;
Kwa Neno lako nimeokolewa.
Unifundishe, Bwana, ninakusihi,
Kulifahamu na kutii daima.
4 Ee unijaze, Bwana, na Roho yako,
Naye atanifungulia macho;
Atafunua kwami Kitabu chako,
Na ndani yake nikuone, Kristo.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
237. ZAMANI, PENTEKOTE
1 Zamani, Pentekote, Mungu, ulituma nguvu ;
Na hivi leo tunaomba kwa baraka yako.
Ee Mungu, tuma nguvu, uwezo wa zamani,
Baraka ya Roho utume leo, Mungu;
Tuma nguvu yako ya Pentekote, Mungu,
Waovu waokoke, na upate heshima.
2 Kwa kazi za uwezo wako tengeneza mioyo;
Uje na kutawala leo kila mutu wako.
3 Ondosha zambi, washa roho, tuwe na uwezo;
Kwa kila moyo wa kuongoja, Mungu, tia nguvu.
4 Na sasa, Mungu, sisi sote tuko mbele yako ;
Baraka yako tunangoja, usitupitie.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
238. NAKUHITAJI, YESU
1 Nakuhitaji, Yesu, Mwokozi wangu mwema,
Sauti yako nzuri inilete-e raha.
Nakuhitaji, Yesu, muchana na usiku;
Unibariki sasa, ninakukaribia.
2 Nakuhitaji, Yesu, unionyeshe njia,
Na unitimizie ahadi za ne-ema.
3 Nakuhitaji, Yesu, uwe karibu nami,
Nipate kulishinda jaribu la Shetani.
4 Nakuhitaji, Yesu, katika mambo yote,
Kwa kuwa bila wewe, maisha hayafai.
5 Nakuhitaji, Yesu, njiani huko chini,
Nipate kuwa kwako milele na milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
239. YESU, MWENYE PENDO KUBWA
1 Yesu, Mwenye pendo kubwa, usinipitie;
Ndani ya maombi yangu, unibarikie.
Yesu, Yesu, unisikilie,
Ukiwabariki wote, usinipitie.
2 Miaka mengi nilifuata njia ya uovu;
Nilikuwa mutumishi wa mudanganyifu.
3 Ninakiri zambi zangu mbele yako, Bwana;
Roho yangu imevunjwa, uponyeshe sasa.
4 Wewe, Yesu, ni Kisima cha furaha yetu;
Nani Muchungaji mwema ila Bwana Yesu?
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
240. NINAKUOMBA, YESU MUPENZI
1 Ninakuomba, Yesu Mupenzi, nina mizigo mingi mizito;
Katika taabu utasaida, unanipenda na kunichunga.
Ninakuomba, Yesu Mupenzi,
Nina mizigo mingi rohoni;
Ninakuomba, Yesu Mupenzi,
Wewe mumoja utasaidia.
2 Ninakuomba, Yesu Mupenzi, wewe Rafiki mwenye mapendo;
Nikikuomba, utasikia, wewe utaondosha matata.
3 Ninapojaribiwa na nguvu, mutu mwingine hatasaidia;
Ninakuomba, Yesu Mupenzi, kweli utashiriki mateso.
4 Siku nyingine vitu vibaya vinanitamanisha hakika;
Ninakuomba unisaidie, Yesu, unishindishe kabisa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
241. EE YESU, NATAKA USAFI KWA ROHO
1 Ee Yesu, nataka usafi kwa roho,
Nataka uishi daima moyoni;
Ondosha sanamu, uchafu wo wote,
Na unisafishe nipate usafi.
Unisaidie sasa kutubu,
Ee, unisafishe nipate usafi.
2 Ee Yesu, tazama na unisaidie,
Nataka kuishi kwa kukupendeza.
Sitaki kufanya mapenzi ya mwili,
Ee unisafishe nipate usafi.
3 Ee Yesu, sikia na jibu maombi,
Ingia moyoni, unibadilishe;
Nataka salama, nataka furaha,
Ee unisafishe nipate usafi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
242. MUNGU, UMETUMA KWETU ROHO
1 Mungu, umetuma kwetu Roho yako Musaidizi;
Kwa kuishi ndani yetu, vile kutujaza roho.
Unijaze Roho yako, Mungu, unijaze sasa;
Ninaomba kwako, Mungu, unijaze Roho yako.
2 Sifahamu namna gani utakavyofanya hivi;
Bali ninakuhitaji unijaze Roho sasa.
3 Mimi ni zaifu sana, ninaanguka mbele yako;
Sasa unijaze nguvu naye Roho yako, Mungu.
4 Unioshe, ’nifariji, vile unibarikie;
Ninaamini Neno lako; Bwana, unijaze Roho.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
243. SEMA NA ROHO YANGU
1 Sema na roho yangu, Bwana, na pendo kubwa;
Uniambie wazi: “Sitakuacha pekee.”
Moyo ufunguliwe kwa kusikia neno,
Na unijaze roho na pendo, sifa kwako.
Sema na roho yangu, Bwana, na pendo kubwa;
Uniambie wazi: “Sitakuacha pekee.”
Sasa tayari mimi kukusikia, Bwana:
“Utashindishwa nami, na utakuwa huru.”
2 Sema na wana wako kuwaonyesha njia,
Na unijaze tele na shangwe na furaha,
Ili watoe roho kutumikia Mungu
Hata kurudi kwako kwa kuwatwaa mbinguni.
3 Kama ulivyoonyesha nia yako zamani,
Uniyafahamishe mapenzi yako kwami;
Uniongoze jinsi kukutukuza, Bwana,
Hata maneno yako nitayatii daima.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
244. SAA YA MAOMBI
1 Saa ya maombi iko tamu, inatuita kwa Baba Mungu;
Kwa kiti chake cha ne-ema tunaonyesha hitaji letu;
Wakati wa huzuni nyingi faraja nzuri tunapata,
Na tunashinda majaribu wakati tunapo-omba Mungu.
2 Saa ya maombi iko tamu, furaha nyingi kwa roho zetu ;
Kuleta kwake Yesu Kristo mizigo inayotusumbusha.
Tutupe kwake masumbuko, aliahidi kuyabeba;
Na raha ataleta kwetu wakati tunapo-omba Mungu.
3 Saa ya maombi iko tamu, kupata nguvu kwa roho zetu ;
Mwokozi wetu mwaminifu yuko tayari kutubariki.
Inamufurahisha kweli wakati tunapomwamini ;
Anasikia na kujibu wakati tunapo-omba Mungu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
245. UKAE NAMI
1 Ukae nami, giza linafika, usiniache, Mungu, ninaomba,
Sina mwingine kwa kunisaidia, Ee Mufariji, ubakie nami.
2 Nakuhitaji wewe sikuzote, ne-ema yako inanishindisha;
Wewe Mwongozi, wewe Musaidia, katika giza ubakie nami.
3 Uzima unapita mbiombio, dunia yote inaharibika;
Vitu vyo vyote vinapogeuka hubadiliki, ubakie nami.
4 Adui zote sitawaogopa kama mukono wako ni karibu;
Uchungu wa mauti uko wapi? Uliushinda, ubakie name.
5 Saa ya mauti nitakukumbuka, kwa damu yako
nimeokolewa :
Unipoke-e kwako na salama, katika kufa ubakie name.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
246. KUTOKA TAABU YA DUNIA
1 Kutoka taabu ya dunia, kutoka vile huzuni hapa,
Salama tunaipokea karibu na kiti cha rehema.
2 Na pale Yesu anangoja kumwanga kwetu baraka yake;
Nafasi tamu ya kupita, karibu na kiti cha rehema.
3 Katika inchi pa’li pote rafiki zetu wanainama
Kuombeana kwa imani karibu na kiti cha rehema.
4 Shetani anatujaribu, kwa saa ya taabu, huzuni kubwa,
Tutakimbia wapi ila karibu na kiti cha rehema?
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
247. MVUA YA MBINGU INYESHE
1 Mvua ya mbingu inyeshe kama ulivyoahidi;
Ju-u ya inchi po pote iwe kwa kutubariki.
Mvua ya mbingu, mvua ya mbingu utume;
Utunyeshe-e baraka, tunakuomba, Ee Mungu.
2 Mvua ya mbingu inyeshe kwa kulegeza udongo;
Ju-u ya bonde, vilima, mvua ya mbingu ifike.
3 Mvua ya mbingu inyeshe, katika dunia yote ;
Watu wa Mungu wawake, mbengu za roho ziote.
4 Mvua ya mbingu inyeshe, tunapokukaribia;
Ututumie baraka, tunakuomba, Ee Mungu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
248. MUNGU WETU MWAMINIFU
1 Mungu wetu mwaminifu ametuahidi sisi
Kusikia na kujibu kama tukiomba kwake.
Mungu atatusikia kama tukiomba kwake;
Twende sasa na imani, kweli atatusikia.
2 Mungu atatupa sisi vitu vyote kututosha;
Kitu gani ni kizuri tutakipokea kwake.
3 Tusi’gope kumwambia mahitaji yetu yote,
Ao makubwa ao madogo, anapenda kusikia.
4 Kwa furaha ao huzuni kila pa’li na saa zote,
Tukimwomba tunajua kwamba atatusikia.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
249. OMBA, OMBA KWA MUNGU PEKEE
1 Omba, omba kwa Mungu pekee, usiache kuomba kwake;
Kweli Mungu aliahidi kukujibu kwa kila kitu.
2 Omba, omba saa ya hitaji, Mungu atasikia kweli;
Hata neno ni dogo sana, umwambie, analijua.
3 Omba, omba saa ya jaribu, utashinda kwa jina lake;
Bwana Yesu anafahamu, atashika mukono wako.
4 Omba, omba na kumwamini, tunapaswa kuomba kwake;
Na imani ngojea Mumgu, usiache, atakujibu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
250. UNIPE USAFI ZAIDI ROHONI
1 Unipe usafi zaidi rohoni,
Nione huzuni zaidi kwa zambi;
Imani zaidi kwa Yesu Mwokozi,
Furaha kwa kazi, vile kwa maombi.
2 Niwe na asante zaidi kwa Mungu,
Na matumaini katika Kitabu,
Machozi zaidi kwa taabu ya Bwana,
Na unyenyekevu, upole, na neema.
3 Unipe uwezo kushinda jaribu,
Na vile uhuru na utakatifu,
Na hamu kuona ufalme wa mbingu,
Ili nifanane na Yesu zaidi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
251. BWANA, FUNGUA MACHO YANGU
1 Bwana, fungua macho yangu kwa kufahamu Neno lako;
Unionyeshe mambo matamu ndani ya Neno lako, Bwana.
Ninainama sasa kwako, unionyeshe kweli yako,
Vile mapenzi yako, Bwana, ninakusihi.
2 Bwana, fungua masikio kwa Neno lako nisikie,
Kwani sauti yako ni tamu, inanichunga kwa jaribu.
3 Bwana, fungua kinywa changu niwe tayari kutangaza
Kwa wapotevu kila pahali, wewe uliwakufilia.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
252. YESU MWOKOZI, MWANA WAKE MUNGU
1 Yesu Mwokozi, Mwana wake Mungu,
Mara nyingine tunakuabudu,
Siku ya leo ulitusaidia,
Tena kwa kesho ututangulie.
2 Nyuma kidogo jua ’taingia,
Katika giza utuangalie;
Na uzilinde roho za Wakristo,
Wewe ni zamu, Yesu Kristo Bwana.
3 Sisi tungali hapa kwa dunia,
Wengine wengi wanatuchukia;
Utupe sisi utulivu wako,
Vile salama, Bwana Yesu Kristo.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
253. UNACHOKA, UNA ROHO NZITO,
1 Unachoka, una roho nzito?
Sema na Yesu, sema na Yesu;
Na furaha imekwisha yote?
Sema na Yesu pekee.
Sema na Yesu, sema na Yesu,
Yeye Rafiki wa kweli;
Si mwingine sawasawa naye.
Sema na Yesu pekee.
2 Unalia kwa huzuni nyingi?
Sema na Yesu, sema na Yesu;
Roho yako inaficha zambi?
Sema na Yesu pekee.
3 Nduku zako wanakuchukia?
Sema na Yesu, sema na Yesu,
Walimukata-a Yesu vile,
Sema na Yesu pekee.
4 Unajaribiwa sikuzote?
Sema na Yesu, sema na Yesu;
Anajua sisi ni zaifu.
Sema na Yesu pekee.
(voir la suite sur la page suivante)
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
5 Unakosa mali ya dunia?
Sema na yesu, sema Yesu;
Anachunga kila ndege vile.
Sema na Yesu pekee.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
254. SASA MANGARIBI
1 Sasa mangaribi, jua limeshuka,
Giza la usiku limetushukia.
2 Yesu, ninataka kupumzika kwako;
Na baraka yako nitafunga macho.
3 Katika usiku tuma malaika
Wanilinde mimi kando ya kitanda.
4 Kisha asubui, hata mangaribi,
Leta nguvu, haki, kwa kukupendeza.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
255. BWANA, KWA USIKU HUU
1 Bwana, kwa usiku huu utubarikie wote;
Tunakiri zambi zetu, usamehe, tunaomba.
2 Giza linatuzunguka, na hatari ni karibu,
Tuma malaika zako kusimama kando yetu.
3 Giza halitakuficha, wewe ni karibu nasi;
Kweli hutalala kamwe, wewe ni Mulinzi wetu.
4 Hata kufa kutafika katikati ya usiku,
Nitakuwa asubui mbele yako kule mbingu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
256. SIKU BARAGUMU YAKE MUNGU
1 Siku baragumu yake Mungu itakapolia,
Pambazuko la milele litanga-a;
Siku ile sisi wa-amini tutaona Yesu,
Ataita kila jina kwa Kitabu.
Ataita kila jina, ataita kila jina,
Ataita kila jina, ataita kila jina kwa Kitabu.
2 Siku ile watu walioamini Bwana Yesu
Watafufuliwa kwanza kwa mawingu;
Kisha wa-amini ha-i watanyanyuliwa vile,
Ataita kila jina kwa Kitabu.
3 Tujitoe kwa kutumikia Bwana yetu Yesu,
Tufundishe watu njia ya wokovu,
Na wakati kazi yetu itakapokwisha huko,
Ataita kila jina kwa Kitabu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
257. SIKU NYINGINE TAABU ’TAKWISHA
1 Siku nyingine taabu ’takwisha, vile huzuni na majaribu;
Siku nyingine tutapumzika, saa ya kurudi kwa Bwana Yesu.
Siku nyingine Yesu Mwokozi atatokea
kutukamata;
Tutasikia sauti yake akituita sisi na wewe.
2 Unasumbuka? Utafurahi! Utasahau kila huzuni.
Utafanana naye Mwokozi, na utamwona uso kwa uso.
3 Tutakutana naye kwa hewa, kisha furaha itatimia;
Tutaonana na ndugu zetu, tutatukuza Kristo milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
258. WATU WA KRISTO, ANGALIENI
1 Watu wa Kristo, angalieni, mwone alama za kuonyesha
Kwamba Mwokozi atatokea, ni yeye tunayemungoja na
hamu.
Atarudi hakika, atarudi hakika,
Ni Yesu mwenyewe waliyemukana ;
Atarudi hakika, atarudi hakika,
Mwenye utukufu atarudi hakika.
2 Huko dunia, giza na zambi zinazunguka watu wa Mungu ;
Mioyo mizito itageuzwa kupata furaha kwa siku ya Bwana.
3 Kuja, Mupenzi, tunakungoja, hamu ya kukuona ni kubwa ;
Tutakutana ndani ya hewa, taraja hii tamu : milele na wewe.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
259. YESU ATAKAPOKUJA TENA
1 Yesu atakapokuja tena kwa kutupeleka kwake,
Atatukuta tayari kweli, ta-a zetu zikinga-a ?
Ndugu, wewe ni tayari sasa kukutana naye
Bwana ?
Saa zote wewe ni mwaminifu?
Leo unatazamia yesu?
2 Atatuita na jina letu kusimama mbele yake;
Ukimutoa habari zako, atakuambia: “Vema”?
3 Hakose sisi ni waaminifu, tukitumikia Bwana?
Na roho safi tunangojea kuja kwake na furaha?
4 Heri ni wale wanaongoja kushiriki utukufu;
Yesu atakapo-onekana, watakwenda naye ju-u.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
260. BONDE LA MAUTI
1 Bonde la mauti halitakuwa siku Yesu atakaporudia,
Bonde la mauti halitakuwa, atatupokea kwake.
Atatupokea kwake kwa kuishi naye milele;
Tuta-acha dunia ya huzuni kupata furaha kwake.
2 Sikitiko halitakuwa kamwe siku Yesu atakaporudia,
Sikitiko halitakuwa kamwe, atatupokea kwake.
3 Na kilio hakitakuwa tena siku Yesu atakaporudia,
Na kilio hakitakuwa tena, atatupokea kwake.
4 Nyimbo za furaha tutamwimbia siku Yesu atakaporudia,
Nyimbo za furaha tutamwimbia, atatupokea kwake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
261. NINANGOJA ASUBUI
1 Ninangoja asubui, ndiyo siku ya baraka,
Siku taabu na huzuni zitakapokwisha pia;
Na pamoja na Mwokozi, mbali na dunia hii,
Nitashinda kumwabudu kwa milele.
2 Ninangoja utukufu, unanga-a toka mbali,
Wa Mwokozi wangu Yesu, ndiye “Nyota ya ’subui” ;
Katika mapambazuko nitaona nuru yake,
Na usiku utakwisha, taabu, zambi, na kuchoka.
3 Nitangoja Bwana yangu, aliyenikufilia;
Tamu ni ahadi yake, “Nitarudi kukuita”.
Kuja kwake ni karibu, ndiyo, ni karibu sana,
Hamu kwaye inazidi, hamu ya kufika kwake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
262. BWANA, NINAKUNGOJEA
1 Bwana, ninakungojea kwa kukutazama,
Bwana, ninakungojea kurudi kwa mimi.
Umekwenda mbinguni kunitengenezea
Nyumba nzuri mbinguni karibu na Baba.
2 Hapa ninaona woga, kuchoka kabisa,
Kweli siku ni karibu utakapokuja.
Kwako tu ni furaha, si machozi na taabu,
Utukufu mukubwa utakaporudi.
3 Hata sasa ninataka nikupe furaha,
Siku chache zinabaki kukutumikia.
Ninangoja kuona macho yako, Ee Bwana.
Shangwe kubwa kuzidi utakaporudi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
263. HAKOSE LEO TU
1 Hakose leo tu, tutaona Yesu Rafiki yetu,
Mwenye kuleta furaha, na mwisho wa taabu zote.
Tufurahi, Yesu atarudia ;
Tuishi kwa leo bila woga, kweli Mwokozi
tutamwona ; Tufurahi, Yesu atarudia.
2 Hakose leo tu, tutakwenda kwetu mbinguni juu ;
Tutafurahi kabisa, akitufikisha leo.
3 Tufazaike nini ? Tutashinda kwani Mwokozi wetu
Yuko pamoja na sisi kwa sasa na sikuzote.
4 Tuwe watoto wake waaminifu, tukimutumikia,
Tukihubiri habari za Yesu Mwokozi wetu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
264. YESU ATATAWALA HAPA
1 Yesu atatawala hapa katika mataifa yote,
Na kila mutu wa dunia atamutambua yeye Bwana.
2 Toka kusini, kaskazini, watainama kwake Bwana;
Hata wafalme na wajinga watasikia Neno lake.
3 Atatawala na salama, watu watamusifu Bwana,
Na watapenda jina lake kama malasi tamu sana.
4 Watu wa makabila yote wataimbia pendo lake;
Vile sauti za watoto zitabariki jina lake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
265. SIKU MWANA WAKE MUNGU ATAKAPORUDIA
1 Siku Mwana wake Mungu atakaporudi hapa
Tutaona utukufu wake wazi;
Ataita watu wake toka mataifa yote,
Makutano ya furaha ya waamini.
Makutano ya furaha,
Watu walioamini watakusanyika wote;
Makutano ya furaha
Ya waamini kwa mungini wa Mwokozi.
2 Na waliokufa mbele wakimusadiki Yesu,
Toka kimya ya kaburi na bahari,
Watapata mwili mupya, watakwenda nasi vile,
Makutano ya furaha ya waamini.
3 Macho yetu yataona muji wetu kwa mbinguni,
Vile muto ukitelemuka kimya;
Na rafiki tutaona waliotutangulia,
Makutano ya furaha ya waamini.
4 Ee Mufalme anakuja, atarudi mbio sana,
Siku ya ahadi yake tutaona;
Tutabadilishwa mbio, kama kupepesa macho,
Kwa milele tutaka-a na Mwokozi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
266. WANANIAMBIA HABARI ZA MBINGUNI
1 Wananiambia habari za mbinguni,
Wanasema nyumba nyingi ni kule,
Wanasema ni pahali pazuri sana,
Wananiambia ju-u ya mbingu.
Inchi ile nzuri sana,
ni mungini wa Mungu Mwenyezi;
Wananiambia ju-u ya nyumba yangu
Inayoningoja pale mbinguni.
2 Wananiambia kwamba rafiki wengi
Wananingojea sana mbinguni;
Kule muto wa uzima wenye kungaa
Unatoka kiti cha Mungu Baba.
3 Wananiambia Mufalme yuko pale,
Nitamutazama uso kwa uso;
Wala laana haitakuwa tena kweli
Kwa mungini wa zahabu mbinguni.
4 Wananiambia Yesu atapangusa
Kila chozi la watoto wa Mungu;
Wanasema taabu haitakuwa tena,
Ni furaha tu pahali pa mbingu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
267. KUNA MUJI MUZURI MBINGUNI
1 Kuna muji muzuri mbinguni, kwa imani tunautazama,
Baba Mungu anapotungoja kwa furaha kutukaribisha.
Tutaona Yesu Bwana, vile ndugu waliomwamini,
Tutaona wao wote kule mbingu, pahali pa Mungu.
2 Tutaimba kwa muji wa ngambo nyimbo za wenye
kubarikiwa;
Taabu itaondoshwa kwa roho, ustarehe pasipo kulia.
3 Kwa mapendo ya Baba wa mbingu na baraka anazozitupa,
Tutapiga asante ya kweli, vile tutamusifu milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
268. IMBA PENDO LA MWOKOZI
1 Imba pendo la Mwokozi, imba neema na rehema;
Anatengeneza nyumba pa’li tutakapoishi.
Tutakwenda mbinguni, tutaimba na kumusifu
Yesu!
Tutaona Bwana, tutamwimbia Haleluya!
2 Wasafiri duniani, sisi watu wa mbinguni;
Kisha tutafika kwake, tuta-acha taabu zote.
3 Ndungu, tuwe waaminifu, kila siku, kila saa;
Tutakapo-ona Yesu, taji zetu tutapata.
4 Twende mbele, tutumike, tutamutazama ju-u;
Mbingu zitafunguliwa; kwa milele tumusifu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
269. NINATAZAMA MBINGU MBALI
1 Ninatazama mbingu mbali, ninaona kwa imani,
Muji ule ni muzuri, safi kama bilauri.
Ee, muji ule wa mbinguni, muji ule ni muzuri,
Kule kuna nyumba nyingi, zinangoja kwa
waamini ;
Nina hamu ya kufika, kwa milele kupumzika.
2 Misingi ya ukuta wake mawe ya bei ya damani;
Njia yake ni zahabu safi kama kioo wazi.
3 Hauhitaji jua wala mwezi kuangaza pale,
Kwa ma-ana nuru iko utukufu wake Mungu.
4 Na kila kitu cha uchafu hakitaingia kamwe,
Wale walioandikwa kwa Kitabu watakuwa.
5 Na watumishi wake Mungu wataona uso wake,
Na watatawala naye kwa milele na milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
270. EE FURAHA KUONANA
1 Ee furaha kuonana na Mwokozi wangu Kristo,
Kutazama uso wake aliyenikufilia!
Nitaona uso wake kule mbingu kwa milele;
Nitaona Mukombozi, utukufu wake wote!
2 Sasa macho yanaona nusu tu katika giza ;
Kule nitaona wazi utukufu wa Mwokozi.
3 Shangwe gani kwake Yesu ! Taabu yote itakwisha,
Yote itatengenea, nuru itashinda giza.
4 Nitaona uso wake, nitajua Bwana wangu,
Aliyenipenda sana, Mukombozi Yesu Kristo.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
271. SIKU ZANGU ZITAKAPOTIMIA
1 Siku zangu zitakapotimia hapa chini,
Nitaona asubui ya uzima,
Nitaona mbinguni Mukombozi wangu Yesu,
Na “Karibu” yake nitasikia.
Nitamutambua Yesu, na karibu naye nitabakia,
Nitamutambua Yesu kwa alama za majeraha yake.
2 Itakua furaha kutazama uso wake
Na uzuri wa kutoka macho yake;
Moyo utafurika kwa uheri na furaha
Kwa pahali aliponifanyizia.
3 Na walio mbinguni wananigojea kwao,
Nakumbuka siku tulipoachana;
Wataimba kabisa kunikaribisha kule,
Hata hivi nitamwona Yesu kwanza.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
272. KUNA MUJI KULE MBINGU
1 Kuna muji kule mbingu, umejengwa naye Mungu,
Pale muto wa uzima ni karibu na kiti cha Mungu.
Tutakusanyika ngambo
kuona Bwana wetu Yesu Kristo ;
Tutakusanyika na waamini kusifu Mwokozi milele.
2 Kule ngambo inchi nzuri, bila zambi na huzuni,
Nyimbo mpya tutaimba, nyimbo kusifu Yesu Mwokozi.
3 Wenye lugha mbalimbali wataabudu Mukombozi.
Makabila ya dunia watasifu Mwokozi pamoja.
4 Sasa sisi ni karibu kutazama muji ule ;
Mungu atatupa raha na kutufurahisha milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
273. TUTAFUFUKA KUSIMAMA
1 Tutafufuka kusimama mbele yake Bwana Yesu;
Habari zetu tutatoa kwake kwa matendo yetu.
Nitaonekana mbele yake, jina langu litaitwa naye;
Sita’gopa, ninaamini damu ya Mwokozi Yesu.
2 Nitapokea taji ya uzima mikononi mwake;
Nitaitupa mbele yake Yesu anayestahili.
3 Tutakutana kwa milele pale, taabu itakwisha;
Mizigo tuta-acha kwa miguu ya Yesu Mukombozi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
274. KUNA MUJI WA FURAHA
1 Kuna muji wa furaha mbali, mbali sana;
Wenye kuamini Bwana watakwenda pale.
Tutaimba kwa milele sifa kwa Yesu Mufalme
Anayestahili yote, sifa, sifa kwake.
2 Kuja ku-ungana nasi, unangoja nini ?
Usibishe Yesu hivi, kuja kumwamini.
Tutakuwa na uhuru toka zambi, toka taabu,
Tutaishi naye Yesu, tutabarikiwa.
3 Kule Baba anachunga watu kwa mapendo,
Hivi tukimbie sana, tuna mashindano.
Atawapa wote taji, wenye kumufuata kweli,
Na tutatawala naye kwake kwa milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
275. TUWAZE MUNGINI WA MBINGU
1 Tuwaze mungini wa mbingu,
ndiyo ngambo ya muto wa nuru,
Watu watakatifu ni kule,
wanavikwa mavazi meupe.
:: Kule ngambo, kule ngambo, tuwaze mungini wa mbingu ::
2 Tuwaze rafiki kwa mbingu,
walitutangulia zamani,
Wataishi karibu na Mungu,
pale wanamwabudu daima.
:: Kule ngambo, kule ngambo, tuwaze rafiki kwa mbingu::
3 Tuwaze Mwokozi wa mbingu,
alikufa na alifufuka;
Sasa anatungoja tufike,
tutamufurahia na shangwe.
:: Kule ngambo, kule ngambo, Tuwaze Mwokozi wa
mbingu::
4 Saa tutakapofika kule
ni karibu, na tutaonana
Na rafiki na ndugu za ngambo,
pamoja na Yesu Mwokozi.
:: Kule ngambo, kule ngambo, tuwaze furaha ya mbingu ::
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
276. JESHI KUU LA MALAIKA
1 Jeshi kuu la malaika wali-imba kule mbingu,
Utukufu kwake Mungu, na salama kwa dunia.
Kila mutu amusifu na kumutukuza sana;
::Tuheshimu Yesu Kristo yeye ndiye Mukombozi::
2 Ee kujeni tumwabudu, ni Mufalme wa wafalme;
Mungu, Baba ya mapendo, alituma Mwana wake.
Alikuwa kama Mungu, alikuja kama mutu;
:: Alitoka kule mbingu kuokoa watu wote::
3 Mushango wa ajabu, Mungu amefika huko;
Ametupa nuru yake na uzima na wokovu.
Aliacha utukufu na alijinyenyekeza,
::Kristo, Mwana wake Mungu, yeye Bwana wa mbiguni ::
4 Leo malaika ju-u wanafurahia Yesu
Sisi tumwabudu vile, yeye tu anastahili.
Tuiname kwake Yesu, yeye pekee ni Mwokozi;
:: Sifa iwe kwake Mungu, yeye Bwana wa milele ::
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
277. MALAIKA ZA MBINGUNI
1 Malaika za mbinguni walitoka kwake Mungu,
Walikuja kutangaza kuzaliwa kwa Mwokozi.
Tuabudu, tuabudu Yesu Kristo Mukombozi.
2 Wachungaji walichunga kundi lao kwa usiku;
Waliona nuru kubwa ikinga-a toka mbingu.
3 Wa-akili toka mbali walifuata nyota yake;
Walikuja na zawadi kuabudu Yesu Kristo.
4 Kwa mutima wako kweli Kristo ni Mufalme vile?
Kila siku na mapendo unatumikia Yesu?
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
278. EE MUJI WA BETELEHEMU
1 Ee muji wa Betelehemu, unalala kimya,
Na nyota nyingi kule mbingu kimya zinapita;
Kwa ndaki zako nuru ya mbingu inanga-a;
Linatimizwa kwako leo tumaini lote.
2 Maria aliza-a Bwana Yesu kwa usiku,
Na malaika walikuja na habari tamu.
Ee, nuru kubwa gani ya nyota ilinga-a
Mbinguni kuonyesha pa’li alipozaliwa !
3 Zawadi kubwa sana Mungu alituletea
Kwa saa alipotutumia Mwana wake hapa;
Atapokea wote wanaomusadiki,
Anafurahi kuingia kuondoa zambi.
4 Mutoto wa Betelehemu, tunaomba sana,
Ondoa zambi na kuosha roho zetu sasa ;
Ukae ndani yetu, kubaki sikuzote,
Rafiki, Mufariji, na Mufalme kwa milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
279. TUNAFURAHI LEO
1 Tunafurahi leo, tunasifu Mungu sana,
Kwa maana alitukumbuka na kutoa Bwana
Aliyekuja kuokoa watu wenye zambi.
Sikieni habari za faraja, vile furaha ;
Ni Habari Njema ya Mwokozi Yesu.
2 Usiku wachungaji walilinda kundi lao,
Tazama, malaika alionekana kwao;
Waliogopa sana wakiona nuru kubwa.
3 “Musiogope”, malaika aliwa-ambia,
“Habari za furaha ninawaletea ninyi;
Amezaliwa kwenu leo Kristo ndiye Bwana.”
4 Na wachungaji waliacha kundi, wakisema,
“Ee, twende zetu kwa haraka kwa Betelehemu,
Tuone neno hili lililofanyika leo.”
5 Walipofika wakakuta mama na Mutoto
Aliyelala kwa sanduku iliyo ya nyama;
Wakatukuza Mungu, wakamushukuru sana.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
280. NYUMBANI MWA NGOMBE
1 Nyumbani mwa ngombe kwa Betelehemu,
Mutoto wa Mungu alipozaliwa;
Kwa nyasi Maria alimulalisha,
Na jeshi la mbingu walimutukuza.
2 Na hakuogopa kulia kwa ngombe,
Mutoto wa Mungu alilala kimya.
Ee ninakupenda kabisa, Mwokozi;
Bakia karibu na mimi saa zote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
281. FURAHA KUBWA KWA DUNIA
1 Furaha kubwa kwa dunia, Mufalme amekuja!
Na tumufungulie mioyo aingie,
Yeye Mufalme wetu, Yeye Mufalme wetu
Mufalme na vile Bwana wetu.
2 Furaha kubwa kwa dunia, Mwokozi ni Mufalme!
Viumbe vyake vyote, imbeni sifa kwake.
Musifu na furaha, Musifu na furaha,
Musifu na wimbo wa furaha.
3 Masikitiko yatakwisha, na laana la dunia!
Kusudi lake Bwana kutubariki sana,
Na kuondosha zambi, na kuondosha zambi,
Kusudi ni kuondosha zambi.
4 Anatawala na rehema, na haki na mapendo!
Tunashanga-a sana kwa pendo lake Bwana,
Na utukufu wake, Na utukufu wake,
Mapendo na utukufu wake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
282. KUNA WIMBO MUZURI
1 Kuna wimbo muzuri, kuna nyota mbinguni,
Kwa sababu Maria anaza-a mutoto ;
Nyota hii inanga-a katika usiku
Kwani amezaliwa Mwokozi Mufalme.
2 Kuna shangwe kabisa kwa usiku wenyewe,
Maana Yesu mutoto ni Mwokozi wa watu;
Ndiyo, nuru ya nyota ’nanga-a vizuri
Kwani amezaliwa Mwokozi Mufalme.
3 Nuru ya nyota ile, tangu siku ya kale,
Inanga-a katika roho za wa-amini ;
Vile wanafurahi kwa wimbo muzuri,
Kwani amezaliwa Mwokozi Mufalme.
4 Tunaifurahia nuru ya nyota ile,
Tunaimba pamoja na majeshi ya mbingu ;
Kwa habari za Yesu tunashangilia,
Kwani amezaliwa Mwokozi Mufalme.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
283. KUJENI KUSIFU NA FURAHA
1 Kujeni kusifu na furaha nyingi,
Kujeni kusifu Yesu ndiye Mwokozi;
Alizaliwa kuwa Mukombozi.
Kujeni kumwabudu, kujeni kumwabudu,
Kujeni kumwabudu Yesu Mwokozi.
2 Bikira Maria aliza-a Yesu,
Ni Mwana wa Mungu, vile Mwana wa mutu;
Aliondoa utukufu wake.
3 Pamoja na jeshi la mbinguni ju-u
Tusifu na kuabudu Yesu daima ;
Mwana wa Mungu anapata mwili.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
284. KWA USIKU WA ZAMANI
1 Kwa usiku wa zamani, yote kimya, takatifu,
Mama na Mutoto Yesu walilala kwa kizizi,
Na salama ya mbingu, na salama ya mbingu.
2 Kwa usiku wa zamani, wachungaji waliona
Nuru kubwa kule mbingu, malaika wakasifu,
Haleluya kwa Mungu, Haleluya kwa Mungu!
3 Kwa usiku wa zamani, wa-akili toka mbali
Walifuata nyota kubwa kutafuta Bwana Yesu.
Wakileta zawadi, wakileta zawadi.
4 Kwa usiku wa zamani, Mungu, tunakushukuru ;
Kwa mapendo ya ajabu, ulituma kwetu Yesu
Kuokoa dunia, kuokoa dunia.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
285. ULIACHA MBINGUNI NA UTUKUFU
1 Uliacha mbinguni na utukufu
Kufika dunia kwa mimi,
Saa ulipozaliwa kwa Betelehemu
Nafasi hukuipata.
Ingia moyoni mwangu,
Bwana, nina nafasi kwawe.
2 Malaika za mbingu walikusifu,
Mufalme mukubwa wa mbingu,
Ulijifanya kuwa bila utukufu,
Na ulijinyenyekeza.
3 Mbweha wana matundu, na ndege vile
Kwa miti vioto vyao;
Kwawe Mwana wa Mungu, sanduku ya nyama
Ni kama kitanda chako.
4 Ulikuja na neno lenye uzima
Kwa kutufungua sisi ;
Watu walikufunga na kukupeleka
Kwa kufa musalabani.
5 Kisha siku nyingine utarudia,
Mufalme wa utukufu ;
Utani-ita kwako, ukiniambia :
‘‘Mbinguni nafasi iko’’ NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
286. KULE MUJI WA DAUDI
1 Kule muji wa Daudi pa’li pa kulisha nyama,
Mama alimulalisha Mwana wake na mapendo;
Mama yule ni Maria, Mwana wake Yesu Kristo.
2 Yesu aliacha mbingu, akakuja duniani,
Nyumba yake, zizi bule; na kitanda chake, nyasi;
Alikuwa masikini na munyenyekevu sana.
3 Siku za utoto wake, vile siku za ujana,
Mwana wa kusikiliza, aliti-i mama yake;
Na watoto wa-amini wanapaswa kuwa hivi.
4 Alikwenda pa’li pote, akifanya kazi njema,
Naye akawaponyesha watu wengi wa ugonjwa;
Akakufa kwa Kalvari kwa ajili yetu yote.
5 Tutamwona waziwazi, kwani ametukomboa;
Mwana yule ni Mwokozi, vile Bwana wa wabwana;
Naye anatuongoza hata atakaporudi.
6 Hatutamukuta tena pa’li pa kulisha nyama;
Tutamwona kule mbingu, Bwana mwenye utukufu;
Kama nyota watu wake watamuzunguka wote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
287. YESU AMEFUFULIWA
1 Yesu amefufuliwa, Haleluya!
Tumusifu sisi sote, Haleluya!
Mufurahi, ’mutukuze, Haleluya!
Malaika, mumwimbie, Haleluya!
2 Yesu ametuokoa, Haleluya!
Kazi yake imekwisha, Haleluya!
Mushindaji wa Shetani, Haleluya!
Tunamutolea sifa, Haleluya!
3 Jiwe halikumufunga, Haleluya!
Alitoka kwa kaburi, Haleluya!
Hakushindwa na mauti, Haleluya!
Alivunja nguvu yake, Haleluya!
4 Yesu ni Mufalme mwema, Haleluya
Yeye hai kutuombea, Haleluya !
Tutamwona kule ju-u, Haleluya !
Tutakuwa kama Yesu, Haleluya !
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
288. YESU ALIPOLALA
1 Yesu alipolala kati’ kaburi,
Giza lilifunika Yesu Mwokozi.
Alifufuka hakika, akavunja nguvu ya mauti;
Mushindaji ju-u ya mamlaka yote
Ni Mufalme wa milele na milele;
Alikuwa amekufa, na tazama, amefufuka!
2 Walinzi wa kaburi walikimbia;
Muhuri na vifungo vilivunjika.
3 Kufa hakukushika maiti yake,
Alilivunja pingu, Yesu Mwokozi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
289. MWOKOZI ANAISHI
1 Mwokozi anaishi, ni hapa duniani;
Ni neno la hakika, ni neno la furaha
Ananihurumia, ananifurahisha,
Aa anaka-a karibu siku zote.
Mwokozi ni hai, ni hai kwa milele,
Anatembea nami kwa safari yangu yote ;
Mwokozi ni hai, tayari kuokoa,
Na ninajua namna gani? Ni hai moyoni mwangu!
2 Ananipenda kweli na kunichunga sana,
Na hata ninachoka, nadumu kumufuata;
Katika mambo yote Mwokozi ndiye Bwana,
Kufika siku atakaponitwa-a.
3 Nasi Wakristo wote, tusifu sikuzote,
Tuimbe Haleluya kwa Kristo na Mufalme;
Anapokea wote wanaofika kwake,
Hakuna anayependa kama yeye.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
290. KRISTO ALIACHA UTUKUFU
1 Kristo aliacha utukufu kufika dunia yenye zambi,
Alivikwa taji ya mi-iba, na alinilipia deni yote.
Yeye ni hai, yeye ni hai,
Amezishinda zambi na kaburi ;
Yeye ni hai, yeye ni hai,
Atarudia kwami.
2 Mushindaji alitoka kufa, na alirudia mbingu kwake;
Atakuja tena kunitwala, ili niende na kuishi naye.
3 Wewe unayesumbuka sana, Mwokozi anakuita sasa,
Uamini Yesu kupokea kwake uzima, shangwe, na salama.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
291. NAJUA YESU ANAISHI
1 Najua Yesu anaishi, yeye ni hai mbinguni kweli;
Sababu alishinda kufa, vile uwezo wa kaburi.
Najua Yesu anaishi, yeye ni hai mbinguni kweli;
Najua Yesu ananipa uzima na uwezo wake.
2 Najua atakuja tena, nina ahadi yake hivi;
Na siku nitakapomwona furaha itakuwa nyingi.
3 Najua anatengeneza pahali nitakapoishi;
Na atakuja kuni-ita na kunikaribisha kwake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
292. KWAKO HESHIMA
1 Kwako heshima, Kristo Mushindaji,
Kwako utukufu, sifa kwa milele.
Toka kwako mbingu yule malaika
Alifingirisha jiwe la karibu.
Kwako heshima, Kristo Mushindaji,
Kwako utukufu, sifa kwa milele.
2 Tazama Yesu akishida kufa,
Yeye ni Mwokozi, yeye Bwana yetu.
Wenye kuamini, mutangaze wazi
Neno lake Kristo ndiye Mushindaji.
3 Sitaogopa, Yesu anaishi
Ninayemupenda, Bwana ya salama.
Ninashinda naye kwa uwezo wake;
Yeye ni uzima, utukufu wangu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
293. RAFIKI WA WATOTO
1 Rafiki wa watoto ni Kristo Bwana Yesu,
Hawezi kugeuka, ni sawa kila siku;
Rafiki za dunia wanageuka sana,
Rafiki ndiye Yesu ni sawa tu daima.
2 Pumziko kwa watoto ni kwake Baba Mungu,
Wenye kupenda Yesu wataingia mbingu;
Mateso, maumivu, na zambi zitakwisha,
Furaha itazidi karibu naye Baba.
3 Na nyumba kwa watoto ni kwa mungini wake,
Anatawala kule na shangwe na salama;
Na hapa duniani si kama kwake kule,
Pahali pa furaha kwa wenye kumwamini.
4 Na taji kwa watoto kuva-a kule mbingu
Ni taji ya kunga-a, na vile utukufu,
Mwokozi atawapa watoto waminifu,
Wenye kupenda Bwana na wenye kumutii.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
294. YESU ANAPENDA KWELI
1 Yesu anapenda kweli, Neno lake linasema;
Yeye ndiye mwenye nguvu, sisi sote ni zaifu.
Ananipenda, ananipenda ;
Ananipenda, Biblia inasema.
2 Anapenda, alikufa kwa kuniokoa kweli;
Ataosha moyo wangu ni-ingie muji wake.
3 Na anatupenda sawa saa ya afya na ugonjwa ;
Anachunga kila siku watu wake kwa dunia.
4 Anapenda, atakuwa Mungu wangu sikuzote ;
Nikipenda Yesu kweli, atanipeleka kwake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
295. NINAFURAHI SABABU MWOKOZI
1 Ninafurahi sababu Mwokozi
Anataganza mapendo kwa wote;
Ni mushangao mukubwa zaidi,
Ananipenda mwenye zambi nyingi.
Ninafurahi ananipenda,
Yesu Mwokozi ananipenda,
Ninafurahi ananipenda,
Ananipenda mimi.
2 Kama nikimusahau Mwokozi
Na nikikwenda kwa njia nyingine,
Saa nitakapokumbuka mapendo,
Nitarudia karibu na Mungu.
3 Wimbo mumoja tu nitamwimbia
Nitakapomutazama Mupendwa,
Nitamwimbia Mwokozi milele :
‘‘Ulinipenda-ajabu la kweli !”
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
296. YESU ANATAKA TUNGAE
1 Yesu anataka tungae kwetu
Kama ta-a ya kuwaka kwa usiku;
Giza linazidi duniani huko;
Wewe nga-a kwako na mimi kwangu.
