Mwongozo wa Utekelezaji - ra-training … Implementation... · Umeandaliwa kwa kushirikiana na...

29
Mwongozo wa Utekelezaji wa wakulima wadogo wa Chai Africa Umezingatia Mwongozo wa mtandao wa Kilimo Endelevu - Sustainable Agriculture Network (SAN)

Transcript of Mwongozo wa Utekelezaji - ra-training … Implementation... · Umeandaliwa kwa kushirikiana na...

Mwongozo wa Utekelezaji wa wakulima wadogo wa Chai Africa

Umezingatia Mwongozo wa mtandao wa Kilimo Endelevu -Sustainable Agriculture Network (SAN)

Shukrani

© 2011 Rainforest Alliance Haki zote zimehifadhiwa

Mwandishi:Reiko Enomoto, Technical Capacity Manager, Sustainable Agriculture Division, Rainforest Alliance

Mtaalamu MwandamiziWinnie Mwaniki, Regional Projects Manager, Rainforest Alliance

Kuchapa na michango ya kiutaalamu:Marc Monsarrat, Manager (East Africa & South Asia), Rainforest AllianceKathrin Resak, Technical Coordinator (Africa & Asia), Rainforest Alliance Sylvia Rutatina, Rainforest Alliance Tanzania Coordinator Washington Ndwiga, Rainforest Alliance Trainer, Partner AfricaMark Omondi, Rainforest Alliance Trainer, Partner Africa Jane Nyambura, Regional Manager, Partner AfricaPeter Mbadi, Project Manager, KTDAAlfrick Sang, Sustainable Agriculture Coordinator, KTDADr. F. N. Wachira, Director, Tea Research Foundation of Kenya Gabriel Tuei, Unilever KenyaZakaria Mitei, Unilever Kenya Livingstone Sambai, Unilever KenyaJagjeet Kandal, Unilever Mark Birch, UnileverRia Kearney, Tata Global BeveragesSebastian Michaelis, Tata Global BeveragesSarah Roberts, Ethical Tea PartnershipJoseph Wagurah, Ethical Tea Partnership

Upigaji Picha: Reiko Enomoto, Rainforest Alliance Kathrin Resak, Rainforest AllianceWinnie Mwaniki, Rainforest AllianceWashington Ndwiga, Partner AfricaTea Research Foundation of Kenya

:

Huu mwongozo wa utekelezaji umeandaliwa, umechapishwa na kusambazwa kutokana na msaada wa Dutch Sustainable Trade Initiative (IDH), Flemish Authorities (FICA), Tata Global Beverages na Unilever Plc.

Umeandaliwa kwa kushirikiana na Africa Now, Kenya Tea Development Agency (KTDA) na Ethical Tea Partnership

Mwongozo wa Utekelezajiwa Wakulima wadogo wa Chai Africa

Utangulizi

Sura ya 1:Mbinu Shirikishi za Uthibitiwa wadudu na magonjwa

Sura ya 2:Taratibu Salama za kushughulika na madawa

Sura ya 3: Uthibiti wa takataka

Sura ya 4:Hifadhi ya mifumoya ekolojia

Sura ya 5:Hifadhi ya maji

Sura ya 6:Hifadhi ya udongo

Sura ya 7:Maisha bora na mazingira mazuri ya kazi

Sura ya 8:Usimamizi wa shamba

1

Uta

ngulizi Utangulizi

kuhusu kilimo endelevu

Chai ni mojawapo ya mazao muhimu katika Mashariki na Kusini mwa Afrika, na pia ni

chanzo cha kipato kwa wakulima wengi wadogo. Pamoja na hayo, iwapo shughuli zisizo

endelevu zikiachwa ziendelee, zitachafua mazingira, zitachakaza maji au udongo na

kunyonya wafanyakazi. Kwa njia hii, uzalishaji wa chai hauwezi kudumu kwa muda mrefu.

.

Ili kuhakikisha kuwa uzalishaji wa chai unaendelea hadi siku zijazo, inabidi kushirikiana

katika kuhamasisha shughuli endelevu katika ngazi ya mkulima mdogo. Ni muhimu

kuhakikisha kuwa kila mzalishaji anachukua jukumu la kuzalisha chai kwa njia endelevu.

Jinsi gani wakulima wanaweza kuzalisha chai kwa

njia endelevu? Huu “Mwongozo wa Utekelezaji”

unaonyesha njia rahisi na zinazotekelezeka za

kilimo endelevu katika mashamba ya wakulima

wadogo wa chai katika nchi za Afrika.

Yaliyomo katika mwongozo huu yamezingatia

“Mwongozo wa Kilimo Endelevu” uliochapichwa

July 2010 na Mtandao wa Kilimo endelevu.

Mwongozo huu umejumuisha maeneo yote muhimu

endelevu. Hii ni nakala muhimu pale mzalishaji

anapoamua kuwa na ithibati (cheti) ya Rainforest

Alliance.

