Kumtangaza Kristo Kwa Mataifa: Jumbe 100 Kuhusu Utume · 2018. 8. 28. · Warumi Rum 1 Wakorintho...

242

Transcript of Kumtangaza Kristo Kwa Mataifa: Jumbe 100 Kuhusu Utume · 2018. 8. 28. · Warumi Rum 1 Wakorintho...

  • 1

  • 2

    Kumtangaza Kristo Kwa Mataifa: Jumbe 100 Kuhusu Utume

    Unaowezeshwa Na Roho Mtakatifu. © 2018 (Swahili), Machapisho Ya AIA.

    Haki Zote Zimehifadhiwa. Hakuna sehemu yoyote ya hiki kitabu inayoweza

    kunakiliwa, kuhifadhiwa katika mfumo wa aina yoyote wa kusoma, au hata

    kutumwa kwa namna yoyote – kielektroniki, kwa mitambo, kwa kudurufu,

    kurekodiwa, au vinginevyo vyote – bila ya kupata ruhusa ya maandishi kabla

    ya kufanya hivyo kutoka kwa mwenye haki miliki. Lakini nukuu fupi

    zitakazotumiwa kwa ajili ya marejeo ya majarida au magazeti zinaruhusiwa.

    Maandiko yote yanayotumiwa katika kitabu hiki, yanatoka katika Biblia ya

    Kiswahili: UNION VERSION, © Chama Cha Biblia Tanzania Na Kenya,

    2004. Haki Zote Zimehifadhiwa.

    Kuna Maandiko yatakayofafanuliwa ili kueleweka vizuri. Mtafsiri atafanya

    hivyo itakapobidi, na Maandiko hayo yatajulikana kwa alama hii: TLR, yaani

    TAFSIRI YA LUGHA RAHISI.

    Maelezo ya Chapisho katika Library of Congress Cataloging-in-Publication

    Data

    Miller, Denzil R., 1946–

    Kumtangaza Kristo Kwa Mataifa: Jumbe 100 Kuhusu Utume Unaowezeshwa

    Na Roho / Denzil R. Miller

    1. Bibilia. 2. Theolojia Ya Vitendo: Stadi Za Kutunga Hotuba. 4. Umisheni 5.

    KiPentekoste. 6. Roho Mtakatifu.