2 Yesu anataka tungae safi,
Tusiache kitu kupunguza nuru;
Anatutazama toka kule mbingu,
Wewe nga-a kwako na mimi kwangu.
3 Yesu anataka tungae kwaye
Watu wengi wasikie Neno lake;
Na watoke giza kuingia nuru,
Wewe nga-a kwako na mimi kwangu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
297. BWANA YESU ATAKUJA
1 Bwana Yesu atakuja kutoka mbinguni,
Atawachukua wote wanaomwamini.
Kama nyota za mbingu watu wote wa Mungu
Watanga-a kwa Yesu Mwokozi milele.
2 Atawakusanya wote wanaomupenda,
Watakuwa mali yake milele mbinguni.
3 Na watoto watakuwa pamoja na Yesu,
Watanga-a kama nyota nyumbani mwa Baba.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
298. WEKA MAKUSUDI MEMA
1 Weka makusudi mema bila kuogopa,
Usimame kwa imara kama Danieli!
Uwe muhodari kama Danieli!
Weka makusudi mema bila kuogopa!
2 Wenye woga hawawezi kuingia mbingu;
Nyosha tu bendera yake, endelea mbele.
3 Watumishi wa Shetani wanashindwa sana,
Wakikuta jeshi la askari za imani !
4 Endelea kwa kushinda, Yesu ni Mufalme!
Taji ya uzima utapata pale kwake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
299. YESU MWOKOZI NATAKA
1 Yesu Mwokozi nataka ningae kila siku,
Nimupendeze kabisa kwa kazi na michezo.
Ningae, ningae, Yesu ’nataka ningae;
Ningae, ningae, mimi ni ta-a kwa Yesu.
2 Yesu Mwokozi ’nataka nipende Mungu sana,
Na kuonyesha mapendo kwa watu wote hapa.
3 Yesu Mwokozi ’nataka nitumikie Mungu;
Hata mutoto ’naweza kumupendeza Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
300. YESU ANA PENDO KUBWA
1 Yesu ana pendo kubwa kwa watoto wa dunia,
Anapenda kuwabarikia sana;
“Usiwazuize kamwe”, alisema, “waje kwangu”,
Kwani yeye ni Mwokozi wa watoto.
Yesu ana pendo kubwa kwa watoto wa dunia,
Hata wa kabila gani, wote ni wenye damani,
Yesu ana pendo kubwa kwa watoto.
2 Yesu aliwakufia pale juu ya musalaba,
Alimwanga damu kuwaosha;
Mutu anayeamini anaokolewa naye,
Na atawachunga wote kwa mapendo.
3 Watu elfu wanakufa kila siku bila Yesu.
Wengi wa watoto hawajasikia;
Omba Mungu, vile kwenda, wasikie Neno jema
La wokovu na furaha ya mbinguni.
4 Tutangaze Neno lake hata linafika pote,
Inchi zote za dunia zisikie;
Kila lugha na kabila wafundishwe wimbo bora
Na mbinguni watasifu Mukombozi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
301. ZAMANI MWOKOZI ALIWAKARIBISHA
1 Zamani Mwokozi aliwakaribisha
Watoto wote na furaha, akawabariki;
Alikemea wanafunzi, akasema kwa mapendo:
“Acha watoto wadogo kuja kwangu.”
2 “Watoto wadogo ninawapenda sana,
Nitawachunga kama Muchungaji wa kondoo;
Na wakinipa roho zao, nitawaokoa wote,
Acha watoto wadogo kuja kwangu.”
3 Aliwapokea na pendo na furaha,
Mikono yake aliweka ju-u yao wote;
Na alitaka wafahamu anapenda kila mutu,
“Acha watoto wadogo kuja kwangu.”
4 Mwokozi aliwaonyesha pendo kubwa,
Lakini hata sasa wengi hawamutambui,
Na hawajasikia bado kwamba Yesu ni Mwokozi,
“Acha watoto wadogo kuja kwangu.”
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
302. BWANA, SASA URUHUSU
1 Bwana, sasa uruhusu watu wako kwenda kwao;
Umetufikisha hapa, umetubariki sana;
Umekusanyika nasi, kwenda nasi kwa mungini.
2 Tunakushukuru sana kwa baraka yako kubwa;
Ndani ya Kitabu chako umetufundisha roho;
Tukikwenda tukumbuke Neno tulilolipata.
3 Umepanda mbegu yako, sasa uitie maji ;
Hivi tutazaa matunda, utukuzwe ndani yetu ;
Utuchunge hata siku tutakapomwona Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
303. MUNGU AWE NANYI SIKUZOTE
1 Mungu awe nanyi sikuzote, awabarikie wote,
Awalinde kwa amani; Mungu awe nanyi sikuzote.
Mungu awe nanyi daima,
hata mwisho wa safari yenu;
Mungu awe nanyi daima,
hata tuonane kule mbingu.
2 Mungu awe nanyi sikuzote, awalishe, awatunze
Chini ya mabawa yake; Mungu awe nanyi sikuzote.
3 Mungu awe nanyi sikuzote, awe ngabo yenu kubwa
Katikati ya hatari; Mungu awe nanyi sikuzote.
4 Mungu awe nanyi sikuzote, atukutanishe tena,
Ama kwetu, ama kwake; Mungu awe nanyi sikuzote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
304. MUMUFANYIE BWANA SHANGWE
1 Mumufanyie Bwana shangwe,
Ee ninyi inchi zote pia;
Mutumikie kwa furaha,
Kuimba sifa mbele yake.
2 Mujue Bwana ndiye Mungu,
Ni yeye aliyetu-umba;
Kwa hivi sisi watu wake,
Kondo-o za malisho yake.
3 Mwingie malangoni mwake
Na katika viwanja vyake;
Mumushukuru na kusifu,
Na kubariki jina lake.
4 Kwa kuwa Bwana ndiye mwema;
Rehema yake ya milele,
Uaminifu wake vile
Ni kwa vizazi na vizazi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
305. NITASIFU MUKOMBOZI
1 Nitasifu Mukombozi na mapendo yake kwami,
Aliyenikufilia kuondosha laana kwangu.
Nitasifu Mukombozi; damu yake alimwanga
Kwa kunisamehe zambi na kulipa deni yangu.
2 Nitawahubiri wote Neno la Mwokozi wangu ;
Kwa mapendo na rehema Yesu alinikomboa.
3 Nitasifu Mukombozi kwa sababu ya uwezo;
Kweli ameshinda na mauti na Hadeze.
4 Nitaimba na kusifu pendo lake kubwa kwami;
Nimepita toka kufa, nimepata kuokoka.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
306. ASANTE, EE MUNGU
1 Asante, Ee Mungu, kwani ulitupenda
Na kutuma Mwokozi kutukufilia.
Haleluya, utukufu! Haleluya kwa Mungu!
Haleluya, utukufu kwa Mungu Mujuu!
2 Asante, Ee Mungu, kwa sababu ya Roho
Anayetuongoza kwa njia ya nuru.
3 Asante na sifa kwa Kondo-o wa Mungu,
Ndiye aliyekufa kwa ’jili ya watu.
4 Ee Mungu, ujaze kila moyo na pendo,
Roho zetu ziwake na moto wa mbingu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
307. NAPENDA KUSIKIA
1 Napenda kusikia jina la Mwokozi Yesu;
Ni tamu sana kila mara, linapita yote
Ee, ninamupenda, Ee, ninamupenda.
Ee, ninamupenda, aliyenipenda kwanza.
2 Napenda jina la Mwokozi aliyenipenda,
Aliyemwanga damu yake kwa kuniokoa.
3 Napenda jina lake Yesu anayenichunga,
Na kutimiza mahitaji yangu sikuzote.
4 Napenda jina lake Yesu anayefariji,
Anayebeba taabu yangu na kunisaidia.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
308. SIFURAHI KWA MALI YA DUNIA
1 Sifurahi kwa mali ya dunia, Ee Bwana ;
Ninataka kujua kweli mimi ni wako ;
Na katika Kitabu cha ufalme wa mbingu
Jina langu ni kule ? Ninataka kujua.
Jina langu ni kule kwa Kitabu cha Mungu ?
Jina langu ni kule ? Ninataka kujua.
2 Zambi zangu ni nyingi, zinazidi kabisa ;
Damu yako, Mwokozi, inatosha kwa mimi.
Ni ahadi ya Mungu : ‘‘Zambi zenu nyekundu zitakuwa
nyeupe hata kama theluji.’’
3 Ninajua mbinguni nyumba zetu ni nyingi,
Mungu anazochunga kwa wenye kuamini.
Ninaamini Mwokozi, zambi zimesafishwa;
Jina langu ni kule, ninajua kabisa!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
309. HATA TANGU ZAMANI
1 Hata tangu zamani (3), tuna Neno lake Yesu.
Neno lake ni kweli (3), Neno lake Bwana Yesu.
2 Alitoka mbinguni (3), kwa kutuokoa wote.
3 Yeye mutakatifu (3), ndiye Mwana wake Mungu.
4 Alikufa kwa zambi (3), hata zambi zetu zote.
5 Alitoka kaburi (3), naye alishinda kufa.
6 Alikwenda mbinguni (3), kwa kutengeneza pa’li.
7 Atarudi upesi (3), kwa kutupeleka kwake.
8 Mungu atapokea (3), wenye kumwamini Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
310. NINAKUOMBA, MUNGU BABA
1 Ninakuomba, Mungu Baba, unisikilize,
Kwa maana sina Musaidizi ila wewe pekee.
Nina-amini kweli Yesu alikufa kwami,
Na damu yake inanifungua toka zambi.
2 Mapigo megi Yesu alivumilia kwami;
Kwa ajili yangu alibeba hata musalaba.
3 Na sasa kazi yangu moja ni kumupokea;
Mwokozi alifanya yote kwa kuniokoa.
4 Ee Yesu, ninakuamini, ninakupokea;
Na ninapata kwako tu uzima wa milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
311. UTAZAME BWANA YESU
1 :Utazame Bwana Yesu, aliyechukua zambi:
:Aliteswa kabisa, akavumilia yote:
2 :Sasa kuja kwake Yesu, atakuokoa wewe:
:Alikufa kwa zambi, alimwanga damu yake:
3 :Kiri zambi zako kwake, na kufuata njia yake:
:Utapata uzima na furaha kwa milele:
4 :Ujitoe sasa kwake, kumutumikia pekee:
:Roho Mutakatifu atakupatisha nguvu:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
312. NINAKARIBIA SASA
1 Ninakaribia sasa musalaba wako, Bwana,
Mwenye zambi na zaifu, bila wewe sina kitu.
Sasa ninakuja kwako, ninaanguka mbele yako
Na unyenyekevu sana; Ee, uniokoe, Bwana.
2 Zambi zimenitawala, nimefugwa nazo sana;
Ninakusikia, Bwana, ukisema: “Kuja kwangu.”
3 Ninakutolea vyote–mali, ndugu, mwili, roho;
Ninatoa vyote kwako, ninataka kuwa wako.
4 Ninaamini damu yako kuniosha niwe safi;
Kweli unanipokea; Haleluya kwako, Yesu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
313. NINAKUSIKIA, BWANA
1 Ninakusikia, Bwana, unani-ita sasa
Kufika kwako nisafishwe kwa damu ya Mwokozi.
Ninakuja Bwana, ninakuja sasa;
Unioshe nisafishwe kwa damu ya Mwokozi.
2 Hata mimi ni muchafu, unipe nguvu yako,
Nipate kuwa safi kweli kwa damu ya Mwokozi.
3 Bwana Yesu anaita, nipate kwake vile
Imani, pendo, na salama, furaha na taraja.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
314. USIMAME NA PIGA BARAGUMU
1 Usimame na piga baragumu,
Unyanyue bendera ya Yesu;
Ujivike silaha za imani,
Kwenda kwa uwezo wake Mungu.
Kwenda mbele chini ya bendera,
Kila mutu awe muhodari;
Kwenda mbele, imba Haleluya!
Yesu Kristo ndiye Mushindaji.
2 Tusimame imara, tupigane
Kwa upanga wa Neno la Mungu;
Na zaidi ya yote tunatwaa
Ngabo ya imani kwa kushinda.
3 Mungu, sasa tunakuomba wewe,
Usaidie tushinde kabisa;
Kisha tutapumzika kwako, Baba;
Utaleta kila mutu taji.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
315. NIMEPATA SALAMA
1 Nimepata salama kutoka mbinguni,
Sasa ninapumzika kwa Yesu;
Na katika mateso na taabu ya hapa
Ninaona salama na kimya.
Nimepata salama, ni salama kutoka mbinguni;
Ni salama ya Mungu kulinda mioyo;
Ndiyo inayopita kusema.
2 Sina mali nyingine kupita salama,
Mungu aliyoleta kwa mimi;
Na salama hii mutu hawezi kutoa,
Itakuwa milele moyoni.
3 Sasa ninapumzika katika salama,
Kwa mikono ya Yesu Mwokozi;
Ninalala usiku pahali po pote,
Bila woga wa kitu cho chote.
4 Na wakati nitakapofika mbinguni,
Nitaona Mwokozi Mupenzi;
Nitapiga asante kwaye kwa salama
Iliyonituliza saa zote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
316. UKAE SIKUZOTE KWAKE YESU
1 Ukae sikuzote kwake Yesu,
Atakusaidia sana kabisa;
Utegeme-e pendo lake vile,
Naye atakuchunga.
Ukae saa zote kwake Yesu,
Kumbuka mapendo yake Mungu;
Ukimwamini atakushindisha;
Na utegeme-e Yesu.
2 Ukae sikuzote kwake Yesu,
Atakuongoza katika nuru;
Utii sauti yake kwa furaha,
Atakubarikia.
3 Ukae sikuzote kwake Yesu,
Uache mateso na taabu kwake;
Anafikili mahitaji yako,
Na atakusaidia.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
317. NINAKUOMBA, YESU
1 Ninakuomba, Yesu, ndiwe Kondoo wa Mungu,
Wewe Mwokozi,
Sasa unisikie, vile unisafishe,
Unitakase niwe wako pekee.
2 Kwa neema yako kubwa unipe mimi nguvu
Kwa kazi yako;
Ulinikufilia, hivi mapendo kwawe
Yawake ndani yangu kama moto.
3 Dunia ina giza, mateso, na huzuni,
Uniongoze;
Ee, ufukuze giza, machozi upanguse;
Usiniache kukufuata mbali.
4 Siku ya kufa kwangu, ninapokwenda ngambo,
Sitaogopa;
Mikono ya mapendo itanibeba kwako,
Niwe pamoja nawe kwa milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
318. NASIKIA, BWANA YESU
1 Nasikia, Bwana Yesu, unabarikia watu;
Ee, unikumbuke vile, unibarikie mimi;
Hata mimi, hata mimi, unibarikie mimi.
2 Bwana, usinipitie, hata nina zambi nyingi;
Ee, usiniache kamwe, uonyeshe neema kwami;
Hata mimi, hata mimi, uonyeshe neema kwami.
3 Bwana Yesu, Mukombozi, nina hamu kubwa sana
Kukutumikia pekee, sasa uni-ite mimi.
Hata mimi, hata mimi, sasa uni-ite mimi.
4 Pendo lako takatifu, damu yako ya damani,
Neema yako bila mwisho, yote unanipa mimi;
Hata mimi, hata mimi, yote unanipa mimi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
319. EE NINAKUPENDA
1 Ee ninakupenda, Mwokozi Mupenzi;
Kwawe nina-acha furaha ya zambi;
Kwa maana wewe ni wangu, nami mutu wako;
Ee, ninakupenda kupita vitu vyote.
2 Ee, unanipenda na sikukujua;
Ulininunua kwa bei ya damani ;
Kwami ulivikwa miiba kama taji yako ;
Ee, ninakupenda kupita vitu vyote.
3 Ee, nitakupenda kwa saa ya maisha,
Na nitakupenda kwa saa ya mauti;
Na saa nitakapofika kwako nitasema:
“Ee, ninakupenda kupita vitu vyote.”
4 Katika furaha na shangwe za mbingu,
Ninakutukuza kwa nyimbo za sifa;
Maneno makubwa nitakayoimba kwako;
Ee, ninakupenda kupita vitu vyote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
320. MAISHA NA MAPENDO YANGU
1 Maisha na mapendo yangu ninayatoa kwako, Bwana;
Na nitakuwa wako peke, Mwokozi, Mungu wangu.
Maisha yangu yawe yako,
uliyekufa kwami, Bwana;
Na kweli kwako nitapata furaha yangu yote.
2 Nina-amini unanipa uzima wako wa milele;
Kwa hivi nitaishi kwawe, Mwokozi, Mungu wangu.
3 Uliyekufa kwa Kalvari kuniokoa toka zambi,
Nataka kujitoa kwako, Mwokozi, Mungu wangu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
321. NINAKUTOLEA, BWANA
1 Ninakutolea, Bwana, roho na maisha yangu;
Hii mikono yangu iwe kukutumikia pekee.
: Ninatoa yote, Yesu, niwe wako kwa milee:
2 Kwa migu-u yangu vile nitakwenda kuhubiri ;
Kwa sauti nitaimba sifa kwako tu daima.
3 Kinywa changu kitangaze Neno lako waziwazi;
Mali yangu iwe yako, sitanyima kitu kwako.
4 Unijaze moyo wangu na mapendo kwawe, Bwana;
Upoke-e mwili wote, niwe wako sikuzote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
322. BWANA YESU ANAITA WATU
1 Bwana Yesu anaita watu wake duniani;
Kwa sauti ya mapendo anaita: “Unifuate.”
2 Mali bule ya dunia si faida kwa milele;
Bwana Yesu anaita, akisema: ‘‘Unipende.’’
3 Katikati ya furaha, katikati ya huzuni,
Anadumu ku-uliza: ‘‘Utazidi kunipenda ?’’
4 Bwana Yesu anaita; tunapenda kusikia
Na kumupa roho zetu kumutumikia pekee.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
323. EE, YESU ATAKUJA TENA
1 Ee, Yesu atakuja tena katika mawingu,
Na sauti kubwa Bwana atashuka toka mbingu;
Macho yetu yataona utukufu wake Mungu;
Ee, Yesu atakuja!
Tutaona utukufu siku ya kuona Yesu;
Tutaimba Haleluya kwa Yesu ndiye Bwana!
2 Ee, Yesu atakuja tena kwa kutupokea;
Tutakwenda kwa mungini wake kule kwa mbinguni;
Atakuja na baraka, kweli tunamungojea;
Ee, Yesu atakuja!
3 Kwa maana Yesu alikufa kwa kutuokoa,
Tunapaswa kwenda sasa kuhubiri watu wote,
Hata wa-amini Yesu kuwa Bwana na Mwokozi;
Ee, Yesu atakuja!
4 Ee, ndugu, wewe ni tayari kwa kuona Bwana?
Zambi zako zimesamehewa, unaamini damu?
Jina lako linaandikwa kwa Kitabu cha ufalme?
Ee, Yesu atakuja!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
324. MATESO MENGI DUNIANI
1 Mateso mengi duniani, hatuna nyumba nzuri hapa;
Lakini kule kwake Baba tutafurahi kwa milele.
Ee, Haleluya kwake Mungu,
sababu ninakwenda mbingu ;
Huzuni na machozi yangu
hayatakuwa tena ngambo.
2 Nilizaliwa bila kitu, muchafu, bule, na zaifu ;
Mutupu nilifika huku, mutupu nitarudi kule.
3 Ninasafiri duniani kufika muji wa mbinguni ;
Mwokozi alikwenda kule kutengeneza nyumba zetu.
4 Naona masumbuko mengi saa zote hapa duniani ;
Lakini kule ni furaha, nitapumzika kwake Baba.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
325. WACHUNGA WALILINDA KUNDI
1 Wachunga walilinda kundi la-o kwa usiku;
Tazama, malaika aliwatokea mbio,
Kutoka kwake Mungu.
2 Na utukufu wake Bwana ukawaangazia;
Wakaogopa sana wakiona nuru ile,
Wakashutuka kweli.
3 Na malaika yake Bwana akawa-ambia:
“Musiogope, kwani ninawaletea ninyi
Habari toka Mungu.
4 “Habari Njema ya furaha itakayokuwa
Kwa watu wote wa dunia, ninaleta kwenu
Habari Njema hii.
5 “Kwa maana mutajua leo tu amezaliwa
Katika muji wa Daudi kwa ajili yenu
Mwokozi Kristo Bwana.
6 “Na hii alama kwenu mutamwona kwa kizizi,
Amelalishwa kwa sanduku ya kulisha nyama;
Mutamukuta pale.”
(voir la suite sur la page suivante)
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
7 Kwa gaf’la makutano ya majeshi ya mbinguni
Walizunguka huyu malaika yake Bwana,
Na walisifu Mungu.
8 “Ee utukufu kwake Mungu, kule kwa mbinguni;
Salama duniani kwa wanaomupendeza;
Ee, sifa kwake Mungu.”
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
326. WACHUNGA WALILINDA KUNDI
1 Wachunga walilinda kundi la-o kwa usiku;
Tazama, malaika aliwatokea mbio.
2 Na utukufu wake Bwana ukawaangazia;
Wakaogopa sana wakiona nuru ile.
3 Na malaika yake Bwana akawa-ambia:
‘‘Musiogope, kwani ninakuja na habari.
4 ‘‘Habari Njema ya furaha itakayokuwa
Kwa watu wote wa dunia ninaleta kwenu.
5 ‘‘Amezaliwa leo tu kwa muji wa Daudi
Mwokozi ndiye Kristo Bwana, kwa ajili yenu.
6 ‘‘Na hii alama kwenu mutamwona kwa kizizi,
Amelalishwa kwa sanduku ya kulisha nyama.”
7 Kwa gaf’la makutano ya majeshi ya mbinguni
Walizunguka malaika wakisifu Mungu.
8 “Ee utukufu kwake Mungu, kule kwa mbinguni;
Salama duniani kwa wanaomupendeza.”
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
327. SIKU MATESO YATAKAPOKWISHA
1 Siku mateso yatakapokwisha,
Kule mbinguni nitakapofika,
Kuwa na Yesu Mwokozi karibu,
Hii ni furaha kupita kipimo.
Hii ni furaha, na utukufu,
Na utukufu, na utukufu,
Kuwa na Yesu Mwokozi karibu,
Hii ni furaha kupita kipimo.
2 Kwa maana nimeamini Mwokozi,
Nitamusifu daima mbinguni ;
Kumutazama kwa macho karibu,
Hii ni furaha kupita kipimo.
3 Ndugu wananingojea mbinguni,
Tutafurahi pamoja milele;
Yesu akinipokea karibu,
Hii ni furaha kupita kipimo.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
NYIMBO ZA WOKOVU
ORDRE NUMERIQUE
ORDRE ALPHABETIQUE
PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA MUNGU
1. E’ YESU MSHINDAJI WA GOLGOTHA
1 E YESU, Mshindaji wa Golgotha, twakusifu! Bendera ya
mapenzi ni alama ya kushinda. Ulichukuwa dhambi zetu
Juu ya msalaba wako. Twakuhimidi, Bwana na Mfalme!
Haleluya!
2 Twashinda na zaidi ya Kushinda kati' yote. Kwa damu yako,
Yesu, na Watuinua moyo. Katika vita na ’jaribu Twaipeleka
kwa furaha Bendera yako nzuri ya Kushinda kati’ vita.
3 Mbinguni Mkombozi ni Mkuu mwenye sifa. Aliondoa
dhambi kwa Kutufilia wote. Mwana Kondoo wake Mungu,
Umestahili kupokea Uweza, Utukufu na Heshima. Haleluya!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
2. KIJITO KIKO CHENYE DAMU
1 KIJITO kiko chenye damu Itokayo Mwokozi, Kiwaoshacho
wakosao :/: Na dhambi na uchafu. :/:
2 Msalabani mnyang’anyi Alikiona hima. Mnyonge mimi
kama yeye :/: Nitakasike pia! :/:
3 Mwokozi wetu, damu yako Daima ina nguvu Ya kuokoa
wenye dhambi :/: Wa makabila yote. :/:
4 Kijito hicho cha ajabu Ni tumaini langu. Upendo wako
nausifu, :/: Nasifu hata kufa. :/:
5 Nimeamini, naamini Uliyenifilia, Msalabani umetoa :/:
Maisha yako Yesu. :/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
3. KISIMA SAFI SANA CHATOKA MSALABA
1 KISIMA safi sana chatoka msalaba, Kimetufungukia,
chatusafisha vema. Twaweza kusikia sauti yake Yesu:
“Unifuate sasa kwa kiti cha neema!”
Kisima cha msalaba, Damu ya Yesu Kristo,
Chatusafisha sisi sote na dhambi na hatia.
2 Ufike, mwenye dhambi, kisima ni karibu! Uache dhambi
zako, upumzike hapa! Katika damu yake kabisa utapona,
Tazama msalaba, kisima kitokako!
3 Kisima hicho safi cha damu ya Mwokozi Kinatutia afya na
nguvu ya kushinda. Mfalme wetu, Yesu, tumhimidi tena!
Furaha yetu yote ni kushukuru Mungu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
4. USIKU KABLA YA KUTESWA
1 USIKU kabla ya kuteswa, Yesu Alikusanya wanafunzi wake;
Alifahamu kwamba saa yake Ya kutolewa ilikaribia.
2 Kwa roho aliona Gethsemane, Mateso yake na huzuni
nyingi; Zaidi alihofu saa ile, Ata’poachwa hata naye Mungu.
3 Alitamani saa ya Pasaka Pamoja na wapendwa wake huku.
Katika pendo lake kubwa sana Aliyashinda majaribu yote.
4 Akautwa’ mkate aka’mega, “Twaeni, mle, hu’ ni mwili
wangu!” Na akawapa wanafunzi wake. Wa heri kila mtu
’aminiye.
5 Ba’daye akawapa na kikombe, Na akasema: “Nyweni nyote
hiki! Ni damu yangu inayomwangika Kwa ondoleo la
makosa yote.’’
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
5. DHAHABU NA FEDHA HAZINIOKOI
1 DHAHABU na fedha haziniokoi, Hazina na mali haziponyi
roho, Lakini kwa damu ya Yesu Mwokozi Nimenunuliwa
nipate uhuru.
Nakombolewa pasipo mali, Kwa neema
nimeokoka! Ni bei ghali: kwa damu yake
Alilipa deni langu.
2 Dhahabu na fedha hazinilipii Madeni makubwa ninayo kwa
Mungu. Mwokozi alinikomboa kwa damu Nipate wokovu
nitoke dhambini.
3 Dhahabu na fedha haziufungui Mlango waku’karibia
Mwokozi, Lakini kwa damu nimeifikia Neema ya Mungu
aliye mkuu.
4 Dhahabu na fedha hazinifikishi Nyumbani mwa Mungu
niliyemwasia, Lakini nimekombolewa kwa damu, Kwa hiyo
nitachukuliwa mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
6. TWA’SIFU MUNGU KWA AJILI YA DAMU
1 TWA'SIFU Mungu kwa ajili Ya damu takatifu, Inayotosha
kuondoa makosa yetu yote.
2 Wakristo wanakusanyika Karibu ya kisima,
Hawapungukiwi kitu kamwe, Wakaa kwa Mwokozi.
3 Tuimbe duniani pote juu ya pendo kubwa, Kwa kuwa
tumefunguliwa kisima cha Golgotha.
4 Kisima hicho: Yesu Kristo; Na maji: damu yake.
Wasumbukao wastarehe, Waburudishwe hapa!
5 Na wenye dhambi wanaitwa Kwa wingi wa rehema, Na
wakosaji na maskini Wasaidiwa sana.
6 Tumeipata tunu kubwa, Neema kwa neema. Apokeaye fungu
lake, Ni mtu wa uheri.
7 Haleluya! Tuna’himidi Mwenyezi na Mwanawe na Roho
’takatifu pia. Haleluya! Amina.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
7. MWOKOZI AMEUTIMIZA WOKOVU
1 MWOKOZI ameutimiza wokovu Kwa neema kubwa, Na juu
ya mwamba wa Neno la Mungu Najenga imani.
Aliniokoa kabisa ! Kwa damu alinisafisha.
Ninamshukuru Mwokozi kwa sababu Alinikomboa
hakika!
2 Mzigo wa dhambi aliuondoa Kwa neema kubwa. Naona
furaha rohoni kabisa, Amani ya Mungu.
3 Naweza kukaa mweupe rohoni Kwa neema kubwa; Na Roho
ya Mungu inaniongoza Njiani daima.
4 Karibu na Yesu nalindwa salama Kwa neema kubwa. Ahadi
za Mungu zanipa furaha Iliyo kamili.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
8. YESU KRISTO ASIFIWE
1 YESU Kristo asifiwe! Alizichukua dhambi, Ne’ma inatoka
kwake kati’ damu. Umeosha moyo wako, Umekuwa safi,
huru, Umeondolewa dhambi kati’ damu?
:/: Kati’ damu:/: Umeosha moyo wako, umekuwa
safi, huru? :/: Kati’ damu:/: Umeondolewa dhambi
kati’ damu?
2 Ukilia, ukijuta, Dhambi hazitoki kamwe; Haki kweli
uta’pata kati damu. Mambo yakusumbuayo Yesu a’ondoa
mara, Unapata ukombozi kati’ damu.
3 Yesu atatuchukua Arusini mwake huko. Umevikwa nguo
safi kati’ damu? Je, wajenga ju’ ya mwamba, Moyo wako u
mzima, Unashinda kila saa kati’ damu?
4 Bwana Yesu asifiwe! Alitoa damu yake, Na kwa damu ya
thamani tutashinda. Asubuhi kubwa ile Vita itakapokwisha,
Tutaimba kwa furaha ju’ ya damu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
9. NAIAMINI DAMU YAKO
1 NAIAMINI damu yako Na msalaba wako, Yesu. Mwokozi
wangu wa pekee, Napata yote kwako.
Uliyoyaahidi Na’pata kwa imani. Huwezi kuniacha
mimi; Napata yote kwako.
2 Kwa damu nimetakasika, Na mto wa uzima wako Waniletea
nguvu tele, Napata yote kwako.
3 Nafungwa kwa upendo wako, Njiani unaniongoza, Na katika
hatari zote Napata nguvu kwako.
4 Ninakupenda, Bwana Yesu, Wanisikia niombapo, Wanipa
jibu la maombi, Napata yote kwako.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
10. DAMU YAKO YENYE BARAKA
1 DAMU yako yenye baraka Inayotuosha makosa, Ilitoka
msalabani, Bwana Yesu, ulipokufa. Nastahili ’pata hukumu,
Na siwezi mimi kujiosha. Unioshe katika damu, Nipate kuwa
safi kabisa!
Safi, safi kweli, Safi, safi kweli! Unioshe katika
damu, Nipate kuwa safi kabisa!
2 Yesu, ulivikwa miiba, Kuangikwa juu ya mti. Ulivumilia
mateso, maumivu na majeraha. Ninataka kijito hicho,
N’ende na nikasafishwe sana! Unioshe katika damu, nipate
kuwa safi kabisa!
3 Baba, kweli nina makosa, Moyo wangu wa udhaifu ; Mimi
mwenye dhambi rohoni Nitaona wapi Mwokozi ? Yesu,
kwako msalabani Naja, ninakuamini sasa. Unioshe katika
damu, Nipate kuwa safi kabisa!
4 Bwana, nimefika karibu, Unilinde kwako milele! Ufungue
kila kikamba, Unijaze moyo mwenyewe! Na karibu ya
msalaba Nitakaa hata kufa kwangu. Unioshe katika damu,
Nipate kuwa safi kabisa!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
11. IKIWA WANANIULIZA MSINGI WA UZIMA
1 IKIWA wananiuliza Msingi wa uzima, Je, twahitaji
kuongeza Kwa kazi yake Yesu? Kwa uhodari nitajibu:
“Msingi wangu ni wa nguvu, Ni damu yake Yesu Kristo,
Inanitosha sana.”
2 U mwamba wa zamani sana, Daima utadumu. Na hata siku
nita’kufa, nitautegemea. Nitakapoondoka huku, Nitaimbia
majeraha, Na damu ya Mwokozi wangu, Funguo la
mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
12. KWA BADALA YANGU KWELI
1 KWA badala yangu kweli Yesu alitoa damu. Mimi huru na
ni heri, Bwana Yesu asifiwe!
Yesu alinikomboa, lakini Si kwa dhahabu na mali
ya dunia; Bali damu ya Mwokozi ni malipo Kwa
ajili yangu, Haleluya!
2 Tu’inue msalaba, Hata wote wataona Mwana wake Mungu,
hapo Alitoa damu yake!
3 Dia kubwa, Yesu Kristo! Wingi sana wa upendo: Yesu
aliacha mbingu, Alitufilia sote.
4 Sitaweza kufahamu Bei ya wokovu wangu, Bali ninajua
sana: Yesu alinikomboa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
13. NANI AWEZA KUNIWEKA HURU?
1 NANI aweza kuniweka huru? Ni Yesu Mwokozi, Yesu
Mwokozi! Nguvu ’kushinda nipate kwa nani? Kwa damu ya
Yesu Mwokozi!
Kuna nguvu, nguvu ya ajabu kuu, Kati’ damu ya
Mwokozi! Kuna nguvu, nguvu ya ajabu kuu, Kati’
damu yake Yesu!
2 Nitawezaje kuvunja tamaa? Kwa damu ya Yesu, damu ya
Yesu! Nikaribie kisima cha ’hai, Kisima cha damu ya Yesu!
3 Nitawezaje kuoshwa moyoni? Kwa damu ya Yesu, damu ya
Yesu! Nitakasike katika kisima, Kisima cha damu ya Yesu!
4 Nitawezaje kutenda vizuri? Kwa nguvu ya Yesu, nguvu ya
Yesu! Nitawezaje kufika mbinguni? Kwa nguvu ya damu ya
Yesu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
14. MWOKOZI WANGU ULIKWENDA JUU
1 MWOKOZI wangu ulikwenda juu Kukaa kuumeni kwake
Baba; Utakusanya sisi sote huko, Mbinguni kwako
utatufikishsa. :/: Makao mema wa’tuandalia, Unatungoja
kwake Mungu Baba. :/:
2 Mwombezi wetu Wewe, Yesu Kristo, Kwa ’jili yetu mbele
yake Baba. Wachunga sana sisi, kundi lako, Na watusaidia
’jaribuni. :/: Na sikuzote unatuombea, Watushindia vita kali
huku. :/:
3 Mikono yako uliwanyoshea Walio wako, siku uli’kwenda; Na
hivyo siku utakaporudi Utabariki wakuaminio. :/:
Ulivyokwenda, utakavyorudi; Niombe, nikakeshe kwa imani!
:/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
15. MUNGU, MOTO WAKO UNIUTUMIE
1 MUNGU, moto wako uniutumie, Ninangoja nguvu yako!
Nipe na uzima na upendo wako, Unijaze, E’ Mwokozi
wangu!
2 Teketeza yote usiyoyapenda, Nisafishe kati’ damu! Na kiburi
yangu uivunje tena, Unioshe, Yesu, niwe safi!
3 Unilinde, Yesu, sikuasi tena, Unifunge kwa upendo! Mimi ni
dhaifu, unitunze kwako, ’niongoze kwa mkono wako!
4 Huko juu kwako tutaona raha, Na huzuni itakwisha.
Nyimbo za shukrani zitajaza mbingu: Utukuzwe, Yesu,
Mkombozi!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
16. YO YOTE UONAYO HUKU
1 YO yote uonayo huku Katika mwendo wako, Yafaa
ku’mwambia Yesu, Atakusaidia.
Kwa kuwa kila aombaye Mwokozi neema yake,
ataokoka na hatia, na atasifu Yesu.
2 Ukichukiwa na wenzako Na ukijaribiwa, Mwokozi Yu karibu
sana, Maombi asikia.
3 Ukiwa mwana mpotevu, Na mbali na Babako, Amani
una’kosa sasa, Urudi kwake Yesu!
4 Ukiwa na makosa mengi, Na roho yako ngumu, Neema yake
yakutosha, Utubu dhambi zako!
5 Ikiwa nguvu mara nyingi Kuomba kwa bidii, Uombe Baba,
kama mwana, Akusikia kweli!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
17. UKAE NAMI, GIZA INAFIKA!
1 UKAE nami, giza inafika! Usiniache, Mungu nakuomba!
Unayejua udhaifu wangu, Nategemea Wewe, ’kae nami!
2 Maisha yangu ni mafupi sana, Uzuri wa dunia utakwisha.
Kuna machozi, kufa huku chini, Wewe Mwokozi wangu,
’kae nami!
3 Nakuitaji Wewe sikuzote, Unayeweza sana kunilinda. Wewe
shujaa wa kushinda wote, Katika hali zote ’kae nami!
4 Unionyeshe msalaba wako, Nione nuru yako kati’ giza! Na
nikiishi au nitakufa, Wewe, Mwokozi wangu, ’kae nami!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
18. MUNGU WETU YU KARIBU
1 MUNGU wetu Yu karibu Kututia nguvu yake. Mbingu ina
maghubari, Tuletee mvua sasa!
Tusikie, Mungu wetu, Tubariki saa hii! Tunangoja,
tunangoja, Tuonyeshe nguvu yako!
2 Mungu wetu Yu karibu, Hapa ni Patakatifu, Sisi sote
tunangoja Kujalizwa naye Mungu.
3 Mungu wetu Yu karibu, Kwa imani tunaomba: “Tuwashie
moto safi Ndani ya mioyo yetu!”
4 Mungu, ufungue mbingu, Twalilia nguvu yako! Tubariki saa
hii Kwa rehema yako kuu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
19. MUNGU, TUNANGOJA WOTE
1 MUNGU, tunangoja wote Roho yako ’takatifu, Tunaomba
kwa imani: “Umtume hapa kwetu!”
Mungu wetu, Mungu wetu, Umimine Roho yako!
Mioyoni mwetu, Bwana, Utimize kazi yako!
2 Washa moto wako tena Ndani ya mioyo yetu, Hata vyote vya
majani Vitateketea sana!
3 Utakase roho zetu, Na kiburi uivunje! Wewe U Mfalme wetu,
Utawale watu wako!
4 Utujaze sikuzote Pendo lako kubwa, Mungu! Sisi tuwe
nyumba yake Roho ya utakatifu!
5 Na karama zake Roho Utuzigawie, Bwana! Na wagonjwa
uwaponye, Wote wakuone, Mungu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
20. BWANA YESU, UNIONGOZE
1 BWANA Yesu, uniongoze Baharini huku chini, Juu ya
mawimbi mengi, Katika dhoruba kali! Bwana Yesu,
uniongoze, Nakutegemea Wewe!
2 Bwana Yesu, uniongoze, Utulize moyo wangu! Neno moja
toka kwako, Mara shwari baharini. Bwana Yesu, uniongoze,
Nipe utulivu wako!
3 Bwana Yesu, uniongoze, Niyashinde majaribu! Mengi ya
kunidanganya, Mengi ya kufunga macho! Bwana Yesu,
uniongoze, Niwe mshindaji kweli!
4 Bwana Yesu, uniongoze, Siku nita’vuka ng’ambo! Nikiona
woga, giza, Nipe nuru na amani! Bwana Yesu, uniongoze,
Uwe nami hata mwisho!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
21. JUU YA MBINGU ZOTE
1 JUU ya mbingu zote, Nyota na jua pia, Hapo yafika kweli
Maombi ya mwenye dua. Roho ya mwanadamu Yamfikia
Mungu, Huko yabisha lango Na kumtafuta Baba.
2 Roho haitaona Raha, amani huku; Kuna bandari njema
Mbinguni kwa Mungu Baba. Moyo utatulia, Nuru itatokea
Tukifuata njia ya sala na maabudu.
3 Hata motto ’dogo Mwenye kuomba Mungu, Hana la
kuogopa; Kuomba kwafaa sana. Tusisahau tena, Pote
twendapo huku Kwamba maombi yetu Yafika kwa Mungu
Baba.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
22. YESU KRISTO, BWANA WANGU
1 YESU Kristo, Bwana wangu, Una amri na uwezo Za
kuziondoa dhambi, Na ’takasa roho yangu.
’nitolee masamaha, ’niokoe na jaribu, Unilinde
hata mwisho, Unitwae kwako juu!
2 Mbele nilikuwa mwovu, Nilikukataa, Yesu, Kwa hakika
sikujua Wewe na upendo wako.
3 Bwana Yesu, usamehe Dhambi nilizozifanya! ’siitike
majaribu, Nguvu yako inilinde!
4 Tangu sasa Wewe, Yesu, U Mwokozi na Rafiki, Nimetengwa
na Shetani, Niwe wako sikuzote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
23. NIKITAZAMA KWA IMANI
1 Nikitazama kwa imani Mwokozi wangu, Yesu, Nawaka kwa
upendo wake, Na ninavutwa kwake; Naona majeraha yake,
Mikono na ubavu wake, Na humo najificha sana, Moyoni
mwa upendo.
2 Imanueli upendwaye, Nilinde sikuzote, Mpaka nihamie
kwako Mbinguni mwa uheri! Milele na milele huko Hapana
la kunizuia Nisimsifu Bwana Yesu Kwa damu na ’jeraha.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
24. E’ MUNGU MWENYE KWELI
1 E' MUNGU mwenye kweli, nakuamini sana, Maneno yako
yote milele yatadumu. “Niite kati’ shida, nitakusaidia.”
Nategemea, Bwana, ahadi yako hiyo.
2 Na katika uchungu ni heri kuamini, Naweka roho yangu
kulindwa nawe, Baba, uliyenifundisha kuita jina lako;
Naona tumaini na tegemeo kwako!
3 Ninavyoomba kweli, najua wasikia. Yaliyo mema kwangu,
najua wayafanya. Katika shida kali waweza kunilinda;
Wanichukua mimi na masumbuko yangu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
25. MVUA YA MBINGU UNYESHE
1 MVUA ya mbingu unyeshe, Kama ulivyoahidi! Juu ya dunia
yote Inye kutubarikia!
Mvua ya mbingu, Mvua ya mbingu utume!
Utunyeshee neema, Tunakuomba, E’ Mungu!
2 Mvua ya mbingu unyeshe, Ituamshe na sisi! Ju’ ya vilima na
bonde Mvua ya mbingu ifike!
3 Mvua ya mbingu unyeshe Katika dunia yote! Watu wa
Mungu wapone, Mbegu za roho ziote!
4 Mvua ya mbingu unyeshe, Tunapokuelekea! Utujalie baraka
Tunakuomba, E’ Mungu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
26. NAKUHITAJI, YESU
1 NAKUHITAJI, Yesu, Mwokozi wangu mwema, Sauti yako
nzuri Iniletee raha!
Nakuhitaji, Yesu, Usiku na mchana! Katika sala
yangu Unibariki sasa!
2 Nakuhitaji, Yesu, Unionyeshe njia! Na unitimizie Ahadi za
neema!
3 Nakuhitaji, Yesu, Uwe karibu nami, Nipate kulishinda
Jaribu la Shetani!
4 Nakuhitaji, Yesu, Katika mambo yote, Kwa kuwa bila Wewe
Maisha hayafai.
5 Nakuhitaji, Yesu, Njiani huku chini, Nipate kuwa kwako
Milele na milele!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
27. UNA UHODARI LEO WA KUMFUATA YESU
1 UNA uhodari leo Wa kumfuata Yesu, Hata ukichekwa sana
Na kuteswa duniani?
2 Una uhodari leo Kuwa mtu wake Mungu? Ukiona haya
sana, Kisha utaona nini?
3 Mji unaonekana Ukijengwa mlimani, Hivyo na imani yetu
Inadhihirika sana.
4 Ukipenda Yesu sana Na kuliko vitu vyote, Unataka kumkiri,
Mbele ya wenzako huku.
