Miaka 50 ya Mahkama Zanzibar

download Miaka 50 ya Mahkama Zanzibar

of 6

Transcript of Miaka 50 ya Mahkama Zanzibar

  • 8/14/2019 Miaka 50 ya Mahkama Zanzibar

    1/6

    MAHKAMA NDANI YA MIAKA 50 ILIYOPITA ZANZIBAR: MAFANIKIO NA

    CHANGAMOTO

    Na ALI UKI, MHADHIRI WA SHERIA, ZANZIBAR UNIVERSITY.

    TAREHE: 16 NOVEMBA, 2014

    Utangulizi

    Mahkama imetimiza miaka 50 tokea Mapinduzi ya Januari 12, 1964. Mahkama1, moja

    katika mihimili mitatu. Katika utekelezaji wa majukumu yake, Mahkama imepita katikavipindi saba tofauti vya uongozi wa nchi ama vimesaidia mafanikio au chachu za

    changamoto. Vipindi vya uongozi ni kuanzia 1964 mpaka 1972 chini ya uongozi wa

    marehemu Sheikh Abeid Amani Karume, kutoka 1972 mpaka 1984 chini ya uongozi wa

    Alhaj Aboud Jumbe, kutoka 1984 mpaka 1985 chini ya uongozi wa Alhaj Ali HassanMwinyi, kutoka 1985 mpaka 1990 chini ya uongozi wa marehemu Sheikh Idris

    Abduwakil, kutoka 1990 mpaka 2000 chini ya uongozi wa Dk. Salmin Amour, kutoka

    2000 mpaka sasa 2010 chini ya uongozi wa Mheshimiwa Amani Abeid Karume na 2010hada sasa chini ya uongozi wa Dk. Ali Mohamed Shein.

    Vipindi tofauti vya uongozi vimetoa misukumo ya mabadiliko, maendeleo na

    changamoto za Mahkama. Misukumo iliyotokea ambayo imeleta athari katika utendajikazi wa Mahkama imesababishwa na mapinduzi fikra za kuendesha mambo wenyewe,

    misukumo na mageuzi ya siasa, uboreshaji wa sekta ya Mahkama, upanuzi wa siasa za

    demokrasia na uhuru wa Mahkama.

    Mkusanyiko huu utasaidia kujenga taswira ya utendaji kazi wa Mahkama na kielelezo

    kikubwa cha mafanikio ya Mahkama. Michango itakayotolewa itakuwa ni kioo na

    itasaidia kuimarisha utendaji kazi wa Mahkama na wala haitokuwa chanzo cha chuki chakutizama sura ya aliyetoa mchango.

    Baadhi ya Vigezo vya Mafanikio na Changamoto zinazoikabili Mahkama Zanzibar

    Mafanikio na changamoto za Mahkama Zanzibar zinaweza kutathminiwa katika vigezo

    tofauti. Baadhi ya vigezo ni hivyi vifuatavyo:

    (i) Kisheria;(ii) Watendaji kazi;(iii) Ubora wa maamuzi (seriousness of judgements)yanayotolewa na Mahkama;(iv) Uhusiano wa uongozi wa Mahkama na watendaji kazi wa Mahkama;(v) Msukumo wa kisiasa katika utendaji kazi wa Mahkama;(vi) Uhuru wa Mahkama;(vii) Uelewa wa sheria wa wananchi;(viii) Imani ya wananchi kwa Mahkama za Zanzibar;

    1 Kifungu cha 5A (1) cha Katiba ya Zanzibar ya 1984 kinasema kwamba Zanzibar itafuata mfumo wa

    mgawanyo wa madaraka kati ya mamlaka tatu, Mamlaka ya Utendaji, Mamlaka ya Kutunga Sheria na

    Kusimamia Utekelezaji wa Shughuli za Umma na Mamlaka ya Kutekeleza Utoaji wa Haki.