2

Uta

nguliziMasharti ya kupata ithibati (cheti)

Kupata wastani wa asilimia themanini ( 80%) kwa kanuni zote

(Jumla ya vigezo ni 99)

Kupata asilimia hamsini (50%) kwa kila kanuni (Kuna kanuni 10)

Kufaulu vigezo vyote vya lazima (Kuna vigezo 15 vya lazima)

1.

2.

3.

Kiwango cha chini cha kufaulu ili kupata ithibati ya Rainforest Alliance ni

kama ifuatavyo.

kwa upande wa wakulima wadogo, vigezo vingi haviwahusu. Katika

mwongozo huu, tumelenga vigezo ambavyo vinawahusu na ni

muhimu kwa wakulima wadogo. Tafadhali tia maanani kuwa

mwongozo huu haujahusisha vigezo vyote vya kanuni na pia

hauhusishi mashamba makubwa.

Yaliyomo katika mwongozo

Sura ya 1:Mbinu Shirikishi za Uthibiti wa wadudu na magonjwa

Sura ya 2: Taratibu Salama za kushughulika na madawa

Sura ya 3: Uthibiti wa takataka

Sura ya 4: Hifadhi ya mifumo ya ekolojia

Sura ya 5: Hifadhi ya maji

Sura ya 6: Hifadhi ya udongo

Sura ya 7: Maisha bora na mazingira mazuri ya kazi

Sura ya 8: Usimamizi wa shamba

Mwongozo huu una sura 8, kila mojawapo inaendana na kanuni za mwongozo

Inaendana na: Kanuni ya 8

Inaendana na: Kanuni ya 6

Inaendana na:Kanuni ya 10

Inaendana na:Kanuni ya 2

Inaendana na:Kanuni ya 4

Inaendana na:Kanuni ya 9

Inaendana na:Kanuni ya 5

Inaendana na:Kanuni ya 1

3

Ukurasa wa 4

Ukurasa 10

Ukurasa 14

Ukurasa 15 Ukurasa 25

Ukurasa 23

Ukurasa 22

Ukurasa 18

Mbin

u shir

ikishi

za ut

hibiti

wa

wadu

du na

mag

onjw

aSura ya 1

4

Upandaji Unapopanda mche wa chai, chagua aina inayostahimili

wadudu na magonjwa kama vile utitiri na Mbu wa chai. Ni

vizuri kupanda aina tofauti za chai, badala ya aina moja.

Unapopanda aina tofauti, kila moja ipandwe kwenye boma

tofauti kurahisisha usimamizi.

Kupanda aina zilizochaguliwa kwa umakini

Kama shamba lilikuwa

limeathirika na ugonjwa wa

mizizi, kama vile Amilaria,

ugojwa huo unaweza bado

kushikiliwa na mizizi ya mashina

yaliyobaki. Kwa hiyo, inatakiwa

kuondoa gamba kuzunguka mti

ili kuzuia chakula kutoka kwenye

majani kwenda kwenye mizizi

kupitia magamba ya mti. Njia hii

itasababisha kuua wadudu

kwenye mizizi. PaliziMagugu yanatakiwa yathibitiwe kwa njia zifuatazo, bila

kunyunyiza madawa.

Kutumia matandazo kwenye chai changa au mashina

yaliyokatwa

Kutumia matandazo kwenye chai changa au mashina

yaliyokatwa

Kung'oa magugu kwa mkono

Mbinu shirikishi za uthibiti wa wadudu na magonjwa

Matumizi ya madawa sio njia pekee ya kuthibiti wadudu na magonjwa. Mashina

ya chai yakitunzwa vizuri yakawa na afya nzuri hasa nchi za Africa, yatastahimili

mashambulizi ya wadudu wa muda mfupi, bila kutumia madawa. Unyunyiziaji wa

madawa unaua wadudu rafiki asilia na kunaweza kusababisha kutokea kwa

mlipuko wa magonjwa yasiyoweza kuthibitiwa. Katika kipengele hiki, tunajifunza

jinsi ya kuthibiti wadudu na magonjwa kwa njia endelevu

Matandazo na chai iliyofunga vizuri

inazuia mwanga kupenya hadi ardhini,

hivyo uthibiti wa magugu yasiote. Palizi

ya jembe inaweza kuharibu mizizi ya

mashina ya chai. Ni vyema kung'oa

magugu kwa mkono.

Matandazo kwenye chai changa

Palizi ya mkono

Kuondoa gamba kuzunguka mti

5

Kukata chaiKukata chai ni muhimu kwa kufanya mashina yawe na afya na yenye kuzalisha. Ina faida

zifuatazo.

Matawi yaliyokatwa yanatoa virutubisho kwenye udongo yanapooza,

yanazuia magugu yasiote,huhifadhi unyevu wa udongo na kuzuia

mmomonyoko.

4.

Unapokata mashina ya chai ya umri mkubwa, zingatia kimo cha sentimita 60. Kama ukikatia chini sana, maji ya mvua yanayoruka kutoka ardhini yanaweza kuwa na vimelea vya magonjwa na kuingia kwenye kidonda

Baada ya kukata, tumia matawi hayo kufunika chai iliyokatwa ili kuzuia chai isiunguzwe na jua au barafu. Baada ya hapo, unaweza kutandaza juu ya udongo kama matandazo. Usiondoe matawi yaliyokatwa kwa ajili ya kuni.