5 Chuki au ’pendeleo Kwako kitu bure tena, Watafuta siku
zote Sifa zake Yesu Kristo.
6 Ujihoji nafsi yako Ukitaka kuokoka! Uliyekataa Mungu,
Tubu dhambi zako leo!
7 Umsihi masamaha, Akuoshe kati’ damu! Omba uhodari tena
Wa kumfuata Yesu!
8 Uchague Yesu leo, Uwe mfuasi wake! Ukitwaa msalaba
Utaipokea taji!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
28. NINATAKA KUFUATA YESU
1 NINATAKA kufuata Wewe, Yesu, sikuzote, ’kiwa katika
furaha Au shida na udhia. Unaponitangulia Ninakuja nyuma
mbio. Ninajua ni karibu Kuwasili huko kwako.
2 Haifai niulize: Bwana, unakwenda wapi? Au kwa kusitasita
Kuishika njia yako. Kweli, hapa kazi moja: Kufuata Wewe
mbio, Kwenda njia ile moja Wewe unionyeshayo.
3 Walakini kama kitu Kinataka kunifunga, Au kuwa mgogoro
Katika safari yangu, ’kate kamba mara moja Ifungayo roho
yangu! Ninataka kuwa huru Kukutumikia vema.
4 Bwana Yesu, unilinde, Uhifadhi nia yangu! Nikichoka kwa
safari, Nong’oneza kwa upendo: ‘‘Mwana, u mtoto wangu,
Uniandamie punde, Utapumzika sana Tena kwangu huko
juu.’’
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
29. UNIVUTE, YESU, NIFUATE NYAYO ZAKO
1 UNIVUTE, Yesu, nifuate nyayo zako, ’kiwa kwa rafiki au
katika wageni, Na mahali pa furaha au sikitiko; Sina budi
kumkaribia Yesu.
Nimfuate, nimkaribie, Siku zote na po pote
nimwandame Yesu! Nimfuate, nimkaribie, Yesu
mbele, mimi nyuma, hata mwisho!
2 Juu ya milima nitasikilia Yesu, Hata mabondeni
nitaandamana naye. Jua, giza, afya, ’gonjwa, utulivu, vita,
Kati’ hayo yote Yesu Yu karibu.
3 Nikiteka maji, au nikilima shamba, Nikika’ nyumbani au
’kiwa safarini, Hata huko soko neno moja ni halisi: Sina
budi kumkaribia Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
30. TARUMBETA LAKE KRISTO LITALIA
1 TARUMBETA lake Kristo linalia pande zote, Na wakristo
wote wanajipangia ’piga vita Ju’ ya mahodari wa Shetani.
Kweli tutashinda, Kwani Yesu Yupo mbele.
Twende, Yesu a’tuita, Twende na wakristo wote!
Twende, tujivumilishe, Yesu Yupo mbele yetu!
2 Neno la Akida wetu lipo: ‘‘Mniandamie!’’ Naye anatangulia,
tunakuja wote mbio. Kwa silaha zake Mungu kila mtu
atashinda, Kwani Yesu Yupo mbele.
3 Na tukiwa mbali ya Akida wetu tutashindwa, Tutafungwa na
adui na pengine kupotea. Walakini kule mbele watu wote
watashinda, Kwani Yesu yupo mbele.
4 Tarumbeta litalia tena, vita itakwisha, Na askari wote
watapata raha na matunzo. Watapumzika na milele
watashangilia, Kwani Yesu yupo mbele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
31. KATIKA SAFARI YETU
1 KATIKA safari yetu Kwenda huko juu Tusilale usingizi,
Tuwe na bidii!
Kaza mwendo, tusifungwe, Twende mbio tu! Yesu
Kristo ni Mwokozi Na Mfalme ’kuu!
2 Bwana Yesu anatupa Maji ya uzima, Maji hai ya milele Ya
kuburudisha.
3 Njia na miiba mingi Inatuumiza, Hofu na hatari nyingi
Zinafadhaisha.
4 Mungu wetu atungoja Huko kwake juu, Yesu ni Mwokozi
wetu, Tufuate Yeye!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
32. HAPO NILIKUWA CHINI
1 HAPO nilikuwa chini Katika dhambi nyingi, Roho yangu
iliona Kufa na giza tele. Mungu alikisikia Kilio changu
huko, Naye akanipandisha, Kuniponya.
:/: Nimeokoka, nimeokoka! Yesu Mwokozi wangu
Aliniokoa:/:
2 Sasa Yesu amekuwa Makimbilio yangu, Na upendo wake
’kubwa Uko moyoni mwangu. Ne’ma yake kubwa sana
Inajaliza roho, Niwe mwaminifu kwake Siku zote!
3 Ewe, mwenye sikitiko, Kuna matumaini: Yesu
anakufahamu, Atakusaidia. Atakupandisha toka Tope la
kuteleza, Upokee ne’ma yake Kwa wokovu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
33. HURU KAMA NDEGE BUSTANINI
1 HURU kama ndege bustanini, Sasa nafurahi kwa sababu
Yesu ni Rafiki yangu ’kubwa; Nina amani siku zote.
2 Aliniokoa na mashaka, Alinipa tunu ya rehema. Mimi ni
mtoto wa Babangu, Na nuru inang’aa sana.
3 Ninataka ku’shukuru Bwana, Alitupa dhambi zangu mbali,
Na sitaziona tena kamwe, Hazitanitawala tena.
4 Jua likifichwa kwa mawingu, Kiti cha rehema ni karibu,
Hapo ndipo shida ziishapo, Na roho yangu yatulia.
5 Radhi kama mwana kwa babake, Kwa salama kama
bandarini Ninapumzika kwa Mwokozi, Mbali na shida na
huzuni.
6 Yesu Yu karibu sikuzote, Achukua mimi na mzigo. Napokea
kwa mkono wake Neema na mateso pia.
7 Nilimpa Yesu moyo wangu, Ninapenda kumtumikia; Neno
lake linapendwa nami, Na nira yake ni laini.
8 Nafurahi sana kanisani Kati ya watoto wa Babangu, Roho
ya neema ni karibu, Kunanifurahisha sana.
(voir la suite sur la page suivante) NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
9 Mimi ni mdogo duniani, Tena msafiri na mgeni. Kwetu ni
mbinguni huko juu; Babangu ananiongoza.
10 Saa za mashaka zitakwisha, Kuja kwake Yesu ni karibu.
Nitaona raha kubwa sana Katika nyumba ya babangu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
34. KWA PENDO LAKE KUBWA
1 KWA pendo lake kubwa Alitafuta mimi, Na alinichukua
Begani mazizini. Na nyimbo zao malaika Zikajaliza mbingu
pia.
Alinitafuta, akaniokoa, Akaniondoa matopeni,
Akanichukua mazizini.
2 Mchunga mwema Yesu Aliniponya roho, Na akaniambia:
‘‘Mtoto upendwaye.’’ Sauti yake ya upendo ikanifarijia
moyo.
3 Ninakumbuka jinsi Alivyotoka damu, Na taji ya miiba,
Mateso na mauti. Na penye msalaba wake Ninashukuru
Bwana Yesu.
4 Namfuata Yeye Katika nuru yake, Waridi za ahadi Zapamba
njia yangu. Milele nitaendelea Kusifu Yesu kwa furaha.
5 Na saa zinapita, Nangoja asubuhi Utakaponiita, niende
kwako juu. Nitasimama kwa amani Mbinguni mbele yako,
Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
35. NIMEFIKA KWAKE YESU
1 NIMEFIKA kwake Yesu, Na rohoni mwangu sasa Jua lake
la neema Linang’aa kila siku.
Roho yangu inaimba, Nimefunguliwa kweli.
Nimekaribia Yesu, Ninaimba kwa furaha.
2 Pepo za neema yake Zinavuma ndani yangu, Na mawimbi ya
wokovu Yananijaliza sasa.
3 Sasa Bwana Yesu Kristo Amefanya kao kwangu. Nimepewa
Mfariji, Roho ya ahadi yake.
4 “Siku Roho afikapo Mtajua kwa hakika Kwamba ninakaa
kwenu”, Hivyo Yesu alisema.
5 Kweli, amefika kwetu, Sasa yumo ndani yetu. Ujitoe kwake
Mungu, Aioshe roho yako!
6 Yesu atakapokuja Katita utakatifu, Nitafananishwa naye,
Nitamshukuru sana.
Zitakuwa nyimbo nyingi Tuta’poingia mbingu, Na
milele tutaimba Na kusifu Mungu wetu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
36. YESU AMENIOKOA
1 YESU ameniokoa, Amenipa utulivu. Kwake ninaona raha,
Ninataka kumsifu.
Haleluya, Haleluya! Nimefika bandarini.
Haleluya, Haleluya! Jina lake ni mnara.
2 Kwa furaha ninaimba Wimbo mpya wa wokovu. Nisichoke
kamwe hapa Kumwimbia Mkombozi!
3 Ni habari za neema Za kupasha pande zote. Mhubiri, enda
mbio Kufikia nchi zote!
4 Yesu, siku nita’kufa Na maisha ni tayari, ’nichukue kwako
juu Penye raha ya milele!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
37. BWANA YESU ALINIOKOA KWELI
1 Bwana Yesu aliniokoa kweli, Ninataka kufuata Yeye sasa.
Kila siku nimtumikie vema, Yeye anipaye yote kwa neema!
Nafuata njia nzuri Ya Mfalme Yesu Kristo, Na
katika njia hiyo Mwendo ni pamoja naye.
2 Sitaifuata njia mbaya tena, Nimewekwa huru kweli naye
Yesu. Kumtumikia ni furaha yangu, Ananishibisha kwa
fadhili zake.
3 Huko mbele ninaona mji mwema, Nimeacha njia ndefu
nyuma yangu. Nuru ya Babangu yaniangazia, Nitembee kwa
salama siku zote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
38. NILIKWENDA MBALI SANA
1 NILIKWENDA mbali sana, ’kufuata njia mbaya,
Nikamsahau Yesu Anayenipenda sana.
Nina raha na furaha, Yesu alinitafuta, Akaniokoa
kweli, Mimi wake siku zote.
2 Na sikufikiri siku Nitakapodhihirishwa Mbele ya Mwenyezi
Mungu, Na kuhukumiwa naye.
3 Dhambi zilinichokeza, Nikageukia Mungu, Akasema neno
zuri La amani na faraja.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
39. YESU AMEINGIA KATIKA ROHO YANGU
1 YESU ameingia katika roho yangu, Amenifungulia kamba
za dhambi zangu. Tena amenijaza Roho Mtakatifu.
Ninamsifu sasa kwa wimbo mpya.
Yesu ni yote kwangu, Yote na’pata kwake.
Ameondoa dhambi, Ametakasa mimi. Shangwe
rohoni mwangu Ni kama maji mengi, Namshukuru
sana Mwokozi wangu.
2 Siku si ndefu tena, kazi si ngumu sasa, Njia yanipendeza,
’kiwa nyembamba sana. Katika hali zote ninamwimbia
Yesu, Yeye Mfalme wangu, ninamsifu!
3 Katika mwendo wangu ninazidishwa shangwe, Hata
wakinicheka, mwovu akijaribu. Hima Mwokozi wangu
atanyakua mimi Toka machoni pao. Haleluya!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
40. AMENIWEKA HURU KWELI
1 AMENIWEKA huru kweli, Naimba sasa: Haleluya! Kwa
msalaba nimepata Kutoka katika utumwa.
Nimeokoka, nafurahi! Na dhambi zangu zimetoka.
Nataka kumtumikia Mwokozi wangu siku zote.
2 Zamani nilifungwa sana Kwa minyororo ya Shetani,
Nikamwendea Bwana Yesu, Akaniweka huru kweli.
3 Neema kubwa! Nilipata Kuacha njia ya mauti, Na nguvu ya
wokovu huo Yanichukua siku zote.
4 Na siku moja nitafika Mbinguni kwake Mungu wangu.
Milele nitamhimidi Na kumwimbia kwa shukrani.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
41. SIKU NYINGI NILIFANYA DHAMBI
1 SIKU nyingi nilifanya dhambi, Sikujua Neno la Mwokozi,
Sikujua maumivu yake Kwa ’jili yangu.
Bwana Yesu alinirehemu, Dhambi zangu
alizichukua. Namsifu Yesu kwa ajili ya msalaba.
2 Niliposikia Neno lake, Moyo wangu ukalia sana. Nikaona
maumivu yake Kwa ’jili yangu.
3 Bwana Yesu ni Mwokozi wangu, Jua na Mfalme na Uzima.
Ninamhibidi kwa ajili ya msalaba.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
42. BWANA YESU AMEVUNJA
1 BWANA Yesu amevunja Minyororo ya maovu, Nimewekwa
huru kweli Mbali na makosa yangu.
Haleluya, Haleluya! Yesu Kristo ni Mwokozi!
Haleluya, Haleluya! Yesu alinikomboa.
2 Nilipoungama dhambi, Nikawekwa huru kweli. Moyo wangu
unawaka Kwa upendo ’takatifu.
3 Kamba zilizonifunga Zimetoka, nafurahi. Dhambi zilizo
’sumbua Zimetupwa mbali sana.
4 Ninataka kuhubiri: “Nimewekwa huru kweli!” Nipeleke kwa
furaha Neno zuri la Mwokozi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
43. JUU YA MWAMBA UMEJENGA KANISA LAKO
1 JUU ya mwamba umejenga Kanisa lako duniani, Umeliweka
huru kweli Katika damu yako, Yesu.
Juu ya mwamba, juu ya mwamba Huru na safi
umelijenga. Juu ya mwamba, juu ya mwamba,
Huru na safi tusimame!
2 Neema kubwa! Nimepata Sehemu yangu kanisani. Vita ya
roho imekwisha, Umenijaza utulivu.
3 Kati’ hekalu lake Mungu Nimefanyika jiwe hai. Ninashiriki
mwili wake Kama kiungo chake Kristo.
4 Ju’ ya msingi huo safi Liwe kanisa lako zima! Vyote
vikiondoka huku, Litasimama, litashinda.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
44. TU WATU HURU, HURU KWELI
1 TU watu huru, huru kweli Katika Yesu Kristo. Tunahubiri
Neno lake Kwa moto ’takatifu. Tuendelee mbele, mbele,
Tukashinde majaribu! Twapiga vita ya imani, Tuvumilie
yote!
2 Tu jeshi kubwa la askari, Tu safi kati’ damu. Mfalme wetu,
Yesu Kristo, Ni Kiongozi wetu. Kwa nguvu yake kubwa mno
Tutadumu hata kufa.Tuendelee mbele, mbele, Tumshukuru
Mungu.
3 Kwa Yesu tuna uhodari Na mamlaka kubwa, Maana
tunayaamini Maneno yake yote. Kisima wazi, cha ajabu,
Kinatoka msalaba, Tuliyakunywa maji yake, Ni maji ya
uzima.
4 Mbinguni, nchi ya asili, Ya haki na amani, Tuta’pofika huko
juu Tutamwimbia Yesu. Na kila chozi litafutwa Na mkono
wa Mwokozi. Kwa shangwe kubwa tutarithi Ufalme wa
ahadi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
45. WAISRAELI WALIKA’BABELI UTUMWANI
1 WAISRAELI walika’ Babeli utumwani, Wakawa na huzuni
tu Kwa ’jili ya Sayuni.
Hapo amri ilifika Waliweza kuondoka, Shangwe
gani mioyoni mwao! Walitwa’ vinubi vyote,
Kwa kuimba wakaenda Hata rithi na nchi yao.
2 Wakati wa utumwa hu’ Vinubi ha’kupigwa, Na walikaa
kimya tu Mahali pa ugeni.
3 Walipotoka Babeli, Ikawa kama ndoto; Furaha nyingi
rohoni, Faraja na uheri.
4 “E’ Mungu amefanyaje?” Wa’nena mataifa, ‘‘Utumwa
wanatoka na Wawekwa huru tena!”
5 Katika ulimwengu hu’ Ni wengi wafungwao. Uhuru ni kwa
Yesu tu Kwa kila ’aminiye.
Ndiye ameleta amri: Tunaweza kuokoka, Shangwe
ku’kwa kila ’aminiye! Njoo sasa, twa’ kinubi,
Tufuate kwa kuimba Hata rithi nchi yetu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
46. HAIFAI KUYASUMBUKIYA
1 HAIFAI kuyasumbukia Mambo yatakayokuwa kesho. Baba
yangu anajua yote, Ni vizuri nikumbuke hivyo. Yeye
mwenye moyo wa upendo Ananipa yafaayo kweli, Kama
sikitiko au shangwe, Na amani yake kila siku.
2 Sikuzote Yu karibu nami, Na neema anapima sawa.
Achukua masumbuko yote, Yeye aitwaye Mungu Baba.
Kunitunza hivyo kila siku, Mambo hayo ame’tadariki.
“Kama siku, kadhalika nguvu!” Ni ahadi niliyoipewa.
3 Mungu, unisaidie tena ’kaa kimya kwako siku zote! Niamini
sana Neno lako, ’sipoteze bure nguvu yako! Na katika
mambo yote huku Nipokee kwa mikono yako Nguvu na
neema ya kutosha, Hata nitakapofika kwako!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
47. NIKIONA UDHAIFU NA IMANI HABA
1 NIKIONA udhaifu na imani haba, Nikijaribiwa sana, Yesu
anilinda.
Anilinda vema, Anilinda vema, Kwani Yesu
anipenda, Anilinda vema.
2 Peke yangu sitaweza kuambata Yeye, Pendo langu ni dhaifu;
Yesu anilinda.
3 Mimi mali yake sasa, alinikomboa, Alitoa damu yake; Yesu
anilinda.
4 Haniachi kupotea, anilinda sana. Kila ’mwaminiye kweli,
Yesu amlinda.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
48. SIWEZI MIMI KUFAHAMU SANA
1 SIWEZI mimi kufahamu sana Neema yake Mungu kwangu,
Zamani nilikuwa mkosaji, Lakini alinisamehe.
Bali namjua Mungu, Anayeweza kunilindia Urithi
wangu juu Hata siku yake Yesu.
2 Siwezi mimi kufahamu sana Upendo wake ’kubwa mno;
Nimeamini Neno lake kweli, Na ninaona raha tele.
3 Siwezi kufahamu kazi kubwa Ya Roho yake ndani yetu,
Anayeweza kufundisha mtu Kutegemea Yesu Kristo.
4 Sijui mimi siku zangu tena Za kutembea duniani. Na labda
nitaona shida huku, Taabu na huzuni nyingi.
5 Sijui mimi kama siku moja Nitakuona kufa huku, Au kwa
hima nitabadilika, Ajapo Bwana na mawingu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
49. NJIA YOTE NAONGOZWA
1 NJIA yote naongozwa Kwa mkono wa Mwokozi, Nionapo
wema wake, Sina shaka, hofu tena. Nina raha ya mbinguni,
Ninakaa kwa salama. :/: Na katika mambo yote Ananitendea
mema. :/:
2 Njia yote naongozwa, Namtegemea Yesu. Anilinda jaribuni,
Anitia nguvu pia. Nikiona kiu hapa, Nikichoka safarini, :/:
Mwamba uliopasuka Unabubujika maji. :/:
3 Njia yote naongozwa Kwa upendo wake bora, Atanituliza
tena Kwa babake huko juu. Miguuni pake Yesu Ninataka
kusujudu, :/: Nakusifu Yeye, kwani Aliniongoza huku. :/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
50. SITASUMBUKA
1 SITASUMBUKA kwa kuwa Mungu Ananitunza daima,
Anachukua mizigo yangu Nyakati zote za mwendo.
Sijaiona nyingine siku, Na jana imetoweka, Na leo
Mungu anazijua Hitaji zote ninazo.
2 Sitasumbuka kwa kuwa Mungu Ni Baba yangu kabisa.
Hawezi kunisahau mimi Ingawa akijificha.
3 Sitasumbuka kwa kuwa Mungu Anishibisha neema, Anipa
yote yanifaayo Kwa roho yangu na mwili.
4 Maua yote anayavika, Na ndege wote wa anga Wanapokea
chakula chao Pasipo shamba na ghala.
5 Ninafurahi katika Bwana, Na kama ndege naimba. Najua
kwamba nyakati zote Babangu ananitunza.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
51. NAONA AMANI GOLGOTHA
1 NAONA amani Golgotha Alipojitoa Mwokozi, :/:Na huko
nina kimbilio Kwa Yesu aliyenipenda.:/:
2 Sitaki ’tamani fahari Na dhambi katika dunia, :/: Sababu
wokovu ninao Katika ’jeraha ya Yesu. :/:
3 Aliziondoa kabisa Mizigo na kamba ya dhambi. :/: Na
niliokoka halisi Kwa Neno la Mungu wa ’hai. :/:
4 Maneno ya Mungu ni kwetu Chakula na dawa ya roho, :/: Na
nguvu ya kusaidia Mkristo katika safari. :/:
5 Ni sasa hekalu la Roho, Anayemiliki moyoni; :/: Na Yesu
ananiongoza Kwa njia ya ahadi zake. :/:
6 Uliye dhambini ufike Kwa Yesu Mwokozi wa wote! :/:
Anakunyoshea mikono Ya pendo kukusaidia. :/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
52. KWA SALAMA BABA MUNGU AWALINDA
1 KWA salama Baba Mungu Awalinda watu wake, Hata nyota
za mbinguni Si salama kama wao.
2 Mungu awalinda hivyo Katika upendo wake.
Wanakumbatiwa naye, Wanarehemiwa sana.
3 Hawavutwi toka kwake Kwa furaha wala shida. Yeye ni
rafiki ’kubwa Wa walio watu wake.
4 Wanalishwa, wanavikwa, Wanafarijiwa naye. Hata nywele
za kichwani Zimehesabiwa zote.
5 Enyi kundi lake dogo, Mungu atawakingiza! Na adui
watashindwa Kwa uwezo wake ’kubwa.
6 Akitoa, akiwapa, Baba yetu hageuki. Na mapenzi yake
ndiyo: Wana wapatishwe wema.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
53. KATI’ MIKONO YAKE YESU
1 KATI’ mikono yake Yesu ananilinda. Katika pendo kubwa
Ninapumzika sana. Sasa sauti nzuri Itokeayo juu
Inanikumbukia mbingu na raha yake.
Kati’ mikono yake Yesu ananilinda. Katika pendo
kubwa ninapumzika sana.
2 Kati’ mikono yake Nitakaa daima, Sitatetema tena, Yeye ni
uwezo wangu. Shaka sinayo sasa, Wala sioni woga, Hata
ikiwa shida, Yesu anifariji.
3 Yesu Mwokozi wangu Alikomboa mimi. Ufa wa mwamba
ule, Nitapumzika humo. Katika saa ngumu Ya majaribu tele
Ninasaburi ’ona Jua la asubuhi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
54. USIOGOPE MATESO YAKO
1 USIOGOPE mateso yako, Mungu anakulinda, Bali tazama
mapenzi yake, Mungu anakulinda!
Mungu anakulinda Siku kwa siku njiani mwake.
Anakulinda salama, Mungu anakulinda.
2 Ukichukuwa mizigo ’zito, Mungu anakulinda, Kati’ hatari
za njia yako Mungu anakulinda.
3 Anakumbuka hitaji zako, Mungu anakulinda. Utashiriki
ujazi wake, Mungu anakulinda.
4 Katika njia ya migogoro Mungu anakulinda. Mfunulie
fadhaa zako, Mungu anakulinda.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
55. TUPATE KWA NANI FARAJA YA ROHO?
1 TUPATE kwa nani faraja ya roho? Kwa Yesu, kwa Bwana
Yesu. U wapi msingi wa kutegemea? Kwa Yesu, kwa Bwana
Yesu.
Kwa Yesu, kwa Yesu Ninashangilia kwa roho na
moyo. Uheri wa huko haufasiriwi, Moyoni
wafahamiwa.
2 Na maji mazima yapatwa kwa nani? Kwa Yesu, kwa Bwana
Yesu. Na wapi twapata mikate nyikani? Kwa Yesu, kwa
Bwana Yesu.
3 Mahali tutapostarehe ni wapi? Kwa Yesu, kwa Bwana Yesu.
Na nguvu ya kuendelea ni wapi? Kwa Yesu, kwa Bwana
Yesu.
4 Ni nani anayebatiza kwa Roho? Ni Yesu, ni Bwana Yesu.
Upendo wa ndugu watoka kwa nani? Kwa Yesu, kwa Bwana
Yesu.
5 Wakristo watakusanyika kwa nani? Kwa Yesu, kwake
mbinguni. Kwa nini watashangilia milele? Kwa Yesu na
pendo lake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
56. YESU, NINAKUTOLEA VYOTE NINAKUWA NAVYO
1 YESU, ninakutolea Vyote ninakuwa navyo, Nikupende,
nifuate Wewe siku zote hapa!
Ninakupa vyote, Ninakupa vyote, Bwana Yesu
upendwaye, Ninakupa vyote.
2 Miguuni pako, Yesu, Ninakusujudu sasa. Ninakutolea vyote:
Roho, moyo na maungo.
3 Najitoa kwako, Yesu, Nafsi yote iwe yako! Bwana Yesu,
nakusihi: Niwashie moto wako!
4 Yesu, ninakupa vyote, Unijaze Roho yako! Nisikie moto
wako Ukiwaka ndani yangu!
5 Vyote ninakupa, Bwana, Viwe mali yako kweli! Na fahari ya
dunia Naiona ni ya bure.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
57. YESU, ULIYEKUFA KWA AJILI YANGU
1 YESU, uliyekufa kwa ajili yangu, Ninajitoa kwako, niwe
mali yako! Bwana, nivute kwako, Nifahamishe pendo, Niwe
dhabihu hai katika shukrani!
2 Yesu, nafika kwako, kao la rehema; Bwana, nitie nguvu kwa
neema yako! Niuchukue tena Kwa radhi msalaba, Ni’tumikie
Wewe, Mkombozi wangu!
3 Bwana, uniumbie moyo haki, safi, Kwako niishi tena hata
kufa kwangu! Niwatafute wenye Dhambi na udhaifu,
Niwapeleke kwako, Bwana wa upendo!
4 Vyote ninavyo huku nimepewa nawe, Ukivitaka, Bwana,
uvitwae vyote! Nina urithi wangu kwako mbinguni juu,
Nitakuona huko kwa furaha kuu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
58. UNIPE RAHA TELE KAMA MTO
1 UNIPE raha tele kama mto, Nipite jangwa huku kwa furaha;
Unipe na imani tena, Yesu, Ningoje siku yako kwa bidii!
2 Kwa siku chache ninaona shida, Dhoruba zinanisumbua
huku. Napanda mbegu zangu nikilia, Lakini nitavuna kwa
furaha.
3 Kwa siku chache ninaburudishwa Mtoni penye njia yangu
huku, Lakini siku kubwa itafika, Nita’inywea chemchemi
yake.
4 Kwa siku chache naitunza taa, Nadumu kwa kuomba na
kungoja. Na siku za uchungu ziishapo, Nitamkuta Yesu
huko juu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
59. YESU, NINAKUTOLEA MOYO NA MAISHA YANGU
1 YESU, ninakutolea Moyo na maisha yangu, Niwe mfuasi
wako, Safi na mtakatifu!
:/: Mungu wangu,:/: Nitakase saa hii!
2 E’ Mwokozi, ’nitakase, Unijaze pendo lako, Na maisha
yangu yote Yawe yako, Bwana wangu!
3 Ninataka kuheshimu Wewe, Mkobozi mwema; Nifanane
nawe, Yesu, Kati’ watu wa dunia!
4 Nikikaa kimya kwako Kama yule Mariamu, Nifundishwe
nawe, Bwana, Sitahangaika tena.
5 Tawi lake mzabibu Ulitunze na ’safisha, Ili kwa uweza wako
Litaza’ matunda mengi!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
60. NI HERI KUONA NDUGU
1 NI heri kuona ndugu Njiani pa kwenda mbingu.
Tukinyong’onyea sana Kwa kuwa tu peke yetu,
Kushirikiana kwa ndugu Kunaturudisha moyo, Na Mungu
atupa nguvu Tukiyainua macho.
2 Twafungamana rohoni, Tulio wa nyumba yake, Huoni
ulimwenguni Kushirikiana kwetu. Na tuna Mwokozi mmoja,
Imani ni moja pia, Watoto wa Baba ’moja Twashika sheria
yake.
3 Furaha ya ulimwengu Haitatuvuta tena, Twaona kung’aa
kwake Ni bure na bila kisa. Lakini tukikusanyika Kwa jina
la Mungu Baba, Atuandalia kweli Karamu ilio bora.
4 Tukivumilia hata Ukomo wa mashindano, Mbinguni
tutawaona Wakristo wapenzi wote. Hatutatawanyika huko,
Tu wote umoja kweli, Milele tuta’pokaa Nyumbani mwa
Baba yetu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
61. ENYI WATU WA SAYUNI
1 ENYI watu wa Sayuni, Kundi dogo la Mwokozi, Yesu
aliwanunua Kuwa mali yake Mungu. Sasa mnapita njia Ya
miiba na hatari Kati’ nchi ya ugeni; Bali mbingu mtafika.
2 Kumwamini, kumpenda Yesu ni uheri wetu; Amri zote
zinashikwa Kwa upendo na imani. Kwa imani twaokoka,
Pendo ni uzima wetu. Yesu utusaidie, Utujaze pendo lako!
3 Juu ya msingi huo, Yesu, unijenge mimi, Na zaidi niungane
Nawe na kanisa lako! Sisi tu matawi yako, Tushirikiane
sana, Na katika kundi zima Iwe nia moja kweli!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
62. MUNGU, NIVUTE KWAKO
1 MUNGU, nivute kwako, Karibu kwako, Hata ikiwa shida
Ikinisukuma! Katika yote hapa ’takuwa wimbo wangu:
Mungu, nivute kwako, Karibu kwako.
2 ’kiwa katika mwendo Jua likichwa, Giza yanizunguka, Peke
yangu mimi, Kwako, E’ Baba yangu, Nafika, nakuomba:
Mungu, nivute kwako, Karibu kwako!
3 Unionyeshe njia Ya kwenda juu, Nijue kupokea Yote toka
kwako! Unifariji sana, Niimbe tena hivi: Mungu, nivute
kwako, Karibu kwako!
4 Katika mambo yote Nikushukuru, Majaribuni pote
Nikumbuke wewe! Unifundishe hivi: Omba katika yote!
Mungu, nivute kwako, Karibu kwako!
5 Nikimaliza mwendo Wa msafiri, Mungu utaniita Kwako
huko juu. Na nitaimba tena Kati’ watakatifu: Umenivuta,
Mungu, Karibu kwako!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
63. YESU, NIVUTE KARIBU NAWE
1 YESU, nivute karibu nawe, ’kiwa kwa shida, ikiwa kwa
raha! Uliyekufa msalabani, :/: ’nifahamishe upendo na
ne’ma! :/:
2 Yesu, nivute, mimi maskini, Sina vipaji vya kukutolea, Moyo
ninao wenye uchafu, :/: Uupokee, ’uoshe kwa damu! :/:
3 Yesu, nivute, nikutolee Yote ninayo, E’ Bwana mpendwa,
Ninakuomba: Uyaondoe :/: Yote yanayonitenga na Mungu!
:/:
4 Yesu, nivute karibu nawe Hata ukomo wa vita na shida!
Tena mbinguni nitakuwapo :/: Karibu nawe, E’ Yesu
Mwokozi! :/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
64. KIMYA, E’ MOYO WANGU
1 KIMYA, E’ moyo wangu, Mbele za Bwana Yesu! Unahitaji
sana ’kaa daima kwake. Njia salama ipi Ulimwenguni huku
Bila kumfuata Yesu na Neno lake?
Uniongoze, Bwana, Katika njia yako! Hata ikiwa
shida Nitawasili kwako.
2 Kimya, E’ moyo wangu, Omba kwa tumaini! Nuru itatokea
Ukiamini Mungu, Na umwambie Yesu Shaka uliyo nayo,
Atakuosha sana, Atakuonya njia.
3 Kimya, E’ moyo wangu, Msikilize Mungu! Akuletea nguvu,
Tena hekima kweli. Na ukiendelea Katika Neno lake, Mungu
atakujaza Nguvu na uthabiti.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
65. HUKO JU’ YA NYOTA ZOTE
1 HUKO ju’ ya nyota zote Kuna nchi yenye mema, Mji wake
ni Yerusalemu; Dhambi haitakuwamo, Wala kufa na
huzuni, Kwake Yesu nitapata kao.
Sikitiko na machozi Hayatakuwako huko, Wala
giza au vita ya dunia. Huko hatutayaona Mambo
ya kutuumiza, U Yerusalemu ’takatifu!
2 Nifikapo mji huo Nitaona Yesu kwanza, Aliyechukua
dhambi zangu. Nitaona uso wake, Nitamshukuru Yeye
Aliyeniweka huru kweli.
3 Huko nitaona tena Jeshi la walioshinda Kwa imani huku
duniani, Na pamoja nao wote Nita’sifu Mungu sana Juu ya
neema yake kubwa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
66. WAKRISTO WA NCHI ZOTE
1 WAKRISTO wa nchi zote Watakusanyika huko Mbinguni
kwa Yesu, mezani pake, Kati’ ufalme wake; Kuona uzuri
wake, Kujazwa neema yake. Wataimba huko ju’ milele na
milele.
Watoka bahari zote, Watoka katika shida, Watoka
milima, Watoka mabonde Kufika kwa Mungu
Baba, Kuvikwa mavazi safi, Kuona Mwokozi wao,
Yeye ali’wafilia ju’ ya msalaba.
2 Watakusanyika wengi Waliookoka huku. Mateso na kufa,
shida na giza Hawata’ona kamwe. Ya kale hayatakuwa, Lo!
Yote ni mapya huko! Itakuwa raha tu pamoja na faraja.
3 Tazama mlango huko Uliokufunguliwa, Na kuna mahali,
Yesu aita: “Njoo nyumbani kwangu!” Wenzetu waliofika
Wanatungojea huko, Malaika wanaimba kutukaribisha.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
67. TUNAKARIBIA KAO LA MBINGUNI
1 TUNAKARIBIA kao la mbinguni, Hata jua likifichwa na
mawingu. Tufuate Bwana Yesu sikuzote, Ni furaha yetu
kumwandama Yeye!
Tunakaribia mbingu kati’ yote, Haleluya! ’sifuni
Mungu! Jipe moyo safarini, kwani Yesu Yu pamoja
nasi hata mwisho!
2 Tunakaribia kao la mbinguni, Hata tukiona pepo na
dhoruba. Bwana Yu karibu, na uwezo wake Ni makimbilio
yetu hatarini.
3 Njia yetu inapita kati’ jangwa, Na miguu inauma mara
nyingi, Walakini tunakwenda tukiimba Na kusifu Yesu,
Mwokozi wetu.
4 Mwendo wetu utaisha siku moja, Tutapata kustarehe huko
juu. Tukiona shaka, shida hapa chini, Tutapata utulivu
kwake Yesu.
Tunakaribia mbingu kati’ yote, Haleluya! ’sifuni
Mungu! Tunataka kufuata hata mwisho. E’ rafiki,
utuandamie!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
68. MBINGUNI KWA MWOKOZI WANGU MWEMA
1 MBINGUNI kwa Mwkozi wangu mwema Nitaamka asubuhi
moja, Nitayaona majeraha yake, Sauti yake nitaisikia.
2 Makao ya milele ni tayari, Ali’waandalia watu wake.
Tutamsifu Yesu sana huko, Aliyetuokoa na hatari.
3 Na nyimbo za wokovu zinaimbwa Mbinguni mbele ya
Mwokozi wetu; Tungesikia huku nusu ndogo, Vitani
tungepata ushujaa.
4 Lakini Yesu Yupo nasi leo, Usiku kama moto mbele yetu. Na
Neno lake ni upanga wetu, Ahadi ni safina ju’ ya maji.
5 Tungoje Yesu siku chache tena! Twakaribia mwisho wa
safari. Tungoje asubuhi huko juu! Atatukaribisha Bwana
Yesu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
69. JE, TUTAONANA TENA HUKO NG’AMBO
1 JE, tutaonana tena Huko ng’ambo ya Yordani, Na pamoja
na wakristo ’ona raha ya milele?
Tuonane, tuonane Huko ng’ambo ya bahari!
Tuonane kwa furaha, Huko shida ikomapo!
2 Je, tutaonana tena, Ba’da ya dhoruba zote Huko katika
bandari Ya salama na amani?
3 Je, tutaonana tena Kati’ mji wa dhahabu, Penye mto wa
uzima Nayo miti ya matunda?
4 Je, tutaonana tena Na kusifu Mungu wetu Miongoni mwa
wakristo Waimbao huko juu?
5 Tutaona na wapenzi Waliotuacha huku? Je, tutawaona wote
Katika makao mema?
6 Tutaona Bwana Yesu Katika kutano huko, Tutakaribishwa
naye Katika karamu kuu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
70. KUNA MJI HUKO JUU
1 KUNA mji huko juu, Umejengwa naye Mungu, Humo kuna
mto ’moja Wenye maji mazima kabisa.
Tutakusanyika huko Kwa raha penye mto mwema
sana, Tutakusanyika na wakristo Penye mto wa
maji mazima.
2 Huko pwani nchi nzuri, Bila dhambi na huzuni, Tutaimba
nyimbo mpya, Nyimbo njema ’kusifu Mwokozi.
3 Kama twamwamini Yesu, Kama hatufichi dhambi, Kama
moyo ni mweupe, Tutafika mtoni pa mbingu.
4 Tu karibu ya kufika Na kuona mto ule. Mungu atatupa raha
Na kutustarehesha daima.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
71. NIMEKWISHA KUINGIA NCHI NZURI
1 NIMEKWISHA kuingia nchi nzuri ya ahadi, Nchi njema ya
wokovu wake Mungu. Huko ni vijito vingi vya baraka na
furaha, Huko shida haifiki.
Nimekwisha kuingia Nchi nzuri ya ahadi. Moyo
wangu hufurahi, Ninaishi kwa neema.
2 Nimefika Kanaani, hapo ni urithi wangu, Na sitaki
kuondoka tena kamwe. Sasa nira ni laini na mzigo si mzito,
Yesu ni furaha yangu.
3 Nimekwisha kuingia nchi ya amani kuu, Hata mwili wangu
unatiwa nguvu. Nchi hiyo ni ya raha na faraja imo pia, Hapo
tunaka’ salama.
4 Nime’ngia nchi hiyo, ndiye Bwana Yesu Kristo, Ninakaa
katika urithi wangu. Kwa imani ninakunywa maji hai ya
kisima, Huku ni furaha kubwa.
5 Nitafika hata mbingu, nchi ya hazina yangu, Dhambi na
mateso hazitakuwako, Wala giza ya usiku, wala sikitiko
chungu, Wala shida, wala kufa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
72. MIMI MGENI KATIKA DUNIA
1 MIMI ngeni katika dunia, Ninasafiri kufika mbinguni. Hata
ikiwa hatari njiani, Nitaishinda pamoja na Mungu. Kama
Ibrahimu majaribuni Nita’vyoshinda kwa nguvu ya Mungu.
Nitavumilia nifike mbinguni, Ndilo kusudi la moyo.
2 Nikitembea gizani kabisa Mimi mnyonge pamoja na Yesu,
Na nikipita motoni, majini, Nakusudia kufika mbinguni.
Mungu ajua mapito jangwani, Naye Mwenyezi atanifikisha.
Nitavumilia nifike mbinguni, Ndilo kusudi la moyo.
3 Tusisumbuke katika safari, Tuwatazame wali’tangulia! Yesu
Mwokozi alitukomboa, Msalabani alitufilia; Naye
atatufikisha mbinguni; Hivi tuimbe kwa muda kitambo:
Tutavumilia tufike mbinguni, Ndilo kusudi la moyo!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
73. NAJUA NJIA MOJA YA KU’FIKIA MBINGU
1 NAJUA njia moja Ya ku’fikia mbingu, Ingawa ikipita
Katika majaribu, Lakini iendako Mjini huko juu, :/: Na njia
hiyo Yesu. :/:
2 Najua na amani Iliyo ya milele, Huwezi kuipewa Kwa fedha
na dhahabu; Ni tunu ya rehema Iliyotoka Baba. :/: Amani
hiyo Yesu. :/:
3 Najua nguvu moja Ya kuniponya roho, Initiayo raha, Amani
na faraja, Inanilinda vema Na nguo yangu safi, :/: Na nguvu
hiyo Yesu:/:
4 Najua na kifiko Mbinguni huko juu, Na siku ni karibu
Kita’poonekana. Yafa’ kukaza mwendo, Kupiga mbio sana!
:/: Kifiko ni mbinguni. :/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
74. MGENI MIMI HAPA MAHALI PA UGENI
1 MGENI mimi hapa Mahali pa ugeni, Na kwetu mbali mno
Katika nchi nzuri. Na ni mjumbe huku Kutoka Mungu wetu,
Nina habari ya Mfalme.
Habari yake nzuri sana, Furaha yao malaika:
“Mpatanishwe sasa Na Mungu Baba yetu!” Habari
yake ndiyo hiyo.
2 Salamu ya Mwokozi Kwa kila mtu hapa: Urudi kwake
Mungu, Utoke utumwani! Ufike kwake Yesu, Tubia dhambi
zako! Habari hiyo ya Mfalme!
3 Mbinguni nchi nzuri, Yapita vitu vyote, Furaha huko tele Na
raha ya milele. Ukiamini Yesu Uta’pokaa huko. Habari hiyo
ya Mfalme!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
75. NILIYE MSAFIRI, MGENI DUNIANI
1 NILIYE msafiri, mgeni duniani; Sioni kwangu hapa, ni huko
ju’ mbinguni. Ninatamani nami kukaa siku zote Pamoja
naye Baba katika utukufu.
Kwangu mbinguni, kwangu, Uzuri wa mbinguni
Wapita yote huku.
2 Mwokozi Yuko huko, Rafiki yangu mwema, Aliyenikomboa
na ku’chukua dhambi. Na hata nikiona furaha siku zote
Ningali natamani makao ya mbinguni.
3 Na nikipewa huku vipawa vya thamani, Na wakiimba
nyimbo za kunifurahisha, Rafiki zangu wote wakipendeza
mimi, Ningali natamani makao ya mbinguni.
4 Upesi nitaona kifiko cha mbinguni, Mwokozi wangu Yesu
atanikaribisha; Na huko nitaona nilivyotumaini, Kinubi
nita’piga kumshukuru Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
76. MGENI MIMI, NINASAFIRI
1 MGENI mimi, ninasafiri Siku chache, siku chache huku
chini. Msinipinge, niwafuate Watakatifu walioshinda! Mgeni
mimi, ninasafiri Siku chache, siku chache huku chini.
2 Nashika njia, napiga mbio, Sina budi kuukaza mwendo
wangu. Na kwa mkono natwaa gongo, Nazo silaha
nimejivika. Nashika njia, napiga mbio, Sina budi kuukaza
mwendo wangu.
3 Ulimwenguni sipati raha, Natamani ku’fikia mji mpya.
Machozi, kufa, maombolezo Sitayaona mbinguni tena.
Ulimwenguni sipati raha, Natamani ku’fikia mji mpya.
4 Mchunga mwema, ninakuomba, ’tangulie, niongoze njia
yote, Kwa kuwa giza na dhambi tena Zaniwekea mitego
mingi! Mchunga mwema, ninakuomba, ’tangulie, niongoze
njia yote!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
77. NAIFUATA NJIA YA KU’FIKIA MBINGU
1 NAIFUATA njia ya ku’fikia mbingu Na mji mwema ule
alio’jenga Mungu. Ninasafiri sasa kutoka duniani Nifike nchi
hiyo ya raha na uzima.
Naifuata njia ya ku’fikia mbingu Na mji mwema
ule alio’jenga Mungu.