  • 8/14/2019 Miaka 50 ya Mahkama Zanzibar

    2/6

  • 8/14/2019 Miaka 50 ya Mahkama Zanzibar

    3/6

    (8)Mahkama za Watoto5: Chini ya Sheria hii, Mahkama ya Watoto imeanzishwa nakesi za Mahkama hii zitasikilizwa na Hakimu wa Wilaya kinyume na awali

    Hakimu wa Mahkama ya Mkoa alipewa uwezo wa kusikiliza kesi zotezinazohusiana na mtoto.

    (9)Uhuru wa Mahkama6: Katiba ya Zanzibar ya 1984 inatambua uhuru waMahkama Zanzibar.(10) Majaji wa Mahkama Kuu kutoondolewa kiholela7. Majaji wamepewakinga maalum ya kuondoshwa katika nyadhifa zao. Awali Jaji wa Mahkama Kuu

    angeliweza kuondoshwa kwa mujibu wa utashi wa rais (at the pleasure of the

    president).(11) Kuanzishwa Sheria ya Mahkama Kuu8No. 2 ya 1985(12) Jaji Mkuu kutokuwa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi ya

    Mahkama: Baada ya malalamiko, Sheria ya Tume ya Utumishi imefanyiwa

    marekebisho na Jaji Mkuu sio mwenyekiti wa Tume.(13) Tume ya Utumishi ya Mahkama kutambuliwa katika Katiba9(14) Ongezeko la majaji: Mahkama Kuu ya Zanzibar ina jumla ya majaji sita

    wakiwemo majaji wanawake.(15) Kuwepo majaji na mahakimu wanawake: Majaji na mahakimuwanawake wamekuwa sehemu wa watendaji wa Mahkama wanaotoa haki.

    (16) Ongezeko la Mahakimu: Idadi ya Mahakimu imefikia 63, 47 wapoUnguja na 16 wapo Pemba.

    (17) Idadi ya Makadhi Imeongezeka: Wapo makadhi 15, 10 wapo Unguja(akiwemo Kadhi Mkuu na Naibu Kadhi Mkuu) na watano wapo Pemba.

    (18) Maslahi ya majaji na mahakimu kuongezwa: Maslahi ya watendajihawa yameboreshwa sana kulinganisha na taasisi nyengine. Lakini mahakimu wa

    Mahkama za Mwanzo wanasikitika.

    (19) Kuondoshwa Mahkama za wananchi (The Peoples Courts No. 11 of1969) ambazo zilizokuwa hazifuati mfumo wa sheria ya utoaji haki.

    (20) Ongezeko la majengo ya Mahkama Unguja na Pemba.(21) Kurejeshwa huduma za mawakili katika Mahkama Zanzibar.(22) Kurejeshwa huduma za mavakil.(23) Idadi ya mawakili walioruhusiwa na Mahkama Zanzibar kuongezeka.

    Zaidi ya mawakili 100 wamesajiliwa na Mahkama Kuu Zanzibar.

    (24) Mashirikiano ya Mahkama naasasi za kiserikali na kiraia kuongezeka.(25) Kuanzishwa Siku ya Mahkama (Law Day).

    5Sheria Namb. 6 ya 2011.6

    Kifungu cha 5A (3) kinasema kuwa hakuna mamlaka itakyoingilia Mamlaka nyengine isipokuwa na kwakadri ilivyoelezwa katika Sheria.7Kifungu cha 95 (5) cha Katiba ya Zanzibar kinasema kwamba Jaji wa Mahkama Kuu ataondolewa kazini

    na Rais ikiwa suala la kuondolewa kwake limepelekwa kwa Tume iliyoundwa kwa madhumuni hayo chini

    ya kijifungu cha (6) cha kijifungu hiki na Tume hiyo imependekeza kwa Rais kwamba Jaji huyo anafaa

    kuondolewa kutokana kazi zake au kutokana na tabia zake mbaya.8Sheria Namb. 2 ya 1985.9Kifungu cha 102 cha Katiba ya Zanzibar kinasema kwamba kutakuwa na Tume ya Utumishi ya Mahkama

    ambayo muundo, kazi na uwezo wake utakuwa kama ilivyoelezwa na Sheria iliyotungwa na Baraza la

    Wawakilishi.

