Mume Kunyonya Matiti Ya Mke Wake - Imaam Ibn ´Uthaymiyn

1
Mume Kunyonya Matiti Ya Mke Wake Fataawa Za Wanachuoni Swali: Je, mke huwa haramu kwa mume wake akinyonya matiti yake mara nne? Imaam Muhammad bin Swaalih bin 'Uthaymiyn: Allaah Kamhalalishia mume kufurahi kwa mkewe atakavyo. Anaweza hata kufanya naye mapenzi kwa njia mbalimbali. Allaah (Ta´ala) Kasema: م م أر وا م رث مؤ "Wake zenu ni konde kwenu. Basi ziendeeni konde zenu vyovyote mpendavyo." (al-Baqarah 02 :223) Zingatia kauli "basi ziendeeni konde zenu vyovyote mpendavyo." Konde ni mahali pa rutuba ambapo ni tupu ya mwanamke. Hivyo ni halali kwa mume kufanya kitendo cha ndoa kwenye tupu ya mke sawa ikifanywa kwa mbele, kwa nyuma, kwa kusimama, kwa kulala au kupitia nafasi nyingine yoyote kwa sharti iwe ni kwenye tupu yake ya mbele. Hali kadhalika, anaweza kufurahi naye kwa kumkumbatia, kumkisi na kumbusu vile apendavyo. Kilichoharamishwa tu ni yeye [mume] kufanya naye kitendo cha ndoa wakati wa hedhi na liwati [nyuma]. Kulingana na kanuni hii ya jumla, anaweza kunyonya maziwa ya mkewe. Hawi [mke] haramu kwake [mume] hata kama lau atakunywa maziwa yake. Haya ndio maoni ya jamhuri. Ili kunyonyesha kuathiri ni lazima mtu awe chini ya miaka miwili. Baada ya hapo hakuathiri kitu chochote. Hali kadhalika ni lazima kunyonyesha kufanyike angalau mara tano ili kuharamike. Vinginevyo hakuathiri chochote. Chanzo: Nuur 'alaad-Darb (16A)

description

Mume Kunyonya Matiti Ya Mke Wake - Imaam Ibn ´Uthaymiyn

Transcript of Mume Kunyonya Matiti Ya Mke Wake - Imaam Ibn ´Uthaymiyn

Page 1: Mume Kunyonya Matiti Ya Mke Wake - Imaam Ibn ´Uthaymiyn

Mume Kunyonya Matiti Ya

Mke Wake

Fataawa Za Wanachuoni

Swali:

Je, mke huwa haramu kwa mume wake

akinyonya matiti yake mara nne?

Imaam Muhammad bin Swaalih bin

'Uthaymiyn:

Allaah Kamhalalishia mume kufurahi kwa

mkewe atakavyo. Anaweza hata kufanya

naye mapenzi kwa njia mbalimbali. Allaah

(Ta´ala) Kasema:

���ؤم �رث �م ���وا �رم أ�� ���م

"Wake zenu ni konde kwenu. Basi

ziendeeni konde zenu vyovyote

mpendavyo." (al-Baqarah 02 :223)

Zingatia kauli "basi ziendeeni konde zenu

vyovyote mpendavyo." Konde ni mahali pa

rutuba ambapo ni tupu ya mwanamke.

Hivyo ni halali kwa mume kufanya kitendo

cha ndoa kwenye tupu ya mke sawa

ikifanywa kwa mbele, kwa nyuma, kwa

kusimama, kwa kulala au kupitia nafasi

nyingine yoyote kwa sharti iwe ni kwenye

tupu yake ya mbele. Hali kadhalika,

anaweza kufurahi naye kwa kumkumbatia,

kumkisi na kumbusu vile apendavyo.

Kilichoharamishwa tu ni yeye [mume]

kufanya naye kitendo cha ndoa wakati wa

hedhi na liwati [nyuma].

Kulingana na kanuni hii ya jumla, anaweza

kunyonya maziwa ya mkewe. Hawi [mke]

haramu kwake [mume] hata kama lau

atakunywa maziwa yake. Haya ndio maoni

ya jamhuri. Ili kunyonyesha kuathiri ni

lazima mtu awe chini ya miaka miwili.

Baada ya hapo hakuathiri kitu chochote.

Hali kadhalika ni lazima kunyonyesha

kufanyike angalau mara tano ili

kuharamike. Vinginevyo hakuathiri

chochote.

Chanzo: Nuur 'alaad-Darb (16A)