MATENDO YA LAZIMA YA MALISHO BORA KITABU KYA MAMA … file1 matendo ya lazima ya malisho bora kitabu...
Transcript of MATENDO YA LAZIMA YA MALISHO BORA KITABU KYA MAMA … file1 matendo ya lazima ya malisho bora kitabu...
1
MATENDO YA LAZIMA YA MALISHO BORA
KITABU KYA MAMA KIONGOZI WA KUNDI
LA AFIA KITABU KYA PILI
Module 2 of 6
2
SHUKRANI
Hanold, Mitzi J. na Wetzel, Carolyn (2009), matendo ya la-zima ya malisho bora.Washington DC. Chakula kwa ajili ya njaa,
inawezekanisha kupitiya musaada yenye ilipewa na of-fisi ya
chakula kwa ajili ya amani, offisi ya democratia, mi-zozano,
musaada wa kibinadamu na chirika ya marekani kwa ajili ya maendeleo ulimwenguni chini ya namba FFP-A-00-08-00072-00
Maonyi yenye kuwa umu ni ya waandishi na haiusishi shirika ya
marekani kwa ajili ya maendeleo ulimwenguni Shukrani kwa maitre Wabangu, Octavio Gonzales, na Petra
Rohr-Rouendaal, na uwaziri wa afia wa serkali ya Congo ya ki democratia pamoja na UNICEF.Acknowledgements
3
Lesson 1: First Foods Not Eating (Picture 1.1)
Mama Mubaya alifata ma shauri ya mama muzuri na
akamnyonyesha mateso kwa maziwa yake tu hadi miezi sita na
yeye mwenyewe alienda kwa mganga kupata vitamine A mu myezi mbili kisha kuzaa na yeye na mtoto wake mateso
wanakuwa na afia bora.
Wakati mateso anaeneza miezi sita, mama mubaya anaaanza kumupa buyi na mateso amekataa kunywa ile buyi. Wajirani
wana muhimiza ma-ma mubaya na kumueleza kama
anamukunywisha mateso buyi mubaya. Mama mateso hadjuwi ginsi ya kufanya
? NI VIZURI KWA MTOTO KUKATAA CHAKULA MPYA ?
? NI WAKATI GANI TUNAHITAJI KUMUPA MTOTO CHAKULA MUPYA ?
4
Not Eating (Picture 1.1)
5
Breast Feeding (Picture 1.2)
• Tangu miezi sita mama Muzuri anamupatiya Furaha chakula
kusudi akomale vizuri
• Anamupikiya buyi ama chakula ya kupondwa, kutiya amo mafuta kisha kuitosha ku moto
• Kutiya mafuta yenye hayikutshamushiwa ku moto inaleta nguvu kuzidi ile mafuta ya kutshamushi-wa
• Mu djuma ya kwanza yenyewe banaanza kumupa mtoto buyi, banamupa pao moja ao mbili ya buyi ya teketeke mara
moja ao mara mbili kwa siku. Kumunyonyesha mtoto mbele
ya kumupa buyi kwa kumuzoesha ku chakula mupya. • Mama Muzuri anapashwa kumunyonyesha mtoto wake Furaha mpaka miaka mbili ao kupita
• Maziwa ya mama ndiyo chakula ya muhimu kwa watoto wa
ile miezi • Inafaa kunyonyesha mtoto kila wakati anapohitaji chakula • Maziwa ya mama inasaidiya kukinga mtoto kwa magonjwa
mbali mbali
? TUTAFANYA NINI KAMA MTOTO ANAKATALA KULA BUYI?
• Kumusemecha vizuri na kumuhimiza akule ile buyi
• Kumuimbiya mimbo kwa kumuhimiza anywe ile buyi
• Kumulisha polepole na kuwa muvumilifu
• Kuongeza maziwa ya mama ndani ya buyi. Inasaidiya mtoto kuzoeya chakula mupya. Atadjuwa harufu na utamu wake
• Tusimukaze mtoto ili akule kwani chakula inaweza kuingiya
ndani ya mafafa wakati mtoto analiya
• Kama unapata chakula yenye mtoto anapenda, inafaa kumupatiya ayo
6
Breast Feeding (Picture 1.2)
7
Adding New Foods (Picture 1.3)
• Siku ine ya kwanza yenye wanamupa Furaha buyi, wana
mupa tu buyi yenye inachanga bun-ga ya chakula yenye
inakuliwa sana na mafuta. Kisha siku ine anaongeza amo chakula ingine
• Anaweza kuongeza amo samaki ya kupondwa, maharagi ya
kupondwa ama chakula ingine
• Inafaa ma siku chache kwa butumbu ya mtoto kuzoeya ile chakula ya mupya
• Kuongeza ingine chakula kasha siku ine kwa kuona kama
butumbu tumbu inaizoweya
• Kama hakuzoweya ile chakula mupya mu ile siku ine, inafaa kuibadirisha na kumuongezeya ingine
? NI CHAKULA GANI TUTAONGEZA KU BUYI DJU YA KUIFANYA
IKUWE YA MALISHO BORA?