Kuthibiti panyaFuko na panya waharibuo mizizi ya chai wanaweza kuthibitiwa

kwa kuchimba mifereji, na kwa kupanda mimea inayowafukuza

kama vile utupa (Tephrosia vogelli), bangi pori (Tagetes minuta),

vitunguu maji na vitunguu saumu. Epuka kuwaua.

Utupa uliopandwa kwenye shamba

Bangi pori

Wasiliana na wataalamu

wa kilimo kama unataka

kutumia majani ya utupa

kama dawa ya kuthibiti

wadudu.

2. Kukata chai kunahamasisha ukuaji wa matawi na majani mapya.

1. Kukata mashina na matawi yenye magonjwa kuzuia kusambaa

kwa magonjwa katika sehemu nyingine ya mmea

3. Kukata chai kunathibiti urefu wa meza hivyo kurahisisha uchumaji.

Mbin

u s

hir

ikis

hi za

uth

ibiti w

a w

adudu n

a m

ago

njw

a

6

Amilaria Shina lililokufa au lenye ufa wenye utando mweupe, ni dalili ya kushambuliwa na Amilaria.

Amilaria ni ugonjwa wa fangasi inayoenezwa kupitia mfumo wa mizizi. Tahadhari

isipochukuliwa ugonjwa utasambaa na kushambulia shamba lote.

Shina lenye ufa karibu na ardhiShina lililokufa

Shina lililokauka au lenye majani ya njano

Shina lenye ufa juu kidogo ya ardhi lenye utando mweupe kama nyuzinyuzi

Kama kuna shina

lililoshambuliwa na Amilaria,

unatakiwa kung'oa shina lote

ikiwemo mizizi na kuacha

wazi juu ya ardhi

Baada ya kung'oa shina lililoadhirika, unaweza kupanda chai

kwa msimu unaofuata. Kama ni sehemu kubwa iliyong'olewa,

eneo linaweza kupandwa kwa mimea inayorutubisha udongo

kama vile nyasi aina ya Guatamala.

Nyasi aina ya Guatamala

Ung'oaji wa shina lote ikiwemo mizizi

Mbin

u s

hir

ikis

hi za

uth

ibiti w

a w

adudu n

a m

ago

njw

a

7

Uthibiti wa mpasuko wa gamba kwenye shina au matawi (phomopsis – stem canker) Kama ukiona mpasuko wa gamba kwenye shina au

matawi, hiyo ni dalili ya shambulio la Phomopsis.

Phomopsis ni ugonjwa wa fangasi unaopenya kupitia

vidonda vilivyo wazi kwenye shina au matawi. Vidonda

hivyo vinaweza kusababishwa na palizi ya jembe au

shambulio la panya.

Tawi lenye vidonda vilivyodidimia

Majani yaliyogeuka kuwa njano

Ili kuthibiti mpasuko wa gamba kwenye shina au matawi, ondoa

matawi yaliyoadhirika na kuyachoma. Uchomaji unaruhusiwa

kwa ugonjwa huu tu kwani ndiyo njia pekee ya kuudhibiti.

Unapochoma, hakikisha unakuwepo ili kuthibiti moto

usisambae.

Kuzuia mpasuko wa gamba kwenye shina au matawi,

unatakiwa kuchagua aina za chai zenye kustahimili phomopsis

wakati unapopanda eneo jipya. Epuka kutumia palizi ya jembe,

kwani jembe linaweza kuumiza mashina bila kutarajia.

Kuchoma matawi yaliyoshambuliwa na Phomopsis

Uthibiti wa kuoza kwa shina (Hypoxylon wood rot). Kuoza kwa shina ni ugonjwa wa fangasi unaoshambulia matawi mama. Matawi

yaliyoadhiriwa huanza kuoza na kuwa na mabaka meusi kwa nje. Kuthibiti kuoza kwa

matawi, ondoa matawi yaliyoshambuliwa na nyunyiza dawa ya ukungu ya kopa kwa ajili ya

fangasi kwenye vidonda. Wakati wa kukata chai yenye umri mkubwa, hakikisha kuwa

unakata kwenye urefu unaotakiwa (sentimita 60) ili kuzuia mdudu kufikia vidonda.

Shina zima lililoadhirika na Hypoxylon

Mabaka meusi kwenye shina

Mbin

u s

hir

ikis

hi za

uth

ibiti w

a w

adudu n

a m

ago

njw

a

8

Mbu wa chai (Helopeltis -Tea mosquito bug)Mbu wa chai wanavyonza majani machanga na kuacha mabaka meusi kutokana na mate

yake. Majani yaliyoshambuliwa yanaadhiri ukuaji.