    Kimefasiriwa Tanzania na Mchgj Simon Joel Vomo

    © 2018 AIA Publications, Springfield, MO, USA

    Printed in

    Chapisho La Miaka Kumi Ya Pentekoste

    Wavuti: www.DecadeofPentecost.org

    www.ActsinAfrica.org

    http://www.decadeofpentecost.org/http://www.actsinafrica.org/

  • 3

    Vitabu vya Biblia ~ Ufupisho Utumiwao Kitabuni Humu ~

    Agano La Kale

    Mwanzo Mwa

    Kutoka Kut

    Walawi Law

    Hesabu Hes

    KumbuKumbu Kumb

    Yoshua Yosh

    Waamuzi Amu

    Ruthu Rut

    1 Samweli 1Sam

    2 Samweli 2Sam

    1 Wafalme 1Fal

    2 Wafalme 2Fal

    1 Nyakati 1Nya

    2 Nyakati 2Nya

    Ezra Ezr

    Nehemia Neh

    Esta Est

    Ayubu Ayu

    Zaburi Zab

    Mithali Mit

    Mhubiri Mhu

    Wimbo Ulio Bora Wim

    Isaya Isa

    Yeremia Yer

    Maombolezo Ombo

    Ezekieli Eze

    Danieli Dan

    Hosea Hos

    Yoeli Yoe

    Amosi Amo

    Obadia Oba

    Yona Yon

    Mika Mik

    Nahumu Nah

    Habakuki Hab

    Sefania Sef

    Hagai Hag

    Zekaria Zek

    Malaki Mal

    Agano Jipya

    Mathayo Mt

    Marko Mk

    Luka Lk

    Yohana Yn

    Matendo Mdo

    Warumi Rum

    1 Wakorintho 1Kor

    2 Wakorintho 2Kor

    Wagalatia Gal

    Waefeso Efe

    Wafilipi Flp

    Wakolosai Kol

    1Wathesalonike 1The

    2Wathesalonike 2The

    1 Timotheo 1Tim

    2 Timotheo 2Tim

    Tito Tit

    Filemoni Flm

    Waebrania Ebr

    Yakobo Yak

    1 Petro 1Pet

    2 Petro 2Pet

    1 Yohana 1Yoh

    2 Yohana 2Yoh

    3 Yohana 3Yoh

    Yuda Yda

    Ufunuo Ufu

  • 4

  • 5

    Yaliyomo

    Vitabu vya Biblia ...................................................................................... 3

    Yaliyomo................................................................................................... 5

    Orodha Ya Walioandika Mahubiri ............................................................ 9 Utangulizi ................................................................................................ 15

    SEHEMU YA 1: KUITANGAZA INJILI.

    1 Kumtangaza Kristo Kwa Mataifa ...................................................... 22 2 Machozi Ya Mavuno ......................................................................... 24

    3 Mtangaze Kristo Kwa Viumbe Vyote ............................................... 26

    4 Tangaza Kwa Mataifa ....................................................................... 28

    5 Ihubiri Injili ....................................................................................... 30

    6 Yesu: Wa Kuigwa Katika Kuvuna Roho .......................................... 32

    7 Mambo Manne Ya Lazima Kwa Ajili Ya Mavuno ........................... 34

    8 Injili Hii Itahubiriwa ......................................................................... 36

    9 Sisi Hatutaacha Kutangaza ................................................................ 38

    10 Kuitangaza Kikamilifu Injili Ya Kristo ........................................... 40

    11 Tumaini Moja Kwa Ajili Ya Dunia ................................................ 42

    SEHEMU YA 2: AGIZO KUU

    12 Amri Ya Kwanza Ya Agizo Kuu: “Ombeni!” .................................... 46

    13 Amri Ya Pili Ya Agizo Kuu: “Nendeni!” ....................................... 48

    14 Amri Ya Tatu Ya Agizo Kuu: “Hubirini!”...................................... 50

    15 Amri Ya Nne Ya Agizo Kuu: “Shuhudieni!” ..................................... 52

    16 Agizo Kuu Haliishi ........................................................................ 54

    17 Kupata Mahali Pako Katika Agizo Kuu ............................................. 56

    18 Kuli Ishi Agizo Kuu ........................................................................ 58

    19 Nendeni Na Kufanya Wanafunzi .................................................... 60

    20 Kulitimiza Agizo Kuu ..................................................................... 62

    21 Usiondoke Nyumbani Bila Huyo! ................................................... 64

    22 Kulielewa Agizo Kuu ...................................................................... 66

    23 Kulitii Agizo Kuu............................................................................ 68

    24 Maneno Makuu Manne Kwa Ajili Ya Mavuno .............................. 70 25 “Watu Wa Agizo Kuu” ................................................................... 72

    26 Mitazamo Kuhusu Agizo Kuu ........................................................ 74

  • 6

    SEHEMU YA 3: ARI KWA AJILI YA WALIOPOTEA

    27 Kusimamiwa Na Msalaba ...............................................................78

    28 Utume Wa Mungu—Utume Wetu ..................................................80

    29 Hivi Sasa Ni Saa Ngapi? .................................................................82 30 Kununua Mashamba Wakati Ambapo Inaonekana Haileti Maana .84

    31 Kuhamasishwa Kwa Ajili Ya Utume ..............................................86

    32 Mawe Matatu Ya Msingi Kwa Ajili Ya Umisheni ..........................88 33 Ni Wakati Wa Mavuno: Hebu Tujihusishe .....................................90