2 Sijauona bado uzuri wake bora Wa mji wa mbinguni, usio
na machozi; Lakini siku moja, kwa shangwe ya milele
Nitamsifu Yesu katika mji ule.
3 Nifikapo mjini, mlango wake wazi, Na hapo malaika
watanikaribisha; Shindano la dunia halitakuwa huko, Na
nitaona raha milele na milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
78. NINA UZIMA WA MILELE
1 NINA uzima wa milele, Na tumaini ni imara, Mbinguni
nitaona Yesu, Mwokozi wangu, kwa furaha.
2 Nina urithi bora huko Unaolindwa hata mwisho. Na kila siku
ya jaribu Natiwa nguvu naye Baba.
3 Namshukuru Mungu wangu! Ananitunza siku zote Katika
shida na taabu, Kwa hiyo sisumbuki tena.
4 Rohoni mwangu ni amani, Naimba kwa furaha kubwa.
Nikiongozwa naye Yesu Naendelea kwa salama.
5 E’ Bwana Yesu, unifunze Ku’tumikia Wewe vema Wakati
ubakio tena Wa mwendo wangu duniani!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
79. MAISHA MAFUPI YA HUKU DUNIA
1 MAISHA mafupi ya huku dunia Yanaifanana safari
chomboni. Twapita bahari katika hatari, Lakini Mwokozi
anatuongoza.
Ikiwa Mwokozi anatuongoza Twaweza kuona
amani na raha, Atatufikisha salama mbinguni,
Na humo hatutakumbuka safari.
2 Twapita katika baridi na pepo, Maneno ya Mungu ni nuri
gizani. Hatari na hofu na chombo kibaya Hatuta’kumbuka
karibu na Yesu.
3 Ingawa mawimbi yapiga kwa nguvu, Tunakaribia bandari
upesi, Na humo hakuna dhoruba na pepo; Safari tutaimaliza
salama.
4 Tutakapofika bandari ya mbingu Tutamshukuru Mwokozi
mkuu. Hatutaziona hatari na hofu Karibu na Yesu
mwenyewe mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
80. ZITAKAPOTIMIA SIKU ZA HUDUMA YANGU
1 ZITAKAPOTIMIA siku za huduma yangu Nitaona asubuhi
ya uzima. Huko juu mbinguni nitamwona Bwana Yesu, Na
“Karibu” yake nitaisikia.
Nitamtambua Yeye, Na karibu na Yesu nitakaa.
Nitamtambua Yeye kwa alama za majeraha yake.
2 Itakuwa furaha kuuona uso wake Na uzuri utokao macho
yake. Moyo utafurika kwa uheri na furaha, Ju’ ya kao
aliloniandalia.
3 Na walio mbinguni wananingojea kwao, Nakumbuka siku
tulipoachana. Wataimba kabisa kunikaribisha huko,
Walakini nitamwona Yesu kwanza.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
81. ALIPOKUFA YESU JU’ YA MSALABA
1 ALIPOKUFA Yesu ju’ ya msalaba wake Akaishinda dhambi
na uwezo wa Shetani. Aliniweka huru, niwe mbali na hatia;
Na tena atanichukua kwake.
Mbinguni niendako Haitakuwa dhambi, Ni nchi
nzuri ya salama mno. Na Bwana, Mungu wetu,
Atatuangazia; Tukusanyane sisi sote humo!
2 Ninafuata njia ya Mwokozi wangu sasa, Aniongoza vema,
anafuta kila chozi. Ananilinda katika hatari za njiani,
Karibu naye vita yatulia.
3 Mbinguni nchi yangu, na bendera ni upendo, Na Roho
arabuni ya urithi wangu huko; Na Neno lake ni chakula
changu safarini; Neema inanipeleka kwake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
82. NINAJUA NCHI NZURI
1 NINAJUA nchi nzuri, Huko Mungu alifanya Nyumba na
makao kwetu; Natamani kufikako.
Mbinguni, kao la malaika! Mbinguni vyote
vinamulika! Mbinguni Mungu atualika
Tukusanyane mbinguni kwake!
2 Katika safari yangu Ninajiuliza sana Kama nami nitafika
Penye Mungu ndiye jua.
3 Kwa neema yake kubwa Nitakaa kwake Mungu, Bwana
Yesu atanipa Taji nzuri ya uzima.
4 Sasa ninapiga mbio, Nifikie nchi hiyo Ya uzima na furaha,
Nchi ya tamani yangu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
83. NINAJUA NCHI HUKO JUU
1 NINAJUA nchi huko juu, Hapo Mungu alijenga mji, Na aita
’moja moja kwake, Waliomaliza mwendo huku.
Shida, kufa na huzuni Hazitakuwapo huko. Yesu
atafuta kila chozi, Tutaona shangwe, nayo tele.
2 Huko hawataingia kamwe Wenye dhambi, wala cha
kinyonge, E’ rafiki, ujihoji leo Kama wewe utaona mbingu!
3 Utazame, mto ungaliko Uwezao kusafisha sana! Ujioshe
kati’ damu safi Ya Mwokozi wetu Yesu Kristo!
4 Nafurahi kwani ninajua Kao langu liko huko juu, Natamani
sana kufikako. Njoo, Yesu, unitwae mbio!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
84. NINAKUMBUKA SAYUNI
1 NINAKUMBUKA Sayuni, Nchi ya heri mbinguni, Bahari
kama kioo Na’furahia rohoni. Nyuma kimeta cha nuru
Naona mji wa mbingu, Nyimbo za nyumba ya Baba
Nasikiliza daima.
Mapambazuko mbinguni Yataondoa utaji, Vyote
tulivyoamini Tutaviona milele.
2 Mauti haina nguvu, Yesu a’vunja uchungu, Naye
aliwakomboa Wote: wafalme, watumwa. Ninamtwika
Mwokozi Dhambi, huzuni na shida; Mbavuni mwake nafasi
Kama bandari salama.
3 Kuna ’jaribu njiani, Mengi ya kunizuia, Na mara nyingi
miiba Inaumiza miguu. Nikikumbuka Sayuni moyo huwaka
kabisa, Mbingu ninaitazama Na ku’himiza safari.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
85. TWAPASHA HABARI YA MBINGU
1 TWAPASHA habari ya mbingu, Mahali pa watu wa heri, Na
tunatamani ku’ona Ufuko wa nchi ya mbingu.
Sikitiko wala shida Hazitakuwapo mbinguni. Huko
juu, huko juu Tutashangilia milele.
2 Twapasha habari ya mbingu Na mji mzuri ajabu, Na jeshi la
watakatifu Waliomaliza safari.
3 Twapasha habari ya pendo, Amani na nguo nyeupe, Na raha
baada ya vita, Makao karibu na Mungu.
4 Twapasha habari ya Yesu, Alituokoa na dhambi. Ingawa ni
shida njiani Atatufikisha mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
86. TUTAONA FURAHA MBINGUNI
1 TUTAONA furaha mbinguni, Ni makao ya watu wa heri.
Tutakuwa pamoja na Mungu Na kusifu Mwokozi wetu.
Tutafurahi na tutaabudu Huko juu kwake Mungu.
Tutafurahi na tutaabudu Siku tutakapofika.
2 Mara nyingi furaha ya hapa Yapinduka machozi machungu,
Walakini hazitakuwapo Sikitiko na shida huko.
3 Kama shida na shaka zafika Kuzuia safari ya hapa,
Tutazame daima mbinguni, Huko juu ni raha yetu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
87. MWISHO WA NJIA YA MUNGU NI MBINGU
1 MWISHO wa njia ya Mungu ni mbingu; Yesu ananiongoza
salama. Kama Shetani akinijaribu Nakitazamia kifiko.
Kwetu mbinguni hatutatawanyika, dhambi na
mateso hayatakuwapo, Na hatutaona machozi na
shida, Ila furaha milele.
2 Tutawaona walioishinda Dhambi, Shetani na mambo
mabaya, Na tutaona Mwokozi mpenzi; Tutafananishwa na
yeye.
3 Nani ataka kufika mbinguni? Yesu ni njia, uzima na kweli.
Njoo kwa Yesu! Akuandalia Kao la milele mbinguni.
:/: Malaika wanangoja :/: Malaika wanangoja huko
mbinguni! :/: Malaika wanangoja:/: kutusalimu:
“Karibu”!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
88. MPONYI APITAYE WOTE
1 MPONYI apitaye wote Amefika hapa. Awaponyesha watu
moyo, Yesu wa upendo.
Jina liyapitalo yote Juu na chini, pote pia, Jina
kubwa, jina jema: Yesu wa upendo!
2 Awasamehe watu dhambi Wakizitubia, Awapokea kwa
neema, Waipate afya.
3 Tukiwa na masikitiko, Yesu afariji. Akitubarikia sana,
Woga waondoka.
4 Watoto walipenda sana Jina lake Yesu, Liwalindalo na
mabaya, Wakijaribiwa.
5 Shetani aogopa sana Jina lake Yesu. Katika vita ju’ ya
dhambi Latutia nguvu.
6 Mbinguni tena kwa furaha Tutamwona Yesu. Tutasahau
shida zote, Tutamshukuru.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
89. NAJUA JINA MOJA ZURI
1 NAJUA jina moja zuri, Lapita kila jina huku, Lanipa raha
na amani, Na jina hilo Yesu.
Yesu, jina zuri mno! Yesu, unapenda wote, Yesu,
tunalindwa vema Katika jina lako.
2 Napenda jina hilo jema, Linanivuta kwake Mungu. Na
katika huzuni yangu Lanifariji sana.
3 Siwezi mimi kueleza Uzuri wake jina hili, Lakini namwimbia
Yesu, Nasifu jina lake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
90. YESU, YESU, JINA KUBWA
1 YESU, Yesu, jina kubwa, Nyimbo zao malaika! :/: Limekuwa
ndani yangu Mto wa furaha bora.:/:
2 Jina lake kama nyota Linanionyesha njia. :/: Katika jaribu,
shida, Na usiku duniani.:/:
3 Ni mikono ya upendo Yenye kunikumbatia. :/: Hapo
najificha vema Kama chombo bandarini.:/:
4 Jina hilo liwe kwangu Wimbo wa safari yangu! :/: Niletewe
wema nalo Toka nchi nzuri juu! :/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
91. YESU, JINA HILI JEMA
1 YESU, jina hili jema Lichukue siku zote! Lina raha na
faraja, Lichukue uendako!
Jina kubwa, jina zuri La matumaini yetu! Jina
kubwa, jina zuri La furaha ya mbinguni!
2 Lichukue jina hilo Lenye nguvu ya kushinda! Ukijaribiwa
huku, Taja jina lake Yesu!
3 Yesu, jina jema mno, Latutia shangwe kubwa, Ni
makimbilio yetu, Ngome, msaada pia.
4 Na kwa jina lake Yesu Kila goti litakunjwa, Watu wote
watakiri Kwamba Yesu ni Mfalme.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
92. YESU! JINA HILI LINAPITA
1 YESU! Jina hili linapita Kila jina duniani pote. Yesu, Yesu!
Jina hilo Ni marhamu iliyomiminwa.
Jina hili ni lenye nguvu ya Kuondoa dhambi zangu
zote. Yesu, Yesu! Jina hilo Lanitia shangwe na
furaha.
2 Si jingine jina duniani Lenye nguvu, kweli na uzima. Yesu,
Yesu! Jina hilo Waliloimbia malaika.
3 Jina hili lina wema mno, Limejaza mbingu tangu mwanzo.
Yesu, Yesu! Jina hilo Litaimbwa duniani pote.
4 Sitaweza kusahahu Yesu, Jina lake ni wokovu wangu. Yesu,
Yesu! Nitamwona Huko kwake tena kwa furaha.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
93. SIKU CHACHE
1 SIKU chache, na tena wakristo Watakwenda kumwona
Mwokozi, Siku chache, na wataipewa Thawabu na taji ya
uzima.
Nangoja sana Bwana Yesu Kama zamu angojavyo
asubuhi. :/: Kwa dalili zote ninaona sasa Kwamba
Yesu Yu karibu ya kurudi:/:
2 Siku chache za vita ya huku, Tena Yesu Mfalme ’takuja;
Tutaona furaha na raha, Atatupeleka kwake juu.
3 Siku chache machozi ya shida, Mungu atayafuta kabisa. Na
baada ya siku si nyingi Kwa lango nitaingia mbingu.
4 Baragumu la mwisho ’talia, Waminifu watachukuliwa;
Wote wataingia mbinguni Kukaa pamoja na Mwokozi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
94. LO! NURU INAPAMBAZUKA
1 LO! Nuru inapambazuka, Na vivuli vya usiku vi’kimbia;
Unaulizwa: “U tayari?” Yesu yuaja upesi!
Na kama vile ’pepo uvumavyo po pote Habari
iendavyo ulimwenguni mwote. Ni neno la furaha,
matumaini yetu: “Yesu yuaja upesi!”
2 Vizazi wengi wamefungwa Katika utumwa, minyororo
’gumu; Uhuru ni kwa Bwana Yesu, Naye yuaja upesi!
3 Na watu wengi waamka, Nuru ya Injili yafukuza giza.
Tutatwaliwa ju’ mbinguni; Yesu yuaja upesi!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
95. NCHI NZURI YATUNGOJA
1 NCHI nzuri yatungoja Huko juu ya mawingu,
Watakapokusanyika wateule. Siku zina’tubakia Zinapita
mbio sana; Waminifu watarithi nchi nzuri.
:/: Lo! Ufalme wake Mungu u karibu!:/: Uwe safi,
roho yangu, Ukakeshe siku zote! Lo! Mfalme wake
Yesu Yu karibu!
2 Twaamini tutaona Nchi ile kwa uwazi, Tunangoja sana
Mkombozi wetu; Kwa dalili tunaona Siku yake ni karibu;
Zinatuarifu Yesu aja hima.
3 Maandiko yanasema: Mkombozi atakuja, Katika mawingu
ataonekana. Haleluya! Haleluya! Atafunga yule mwovu,
Aliyejaribu kutuangamiza.
4 Katika kungoja Yesu Watu wengi wamechoka; Waamshe,
uwaonye kwa dalili! Kwani Neno lake Mungu Latimizwa
mbio sana, Tunaona kwamba Yesu Yu karibu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
96. MWOKOZI WETU ALIAHIDI
1 MWOKOZI wetu aliahidi Ya kwamba atakuja siku moja
Kutupeleka mbinguni kwake. Yawezekana upesi sana.
Sioni shaka, nina amani Kwa Mkombozi na damu
yake, Na Roho yake Mtakatifu Ni arabuni ya ’rithi
wangu.
2 Wajumbe wengi wa Bwana Mungu Watumwa sasa duniani
pote. Waitangaza habari njema Ya Yesu Kristo na pendo
lake.
3 Na watu wengi wanaamini, Wanaitika mwito wake Mungu.
Kwa roho moja twakaza mwendo, Tufikilie thawabu yetu.
4 Twakaribia wakati ule Wa kuja kwake Bwana Yesu Kristo;
Na tujiweke tayari wote Kuchukuliwa mbinguni kwake!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
97. BADO KIDOGO JUA LITAPANDA
1 BADO kidogo jua litapanda, Siku tuta’pofika huko juu.
Huko mbinguni tutapumzika Na ’pata raha na furaha ya
milele.
Tutamlaki Bwana Yesu Kristo, Aliyetuokoa kweli
hapa chini. Huko mbinguni tutamwona Yeye,
Tutamsifu kwa upendo wake ’kuu.
2 Bado kidogo tutaona vyote Vitageuka kuwa vipya tena, Na
hapo Yesu, Mkombozi wetu, Atatufungulia lango la
mbinguni.
3 Safari yetu ina majaribu, Tutafurahi kwa kufika mbingu.
Hatutaona giza, shaka tena, Tutamshangilia Mkombozi
wetu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
98. SIKU MOJA TUTAONA UTUKUFU
1 SIKU moja tutaona Utukufu wake Yesu, Kama nuru ya
umeme Atakavyoonekana.
Uhubiri Neno lake, Kwa bidi’ mahali pote! Siku ni
karibu sasa : Bwana Yesu atakuja.
2 Tangu kale tumengoja Siku ya uhuru wetu. Hata nguvu ya
mauti Itaisha siku ile.
3 Heri gani ya wakristo Kumlaki Bwana Yesu! Watavikwa
nguo safi Huko juu kwa Mwokozi.
4 Pasha hi’ habari njema, Na wagonjwa uwaponye! Uokoe
wapotevu! Wende mbio, usikawie!
5 Kwa dalili tunaona Kwamba Yesu Yu karibu, Na Mfalme
atakuja ’tupeleka kwake juu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
99. SIKU MOJA NITAMWONA BWANA YESU
1 SIKU moja nitamwona Bwana Yesu uso wake. Na milele
kwa furaha Nitaka’ karibu naye.
Nitamtazama Yesu Ju’ ya nyota zote pia, Huko
kwa ukamilifu Nitajua nguvu yake.
2 Hapa ninaufahamu Kwa sehemu wema wake, Huko
nitamtazama Na kushiba kwa kuona.
3 Shangwe gani kwake Yesu! Shida zote zitaisha, Giza
haitakuwapo, Na huzuni itakoma.
4 Yesu atafika mbio, Lo! Mwenyewe atashuka! Tutanyakuliwa
juu Ili kumlaki Bwana.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
100. LO! BENDERA INATWEKWA
1 LO! Bendera inatwekwa, Yatutangulia! Tusione hofu, wenzi,
Twende kwa kushinda!
Bwana Yesu atakuja, Tuilinde ngome! Kwa uwezo
wake Yesu Tutashinda yote.
2 Ibilisi azunguka, Akitutafuta; Anataka tuanguke, Tufe,
tupotee.
3 Vita kubwa, vita kali Inaendelea, Tuwe watu wa ’hodari!
Twende, tutashinda!
4 Basi, kwa bendera yake Tunashikamana. Atutie nguvu yake
Hata kuja kwake!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
101. E’ MLINZI, TWAULIZA
1 E’ mlinzi, twauliza: “Yesu atakuja lini? Asubuhi ya Sayuni
Ni karibu? Tuambie!’’- ‘‘Msafiri, yainue Macho yako,
angalia! Asubuhi ni karibu, Usimame, usimame!’’
2 Siku heri ya sabato Ya milele ni karibu, Na dalili yake Yesu
Hapo itaonekana. Na rohoni tunaona Nchi nzuri ya ahadi.
Asubuhi ni karibu, Na ahadi zatimia.
3 Katika Yerusalemu, Mji mpya wa mbinguni, Yesu
atatumiliki Kwa upendo na amani. Baragumu italia, Nasi
tutaisikia. Yesu ni karibu sana Kutukaribisha kwake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
102. SAYUNI, ULAKI BWANAKO
1 SAYUNI, ulaki Bwanako, Umshangilie Mfalme! Jipambe
kwa Bwana arusi, Ujitengeneze tayari!
Furahi, furahi! Umshangilie Bwanako! Furahi,
furahi! Umsujudie Mfalme!
2 Kutoka ’tukufu wa Baba Na kiti cha enzi mbinguni Mwokozi
alitufikia Kulazwa mtoto horini.
3 Akawa dhabihu kamili, Akasulibiwa Golgotha, Akafa kwa
’jili ya wote, Tupewe wokovu wa Mungu.
4 Alitushindia mauti Na kumharibu Shetani; akaufunua
uzima, Tupate kuishi milele.
5 Afika kwa wenye huzuni Kuwapa faraja na heri, Na
atamiliki milele, Mfalme wa pendo na haki.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
103. SIKU KUBWA YA MASHANGILIO
1 SIKU kubwa ya mashangilio Inatufikia tena. Usikie neno
hili zuri: “Yesu amefika kwetu!”
Imba duniani pote pia, Imba, wote wasikie! Sifa
zina Mungu wetu juu, Na amani kwetu!
2 Utajiri, fedha na dhahabu Sina ya kukuletea, Ilakini roho
yangu tupu Nina’kutolea, Yesu.
3 Sisi sote tumsifu Mungu Kwa upendo wake kwetu!
Alitutumia Mkombozi, Mwana wake Yesu Kristo.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
104. LO! HORINI BETHLEHEMU
1 LO! Horini Bethlehemu, Ndani ’nyumba ya ng'ombe, Bwana
Yesu alilala Usingizi wa kitoto. Nyota zilizo mbinguni Kimya
ziliangazia Bwana Yesu, Mtulivu, Juu ya ulalo wake.
2 Wachungaji wa kondoo Walikuja kumwabudu, Na majusi
walifika Wakamtolea tunu. Mungu mwenye macho
Yanayotazama nchi yote, Alivunja makusudi Ya kuua ya
adui.
3 Nakupenda, Bwana Yesu, Kwani unaufahamu Udhaifu wa
mtoto, Hali yake ya kitoto. Nawe sasa unaweza Kunisaidia
sana Kila saa ya hatari, Majaribu na mashaka.
4 Nakuomba, Bwana Yesu, Unilinde njia yote, Uwe mwenzi
wangu mwema Kila saa na dakika! Usichoke nami kamwe,
Nami sitaona hofu; Yesu unikumbatie Siku zote na milele!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
105. WAKATI WA NOELI
1 WAKATI wa Noeli Nafika kwenye hori, :/: Alipolala Yesu,
Maskini, mtulivu. :/:
2 Mwokozi wangu mwema, Kwa pendo ulifika, :/: Nitoke
dhambi zangu, Nipate kuwa wako:/:
3 Nakuhitaji, Yesu, Rafiki wa watoto: :/:Sitaki kuumiza Kwa
dhambi Wewe tena. :/:
4 Nitashukuru Yesu Milele na milele. :/: Maana alifika
Kutuokoa sisi. :/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
106. TUIMBE ASUBUHI HII
1 TUIMBE asubuhi hii Juu ya siku manabii Walioitabiri! Ni
siku kubwa, siku nzuri, Upendo umedhihirika, Upendo wake
Mungu. Sisi sote tufurahi, Tumwimbie na kusifu Yesu,
Mkombozi wetu!
2 Yu sura yake Mungu Baba, Lakini mtu, ili sisi Tupate
kumjua. Yuaja na amani kwetu, Kuwatafuta wapotevu Na
kuwaponya wote. Sisi sote tuungane Naye Yesu na tupate
Pendo na uzima wake!
3 Ataliona sikitiko Na kufahamu shida yetu Asaidie sisi!
Atafundisha haki, kweli, Na kutufahamisha pendo Katika
kufa kwake, Sisi sote tuokoke, Na tufufuliwe naye, Mbingu
zitufunguliwe!
4 Aliye jua la neema Afika na wokovu kwetu, Na atuangazia.
Mchunga wetu yupo nasi, Anatutaka tuwe wake, Tumfuate
kweli! Sisi wake tumjue, Tuingie kwake juu, Tufanane naye
Yesu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
107. ALIPOTESWA YESU PEKE’
1 ALIPOTESWA Yesu peke’ Katika Gethsemane, Akakinywea
kwa upendo Kikombe cha uchungu.
Mwokozi wangu Alichukua yote, Uzima wake
ali’toa; Kutuokoa alitufilia.
2 Akasimama peke yake Kuchekwa na kupigwa, Kichwani
akatiwa taji Iliyo ya miiba.
3 Akachukua msalaba Njiani kwa Golgotha, Na akajeruhiwa
sana Kwa ’jili yetu sisi.
4 Na sasa, wewe mwenye dhambi, Tazama pendo lake! Neema
kubwa yakungoja, Uache dhambi zako!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
108. MWANA-KONDO’ WA MUNGU
1 MWANA-KONDO’ wa Mungu, Uli’filia sisi Juu ya msalaba
Kati’ macheko mengi. Umeondoa dhambi Na umeshinda
kufa. Utupe raha, Yesu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
109. YESU, UNIONYE TENA MSALABA WAKO!
1 YESU, unionye tena Msalaba wako! Huo ni kisima safi
Chenye kusafisha.
Msalaba wako, Yesu, Nausifu sana. Yesu, unilinde
huko Hata nikuone!
2 Huko niliona kwanza Ne’ma yako kubwa, Nuru ikafika
kwangu ’toka msalaba.
3 Yesu, unilinde huko, Unifahamishe Jinsi ulivyochukua
Dhambi zangu zote!
4 Unilinde siku zote Penye msalaba, Nikuone, nikupende Sasa
na milele!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
110. MWAMBA ULIOPASUKA
1 MWAMBA uliopasuka, Ndani yako nijifiche! Maji yale,
damu ile Itokayo mbavu zako, Iwe dawa ya kuponya Roho
yangu na ubaya!
2 Kazi za mikono yangu Haziwezi kukomboa. Hata ningelia
sana Na kutenda kazi nyingi Singeweza kuokoka, Peke yako
U Mwokozi.
3 Ndani yangu sina kitu, Naushika msalaba. Uchi mimi,
univike! Sina nguvu, ’nichukue! Ni mchafu, unioshe! Wewe
U Mwokozi wangu.
4 Kwa maisha yangu yote Hata nitatoa roho, Hata saa ya
kuitwa Mbele ya Mfalme wangu, Mwamba uliopasuka,
Nijifiche ndani yako!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
111. E’ YESU, SITAUSAHAU
1 E' YESU, sitausahau Uchungu wako ’kubwa, Ulipoteswa
Gethsemane Usiku peke yako.
Mateso uliyoyaona, Uchungu na machozi, Usiku
ule Gethsemane, Siyasahau kamwe.
2 Naona Wewe Gethsemane, Ulivyoteswa huko Kwa ’jili ya
makosa yangu, Na kuitoa damu.
3 Huzuni nyingi uliona Katika teso lako Ulipoachwa peke
yako Na wanafunzi wako.
4 Na ukiona roho yangu Haina pendo kwako, Uniongoze
Gethsemane, Nione teso lako!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
112. ULINDE ROHO NA NAFSI YANGU
1 ULINDE roho na nafsi yangu Chini ya damu, chini ya damu!
Makosa, hofu na shaka ziwe Chini ya damu yako!
Chini ya damu yako, Yesu, Ndani ya mto huo safi,
Unilinde kwa siku zote, Chini ya damu yako!
2 Makimbilio ya mwenye dhambi Chini ya damu, chini ya
damu, Ni ukombozi kwa watu wote Chini ya damu yako!
3 Nijaze nguvu na pendo lako Chini ya damu, chini ya damu,
Nipate tena kutii Wewe Chini ya damu yako!
4 Amani kubwa moyoni mwangu Chini ya damu, chini ya
damu, Karama zako zanipa raha Chini ya damu yako.
5 Nijazwe Roho Mtakatifu Chini ya damu, chini ya damu,
Daima niwe na moyo safi, Chini ya damu yako.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
113. MSALABANI MWOKOZI WANGU
1 MSALABANI Mwokozi wangu Alijitoa kuniokoa, Na damu
yake ilimwagika Kwa ’jili yangu, kunikomboa.
E’ Golgotha, E’ Golgotha, Alipoteswa Bwana Yesu!
E’ Golgotha, E’ Golgotha, Nilipopata raha kweli!
2 Na nchi ile ilitetema, Mbinguni jua likafunikwa Wakati Yesu
alipokufa, Akichukua hatia yangu.
3 Likapasuka pazia lote, Kwa hiyo Neno limetimizwa. Naona
njia ya mbingu wazi: Nikutakaswa kwa damu yake.
4 Mwokozi wangu, upendo gani: Uliutoa uzima wako!
Kunikomboa ulisikia Mateso yote ya msalaba.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
114. IMBA HABARI NJEMA
1 IMBA habari njema: Mungu apenda wote! Uihubiri damu,
Ituponyayo roho! Taja karama kubwa: Mwana alitujia,
Pasha habari hiyo Kwa kila mtu!
Yesu msalabani Alifilia wote, Alitupatanisha Na
Mungu, Baba yetu. Pazia la hekalu Likapasuka
huko, Njia imefunguka Kwa wewe, nami!
2 Uwaimbie wenye Shida na sikitiko Na wapigao vita Katika
majaribu! Imba katika miji, Pasha habari njema: Yesu
awatafuta Kwa pendo kubwa!
3 Imba katika giza, Halifikapo jua, Uwaimbie wote, Watu wa
kila hali! Imba mapema sana, Na adhuhuri pia, Sifu
Mwokozi hata Usiku waja!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
115. PENDO LA MUNGU NI KUBWA
1 PENDO la Mungu ni kubwa, Pasha habari hiyo! Pendo la
Mungu ni kubwa, Mwanzo wa nyimbo zote. Malaika
waliimba, Wachunga wakasikia. Tunafurahi kujua: Pendo la
Mungu ni kubwa.
Pendo kuu, Pendo kuu, Pendo kuu, Pendo la
Mungu ni kubwa!
2 Pendo la Mungu ni kubwa Kwako uliye mbali. Pendo la
Mungu ni kubwa, Anakuhurumia. Ukiendee kisima
Kinachotoka Golgotha, Utaupata uzima Katika pendo la
Mungu.
3 Pendo la Mungu ni kubwa, Latufikisha mbingu. Pendo la
Mungu ni kubwa, Tutafurahi sana! Huko hakuna jaribu
Wala ugonjwa na kufa. Tumeokoka sababu Pendo la Mungu
ni kubwa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
116. TUIMBIE, TUMSIFU YESU JU’ YA MSALABA
1 TUIMBIE, tumsifu Yesu ju’ ya msalaba! Aliteswa na akafa,
Yote kwa ajili yetu. Akashinda, ’kafufuka, Ni Mwokozi
’kamilifu.
2 Yesu alitukomboa, Na akawa haki yetu. Dhambi aliziondoa,
Akatupa tumaini: Tutarithi utukufu, Nuru, raha na uheri.
3 Yesu alipofufuka Akatushindia kufa, Akapewa nguvu zote
Duniani na mbinguni. Sisi sote tumepona Kwa kupigwa
kwake Yesu.
4 Tushukuru Mungu Baba Kwa ajili ya upendo! Tumsifu Yesu
Kristo Kwa neema yake kubwa! Tumfungulie moyo Kwake
Roho ’takatifu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
117. NILIPOFIKA GOLGOTHA
1 NILIPOFIKA Golgotha, Nikaiona huko Neema kubwa kama
mto, Neema ya ajabu.
Neema ya Golgotha Ni kama bahari kubwa,
Ne’ma tele na ya milele, Ne’ma ya kutosha!
2 Nilipofika moyo wangu Ulilemewa sana, Sikufahamu bado
vema Neema yake kubwa.
3 Nilipoona kwamba Yesu Alichukua dhambi, Neema
ikadhihirika, Na moyo ukapona.
4 Mbinguni nitakapofika, Furaha itakuwa Kuimba juu ya
neema Milele na milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
118. NI MWOKOZI MUZURI NINAYE
1 NI Mwokozi mzuri ninaye, Alikufa kuniokoa. Alitoa uzima
wake Kwa ajili ya watu wote.
Alikufa msalabani, Alikufa msalabani. Kwa ajili ya
dhambi zangu zote Alikufa msalabani.
2 Aliacha makao juu, Akafika ulimwenguni; Aliteswa kwa ’jili
yangu Na kunifungulia mbingu.
3 Dhambi zangu ali’chukua, Kujitwika huzuni yangu, Na
alijeruhiwa ili Aniponye na ’nipa raha.
4 Bwana Yesu alifufuka, Akarudi mbinguni kwake; Na yuaja
upesi tena Achukue walio wake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
119. TUIMBIE MSALABA WA MWOKOZI
1 TUIMBIE msalaba wa Mwokozi, Damu yake inatusafisha
sana! Tunaweza kuwa huru, kwani Yesu Alikufa ili
ku’ondoa dhambi.
Haleluya, anipenda! Haleluya, nafurahi! Haleluya,
siku moja Nitamwona Yesu!
2 Twafurahi, kwa neema yake kubwa, Alikuja ili tuwe na
uzima. Kama njia ni nyembamba duniani, Yesu atatupa
nguvu na ’hodari.
3 Tuuimbe moto ule ’takatifu Uli’tupwa na Mwokozi duniani!
Tuvipige vita vilivyo vizuri, Nasi tutapewa taji ya uzima!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
120. MSALABANI NILIMWONA YESU
1 MSALABANI nilimwona Yesu, Mwokozi wangu
aliyeniponya; Rohoni mwangu giza ikatoka, Ninafuata Yesu
sasa.
Nimeokoka kutoka dhambi, Na siku zote ninaimba
kwa furaha. Ni vita kali kushinda yote, Lakini
Yesu Yu karibu.
2 Mwokozi wangu ananipa nguvu, Nikiuona udhaifu huku. Na
vita yote itakapokwisha, Nitaipata raha kwake.
3 Mwokozi wangu, ninakufuata, Furaha yako inanituliza. Na
siku moja utakuja tena Kunichukua huko kwako.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
121. YESU NI FURAHA YANGU
1 YESU ni furaha yangu, Amejaa pendo kweli. Anaweza
kusimika Kila mwenye udhaifu. Ananipa ujasiri, Nguvu,
raha na faraja. Hata nikionja kufa, Yesu ni Mchunga
wangu.
2 Nimefungwa na Mwokozi Kwa kifungu cha upendo, Hata
kufa hakuwezi Kunitenga naye Yesu. Mimi wake siku zote,
Ninataka kumtii. Kwa neema nimepona, Nisitumikie
dhambi.
3 Kwa mikono ya upendo Ninakumbatiwa naye, Sitaweza
kutafsiri Pendo lake kubwa kwangu. Napokea nguvu yake,
Yanijaza moyo wangu. Yesu ananiongoza Katika safari
yangu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
122. MWOKOZI KAMILI NI YESU PEKEE
1 MWOKOZI kamili ni Yesu pekee, Mwokozi mzuri halisi.
Katika wokovu wa Mungu mkuu Ninalindwa naye kabisa.
Katika wokovu nalindwa salama, Naishi kwa
maji ya ’hai. Upendo wa Mungu unanizunguka
:/: Na kanihifadhi daima. :/:
2 Baraka ya mbingu inanijaliza Kwa Roho ya Utakatifu.
Nasifu Mwokozi katika furaha, Wokovu umenifikia.
3 Mwokozi mzuri ni Yesu pekee, Aniondoaye mizigo. Njiani
ananiongoza vizuri, Anipa na nguvu ya mwendo.
4 Nitakapomwona Mwokozi mbinguni Baada ya shida za
huku, Nitamhimidi na kumshukuru Bwanangu
ninayempenda.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
123. MWOKOZI MZURI NINAYE
1 MWOKOZI mzuri ninaye, Zamani sikumfahamu, Na sasa
ninamhubiri, Wengine wapate kuona.
Wote watamwona, Wote watamwona Mwokozi
mzuri ninaye; Lo! Wote watamwona.
2 Shetani akinizuia Nisimfuate Mwokozi, Najua Bwanangu
hodari Hutaka kunisaidia.
3 Apita wo wote kwa wema, Mfano ’tukufu wa Baba, Lakini
anitaja ndugu, Niliye maskini kabisa.
4 Natoa maisha na pendo Kwa Yesu aliyenipenda. Katika
ishara za Mungu Upendo wapita yo yote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
124. NAONA PENDO KUBWA MNO
1 NAONA pendo kubwa mno, Latoka kwa Mwokozi wangu, Ni
tele kama maji mengi Yatembeayo baharini. Lanitolea
tumaini Ya kwamba nitatiwa nguvu; Na niwe mhodari tena
Kwa pendo kubwa la Mwokozi!
Haleluya! Ni pendo kubwa Linalotoka moyo wako!
E’ Mungu wangu, nakuomba: Nijaze pendo lako
tele!
2 Na pendo hilo kubwa mno Huyaondoa majivuno, Na
kunifunza haki, kweli, Uongo wote niuvue! Hunituliza moyo
wangu, Huruma nayo hunitia. Na sote tuwe na umoja
Katika pendo la Mwokozi.
3 Nijazwe pendo hilo kubwa, Linibidishe siku zote! Rononi
niwe na juhudi Nitumikie Bwana Yesu! Hazina yako
’nipeleke Kwa watu waliopotea, Wafahamishwe pendo
kubwa Ulilo nalo, Mungu wangu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
125. HALELUYA! NAFURAHI
1 HALELUYA! Nafurahi, Ninaimba kila siku Sifa zake Mungu
wangu, Aliyeniweka huru. Haleluya! Bwana Yesu Aliniokoa
kweli! Haleluya! Mimi wake, Yeye ni Mwokozi wangu!
2 Heri! Niliyeokoka Kwa neema yake kubwa Ninataka
kumsifu Mungu na wokovu wake. Wakinung’unika wote,
Sitawafuata wao; Nitasifu Mungu wangu Siku zote na milele.
3 Kama ndege waimbavyo Asubuhi bustanini, Na sauti ya
mawingu Ivumavyo baharini, Hivyo nitamshukuru Bwana
wangu kwa furaha. Roho yangu itaimba: Haleluya! Sifu
Mungu!
4 Haleluya! Furahini Mbele yake Mungu wetu! Na watakatifu
wote, Mwimbieni jina lake! Malaika wote pia Msifuni Bwana
Mungu! Mbingu zote zitajibu: “Haleluya, Haleluya!”
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
126. E’ MTAKATIFU, MUNGU WA MAJESHI
1 E’ MTAKATIFU, Mungu wa majeshi, Leo asubuhi tunaimba
mbele yako! E’ Mtakatifu, Mungu wa rehema, Bwana
Mwenyezi, tunakuabudu!
2 E’ Mtakatifu, huko ju’ mbinguni, Lo! Wazee huzitupa taji
mbele zako. Jeshi la mbinguni wanakusujudu Uliye hai sasa
na milele.
3 E’ Mtakatifu! Mtu mwenye dhambi Hataweza kuuona
utukufu wako. Wewe tu ni mwema, tunakuheshimu, E’
mwenye nguvu, pendo na uwezo.
4 E' Mtakatifu, jina lako kubwa Lisifiwe hapa chini, juu na po
pote! Mungu wa neema, nguvu na uwezo, Mwenye baraka,
tunakushukuru!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
127. NIMEUONA MTO SAFI
1 NIMEUONA mto safi, Kisima cha ajabu, Ni damu yake Yesu
Kristo, Inayonitakasa.
Nimeuona mto safi Unioshao moyo wangu.
Namshukuru Mungu wangu, Aliniweka huru
kweli!
2 Kwa nia na dhamiri safi Naendelea mbele, Ninasafiri kwenda
mbingu Kuona raha yake.
3 Neema kubwa, nimeonja Uheri wa mbinguni, Maana damu
yake Yesu Imeniponya moyo!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
128. NINA RAFIKI MWEMA, NAYE ALINIFILIA
1 NINA Rafiki mwema, naye alinifilia; Alinivuta kwake na
amenifanya mpya. Ni mali yake Yesu tu, ninaongozwa naye,
Alikomboa mimi kwa agano la upendo.
2 Nina Rafiki mwema, na aliondoa dhambi, Aliniweka huru na
kunipa Roho yake. Na vitu vyote ninavyo ninavitoa kwake,
Maisha yangu ni yake tu, yaimba sifa zake.
3 Nina Rafiki mwema na anayeweza yote, Pamoja naye Yesu
tu nashinda majaribu, Atanitwaa kwake ju’ mbinguni kwa
furaha, Nitastarehe katika makao ya milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
129. NINATAKA KUMSIFU YESU KRISTO
1 NINATAKA kumsifu Yesu Kristo Aliyeondoa dhambi zangu
zote. Twende sote sasa tumsifu Yeye Na pendo kubwa la
Mwokozi!
Haleluya! Yu Mfalme ’kuu! Haleluya! Asifiwe!
Alinisamehe dhambi zote; Anilinda kwa salama!
2 Na baraka yake anaimimina, Kama mvua ikunyavyo juu
yangu. Nastarehe mikononi mwake Yesu, Rehema yake
inatosha.
3 Siku moja nitamwona Yesu Kristo Kati’ nchi nzuri sana ya
furaha, Macho yangu yatamtazama Yeye, Kuona sura ya
Mfalme.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
130. NINATAKA KUMSIFU YESU BWANA
1 NINATAKA kumsifu Yesu, Bwana wangu mwema. Aliteswa
hata kufa, Ili niwe huru kweli.
Mwimbieni Bwana Yesu kwa upendo wake ’kubwa!
Alilipa deni langu, Nimewekwa huru kweli.
2 Ninataka ’shuhudia Pendo kubwa la Mwokozi, Jinsi
alivyoniponya Nilipopotea mbali.
3 Ninasifu Mwokozi Kwa uwezo wake bora; Naye anitia nguvu
Nimshinde yule mwovu.
4 Ninataka kumwimbia Yesu Kristo, Bwana wangu. Aliniokoa
kweli, Niwe heri siku zote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
131. MIMI MKRISTO, NITA’VYOKUWA
1 MIMI mkristo, nita’vyokuwa Katika yote mpaka kufa. Mimi
mkristo, ’navyoshuhudu, Dunia yote ikinicheka. Mimi
mkristo kwa moyo wote Sababu ninampenda Kristo,
Aliyekufa kwa ’jili yangu, Anastahili kupendwa nami.
2 Mimi mkristo, neema kubwa! Niliokoka kutoka dhambi.
Mimi mkristo, hata ikiwa Katika shida na mapigano. Mimi
mkristo, na ni askari, Nafanya vita kushinda dhambi. Akida
wangu ni Bwana Yesu, Pamoja naye ’tashinda yote.
3 Mimi mkristo, na ni mgeni, Nimeifunga safari yangu; Na
sitamani yaliyo huku, Ninatafuta yaliyo juu. Mimi mkristo,
na nchi yangu Ni huku juu katika mbingu, Hamna njaa na
shida humo. Wakristo wote washiba mno.
4 Mimi mkristo! Ni neno zuri La kufariji moyoni mwangu,
Linanitwaa ju’ ya huzuni, Nipumzike kwa Mungu wangu;
Mkristo katika kila hali, Na nikiitwa na kufa tena, Kwa raha
kubwa nitakubali Kuchukuliwa mbinguni juu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
132. YESU MWOKOZI, UNANIPENDA
1 YESU Mwokozi, unanipenda, Na pendo lako ni kubwa
kabisa. Ulinivuta karibu nawe, Mimi ni wako daima
dawamu.
2 Yesu Mwokozi, unanipenda, Na pendo lako lapita akili.
Linanifunza kuzifahamu Raha, upole na utu adili.
3 Yesu Mwokozi, unanipenda, Mimi maskini, dhaifu,
mnyonge. Nimetakaswa kwa damu yako; Ninakuomba,
’nijaze upendo!
4 Yesu Mwokozi, unanipenda, Umenitilia wimbo kinywani Wa
kukusifu hata milele, Nitakuona halisi mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
133. UFURAHI, MOYO WANGU
1 UFURAHI, moyo wangu, Heri nyingi umepata! :/: Sikitiko
limekwisha, Yesu ni wangu nami wake. :/:
2 Ameponya roho yangu, Yeye ni mpozi mwema; :/: Na kwa
Roho ’takatifu Anabatiza watu wake. :/:
3 Jina langu ni mbinguni, Yesu ameliandika. :/: Mimi mali ya
Mwokozi Hata milele na milele.:/:
4 Na moyoni mwangu sasa Ninaimba: ‘‘Mungu, Baba!’’ :/:Ni
furaha kubwa sana, Nina rafiki kila saa. :/:
5 Nimeondolewa dhambi, Nisitende ovu tena! :/: Kwani Yesu
aokoa Kila wakati na dakita. :/:
6 Nyimbo za kusifu Mungu Zinajaa mbingu zote. :/: Moyo
wangu unajibu: ‘‘Amina. Mungu asifiwe’’ :/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
134. WATU WA MUNGU, MSHANGILIENI
1 WATU wa Mungu, mshangilieni kabisa, Na mwimbieni
Mfalme wa mbingu na nchi! Mungu Yu nasi Kwa pendo
kubwa, kamili Ili tupate wokovu.