Majani yaliyoathirika kutokana na Mbu wa chai

Mbu wa chai

Majani yaliyofyonzwa na Mbu wa chai

Kuondoa majani yote machanga

Kuthibiti shabulio la Mbu wa chai, inashauriwa

kuchuma majani yote machanga na kuacha

majani yaliyokomaa shambani. Hii njia inaitwa

“uchumaji wa kugandamiza”. Kwa kuondoa

majani yote machanga ambayo yangeliwa na

Mbu wa chai, idadi yao inaweza kuthibitiwa. Ili

kuzuia kushambuliwa na Mbu wa chai, ni

muhimu kuchagua aina ya chai zinazostahimili

shambulio la Mbu wa chai unapopanda chai

changa.

Vidukari (Aphids)Vidukari ni wadudu wanaoshabulia majani machanga.

Uchumaji wa kugandamiza na kupunguza siku za

kuchuma ni njia madhubuti ya kudhibiti wingi wao.

Majani yaliyoshambuliwa na vidukari

Vikobe (Ladybirds) ni maadui

asilia wa vidukari. Vikobe

wanawala vidukari na kuthibiti

idadi yao. Kunyunyiza dawa

hakutauwa tu vidukari bali pia

vikobe. Kwa kutokunyunyiza

dawa, unalinda vikobe na

kudumisha njia asilia ya uthibiti

wa vidukariVikobe wanawala vidukari

Mbin

u s

hir

ikis

hi za

uth

ibiti w

a w

adudu n

a m

ago

njw

a

9

Utitiri (mites)

Kuna aina nyingi za utitiri kama vile utitiri wa

zambarau, utitiri wekundu n.k. Majani

yaliyoadhirika kwa utitiri yanabadilika rangi

na kuwa ya kahawia

Shamba lililoharibiwa na utitiri wekundu

Majani yaliyoadhirika na utitiri wekundu

Uwekaji wa mbolea ya kutosha

Mashina yenye afya yanaweza kustahimili adhari za utitiri.

Uwekaji wa mbolea ya kutosha unaimarisha mashina ya

chai. Upandaji wa aina za chai zenye kustahimili ni njia ya

kuzuia shambulizi la utitiri

Tuthibiti wadudu na magonjwa kwa njia

endelevu katika mashamba yetu na kudumisha

mashina yenye afya na yanayotoa mazao

mengi

Mbin

u s

hir

ikis

hi za

uth

ibiti w

a w

adudu n

a m

ago

njw

a

Tara

tibu s

alam

a za

ku

shughulika

na

mad

awa

Taratibu salama za kushughulika na madawa

Sura ya 2

Wakulima wenye ithibati (cheti) wasifanye shughuli zenye kuathiri afya zao au afya za watu

wengine. Kama unatumia madawa kwenye mboga au wanyama, yanatakiwa yawekwe na

yashikwe kwa usalama na pia yatumike katika njia salama, kwa ajili ya usalama wako, wa

familia yako na majirani.

Hairuhusiwi kunyunyiza madawa bila kutumia vifaa vya kujikinga.

Hiki ni kigezo cha lazima.Usipokidhi kigezo hiki utaadhiri vikubwa upatikanaji wa ithibati wa kikundi husika

Kumbuka:

Kichuja sumu (Sio kizuia vumbi. Kizuia vumbi hakina chujio la sumu)

Koti la mvua au kizibau cha kukinga mgongo

Glovu za plastikimgongo

Aproni iliyotengenezwa kwa mfuko wa plastiki (inashauriwa kama kizuia dawa cha ziada kama koti halifuniki miguu vizuri)

Kumbuka: Tumia mfuko wa plastiki ambao haukutumika kwa bidhaa za madawa (nafaka n.k.) Usitumie mfuko wa mbolea

Buti za plastiki

Kizuia vumbi

Miwani kwa ajili ya kukinga macho

Kumbuka kwamba sehemu zote za mwili zinatakiwa kufunikwa

Vifaa vya Kujikinga (PPE)

10

Unaweza kuvuta madawa kupitia mdomo au pua.

Mchanganyiko wa dawa unapovuja, utalowanisha nguo zako na hivyo kuguza ngozi yako

Mchanganyiko utalowanisha mikono yako na kuingia mwilini kupitia ngozi

Kama hutavaa buti, dawa pia itaguza ngozi yako

Koti lisilopitisha maji

Tara

tibu s

alam

a za

ku

shughulika

na

mad

awa

Kuvaaa vifaa vya kinga ni muhimu sio tu wakati wa kunyunyizia mboga, bali pia wakati wa kunyunyiza dawa kwa ng'ombe na uwekaji wa mbolea.

Utunzaji salama wa madawa

Madawa

Madawa

Inakuwaje kama ukihifadhi madawa ndani ya vyumba mnamoishi? Hewa ya sumu inayotoka kwenye madawa yaliyohifadhiwa inaweza kuathiri afya ya familia yako

Kama ukitunza madawa jikoni mwako, mwanafamilia anaweza kuchukua na kuweka kwenye chakula bila kufahamu kama ilikuwa ni dawa

Kama ukitunza madawa chumba cha kulala, watoto wanaweza kuziona na kuzinywa kwa kufikiri ni kinywaji.