• Kuongeza mafuta na lutuba ya kalanga ndani ya buyi • Kuongeza bipande ya nyama yenye kupondewa, mayayi na
mboka ya majani yenye kuponde-wa
• Kuongeza chakula ya mizizi ao matunda yenye na rangi ya manjano ao ya mwekunda ndani ya buyi kwa kumuongezeya
mtoto vitamine A ndani ya mwili • Kuongeza matunda, chakula ya mizizi ao mboka ya majani
yenye kutwangiwa
8
Adding New Foods (Picture 1.3)
9
Quantity of Food for Each Feeding (Picture 1.4)
• Tangu miezi sita hadi munane, analisha mtoto wake mara tatu kwa siku
(busubuy, kisha midi na mangaribi) • Tangu miezi sita hadi munane, mama anamupa mtoto wake kopo ya buyi
yenye kuwa mapawo ine ya supu kwa kila chakula. Ndani ya ko-po ya plastic, buyi inapasha kuwa ku mustari wa pili kuanziya chini na ndani ya kopo ya musaada buyi inapashwa kuwa kati ya kuanziya chini na mukono wa
kopo kwa kila chakula • Tangu miezi kenda hadi kumi na moja, analisha mtoto wake mara ine kwa
siku • Tangu miezi kenda hadi kumi na moja, mama anamupa mtoto wake ndani ya
kopo ya plastic, buyi inapasha kuwa ku mustari wa pili kuan-ziya chini, na ndani ya kopo ya musaada buyi inapashwa kuwa ku mukono wa chini wa ile
kopo kwa kila chakula • Mama anaanza kumupa mtoto wa miezi kenda hadi kumi na moja ma
chakula ingine kidogo kidogo kati ya ma chakula • Mama anaikala karibu na mtoto wake na anamufundisha namna ya kula • Mama anaweka akili yake yote kwa mtoto wake • Ginsi mtoto eko anakomala ndjo ginsi mama muzuri ana muongezeya
chakula kwa kiasi na mara ya kula
• Tangu miezi kenda hadi kumi na moja, anamupa mtoto chakula yenye mtoto anaweza kula yeye mwenyewe kwa mikono yake kama vile papayi, hembe,
bitika, chungwa • Kuendeleye kumunyonyesha mtoto wakati wote mwenye anahitaji hadi
miaka mbili na kupita • Maziwa ya mama ina maji yote yenyewe mtoto wa chini ya mwaka moja
anahitaji. Kama mtoto analomba maji ya kunywa, inafaa kumupa-tiya maji ma safi yenye kuwa na dawa ya kuisaficha
• Kumupa mtoto buyi mu kopo ama mu sahani kwa kujuwa kiasi gani anakula
KAZI : KUONESHA GINSI YA
KUPIKA BUYI YA KWANZA YA
Mazoezi
Chunguza Onya Uliza Angaliya
10
Quantity of Food for Each Feeding (Picture 1.4)
11
Lesson 2: Feeding During the Second Year (12-23
months)
Still Hungry (Picture 2.1)
Katika picha hii tunahadisi hii: Saa kidogo kisha kula, mateso
anasikiya tena ndjala. Ma-ma mubaya anamupikiya mateso kila
siku buyi mingi mara tatu. Hawezi kumaliza ile buyi yote kwa
mara moja. Kisha saa kidogo, mateso anasikiya tena ndjala. Mama muba-ya anasilika na anapenda meteso akule chakula
mingi kwa mara moja sababu hana na wakati wakupiga saa
yote. Hana na wakati wakupiga chakula mara tano kwa siku
? MUNAWAZA KAMA MAMA MUBAYA ANA SHERIYA YA KUMUKASIRIKIYA MATESO?
? MARA NGAPI KWA SIKU TUNAWEZA KUMUPATIYA MTOTO WA MWAKA MOJA HADI MBILI CHAKULA ?
? KIASI GANI MUNAWEZA KUWAPA KWA KILA CHAKULA ?