2 Ona ajabu! Mwokozi aliyejidhili! Pendo kamili na neema
nyingi ya Mungu: Alizaliwa, Akawa Mwana Adamu,
Atukomboe na dhambi!
3 Sisi wakristo tumwimbie tena pamoja Yesu Mwokozi aliye
dhabihu ya kweli! Na atukuzwe Hapa na huko mbinguni,
Kwani alitufilia!
4 Yesu Mfalme, kwa pendo uliniokoa, Nikufuate, nikutumikie
daima! Huko mbinguni Nitakusifu milele Katika watakatifu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
135. SIFU BWANA, NINYI WATU WAKE
1 SIFU Bwana, ninyi watu wake wote Kwa neema yake juu
yenu! Yesu Kristo Yu karibu, atulinda Na ’ongoza njia yote.
Sifu Mungu! Sifu Mungu, Kwa sababu analinda
sisi sote! Sifu Mungu! Sifu Mungu Kwa ulinzi
wake mwema!
2 Yesu alikusamehe dhambi zote, Akuponya udhaifu wako;
Amekufariji, amefuta chozi, Na neema yakutosha.
3 Anakutilia afya, nguvu mpya, Akuvika vazi la kushinda.
Katika mapito yake waongozwa Na kulindwa kwa salama.
4 Kaa ndani yake Bwana Yesu Kristo, Haki yetu, utakaso
wetu, Na wokovu na hikima vilevile, Mkombozi ’timilifu.
5 Bwana Yesu atakuja siku moja, Atukaribishe wote kwake.
Tutamtukuza Yeye, Bwana wetu, Kwani alitukumboa.
Uje mbio! Uje mbio! Bwana Yesu, utukaribishe
kwako! Uje mbio! Uje mbio! Tunaomba wote: Uje!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
136. TUINUE MOYO TUKISIFU YEYE
1 TUINUE moyo tukisifu Yeye, Aliyechukua dhambi zetu!
Yesu, Mkombozi, asifiwe, Aliyetufia sisi!
Yesu! Tumwabudu Yeye! Yesu! Sifu jina lake!
Tuimbe kwa furaha Duniani pote! Tumsifu,
tumwabudu Yesu!
2 Malaika wote, msifuni Yesu! Nasi tushukuru Mkombozi!
Watu wote wasikie sasa Kwamba Mungu ni upendo!
3 Tushukuru Bwana Yesu, sisi sote, Tukumbuke pendo lake
kuu! Lisifiwe jina lake jema Siku zote na milele!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
137. NAFURAHI KWA SABABU KATI' DAMU
1 NAFURAHI kwa sababu Kati’ damu ya Yesu Moyo
umetakaswa, Nimepata amani.
Haleluya! Haleluya! Mkombozi asifiwe! Haleluya!
Haleluya! Haleluya! Amina!
2 Sina nguvu, ni dhaifu Bila Yesu Mwokozi, Ila kwa nguvu
zake Nasimama imara.
3 Moyo wangu, ufurahi, Mimi mtu wa Yesu! Nampenda daima
Na kumtumikia.
4 Pendo kubwa la Mwokozi Lanijaza rohoni. Nina raha kamili,
Moyo unastarehe.
5 Sifu Mungu, Baba yetu, Yesu Kristo Mwokozi, Roho
Mtakatifu! Haleluya, Amina!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
138. SASA TAYARI KWETU SIKU YA KUOKOKA
1 SASA tayari kwetu Siku ya kuokoka, Yesu alitimiza Yote
msalabani. Wengi wanamjia Yesu Mwokozi wao, Wapate
kustarehe, Wapone nafsi zao.
Mwana-Kondo’ wa Mungu Tunakusifu sana!
Uzima uliweka Kwa ’jili yetu sisi. Umetufanya
kuwa Mitume yake Mungu. Kati’ majina yote
Lako ni kubwa mno.
2 Wewe kwa damu yako Ulikomboa sisi, Na jua la neema
Linatuangazia. Tumefahamu sasa Pendo la Mungu wetu.
Damu imetuunga Kati’ agano jipya.
3 Njoo upesi nawe Uliyesitasita! Mungu atakujaza Neema yake
kubwa, Raha rohoni mwako Inayokutuliza, Matumaini,
nguvu, Pendo lililo bora.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
139. NINA FURAHA KUBWA, NAPUMZIKA
1 NINA furaha kubwa, Napumzika sana, Kwa kuwa nimefika
Kwa Mungu, Baba yangu. Ameniweka huru Na mbali na
utumwa, Na sasa nakaa salama.
2 Zamani nilidhani Kuacha dhambi zote, Lakini sikuweza
Kushinda peke yangu. Ninamwamini sasa Mwokozi wangu,
Yesu, Na yeye ananishindia.
3 Mwokozi wangu, Yesu, Aliyenifilia, Aliokoa mimi, Angali
anipenda; Nahesabiwa haki Katika damu yake, Inayosafisha
kabisa.
4 Na nikijaribiwa Na mwili wangu tena, Ninakumbuka Yesu,
Apita vitu vyote. Neema yake kubwa Kuliko dhambi zangu.
Ninamshukuru Mwokozi.
5 Na sasa Bwana Yesu Akaa ndani yangu, Neema yake kubwa
Yanizunguka mimi. Sitasumbuka tena, Nimejiweka kwake,
Na Mungu anilinda vema.
6 Shetani akitaka Kufanya vita sasa, Sitaogopa yeye Na
mamlaka yake. Maneno yake Mungu, Ni yenye nguvu sana
Kwa wote wanaoamini.
7 Ninaenenda sasa Kwa jina lake Yesu, Salama nitafika
Nyumbani mwa Babangu. Lakini safarini Naimba siku zote,
Nikimshukuru Mwokozi. NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
140. UKICHUKULIWA NA MASHAKA YAKO
1 UKICHUKULIWA na mashaka yako Na kuona hofu
kwamba utakwama, Uhesabu mibaraka yake Mungu, Na
utashangaa kwa rehema yake.
Uhesabu mibaraka yote Mungu aliyoyakubariki!
Ukumbuke mambo yote pia, Na utashangaa kwa
rehema yake!
2 Na ukiudhiwa na huzuni nyingi, Ukiona msalaba ni mzito,
Uhesabu mibaraka kuchwa pia, Na kwa moyo wote utasifu
Mungu.
3 Wengi watamani mali ya dunia; Utajiri wako ni Mwenyezi
Mungu. Uhesabu mibaraka na kumbuka: Mali haiwezi
kufungua mbingu.
4 Na katika mambo yote huku chini Ukumbuke pendo kubwa
la Mwokozi! Na ujumlishe mibaraka yote, Tena mwisho
atakuchukua kwake!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
141. MWOKOZI WETU ANATUPA FURAHA
1 MWOKOZI wetu anatupa Furaha duniani, Atuongoza kwa
neema Na anatushibisha. Tazama, Yupo pamoja nasi, Neema
haitaisha kamwe! Haleluya, Haleluya, Haleluya, Amina!
2 Ni vema kumpenda Mungu Aliyetukomboa, Vizuri kuwa mtu
wake, Sitapotea kamwe. Furaha yetu itabakia, Ikiwa vyote
vingetoweka. Haleluya, Haleluya, Haleluya, Amina!
3 Ikiwa giza mara nyingi, Na jua likifichwa, Na tukijaribiwa
huku, Twajuwa ni kwa muda. Mbinguni hatutaona kamwe
Huzuni wala machozi tena. Haleluya, Haleluya, Haleluya,
Amina!
4 Na tusisumbukie tena Chakula wala nyumba, Maana vyote
twavipata Kwa ne’ma yake Mungu. Njiani yote atuongoza,
Aichukuwa mizigo yetu. Haleluya, Haleluya, Haleluya,
Amina!
5 Ikiwa vema huku chini Kutegemea Yesu, Furaha gani huko
juu Kuona uso wake! Tutaiona furaha tele, Na utukufu
hautaisha, Haleluya, Haleluya, Haleluya, Amina!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
142. KWA NAMNA NYINGI NILITAFUTA
1 KWA namna nyingi nilitafuta Kupata raha moyoni
mwangu. Unyonge wangu haukukoma Ila kwa Bwana Yesu.
2 Na moyo wenye hatia nyingi Nilimwendea Mwokozi wangu,
Na alinipa wokovu wake Na nguvu ya kushinda.
3 Kwa pendo kubwa Mwokozi wangu Aliuweka uzima wake,
Si kitu mimi ulimwenguni, Nina wokovu kwake.
4 Ijapo ninachukiwa huku Ni mteule wa Bwana Yesu,
Napenda sasa kumfuata, Nifike kwake Mungu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
143. HERI HALISI, YESU NI WANGU
1 HERI halisi, Yesu ni wangu! Yeye Mchunga, mimi ni wake.
Heri yakini, yote ni heri, Roho na moyo zimeokoka.
Yesu ni wimbo na raha yangu, Nitamsifu hata
milele! Na nitamwona huko mbinguni. Yesu ni
wangu na mimi wake.
2 Nilijitoa kwa Bwana Yesu, Na nilipewa wokovu wake. Huko
mbinguni kuna furaha Juu ya mtu aliyetubu.
3 Sasa naweza kusifu Yesu, Na roho yangu inafurahi. Mimi si
kitu mbele ya Mungu, Bali ni heri. Namshukuru!
4 Nimebatizwa katika Roho, Shangwe ya mbingu imo rohoni.
Moto moyoni, pia kinywani, Nashuhudia pendo la Mungu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
144. SAWA NA KISIMA SAFI
1 SAWA na kisima safi, Chenye maji mengi, mema, Ni upendo
wa Mwokozi, Ukaao ndani yake.
Yesu amelifungua Lango zuri la mbinguni Ili
niingie humo Kwa neema yake kuu.
2 Kama ndege awindavyo Mara nyingi nili’umwa, Moyo
wangu ulilia, Yesu hakunifukuza.
3 Ni ajabu kubwa kweli, Alinisamehe yote! Juu ya rehema
yake Ninaimba kwa furaha.
4 Asubuhi ya uzima Nitafika mlangoni; Kwa ajili ya upendo
Nitapata kuingia.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
145. MUNGU WANGU MKUU WANIJAZA
1 MUNGU wangu mkuu, Wanijaza Mwenyewe, Na uzima u
katika Wewe. Nina raha moyoni Na amani halisi, Ninaishi
katika upendo.
2 Sasa ninakusifu Wewe, Yesu Mwokozi, Unakaa rohoni
daima. Kila ’nachohitaji Wanijaza kwa pendo. Wewe yote,
na mimi si kitu.
3 Jina lako ni “Pendo”, Kulijua hakika Kunafanya safari
nyepesi. Mimi mtu dhaifu, Ila kwako ni nguvu; Niongoze
katika safari!
4 Mbele ya uso wako Giza yote yatoka; Nuru inaangaa moyoni.
Yamepita ya kale, Sasa yote ni mapya. Ni maisha ya heri
ajabu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
146. KARIBU NA WENZANGU NILIPOTEA
1 KARIBU na wenzangu nilipotea njia, Rohoni mwangu njaa,
na sikuona raha, Lakini sasa Yesu ni Mchungaji wangu,
Naandamana naye siku zote.
2 Katika shamba lake nimefuata Yesu, Ninapajua anapolisha
kundi lake. Na penye maji hai napunzika sana, Naona raha
hapo siku zote.
3 Lakini Mchungaji apita vitu vyote, Uzima aliweka kwa ’jili
ya kondoo. Nikumbukapo Yesu, sioni kitu tena Cha
kupendeza ila Yeye, Bwana.
4 Naimba kwa furaha rohoni mwangu hivi: “Upendo wako,
Yesu, ninausifu sana!” Na jina lake Yesu ni kama manukato;
Ananilinda vema siku zote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
147. MWENYEZI MUNGU WA ZAMANI ZOTE
1 MWENYEZI Mungu wa zamani zote Ni kimbilio la vizazi
vyote. Katika vita anawashindia Na ku’okoa watu wake
wote.
Mfalme ’kubwa ndiye Mungu, Vitani anatushindia.
Kwa shangwe kubwa tumsifu Na tumwimbie
Mungu wetu!
2 Mwenyezi Mungu wa zamani zote Aliokoa watu utumwani,
Kwa njia kavu katika bahari Wakafikishwa ng’ambo kwa
salama.
3 Mwenyezi Mungu wa zamani zote Karmeli alishinda yule
Ba’li, Akasikia ombi la Eliya, ’katuma moto juu ya sadaka.
4 Mwenyezi Mungu wa zamani zote Akawa naye Daudi vitani;
Aki’tupia jiwe Goliati, Shujaa alikufa mara moja.
5 Mwenyezi Mungu wa zamani zote, Ushenzi wote utashindwa
naye. Atamseta yule mdanganyi, Shetani, chini ya miguu
yake.
6 Mwenyezi Mungu wa zamani zote Atuongoza kwa mikono
yake; Anatulinda hatarini huku, Mbinguni tutafika kwa
salama.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
148. NGUVU ILE ILISHUKA JU' YA WANAFUNZI
1 NGUVU ile ilishuka ju’ Ya wanafunzi wote Mjini mwa
Yerusalem’ Siku ya Pentekoste, Lo! Nguvu hiyo ya Mwokozi
Ni sawa leo; shukuru Mungu!
Karama, karama, karama yake Mungu Ni sawa
hata leo, ni sawa hata leo! Karama, karama,
karama yake Mungu Ni sawa hata leo!
2 Yesu aliwapa ahadi: “Mtapokea nguvu!’’ Na Roho akashuka
na Wakamsifu Mungu. Walio wenye udhaifu, Wakahubiri
kwa uthabiti.
3 Roho yule aingiapo Anatutia nguvu, Tupate kwa imani ku’
Kushinda yule mwovu. Kwa moyo wenye moto safi Tuite
watu kwa Mkombozi!
4 Uingie sasa rohoni, Uwashe moto wako, Tupate kusimama
kwa Usafi siku zote! Ufike sasa kama mbele Wakati huo wa
Pentekoste!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
149. UZIMA NINAO MOYONI DAIMA
1 UZIMA ninao moyoni daima, Uzima ni Yesu Mwokozi,
Aliyeingia rohoni hakika, Akanitilia ’hodari.
Nashiba rohoni kwa raha ya Mungu, Na moto wa
mbingu ulimo. Napata kukaa nuruni kabisa, Na
nuru ni Yesu Mwokozi.
2 Baraka zilizo katika wokovu Nilizozipata kwa bure,
Nilipoungama makosa na dhambi Kwa Yesu Mwokozi wa
wote.
3 Mwokozi aliniondoa porini; Natunzwa shambani mwa
Mungu. Na sasa kwa mvua na jua la mbingu Ninamzalia
matunda.
4 Naona maisha ni yenye maana: Ni ku’tumikia Mwokozi.
Kuishi ni Kristo na kufa faida Kwa kila mkristo wa kweli.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
150. NATAKA KUPOKEA BARAKA YAKE MUNGU
1 NATAKA kupokea baraka yake Mungu, Nataka kubatizwa
kwa Roho ’takatifu. Ju' ya ahadi yake napumzika sana,
Aliahidi mimi kupata Roho yake.
Sawa na bahari, sawa na bahari Ni neema yake
anileteayo. Anayenijaliza, Anayeniponyesha, Ni
Mwokozi wangu. Asifiwe sana!
2 Kanisa lake Mungu linaipata mvua, Vijito vya baraka
vinamiminwa sasa. Furaha ya uzima ni kubwa kati yetu.
Tuimbe haleluya! Tumshukuru Yesu!
3 Mawimbi ya wokovu yanatujia sasa. E’ Mungu, tunaomba:
Ujaze sisi sote! Watakatifu wako watakasike sana! Tuimbe
haleluya! Tumshukuru Yesu!
4 Mawimbi ya wokovu yaliyofika kwetu, E’ Mungu, uyatume
ulimwenguni mwote, Maelfu kati’ watu wapate kuokoka,
Waimbe haleluya, Wamshukuru Yesu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
151. MWOKOZI, MOTO SAFI, WAZI, TUNATAKA MOTO
1 MWOKOZI, moto safi, Tunataka moto wako juu yetu!
Twaomba kwako leo, Mungu: Washa moto ndani yetu,
washa moto! Tazama sisi hapa leo, Na tupe Roho yako,
Mungu! Tupate Pentekoste yetu! Tunangoja moto wako juu
yetu!
2 E’Mungu wetu, usikie, Tunaomba moto wako juu yetu!
Twadumu katika kuomba: Washa moto ndani yetu, washa
moto! Tunahitaji nguvu yako Ili tutakasike sana Na
kuyashinda majaribu. Tunangoja moto wako juu yetu.
3 Mioyo iliyo baridi Inataka moto wako juu yao. Hitaji zote
tutajazwa, Tukipata moto wako ndani yetu. Siwezi mimi
peke yangu Kushinda mambo ya Shetani, Lakini ninaomba,
Mungu: Washa moto ndani yangu, washa moto!
4 Naomba moto juu yangu Ili nihudumu huku kwa upendo;
Nauhitaji moto wako, Niwe na bidii nyingi na ’hodari. Ju’ ya
madh’bahu takatifu Nakuwekea moyo wangu, Mungu,
Washa moto, washa moto, washa moto!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
152. YESU ALIPOLALA KATI’ KABURI
1 YESU alipolala Kati’ kaburi, Giza ilifunika Yesu Mwokozi.
Alifufuka hakika, akavunja nguvu ya mauti,
Mshindaji ju’ ya mamlaka yote; Ni Mfalme wa
milele na milele, Alikuwa amekufa, Na tazama
amefufuka!
2 Walinzi wa kaburi Walikimbia, Muhuri na vifungo
Vilivunjika.
3 Kufa hakukushika Mawindo yake. Alilivunja pingo, Yesu
Mwokozi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
153. YESU KRISTO ALIFUFUKA
1 YESU Kristo alifufuka, Akatoka kaburini. Furahini na
msifuni, Kwani alishinda kufa!
Habari njema: Alifufuka katika wafu! Yesu Yu hai,
Naye atakuja tena.
2 Nguvu za mauti na dhambi Yesu Kristo ali’shinda; Nasi sote
tutashinda kwa Nguvu yake ya ajabu.
3 Kundi dogo, msiogope, Bwana Yesu ni Uzima! Aliziondoa
dhambi na Anawafariji moyo.
4 E’ wakristo, shangilieni, Yesu aliyefufuka Yu karibu,
atakuja na Atatufufua sote!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
154. E’ RAFIKI, SHAKA ZAKO ZIPELEKE KWAKE
1 E’ RAFIKI, shaka zako Zipeleke kwake Yesu!
Aliyemwamini Yeye Hataona haya kamwe.
Naamini, naamini, Ninakuamini, Yesu. Naamini,
naamini, Naamini Neno lako.
2 Dhambi zote ziungame Na kwa damu utakaswe, Akuvike
haki yake! Atakufikisha kwake.
3 Masumbuko yako yote Uyaweke mbele yake! Ukipita
uvulini, Bwana Yesu yupo nawe.
4 Na furaha yako pia Ijulike kwake Yesu, Yeye, Bwana ju’ ya
yote, Akubarikie yote!
5 Ujitoe kwake Yesu: Roho, mwili na akili! Vyote vya maisha
yako Anataka ku’takasa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
155. KATIKA MATUMAINI KWA MUNGU
1 KATIKA matumaini Kwa Mungu wangu Nakaa katika raha
Na utulivu. Na Yeye ni mwamba wangu, Imara sana; Katika
dhoruba zote Ananilinda.
2 Mwenyezi ni ngome yangu, Sitatetema; Siwezi kuhofu tena
Huzuni, shida. Ikiwa ni vita kali, Sitaogopa; Ni msaidizi
wangu Karibu nami.
3 Mahali pa kustarehe Kwa Yesu Kristo; Napata amani, raha,
Furaha kubwa. Faraja katika shida, Gizani nuru, Na katika
pepo nyingi Bandari nzuri.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
156. WALIAMINIO NENO LAKE MUNGU
1 WALIAMINIO Neno lake Mungu Watapata nguvu kuwa
washindaji, Kwani Bwana Yesu alituahidi Atathibitisha
Neno kwa ishara.
Shinda, shinda, nguvu ya kushinda! Shinda,
shinda, shinda kila saa! Mungu atatupa nguvu ya
kushinda, Tumtii Yesu, nasi tutashinda!
2 Kati’ vita kali Tuwe na ’hodari, Mungu ndie nguvu yetu ya
ajabu! Tu’amini Neno: Na ishara kubwa Zitafuatana na
waaminio.
3 Nguvu ya kupiga vita ya imani, Nguvu ya kupinga hila za
Shetani! Yesu amesema: Na ishara kubwa Zitafuatana na
waaminio.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
157. HAIDHURU KWANGU HUKU CHINI
1 HAIDHURU kwangu huku chini Utajiri au umaskini, Ila
Bwana Yesu awe nami; Ninatunzwa naye siku zote.
2 Haidhuru kama ninakuta Shida nyingi katika safari, Ila
Mchungaji wangu mwema Anilinde na kuniongoza.
3 Haidhuru kama tunakaa Katika baridi au hari, Kwa sababu
ukombozi wetu Unakaribia. Haleluya!
4 Haidhuru kama sitapata Utukufu na heshima huku;
Nikifanywa kama takataka, Yanipasa kupendeza Bwana!
5 Haidhuru kama njia yangu Inanichokeza mara nyingi, Basi,
nisigombe na wenzangu, Na pamoja tutashangilia!
6 Haidhuru kama tukiona Sisi si wakubwa huku chini. Tuwe
watumishi wake wema, Na tutaingia kwake Bwana!
7 Haidhuru kama twasafiri Katika dhoruba ya bahari, Kwani
Yesu ni nahodha wetu, Atatufikisha bandarini.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
158. HERI MTU ANAYE AMINI MUNGU BABA
1 HERI mtu anayeamini Mungu Baba na Yesu Mwokozi! Heri
mtu aifuataye Njia nzuri ’endayo mbinguni!
Usifiwe, Yesu Kristo! U Mwokozi mzuri kabisa!
Usifiwe, Yesu Kristo! Bwana, nitakuona mbinguni.
2 Kwa furaha tunakusanyika Kusikia Maneno ya Mungu, Na
mbinguni karibu ya Yesu Tutamshangilia daima.
3 Kuamini pasipo kuona Inafaa katika safari. Siku moja
atatuchukua, Tutakaa milele mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
159. NASIKIA BWANA YESU ANIITA
1 NASIKIA Bwana Yesu Aniita ku’fuata. Aliponitangulia
Nifuate Yeye njia yote!
Nifuate nyayo zake, Nifuate nyayo zake, Nifuate
nyayo zake, Nifuate Yeye njia yote!
2 Nifuate njia yote, Na kwa maji nibatizwe, Na kujazwa Roho
wake! Nifuate Yesu njia yote!
3 Nifuate, nihubiri Neno lake la uzima Kati’ watu wa dunia!
Nifuate Yesu njia yote!
4 Nifuate Bwana Yesu Katika mateso, kufa, Na nifufuliwe
naye! Nifuate Yesu njia yote!
5 Atanipa ne’ma yake Kwa kudumu hata mwisho, Hata
nitakapomwona Bwana Yesu huko ju’ mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
160. AHADI ZOTE ZA MUNGU WETU
1 AHADI zote za Mungu wetu Zinasimama hata milele.
Milima yote ikianguka, Ahadi hazipunguki.
Ahadi zake zinasimama, Hazipinduki hata milele.
Ikiwa nyota zingezimika, Ahadi zake zinadumu.
2 Ahadi zake zinasimama Katika shida, katika giza. Na
nikichoka kwa vita kali, Ahadi hazipunguki.
3 Ahadi zake zinasimama Katika homa, katika kufa.
Nafarijiwa na Baba yangu, Ahadi hazipunguki.
4 Ahadi zake zinasimama; Nitaamshwa katika kufa. Kwa
Baba nitapokea taji; Ahadi hazipunguki.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
161. UMESHIRIKIANA NAYE YESU
1 UMESHIRIKIANA naye Yesu Kama tawi ndani yake
mzabibu? Una raha iliyo timilifu, Umejazwa Roho yake
’takatifu?
Umeshirikiana naye Yesu Kama tawi ndani yake
mzabibu? Kuna raha na starehe Katika kuomba
Mungu; Akutia nguvu ya kushinda yote.
2 Umepata imani ishindayo Katika mashaka, shida huku
chini? Umepata neema ya kudumu Inayokulinda katika
hatari?
3 Kwake Yesu mahali pa amani, Huko ndiko pa kuburudika
sana; Atujaza mioyo utulivu, Tunakaa raha na mstarehe pia.
4 Twafurahi kwa wema wake wote, Twamsifu kwa ulinzi wake
pia. Hata tukiudhiwa huku chini, Atatufikisha kwake huko
juu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
162. BWANA YESU UWE NAMI
1 BWANA Yesu, uwe nami, Bila Wewe nina hofu, Unikaribie
sana, Uwe Kiongozi wangu!
Sitaona hofu tena, Yesu Kristo Yu karibu.
Ninataka kufuata Njia yako siko zote.
2 Bwana Yesu, uwe nami, Kwani mimi ni dhaifu; Na unifariji
moyo Kila siku ya huzuni!
3 Bwana Yesu, uwe nami Siku zote safarini, Zikiwako shida
huku Au raha na amani!
4 Bwana Yesu, uwe nami! Nahitaji nuru yako Hata nitafika
mbingu, Kao letu la milele!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
163. AHADI ZOTE ZA MUNGU ZINASIMAMA
1 AHADI zote za Mungu Zinasimama kweli, Na zilitiwa
muhuri Kwa damu yake Yesu.
Mbingu zikiondoka, Nchi ikitoweka, ’aminiye
’taona: Ahadi zinadumu.
2 Fanya kama Ibrahimu: Uangalie juu! Nyota ukizihesabu,
Imani itaota.
3 Katika giza njiani Tutaamini tu. Muda kitambo, na tena Jua
litaangaa.
4 Watu wakitusumbua, Tutaamini tu. Yesu atusaidia
Majaribuni pote.
5 Kama rafiki wakosa, Tutaamini tu. Yesu, Rafiki mkubwa,
Atabaki daima.
6 Katika mambo yo yote Tutaamini tu. Tutaviona mbinguni
Tulivyoviamini.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
164. ISRAELI WAKE MUNGU, KIMYA SANA
1 ISRAELI wake Mungu, kimya sana, Wa’zunguka Yeriko
kwa imani. Malaika wake aliwaongoza, Na waliendelea kwa
kushinda.
Twende kwa kushinda, twende kwa kushinda! Kwa
damu yake Yesu twende kwa kushinda! Tegemea
Mungu, anatuongoza, Na kwa imani twende kwa
kushinda!
2 Na Daudi, mchungaji, alikwenda Mbele yake Goliathi bila
woga; Kwa imani alitupa jiwe lake, Kwa jina lake Mungu
akashinda.
3 Danieli aliomba kila siku, Hakuhofu pango la simba kamwe;
Katika imani aliomba Mungu, Akaokoka katika hatari.
4 Hata safarini huku kwenda mbingu Nikipita katika jangwa
kavu, Na kupatwa na ’jaribu mbalimbali, Najua kwa imani
nitashinda.
5 Na imani inashinda hali zote, Inaruka juu ya mambo yote.
Niliye dhaifu sitahofu kamwe, Kwa kuwa Mungu ananiokoa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
165. NITAZAMAPO KWA IMANI MWOKOZI
1 NITAZAMAPO kwa imani Mwokozi wangu, nafurahi,
Naona utajiri wake Anao Mungu, Baba yangu. Haleluya!
Furaha kubwa, Aniongoza siku zote! Nikiuona udhaifu,
Anichukuwa mikononi.
2 Sitasumbuka mimi tena, Furaha inanijaliza; Na kwa upendo
na rehema Anisikia, nikiomba. Haleluya! Ananitunza,
Ninastarehe kwa salama. Na ukitaka raha yake, Mfungulie
moyo wako!
3 Nilipokaa kati’ dhambi Nikaliona sikitiko, Lakini shaka na
hukumu Zimeondoka kwangu sasa. Haleluya! Anipa nguvu
Ya kuyashinda majaribu. Rohoni mwangu nina raha,
Nalindwa nayo siku zote.
4 Dhihaka na mateso yote Si kitu kwangu kwa sababu
Nafarijiwa na Mwokozi, Nakumbatiwa na babangu.
Haleluya! Mwokozi wangu Ananitunza kwa neema. Nikiwa
na ’dhaifu tena, Natiwa nguvu kwa imani.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
166. TUKIENDA PAMOJA, KUSHIKANA
1 TUKIENDA pamoja, Kushikana na Mungu, Tunapata
amani na raha; Tukifanya daima Yanayompendeza, Yu
karibu kutusaidia.
Raha, furaha Twazipata kwa Yesu, Tukidumu
katika Kuamini, kutii.
2 Ikiwapo dhoruba, Na mawimbi ya’vuma, Yanakoma kwa
Neno la Yesu. Tukiona jaribu Na kuhofu adui, Tutashinda
kwa nguvu ya Yesu.
3 Tukibeba mizigo Anatustarehesha, Tunapata furaha halisi.
Masumbuko yatoka, Giza inageuka Kuwa nuru njiani mwa
Mungu.
4 Tuna raha ya Mungu Katika mashindano Tukitii na
tukiamini. Jua lake la pendo Linawaangazia Watiio na
waaminio.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
167. NINAJUA RAFIKI MWEMA, ANITUNZA
1 NINAJUA Rafiki mwema, Anitunza sana kila siku.
Ayaponya majeraha Na machozi ayafuta. Jina lake ni Yesu
Kristo.
Najua Rafiki mwema, Na Yeye ajaa ne’ma.
Nikiomba asikia, Afariji nikilia. Ndiye Yesu, na si
mwingine.
2 Nimepata Rafiki mwema, Afariji na kunipa raha.
Nikitegemea Yeye Sitahofu maadui; Na rafiki ni Yesu Kristo.
3 Nifikapo mtoni pale Paitwapo ‘‘kufa’’ na ‘‘mtego’’,
Sitafadhaika hapo, Yesu atakuwa nami; Ni Rafiki mkubwa
mno.
4 Pwani nzuri ya huko juu Nifikapo kwa neema kuu, Nitaimba
kwa kinubi, Nitasifu Yesu sana Kwa upendo na urafiki.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
168. NINA USHIRIKA NA FURAHA KUBWA
1 NINA ushirika na furaha kubwa, Namtegemea Bwana Yesu.
Wingi wa uheri kwa waaminio: Kustarehe mikononi mwake!
Raha, raha, raha kwa Yesu, na amani! Raha, raha,
Nastarehe mikononi mwake.
2 Raha ya ajabu ni rohoni mwangu, Namtegemea Bwana
Yesu. Nuru huangaza njia niendayo; Nastarehe mikononi
mwake.
3 Woga na huzuni zinatoka kwangu, Nikitegemea Bwana
Yesu. Ninafarijiwa siku zote naye, Nastarehe mikononi
mwake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
169. ASKARI WA IMANI SISI
1 ASKARI wa imani sisi, Kwa shangwe tunaendelea, Hata vita
’kiwa kali Tuna nguvu na ’hodari. Tuna upanga wa imani,
Ni neno lake Mungu wetu; Na kwa jina lake Yesu
Tunashangilia sasa.
Mbio tutaacha huku, Vita ikiisha. Tutaingiamo
mbingu Kustarehe humo. Wao washindao huku,
Watapewa taji Kwa mkono wa Mwokozi,
Anayewapenda.
2 Tuvae kila mtu sasa Silaha zote zake Mungu. Na mishale ya
Shetani ’tazimika mbele yetu. Tukimtii Bwana wetu,
Twaendelea kwa ’hodari, Na kwa nguvu za ahadi Tutakuwa
washindaji.
3 Na ukipungukiwa nguvu, Katika vita ukishindwa, Yesu
atakutilia Nguvu mpya ya kushinda. Kwa nyimbo za
kushangilia, Utahimili shida zote, Na kupata kuokoa Wenye
dhambi na makosa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
170. NIKIONA SHIDA HUKU KATIKA SAFARI
1 NIKIONA shida huku Katika safari, Yesu aninong’oneza
Neno la faraja. Ananipa raha tele Na furaha ya ajabu.
Ninaandamana naye Sasa na milele.
2 Tena njia ikienda Juu ya milima, Ninakaribia mbingu, Nuru
inang’aa. Na katika nuru hii Ninaona kwa uwazi Nchi ya
ahadi yake Na urithi wangu.
3 Kwa imani ninaimba, Hata hatarini, Njia ’kiwa ndefu huku,
Nitavumilia. Nyota za ahadi zake Zinang'aa kwa usiku,
Zinaniongoza vema Hata huko juu.
4 Kama Musa ali’ona Nchi ya ahadi, Kadhalika natazama
Nchi yangu juu; Ninaisalimu sasa Kwa uheri na imani.
Natamani kufikako, Kwa urithi wangu.
5 Vya hatari vikifika Kati’ njia tena, Yesu Yu pamoja nami,
Anichunga vema. Ninaendelea mbele, Na mbinguni nifikapo
Nyimbo nzuri nitaimba Na wakristo wote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
171. MWENYEZI MUNGU NGOME KUU
1 MWENYEZI Mungu ngome kuu, Silaha ya imara! Katika
shida na huzuni Twategemea Yeye. Mwovu akikaribia
Kututia woga, Akijithibitisha Kwa hila na jeuri,
Tusimwogope yeye!
2 Kwa nguvu yetu tu dhaifu, Na tungeshindwa hima, Ila
Mwenyezi Yupo nasi, Twaambatana naye. Ukitaka jina lake,
Ndilo Yesu Kristo; Aliye Mshindaji Na mwenye mamlaka,
Mfalme wa milele.
3 Dunia yote ikijaa Majeshi ya gizani, Tuliye naye Mungu
wetu, Hatutaona hofu. Mwovu amehukumiwa, Hana nguvu
tena Ya kutuangamiza Maungo wala robo; Ashindwa na
Mwenyezi.
4 Maneno yake Mungu wetu, Tushikamane nayo! Hatushindii
vya dunia, Vya juu twatafuta. Tu hodari siku zote, Hata
hatarini; Uzima twauweka Kutii Mungu wetu: Ufalme una
Yeye.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
172. SISI TU VIUNGO VYA MWILI 'MOJA
1 SISI tu viungo vya mwili ’moja, tunasaidiana. Utumishi
wetu tunaupenda na twasaidiana.
Twasaidiana sote, Twasaidiana sote. Twamaliza
kwa Shangilio na Kwa bidii kazi yetu.
2 Twafurahi kwa utumishi, hata tukiwa peke yetu; Walakini
heri zaidi kama tukisaidiana.
3 Ikiwezekana kwa mchwa ’dogo kujenga kisuguu, Sisi nasi
kwa nguvu yake Mungu tutamaliza kazi.
4 Na umoja wetu ni wa thamani, unapendeza Mungu;
Anatubariki kwa neema, anatupa tunu kubwa.
5 Twakuomba, Bwana, ’tuunganishe, tujaze pendo lako! Na
kwa Roho yako utubatize, tuhudumie Wewe!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
173. MAISHA KATIKA DUNIA
1 MAISHA katika dunia Ni kama kupanda na ’vuna:
Apandaye katika mwili Atavuna uharibifu; Tukitumikia
Mwokozi Tutapata thawabu mbinguni; Yafaa kuishi na kufa
Katika Maneno ya Mungu.
2 Kwa neema kubwa kabisa Tumekubaliwa na Mungu, Kwa
neema kubwa zaidi Twapata kumtumikia. Kuishi kwa ’jili
ya Yesu Kati’ yote ya dunia hii Na kuitangaza Injili Ni faida
kwetu kabisa.
3 Wakristo wata’poingia Mbinguni kusifu Mwokozi, Na mimi
nataka kufika Kuimba pamoja na wao. Tutamshukuru
Mwokozi aliyetununua kwa damu; Waliohudumu kwa pendo
Watamhimidi milele!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
174. PENDO KUBWA LA BABANGU LINANG'AA
1 PENDO kubwa la Babangu Linag’aa sikuzote, Walakini
anataka Sisi tuwe nuru huku!
Nuru yetu iangae Mbele ya wenzetu huku, Hata
mtu ’moja moja Aione njia njema!
2 Dhambi zimetia giza Huku chini duniani, Walakini watu
wengi Wanatazamia nuru.
3 Ndugu yangu, angalia, Taa yako iwe safi! Na kwa nuru
waokoe Wenzi waliopotea!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
175. SHAMBA LA MUNGU LIMEIVA
1 SHAMBA la Mungu limeiva, Li tayari sasa kuvunwa.
Wavunaji, mfike mbio Kuyavuna mavuno yake!
Bwana Yesu, twakuomba, Uwatume watenda kazi
Wakusanye miganda yote Kwako Yesu, Mwokozi
mwema!
2 Uwatume mapema sana, Na wengine kati’ mchana, Hata saa
ya magharibi Uwaite wavuni wako!
3 E’ mkristo, anakuita, Wende mbio, usichelewe! Macho yako
uyainue, Kwani Yesu aja upesi!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
176. MUNGU AKUTAKA KATI’ SHAMBA LAKE
1 MUNGU akutaka kati’ shamba lake, Nenda na wengine
kumtumikia! Ujitowe kweli kwake Mungu wetu! Uhubiri
Neno lake pande zote!
2 Ukumbuke Yesu, jinsi apendavyo! Anawatafuta waliopotea.
Uwapende nawe kwa upendo wake, Naye atakupa nguvu na
baraka!
3 Uliyemwamini, nenda mbio sana Kati’ shamba lake,
usingoje bure! Utumike vema, omba kwa bidii, Na thawabu
yako utaipokea!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
177. NIPE HABARI YA YESU, UIANDIKE ROHONI !
1 NIPE habari ya Yesu, Uiandike rohoni! Uniimbie zaburi Ya
kumsifu Mwokozi, Sifa iliyotangazwa Na malaika zamani:
Mungu wa ju’ atukuzwe, Iwe amani duniani!
Nipe habari ya Yesu, Uiandike rohoni! Uniimbie
zaburi Ya kumsifu Mwokozi!
2 Nipe habari ya Yesu, Jinsi alivyohimili Shida, jaribu na teso
Na umaskini na bezo! Maradhi zangu na dhambi
Aka’chukuwa mwenyewe, Kila wakati tayari Kusaidia
wahitaji.
3 Nipe habari ya Yesu, Ya msalaba na kufa, Taja kaburi
mwambani, Alipotoka Mwokozi! Pendo la Yesu ni kubwa,
Aliyekufa Golgotha, Akafufuka hakika, Namshukuru siku
zote!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
178. YESU KUTOKA MBINGUNI ALIINGIA
1 YESU kutoka mbinguni Aliingia huku Nchi ya giza na
dhambi, Ili atuokoe.
Nenda, nenda! Fanya mapenzi ya Yesu! Omba
kupata sehemu Kati’ mavuno makubwa!
2 Wanapotea gizani Wengi wa ndugu zako. Nenda kapashe
habari: “Leo wokovu uko!”
3 Nenda kawahubirie Watu wa mataifa Neno la Yesu
Mwokozi! Anakuita leo.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
179. SIKU MOJA MAVUNO YATAISHA KABISA
1 SIKU moja mavuno Yataisha kabisa, Baada ya hayo
hukumu. Jua litazimika Siku hiyo ya mwisho, Na hutasikia
injili.
Atakusanya ngano Kwa furaha ghalani, Bali
makapi yote Yatatupwa motoni. Rafiki, utakuwa
wapi?
2 Mahubiri na nyimbo Za wokovu wa Mungu
Zitakaponyamaza huku, Uliyelikataa Neno zuri la Mungu,
Utakaa wapi milele?
3 Watu wote wa Mungu Wafikapo mbinguni Kukaa pamoja
na Yesu, Wataimba kabisa Kwa sauti ya nguvu
Kumshangilia Mwokozi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
180. BWANA YESU ANATUULIZA
1 BWANA Yesu anatuuliza: “Nimtume nani mavunoni? Watu
wenye dhambi wapotea; Watolee Neno la neema!”
‘‘Mungu wangu, sema nami! Uniguze sasa kwa
makaa! Mungu wangu, sema nami! Mimi hapa,
unitume sasa!"
2 Mtumishi wake Bwana Mungu Alisema: ‘‘Mimi sistahili.’’
Aliposikia moto safi, Akasema: ‘‘Unitume mimi!’’
3 Mataifa mengi wanakufa, Hawajui Yesu na wokovu.Twende
kwao mbio, tuhubiri Neno la wokovu wake Yesu!
4 Siku za mavuno zitapita, Watumishi watarudi kwao. Bwana
wao atawapokea Na kusema: “Ulifanya vema!”
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
181. TUTAZAME KULE MBELE
1 TUTAZAME kule mbele, Asubuhi inakuja! Tuamini Mungu
wetu, Atafanya kazi yake, Kufukuza mashetani, Kumiliki
nchi yote. Tutashinda tukiomba, Mungu anatusikia.
2 Tarumbeta linalia, Tuamke sote sasa! Mungu wetu anataka
Sisi sote tutakaswe! Kila mtu awe safi Katika kanisa lake!
Uliache nung’uniko, Utapata nguvu yake!
3 Imba ninyi, watu wake, Bwana Yu pamoja nasi! Tutashinda
majaribu Kwa uwezo wake Yesu. Twende tumhudumie Kwa
kumpa mali yetu; Hata roho na akili Zimtumikie Bwana!
4 Watu wengi hawajui Njia yakufika mbingu, Wanakuwa
wamefungwa Kwa mikono ya Shetani. Twende
tukawatafute, Tuwavute kwa Mwokozi, Na kuomba na
kukesha Hata kuja kwake Yesu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
182. KISA CHA KALE NIPE HABARI
1 KISA cha kale nipe, Habari ya mbinguni, Ya Bwana
Mtukufu, Ya pendo lake Yesu! Niambie Neno lake, Nipate
kusikia, Mnyonge mimi huku, Mjinga, mkosaji.
Kisa cha kale nipe, Kisa cha kale nipe, Kisa cha
kale nipe, Cha pendo lake Yesu!
2 Sema kwa taratibu Nipate kuelewa Habari ya wokovu Na
damu ya Mwokozi! Simulia mara nyingi, Nisije kasahau,
Niikumbuke tena Maisha yangu yote!
3 Taja habari hiyo Kwa wema na kwa pendo, Mwokozi alikufa
Kutukomboa sote. Na ikiwa unataka Kunifariji mimi,
Nisimulie ile habari ya zamani!
4 Nipe habari hiyo Ikiwa waniona Ninaipendelea Fahari ya
dunia! Siku nitakapokufa ’tapenda kusikia Habari ya
zamani: Mponyi mwema Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
183. PANDA MBEGU NJEMA ANZA ASUBUHI
1 PANDA mbegu njema, anza asubuhi, Na uwaokoe watu wa
Shetani! Kwa wakati wake vuno litaiva, Chumo utapata kwa
furaha kuu.
:/: Twende tukavune, twende tukavune, Kwa
furaha kubwa twende tukavune! :/:
2 Panda mbegu njema juu ya milima! Na tuendelee hata
mabondeni! Neno lake Mungu litawafungua Watu wa gizani,
kwa furaha kuu.
3 Panda mbegu njema hata kwa machozi, Ukumbuke Yesu,
leo uhubiri! Bwana wetu, Yesu, atakuja tena Na thawabu
yetu kwa furaha kuu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
184. NITAKWENDA MAHALI PA GIZA
1 NITAKWENDA mahali pa giza na dhambi Kuhubiri Injili ya
nuru, Ili watu wasiosikia habari Wafahamu upendo wa
Yesu.
Nitakwenda mahali pa giza na dhambi, Hata wote
wapate kuona wokovu.