Madawa

Kama ukiweka madawa sehemu iliyo wazi bila kofuli, watoto wanaweza kuyafikia na kuyachukua wakati wanacheza, au yanaweza kuibiwa.

Madhara ya kutotunza madawa kwa uangalifu yanaweza kusababisha kifo kwa mwanafamilia

Madawa

11

Kwa uwekaji wa mbolea, unatakiwa kuvaa angalao glovu, buti na aproni

Tara

tibu s

alam

a za

ku

shughulika

na

mad

awa

Ni vyema kununua kiwango kile cha madawa kinachohitajika kutumiwa wakati huo, ili isikulazimu kutunza madawa nyumbani. Pale unapotakiwa kutunza madawa yaliyobaki, zingatia yafuatayo hapa chini jinsi ya kuhifadhi madawa kiusalama kwa ngazi ya shamba la mkulima mdogo

Sehemu ya hifadhi iliyotengenezwa kwa pipa la chuma

Stoo iliyotengenezwa kwa kibanda cha zamani cha kuku

1. Kama unahitaji kutunza chupa za madawa, sio lazima kujenga ghala la kuhifadhia au jengo. Kibanda kidogo kinaweza kutosha kwa mkulima mdogo. Kwa mfano, unaweza kulitengeneza pipa la chuma, sanduku la chuma, mbao au kibanda cha kuku kisichotumika kwa kuyatunzia. Ni muhimu kuwa kifaa hicho hakiwekwi ndani ya nyumba.

Ukubwa na muundo

2. Vifaa visivyopitisha majiUnaweza kutengeneza stoo kwa kutumia vifaa vinavyopatikana katika sehemu husika ambavyo havipitishi maji. Paa lake lisiwe linapitisha maji. Kama unatumia mbao, unatakiwa kutandaza karatasi ya plastiki ili kama dawa ikimwagika bahati mbaya isivyonzwe na mbao hizo.

Ndani ya kibanda cha mbao kumetandazwa karatasi ya plastiki.

3. KufungiaStoo inatakiwa kufungwa, na ufunguo unatakiwa kutunzwa kwa umakini. Ni muhimu kuifunga ili watoto au watu wengine wasifungue na kuyachukua madawa yaliyo ndani.

4. Alama ya tahadhariWeka alama ya tahadhari kwenye stoo ili ijulikane wazi kwa yeyote kuwa kuna vitu vya hatari ndani.

Shelfu ya mbao iliyotandazwa karatasi ya plastiki

12

Tara

tibu s

alam

a za

ku

shughulika

na

mad

awa

Kupanda wigo hai

Unaponyunyiza madawa, unatakiwa kuhakikisha kuwa watu wapitao jirani na shamba lako

hawaadhiriwi na dawa zisambaazo kutoka shambani. Kuzuia kuzambaa kwa madawa,

inashauriwa kupanda wigo hai kuzunguka shamba lako. Wigo hai pia unahifadhi viumbe hai

na kuunganisha mifumo ya ikolojia shambani.

Wigo hai

Shamba la chai

Shamba la chai

Shamba la

Wigo hai

Wigo hai

Umbali kati ya nyumba na maeneo ya uzalishajiKama familia yako au wafanyakazi wanaishi shambani, ni muhimu kuacha umbali kidogo

kutoka kwenye nyumba na shamba. Kama mashamba ya chai au bustani ya mboga iko

jirani na nyumba, watu waishio ndani ya nyumba au watoto wanapocheza hapo nyumbani

wataadhiriwa na madawa yatakayokuwa yanasambaa wakati wa kunyunyiza. Unaweza

kuzuia kusambaa huko kwa kuacha umbali kidogo na kupanda wigo hai.

Umbali kutoka shambani na nyumba

Shamba lililo karibu kabisa na nyumba

13

Uthibiti wa takatakaSura ya 3

Uth

ibiti w

a ta

kata

ka

Takataka zinaweza kuwa na manufaa tena, kama

zitatumika kwa shughuli nyingine au kutengeneza

kitu kingine.Kutokuthibiti taka kunachafua hewa,

maji na udongo shambani mwako. Kama ukichoma

taka za plastiki au makasha matupu ya dawa, hewa

ya sumu hutoka na kuathiri afya ya familia yako.

Tuthibiti takataka inavyotakiwa ili kuwa na mazingira

safi shambani mwako.

Kuchoma takataka hairuhusiwi

Uthibiti wa taka hai (taka zinazooza)

Taka za jikoni na samadi za mifugo zinaweza

kuozeshwa kutengeneza mboji. Unapoziozesha,

hakikisha unazigeuza kila wiki 2-3 ili kupitisha

hewa na kuhifadhi joto la kutosha ili kuziozesha

Uthibiti wa takataka za plastiki na makasha ya madawaTaka za plastiki na makasha ya madawa zikusanywe tofauti. Safisha makopo ya

madawa mara tatu na yatoboe kabla ya kuyahifadhi. Baada ya kuzitenga, kampuni au

uongozi wa mradi (Group Administrator) izichukue na kuziteketeza kwa njia ambayo

haitachafua mazingira.