  • 8/14/2019 Miaka 50 ya Mahkama Zanzibar

    4/6

    Changamoto za Mahkama Zanzibar

    (1)Rushwa:Tuhuma za harufu ya rushwa kuwepo kwa baadhi ya watoa maamuziwa Mahkama. Ni vigumu kuithibitisha kwasababu wanaolalamika hawapo tayari

    kutoa ushahidi. Vile vile, malalamiko yanasikika baada ya kutolewa maamuzi nasio wakati kesi inaendelea. Aidha, kuwepo watu wa kati wa kuunganisha rushwa(middlemen)baina ya baadhi ya watoa haki na wahusika wa kesi/shauri. Rushwa

    ya Mahkama imegawika mafung yafuatayo: (a) rushwa ya muhali (b) rushwa ya

    fedha na (c) rushwa ya hisia (perceived corruption).(2)Tuhuma za ushawishi wa wanasiasa kuingilia utendaji kazi wa Mahkama

    Zanzibar. Inadaiwa kwamba mwenendo na maamuzi ya kesi yanashika (influence)

    na nguvu za wanasiasa wa ngazi tofauti.

    (3)Mahkama kuwa masafa marefu na wananchi: Inakuwa vigumu wananchikwenda mahkamani. Kwa mfano, mkaazi wa Tumbatu au Nungwi inambidi

    asafiri hadi Mfenesini ikiwa kesi/shauri linalomhusu lipo katika Mahkama ya

    Mkoa, Mfenesini. Tatizo la masafa linaumiza zaidi kesi inapoingia hatua ya rufaakatika Mahkama ya Mkoa au Mahkama Kuu ya Zanzibar.

    (4)Majengo ya Mahkama ni mabovu na makongwe: Mfano wa jengo la Mahkamala Makunduchi na Mfenesini.

    (5)Ukosefu wa nafasi katika majengo ya Mahkama: Kwa mfano, jengo laMahkama Kuu, Zanzibar lilijengwa mwaka 1908 kukidhi idadi ya wananchi ya

    wakati huo, lakini halijafanyiwa utanuzi na linafanyiwa mabadiliko ya ndani

    (internal modification).Baadhi ya Mahakimu hulazimika kutumia chumba kimojakuendesha kesi tofauti tena kwa wakati mmoja. Jengo la Mahkama ya Wilaya ya

    Mwanakwerekwe halitoshi na Afisi ya Waendesha Mashtaka ni ndogo mno.

    (6)Uelewa mdogo wa sheria: Idadi kubwa ya wananchi hawafahamu sheria nabaadhi ya wakati wanatarajia Mahkama iamue kwa kufuata matamanio yao.

    (7)Ukosefu wa Maktaba:Mahkama haina maktaba ya kisasa, ukosefu wa ripoti zasheria na vitabu vya sheria vitakavyowasaidia majaji na mahakimu kuongeza

    uwezo.(8)Ukosefu wa usafiri kwa Mahakimu:Kinyume na majaji, mahakimu hulazimika

    kutumia usafiri wa umma na baadhi ya wakati kujikuta wapo pamoja ndani ya

    gari na ndugu au jamaa ya wahusika kesi jambo ambalo huwatia hofu ua usalamawao.