    34 Mavuno Yameiva, Tayari Kuvunwa ...............................................92

    35 Shauku Ya Mungu Kwa Ajili Ya Mataifa .......................................94

    36 Kuchochea Shauku Yetu Kwa Ajili Ya Waliopotea .......................96

    37 Kushirikiana Na Mungu Katika Utume Wake ....................................98

    38 Yule Mwanamke “Asiye Wa Maana” ........................................... 100

    39 Mungu Mwenye Kutafuta ............................................................. 102

    40 Mapigo Ya Moyo Wa Mungu Kwa Ajili Ya Watu Waliopotea .... 104

    41 Umisheni, Moyo Wa Mungu ......................................................... 106

    42 Kweli Kuu Nne Kuhusu Mavuno .................................................. 108

    43 Kujitoa Kwa Ajili Ya Dunia .......................................................... 110

    44 Hazina Za Ufalme ......................................................................... 112

    45 Kipaumbele Cha Mavuno.............................................................. 114

    SEHEMU YA 4: ROHO MTAKATIFU NA UMISHENI

    46 Swali La Pentekoste ...................................................................... 118

    47 Umisheni Unao-ongozwa Na Roho Mtakatifu .................................. 120

    48 Mapenzi Ya Mungu Kwa Ajili Yako ............................................ 122 49 Kuwezeshwa Kuzungumza ........................................................... 124

    50 Ishara Za Kimisheni Za Pentekoste ............................................... 126

    51 Kumtegemea Roho Katika Umisheni ............................................ 128

    52 Mtakuwa Mashahidi Wangu ......................................................... 130

    53 Roho Asema, “Nendeni!” .............................................................. 132

    54 Moto Uendelee Kuwaka ................................................................ 134

    55 Kusukumwa Na Roho Kuitangaza Injili ....................................... 136 56 Nguvu Yako Ili Kushuhudia ......................................................... 138

    SEHEMU YA 5: WITO WA MUNGU

    57 Miguu Inayopendeza ..................................................................... 142 58 Yesu Anaita ................................................................................... 144

    59 Wito Mkuu Wa Kristo ................................................................... 146

  • 7

    60 Mwokozi Anayetuma .................................................................... 148 61 Tumebarikiwa Ili Kutii .................................................................. 150

    62 Waliotumwa Na Kristo ................................................................. 152

    63 Mungu Anayeita ............................................................................ 154 64 Kuchaguliwa Kwa Ajili Ya Utume Wake ..................................... 156

    65 Imani Zenye Kina Sana Kuhusu Umisheni ................................... 158

    66 Mungu Anaita! Je, Unasikiliza? .................................................... 160

    67 Wito Wa Mungu............................................................................ 162 68 Kuitwa Kufanya Kazi Kwa Ajili Ya Ufalme .................................. 164

    SEHEMU YA 6: KUINGIA KUTENDA KWA AJILI YA UMISHENI

    69 Kufuata Mfano Wake Yesu ........................................................... 168

    70 Vitu Vitano Muhimu Kwa Umisheni ............................................ 170

    71 Shughuli Tatu Za Umisheni Za KiMkakati ................................... 172

    72 “Dunia Ya Tusipo” ........................................................................ 174

    73 Nguvu Ya Mmoja.......................................................................... 176

    74 Changamoto Mbili Kubwa Za Kimishenari .................................. 178

    75 Mpango Wa Mungu Wa Umishenari ............................................ 180

    76 Zaburi Ya Kimsihenari Kwa Kila Mtu .......................................... 182

    77 Injili Kuenea Bila Kuzuiwa ........................................................... 184

    78 Karima Kuu Ya Mungu Kwa Afrika ............................................. 186

    79 Kipimo Cha Kanisa La Kimisheni ................................................ 188

    80 Kauli Mbiu Ya Umisheni .............................................................. 190

    81 Hatua Tisa Kuelekea Eneo La Umisheni ...................................... 192

    82 Kuvuna Mataifa: Nini Kinachohitajika ......................................... 194

    83 Wakati Wa Kupanda Na Kuvuna .................................................. 196 84 Utume Wa Kutuma Wa Kanisa ..................................................... 198