12
Still Hungry (Picture 2.1)
13
Feed First (Picture 2.2)
• Mama muzuri na bwana yake wanamupatika mtoto wao Furaha chakula ndani ya sahani kwa kuweza kutambuwa
kiasi kyenyewe anakula
• Tangu mwaka moja mtoto anapata nguvu mingi ndani ya
chakula kuliko ndani ya maziwa ya kifuwa ya mama yake • Tangu mwaka moja, mama Muzuri anapatiya mtoto wake
Furaha mbele chakula kisha anamunyonyesha
• Mama muzuri anamunyonyesha mtoto wake Furaha wakati
wote, busiku na mchana wakati anahitaji. Na ataendeleya hivi hadi miaka mbili
14
Feed First (Picture 2.2)
15
Quantity and Frequency Increased (Picture 2.3)
• Tangu mwaka moja hadi miaka mbili anamupatiya furaha
mara tatu chakula ya jamaa • Anamuongezeya chakula ingine ya kidogo mara moja wakati • Furaha ana miezi kumi na mbili hadi kumi na saba.
• Anamuongezeya chakula ingine ya kidogo mara mbili wakati
Furaha anakuwa na miezi ya kupita kumi na saba
• Anaendeleya kumusaidiya na kumuhimiza Furaha akule chakula
• Anaongeza kiasi na mitindo ya chakula
? KAMA FURAHA ANAGONJWA, MAMA YAKE ATAELENDELEYA KUMUPATIYA CHAKULA KWA KILE KILE KIASI?
• Mama Muzuri atamulicha kwa kile kile kiasi, atamupatiya
maji mingi na kumunyonyesha kupita wakati wa kawaida • Wakati mutoto ana gonjwa bwaki (ni kwa sababu hakupata
chakula muzuri kwa wakati murefu) an-aweza kupoteza
hamu ya kula chakula • Mama Muzuri anahitaji kumuhimiza Furaha kutumiya chakula na kumuongezeya chakula ingine
• Wakati na kisha magonjwa mama Muzuri anapashwa
kumupatiya mtoto chakula mingi kupita wa-kati wa kawaida kwa kumusaidiya mtoto kurudisha nguvu
16
Quantity and Frequency Increased (Picture 2.3)
17
Daily Nutrients Needed (Picture 2.4) ─ 5 minutes
• Kwa kila chakula Furaha atakula kipande ya kopo ya plastic
ama kopo ya musaada kati ya mikono yake
• Kunakuwa vitu vya lazima vyenye mtoto wa mwaka moja hadi mbili anahitaji kula kama vile: maharagi, mandjekele,
kunde, maboke, mboka ya majani ya rangi ya maji ya
sombe.
• Matunda kama vile chungwa, bitika, mahembe. • Mafuta ama blue band. Nyama, mayayi, maziwa, samaki. • Chakula ya rangi ya mwekunda ao manjano kama vile
mahembe, bitika, chungwa, papayi, ndizi; byote bya kuivya
• Chakula ingine kidogo kidogo sawa vile mikate, kalanga, matunda ao mihindi
KAZI : KUONESHA KIASI KYA CHAKULA KYENYEWE MTOTO ANAHITAJI KULA KWA
SIKU
Mazoezi
Chunguza Onya Uliza Uliza
18
Daily Nutrients Needed (Picture 2.4)
19
Lesson 3: Sanitary Food Preparation and Cleanup
Worms and Sickness (Picture 3.1)
Katika picha hii tunahadisi hii: Mama Mubaya anapima kufata ma shauri yenye alipewa na mama Muzuri. Anamupigiya Mateso buyi, chakula ya jamaa na ma chakula ingine kidogo
kidogo, lakini Mateso eko wakati wote mugonjwa na an-agonda. Wakati moja Mateso anaharisha kwa masiku mingi na
anapoteza hamu ya kula chakula. Wakati mwingine, mitchango inaonekana ndani ya choo kubwa ya mateso. Mama mukwe wa
mama Mubaya na wengine wandugu yake wa jamaa wanamueleza kama asifazaike kwani watoto wote
wanagonjwaka, na kuhara haina hatari. Asifazaike kabisa
sababu ya hiyi vitu
? MUNAFIKIRI NINI KWA HIYI MASWALI YENYE MAMA MUKWE
WA MAMA MUBAYA ANASEMA?MUNAFIKIRI KAMA KUHARA
NI SHIDA KUBWA?
? KUPITIYA HIYI PICHA, MUNAONA VITU VINGINE VYENYE VIN-AFANYA MATESO AUGUWE KILA SIKU?
20
Worms and Sickness (Picture 3.1)
21
Spoiled Foods and Hands (Picture 3.2)
• Kuna njia mingi yenyewe mtoto anaweza kupata magonjwa
ao kuhara • Njia ya kwanza ni kupitiya bitu byenyewe anatiya kukinywa • Kula vitu vyenye havifinikwi, vya baridi vienyewe kufanya
zidi ya saa tatu inaweza kuleta magonjwa
• Kutumiya mikono michafu mbele ya kula ama mbele ya
kupika chakula inaweza kuleta magonjwa • Hiyi mienendo inaweka mtoto ku hatari ya kutokukuwa
muzuri na kupata bwaki kwa urahisi.