Zisiachwe shambani.

Mfuko kwa ajili ya makasha ya madawa

Mfuko kwa ajili ya taka za plastiki

Chombo cha kukusanyia taka za plastiki

14

Hifad

hi ya

mfu

mo

wa

iko

lojia

Kama una maeneo yafuatayo shambani mwako, ni ekolojia muhimu ya kuhifadhiwa

Eneo lenye miti ya asili

Eneo lenye wanyama adimu au mimea

Kijito au mto

Chanzo cha maji

Eneo chepechepe au oevu

Mbuga za hifadhi au maeneo

yaliyotengwa na serikali

Maeneo haya yanatakiwa kuhifadhiwa kwa

sababu yanatunza aina ya viumbe mbalimbali

ambavyo ni muhimu, na kuyapoteza maeneo

haya kutaharibu vibaya mazingira kama vile

upotevu wa viumbe adimu, mmomonyoko wa

udongo na uchafuzi wa maji.

Kwa hiyo, yasibadilishwe kuwa shamba la

chai.

Usikate miti, usiwinde, usilimeIli kuyalinda maeneo hayo, inatakiwa kutokukata miti kwa ajili ya kuni kutoka katika maeneo

hayo, kuwinda wanyama, kulima mazao au kunyunyiza madawa. Hii inahitaji mawasiliano

ya kiufasaha kwa wafanyakazi wote na wanafamilia

Hifadhi ya mfumo wa ikolojiaSura ya 4

Kutokuharibu maeneo hayo ya asili ni kigezo cha lazima..

NB:

15

Hifad

hi ya

mfu

mo

wa

iko

lojia

Upandaji wa miti ya asiliIli kuhifadhi bionuwai ya eneo, unaweza kupanda miti ya asili mpakani mwa shamba, kando

ya vyanzo vya maji na maeneo ya mitelemko mikali. Ni muhimu kupanda miti ya asili, na

siyo miti ya kigeni kwa sababu miti ya asili inaboresha hali ya hewa ya eneo husika na hali

ya udongo, na inaweza kutunza bionuwai maalum.

Mtelemko mkali uliopandwa miti ya asili

Upandaji wa miti ya asili

Mfano wa miti ya asili katika Africa Mashariki

Kuacha ukanda wa bafa Inashauriwa kuacha ukanda wa bafa au uoto wa asili kati ya shamba na maeneo

yaliyohifadhiwa ili kuhakikisha kwamba dawa hazitapenya na pia shughuli za kilimo

hazitayaharibu maeneo hayo

Msitu

Ukanda wa bafa

Shamba

Eneo chepechepe au oevu

Ukanda wa bafa

Shamba

16

Kifabakazi MpodoMueri, MkomahoyaMruka MfurufuruMianziMwangati Mvengi au Mzambarau mwitu Mfuu

Unaweza kuwa na bustani ya miti ya asili ili kuzalisha miche mwenyewe

Hifad

hi ya

mfu

mo

wa

iko

lojia

Kuunganisha mifumo ya ikolojia

Ili wanyama na ndege waweze kutoka sehemu moja hadi nyingine, wanahitaji misitu

iliyounganika. Kama msitu ukitenganishwa kwa mashamba, wanyama hawawezi kupita kwa

uhuru. Kama vyanzo vya maji havijaunganishwa na msitu, wanyama hawawezi kuyafikia

hayo maji.

Misitu iliyounganishwa ambayo wanyama na ndege wanaweza kupita

Viraka vya misitu vilivyounganika

Kuunganisha mifumo ya ikolojia unaweza

kupanda miti pembeni mwa shamba ili

kuunganisha viraka vya msitu, au kuhifadhi

maeneo ya ushoroba (corridor) ya misitu

17

Uhuru wa ndege na wanyama kupita

Kuzuia mwingiliano

Misitu iliyoharibiwa na kutenganishwa kwa mashamba ambapo wanyama na ndege hawawezi kupita

Kuzuia mwingiliano

Hifadhi ya majiSura ya 5

Hifad

hi ya

maj

i

Kuosha vifaa

Maji ni raslimali muhimu kwa maisha yetu na kwa kilimo. Katika sura hii, tutajifunza jinsi ya kuyafanya yawe safi na jinsi ya kulinda vyanzo vya maji

Baada ya kunyunyiza dawa, unatakiwa kuosha bomba lililotumika na vifaaa vyako vya kujikinga. Maji yaliyotumika kuoshea vifaa hivyo yana sumu, kwa hiyo usipoyathibiti vizuri, yanaweza kuchafua mazingira.

Vifaa visisafishwe kwenye mito, mferej au bwawa.

Unaponyunyizia bustani za mboga,

safisha vifaa na mwaga maji hayo

shambani.

Unaponyunyizia au kuosha mifugo, safisha vifaa na mwaga maji hayo kwenye shimo. Shimo hilo liwe limejazwa mkaa, ambao husaidia kuchuja hayo maji. Usikate miti ya asili kutengeneza mkaa.