    (9)Bajeti ya Mahkama ni finyu:Bajeti ya Serikali imekuwa ndogo na kikomo chabajeti (ceiling) kinatolewa na Wizara ya Fedha. Aidha fedha zinazoinishwa na

    Baraza la Wawakilishi zinapatikana kwa asilimia chache. Kwa mfano mwaka wafedha 2010/2011, jumla ya shilingi 550,000/- za bajeti ya maendeleo

    ziliidhinishwa lakini zilizopatikana ni shilingi 275,000,000/-, mwaka wa fedha

    2012/2013 jumla ya fedha za bajeti ya maendeleo zilizoinishwa na Baraza la

    Wawakilishi ni shilingi 100,000,000/- lakini zilizopatikana ni asilimia 17 tu yafedha hizo. Mwaka wa fedha 2013/2014 jumla ya fedha za bajeti ya maendeleo ni

    shilingi 150,000,000/- lakini hapana uhakika wa kupatikana fedha zote.

    (10) Mashahidi kutofika mahkamani: Imekuwa tabia baadhi ya mashahidikutofika mahkamani kutoa ushahidi. Hii inaathiri mno maamuzi ya Mahkama.

  • 8/14/2019 Miaka 50 ya Mahkama Zanzibar

    5/6

    (11) Ucheleweshaji wa kesi: Baadhi ya watendaji wa Mahkamawanatuhumiwa kuchangia kwa kiasi kikubwa kesi kuchelewa kwa visingizio

    tofauti.(12) Mzigo mkubwa wa kesi kwa mahakimu: Kwa mfano, hakimu wa

    Mahkama ya Mkoa alikuwa na wastani wa kesi 59 kwa mwaka 2012.10

    Hakimu

    wa Mahkama ya Wilaya alikuwa na wastani wa kesi 178 kwa mwaka 2012.

    11

    Hakimu wa Mahkama ya Mwanzo alikuwa na wastani wa kesi 104 kwa mwaka2012.

    12Wastani wa kesi wa Jaji wa Mahkama Kuu ni 14 kwa mwaka 2012

    13

    (13) Utafiti hafifu na uwezo mdogo wa watendajiwa Mahkama. Baadhi yamaamuzi ya Mahkama katika ngazi zote yanaonyesha kukosekana utafiti wa kinawa marudio na uchambuzi makini. Baadhi ya mawakili waliohojiwawalisema

    kwamba inasikitisha kuona kwamba watendaji wa Mahkama wa ngazi zote

    wanashindwa kufahamu utaratibu wa mwenendo wa kesi (procedure)na kuathiri

    haki. Aidha. makadhi wanalalamikiwa kutotumia kitabu au vitabu vya aina moja.Kila kadhi anategemea kitabu anachokipendelea binafsi. Hii inasabisha tofauti ya

    maamuzi kwa mujibi wa vitabu vya marejeo.

    (14)

    Majaji na mahakimu kufunga ushahidi:Baadhi ya wakati, majaji aumahakimu kufunga ushahidi. Jukumu la kufunga ushahidi la la upande wa

    mashtaka. Athari yake ni kukatwa rufaa, mfano Mahkama ya Rufaa Tanzania

    lakini maamuzi ni kesi ianze kusikilizwa tena jambo ambalo linaathiri mno

    upatikanaji wa mashahidi kwa mara ya pili.(15) Mahakimu wapya kutopata mafunzo ya Mahkama: Baadhi ya

    mahakimu wanaajiriwa moja kwa moja kutoka Chuo Kikuu na bila ya kupata

    mafunzo wanapewa kesi. Matokeo yake ni ukiukwaji wa utaratibu katikaupatikanaji wa haki. Inadaiwa kwamba baadhi ya mahakimu wapya hawajiamini

    na wanababaika mno anapokuwa wakili mbele yao.

    (16) Majaji na Mahakimu:Utafiti umeonyesha kwamba baadhi ya mawakiliwanalalamika kwamba majaji na mahakimu wanaegemea zaidi upande wamashtaka katika kuendesha kesi na baadhi ya wakati majaji/mahakimu

    wanajisahau na kuuliza maswali kama wanawasilisha kesi (make submission,)

    wanauliza maswali ya kujenga kesi ya upande wa mashtaka dhidi yawalalamikiwa.