• Vitu vichafu umuleteya mtoto kuhara na mitchango
? MUNAFIKIRI KAMA JAMAA INAWEZA KUFANYA KITU KWA KUEPUKI-SHA WATOTO WAO WAPATE MAGONJWA YA
BWAKI? NAMNA GANI?
• Vitu vyenye wenye kuusika na afya ya watoto katika ma
jamaa wanaweza kufanya vina weza kuleta tafauti saana
kwa maisha ya watoto • Kila maisha ni ya mafaa na inakuwa na lazima saana. Maisha ya mtoto inahitajika ku-kingwa na kila hatari
• Kwa kuwa na usafi na kufanya vitu visafi tunaweza kusaidiya
watoto kushinda ma-gonjwa na kuishi vizuri
Spoiled Food and Hands (Picture 3.2)
22
23
Preparing Hands, Foods and Utensils (Picture 3.3)
• Kusafisha na maji na sabuni inatosha butchafu, mayayi ya mitchango na vitu vyenye kuleta magonjwa kupitiya chakula
na vyombo vya kupikiya
• Maji yenyewe haitoshi kusafisha mikono, mpaka sabuni ao majifu ndjo inaweza kuuwa vidudu vyenye kuleta magonjwa
• Wenye kupika chakula wanapashwa kunawa maji na sabuni
ama majifu mbele ya kupika chakula ao mbele ye kuokesha
watoto • Wenyewe kuhudumiya watoto wanapashwa kusukula mikono ya watoto wao na maji na sabuni mbele ya kuwalisha
chakula
• Chakula yote ya kuliwa mubichi inapashwa kusafishiwa na sabuni na maji masafi kwa kusaidiya kuuwa mayayi ya mitchango yenye inaweza kuletewa na ile chakula
24
Preparing Hands, Foods and Utensils (Picture 3.3)
25
Cook Food Well and Cover (Picture 3.4)
• Chakula yenyewe haipikiwe inaweza kuwa na mayayi ya
mitchango. Ile mayayi inakufa kama chakula inapikiwa ku moto
• Jamaa inapashwa kula chakula yenye kupikiwa na wakati ingali moto. Musiache buyi ao supu ipole mbele ya kuikula
• Kufinika tchakula hadi wakati wa kuikula. Kisha kula, ile chakula
inabaki inafaa kuifinika na mufuniko ama nguo kusudi ma inzi isiingiye ndani. Inzi inaleta ku chakula choo kubwa na uchafu
kidogo saana yenye macho haiwezi kuona
• Tuchunge chakula fasi muzuri na ya baridi, mbali na bulongo. Funika chakula na kipande kya nguo kisafi kwa kufanya ikuwe
baridi
• Kutchamusha kila siku chakula yenyewe tuliweka ili ikuwe moto mbele ya kuikula
• Tuchunge chakula mu kabati ama kuifunika
• Kutupa chakula yenyewe ilibaki muda wa saa tatu
• Kutchamusha chakula ya maji maji kama vile buyi ama supu
yenye ili tchungiwa. Kama ile buyi ama supu ilisha fanya saa tatu
inafaa kuitupa
• Chakula ya nguvu kama vile ugali, wali, samaki, nyama, viazi
inastahili kuliwa ata iko baridi. Lakini kama inaisha fanya saa ta-
tu, tunastahili kuitupa.
KAZI : KUONESHA GINSI YA KUFIKA CHAKULA NA MITINDO YA MIFINIKO
YENYEWE TU-NAWEZA KUTUMIYA
Mazoezi
Chunguza Onya Uliza Uliza
26
Cook Food Well and Cover (Picture 3.4)
27
Lesson 4: Vitamin A
Too Expensive (Picture 4.1)
Katika picha hii tunahadisi hii: Mama Mubaya alisikiya
mafundisho kutoka kwa wa ma-ma viongozi wa gundi la afya kama inafaa kuongeza chakula ya rangi mbali mbali kwa
chakula yake. Anakutana muuzishadji mumoja anauzisha
chakula ya rangi mbali mbali. Huyu muuzishadji anamueleza kama ile chakula inasaidiya mtoto kuwa na afia bora. Mama Mubaya anaangaliya ile chakula na anafazaika saana sababu
hawezi kununuwa ile chakula yote kila djuma hata akipenda
mtoto wake akuwe na afia bora.
Siwezi kununuwa hiyi chakula yote kasema mama Mubaya, akatoka karibu na yule muuzishadji kwani hana pesa nyingi.