2 Akitaka niende kwa watu wagumu Na kuacha rafiki na
ndugu, Hata wakinitaja: ‘‘’pumbavu’’ na ‘‘bure’’, Nachagua
mapenzi ya Yesu.
3 Uliyezipoteza dakika na saa Kwa tamaa ya mambo ya huku,
Uamke na uwaokoe wenzako, Hata wasipotee kwa dhambi!
4 Watu wengi wangali watumwa gizani, Wanangoja kupata
uhuru. Yesu ananituma, Niende upesi Kuhubiri maneno ya
nuru.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
185. NEEMA KUBWA YA MUNGU WETU
1 NEEMA kubwa ya Mungu wetu: Alikutuma kwa kazi yake
Kwenda kuzipanda mbegu njema Katika roho za wenzako!
Nenda, E’ mvunaji, Nenda, E’ mvunaji! Nenda
kapande mbegu njema, Nenda, E’ mvunaji!
2 Njia ikionekana ndefu, Neno la Mungu ni aminifu: ‘‘Kwa
macho yangu nakuongoza, Jangwani nitafanya njia.’’
3 Ikiwa ndugu hawakuoni, Mtumikie Mwokozi vema! Bwana
anayetazama wewe, Anampenda mwaminifu.
4 Hata ukiwa mdogo sana, Nenda upesi shambani mwake,
Labda utaliokota suke Lililoachwa na wenzako.
5 Neno na nyimbo hazitatosha Kuwaamsha wafanya dhambi,
Bali mwenendo ulio safi Utawavuta ndugu zako.
6 Na usichoke kupanda mbegu Katika pendo na tumaini!
Ukizipanda kwa shida nyingi, Kwa shangwe kubwa utavuna!
7 Siku za kazi zita’pokwisha Tutahamia mbinguni juu;
Tutawaona wenzetu wote Tuliovuta kwa Mwokozi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
186. FANYIA MUNGU KAZI, MBIO USIKU
1 FANYIA Mungu kazi, Mbio usiku waja! Mtumikie Mungu
Siku zako zote! Anza mapema sana, Dumu mchana kutwa!
Mbio usiku waja, Kazi itakwisha.
2 Fanyia Mungu kazi Kama kungali jua, Usipoteze bure Siku
zako huku! Uyatimize yote Bila kukosa neno! Mbio usiku
waja, Kazi itakwisha.
3 Fanyia Mungu kazi, Saa yapita mbio! Fanya bidii sana
Kuokoa ndugu! Mtumikie Mungu Kwa nguvu yako yote!
Mbio usiku waja, Kazi itakwisha.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
187. TU WAVUNAJI WAKE MUNGU
1 Tu wavunaji wake Mungu, Kwa neno lake tunakwenda
Kuvuna ngano zake Yesu alizojinunulia. Kwa shangwe
tunaliingiza mwake vuno lake. Tunamsifu Yesu aliyekomboa
vuno lake.
Twende kati’ shamba lake, Bwana a’tuita! Vuno
linaiva sana, Usikie mwito! Siku zetu za mavuno
Zinatupitia mbio. Siku zetu, Siku zetu Zinabaki
chache.
2 Tu wavunaji, twende sasa Tukalivune vuno lake, Na kwa
bidii na imani tukusanye ngano ghali! Katika pendo kubwa
mno Anawataka wote, Yesu, Na tukiacha suke dogo ataona
mara moja.
3 Wakati wetu ni mfupi, A’ita tena, twende mbio! Atujalize
uhodari, nguvu ya kuvumilia! Usichelewe bure sasa,
Watenda kazi ni wachache! E’ mvunaji wake Yesu, utumike
kwa bidii!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
188. WENGI WAKASEMA: “BADO”
1 WENGI wakasema: “Bado”, Walipoitwa na Mwokozi,
Lakini tena wakaona Wamechelewa kuokoka.
Njoo mbio, njoo mbio, Yesu akuita leo! Njoo mbio,
njoo mbio, Usichelewe, ndugu yangu!
2 Nawe usemaye: “Bado”, Unapoitwa naye sasa, Rafiki, labda
utakuta Mlango umekwisha fungwa.
3 “Bado leo”, alisema Kijana ’moja kwa ujinga. Usiku alikufa
mara, Na akaenda hukumuni.
4 “Bado leo”, wamwambia Rafiki yako bora, Yesu. Ataondoka
kwa huzuni, Utafanyaje bila Yeye?
5 “Bado leo”, ukumbuke Ni neno la hatari kwako! Waweza
kupotea pia, Kukosa kuingia mbingu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
189. UNIHUBIRI HABARI NJEMA
1 UNIHUBIRI habari njema, Neno la ukombozi, Hata ikiwa
siufahamu Wingi wa neema! Nilipokuwa katika giza, Ndipo
Mwokozi alinijia, Na akanipa wokovu, Raha na tumaini.
Mimi kipofu, naona sasa, Anasikia maombi yangu,
Naye hatanisahau, Kwani ananipenda.
2 Amefungua mkono wake, Kuna wokovu humo; Ukilemewa
moyoni mwako, Uje kwake Yesu! Uliyechoka kwa dhambi
zako, Umtazame Mwokozi wako, Na utapata wokovu, Njoo,
anakupenda.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
190. KISIMA CHA LEHI KINGALI
1 KISIMA cha Lehi kingali Kwa kila aliye na kiu. Kinatoa
maji mazima Yaliyo ya kuburudisha.
Kisima chema Cha maji safi Hakikauki hata
milele. Ni heri yangu, Napumzika, Na roho
yangu inatulia.
2 Ulie na kiu rohoni, Ukinyong’onyea njiani, Tazama kisima
jangwani Kilicho na afya, uzima!
3 Mtungi ukiwa mtupu, Ukipungukiwa imani, Ufike kisima
cha maji Yabubujikayo daima!
4 Na penye kisima cha Lehi Upange na kupumzika! Uketi
kivulini mwake, Na moyo utaburudishwa!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
191. YAPIGWA HODI KWANGU, MGENI
1 YAPIGWA hodi kwangu, mgeni a’fika, Akiniomba:
‘‘Nifungulie! Umande umeshuka kichwani usiku, Na nywele
zangu zimelowa maji.’’
2 A! Huyu si mgeni, ni Yesu Mwokozi, Sauti yake nzuri na’jua.
Ninamfungulia, naona ni Yesu; Na siku hiyo sitaisahau.
3 Anong’oneza sasa rohoni: ‘‘U wangu’’, Karibu naye
ninatulia. Ananitia nguvu, baraka ya mbingu; Daima
nitakaa kwake Yesu.
4 Ni kweli, mimi ni wa Mwokozi milele, Amenitaja: ‘‘Ndugu,
mpenzi.’’ Ananikarimia hazina za mbingu, Ninaingoja siku
ya arusi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
192. SAUTI MOJA ILINIULIZA
1 SAUTI moja iliniuliza: ‘‘Wajua nilikufanyia nini? :/: Kwa
’jili yako niliteswa sana; Ufike kwangu, kwani nakupenda!’’
:/:
2 ‘‘Nilipokuwa huku duniani Wakanitia taji ya miiba, :/: Na
sikupambwa fedha na dhahabu, Lakini majeraha na
uchungu.’’:/:
3 ‘‘Golgotha nilifika siku moja, Na nilikufa ju’ ya msalaba. :/:
Tazama, katika mikono yangu Nimekuchora, E’ mtoto
wangu.’’:/:
4 Heleluya, rohoni ninaimba! Nimejiweka mikononi mwake.
:/: Na Yesu ananiongoza sasa, Nifike nchi nzuri huko juu. :/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
193. NI NENO ZURI LA ’AMINIWA
1 NI neno zuri la ’aminiwa, Listahililo kukubaliwa, Ya
kwamba Yesu alitujia Awaokoe wenye makosa.
2 Wa kwanza mimi wa wenye dhambi, Lakini ninafurahi sasa
Sababu Yesu, Mwokozi wangu, Aliniosha kwa damu yake.
3 Mwokozi wetu Yu nasi hapa, Atenda kazi kwa nia yake;
Awasha moto rohoni mwetu, Uwezo gani utampinga?
4 Viziwi wanasikia sasa, Viwete wanatembea sawa, Wenye
ukoma watakasika, Injili yake yahubiriwa.
5 E’ Bwana Yesu, tupulizie, Tujaze Roho Mtakatifu!
Uwaamshe waliokufa Katika dhambi, uwaangaze!
6 Fungua mbingu, unyeshe mvua Panapo kiu na jangwa tupu!
Uligeuze, likachanue Na kufurahi kwa shangwe kuu!
7 Na mataifa wakusujudu Mahali pa miguuni pako! Amina.
Wako ni utukufu Na sifa zote! Haleluya!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
194. USIKIE BWAN YESU ANAYEKUITA LEO
1 USIKIE Bwana Yesu Anayekuita leo! Aliteswa, alikufa Kwa
ajili yako wewe.
Usikie Bwana Yesu! Anabisha mlangoni.
Umfungulie moyo, Umkaribishe sasa!
2 Siku zote ulicheza, Kupendeza mwili wako; Ulimsahau Yesu,
Naye alikufilia.
3 Unasema: “Nitakuja Kusikia Neno lake”. E’ rafiki,
ukumbuke, Unaweza kufa leo!
4 Yesu akuita leo Kwa neema na upendo. Leo siku ya wokovu,
Umfungulie moyo!
5 Tunampa Bwana Yesu Moyo na wakati wetu. Yeye ni
Mfalme wetu Wa milele na milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
195. TUNASIKIA LEO HABARI, INAWAITA WATU
1 TUNASIKIA leo habari, Inawaita watu wafike; Watu wa
hapa, watu wa mbali, Wote wapate sasa wokovu!
2 Mtu wa dhambi, uje upesi, Yesu angoja kukuokoa! Tena kwa
nini unachelewa? Leo ni siku ya kuokoka.
3 Ulikimbia Yesu Mwokozi Aliyekukomboa kwa damu.
Usikimbie mbali zaidi, Ila urudi, uje upesi!
4 Katika dhambi hutaiona Raha halisi, hata kidogo. Yesu
mwenyewe atakujaza Raha ya kweli ndani ya roho.
5 Mtu wa heri katika shida, Katika mambo yote ya huku, Ni
hali ya mkristo wa kweli, Mtu wa heri hata milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
196. USIYEFANYA BIDII KABISA
1 USIYEFANYA bidii kabisa, Hutaingia mbinguni. Uikinge
roho kwa Neno la Mungu, Usipotee milele! Njia ni
nyembamba na mlango ’dogo, Ujitahidishe kuingia humo!
Ukubali leo wokovu wa Mungu Ili ufike mbinguni!
2 Vizuio vingi katika safari, Mwovu anakujaribu. Uvishinde
vyote vinavyozuia, Vyote katika dunia! Usimfuate kila
aitaye, Ungeweza kupoteza roho yako! Bwana Yesu
anakupenda daima; Ujitahidi kabisa!
3 Pasipo imani huwezi kufika Hata bandari salama Wala
kuingia katika uzima; Hilo ni Neno la Mungu. Kwa imani
tupu utaokolewa, Usikie sasa Neno la wokovu! Tubu dhambi
zako, amini Mwokozi; Hiyo ni njia, hakika.
4 Mungu anaita, wo wote wafike, Waupokee uzima! Atakupa
nawe hazina ya mbingu, Ukitafuta kwa kweli. Mungu Baba
anapenda roho yako, Yesu anataka kuokoa wewe, Roho
’takatifu anakuamsha. Ukiitika u heri!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
197. HAPO NILIPOKUWA DHAMBINI
1 HAPO nilipokuwa dhambini, niliumwa katika roho. Sasa
ninafurahi kwa shangwe Kwani Yesu ameniponya.
Ndiyo kazi kubwa ya ajabu: Mwokozi aliniokoa!
Naye anapenda watu wote, Atakuokoa wewe.
2 Dhambi zote nilizozitenda Zimefutwa na Bwana Yesu.
Sikitiko kwa ’jili ya dhambi Zilikoma nilipotubu.
3 Sasa mimi sitaki kurudi, Nachukia kabisa dhambi. Nimeonja
furaha ya Mungu Na amani na raha yake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
198. E’ MTU MWENYE KIU, UFIKE KWAKE
1 E’ MTU mwenye kiu, Ufike kwake Yesu, :/: Upate maji ya
uzima, Hutaona kiu kamwe! :/:
Njoo kwa Yesu, Uyanywe maji hai! Ufike, na
utapewa Uzima na uhodari!
2 Tazama, ndugu wengi Zamani wamekunywa! :/: Na heri
kubwa, maji hayo Hayatakauka kamwe! :/:
3 Na kunywa wewe tena, Upate nguvu sana! :/: Tumia katika
shindano Upanga wa Neno lake! :/:
4 Na mwendo wa imani Uta’poumaliza, :/: Utayakunywa maji
bora Kwa Mungu mbinguni juu. :/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
199. NJONI WOTE MTESWAO!
1 NJONI wote mteswao! Wote wenye sikitiko Kwa ajili ya
makosa, Mje sasa kwa Mwokozi! Kwake mtaona raha,
Utulivu na amani. Matulizo mioyoni Mtapata kwake Yesu.
2 Hataacha sikitiko Kulemea moyo wako; Yesu ni Mchunga
mwema, Akuficha mazizini. Pendo lake lina nguvu,
Huchukua masumbuko, Hufariji roho yako, Hukutwaa
kwake Mungu.
3 Yesu kama nyota nzuri Ing’aayo asubuhi, Mtu amfuataye
Ataona njia wazi. Hata nyota za mbinguni Zikiteketea zote,
Nyota hiyo ya milele Haitazimika kamwe.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
200. NJONI WOTE, MLE, MNYWE
1 “NJONI wote, mle, mnywe!” Yesu anasema hivyo. “Nimetoa
mwili wangu Kwa ajili yenu ninyi.” Kila mtu mwenye njaa
Aje na apate kula! Na aliye na makosa Atasamehewa yote.
2 Ninakuja kwako, Yesu, Unithibitishe moyo! Uliona
umaskini, Niwe mwenye utajiri. Nishibishe mema yako Na
karama takatifu! Unijaze Roho yako Kama ulivyoahidi!
3 Yesu, ninakuja kwako Niungane nawe, Bwana! Mimi
mwenye udhaifu, Nakutegemea Wewe. Na kwa damu yako,
Yesu, ninatakasika sasa. Nashiriki mwili wako Katika agano
jipya.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
201. NJOO, MWENYE HUZUNI NYINGI
1 NJOO, mwenye huzuni nyingi! Yesu anakungoja. Uje, atoe
mzigo wako, Ata’okoa wewe!
Njoo, uliye na huzuni! Njoo kwa Mungu wa neema!
Roho ya Mungu anakuita, Yesu anakungoja.
2 Njoo, mwenye makosa mengi! Yesu anakungoja. Kwake
neema na pendo tele! Ata’okoa wewe.
3 Njoo, leo uache dhambi! Yesu anakungoja. Ukilemewa
moyoni mwako, Uje kwa Yesu mbio!
4 Njoo, sasa, E’ mwenye dhambi! Yesu anakungoja. Na
ukitaka kumfuata, Ata’okoa wewe.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
202. NJOO KWA YESU MWOKOZI
1 NJOO kwa Yesu Mwokozi, Unayeteswa rohoni! Damu
iliyomwagika Itakuosha kabisa.
Njoo kwa Yesu Mwokozi, Naye atakuokoa!
Ulimwenguni ni dhiki, Kwake ni raha halisi.
2 Mbona kukawa dhambini Bila uzima wa Mungu? Uje upesi
kwa Yesu ili upate amani!
3 Saa zapita upesi, Hazitarudi kabisa. Bado kidogo na tena
Utapelekwa kuzimu.
4 Yesu atamchukua Bibi-arusi mbinguni, Na tutaimba milele
Sifa za Mwana-Kondoo.
Huko karibu na Yesu, Mbali ya mambo ya nchi,
Huru na heri rohoni Nitafurahi milele!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
203. HATUA MOJA KATI YA WEWE NA MWOKOZI
1 HATUA moja kati Ya wewe na Mwokozi. Wakawilia nini?
Ufike kwake leo!
Hatua moja, hatua moja, Njoo, akungoja! Njoo
kutubu dhambi, Atasamehe zote! Usikatae tena
Wokovu wake Mungu!
2 Hatua moja mbele, Anakungoja sasa. Amini Neno lake, Na
utapata raha!
3 Hatua moja mbele, Uzima uta’ona. Siku si nyingi huku,
’jitoe kwake Mungu!
4 Hatua moja mbele, Kwa nini kukawia? Omba: E’ Bwana
Yesu, Unipokee sasa!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
204. PENDO LA MWOKOZI KUBWA MNO!
1 PENDO la Mwokozi kubwa mno! Yesu akuita, Ufike kwake
sasa!
Akungoja, ’kubishia, ufungue! Akungoja, ’kubishia,
ufungue!
2 Amengoja wewe siku nyingi, Analia sana Juu ya dhambi
zako.
3 Kwa huruma nyingi akuita. ’geukie Mungu, Anakungoja
sasa!
4 Yesu atakupa raha kubwa Na uzima tele Ulio wa milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
205. YESU MWOKOZI AITA KWA PENDO
1 YESU Mwokozi aita kwa pendo Mimi na wewe na wote, Na
Yu tayari kukukaribisha Wewe uliye dhambini.
Urudi, urudi, Sasa urudi kwa Yesu! Anakuita na
anakungoja. Leo urudi kwa Yesu!
2 Mbona kukawa anapokuita? Anakungoja, ufike! Kuna
nafasi karibu na Yesu; Njia ni wazi kwa wote.
3 Nyakati zetu zapita upesi, Hazitarudi kabisa. Njoo kwa Yesu,
upate amani, Leo ungali mzima!
4 Ona upendo mkubwa wa Yesu, Unaenea kwa wote! Na kwa
neema anatukumbuka Wewe na mimi na wote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
206. RAFIKI YANGU TAZAMA
1 RAFIKI yangu, tazama, Wapita njia ya wapi! Milele, je?
utakaa wapi Ukikataa Mungu?
Ujiandae sasa, Utakutana na Mungu! Lazima uwe
tayari kwa Sababu utamwona!
2 Dunia haina raha, Amani wala salama. Fahari yake
ikikuloga, Utapotea njia.
3 Lo! Yesu anakuita! Kwa nini unachelewa? Ushike njia ufike
kwake! Ataja jina lako.
4 Uache haya na hofu, Mwokozi anakupenda! Kwa damu
alikomboa wewe, Anakutaka sasa.
5 Ikiwa unachelewa Kupatanishwa na Mungu, Utamkuta
Mwokozi kama Mwamuzi mwenye haki.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
207. UMGEUKIE MWOKOZI, JITENGE NA OVU
1 UMGEUKIE Mwokozi, Jitenge na ovu na dhambi! Babako
angoja ufike; Usiangamie milele!
2 Kijana, unafurahia Maisha na mambo ya nchi. Baada ya
muda kitambo Utahukumiwa na Mungu.
3 Kwa nini kujiangamiza Katika tamaa za huku? Usijipoteze
dhambini! Dunia isikuharibu!
4 Umkimbilie Mwokozi, Atakupokea kwa pendo, Na utaokoka
hakika Kwa nguvu ya damu ya Yesu!
5 Walio mbinguni waimba, Wanayo mavazi meupe; Hutaki
sehemu pamoja Na wao nyumbani mwa Baba?
6 Je, mwisho utaona wapi Mahali pa kujisetiri? Dunia
itakapochomwa Utakosa makimbilio.
7 Ujipatanishe na Mungu, Na usichelewe, rafiki! Ukimkataa
Mwokozi, Utatupwa nje gizani.
8 Chagua pasipo kukawa! Mwokozi atakupokea. Angoja ufike
kutubu; Atakutakasa kwa damu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
208. PIGA MAKENGELE YA FURAHA LEO
1 PIGA makengele ya furaha leo Kwa sababu mtu ametubu!
Mwana mpotevu amerudi sasa, Baba amemsamehe yote.
Nyimbo za furaha ya mbinguni, Nyimbo za furaha
za wakristo! Tuna’sifu Mungu kwa sababu sasa
Mtu huyu amwamini Yesu.
2 Piga makengele, ni furaha nyingi; Mkosaji amefunguliwa!
Yesu alivunja minyororo yake, Alimpa roho ya kimwana.
3 Piga makengele! Hiyo ni habari Ya kupasha mbali na karibu.
Mtu amepata kuwa mtu mpya, Dhambi zake zimeondolewa!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
209. UWATAFUTE WANAOPOTEA
1 UWATAFUTE wanaopotea, Na kwa upendo watoe
dhambini! Lia pamoja na wenye huzuni, Uwapeleke kwa
Yesu Mwokozi!
Uwatafute wanaopotea! Yesu Mwokozi
awahurumia.
2 Anatafuta waliokimbia, Anawangoja warudi upesi.
Uwafundishe kwa pendo na kweli Ju’ ya neema na haki ya
Yesu!
3 Ndani ya roho na katika siri Labda waona shauku ya
Mungu. Uwaongoze kwa Yesu Mwokozi, Wafahamishe
upendo wa Mungu!
4 Uwatafute wanaopotea! Mungu atoa upendo na nguvu.
Uwapeleke kwa Yesu Mpozi, Mwenye huruma na afya kwa
wote!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
210. IMBA INJILI YA YESU KWA MOYO
1 IMBA Injili ya Yesu Kwa moyo na roho kabisa! Lango la
neema yake Ni wazi kwa watu wote.
Imba, imba Injili, Na watu wasikilize! Imba Injili
ya Yesu, Maneno ya pendo lake!
2 Imba Injili ya Yesu! Yaleta uhuru kwa wote. Imba habari ya
damu Inayotakasa moyo!
3 Imba Injili ya Yesu, Kwa wimbo utawafundisha! Imba
habari ya Yesu! Aweza kuwaokoa.
4 Imba Injili ya Yesu, Ya raha na matumaini! Imba habari ya
haki, Wapate kujua Mungu!
5 Imba Injili ya Yesu, Hubiri amani kwa wote! Na tumsifu
Mwokozi Afanyaye yote vema!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
211. NJOO KWA YESU USISHANGAE
1 NJOO kwa Yesu, usishangae! Akuonyeshe njia ya mbingu.
Msikilize, anakusihi: Mtu wa dhambi, njoo!
Heri, heri, tutakusanyika Kwake Mungu kwa
furaha kuu! Shida na shaka hazitakuwa Kwetu
mbinguni juu.
2 Yesu aita, wote wafike, Atatuliza wenye huzuni, Kuwatolea
pendo na raha. Usikiaye, njoo!
3 Sasa wakati wa kuokoka, Uje upesi, umkubali! Mwenye
masikitiko na dhambi, Njoo kwa Yesu sasa!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
212. SAUTI YA YESU NILIISIKIA, KWA PENDO
1 SAUTI ya Yesu niliisikia, Kwa pendo aliniambia: ‘‘Ufike,
nataka kukusaidia, Nangoja, nangoja, ufike!’’
Njoo kwa Yesu, ufike upesi, Uupokee wokovu wa
Mungu! Mbona kukawa dhambini, rafiki? Yesu
anakuita, njoo!
2 Ukiwa na hofu kufika kwa Yesu, Uliye na dhambi rohoni,
Kumbuka ya kuwa huruma ni tele; Ufike kwa Yesu, angoja!
3 Ukiwa maskini, dhaifu kabisa, Mwokozi anakufahamu.
Anakuambia: ‘‘Pokea neema, Uache mzigo wa dhambi!’’
4 Na kama nilivyo ninamfikia Mwokozi aliyenipenda.
Ninaupokea wokovu na raha; Kwa shangwe ninamshukuru!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
213. KAMA UNATAKA KUWA MTU WAKE YESU
1 KAMA unataka kuwa mtu wake Yesu, Kama unataka
kufuata Yeye, Kama unataka Yeye akusaidie: Mpe Yesu
moyo wako!
Ataondoa dhambi zako zote, Na utaipokea nguvu
yake! Ukiokoka utaona kwamba Ni vizuri
kufuata Yesu kweli.
2 Kama unataka kuwa mtu mwenye heri, Ufungue moyo,
Yesu aingie! Kama unataka utulivu na faraja, Mpe Yesu
moyo wako!
3 Kama unataka kumtumikia Yesu Na kuifuata njia yake
hapa, Kama unataka kuingia huko mbingu: Mpe Yesu moyo
wako!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
214. NAMTAFUTA MWANA WANGU
1 NAMTAFUTA mwana wangu, Mtoto yu wapi leo?
Aliyenifurahisha mbele, Ningali ninampenda.
Mwanangu yu wapi leo? Mwanangu yu wapi leo?
Mwanangu, urudi, ninakutafuta, Mwanangu,
mpendwa wangu!
2 Uliyekuwa safi sana Katika utoto wako, Uliichafua roho
yako Kwa dhambi na njia mbaya.
3 Ninatamani kukuona Katika usafi tena, Na kukusikia
ukiomba Na kumshukuru Yesu.
4 Nitafutie mpotevu Kwa pendo na tumaini! Unisalimie
mwana wangu, Ya kwamba ninamngoja!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
215. MWENYEZI MUNGU ANAFANYA ISHARA
1 MWENYEZI Mungu anafanya Ishara kubwa duniani,
Anaondoa minyororo Inayofunga watu huku. Avunja nyavu
za Shetani, Na wakosaji waokoka.
2 Maneno yake yana nguvu Kushinda yote ya zamani. Na
watu wanapiga mbio Kuomba ne’ma ya Mwokozi.
Wakiyapata masamaha, Waimba wote: “Sifu Mungu!”
3 Tazama, ndugu wengi sana Wanafuata Yesu leo; Katika kila
nchi sasa Maelfu wanapenda Mungu. Wengine wanavutwa
naye Mwenyezi Mungu, Baba yetu.
4 Inua macho, mvunaji, Mavuno yanaiva sana! Uende
kutafuta watu, Uwapeleke kwake Yesu! E’ ndugu wote,
amkeni, ’kawaokowe wenye dhambi!
5 Wengine wanapoingia Ufalme wako, Yesu Kristo, Nisibakie
huku chini, Neema hiyo nakuomba! Nakaa mikononi
mwako, Unifikishe huko kwako!
6 Najua siku ni karibu Mwokozi atakaporudi, Awachukue
watu wake Mpaka nchi ya amani. E’ siku ya uheri bora,
Nakutamani. Uje mbio.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
216. NAFASI INGALIKO ARUSINI
1 NAFASI ingaliko arusini Ita’yokuwa kwake Mungu Baba.
Njoo kwake, Nafasi ingaliko!
2 Njiani mwako jua linakuchwa, Jioni inakaribia sasa. Njoo
mbio, Nafasi ingaliko!
3 Karamu ya arusi ni tayari, Na Bwana anakualika wewe.
Njoo mbio, Nafasi ingaliko!
4 Wanaingia watu wengi huko, Ufanye hima, uingie nawe!
Njoo mbio, Nafasi ingaliko!
5 Tazama, lango limefunguliwa, Neema gani: Utakaribikshwa!
Njoo mbio, Nafasi ingaliko!
6 Ufike mbio, utaona heri, Yesu atoa wingi wa neema! Njoo
mbio, Nafasi ingaliko!
7 Je, utaona shangwe ya mbinguni? Bwana-arusi akungoja
sana. Njoo mbio, Nafasi ingaliko!
8 Uliyesitasita unaitwa, Ujiazimu kuja kwake Mungu! Njoo
mbio, Nafasi ingaliko!
9 Ukichelewa, lango litafungwa, Na utalisikia neno hili:
‘‘Ondokeni! Sikuwajua ninyi!’’
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
217. BWANA YESU ATAKUJA KUTOKA MBINGUNI
1 BWANA Yesu atakuja Kutoka mbinguni, Atawachukua
wote Wanaomwamini.
Kama nyota za mbingu Watu wake watang’aa
Katika taji yake, Kuwa sifa ya Yesu.
2 Atawakusanya wote Waliompenda, Watakuwa tunu yake
Milele mbinguni.
3 Na watoto watakuwa Pamoja na Yesu, Watang’aa kama lulu
Nyumbani mwa Baba.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
218. MTOTO MIMI NI MASKINI
1 MTOTO mimi ni maskini, Lakini nafurahi Kwa kuwa Baba
yangu mwema Ananitunza vema.
2 Babangu anipenda sana, Anionyesha njia. Upendo wake
unapita Uzuri wa dunia.
3 Katika shida na huzuni Naimba kwa furaha: “Nina
makimbilio yangu Kwa Mungu Baba yangu”
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
219. HATUMJUI RAFIKI MWEMA
1 HATUMJUI rafiki mwema, Ila Yesu, ila Yesu; Yeye
mwenyewe atufahamu, Yeye Bwana peke yake.
Yesu anatujua, pia Yesu anatuonya njia. Yesu
Rafiki kupita wote, Wote pia wa dunia.
2 Hatumjui rafiki mwema Kama Yesu, Bwana Yesu. Na pendo
lake ni la ajabu, Linadumu siku zote.
3 Je, ataweza kutusahau? Hataweza ku’sahau. Twafarijiwa
kwa pendo lake Kila siku, kila siku.
4 Nani ashika agano lake? Bwana Yesu peke yake. Alikataa
kusaidia? Hataweza kukataa.
5 Nani Rafiki mpendwa wangu? Bwana Yesu peke yake.
Anastahili kupata sifa Huku chini na mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
220. YESU, WEWE U MCHUNGA WETU
1 YESU, Wewe U mchunga wangu, Twakuomba: Utulinde!
Utulishe sisi kundi lako, Tukashibe Neno lako!
Yesu mwema, Yesu mwema, Tushibishe kwa
neema! Yesu mwema, Yesu mwema, Tushibishe
kwa neema!
2 Tuongoze kwa mapito yako Hata maji matulivu! Tuhuishe
roho zetu huko Tukajazwe uhodari!
Yesu mwema, Yesu mwema, Ututie nguvu yako!
Yesu mwema, Yesu mwema, Ututie nguvu yako!
3 Yesu, uwe nasi hata mwisho, Tutakapokata roho! Tupeleke
katika makao Uliyotuandalia!
Yesu mwema, Yesu mwema, Tufikishe hata kwako!
Yesu mwema, Yesu mwema, Tufikishe hata kwako!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
221. E’ MTOTO, YAINUE MACHO YAKO
1 E’ MTOTO, yainue Macho yako mbinguni! Bwana Yesu huko
juu, Kwa upendo akuone.
2 Ukiomba asikia, Akulinda mashakani; Na anakuandalia Kao
zuri huko kwake.
3 Penda Yesu, mfuate, Tii Neno lake pia! Tena malaika wake
Watakuchukua kwake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
222. BWANA YESU ANASEMA, DHAIFU WEWE
1 BWANA Yesu amesema: “Dhaifu wewe sana. Mimi ni
mchunga mwema.” Na kwa hiyo namwandama.
Yesu alikufa kwa ajili yangu, Aliziondoa dhambi,
Furaha kubwa kwangu!
2 Pendo la Mwokozi wangu Limeyeyusha moyo. Ametoa
dhambi zangu Na kiburi na uchoyo.
3 Sina kitu mkononi Cha kunifaidia; Udhaifu u moyoni, Yesu
ninamlilia.
4 Mungu akisaidia Nitamaliza mwendo. ‘‘Yesu alinifilia’’,
Nitaimba huko ng’ambo.
5 Siku moja nitafika Mbinguni huko juu, Nitaimba kadhalika
Katika shukrani kuu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
223. NI UHERI BORA KUMWAMINI BWANA
1 NI uheri bora kumwamini Bwana Yesu Kwa wakati wa
ujana wetu, Kabla hatujazionja Dhambi na mashaka
Zinazoharibu roho zetu.
Ni uheri bora kumwamini Bwana Yesu, Na
kumfuata kila siku. Na ujana wetu
ukitukimbia tena, Shangwe ya wokovu
itabaki.
2 Ni uheri bora kumtii Bwana Yesu Kwa wakati wa ujana
wetu. Hivyo tutakuwa na dhamiri safi, njema Kwa maisha
yetu yote pia.
3 Ni uheri bora kumtumikia Yesu Kwa wakati wa ujana wetu.
Bwana Yesu akumbuka kila tendo dogo, Atalipa kwa neema
yake.
4 Ni uheri bora kumngoja Bwana Yesu Kwa wakati wa ujana
wetu. Atatuchukua kwake kwa furaha kubwa, Tutakuwa
naye siku zote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
224. YESU, MWENYE PENDO KUBWA
1 YESU, mwenye pendo kubwa, Usinipitie! Katika maombi
yangu Unibarikie!
Yesu, Yesu, unisikilie! Ukiwabariki wote,
Usinipitie!
2 Ninakiendea sasa Kiti cha neema; Kutokuamini kwangu
U’ondoe vema!
3 Nakutegemea, Bwana, Njia unionye! Roho yangu
imevunjwa, Yesu, uniponye!
4 Wewe, Yesu, ni kisima Cha furaha yetu. Nani ni Mchunga
mwema, Ila Bwana wetu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
225. LO! BENDERA MBELE YAKO
1 LO! Bendera mbele yako, usihofu sasa! Usimame kwa imara
kama Danieli!
Uwe mhodari kama Danieli! Weka makusudi
mema bila kuogopa!
2 Wenye hofu hawawezi kuingia mbingu. Tweka tu bendera
yetu, endelea mbele!
3 Mashujaa wa Shetani wangeshindwa sana Wakikuta jeshi la
askari wa imani.
4 Endelea kwa kushinda, Yesu ni Mfalme! Taji ya uzima
utapata huko juu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
226. MACHO YANGU KUMTAZAMA
1 MACHO yangu ya kumtazama, Masikio ya kumsikia, Na
miguu ya kumfuata Yesu, Rafiki yangu!
2 Roho yangu yampenda Yesu, Na ulimi unamshukuru, Kwa
mikono namtumikia Yesu, Rafiki yangu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
227. MUNGU ALIYE MBINGUNI
1 MUNGU aliye mbinguni Alitupa kiongozi, Naye ni rafiki wa
watoto wote. Ukijua jina lake, Ulitaje sasa hivi! Anapenda
wote, hata wewe, nami.
Mbingu na ufalme wake Wa wototo wote sasa!
Mbio tuishike njia Iendayo kwake Yesu Ili tuione
raha ya mbinguni!
2 Yesu mwenye pendo kubwa Awakumbatia wote,
Anawabariki kwa huruma yake. Hatuoni huku chini Mtu
mwema kama Yeye, Hasahau mtu, hata mnyang’anyi.
3 Yesu ni Mchunga mwema, Anawakusanya sasa Mkononi
mwake wana wa kondoo. Kifuani mwake tena
Anawachukua wote Hata kwa ufalme wake huko juu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
228. WAKATI WA UTOTO WAKO
1 WAKATI wa utoto wako, Hujapoona shida bado, Sauti
ilikuambia: “Unipe sasa moyo wako!”
Wajua ni nani huyu Anayekuita sasa? Ni Yesu,
Rafiki yako; Anakuita: ‘‘Njoo kwangu!’’
2 Na katika ujana wako Wausikia mwito wake, Na jinsi
utakavyoshinda Shetani akikujaribu.
3 Wakati wa uzee wako Dhambini ukiendelea Hata kukaribia
kufa, Mwokozi akuita tena.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
229. MWOKOZI, MFALME, ULISULIBIWA
1 MWOKOZU Mfalme, ulisulibiwa, E’ Pasaka wetu,
ulidhihakiwa. Ukatoka damu, ’kaona uchungu Ulipotimiza
mapenzi ya Mungu. Huku Gethsemane ulihuzunika, Kwa
neno la mbingu ukafarijika. Katika kuomba ukatiwa nguvu,
Na mwisho ukafa tupate wokovu.
2 Kwa ’jili ya mimi ulijeruhiwa, Ukaonja kufa, nipate uzima.
Ulijisahau, ukanikumbuka, Uliwaombea waliokutesa. Na
ulijitoa dhabihu ya kweli, Na kuusikia uchungu mkali. Kwa
pendo kamili ulikusudia Kuonja mauti kwa ’jili ya wote.
3 Je, kupatanishwa na Mungu ni nini? Ni kwamba laana la
dhambi lakoma. Kufika karibu na Mungu ni nini? Ni kuwa
rafiki wa Mungu wa mbingu. Na sasa ufike kutoka
dhambini, Utie hatia na dhambi nuruni! Mwokozi mpendwa
akuhurumia, Atakufungua na ’kusaidia.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
230. GOLGOTHA MWOKOZI ALITUNDIKWA
1 GOLGOTHA Mwokozi alitundikwa Mtini kwa ’jili ya wote.
Na damu akaitoa Mwokozi Ili kutangua dhambi.
Penye msalaba niliokolewa Kwa damu ya Yesu
iliyotolewa. Mwamuzi mwenyewe alinikomboa,
Akanilipia deni.
2 Golgotha nami nimesulibiwa Pamoja na Yesu Mwokozi; Na
njia kwa Mungu Baba ni wazi, Pazia limepasuka.
Nimesulibiwa pamoja na Kristo, Na mtu wa kale
alikufa hapo. Na mambo ya kale yamekwisha ’pita,
Lo! yote ni mapya sasa!
3 Niliunganishwa naye Mwokozi, Na sasa ni hai kwa Mungu.
Kuishi ni Kristo, siri ajabu, Na kufa faida kwangu!
Kwa damu ya Yesu nimetakasika, Hatia na dhambi
zimeondolewa. Shetani hawezi kunidhuru tena,
Nimewekwa huru kweli.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
231. MWOKOZI ALITOA DAMU KWA'JILI YA WAOVU
1 MWOKOZI alitoa damu kwa ’jili ya waovu, Msalabani
alikufa Kuniokoa mimi.
E’ Yesu, niokoe sana, Nifunze kuamini! Na
unilinde tena, Bwana, Nisipotee kamwe!
2 Alijitwika dhambi zetu, Huzuni na maradhi; Neema kubwa,
wema wingi, Upendo wa ajabu!
3 Na hapo jua likafichwa, Ikawa giza kuu; Muumba alitufilia
Kutulipia deni.
4 Magoti yangu nayapiga Msalabani pake, Na kwa machozi
natazama Mateso yake huko.
5 Nitakurudishia nini, Mwokozi wangu mwema? E’ Bwana,
nikutumikie Maisha yangu yote!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
232. NILIPOFIKA KWA BWANA YESU
1 NILIPOFIKA kwa Bwana Yesu, Nikapaaza sauti yangu:
“Yesu Mwokozi, unirehemu!” Akaniokoa. :/: Yesu asifiwe! :/:
Alisikia kilio changu, Yesu asifiwe!
2 Nilipofika kwa Bwana Yesu, Nikamsihi Mwokozi wangu:
“Unitakase, nifanye safi!” Akanisikia. :/: Yesu asifiwe! :/:
Alisikia maombi yangu, Yesu asifiwe!
3 Ona kisima cha msalaba, Leo kingali chabubujika Kuniokoa
na kusafisha! Yesu asifiwe! :/: Yesu asifiwe! :/: Aniokoa,
anisafisha, Yesu asifiwe!
4 Njoo kwa Yesu, kisima hicho, Unywe, uoshwe katika maji!
Kiu yapoa, na watakaswa, Yesu asifiwe! :/: Yesu asifiwe! :/:
Kiu yapoa, na watakaswa, Yesu asifiwe!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
233. TAZAMA MWOKOZI ALIYEKUFILIA
1 TAZAMA Mwokozi aliyekufilia Ili wewe upate uzima!
Tazama, kwa pendo atakusaidia, Usidumu dhambini daima!
Yainue macho! Tazama Mwokozi aliyekufilia, Ili
upate uzima!
2 Mwokozi alisulibiwa ju’ ya mti Ili sisi tupate wokovu.
Alitukomboa kwa damu yake safi, Kwake Yeye twapata
wongofu.
3 Hakuna majuto yaweza’ kutuponya, Ila damu ya Yesu
Masiya. Ufike kwa Yesu apate kukuonya Jinsi yaondokavyo
hatia!
4 Rafiki, waitwa na Mungu kwa wokovu, Anataka ufike upesi.
Kwa nini kukawa, Ufike bila hofu, Uondoke katika hatari!
5 Ufike, pokea uzima wa milele, Bwana Yesu ali’tuletea!
Karama ya mbingu ni tumaini letu, Ipokee na hutapotea!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
234. UTUKUFU WA MBINGUNI NI WA HERI
1 UTUKUFU wa mbinguni Ni wa heri na amani, Dhambi
hazitakuwamo. Vitu vyote vilivyomo Ni vya tunu na
thamani, Dhambi hazitakuwamo.
Dhambi hazitaingia Mbingu ya utakatifu.
Ukidumu mwenye dhambi Bila kutakaswa huku,
Hutaingia mbinguni.
2 Kama unatumaini Kufikia nchi ile Na kuona Bwana Yesu,
Utafute utakaso Na kupata moyo safi! Dhambi
hazitakuwamo.
3 Unaweza ’tenda dhambi Na kukana Bwana Yesu, Walakini
ukumbuke: Dhambi zako zitafunga Lango la mbinguni,
kwani Dhambi hazitakuwamo.
4 Na ukiwa mkaidi hata sa’ ya kufa kwako, Utaitwa
hukumuni, Na utaambiwa huko: “Ondokeni, siwajui!"
Dhambi hazitakuwamo.
Ukitaka kufikako Mbingu ya utakatifu, Tubu sasa,
acha dhambi, Utafute moyo safi, Na utaingia
mbingu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
235. TUMEKOMBOZWA KATIKA NCHI
1 TUMEKOMBOZWA katika nchi, Usikilize vema, rafiki! :/:
Tumeokoka tufike juu, Taji kutiwa, furaha kuu! :/:
2 Tumekombozwa katika watu, Hata tu’chekwe kitambo
huku. :/: Twavumilia katika shida, Twatazamia ’heri wa
mbingu. :/:
3 Tumekombozwa, tuwe wa huru, Tukichokozwa haitudhuru.
:/: Tutaondoka, ’hamia mbingu, Tutasimama mbele ya
Mungu. :/:
4 Tumekombozwa, furaha kuu, Twaandaliwa karamu kuu! :/:
Salamu hiyo uitangaze, Wafike mbio na waokoke! :/:
5 E’ mama, baba, mbona kungoja? Ndugu na dada, fika
pamoja! :/: Mwenye kukawa hataingia, Leo waitwa na Yesu
pia. :/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
236. DHAIFU, MWENYE DHAMBI
1 DHAIFU, mwenye dhambi, Nilipotea njia, Lakini Bwana
Yesu alinihurumia. Nategemea Yeye, Najua pendo lake,
Ajaza roho yangu, ninavyo vyote mwake.
Ajaza roho yangu, Apita vitu vyote. Amani na
upendo Ni zangu siku zote. Ajaza roho yangu,
Neema kubwa kwangu! Namhimidi Yesu: Yu yote
ndani yangu.
2 Sitaki dhambi tena, haiku’faidia; Rafiki yangu, Yesu,
ananisaidia. Alitangua dhambi kwa msalaba wake, Kwa
Yeye ukombozi, na vyote vimo mwake.
3 Napenda kufuata daima nyayo zake, Nibadilishwe sana,
nifananishwe naye! Na tena siku moja atanikaribisha
Nyumbani mwake Baba, na atanijaliza!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
237. MWOKOZI WANGU NI MWAMBA BORA
1 MWOKOZI wangu ni mwamba bora, Ahadi kama milima;
Zaniletea amani tele, Na mibaraka daima. Katika mwamba
ni raha kuu, Baraka tele kutoka juu. Nakaa humo,
ninastarehe, Ni heri sana milele.
2 Makimbilio ni mwamba huo Katika teso lo lote; Nisikimbie
adui ’kuu, Nishinde katika vyote! Dunia yote ikitingika,
Ahadi zake hazipunguki. Nakaa humo, ninastarehe, Ni heri
sana milele.