    (17) Majalada ya kesi kufichwa: Utafiti unaonyesha kwamba baadhi yamakarani ama kwa kupewa maelekezo na majaji au mahakimu auwanawasingizia, huficha majalada ya kesi ili kudhoofisha utendaji wa haki.

    (18) Baadhi ya Majaji na mahakimu kuwachagulia wakili wahusika wakesi: Ushahidi unaonyesha kwamba watoa haki huwapigia simu mawakili na

    kuwaelekeza kupokea kesi kutoka kwa mlalamikaji au mlalamikiwa. Kitendo hikikinadhoofisha haki kutendeka na kuonekana kutendeka.

    (19) Vitisho dhidi ya wahusika wa kesi:Utafiti unaonyesha kwamba baadhiya majaji na mahakimu ni wakali sana na hutoa kauli zinazowatisha au

    kuwakatisha tama wahusika wa kesi.

    10Tanzania Human Rights Report, Part II on Zanzibar, 2012, pg 321.11Ibid.12Ibid, pg. 322.13Ibid, pg 321.

  • 8/14/2019 Miaka 50 ya Mahkama Zanzibar

    6/6

    (20) Mahudhurio ya majaji na mahakimu kazini: Utafiti unaoyeshakwamba mahudhurio ya waheshimiwa hawa yanalalamikiwa. Wanafika na

    kuondoka kazini kwa kufuata ratiba binafsi za mambo yao.(21) Kigezo kinachotumiwa na Jaji Mkuu kupanga kesi:Utafiti unaonyesha

    kwamba Mheshimiwa Jaji Mkuu hana kigezo maalum cha kupanga kesi kwa

    majaji wa Mahkama Kuu. Baadhi ya wakati, majaji wanalalamikiwa kukataakupokea kesi bila ya sababu ya msingi ya sheria.(22) Wazee wa Mahkama: Inalalamikiwa kwamba Vifungu vya 239, 240,

    242, vya Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Namb. 7 ya 2004 hakifuatwi

    katika kuteua wazee wa Mahkama na wengine hawana uwezo wa kusoma.(23) Uteuzi wa Majaji:Inashauriwa kwamba mawakili wakazingatiwa katika

    uteuzi wa majaji wa Mahkama Kuu ili kupatikana watendaji wazuri wa kutoa

    haki.

    (24) Kuondoshwa kazini mahakimu:Utafiti unaonyesha kwamba baadhi yamahakimu waliondoshwa kazini kwa visingizio vya siasa.

    (25) Imani ndogo ya wananchi kwa Mahkama:Utafiti umeonyesha kwambawananchi wa Zanzibar wana imani ndogo ya uwezo na uadilifu wa baadhi yawatendaji wa Mahkama na wanasikika wakisema kwamba haki itapatikana

    Mahkama ya Rufaa ya Tanzania na Haki haipatikani Mahkama za

    Zanzibar

    (26) Vifaa vya kisasa vya teknolojia katika shughuli za Mahkama.Hitimisho

    Yaliyoelezwa katika mada hii ni machache kati ya mafanikio na changamoto za

    Mahkama. Mafanikio na changamoto nyengine zitaelezwa na washiriki. Ni muhimu

    Mahkama ikawa makini kusikiliza hususan changamoto ili kuzifanyia kazi kwa

    madhumuni ya kufanikisha utendaji wa haki. Maoni yatakayotolewa na washirikiyasitumike kama daraja la kujenga chuki baina ya washika dau wa sekta ya Sheria.

    Inawezekana baadhi ya mafanikio na changamoto zimesababishwa na Sheria ziliopo.Uongozi wa Mahkama ujitahidi kuboresha baadhi ya mambo na kushinikiza

    kuongezwa zaidi bajeti ya Mahkama ambayo imekuwa kikwazo cha utendaji haki

    hapa Zanzibar.