Angalipendeleya akuwe na pesa mingi.
? MUNAWAZA KWA IYI SHIDA INAKUWA NA MAMA MUBAYA?
? KUKO WAKATI MUMOJA NA NYINYI MUNA KUWA NA SHIDA HIYI?
? SHAURI GANI MUNAWEZA KUMUPA MAMA MUBAYA?
28
Too Expensive (Picture 4.1)
29
Foods with Vitamin A (Picture 4.2)
• Nyama ya mafuafua, minofu ya nyama ya rangi mwekunda, samaki, viazi ya kishenzi na papayi ina Vitamine A mingi
• Mafuta ya ngazi, ndizi na mandjekele ina Vitamine A mingi
lakini haizidi nyama ya mafuafua, minofu ya nyama ya rangi
mwekunda, samaki, viazi ya kishenzi na papayi • Chakula ya majani sawa vile sombe, lenga lenga, matembele, kisinsa na ngai-ngai ina Vitamine A lakini haipiti
mafuta ya ngazi, ndizi na mandjekele
• Hembe ya kuivya ina Vitamine A lakini Haipiti iyi ma chakula yote tulitaja uku juu
• Hii ma chakula yote ina Vitamine A yenye kusaidiya kukinga kwa magonjwa mbalimbali. Vitamine A inasaidiya mtoto
kuwa na afia bora • Wazazi wanahitaji kuwapa watoto chakula yenye Vitamine A
kwa wingi (sawa vile ile chakula yenye kuwa ku mustari wa kwanza) mara moja kwa juma. Iyi chakula iko na Vitamine A
mingi na haistahili kuliwa kila siku • Wazazi wanaweza pia kuwapa watoto wao chakula yenye
Vitamine A kidogo lakini wanahitaji kuwapa ayo kila siku ao
mara mingi kwa juma • Chakula yenye rangi ya mwekunda ao ya manjano ndani na
inje iko na Vitamine A mingi
• Mboka ya majani ama mafuta ya ngazi inapoteza Vitamine A
kama inatchamushwa kwa motomingi na muda mu-refu saana. Tunahitaji kuipika kwa muda kidogo
• Kama ikiwezekana tukule mboka ya majani bila kupika
inaweza kuwa vizuri saana kwani Vitamine A iko mingi
• Matunda ya kuivya saana na inakuwa teketeke inaupungufu wa Vitamine A, inafaa kula matunda ya kuivya lakini apana ya kuivya saana.
30
Vitamin A (Picture 4.2)
31
Night Blindness (Picture 4.3)
• Alama yenye kuonesha kama Vitamine A inakosa ku mwili ni upungufu wa kuona wakati busiku bunaanza kuingiya
• Kama chakula yenye Vitamine A kwa uwingi ama vidonge
vya Vitamine A havipewi kwa mtu mwenye kuonesha alama
hiyi, anaweza kuwa kipofu • Ma nukta itatoka ku ile fasi mweupe ya macho • Kama upungufu wa Vitamine A uki endeleya kwa mtoto ao
mukubwa atabakiliya kipofu lote
• Vitamine A inasaidiya ku kinga macho na kuiweka na afia njema
• Watoto wengi wanakuwa na upungufu wa Vitamine A lakini hawana alama ya kutokuona muzuri wakati wa usiku
kuingiya ama nukta kwa macho lakini wanakamatika na magonjwa saa yote na ma-gonjwa mbalimbali
? KWA NINI NI LAZIMA KWA WAZAZI KUTAFUTA MATUNZO KWA WATOTO WAO WAKATI WANA ONESHA HII MA ALAMA TUNATAJA HAPA JUU ?