    85 Watawezaje Kusikia? .................................................................... 200

    86 Kwa Njia Yoyote Iwezekanayo .................................................... 202 87 Kanuni Nne Za Mavuno ................................................................ 204

    88 Sabini Na Mbili Pamoja Na Wewe ............................................... 206

    89 Kuwa Mkristo Wa Dunia Nzima ................................................... 208 90 Hadithi Kuu Iliyowahi Kusimuliwa .............................................. 210

    91 Roho Mtakatifu: Mwongozaji Katika Umisheni ........................... 212

    92 Kila Mahali! .................................................................................. 214

    93 Gharama Ya Umisheni .................................................................. 216 94 Masomo Ya Umisheni Toka Kwa Eliya ....................................... 218

  • 8

    SEHEMU YA 7: MAOMBI NA VITA YA KIROHO

    95 Kuhamasishwa Kwa Ajili Ya Umisheni ....................................... 222

    96 Maombi Na Utume Wa Mungu ..................................................... 224

    97 Kumshinda Adui ........................................................................... 226 98 Tuwasaidie Kwa Maombi Yetu ..................................................... 228

    99 Maombi Yenye Kufungua ............................................................. 230

    100 Maombi Na Kazi Ya Umisheni ................................................... 232

    Orodha Ya Maandiko Yaliyotumiwa .................................................... 235

    Vitabu Vingine Vya Miaka Kumi Ya Pentekoste ................................. 239

  • 9

    Orodha Ya Walioandika Mahubiri

    AC Al Crane Mchungaji wa Assemblies of

    God, Crowley, Texas. USA

    (Mahubiri Namba 71)

    BD Brett Deal Mishenari wa Assemblies of God

    huko Senegal (Mahubiri Namba

    58, 72)

    BVW Barbara VanWyke Mishenari wa Assemblies of God

    huko Botswana (Mahubiri Namba

    90)

    CGS Christopher Gornold-Smith Mishenari wa Assemblies of God

    katika taasisi ya International

    Media Ministries (Mahubiri

    Namba 20)

    CK Claver Kabandana Rais wa Pentecostal Assem-blies

    of God huko Rwanda (Mahubiri

    Namba 6)

    DB Darlene Banda Mkuu wa Chuo, Assemblies of

    God Bible College huko Lusaka,

    Zambia (Mahubiri Namba 70)

    DC Don Corbin Mkurugenzi Wa Wamishenari

    Afrika Nzima (1985-2002)

    (Mahubiri Namba 30, 31, 95)

    DG Dean Galyen Mishenari wa Assemblies of God,

    Afrika (Mahubiri Namba 34)

    DM Daniel Mbiwan Mwangalizi Mkuu wa Full Gospel

    Mission huko Cameroon

    (Mahubiri Namba 77)

    DMc Daniel McGaffee Mchungaji wa Chi Alpha Chuoni,

    Chuo Kikuu Cha Jimbo Chico,

    Chico, California, Marekani

    (Mahubiri Namba 96)

    DRM Denzil R. Miller Mkurugenzi Wa Acts in Africa

    Initiative, Springfield, Missouri, Marekani (Mahubiri Namba 1, 7,

    8, 9, 10, 21, 24, 25, 26, 35, 36, 50,

    52, 53, 65, 66, 78, 79, 80, 81, 82,

    83, 84, 94, 97)

  • 10

    EC Edward Chitsonga Rais wa Malawi Assemblies of

    God (Mahubiri Namba 3)

    EG Edwin Gbelly Rais wa Liberia Assemblies of

    God (Mahubiri Namba 37, 64)

    EKA Emmanuel Kwasi Amoafo Kasisi Mwambata wa Kanisa

    Anglikana Kenya Mtaa wa Christ

    Church, Nairobi, Kenya

    (Mahubiri Namba 16)