Shimo lililojazwa mkaa

Kumbuka pia kuosha vifaa vya kinga. Yathibiti maji yaliyooshea kama ilivyoelezwa hapo juu.

18

Ndoo itumikayo tu kwa kuoshea vifaa

Uthibiti wa maji taka nyumbani

Kuoshea nguo kwenye mito kunayachafua maji. Kumwaga maji taka ya jikoni nje ya nyumba kunachafua mazingira na kusababisha mazalia ya mbu. Maji taka ya nyumbani yanatakiwa kuthibitiwa vizuri.

Maji machafu ya majumbani yanapokuwa machache, yanaweza kuthibitiwa kwa kuyamwaga kwenye mtaro uliochimbwa kwenye bustani. Mtaro unatakiwa upandwe migomba au magimbi, vyote viwili vinavyonza maji vizuri.

Bomba(kama mita 1)

Kumwaga maji machafu kwenye mtaro uliochimbwa kwenye eneo la bustani

Mtaro Migomba Magimbi

Maji Machafu

Kama ukiona maji yametuwama kwenye bustani, kiwango cha maji machafu ni kingi ukilinganisha na uwezo wa udongo kuyafyonza, au aina ya udongo hauna uwezo mkubwa wa kufyonza maji. Kwa hali hii, unaweza kuchimbia bomba ili maji yapenye ndani ya ardhi badala ya kuelea juu ya udongo bustanini.

19

Hifadhi ya m

aji

Ung’oaji wa mikaratusi (eucalyptus) jirani na chanzo cha majiMiti ya mikaratusi ni chanzo cha kuni, lakini

ikipandwa jirani na ardhi chepechepe (oevu), mto,

kijito au kisima, inafyonza maji mengi kiwango cha

kukausha chanzo cha maji. Kama kijito au kisima

kikikauka, kitaadhiri maisha ya familia yako na

wanajamii wengine. Tunatakiwa kulinda vyanzo vya

maji.

Kukata miti ya mikaratusi iliyopandwa jirani na mto

Baada ya kuondoa miti ya mikaratusi kijito hiki kilianza kurudi katika hali yake

Kijito kinakauka kwa sababu ya mikaratusi

Miti ya mikaratusi

Hakuna kulima jirani na vyanzo vya majiInashauriwa kutokulima jirani na vyanzo vya maji. Unaponyunyiza madawa, yanapenya

hadi kwenye maji na kuyachafua. Kulima jirani na vyanzo vya maji kunasababisha udongo

kumomonyoka kwenda kwenye maji.Tuhifadhi maeneo kandokando ya vyanzo vya maji

kwa kuacha uoto wa asili au kupanda tu mazao ambayo hayahitaji kutifuatifua udongo na

yasiyonyunyiziwa madawa.

Udongo uliomomonyoka

Upenyaji wa madawa

20

Hifadhi ya m

aji

Uvunaji wa maji

Maji ni muhimu kwa maisha, na tunahitaji kuwa na maji ya kutosha kwa maisha yetu. Uvunaji wa maji ya mvua ni njia ya unafuu na madhubuti ya kupata maji. Unaweza kukinga maji yanayodondoka kwenye paa la nyumba na kuyahifadhi kwenye pipa. Yanaweza kutumika kwa matumizi mbalimbali ya nyumbani ikiwemo kunywa baada ya kuyatibu au kuyachemsha. Mvua ni chanzo muhimu cha maji hivyo inabidi tujue jinsi ya kukitumia vyema.

Hakuna kutupa taka kwenye vyanzo vya maji

Kutupa taka kwenye vyanzo vya maji hairuhusiwi. Tunatakiwa kutunza vyanzo vya maji ili kuyafanya masafi kwa maisha ya wanyama na jamii

Kutokutupa taka kwenye vyanzo vya maji ni kigezo cha lazima

NB:

21

Hifad

hi ya

maj

i

Hifadhi ya udongo

Sura ya 6

Uthibiti wa mmomonyoko wa udongo

Hifad

hi ya

udo

ngo

Pale penye mtelemko mkali, udongo huwa na tabia ya kumomonyoka siku hadi siku. Kama hutathibiti mmomonyoko huo, utazidi kuwa mbaya zaidi.

Ili kuthibiti mmomonyoko, unaweza kupanda mawewe (Napier grass) na miti ya asili kwenye maeneo yaliyo katika adhari ya mmomonyoko. Mawewe yanashikilia udongo vizuri na yanasaidia kama malisho ya mifugo.

Mawewe

Kutokuchoma motoUchomaji moto unaribu mboji na viumbe hai

kwenye udongo, na kufanya udongo wako

kupoteza rutuba. Kuandaa mashamba kwa

kutumia moto hairuhusiwi.

Kutokuchoma moto ili kuandaa mashamba ni kigezo cha lazima

NB:

22

Mgema uliofunikwa kwa mimea

Udongo ni kiini cha kilimo. Tunatakiwa tuhakikishe kwamba udongo shambani haupotei kwa

njia ya mmomonyoko.