• Upungufu wa kuona wenye unatokana na ukosefu ama
upungufu wa Vitamine A inaonesha alama ya kusema kama mwili una hitaji musaada
• Kama mwili haukupata ule musaada wa Viatmine A, mtoto
atakua kipofu milele
• Vitu sisi wazazi tutafanya inaweza kuleta faida na mabadiriko kwa afia na maisha ya watoto wetu
32
Night Blindness (Picture 4.3)
33
Vitamin A Supplements (Picture 4.4)
• Mama mwenye kutoka kuzaa anahitaji kupata kidonge ya Vitamine A mu miezi mbili yenye kufata kuzaa, itamusaidiya kuwa na afia nzuri na kwa hiyo tutakuwa na uhakika kama
mtoto wake atapata Vitamine A kupitiya maziwa ya mama
yake • Wakati mtoto anaeneza miezi sita inafaa kumupatiya kidonge ya Vitamine A, na kisha iyo anahitaji kupata
kidonge ya Vitamine A kila miezi sita hadi atafikisha miaka
tano mtoto mwenye suluba, magonjwa ya nguvu ama bwaki anapashwa kwenda ku senta ya afia kwa kupewa vidonge
ya Vitamine A • Watoto wagonjwa na wale wanaotoka mu magonjwa
wanapashwa kula chakula yenye Vitamine A mingi kwa kuwasaidiya kurudisha kilo yao yenye walipoteza sababu ya
magonjwa • Vitamine A inasaidiya kukinga kwa magonjwa zaidi ile ya
nguvu na inasaidiya kufupisha muda wa magonjwa
KAZI : KUONESHA CHAKULA YENYE
VITAMINE A KWA UWINGI
Mazoezi
Chunguza Onya Uliza Angaliya
34
Vitamin A Supplements (Picture 4.4)
35
Lesson 5: Nutrition Rich Foods
Seeing is Believing (Picture 5.1)
Katika picha hii tunahadisi hii: Bwana wa mama Mubaya alitambua kama muke wake aliongeza chakula ingine nyingi ya
mupya katika chakula ya jamaa, ijapokua mbele hakukubaliana
na mke wake, lakini alitambua mabadiriko mingi katika afya ya mateso, na sasa mtoto mateso anakua na nguvu na afya nzuri.
Jamaa nzima inakuwa na afia nzuri tangu wakati walianza
kutumiya chakula mupia. Kumwanzo sikuwa nakubali kama hiyi
chakula ya mupia inaweza kusaidiya watoto, Sasa nimeona na nimekubali kasema bwana yake ya mama mubaya.
• Baba mateso anacheza na watoto wake • Baba mateso anafurahi namna gani watoto wanaguwa na kukomala vizuri
• Baba mateso anamupa moyo na kumueleza bibi yake
aendeleye kwa ile njia
? MUMEONA MABADIRIKO GANI MAZURI NDANI YA AFYA YA WATOTO WENU?
? CHAKULA GANI UNAWAZA INAWEZA KUONGEZEWA KATIKA CHAKULA YA MUTOTO WAKO KILA JUMA
37
Seeing is Believing (Picture 5.1)
38
Malnutrition (Picture 5.2)
• Katika picha ya kwanza tunaona kama chakula ya mtoto ni
ile ile moja. Chakula ile hamupatikani vifaa vingi vya afia kama vile maharagi, mandjekele ama mandizi.
• Anapata magonjwa kwani mwili wake umekosewa vifaa vya
afya ambavyo vinaweza kumusaidiya kujikinga
• Chakula yenyewe haina vifaa vya afia vyenye anakula inamuweka muzaifu kwa magonjwa
• Magonjwa ina fanya mtoto anapoteza hamu ya kula chakula
• Mtoto anapoteza kilo yake, mwili wake unashindwa kupikanisha magonjwa na anende-leya kugonjwa na kula
kidogo
• Mwisho anagonjwa saana na anakuwa mu hatari ya kufa • Kula mubaya inafanya apoteze kilo na akuwe mu hatari ya kufa
? MUNAWAZA KAMA MAMA ANAPASHWA KUBADIRISHA
NAMNA YA KUL-ISHA WATOTO WAKE? SABABU GANI?
• Maisha ya mtoto ni ya lazima kubwa na inastahili • Mupango wenyewe mama anakamata inaweza kuokowa
maisha ya mtoto
39
Malnutrition (Picture 5.2)
40
Nutrient Rich Foods for Children Ages 12 to 23 Months
(Picture 5.3)
• Tupatiye watoto chakula yote yenye kuwa ndani ya miviringo yote. Kama hautaweza kumupa ile mitindo yote ya chakula mara moja, umupe ile ulisahau kama vile chakula kidogo
kodogo muma wakati ingine mbele ya chakula ya jamaa. Ile
itamusaidiya kuwa na afia na malisho bora • Chakula moja yenye inapatikana mu miviringo mingi iko na vifaa vingi vya afia. Kama ukitumiya ile chakula, si lazima
uongeze tena ma chakula yenye kuwa mu miviringo in-gine • Mufano Figo ya nyama iko tajiri kwa Vitamine A na kiungo
kya kuongeza damu (fer). Samaki iko tajiri kwa viungo vya
kujenga (proteins), vitamine A na viungo vya kuongeza damu. Mboka ya majani ya rangi ya maji ya sombe iko tajiri kwa vitamine A na viungo vya kuongeza damu. Hembe iko
tajiri kwa vitamine A na viungo vyenye kurahisisha utumivu
wa viungo vya kuongeza damu mu mwili
? KUNA CHAKULA AMBAYO AINA VIUNGO VYA MAFAA YOYOTE NA AM-BAYO AISTAHILI KUWAPA WATOTO?