3 Nakaa mbali ya udhalimu, Hatia, dhambi, hukumu. Na kwa
imani nikisimama, Adui atakimbia. Nayo mawazo ya giza
tupu Hayatapata nafasi huko. Nakaa humo, ninastarehe, Ni
heri sana milele.
4 Nafurahia baraka zote Za ulimwengu wa roho. Karama hizo
nalizipewa Katika kufa kwa Yesu. Hakuna woga na shaka
huko, Hayatakuwa manung’uniko. Nakaa humo,
ninastarehe, Ni heri sana milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
238. NIFANANISHWE NAWE MWOKOZI
1 NIFANANISHWE nawe Mwokozi, Ni haja yangu iliyo kuu.
Ninakuomba, na kwa machozi, Nikufuate, Bwana wa juu!
Nifananishwe nawe Mwokozi, Mwenye upendo,
safi halisi! Unitakase, Unijalize! Nifananishwe
nawe zaidi!
2 Nifananishwe nawe Mwokozi, Mwenye rehema, pendo ajabu!
Niwapeleke kwa Mkombozi Walioshindwa na majaribu!
3 Nifananishwe nawe Bwanangu, Mtakatifu, mwenye saburi!
Niwe mnyofu kazini mwangu, Mtu thabiti bila jeuri!
4 Nifananishwe nawe Mwokozi! Ninakuomba: Unijalize! Vyote
ninavyo nakutolea, Uniongoze, uniagize!
5 Nifananishwe nawe Mwokozi! Nimiminie pendo moyoni!
Nibadilishe, E’ Mkombozi, Niwe tayari kwenda mbinguni!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
239. NENO BAYA LISITOKE KAMWE
1 NENO baya lisitoke Kamwe kwa ulimi wako! Pendo
likuchunge pote, Hata na maneno yako!
Amri ya Yesu ni ‘‘Mpendane’’! Kama watoto wema
tumtii! Amri ya Yesu ni ‘‘Mpendane’’! Kama
watoto tumtii!
2 Pendo ni la mbingu, safi, Urafiki ’takatifu. Tusiyaharibu
tena Kwa maneno yetu ’gumu!
3 Neno moja la hasira Au tendo la uovu Kwa upesi linavunja
Fungu la upendo safi.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
240. NAVUTWA KWAKE YESU
1 NAVUTWA kwake Yesu na ninamfurahia, Uzuri wake
unapita vyote vya dunia. Siwezi kuupima kweli kwa fikara
zangu. Uzuri wake unazidi kuwa bora kwangu!
Siwezi kueleza Uzuri wake huku, Lakini
niaufahamu Huko ju’ mbinguni.
2 Upendo wa ajabu mno nausifu sana, Ukanivuta kwa upole,
nije kwake Bwana! Ukaondoa mimi katika unyonge wangu,
Upendo wake unazidi kuwa bora kwangu!
Siwezi kueleza Upendo wake huku, Lakini
nitaufahamu Huko ju’ mbinguni.
3 Wokovu wake wakupendwa mno nausifu, Uliondoa woga,
ukanipa utulivu. Napenda Yesu aliyechukuwa dhambi
zangu, Wokovu wake unazidi kuwa bora kwangu.
Siwezi kueleza Wokovu wake huku, Lakini
nitaufahamu Huko ju’ mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
241. SITASHAWISHIWA TENA NA DUNIA HUKU
1 SITASHAWISHIWA tena na dunia huku, Mema yote ni kwa
Yesu, nampenda Yeye. Katika safari yangu, Bwana Yesu
wimbo wangu. Mbali, kwetu, kila saa namsifu Yesu.
2 Mimi mtu heri sasa, nampenda Yesu. Vyote nimempa Yeye,
namtumikia. Tumaini langu kuu nimeweka huko juu. Mbali,
kwetu, kila saa Namtumikia.
3 Njia yote kwenda mbingu Nifuate Yesu! Nifanane naye
Bwana, Niwe nuru huku! Nimkiri Yesu pote na katika hali
zote! Mbali, kwetu, kila saa nifanane naye!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
242. MAISHA YANGU YOTE NI MALI YA MWOKOZI
1 MAISHA yangu yote Ni mali ya Mwokozi. Maungo, roho na
akili, Yeye ameyabadili. Siku zangu zote Ni mali ya
Mwokozi.
Wakati wangu wote Ni mali ya Mwokozi. Machoni
pake ni amani, Natumika kwa shukrani. Namsifu
Yesu, Amenihurumia!
2 Maisha yangu yote Ni mali ya Mwokozi. Naomba niwe
mpendevu, Nitafute wapotevu! Aliwanunua Kwa damu
takatifu.
3 Maisha yangu yote Ni mali ya Mwokozi. Unijalie kati’
mwendo Kuongoza kwa upendo Wana wapotevu, Wapate
kuokoka.
4 Maisha yangu yote Ni mali ya Mwokozi. Nakaa miguuni
pake, Siku moja huko kwake Inapita elfu Pengine bila Yesu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
243. UKICHOKA KWA SAFARI NGUMU
1 UKICHOKA kwa safari ngumu, Sema na Yesu, sema na
Yesu! Waogopa kwamba hutadumu, Sema na Yesu daima!
Sema na Yesu, sema na Yesu, Yeye Rafiki amini!
Akupenda kwa upendo bora. Sema na Yesu kwa
yakini!
2 Ukilia ’chozi ya majuto, Sema na Yesu, sema na Yesu!
Ukiteswa ju’ ya dhambi nzito, Sema na Yesu daima!
3 Je, wahofu jua likifichwa? Sema na Yesu, sema na Yesu!
Kwa taabu ukihuzunishwa, Sema na Yesu daima!
4 Ukisumbukia kufa kwako, Sema na Yesu, sema na Yesu!
Ukiteswa kwa maisha yako, Sema na Yesu daima!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
244. SAFARI YANGU HUKU
1 SAFARI yangu huku ikiwa hatarini, Na ikipita katika giza
na jaribu, Najua kwa hakika: Mwokozi Yu karibu,
Ninamfuata mahali po pote.
Nikiwa pamoja na Yesu sina hofu. Anipa furaha na
heri rohoni mahali pote. Ikiwa nitayashiriki
mateso yake, Nitamfuata Mwokozi hata mwisho.
2 Nikitangaza Neno la Mungu duniani Katika mataifa walio
wakaidi, Nina furaha kubwa moyoni mwangu, kwani
Mwokozi Yu nami mahali po pote.
3 Na Bwana akitaka nibaki hapa kwangu, Wengine
wakitumwa mahali pa ugeni, Kusudi langu moja: nidumu
mwaminifu, Na nimfuate mahali po pote!
4 Si lazima nijue makusudio yote, Ni kazi yangu huku
kumfuate Yeye. Ikiwa nitabaki, ikiwa nitakwenda,
Nitamfuata Mwokozi po pote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
245. MIKWAJU ITIAPO GIZA NA KIVULI
1 MIKWAJU itiapo giza na kivuli Katika nchi ya Bersheba ya
zamani, Alitembea Ibrahimu asubuhi, Na maumivu na
huzuni ni rohoni, Kwa kuwa aliitwa na Mwenyezi Mungu
Kutii amri yake bila nung’uniko. Na hapo akaomboleza: “E’
Bwanangu, Wataka nitakutolea mwana wangu?”
2 Sauti ya Bwanake aliifahamu: “Mtwae sasa mwana wako wa
pekee, Ukamtoe mwana juu ya madh’bahu; Kafara ya
thamani ukanitolee!” Na moyo wake ukamtulia sana,
Akitukuza Mungu na kutumaini Ya kuwa Yeye atamfufua
mwana; Alimjuwa Yeye aliye mwamini.
3 Akaamka Ibrahimu alfajiri, Akatandika punda, akatwaa
kuni. Pamoja na mwanawe tena ’kasafiri, Na roho yake
ikalia kwa huzuni. Mwanawe Isak’ aliyemfurahia: Kipeo cha
furaha ya uzee wake, Matumaini yake yote ya dunia, Kafara
atakayotoa kwa Bwanake.
4 Katika njia ya mlima wa Moriya Mtoto akamsaili baba yake:
“Tazama moto uko, kuni ziko pia, Kondoo mume kwa
kafara yuko wapi?” Na Ibrahimu akajibu kwa imani
Isiyoona shaka wala kudhania: “Kondoo mume kwa kafara
ya shukrani, Ninasadiki Mungu atajipatia.”
(voir la suite sur la page suivante)
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
5 Je, awezaje Ibrahimu kusahau Wakati huo wa uchungu na
huzuni, Na jinsi akajenga huko madhabahu, Na tena
akamweka mwana ju’ ya kuni? Akakitwaa kisu amchinje
mwana, Halafu aliposikia neno tamu: ‘‘Usifanyie neno sasa
kwa kijana, Najua wanipenda sana Ibrahimu!’’
6 Akainua macho yake kwa haraka, Tazama dume la kondoo,
nyuma yake, Aliyenaswa pembe zake kwa kichaka!
Akamtoa akomboe mwana wake. Na malaika akamwita,
akasema: ‘‘Umenitii nami nitakubariki. Na kwa uzao wako
mataifa tena wa’barikiwa kwani umenisadiki.’’
7 Machozi yamekuwa mengi tangu hapo; Wakristo
wamekamilika kwa jaribu. Na mlimani mwa Moriya
wazikapo Matumaini yao, pendo na nasibu. Lakini juu ya
mlima wa kafara Mwenyezi Mungu abariki watu wake.
Awajulisha nguvu zake na ishara, Awajaliza Roho ya ahadi
yake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
246. HESHIMA NA SIFA ZINA BABA MBINGUNI
1 HESHIMA na sifa Zina Baba mbinguni, Aliyetupenda
Zamani na sasa!
Haleluya, usifiwe! Haleluya! Amina. Haleluya,
usifiwe! Haleluya! Amina.
2 Heshima na sifa Zina Yesu Mwokozi, Alitufilia Kwa ’jili ya
dhambi!
3 Heshima na sifa Zina Roho wa kweli, Anashuhudia
Mwokozi na damu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
247. NAPENDA SANA KUMSHUKURU MWOKOZI
1 NAPENDA sana kumshukuru Mwokozi wangu kwa nia
huru; Kwa wimbo wangu nashuhudia Upendo wake na damu
pia.
2 Nikidhukuru mateso yake Msalabani na kufa kwake, Nataka
katika wimbo wangu Kumtolea shukrani yangu.
3 Naimba sasa, nina faraja, Katika Yesu nina taraja. Ni
mambo tunayofunuliwa, Kwa wenye dhambi yamefichiwa.
4 Kwa Neno lake aniambia Ya kwamba ananihurumia, Na
ukombozi ninao sasa Kwa damu iliyonitakasa.
5 Na msione ajabu sana Ya kuwa namshukuru Bwana!
Ninamwimbia kidogo sasa, ’taendelea mbinguni hasa.
6 Anipa vyote kwa pendo lake, Urithi wangu wachungwa
kwake Hata wakati wa kuhamia Mbinguni, na nitashangilia.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
248. YESU AKINIONGOZA SITAANGUKA
1 YESU akiniongoza Sitaanguka, sitaanguka. Ni Mfalme
mtukufu, Mwokozi wangu, Mwokozi wangu.
Wakati huu, hata milele Apita vyote vya dunia.
Yesu amenichagua, Mwokozi wangu, Mwokozi
wangu.
2 Yesu amenipa raha, Ni kiongozi, ni kiongozi. Anaka’ moyoni
mwangu, Yesu Mwokozi, Yesu Mwokozi.
3 Nilikuwa kama chungu Kilichovunjwa, kilichovunjwa. Sasa
nimeokolewa Na Bwana Yesu, Na Bwana Yesu.
4 Nitakapofika mbingu Nitamsifu, nitamsifu Yesu kwa upendo
wake, Mwokozi wangu, Mwokozi wangu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
249. ZAMANI MJINI MWA YERUSALEMU
1 ZAMANI mjini mwa Yerusalemu Waisrael’ waliabudu.
Wakristo wa sasa wanakusanyika Kuomba, kusifu Mwokozi.
Msifuni, msifuni Mungu wetu, Kwani ametutendea
mema! Tutamsifu tu Aliyetoka ju’, Shangilieni
Mwokozi mwema!
2 Mwokozi Yu nasi, ame’fumbulia Uweza wa kutuokoa. Na Yu
mwaminifu, atusikiliza, Apenda kutupa baraka.
3 Twaomba baraka na mvua ya mbingu Kuithibitisha Injili!
Wagonjwa wapone, vipofu waone, Tupate ’batizo wa Roho!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
250. IKAWA SIKU KUBWA KWANGU
1 IKAWA siku kubwa kwangu Aliponiokoa Yesu. E’ roho
yangu, umsifu Mwokozi wako, Yesu Kristo!
Siku kuu, siku kuu Aliponiokoa Yesu! Na kwa
neema na upendo Akaondoa dhambi zangu! Siku
kuu, siku kuu Aliponiokoa Yesu!
2 Nimeokoka, nafurahi! Ananitaja mwana wake! Alinivuta
kwa upendo, Nikafuata mwito wake.
3 Ni shangwe ku’ moyoni mwangu Nikifuata Bwana Yesu.
Anipimia ne’ma sawa Wakati wote ma maisha.
4 Kwa pendo kubwa na rehema Ananitunza siku zote.
Sitasahau siku ile Aliyoniokoa Yesu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
251. HERI MIMI KWANI MKOMBOZI WANGU
1 HERI mimi kwani Mkombozi wangu Alitoa dhambi zote!
Shangwe na furaha zanijaza mno, Kila siku nafurahi!
Kila siku nafurahi! Kila siku nafurahi! Heri mimi
kwani Mkombozi wangu Alitoa dhambi zote!
2 Heri mimi, Yesu alinifilia; ni furaha ku’; Yu hai! Ni Rafiki
kweli anayetuweka Huru toka minyororo.
Kila siku nafurahi! Kila siku nafurahi! Heri mimi,
Yesu alinifilia; Ni furaha ku’: Yu hai!
3 Heri mimi kwani ananiongoza; Nafuata nyayo zake.
Nikiyasikia tu maneno yake, Sitaweza kupotea.
Kila siku nafurahi! Kila siku nafurahi! Heri mimi
kwani ananiongoza, Sitaweza kupotea!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
252. NINAKUSHUKURU MUNGU KWA FADHILI ZAKO
1 NINAKUSHUKURU Mungu Kwa fadhili zako zote, Kwa
furaha na uchungu, Kwa neema njia yote! Kwa kipupwe na
masika, Kwa wakati wa machozi Na kwa raha kadhalika
Na’shukuru Mkombozi!
2 Ninakushukuru Bwana Kwa kunifunua siri, Kwa kusikiliza
sana Ombi, na kulifikiri! Na kwa msaada wako, Kwa wakati
wa jaribu. Kwa agano la Mwanako Nashukuru! U karibu.
3 Nashukuru Wewe pia Kwa uzuri wa mbinguni, Nuru
uliyoitia, Na kwa jambo la huzuni! Kwa jaribu na kwa giza
Na kwa siri ya imani, Tena kwa kunijaliza Ninakuwa na
shukrani!
4 Kwa waridi za njiani Na miiba yao pia, Kwa mahali pa
amani Uliopotuandalia, Kwa agano la upendo, Kwa kutupa
tumaini, Kwa kifiko cha mwenendo: Nashukuru! U amini!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
253. SIKU YA FURAHA INATUFIKIA
1 SIKU ya furaha inatufikia, Siku nzuri katika nchi. Mungu
asifiwe Mbali na karibu! Malaika wanamshukuru Bwana.
2 Huko Bethlehemu alipozaliwa Yesu Kristo Mwokozi wetu,
Pendo la Mwenyezi Likadhihirika; Raha ya mbinguni
imefika kwetu!
3 Ni karama kubwa tuliyoipewa Kwa mkono wa Baba Mungu.
Roho Mfariji anatuongoza, Atuonya njia iendayo kwake.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
254. E’ ROHO YANGU, SIKILIZA VEMA
1 E’ ROHO yangu, sikiliza vema, Wimbo wa juu unatufikia!
Shangwe na raha unatuletea, Amezaliwa Mkombozi wetu.
Ahimidiwe Mungu wa mbingu! Na duniani iwe
raha na amani!
2 Ninafurahi kwani wimbo huo Tungali tunausikia huku. Na
kwa upendo Mungu anaita: ‘‘Mfike kwangu, nitawapa
raha!’’
3 Katika nchi, mbali na karibu, Sauti ya Mwokozi inavuma.
Watu wa dhambi wanakuja kwake, Awapokea na awaokoa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
255. ZIMETIMIZWA AHADI NJEMA
1 ZIMETIMIZWA ahadi njema: Amezaliwa Mwokozi wetu!
Na yote Mungu aliyosema Kwa manabii kwa ’jili yetu,
Tumeyapata na kuyaona Katika Yesu, mwanawe Mungu.
Alitujia na tumepona, Twaweza wote kufika mbingu.
2 Alijidhili kuwa maskini, Na alifika ulimwenguni, Mwokozi
wetu, twaiamini. Walimlaza katika hori. Na utukufu kwa
Baba yake Aliuacha, rehema kuu! Na twende sote horini
kwake, Tumsujudu Aliye juu!
3 Mtoto huyo - mfano wetu, Si mtu tu, bali Mungu pia. Akawa
mwenye kutukomboa, Na Golgotha alitufilia. Tumepotea
vibaya sana Katika dhambi na ukaidi, Kwa umaskini wa
Yesu Bwana Twapata kuwa wote tajiri.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
256. ASUBUHI NA MAPEMA SIKU YA HABARI
1 ASUBUHI na mapema Siku ya habari njema Twende sote
Bethlehemu! Mungu ameturehemu!
2 Nyota kubwa inang’aa Ju’ ya nyumba ana’kaa Mwana wake
wa pekee. Mbele yake tujiweke!
3 Wachungaji wasikia Nyimbo zao malaika: ‘‘Asifiwe Mungu
juu, Duniani raha kuu!’’
4 Mariamu anachoka, Safarini wana’toka, Analaza mwana
ndani Ya sanduku la majani.
5 Wachungaji wanafika, Na magoti wana’piga; Waliacha
kundi lote Kushukuru Yesu wote.
6 Mwana yule ni Mwokozi, Msaada, Mkombozi. Neno la
kuaminiwa, Mungu ametushukia!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
257. SIKU YA KUISIKIA PARAPANDA
1 SIKU ya kuisikia parapanda yake Mungu, Ikiita wateule
wake wote, Kwa neema tutakaribishwa na Mwokozi wetu
Katika kutano kubwa huko juu.
Tutakaribishwa kwake, tutakaribishwa kwake,
Tutakaribishwa kwake Katika kutano kubwa huko
juu.
2 Mungu atawafufua wafu wake siku ile, Na wakristo hai
watabadilika, Wote watanyakuliwa kumkuta Bwana Yesu,
Tutakusanyika wote huko juu!
3 Wimbo wa mbinguni kama maji utakapovuma, Utukufu
wake Yesu tuta’ona. Nami pia kwa neema nitafika siku ile
Kusikia neno lake la ‘‘Karibu!’’
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
258. MKUTANO ’KUBWA GANI MLIMANI
1 MKUTANO ’kubwa gani Mlimani mwa Sayuni Asubuhi ya
milele? Hawa walinunuliwa, Tena walitakasiwa, Wawe
malimbuko kwa Mwokozi.
2 Hata kufa huku chini Walikuwa waamini, Walimfuata
Yesu. Sasa wanaka’ mbinguni, Wametoka jaribuni,
Wamerithi raha ya kipeo.
3 Ukamili wa uzuri Wa muziki na zaburi Unatoka huko juu!
Ni sauti tamu mno Ya kinubi na ya wimbo Kandokando ya
Mwokozi wetu!
4 Wimbo huo ni wa nani, Wa sauti ya tufani, Wa kutia raha
kuu? Ndio wimbo mpya ule Uimbwao sasa kule Ili kuhimidi
Mkombozi.
5 Bwana, unilinganishe, Na ulimi u’safishe, Nami nikaimbe
huko! Nipe vazi la rohoni, Safi sana, la kitani Lifaalo asubuhi
hiyo!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
259. NAFIKIRI SIKU TUTAKAYOFIKA MBINGUNI
1 NAFIKIRI siku tutakayofika Mbinguni huko kwetu, Na
malaika kwa furaha Watatukaribisha.
Wataimba wimbo wa kutupokea: ‘‘Karibuni!
Karibuni wote kwetu!’’ Malaika wa Mungu
watatulaki kwa nyimbo za furaha: ‘‘Twawasalimu!
Karibu kwetu!’’
2 Mkutano ’kubwa umekwenda mbele Na sasa uko kule.
Huimba kwa sauti kuu Ukimsifu Mungu.
3 Sisi nasi tutakusanyika huko Yerusalemu mpya, Na
mkutano wa wakristo Utatuamkia.
4 Bwana Yesu naye atatupokea, Atatukumbatia Katika
nyumba ya mbinguni Iliyo ya milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
260. MWENYEZI AMEJENGA MJI
1 MWENYEZI amejenga mji, Mfalme wa huko ni Yesu,
Yohana aliouona Kushuka kutoka mbinguni. Ukuta ukawa
wa jaspi, Na njia ya dhahabu safi. Wakati nitakapohama,
Nitachukuliwa Sayuni.
Mjini mle mtakatifu Yesu atuandalia makao. Sasa
nangoja, nautamani Mji mzuri kutoka mbinguni.
2 Na dhambi hazitafikapo, Uchafu hautaingia, Mateso,
ugonjwa na kufa Hazitakuwapo mjini. Na mle tutayasahau
Mashaka, ’jaribu na vita; Hatutaachana milele. Hakuna
uchungu rohoni!
3 Mjini hatutayaona Kilio na maombolezo. Na huko
hatutadanganywa, Haitakuwapo husuda. Na wana wa
Mungu waona Uzuri na utakatifu; Nitakapofika mjini
Nitashangilia daima.
4 Wapenzi, rafiki na wale Waliomaliza safari, Watashangilia
kabisa Kwa ’jili ya damu ya Yesu. Na tutawaona mjini
Katika makao ya raha. Tumaini letu ni hili: Tutakusanyika
mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
261. MSAFIRI ULIE NJIANI
1 MSAFIRI uliye njiani, Watamani nyumba ya Babako.
Sikiliza nyimbo za mbinguni! U karibu sana kufikako.
Utakuwako huko, Katika mkutano wa wakristo
Huko mbinguni kwa raha ipitayo fahamu?
Utakuako huko Wakati wa kuimba wimbo mpya
Wa kumsifu Mwokozi siku zote?
2 Sikiliza sasa makengele Yapigwayo huko juu kwetu, Ili
kutuita sisi mbele Ya jioni ya maisha yetu!
3 Labda siku ile ni karibu Nitakapokwenda, nitahama! Sitaona
tena majaribu, Nitajazwa kwa kumtazama.
4 Lango la mbinguni wazi sasa, Yesu amelifungua kwako.
Utaweza kuokoka hasa, Usiahirishe heri yako!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
262. KITAMBO BADO- VITA ITAISHA
1 KITAMBO bado — vita itaisha, Kitambo, na dhoruba
zitapoa. Na tena nitalaza kichwa changu Mbavuni mwake
anayenipenda. :/: Nitaziona raha na amani, Mbinguni
hazitakuwapo dhambi. :/:
2 Kitambo bado — roho yaumizwa, Kitambo katika usiku
huku. Machozi nina’toka mara nyingi Sababu sijaona bado
Yesu. :/: Lakini asubuhi ya milele Huko mbinguni sitalia
tena. :/:
3 Kitambo bado — ya kuchoka huku, Kitambo — tena
nitaona Yesu. Na huru mbali na hatari zote Nitastarehe
mikononi mwake. :/: Uvuli wote utaondolewa Kwa nuru
huko kamilifu kweli. :/:
4 Mateso yangu hayadhuru tena, Nitasahau yote kwake Yesu.
Nikisumbuka muda duniani, Mbinguni sitaona shida, kufa.
:/: Na Mungu atafuta kila chozi, Ataondoa maumivu yote. :/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
263. ENYI KUNDI LAKE MUNGU
1 ENYI kundi lake Mungu, Muda haba mhimili! Kati’ nchi ya
milele Mtaona raha tele. :/: Muda haba, muda haba, Tena
vita itakwisha. :/:
2 Usilogwe na dunia, Usiache Mungu wako! Katika mabaya,
mema Ufuate Bwana Yesu. :/: Siku zote, siku zote! Hivyo
utashinda vyote. :/:
3 Ukichoka safarini, Ukiona njia ndefu Na hatari za jangwani,
Mungu akuburudisha. :/: Raha huko, raha huko Yatuliza
msafiri. :/:
4 Kwa imani tunaona Nchi yetu ya ahadi. Ni habari nzuri
sana: Majaribu yatakoma. :/: Mbio sana, mbio sana Huko ju’
tutaonana. :/:
5 Tukiitwa na mauti Kwa furaha tutahama. Tulivyovitumaini,
Ng’ambo huko tutaona. :/: Heri tele, heri tele: ’ona raha ya
milele! :/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
264. E' MSAFIRI JANGWANI, TAZAMA JUU
1 E’ MSAFIRI jangwani, Tazama juu mbinguni! Hapo utaona
nyota Za faraja na tumaini.
Huko hutayaona Machozi wala shida. Mungu
atatuliza Msafiri mbinguni kwake.
2 Ukisumbuka gizani Katika pepo, dhoruba, Bado wakati
mfupi, Nuru itatokea tena.
3 Ukililia wapendwa Waliokutangulia, Utakutana na wote,
Hutalia machozi tena.
4 Na penye moyo wa Yesu Utastarehe daima, Hutakumbuka
mbinguni Shida, kufa na sikitiko.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
265. TU WASAFIRI, TWAKARIBIA NCHI
1 TU wasafiri, twakaribia Nchi ya mbingu kwa Mungu Baba.
Tusiogope bonde la kufa, Yesu atuongoza kwake!
:/: Tu wasafiri :/: Tutakutana nyumbani mwa Baba.
E’ Bwana Yesu, utuongoze, Tufike sote mbinguni!
2 Wengi katika wapendwa wetu Wamevuka mto wa kufa.
Walifuata mwito wa Mungu. Wakahamia nchi nzuri.
3 Katika mwendo wa duniani Walitazama Mwokozi wao, Na
waliacha mambo ya huku, Walipendeza Bwana Yesu.
4 Ndugu wapendwa, tuendelee, Hata ikiwa shida njiani! Yesu
ni njia, kweli, uzima; Tumfuate siku zote!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
266. AYALA NAYE ANAYO SHAUKU YA MAJI
1 AYALA naye anayo shauku Ya maji ya kisima; Na vivyo
hivyo ninaona kiu Kwa Mungu wa uzima.
Kama ayala aonavyo Shauku mito ya maji safi, Na
vivyo hivyo rohoni mwangu Naona kiu kwa Mungu
wangu.
2 E’ Mungu wangu, Mungu wa fadhili, Nakutafuta Wewe! Je,
nikuone lini kwa ’kamili, Niburudishwe nawe!
3 Nazifikiri siku za zamani Niliposhangilia. Nijaze tena raha
na amani, Nakutumainia!
4 Na usifadhaike moyo wangu, Amini Mungu wako! Fadhili
zake hata huko mbingu Zatosha sana kwako!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
267. BABA NAKUOMBA LEO NA MAPEMA
1 BABA, nakuomba leo na mapema: Niongoze pote kwa
mapito mema!
Baba yangu, sikiliza Ombi langu leo! Baba,
nakusifu! Unanisikia.
2 Nistahimilipo kazi za mchana, Unitie nguvu, nakuomba,
Bwana!
3 Hata jua kuchwa liagapo njia, Baba, nakuomba: Unilinde
pia!
4 Maadui wengi watuwindawinda, Kwa maisha yetu Mungu ni
mlinda.
5 Katika utoto na ujana tena, Na uzee pia: Omba, kesha,
shinda!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
268. E’ YESU, INGIA ROHONI KABISA
1 E’ YESU, ingia rohoni kabisa, Uniweke huru na kunitakasa,
Nipate kushirikiana na Wewe Katika mateso na raha daima!
:/: E’ Bwana, nijaze Upendo wa mbingu Nao
uthabiti, Niwe mshindaji! :/:
2 Siombi ufalme, siombi heshima, Naomba kupewa neema
daima, Nijue yakini ya Neno la Mungu: Mtoe miili na iwe
dhabihu!
3 Nishike rohoni, unichungulie, Na katika yote unisaidie,
Nipate kabisa kusudi na nia Kujitoa kwako, kukutumikia!
4 Hakuna la huku litanizuia Nisilingamane na Yesu Masiya.
Nitumainije kufika mbinguni Nisiposhiriki Mwokozi
mpendwa!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
269. KATIKA BONDE NA MILIMA
1 KATIKA bonde na milima, Kwa mataifa mahali pote,
Peleka Neno la wokovu! Msifu Yesu sana!
Msifuni Bwana, Msifuni Bwana! Na tangazeni
Neno lake, ’sifuni Yesu sana!
2 Mapema na jioni pia Hubiri Neno la Bwana Yesu! Tangaza
njia ya wokovu, Msifu Yesu sana!
3 Lo! Paradiso malaika Wanahimidi Mwokozi wetu. Tuimbe
nasi sifa yake, Tu’sifu Yesu sana!
4 Usiyeona kufa bado, Uipokee neema leo! Ujisafishe kati’
damu, Msifu Yesu Kristo!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
270. SIMAMA FANYA VITA PAMOJA NA MFALME
1 SIMAMA, fanya vita Pamoja na Mfalme! Bendera tuishike
Iliyo ya Mwokozi! Mwenyezi huongoza Majeshi yake huku.
Adui wote pia Washindwa mbele yake.
2 Sikia baragumu, Linatuita sasa! Tuendelee mbele, Kusudi ni
kushinda! Tusiogope kamwe Hatari ya shindano, Pigana na
adui kwa nguvu yake Mungu!
3 Simama, fanya vita Kwa jina lake Yesu! Hatuna nguvu sisi,
Tunamtegemea. Na kwanza tuzivae Silaha zake Mungu!
Tukeshe siku zote, Tuombe kwa bidii!
4 Shindano letu hapa ’takwisha siku moja; Twapiga vita leo,
Baada pumziko. Na kila mshindaji Atapokea taji, Na
utukufu tele Karibu na Mfalme.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
271. UWATAFUTE WENZAKO WAPOTEAO
1 UWATAFUTE wenzako Wapoteao mbali! Yesu mwenyewe
apenda Kuwaokoa wote.
Uwatafute wenzako Wapoteao mbali! Pasha
habari ya Yesu Na ya wokovu wake!
2 Uwatafute wenzako Kwa neno la upendo! Mungu atalibariki
na kulithibitisha.
3 Uwatafute wenzako Kwa ’jili ya Mwokozi! Aliwakomboa
wote, Ni mali yake kweli.
4 Uwatafute wenzako Kabla ajapo Yesu! Wasipotee kabisa,
Uwaokoe mbio!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
272. NANI NI WA YESU? AMTUMIKIE
1 NANI ni wa Yesu? Amtumikie! Atafute watu na kuwahubiri!
Nani anataka kujitoa leo, Kufuata Yesu katika mateso?
Nani ni wa Yesu? Amtumikie! Nani atakaye, na
amwitikie! Mimi ni wa Yesu, nimtumikie, Nitafute
watu, kwake warudie!
2 Kwa upendo wake tunalazimishwa Kutafuta wenye dhambi
na makosa. Tunaendelea kuwavuta kwake, Hata wanaomba:
Mungu tuokoe!
3 Yesu alitununua sisi sote Ju’ ya msalaba na kwa damu yake.
Kwake tumepata raha na uhuru; Tunataka sasa kuwa
waminifu!
4 Hata vita ikiongezeka huku Tunayo bendera ya kushinda
kwetu. Siku ya hatima inakaribia, Itaibadili vita iwe
shangwe.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
273. NI UHERI KUMWAMINI MUNGU
1 NI uheri kumwamini Mungu Kama Ibrahimu wa zamani.
Hakutiwa shaka kwa uchungu, Ila alitii kwa imani. Ni uheri
kuendea sawa Katika mapito ya sheria. Ukijaribiwa na
kukawa, Mwisho Mungu atakujalia.
2 Mashujaa wote wa Biblia Hawakufurahi kwa anasa.
Wakafunzwa kutumainia Mungu na uweza wake hasa. Tena
wakaenda kwa imani ya kutetemesha ulimwengu,
Wakashinda giza na Shetani. Sifa na heshima zina Mungu!
3 Yesu atakayekuzwa naye Kwanza adhiliwe kuwa vumbi;
Mwana wake mwema na ambaye Baba humpenda, humrudi.
Hivyo Mungu awakamilisha Watu wake kwa mateso huku,
Na zaidi kuwafahamisha Kulijua pendo lake kuu.
4 Na ikiwa raha ya dunia Yatoweka katika jaribu, Mwaminifu
atafurahia Mungu wake, kwani Yu karibu. Na mavuno ya
taabu yake Yakichomwa na kuharibika, Atategemea Bwana
wake, Na kwa hiyo hatanung’unika.
5 Jipe moyo, enyi kundi dogo, Na msiogope hatarini! Shika
Neno la Mwenyezi Mungu, Litawaongoza safarini! Haleluya,
kwani majaribu Yahimiza msafiri mwendo, Hata ataona
kwa karibu Mji wa amani na upendo!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
274. NINAFURAHIA KISIMA DAIMA
1 NINAFURAHIA kisima daima, Kisima cha damu ya Yesu.
Katika upendo nalindwa salama, Nasifu Mwokozi mpendwa.
Kisima cha maji kinabubujika, Kinaniletea uzima.
Na kando ya maji ninaburudika, Ninashangilia
daima.
2 Nakaa karibu ya kisima hiki, Naishi kwa maji ya ’hai.
Yananilietea kupita kipimo Uzima na shangwe rohoni.
3 Nakaa karibu na kisima hiki, Naishi katika uheri. Ufike
upesi uliye na kiu, Kisima kinabubujika!
4 Nakaa karibu ya kisima hiki, Naona furaha na raha. Na
kando ya maji nafasi kwa wote, Waweza kupona kabisa.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
275. E’ MUNGU MWENYE HAKI UNIONGOZE
1 E’ MUNGU mwenye haki, Uniongoze huku Katika mambo
yote Yanayokupendeza! Nikiwa huku bila Wewe, Vitisho,
hofu na mashaka Yananitia tetemeko mpaka kufa.
2 Ni heri siku zote Kutegemea Yesu Na kuenenda sawa Katika
nyayo zake, Kwa kuwa Yeye ni Mchunga Anayeniongoza
vema, Nipate kuingia katika raha yake.
3 Safari yangu sasa Yaelekea mbingu, Mwokozi yuko huko,
Lazima nifikeko Na siku nitakapofika ’tashangilia kwa
furaha Kuona Yeye aliyeninunua kwake.
4 Ulimwenguni humu, Matata na kuchoka. Nikihitaji kitu
Nafadhahika bure, Lakini siku ile kuu Nita’pomwona
Mkombozi, Natumaini sitakosa thawabu yangu!
5 Mbinguni sitaona Adui zangu tena. Hayatakuwa mambo Ya
kupokonya pale. Sauti nitamtolea, Kusema: Mungu,
Haleluya! Mikono nitaipepea kwa shangwe kuu!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
276. MATENDO YA MUNGU YAPITA FAHAMU
1 MATENDO ya Mungu yapita ’fahamu, Ni nani ayaona wazi?
Lakini najua mapito ya Mungu Kwa mimi yafaa halisi.
2 Njiani sijui maana ya yote, Lakini nitayafahamu. Kwa nini
kuzisumbukia kwa bure Taabu na shida za muda?
3 E’ Bwana, unayo magari maelfu, Na lenye linalonifaa,
U’lichagulie mwenyewe, Bwanangu, Nifike salama
mbinguni!
4 Na kama Elia upesi kabisa Nitakavyoacha dunia, Uchungu
na shida za huku ’takwisha, Milele nitashangilia.
5 Tutamsujudu Mwokozi daima, Kuimba maelfu pamoja: E’
Mungu, U haki na mwenye neema Katika shauri na tendo.
6 Halafu nangoja kwa uvumilivu Kujua maana kwa wazi. Na
matumaini ni yenye uzima: Urithi ninao mbinguni.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
277. NITAOGOPA NINI GIZANI DUNIANI?
1 NITAOGOPA nini gizani duniani? Sikuachiwa peke’ mbali ya
tumaini! Mwokozi Yu karibu, asiyebadilika. :/: Hutunza
ndege ndogo na mimi kadhalika :/:
Namshukuru Mungu asiyebadilika. Hutunza ndege
ndogo na mimi kadhalika.
2 “E’ usifadhaike moyoni mwako, mwana”, Anong’oneza
Yesu, “Nitegemee sana!” Na hapo woga wangu waruka kwa
hakika. :/: Hutunza ndege ndogo na mimi kadhalika:/:
3 Na nikijaribiwa na jua lifichwapo, Hata sioni raha, wala
faraja hapo, Nakimbilia Yesu, na yote yapinduka. :/:
Hutunza ndege ndogo na mimi kadhalika :/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
278. NINAINUA MACHO YANGU KWA MUNGU
1 Ninainua macho yangu Kwa Mungu aketiye juu, Aliye
msaada wangu, Njiani pangu nuru kuu. Aliyefanya vyote,
Maombi huyasikia. Katika njia zangu zote Atanilinda pote
pia.
2 Bwanangu asiache tena Mguu wangu usogezwe, Kwa kuwa
ni Mlinzi mwema, Naye hatasinzia kamwe. Alinda roho
yangu Nisije nikapotea. Hitaji za maisha yangu Baraka yake
ya’enea.
3 Aniokoa na uovu, Na roho yangu imepona. Kwa Yeye nguvu
na wokovu, Nilizionja naku’ona. Ananilinda pote: Kutoka
na kuingia; Anijaliza mema yote Nikiwa kutumainia.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
279. UPENDO WAKE MUNGU UNATUUNGANISHA
1 UPENDO wake Mungu Unatuunganisha. ’shirika wa
watakatifu — Uheri wa mbinguni.
2 Katika sala zetu Twakaribia Baba Kwa tumaini, ujasiri Na
kwa imani moja.
3 Upendo wa kikristo Ha’vunji urafiki. Twalia naye wa
uchungu, Furaha twa’shiriki.
4 Tunaachana huku Kwa sikitiko sana. Kwa shangwe tena
kwake Mungu Twaweza kuonana.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
280. JINA LAKE YESU KRISTO LINADUMU
1 JINA lake Yesu Kristo Linadumu siku zote; Jina hili la
milele Haliwezi kunyauka; Linafaa watu wote, Na wazee na
vijana; Linaweza kuongoza Kila mtu kwake Mungu.
Jina hili nalipenda, Limewasha moyo wangu; Na
kwa jina hili jema Nimepata kuokoka.
2 Jina hili linavuma Pande zote za dunia, Na kwa wote linaleta
Tumaini na faraja. Jina hili laondoa Machukio na ubaya,
Hata milki ya Mwokozi itaanza kutawala.
3 Na katika giza huku Jina hili linang’aa, Laonyesha msafiri
Njia wazi ya uzima. Jua likitiwa giza, Jina hili litadumu; Na
milele lisifiwe Hapa na mbinguni juu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
281. YOTE NINAYO NILIYAPOKEA KWA WEMA
1 YOTE ninayo niliyapokea Kwa wema wake unaonea. Nasifu
Yesu, namtegemea, Aliniokoa kwa neema.
Niliyekuwa nimetoroka, Kwa pendo lake
nimeokoka. Yesu Yu mwema Na mwenye rehema,
Nimeokolewa kwa neema!
2 Nilitembea zamani dhambini Katika njia ya kufa, lakini
Yesu alinitafuta porini, Akaniokoa kwa neema.
3 Natakasiwa na Yesu Mwokozi, Si kwa majuto na si kwa
machozi, Bali kwa damu, ninao ’kombozi; Nimeokolewa kwa
neema.
4 Raha ya mbingu imeniingia, Kwa shangwe kubwa
ninafurahia Yesu, kwa kuwa anirehemia; Nimeokolewa kwa
neema.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
282. UKIONA KIU SANA UJALIVU WA MWOKOZI
1 UKIONA kiu sana ujalivu wa Mwokozi, Roho yake safi pia,
Liamini Neno la Babako na atakujazi, Nawe utashangilia.
Atakujaliza hata utashiba. Bwana Yesu akuita:
‘‘Njoo bila ’sitasita!’’ Atakujaliza hata utashiba
Roho na uwezo wake.
2 Vichukue vyombo vyako, uvioshe safi sana Kisimani pa
Golgotha! Afadhali kujitoa lote kwa Mungu Bwana, Na
imani itaota.
3 Na mafuta ya neema hayakomi. Asifiwe! Tunakuwa na
shukrani! Anataka kumimina Roho ya ahadi yake. Mpokee
kwa imani!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
283. NIMEYASIKIA MENGI ALIYOYAFANYA
1 NIMEYASIKIA mengi aliyoyafanya Yesu Katika maisha
yake huku chini: Pote alitenda mema, alisaidia wote. Kwa
furaha ninaimba: ‘‘Yesu Yeye yule leo!’’
Yesu Kristo Yeye yule Jana, leo, siku zote.
Hutafuta wapotevu, Huokoa na waovu. Mwokozi
wetu Yeye yule!
2 Na kipofu yule, jina lake ndilo Bartimayo, Aliposikia Yesu
Yu karibu, Kwa imani akaomba, akapona kwa neema.
Nafurahi kwa kuimba: ‘‘Yesu Yeye yule leo!’’
3 Watu wote wenye dhambi na wagonjwa na maskini
Wanaitwa kwake Yesu kwa rehema. Uiguse nguo yake, sawa
mwanamke yule, Utapewa nguvu yake, Kwani Yesu Yeye
yule!
4 Nimeyasikia tena jinsi alivyoombea Maadui wake ju’ ya
msalaba. Aliteswa kwa miiba, aliona maumivu. Ninaimba
kwa furaha: ‘‘Yesu Yeye yule leo!’’
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
284. USIMTAFUTE YESU KATI' WAFU
1 USIMTAFUTE Yesu Kati’ wafu kaburini! Yu mzima,
tumsifu, Hakushindwa na kuzimu! :/: Yesu hai, Yesu hai,
Mshindaji wa mauti! :/:
2 Maadui walifunga Bwana Yesu kaburini, Mungu alimfufua
Mwana wake. Furahini! :/: Yesu hai, Yesu hai, Imba hivyo
duniani! :/:
3 Yesu hai, ni habari Ya kupasha pande zote. Yu Mwokozi
wetu kweli, Alitufilia sote. :/: Yesu hai, Yesu hai, Mkombozi
asifiwe! :/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
285. NENO LA MUNGU NDANI YA BIBLIA
1 NENO la Mungu ndani ya Biblia Limetolewa na Mwenyezi
Mungu. Biblia yetu inatuambia: Njoo kwa Yesu, Mkombozi
wetu!
Neno la Mungu tulilolipewa, Njia ya mbingu
limetuonyesha; Nuru gizani ya kutuongoza Katika
mwendo wetu kwenda mbingu.
2 Siku za giza zinakaribia, Kama walivyosema manabii. Biblia
yetu itatuangaza Na kutuonya njia hata mwisho.
3 Katika Neno la Biblia yetu Tunaupata utajiri wote. Mbingu
na nchi zitaangamia, Neno la Mungu litashinda yote.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
286. YESU, ULIKARIBISHWA ARUSINI
1 YESU, ulikaribishwa Arusini huko Kana; Hapo
ikadhihirishwa Nguvu yako kwa ishara.