    EML Enson Mbilikile Lwesya Mwanatimu wa AIA; Mwenyekiti

    wa Tume Ya Umisheni wa Dunia

    Ya AAGA Na Mchungaji

    Kiongozi wa Kanisa la

    International Christian Assembly,

    Lilongwe, Malawi (Mahubiri

    Namba 49)

    EYA Emil Yaovi Adote Rais wa Benin Assemblies of God

    (Mahubiri Namba 69)

    GB Greg Beggs Mkurugenzi wa Wamishenari

    Afrika Nzima (Mahubiri Namba

    2, 27, 57)

    GC Gaylan Claunch Makamu Askofu Na Mkurugenzi

    Wa Umisheni, Jimbo la North

    Texas la Assemblies of God

    Marekani (Mahubiri Namba 40,

    42)

    GM Greg Mundis Mkurugenzi Mkuu Wa Umisheni

    Wa Assemblies of God Duniani,

    Springfield, Jimbo la Missouri,

    Marekani (Mahubiri Namba 51)

    JB Jason Branson Mchungaji wa Kanisa la First

    Assembly of God, LaGrange,

    Jimbo la Georgia, Marekani

    (Mahubiri Namba 29)

    JDE Jimmy D. Easter Mtumishi Wa Assemblies of God

    (Mahubiri Namba 59, 73)

    JF Jerry Falley Mkurugenzi wa taasisi ya Link-

    Up Africa, Springfield, Missouri,

    Marekani (Mahubiri Namba 5, 61,

    62)

  • 11

    JL Jimmy Lemons Mratibu wa Nchi

    Zinazozungumza Kifaransa katika

    Chuo cha Pan Africa Theological

    Seminary huko Togo (Mahubiri

    Namba 76)

    JLE John L. Easter Mkurugenzi wa taasisi ya Africa’s

    Hope, Springfield, Missouri,

    Marekani (Mahubiri Namba 32,

    74)

    JM Jim Mazurek Mishenari wa Assemblies of God

    huko Chile (Mahubiri Namba 63)

    JN Jeff Nelson Mishenari Mkazi katika Evangel

    University, Springfield, Missouri,

    Marekani (Mahubiri Namba 54)

    JO Jerry Orf Mchungaji wa Kanisa la First

    Assembly of God, Mansfield,

    Missouri, Marekani (85, 98)

    JS Jerry Spain Mkurugenzi wa Wamishenari

    Eneo la Afrika Mashariki (1992-

    2000) (Mahubiri Namba 44, 45)

    JTG Joegbéan Tokpah Rais wa Guinea Assemblies

    Gbanamou God (Mahubiri Namba 48)

    LB Lipenga Banda Katibu Mkuu wa Zambia

    Assemblies of God (Mahubiri

    Namba 46)

    LC Lazarus Chakwera Rais wa Malawi Congress Party;

    Rais wa Malawi Assemblies of

    God (1989-2013) (Mahubiri

    Namba 47)

    LE Lavonna Ennis Mishenari wa Assemblies of God,

    The Gambia (Mahubiri Namba

    93)

    LT Loren Triplett Mkurugenzi wa Umisheni,

    Assemblies of God Duniani

    (1989-1997) (Mahubiri Namba

    43, 67)

  • 12

    MO Michel Ouedraogo Rais wa Burkina Faso Assemblies

    of God (Mahubiri Namba 86)

    MRT Mark R. Turney Mkurugenzi Mwenza, Acts in

    Africa Initiative; Katibu Mkuu

    Wa Muungano wa Assemblies of

    God Afrika (Mahubiri Namba 11,

    26, 55, 68, 88)

    NB Nate Beggs Mishenari wa Assemblies of God

    Afrika (Mahubiri Namba 17)

    PFM Paul Frimpong-Manso Askofu Mkuu wa Ghana

    Assemblies of God (Mahubiri

    Namba 19, 33, 91)

    PW Peter Watt Askofu Mkuu wa Assemblies of

    God Afrika Kusini (Mahubiri

    Namba 99, 100)