• Watoto hawana lazima ya vinywaji vya sukari sawa vile chai, kahawa, soda.
• Vinywaji vile havina vifaa vya kujenga na havipashwe kupewa kwa watoto.
41
Nutrient Rich Foods for Children Ages 12 to 23 Months (Picture 5.3)
42
Nutrient-Rich Meal Recipe (5.4)
• Nyama nyekundu, maharagi na sombe viko tajiri kwa viungo
vya kuongeza damu. Chakula hii ina-saidiya watoto kujikinga na ukosefu wa damu na inawapa watoto damu yenye nguvu
• Chungwa, ndimu, papayi, na tomate viko tajiri kwa viungo
vyenye kurahisisha mwili utumiye fer (Vitamine C). Hii
chakula ina saidiya mwili kutumiya fer muzuri • Mafuta ya ngazi, ndimu, papayi na sombe viko tajiri kwa vitamine A. Chakula hii ina saidiya mtoto kujikinga na
magonjwa mbalimbali piya na kuepuka kuwa kipofu
• Nyama, samaki, maharagi viko tajiri kwa vifaa vya kujenga mwili. Vina saidiya watoto ku komala haraka na kurudisha
haraka afia kisha magonjwa. • Chunvi yenye iode inasaidiya kukinga magonjwa ya limengu. • Mafuta ya ngazi inasaidiya kuleta nguvu kwa mtoto.
• Maziwa ya mama inabaki njia ya kwanza kwa malisho bora
ya mtoto
• Kama mama anakula chakula nzuri na kuongezewa fer itamusaidiya kuwa na nguvu wakati wa ku-nyonyesha pia
itasaidiya maziwa kuwa na vifaa vya lazima kwa afia ya
mtoto.
• Mama akikula chakula yenye kuwa na vifaa vyote vya afia, atakuwa na afia nzuri wakati eko ana nyonyesha
KAZI : KUONESHA GINSI YA KUPITA
CHAKULA YENYEWE INAPATIKANA VIFAA
VYOTE VYA AFIA
Mazoezi
Chunguza Onya Uliza Angaliya
43
Nutrient Rich Recipe (Picture 5.4)
44
Lesson 6: Growth Monitoring
Four Children of the Same Age (Picture 6.1)
Katika picha hii tunahadisi hii: Mangaribi moja watoto wa mugini walikuwa wakicheza pamoja, jirani moja akaona kama
kabla wale watoto walikuwa na miaka sawa, lakini ki-mo yao
ilikuwa inaachana. Furaha alikuwa murefu na munene, watoto wengine waliku-wa wagonde lakini Mateso anaonekana kuwa
na afia njema lakini eko na kimo mufupi saana kuliko furaha.
Jirani akasema na mwenzake ; angaliya ginsi mungu alifanya.
Bato-to betu batakuwa bafupi na bembamba kila siku mpaka tu Furaha ndjo atakuwa murefu na wa nguvu
• Mtoto wa mama muzuri ni mrefu na anaonekana kuwa na
kilo mingi na afia njema kuliko wale watoto wawili wa ile ngambo ya mwisho
• Mtoto wa tatu na wa ine wana konda sana.
• Mateso ni mfupi na anaonekana kuwa na afia nzuri
? MUNAWAZA KAMA WATOTO WANATAFAUTI YA
UREFU NAYA KILO? MUNAWAZA KAMA NI MUNGU
ALIFANYA VILE ?
? MUNAWAZA KAMA BABA MUBAYA ANAWEZA
KUFANYA TAFAUTI NDANI YA MAISHA NA AFIA YA
MTOTO WAKE ?