2 Leo tunakuhitaji, Wabariki ndugu hawa: Bwana na bibi-
arusi! Ndoa yao iwe sawa!
3 Katika taabu, raha Wafungane kwa upendo! Watumike kwa
furaha, W’andamane kati’ mwendo!
4 Yesu, U mlinzi wao, Uwalinde na mabaya! Uhifadhi nyumba
yao! Tunaomba mema haya!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
287. TUNAMTIA MIKONONI MWAKO MTOTO
1 TUNAMTIA mikononi mwako Mtoto huyu, umtunze sana,
Na kila siku kwa neema yako Umbariki, Bwana Yesu Kristo!
2 Ulimwenguni kuna majaribu Mahali pote, shida na mitego.
Lakini uwe mchungaji wake, Na umwongoze, E’ Rafiki
mwema!
3 Mwokozi kwa upendo ’mchukue, Asije akashindwa safarini!
Na umlinde kwa rehema yako, Apate kuwa wako siku zote!
4 Utume nuru ya neema kwake Na maji ya uzima toka kwako
E’ Bwana Yesu. Twakuomba Leo ulinde mwana wetu kwa
salama.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
288. MUNGU WETU, UTULINDE
1 MUNGU wetu, utulinde Na utubariki sote! Bwana,
uturehemie, Tutolee nuru pote! Utuangazie uso, Tupe na
amani yako! Mungu Baba, Roho, Mwana, Tunakushukuru
sana!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
289. NINATAMANI KWENDA MBINGU
1 NINATAMANI kwenda mbingu nchi yangu Niliyopewa na
Mungu kwa imani. Ni shangwe bora kuona mji ule; Kwa
kwenda kule sitaogopa kitu.
E’ Baba yangu, niongoze, Unisafishe kwa damu ya
Mwokozi! Nifananishwe na theluji, Unibatize kwa
Roho ’takatifu!
2 E’ Mungu, tumepata Mwana Yesu Kristo, Kipawa kweli
kinachoshinda yote. Anahubiri amani kwao wote Walio
huku karibu, nao mbali.
3 Kwa Yesu tumepata mwisho wa upendo Na njia ya
kumwendea Baba Mungu. Si wapitaji na tena si wageni,
Tunatumika kwa roho ya upendo.
4 Amani kwetu na matumaini tele, Salamu toka kwa Mungu
wa milele Ni posho ya watumishi wa upendo; Tunaurithi
uzima wa milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
290. BARAGUMU LITALIA SANA
1 BARAGUMU litalia sana, Watu wote watalisikia. Waliokufa
watafufuka Na wazima watabadilika. :/: Nani anayeweza?
Yesu, Mweza yote. :/:
2 Na wenye uwezo wa dunia Watatetemeka siku ile, Na
hawataweza kuinuka Kutazama uso kama jua. :/: Nani
anayeweza? Yesu, Mweza yote. :/:
3 Najua Mchunga wangu mwema, Anichunga kwa maisha
yangu. Na siku ya mwisho nikishinda, Sitaona uchungu wa
kufa. :/:Nani Mchunga mwema? Yesu, Mweza yote. :/:
4 Mbinguni hakitafika kitu Cha uchafu, dhambi na kuasi.
Wasiomwamini Bwana Yesu, Gadhabu ya Mungu
yawangoja. :/: Nani atahukumu? Yesu, Mweza yote. :/:
5 Mimi Yesu mzabibu kweli, Baba Mungu ndiye mkulima, Na
ninyi matawi ndani yangu, Na hamwezi neno bila mimi. :/:
Nani ni mzabibu? Yesu, Mweza yote. :/:
6 Unayempenda Baba Mungu, Lazima upende ndugu yako;
Ukiwa hupendi ndugu yako, Huwezi kupenda Baba Mungu.
:/:Nani aliyesema? Yesu, Mweza yote. :/:
(voir la suite sur la page suivante)
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
7 Nawapenda, mwisho wa upendo, Na ninyi mpate kupendana;
Hivyo mataifa wataona Ya kwamba m watu wangu kweli. :/:
Nani mwenye upendo? Yesu, Mweza yote. :/:
8 Sisi watumishi wake Mungu Tu watu maskini kati’ yote.
Tutakapowekwa pa kuume Kelele la sifa litashinda. :/:
Tutamsifu nani? Yesu, Mweza yote. :/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
291. MIMI MWENYE HATIA NILIKOMBOLEWA
1 MIMI mwenye hatia nilikombolewa, Mwokozi alipojitoa.
Dhambi zangu na zako alizichukua, Kwa damu aliniokoa.
Dhambi zimetundikwa msalabani Alipojitoa,
Mwokozi. Alidharauliwa na kukataliwa
Atupatanishe na Mungu.
2 Yesu mwenye upole na mwenye upendo Ananitakasa rohoni.
Nimepata uhuru kwa Yesu Mwokozi, Alikufa msalabani.
3 Namwambata Mwokozi, sitaki kumwacha, Kwa kuwa
alinifilia. Nakusifu, E’ Yesu, unayenipenda, Daima
nakushangilia.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
292. KATIKA DAMU TAKATIFU YA MWOKOZI
1 KATIKA damu takatifu ya Mwokozi wangu Nimesafishwa.
Na nguvu ya Mwokozi wangu tu Yaweza kunilinda safi.
Mungu ahimidiwe, Mungu ashukuriwe Kwa ajili
ya wokovu na nguvu ya kushinda! Mungu
ahimidiwe, Mungu ashukuriwe Kwa ajili ya
wokovu wake!
2 Kwa wingi wa neema yake tu Nimeokoka, nimeokoka.
Wokovu ni kwa ’jili yako na Kwa kila ’aminiye kweli.
3 Kwa nguvu yangu sitashinda na Siwezi neno, Siwezi neno.
Ninajuliwa na Mwokozi na Atanisaidia pote.
4 Babangu mwema anipenda na Ananilinda, Ananilinda.
Sitaogopa giza huku kwa Maana Yu pamoja nami.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
293. NCHI NZURI YA RAHA AJABU
1 NCHI nzuri ya raha ajabu, Kwa imani twaona si mbali. Baba
atungojea sababu Ametuandalia mahali.
:/: Tukutane sisi sote Huko juu nyumbani mwa
Baba! :/:
2 Huko juu kwa raha, amani Tutaimba na kushangilia,
Kutolea Mwokozi shukrani Kwa sababu alitufilia.
3 Baba wetu mpendwa na mwema Kwake kuna furaha ya tele.
Twamsifu kwa kuwa neema Yatutosha kabisa milele.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
294. UTUME ROHO YAKO JUU YETU
1 UTUME Roho yako juu yetu Kama ulivyofanya hapo kale!
:/: Uwashe moto wako ndani yetu, Tusiwe watu wa
uvuguvugu! :/:
2 Utume Roho yako juu yetu Kama ulivyofanya siku ile. :/:
Mtume Petro alipohubiri Katika nyumba yake Kornelio! :/:
3 Utume Roho yako juu yetu, Utupe nasi Pentekoste yetu! :/:
Maelfu wenye dhambi waokoke, Na Neno lako lienee pote!:/:
4 Utume Roho yako juu yetu! Mikono yako uinyoshe sasa,:/:
Ishara za ajabu zifanyike, Wagonjwa uwaponye kati yetu! :/:
5 Uwaamshe waliosinzia, Waliochoka huku safarini! :/: E’
Bwana utujie kama kale Ulivyowabariki watu wako! :/:
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
295. E’, FURAHINI WATU WAKE MUNGU
1 E', furahini watu wake Mungu! Mwokozi wetu alituokoa.
Neema kubwa, pendo la ajabu! Tusifu Mungu sana siku zote!
E’ Mungu ana mamlaka yote, Ni ngao na
makimbilio yangu; Ni Baba yangu, na anasikia
Maombi yangu. Asifiwe!
2 E’, furahini watu wake Mungu! Tuimbe nyimbo za furaha
nyingi! Tusiogope ila tumwamini Na twende mbele kwa
uweza wake!
3 E’, furahini watu wake Mungu! Tukimshangilia Mungu
wetu, Jirani zetu wasioamini Watatamani kumjua Yesu.
4 E’, furahini watu wake Mungu! Mfalme wetu Yu pamoja
nasi. Kitambo bado — na tutahamia Mbinguni kwake
Mkombozi wetu.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
296. DHAMBI, HATIA ZIMEONDOLEWA
1 DHAMBI, hatia zimeondolewa, Yote ya kale yamepita sasa.
Damu ya Yesu imenisafisha; Ninamfurahia Mkombozi
wangu.
Mavazi safi na kao nzuri Ninayo huko ju’
mbinguni. Thawabu nita’pewa huko, Ni taji ya
uzima. Na Yesu ni Mwokozi wangu. Alinikomboa,
Alilipa deni langu. Pendo lake kubwa Nina’sifu
siku zote, Ninamfurahia Mkombozi.
2 Siku za nung’uniko zimekwisha, Nimeokoka katika utumwa.
Sasa naona raha na furaha Sababu Bwana Yesu
alinikomboa.
3 Shaka na hofu zimeondolewa, Na siogopi kufa kwangu tena.
Katika Yesu nina tumaini, Na ninalindwa vema naye
sikuzote.
4 Roho ya Mungu amenijaliza, Anifariji katika mwenendo.
Yesu Mwokozi Yu karibu nami, Aliye ngao yangu na
makimbilio.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
297. NIPE SAA MOJA NAWE YESU
1 NIPE saa moja nawe Yesu Nikichoka huku duniani! Hata
nikiona vita kali, Wanistarehesha sikuzote.
Nipe saa moja nawe Yesu, Kwani giza iko duniani!
Natamani kukukaribia, Kusikia Neno lako zuri.
2 Nipe saa moja nawe Yesu Katika jaribu na taabu! U
makimbilio yangu mema Katika hatari na ghasia.
3 Nipe saa moja nawe Yesu Uliyechukua dhambi zangu.
Ninataka kueleza yote, Kwani unanifahamu sana.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
298. NINAO WIMBO WAKUNIFURAHISHA
1 NINAO wimbo wa kunifurahia Wa Mwokozi, wa Mwokozi.
Namshukuru kwa roho yote pia, Mwokozi mzuri ninaye!
Mwokozi — wimbo wangu, Mwokozi, Mwokozi!
Mahali pote na siku zote Nitamsifu Yesu kati’ yote.
Mwokozi ni wimbo wangu Wa huku na Mbinguni.
2 Na jina moja ni lenye pendo tele: Yesu, Yesu, ndilo jina!
Anipa yote niliyokosa mbele, Mwokozi mzuri ninaye.
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
299. JE, UMELISIKIA JINA ZURI
1 Je, umelisikia jina zuri, Jina la Mwokozi wetu? Linaimbiwa
duniani pote Na katika watu wote.
Yesu, jina hilo linapita Majina yote kwa uzuri! Ni
lenye nguvu ya kutuokoa Na hatia na makosa.
2 Linafariji moyo wa huzuni, Latutia raha kuu. Katika shida
na hatari huku Jina hili latulinda.
3 Katika giza huku jina hili Linang’aa kama nyota, Lanipa
utulivu na ’hodari Siku zote hata kufa.
4 Majina yote yasahauliwa, Ila jina lake Yesu Milele litang’aa
huko juu. Yesu, jina nzuri mno!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
300. MUNGU AWABARIKIE NYOTE
1 MUNGU awabarikie nyote Na awe pamoja nanyi! Awalinde
kwa amani! Mungu n’ awe nanyi siku zote!
Mungu n’ awe nanyi dahari Hata mwisho wenu wa
safari! Mungu n’ awe nanyi dahari Hata tuonane
huko juu!
2 Mungu wetu awalinde pote Na kuwahifadhi vema Kwa
mikono ya rehema! Mungu n’ awe nanyi siku zote!
3 Mungu awaangazie nuru, Na awashibishe sana Kwa fadhili
zake Bwana! Mungu n’ awe nanyi siku zote!
4 Mungu awainulie uso! Na wakati wa kuhama Mpelekwe kwa
salama! Mungu n’ awe nanyi siku zote!
5 Mungu awabarikie nyote, Awalinde mwe huru, Awaangazie
nuru! Awainulie uso wake!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
ORDRE NUMERIQUE
1 à 140
141 à 280
281 à 327
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
1 à 140
1 2 3 4 5 6 7 8 9 10
11 12 13 14 15 16 17 18 19 20
21 22 23 24 25 26 27 28 29 30
31 32 33 34 35 36 37 38 39 40
41 42 43 44 45 46 47 48 49 50
51 52 53 54 55 56 57 58 59 60
61 62 63 64 65 66 67 68 69 70
71 72 73 74 75 76 77 78 79 80
81 82 83 84 85 86 87 88 89 90
91 92 93 94 95 96 97 98 99 100
101 102 103 104 105 106 107 108 109 110
111 112 113 114 115 116 117 118 119 120
121 122 123 124 125 126 127 128 129 130
131 132 133 134 135 136 137 138 139 140 NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
141 à 280
141 142 143 144 145 146 147 148 149 150
151 152 153 154 155 156 157 158 159 160
161 162 163 164 165 166 167 168 169 170
171 172 173 174 175 176 177 178 179 180
181 182 183 184 185 186 187 188 189 190
191 192 193 194 195 196 197 198 199 200
201 202 203 204 205 206 207 208 209 210
211 212 213 214 215 216 217 218 219 220
221 222 223 224 225 226 227 228 229 230
231 232 233 234 235 236 237 238 239 240
241 242 243 244 245 246 247 248 249 250
251 252 253 254 255 256 257 258 259 260
261 262 263 264 265 266 267 268 269 270
271 272 273 274 275 276 277 278 279 280 NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
281 à 327
281 282 283 284 285 286 287 288 289 290
291 292 293 294 295 296 297 298 299 300
301 302 303 304 305 306 307 308 309 310
311 312 313 314 315 316 317 318 319 320
321 322 323 324 325 326 327
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
ORDRE ALPHABETIQUE
A B C D E F H I J K M
N O P R S T U V W Y Z
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
TITRES DES CANTIQUES
A
ABUDU MUFALME
ASANTE, EE MUNGU
ASKARI WA MWOKOZI
ASKARI WAHODARI
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
B
BABA WANGU MUFALME
BIBLIA INASIMAMA SANA
BONDE LA MAUTI
BWANA, FUNGUA MACHO YANGU
BWANA, KWA USIKU HUU
BWANA, MUFALME WA UZIMA
BWANA, NINAKUNGOJEA
BWANA, SASA URUHUSU
BWANA, UPOKEE MAISHA YANGU
BWANA YESU ALIKUJA
BWANA YESU AMESEMA
BWANA YESU ANAITA WATU
BWANA YESU ATAKUJA
BWANA YESU UNIONGOZE
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
C
CHINI YA BENDERA YAKE YESU
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
D
DAMU YA KRISTO IMENIOKOA
DAMU YAKO YENYE BARAKA
DUNIA ’NALALA
DUNIA YA ZAMBI HAILETI FURAHA
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
E
EE ASKARI, TWENDE
EE BENDERA INATWEKA
EE BABA, NITAKUWA KAMA YESU
EE BWANA, NIWE MUFUATA WA KWELI
EE BWANA, TUNASIFU MAPENDO YAKO
EE BWANA, ULIVUMILIA
EE BWANA YESU, MWUMBA WA DUNIA
EE FURAHA KUONANA
EE KRISTO, KWAKO ROHO YANGU
EE KUJA, MUTU WA MAKOSA
EE KUNDI LA MUNGU, MUSIYAOGOPE
EE MARA NGAPI TUNASUMBUKA
EE MUJI WA BETELEHEMU
EE MUNGU BABA, NINAKUTUKUZA
EE MUNGU NDIYE NGUVU YETU
EE MWOKOZI, UNILINDE
EE NINAKUPENDA
EE NINATAKA KUSIKIA
EE NINI, MUNGU WETU
EE NITAKIMBIA KWA MWAMBA
EE SALAMA YA MILELE
EE SIKU YA KUOKOLEWA
EE SIKU YA PUMZIKO
EE, TARAJA YAKO NI WAPI
EE YEHOVA, MUNGU WANGU
EE, YESU ATAKUJA TENA
EE YESU, NATAKA USAFI KWA ROHO NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
F
FANYA MAPENZI
FANYIA MUNGU KAZI
FURAHA KUBWA KUTANGAZA SIFA
FURAHA KUBWA KWA DUNIA
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
H
HAKIKA YESU MWAMBA NGUVU
“HAKOSE KESHO NITA-AMINI
HAKOSE LEO TU
HAKUNA RAFIKI KAMA YESU
HATA JUMA HILI, BWANA
HATA NINALIA
HATA TANGU ZAMANI
HATUA MOJA INAKUTENGA NA MWOKOZI
HERI KABISA
HESHIMA NA SIFA
HUZUNI YANGU NI KITU KWELI
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
I
IMBA NENO LA MUNGU
IMBA PENDO LA MWOKOZI
INATUSHINDA KUFAHAMU
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
J
JESHI KUU LA MALAIKA
JINA LA PENDO KUBWA
JINA LAKE YESU KRISTO
JUA LA ROHO
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
K
KAMA UKITAKA
KAMA ULIVYOAGIZA, BWANA
KAMA UNA MAHITAJI
KATI’ MIKONO YAKE YESU
KIONGOZI, MWANA WA MUNGU
KISIMA CHENYA DAMU SAFI
KITU KISI-INGIE
KRISTO ALIACHA UTUKUFU
KUJA KWA YESU
KUJA, MUFALME WETU
KUJENI KUSIFU NA FURAHA
KUKUFIKILI WEWE, YESU
KULE MUJI WA DAUDI
KUNA MUJI KULE MBINGU
KUNA MUJI MUZURI MBINGUNI
KUNA MUJI WA FURAHA
KUNA WIMBO MUZURI
KUTOKA TAABU YA DUNIA
KUTUMIKA KAZI KWA MWOKOZI
KWA KILIMA CHA KALVARI
KWA KONDO-O TUNAPUMZIKA
KWA MUKATE NA KWA MVINYO
KWA MUNGU MUJU-U
KWA PENDO LAKE KUBWA
KWA USIKU WA ZAMANI
KWAKO HESHIMA
KWAKO PEKEE, BWANA, NI SALAMA TAMU
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
KWAMI MUCHUNGAJI NI BWANA YESU
KWELI MAJI HAYAWEZI
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
M
MAISHA NA MAPENDO YANGU
MALAIKA ZA MBINGUNI
MANENO YA MUNGU NI TA-A
MAPENDEZI YA DUNIA
MAPENDO YAKE MUNGU
MATESO MENGI DUNIANI
MATESO YANAKUSUMBUSHA
MIMI MWENYE MAKOSA
MIMI WAKO, BWANA
MOYO ULIGEUZWA NA VILE MAISHA
MOYO WANGU UNA WIMBO LEO
MUCHUNGAJI YESU
MUFALME WA MAPENDO
MUFALME WA UTUKUFU
MUGANGA AMEKUJA
MUKATE WA UZIMA, BWANA
MUMUFANYIE BWANA SHANGWE
MUMUKARIBIE MUNGU
MUNGU ALIPOSIFIWA MBINGUNI
MUNGU AWE NANYI SIKUZOTE
MUNGU MUTAKATIFU
MUNGU NI PAHALI POTE
MUNGU, UMETUMA KWETU ROHO
MUNGU WETU MWAMINIFU
MUSIFU MUNGU KWA BARAKA
MUSINGI WA KANISA
MUSINGI WA NGUVU NI YESU
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
MUTAZAME UTUKUFU WA MWOKOZI
“MUTU WA MASIKITIKO”
MVUA YA MBINGU INYESHE
MWAMBA ULIOPASUKA
MWENYE KUSIKIA
MWOKOZI ALIAHIDIA
MWOKOZI ALINIAMBIA
MWOKOZI ALITUKUFIA
MWOKOZI ANAISHI
MWOKOZI ANANIONGOZA
MWOKOZI WANGU ALINIMWANGIA DAMU
MWOKOZI WETU NA MUPENZI
MWOKOZI YESU ALIKWENDA
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
N
NA HALI YANGU NINAKUJA
NAFSI YANGU, ANGALIA YESU
NAJUA JINA MOJA ZURI
NAJUA YESU ANAISHI
NAKUHITAJI, YESU
NANI ANAYENINYANYUA?
NANI NI WA YESU?
NAONA SASA DAMU YA KONDO-O
NAPENDA KUIMBIA BWANA SIFA
NAPENDA KUSIKIA JINA LA BWANA
NAPENDA KUSIKIA
NAPENDA KUTANGAZA
NASIKIA BWANA YESU
NASIKIA, BWANA YESU
NATAKA SANA KUSIKIA
NAVUTWA KWAKE YESU
NE-EMA, NENO TAMU
NEEMA YA BWANA NI KUBWA SANA
NENO TAKATIFU SANA NI BIBLIA
NI AHADI YA MUNGU
NIKUTAMU SANA KWANGU
NI NEEMA YA KUNISHANGAZA
NI TAMU SANA JINA LA MWOKOZI
NIKIONA UZAIFU NA IMANI NDOGO
NIKIPATA ULIMWENGU WOTE
NILIKUBALI KUTOA UZIMA WANGU
NILIPOFIKA KWA MUSALABA
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
NILIPOSIKIA YESU AKI-ITA
NILIZAMA KWA MAKOSA
NIMEAHIDI, YESU
NIMEKOMBOLEWA KABISA
NIMEPATA SALAMA
NINA MWOKOZI ANAYENIOMBEA
NINA NENO TOKA BWANA
NINA RAFIKI MWEMA
NINA USHIRIKI NA FURAHA KUBWA
NINAFIKILI, MUNGU BABA WANGU
NINAFURAHI SABABU MWOKOZI
NINAHESHIMU YESU KRISTO
NINAJUA RAFIKI MWEMA
NINAKARIBIA SASA
NINAKUOMBA, MUNGU BABA
NINAKUOMBA, YESU MUPENZI
NINAKUOMBA, YESU
NINAKUSHUKURU, BWANA
NINAKUSIKIA, BWANA
NINAKUTA BWANA YESU
NINAKUTOLEA, BWANA
NINANGOJA ASUBUI
NINAPENDA KUMUSIFU BWANA YESU
NINAPO-ONA MWOKOZI WA WATU
NINASHANGA-A KABISA
NINASIKIA MUCHUNGAJI
NINASIMAMA KWAKE KRISTO
NINATAKA BWANA YESU
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
NINATAKA KUMUFUATA YESU
NINATAZAMA MBINGU MBALI
NINATIMIA NDANI YAKO
NINI ITANISAFISHA?
NISADIKI YESU KRISTO SIKUZOTE
NITAFIKA KWAKE BWANA
NITAIMBA NA KUSIFU
NITASIFU MUKOMBOZI
NIWE KARIBU NAWE
NJIA YOTE NAONGOZWA
NYUMBANI MWA NGOMBE
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
O
OMBA, OMBA KWA MUNGU PEKEE
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
P
PAHALI PA SALAMA TAMU
PAHALI POTE NINAPOKWENDA
PANDA MBENGU NJEMA
PASHA HABARI ZA YESU
PENDO LA BABA WA MBINGU
PENDO LA MUNGU NI KUBWA
PENDO LA MUSHANGAO
PENDO LAKO, BWANA YESU
PENDO LILIKUSUKUMA
PIGA MAKENGELE
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
R
RAFIKI, MUYASIKILIZE
RAFIKI WA WATOTO
REHEMA YA KUHANI WETU
ROHO YANGU INAJA-A NA FURAHA
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
S
SAA YA MAOMBI
SAFARI YANGU HUKO
SASA MANGARIBI
SEMA NA ROHO YANGU
SHAMBA LA MUNGU NI TAYARI
SIFA KWA BWANA, MWENYEZI
SIFU! SIFU!
SIFURAHI KWA MALI YA DUNIA
SIKU BARAGUMU YAKE MUNGU
SIKU MATESO YATAKAPOKWISHA
SIKU MWANA WAKE MUNGU ATAKAPORUDIA
SIKU NYINGI NILIFANYA ZAMBI
SIKU NYINGINE TAABU ’TAKWISHA
SIKU ZANGU ZITAKAPOTIMIA
SIMAMA KWA MUFALME
SINA AKILI NYINGI KUFAHAMU
SINA WOGA KWENDA NA MWOKOZI
SISI NI HURU
SIWEZI MIMI KUFAHAMU SANA
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
T
TAMU SANA NI MANENO YA HABARI NJEMA
TANGAZA NENO HILI
TAZAMA YESU NI KONDO-O
TOKA GIZA
TUKIKWENDA PAMOJA
TUMEPATA NENO ZURI
TUNAFURAHI LEO
TUNAIMBA SASA NYIMBO KWAKE YESU
TUNAKUSHUKURU, MUNGU
TUNAPENDA SAA HII TAMU
TUNASIFU BWANA YESU
TUNATAKA KUPA KWAKO SIFA
TUNAZIKWA KWA KABURI LA MWOKOZI
TUNAZUNGUKA MEZA
TUSIFU JINA LAKE YESU
TUSIFU MUNGU WA MBINGUNI
TUTAFUFUKA KUSIMAMA
TUWAZE MUNGINI WA MBINGU
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
U
UCHUNGE WAKATI
UKAE NAMI
UKAE SIKUZOTE KWAKE YESU
UKICHUKULIWA NA MASHAKA YAKO
ULIACHA MBINGUNI NA UTUKUFU
ULIAGIZA, YESU BWANA
UMEKUJA KWAKE YESU
UMESOMA HABARI ZA MUSALABA
UNACHOKA KWA MATATA
UNACHOKA, UNA ROHO NZITO,
UNAKUBALI KUACHA MAKOSA?
UNATAKA SALAMA
UNIPE USAFI ZAIDI ROHONI
UNITEMBEZE, BWANA WANGU
USIACHE ZAMBI
USIKIE BWANA YESU
USIKIE YESU KRISTO
USIMAME KWA AHADI ZAKE
USIMAME NA PIGA BARAGUMU
USIOGOPE MATESO YAKO
UTAFURAHI KUWA NA UHURU?
UTAZAME BWANA YESU
UTAZAME MWOKOZI
UWATAFUTE WANAOPOTEA
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
V
VIKA MWOKOZI TAJI
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
W
WACHUNGA WALILINDA KUNDI
WACHUNGA WALILINDA KUNDI
WAISRAELI KULE KWA MISRI
WAKATI SALAMA INAPOJAZA ROHO
WANANIAMBIA HABARI ZA MBINGUNI
WATU WA KRISTO, ANGALIENI
WATU WA MAKOSA
WATU WA MUNGU, MUMALIZE KAZI
WATU WANAKUZARAU
WEKA MAKUSUDI MEMA
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
Y
YESU ALINIOKOA TOKA ZAMBI
YESU ALIPOLALA
YESU AMEFUFULIWA
YESU ANA PENDO KUBWA
YESU ANAPENDA KWELI
YESU ANATAKA TUNGAE
YESU ATAKAPOKUJA TENA
YESU ATATAWALA HAPA
YESU KWA MUJI WA BETELEHEMU
YESU, MUCHUNGAJI WETU MWEMA
YESU, MWANZO WA UZIMA
YESU, MWENYE PENDO KUBWA
YESU MWOKOZI ALINIKUFIA
YESU MWOKOZI ANAITA WATU
YESU MWOKOZI, MWANA WAKE MUNGU
YESU MWOKOZI NATAKA
YESU MWOKOZI WETU MWEMA
YESU NI RAFIKI YANGU
YESU NI RAFIKI YETU
YESU, NINAKUTOLEA
YESU, NINAUCHUKUA MUSALABA
YESU, NIVUTE KARIBU NAWE
YESU, UNAPITA NDUGU
YESU UNAYENIPENDA
YESU UNITAZAMISHE
YESU, YESU, YESU, JINA TAMU SANA
YOTE KWA MWOKOZI WANGU
YOTE NINAYO NILIYAPOKEA NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
Z
ZAHABU NA FEZA
ZAMANI MUKE MWENYE UGONJWA
ZAMANI MWOKOZI ALIWAKARIBISHA
ZAMANI NILI-ISHI KWA ZAMBI
ZAMANI, PENTEKOTE
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
ORDRE NUMERIQUE
1 à 140
141 à 280
281 à 300
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
1 à 140
1 2 3 4 5 6 7 8 9 10
11 12 13 14 15 16 17 18 19 20
21 22 23 24 25 26 27 28 29 30
31 32 33 34 35 36 37 38 39 40
41 42 43 44 45 46 47 48 49 50
51 52 53 54 55 56 57 58 59 60
61 62 63 64 65 66 67 68 69 70
71 72 73 74 75 76 77 78 79 80
81 82 83 84 85 86 87 88 89 90
91 92 93 94 95 96 97 98 99 100
101 102 103 104 105 106 107 108 109 110
111 112 113 114 115 116 117 118 119 120
121 122 123 124 125 126 127 128 129 130
131 132 133 134 135 136 137 138 139 140 NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
141 à 280
141 142 143 144 145 146 147 148 149 150
151 152 153 154 155 156 157 158 159 160
161 162 163 164 165 166 167 168 169 170
171 172 173 174 175 176 177 178 179 180
181 182 183 184 185 186 187 188 189 190
191 192 193 194 195 196 197 198 199 200
201 202 203 204 205 206 207 208 209 210
211 212 213 214 215 216 217 218 219 220
221 222 223 224 225 226 227 228 229 230
231 232 233 234 235 236 237 238 239 240
241 242 243 244 245 246 247 248 249 250
251 252 253 254 255 256 257 258 259 260
261 262 263 264 265 266 267 268 269 270
271 272 273 274 275 276 277 278 279 280 NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
281 à 300
281 282 283 284 285 286 287 288 289 290
291 292 293 294 295 296 297 298 299 300
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
ORDRE ALPHABETIQUE
A B D E G H J K L
M N P R S T
U W Y Z
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
A
AHADI ZOTE ZA MUNGU WETU
AHADI ZOTE ZA MUNGU ZINASIMAMA
ALIPOKUFA YESU JU’ YA MSALABA
ALIPOTESWA YESU PEKE’
AMENIWEKA HURU KWELI
ASKARI WA IMANI SISI
ASUBUHI NA MAPEMA SIKU YA HABARI
AYALA NAYE ANAYO SHAUKU YA MAJI
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
B
BABA NAKUOMBA LEO NA MAPEMA
BADO KIDOGO JUA LITAPANDA
BARAGUMU LITALIA SANA
BWANA YESU ALINIOKOA KWELI
BWANA YESU ANASEMA, DHAIFU WEWE
BWANA YESU AMEVUNJA
BWANA YESU ANATUULIZA
BWANA YESU ATAKUJA KUTOKA MBINGUNI
BWANA YESU, UNIONGOZE
BWANA YESU UWE NAMI
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
D
DAMU YAKO YENYE BARAKA
DHAHABU NA FEDHA HAZINIOKOI
DHAIFU, MWENYE DHAMBI
DHAMBI, HATIA ZIMEONDOLEWA
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
E
E’, FURAHINI WATU WAKE MUNGU
E’ MLINZI, TWAULIZA
E' MSAFIRI JANGWANI, TAZAMA JUU
E’ MTAKATIFU, MUNGU WA MAJESHI
E’ MTOTO, YAINUE MACHO YAKO
E’ MTU MWENYE KIU, UFIKE KWAKE
E’ MUNGU MWENYE HAKI UNIONGOZE
E’ MUNGU MWENYE KWELI
E’ RAFIKI, SHAKA ZAKO ZIPELEKE KWAKE
E’ ROHO YANGU, SIKILIZA VEMA
E’ YESU, INGIA ROHONI KABISA
E’ YESU MSHINDAJI WA GOLGOTHA
E’ YESU, SITAUSAHAU
ENYI KUNDI LAKE MUNGU
ENYI WATU WA SAYUNI
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
F
FANYIA MUNGU KAZI, MBIO USIKU
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
G
GOLGOTHA MWOKOZI ALITUNDIKWA
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
H
HAIDHURU KWANGU HUKU CHINI
HAIFAI KUYASUMBUKIYA
HALELUYA! NAFURAHI
HAPO NILIKUWA CHINI
HAPO NILIPOKUWA DHAMBINI
HATUA MOJA KATI YA WEWE NA MWOKOZI
HATUMJUI RAFIKI MWEMA
HERI HALISI, YESU NI WANGU
HERI MIMI KWANI MKOMBOZI WANGU
HERI MTU ANAYE AMINI MUNGU BABA
HESHIMA NA SIFA ZINA BABA MBINGUNI
HUKO JU’ YA NYOTA ZOTE
HURU KAMA NDEGE BUSTANINI
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
I
IKAWA SIKU KUBWA KWANGU
IKIWA WANANIULIZA MSINGI WA UZIMA
IMBA HABARI NJEMA
IMBA INJILI YA YESU KWA MOYO
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
J
MWOKOZI MZURI NINAYE
JE, UMELISIKIA JINA ZURI
JINA LAKE YESU KRISTO LINADUMU
JUU YA MBINGU ZOTE
JUU YA MWAMBA UMEJENGA KANISA LAKO
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
K
KAMA UNATAKA KUWA MTU WAKE YESU
KARIBU NA WENZANGU NILIPOTEA
KATI’ MIKONO YAKE YESU
KATIKA BONDE NA MILIMA
KATIKA DAMU TAKATIFU YA MWOKOZI
KATIKA MATUMAINI KWA MUNGU
KATIKA SAFARI YETU
KIJITO KIKO CHENYE DAMU
KIMYA, E’ MOYO WANGU
KISA CHA KALE NIPE HABARI
KISIMA CHA LEHI KINGALI
KISIMA SAFI SANA CHATOKA MSALABA
KITAMBO BADO- VITA ITAISHA
KUNA MJI HUKO JUU
KWA BADALA YANGU KWELI
KWA NAMNA NYINGI NILITAFUTA
KWA PENDO LAKE KUBWA
KWA SALAMA BABA MUNGU AWALINDA
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
L
LO! BENDERA INATWEKWA
LO! BENDERA MBELE YAKO
LO! HORINI BETHLEHEMU
LO! NURU INAPAMBAZUKA
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
M
MACHO YANGU KUMTAZAMA
MAISHA KATIKA DUNIA
MAISHA MAFUPI YA HUKU DUNIA
MAISHA YANGU YOTE NI MALI YA MWOKOZI
MATENDO YA MUNGU YAPITA FAHAMU
MBINGUNI KWA MWOKOZI WANGU MWEMA
MGENI MIMI HAPA MAHALI PA UGENI
MGENI MIMI, NINASAFIRI
MIKWAJU ITIAPO GIZA NA KIVULI
MIMI MGENI KATIKA DUNIA
MIMI MKRISTO, NITA’VYOKUWA
MIMI MWENYE HATIA NILIKOMBOLEWA
MKUTANO ’KUBWA GANI MLIMANI
MPONYI APITAYE WOTE
MSAFIRI ULIE NJIANI
MSALABANI MWOKOZI WANGU
MSALABANI NILIMWONA YESU
MTOTO MIMI NI MASKINI
MUNGU AKUTAKA KATI’ SHAMBA LAKE
MUNGU ALIYE MBINGUNI
MUNGU AWABARIKIE NYOTE
MUNGU, MOTO WAKO UNIUTUMIE
MUNGU, NIVUTE KWAKO
MUNGU, TUNANGOJA WOTE
MUNGU WANGU MKUU WANIJAZA
MUNGU WETU, UTULINDE
MUNGU WETU YU KARIBU
MVUA YA MBINGU UNYESHE NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
MWAMBA ULIOPASUKA
MWANA-KONDO’ WA MUNGU
MWENYEZI AMEJENGA MJI
MWENYEZI MUNGU ANAFANYA ISHARA
MWENYEZI MUNGU NGOME KUU
MWENYEZI MUNGU WA ZAMANI ZOTE
MWISHO WA NJIA YA MUNGU NI MBINGU
MWOKOZI ALITOA DAMU KWA'JILI YA WAOVU
MWOKOZI AMEUTIMIZA WOKOVU
MWOKOZI KAMILI NI YESU PEKEE
MWOKOZI, MFALME, ULISULIBIWA
MWOKOZI, MOTO SAFI, WAZI, TUNATAKA MOTO
MWOKOZI MZURI NINAYE
MWOKOZI WANGU NI MWAMBA BORA
MWOKOZI WANGU ULIKWENDA JUU
MWOKOZI WETU ALIAHIDI
MWOKOZI WETU ANATUPA FURAHA
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
N
NAFASI INGALIKO ARUSINI
NAFIKIRI SIKU TUTAKAYOFIKA MBINGUNI
NAFURAHI KWA SABABU KATI' DAMU
NILIYE MSAFIRI, MGENI DUNIANI
NIMEFIKA KWAKE YESU
NIMEKWISHA KUINGIA NCHI NZURI
NIMEUONA MTO SAFI
NIMEYASIKIA MENGI ALIYOYAFANYA
NINA FURAHA KUBWA, NAPUMZIKA
NINA RAFIKI MWEMA, NAYE ALINIFILIA
NINA USHIRIKA NA FURAHA KUBWA
NINA UZIMA WA MILELE
NINAFURAHIA KISIMA DAIMA
NINAINUA MACHO YANGU KWA MUNGU
NINAJUA NCHI HUKO JUU
NINAJUA NCHI NZURI
NINAJUA RAFIKI MWEMA, ANITUNZA
NINAKUMBUKA SAYUNI
NINAKUSHUKURU MUNGU KWA FADHILI ZAKO
NINAO WIMBO WAKUNIFURAHISHA
NINATAKA KUFUATA YESU
NINATAKA KUMSIFU YESU BWANA
NINATAKA KUMSIFU YESU KRISTO
NINATAMANI KWENDA MBINGU
NIPE HABARI YA YESU, UIANDIKE ROHONI !
NIPE SAA MOJA NAWE YESU
NITAKWENDA MAHALI PA GIZA
NITAOGOPA NINI GIZANI DUNIANI?
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
NITAZAMAPO KWA IMANI MWOKOZI
NJIA YOTE NAONGOZWA
NJOO KWA YESU MWOKOZI
NJOO KWA YESU USISHANGAE
NJOO, MWENYE HUZUNI NYINGI
NJONI WOTE, MLE, MNYWE
NJONI WOTE MTESWAO!
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
P
PANDA MBEGU NJEMA ANZA ASUBUHI
PENDO KUBWA LA BABANGU LINANG'AA
PENDO LA MUNGU NI KUBWA
PENDO LA MWOKOZI KUBWA MNO!
PIGA MAKENGELE YA FURAHA LEO
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
R
RAFIKI YANGU TAZAMA
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
S
SAFARI YANGU HUKU
SASA TAYARI KWETU SIKU YA KUOKOKA
SAUTI MOJA ILINIULIZA
SAUTI YA YESU NILIISIKIA, KWA PENDO
SAWA NA KISIMA SAFI
SAYUNI, ULAKI BWANAKO
SHAMBA LA MUNGU LIMEIVA
SIFU BWANA, NINYI WATU WAKE
SIKU CHACHE
SIKU KUBWA YA MASHANGILIO
SIKU MOJA MAVUNO YATAISHA KABISA
SIKU MOJA NITAMWONA BWANA YESU
SIKU MOJA TUTAONA UTUKUFU
SIKU NYINGI NILIFANYA DHAMBI
SIKU YA FURAHA INATUFIKIA
SIKU YA KUISIKIA PARAPANDA
SIMAMA FANYA VITA PAMOJA NA MFALME
SISI TU VIUNGO VYA MWILI 'MOJA
SITASHAWISHIWA TENA NA DUNIA HUKU
SITASUMBUKA
SIWEZI MIMI KUFAHAMU SANA
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
T
TARUMBETA LAKE KRISTO LITALIA
TAZAMA MWOKOZI ALIYEKUFILIA
TU WATU HURU, HURU KWELI
TU WASAFIRI, TWAKARIBIA NCHI
TU WAVUNAJI WAKE MUNGU
TUIMBE ASUBUHI HII
TUIMBIE MSALABA WA MWOKOZI
TUIMBIE, TUMSIFU YESU JU’ YA MSALABA
TUINUE MOYO TUKISIFU YEYE
TUKIENDA PAMOJA, KUSHIKANA
TUMEKOMBOZWA KATIKA NCHI
TUNAKARIBIA KAO LA MBINGUNI
TUNAMTIA MIKONONI MWAKO MTOTO
TUNASIKIA LEO HABARI, INAWAITA WATU
TUPATE KWA NANI FARAJA YA ROHO?
TUTAONA FURAHA MBINGUNI
TUTAZAME KULE MBELE
TWAPASHA HABARI YA MBINGU
TWA’SIFU MUNGU KWA AJILI YA DAMU
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
U
UFURAHI, MOYO WANGUUKAE NAMI, GIZA INAFIKA!
UKICHOKA KWA SAFARI NGUMU
UKICHUKULIWA NA MASHAKA YAKO
UKIONA KIU SANA UJALIVU WA MWOKOZI
ULINDE ROHO NA NAFSI YANGU
UMESHIRIKIANA NAYE YESU
UMGEUKIE MWOKOZI, JITENGE NA OVU
UNA UHODARI LEO WA KUMFUATA YESU
UNIHUBIRI HABARI NJEMA
UNIPE RAHA TELE KAMA MTO
UNIVUTE, YESU, NIFUATE NYAYO ZAKO
UPENDO WAKE MUNGU UNATUUNGANISHA
USIKIE BWAN YESU ANAYEKUITA LEO
USIKU KABLA YA KUTESWA
USIMTAFUTE YESU KATI' WAFU
USIOGOPE MATESO YAKO
USIYEFANYA BIDII KABISA
UTUKUFU WA MBINGUNI NI WA HERI
UTUME ROHO YAKO JUU YETU
UWATAFUTE WANAOPOTEA
UWATAFUTE WENZAKO WAPOTEAO
UZIMA NINAO MOYONI DAIMA
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
W
WAISRAELI WALIKA’BABELI UTUMWANI
WAKATI WA NOELI
WAKATI WA UTOTO WAKO
WAKRISTO WA NCHI ZOTE
WALIAMINIO NENO LAKE MUNGU
WATU WA MUNGU, MSHANGILIENI
WENGI WAKASEMA: “BADO”
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
Y
YAPIGWA HODI KWANGU, MGENI
YESU AKINIONGOZA SITAANGUKA
YESU ALIPOLALA KATI’ KABURI
YESU AMEINGIA KATIKA ROHO YANGU
YESU AMENIOKOA
YESU, JINA HILI JEMA
YESU! JINA HILI LINAPITA
YESU KRISTO ALIFUFUKA
YESU KRISTO ASIFIWE
YESU KRISTO, BWANA WANGU
YESU KUTOKA MBINGUNI ALIINGIA
YESU MWOKOZI AITA KWA PENDO
YESU MWOKOZI, UNANIPENDA
YESU, MWENYE PENDO KUBWA
YESU NI FURAHA YANGU
YESU, NINAKUTOLEA MOYO NA MAISHA YANGU
YESU, NINAKUTOLEA VYOTE NINAKUWA NAVYO
YESU, NIVUTE KARIBU NAWE
YESU, ULIKARIBISHWA ARUSINI
YESU, ULIYEKUFA KWA AJILI YANGU
YESU, UNIONYE TENA MSALABA WAKO!
YESU, WEWE U MCHUNGA WETU
YESU, YESU, JINA KUBWA
YO YOTE UONAYO HUKU
YOTE NINAYO NILIYAPOKEA KWA WEMA
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU
Z
ZAMANI MJINI MWA YERUSALEMU
ZIMETIMIZWA AHADI NJEMA
ZITAKAPOTIMIA SIKU ZA HUDUMA YANGU
NYIMBO ZA MUNGU PAGE D'ACCUEIL NYIMBO ZA WOKOVU