Maisha bora na mazingira mazuri ya kazi

Sura ya 7

Nyumba za wafanyakazi

Kama unaajiri wafanyakazi shambani mwako, wawe wanatendewa haki. Wafanyakazi wako

wanahitaji mazingira safi na salama

Mai

sha

bora

na

maz

ingi

ra

maz

uri y

a ka

zi

Kama una wafanyakazi wapatiwao nyumba, tuhakikishe kwamba zina usalama na ni bora.

1. Vyumba

Vyumba ambavyo wafanyakazi na familia zao wanamoishi au kulala visihifadhi madawa,

mbolea au makasha yake au mifuko. Kusiwe na maji yanayovuja kutoka darini au ukutani

Dari iliyoharibika inayovuja majiMadawa na mbolea chumbani Mifuko ya mbolea kwenye ukuta

2. Jiko

Jiko linapokuwa halina

sehemu ya kupitisha moshi,

moshi unaosambaa kwenye

chumba husababisha madhara

kiafya, kuharibu mapafu na

macho ya wafanyakazi na

familia zao. Jiko lenye bomba

la kutolea moshi linalinda afya

zao na kuboresha maisha yao.

Wafanyakazi wanaumizwa na moshi uliojaa chumbani

Boresha jiko ili moshi utoke kupitia kwenye bomba. Jiko hili lililoboreshwa pia linatumia kuni chache

Moshi

3. Choo

Nyumba za wafanyakazi ziwe na vyoo visafi

23

4. Sehemu ya kufulia

Nyumba za wafanyakazi ziwe

na sehemu ya kuoshea nguo.

Hawatakiwi kwenda mtoni

kufua nguo zao

Karo la kufulia Kufulia nguo mtoni

Huduma ya maji salama Wafanyakazi waishio au wafanyao kazi

shambani wanatakiwa kupata maji safi

na salama ya kunywa. Mara zote

yawepo maji yaliyochemshwa au yaliyo

salama kwa ajili yao.

Watoto Shambani

Usiajiri watoto chini ya miaka 15 kama mfanyakazi shambani

Kusaidia kufanya kazi shambani tu masaa ya nje na muda wa masomo

Watoto chini ya miaka 15

wanaweza kusaidia kwenye

shamba la familia, ili mradi

wanahudhuria shule na

hawafanyi shughuli za hatari

Kutokuajiri watoto chini ya miaka 15 ni kigezo cha lazima

NB:

24

• Chini ya miaka 15

• Kuajiriwa kama mfanyakazi shambani

• Kutokuhudhuria shule kwa sababu ya kazi

Mai

sha

bo

ra n

a m

azin

gir

a m

azuri

ya

kazi

Usimamizi wa shambaSura ya 8

Usi

mam

izi w

a sh

amba

Utunzaji wa kumbukumbuInashauriwa kuweka kumbukumbu ya shughuli muhimu. Kwa kuweka kumbukumbu,

unaweza kurejea shughuli zilizopita, kuzichunguza na kupata njia ya kuziboresha. Kwa

kuangalia rekodi, wakaguzi wa ndani na wa nje wataona kuwa unasimamia shamba lako

vizuri.

Hizi ni kumbukumbu zinazotakiwa kuwekwa

katika ngazi ya shamba.

Madawa yaliyotumika

Mbolea zilizotumika

Vibarua/Wafanyakazi

Mafunzo kwa wafanyakazi

Upandaji wa miti

Tarehe za kuchuma na chai iliyochumwa.

•••

••

Shamba

Tarehe

Aina ya dawa au mbolea

Kiasi

Dozi

Jina la mhusika aliyefanya

kazi hiyo

Aina ya kifaa

kilichotumika

Kumbukumbu za kuweka za

matumizi ya madawa na mbolea

Tarehe

Mada

Mkufunzi

Majina ya waliohudhuria

Sahihi au dole gumba ya

waliohudhuria

Kumbukumbu gani

ziwekwe kwa mafunzo

ya wafanyakazi

••••••

Tarehe

Jina

Aina ya kazi

Masaa ya kazi

Mshahara

Kumbukumbu za

kutunza za wafanyakazi

walioajiriwa

••

••

UhakikiWakulima na vikudi daima wasichanganye chai isiyo na ithibati (cheti) na yenye ithibati

katika hatua yoyote. Chai yenye ithibati inatakiwa itengwe katika ahatua zote za uzalishaji:

kwenye banda, wakati wa kusafirisha, katika mapokezi kiwandani, wakati wote wa

uzalishaji kiwandani hadi usafirishaji wa chai iliyotengenezwa.

Usichanganye chai iliyo na ithibati na isiyo na ithibati ni kigezo cha lazima

NB:

Usafiri tofauti wa chai iliyotoka kwenye mashamba yenye ithibati Njia (line) tofauti ya

kutengeneza chai iliyo na ithibati

Chai zenye ithibati zilizofungwa na kutengwa ili kutambuliwa 25