45
Four Children of the Same Age (Picture 6.1)
46
Growth Monitoring Activities (Picture 6.2)
• Wazazi wanapashwa kupeleka watoto wao wa chini ya miaka
tano ku kipimo ili wapate kujua nam-na gani afia ya watoto ikonaendeleya
• Kwa watoto wa chini ya miaka mbili, tuwapeleke ku kipimo
kila mwezi
• Kwa watoto wa miaka mbili hadi tano, tuwapeleke ku kipimo
kisha kila miezi tatu • Kisha kupima kilo na urefu wa mtoto, mganga atamueleza
mzazi kama mtoto eko anakuwa muzuri
• Mganga anamupatiya mama muzuri mashauri kuhusu nini
anapashwa kufanya na mama Muzuri anamuuliza mganga vitu gani anahitaji kufanya
• Malisho ya mtoto mu miaka tano tangu kuzaliwa kwake
itasababisha kuguwa kwake na afia yake mu maisha yake yote
• Mungu anaumba watu wa urefu na mufano mbalimbali lakini watoto wote wanapashwa kurefuka na kuongezeka kilo mu
miaka tano tangu kuzaliwa. Kama watoto hawarefuki na kuongezeka kilo mu ile wakati, nilusema kuko kitu kimoja
kyenyewe hakiendeki
• Wazazi wanahitaji kusaidiya watoto wakati wanagonjwa na kufanya ginsi yote ya kuwasaidiya
Mungu aliwapa wazazi mamalaka ya kuweza kufanya kitu
kuhusu kutengeneza maisha ya watoto wao
47
Growth Monitoring Activities (Picture 6.2)
48
Growth Charts (Picture 6.3)
• Kuguwa kwa mtoto kunapimiwa na mganga kupitiya mustari
wa njia yake ya afia • Kwa kila kipimo, mganga anatiya nukta kwa ile fasi. kisha myezi mingi mganga anachanja kistari kienye kuunganisha
vile vipimo vya myezi yote kwa kuonesha ginsi mtoto eko
anaguwa • Kuna njia moja yenye kuonesha namna gani mtoto anahitaji kuguwa na ile njia inaanza tangu mwanzo wa kadi mpaka
mwisho
• Mustari wa njia ya kila mtoto unapashwa kubakiya ndani ya njia ya rangi ya maji ya sombe na kupanda kila mwezi
• Kama mustari uko unapanda, ile ina onesha kama mtoto eko na guwa vizuri
• Kama mustari haupandi kisha zidi ya mwezi moja ao kama unashuka, inaonesha kama mtoto haguwi mzu-ri na mama
yake anahitaji kukamata hatuwa haraka saana • Katika ma kadi ya afia ya watoto wenye kuwa chini (Mateso
na mwenzake), mistari ya njia ya afia yabo ni yenye kuwa mu ma rangi ya manjano ao ya mwekunda na ni ya kushuka.
Ile inaonesha ma jamaa yao ka-ma hawaguwi muzuri
• Kama mtoto haguwi muzuri, mganga atakupatiya mashauri ginsi mtoto aguwe muzuri
? WAKATI MTOTO WAKO ANAGONJWA AMA ANA MAGONJWA YENYEWE HAUJUWI GIN-SI YA KUITUNZA UTAFANYA NINI?
• Omba mashauri kwa waganga, wao wanaweza kukupa
madawa ama mashauri kwa kuweza kuboresha afia ya mtoto wako
• Waganga wataweza kukueleza chakula bora kwa afia ya
mtoto wako • Kama mtoto ni mgonjwa saana, inafaa kumupeleka ku
nyumba ya matunzo ya mganga kule atapata mati-babu mazuri
49
Growth Charts (Picture 6.3)
50
More Activities (Picture 6.4) ─ 5 minutes
• Kwenye kipimo kuna ma huduma ingine yenyewe waganga
wataweza kuwafanyia • Kama inahitajika kumupa mtoto kinga, waganga watamupa
kinga
• Kama inahitajika kumupa mtoto dawa ya kuuwa mitchango, waganga watamupa
• Kama mama ni mudja muzito ao kama eko ananyonyesha, waganga watamupa madawa yenye kufahi
• Waganga watamueleza kila mama namna mtoto wake eko anaguwa na kumupa mashauri ginsi ya kuboresha kuguwa
kwa mtoto wake
• Mganga atamweleza mama namna ya kukinga mtoto wake kwa magonjwa na namna ya kumutunza wakati wa shida fulani
51
More Activities (Picture 6.4)
52
Our Responsibility (Picture 6.5)
• Kwa watoto wa chini ya miaka mbili, tuwapeleke ku kipimo kila mwezi
• Kwa watoto wa miaka mbili hadi tano, tuwapeleke ku kipimo kisha kila miezi tatu
• Mama (ao mama) wanasaidiya kukamata kichwa ya mtoto
wakati mganga anamupima urefu, anamu-hakikisha mtoto usalama wake, anasaidiya kukamata mtoto wakati mganga anamupatiya kinga
• Ni wakati wenu wakuuuliza mganga kuusu afia ya watoto
wenu • Ni muzuri kuuliza na kusikiliza madjibu yenye munapewa • Kwa kwenda wakati wote na mtoto ku kipimo, wazazi
watadjuwa vizuri ginsi watoto wao weko naguwa
kulinganisha na wengine watoto • Kama mtoto anaanza uzaifu, mganga atamueleza mama namna ya kufanya
KAZI : KUONESHA GINSI YA KUSAIDIYA
MGANGA WAKATI ANAPIMA KILO NA UREFU WA WATOTO
Mazoezi
Chunguza Onya Uliza Angaliya
53
Our Responsibility (Picture 6.5)