    PY Paul York Mkufunzi Wa Umisheni Katika

    Tamaduni Tofauti, Chi Alpha,

    Marekani (Mahubiri Namba 56)

    RSK Reuben S. Kachala Kiongozi wa Kituo cha

    Uhamasishaji, huduma ya Frontier

    Missions International, Lilongwe,

    Malawi (Mahubiri Namba 23, 89)

    SC Sarah Cariens Mishenari wa Assemblies of God,

    Afrika Kusini (Mahubiri Namba

    18)

    SE Scott Ennis Mishenari wa Assemblies of God

    nchini The Gambia (Mahubiri

    Namba 4, 60, 92)

    SH Scott Hanson Kiongozi Mkakati wa Assemblies

    of God Afrika Kwa Ajili Ya

    Kuwafikia Watu Ambao

    Hawajafikiwa, (Mahubiri Namba

    22, 75)

    SP Steve Pennington Mkurugenzi wa Wamishenari wa

    Assemblies of God katika Afrika

    Mashariki (Mahubiri Namba 38,

    39, 87)

  • 13

    UA Uche Ama Mwana Timu wa AIA na

    Mkurugenzi wa Umisheni wa

    Nchi za Nje wa Assemblies of

    God Nigeria (Mahubiri Namba

    12, 13, 14, 15)

    WS Waly Sarr Rais wa Senegal Assemblies of

    God (Mahubiri Namba 41)

  • 14

  • 15

    Utangulizi

    Kanisa la Assemblies of God katika Afrika linajizatiti na kuhamasisha

    kuhusu umisheni. Katika kipindi chao cha Miaka Kumi ya Mavuno, kuanzia

    mwaka wa 2010 hadi 2020, makanisa hamsini ya kitaifa ambayo yanaunda

    Muungano wa Assemblies of God Afrika (AAGA) yamejizatiti kutuma

    wamishenari wengi katika maeneo mengi ambayo hayajafikiwa, na yenye

    watu wengi ambao hawajafikiwa katika nchi zao wenyewe na katika nchi

    jirani. Katika juhudi hizo, makanisa ya kitaifa na ya mahali pamoja hujikuta

    katika ngazi au hatua mbalimbali za maendeleo. Mengine yamekwisha

    simika na kujenga idara zenye nguvu za umisheni na wanatuma hata

    wamishenari kwenda shambani. Mengine ndiyo kwanza yameanzisha

    utaratibu huo. Kwa hali yoyote ile, wote wamejizatiti kufanya sehemu yao

    katika kutuma ujumbe wa Kristo kwa watu wasiofikiwa na maeneo ambayo

    hayajafikiwa, katika Afrika na hata kwingineko.

    Mungu ameibariki sana Assemblies of God ya Afrika. Kanisa hili kwa

    sasa linatoa taarifa kwamba kuna washirika milioni 22 yenye kukutania

    katika makanisa 8,100 katika bara zima. 1 Lakini, Yesu alifundisha kwamba

    Baraka za namna hiyo huambatana na wajibu au majukumu mengi. Alisema

    hivi: “Yeye aliyepewa vingi, vingi vitahitajika kutoka kwake” (Luka 12:38,

    TLR). Hakika, hayo yanalihusu kanisa la Assemblies of God Afrika. Moja

    ya majukumu makubwa (na changamoto) ni kuhamasisha na kuwatuma

    jeshi kubwa la wamishenari kwenda shambani – halafu, kuwategemeza kwa

    maombi na fedha. Hebu fikiri kitu gani kingetokea kama ari au shauku ya

    kuyafikia mataifa kwa ajili ya Kristo ingepandwa katika mioyo ya hao

    washirika wote milioni 22 wa Assemblies of God Afrika.

    Ili jambo hili litokee, kuna mambo mawili ambayo lazima yatokee.

    Kwanza, Assemblies of God ya Afrika lazima iendelee kukutana na kupokea

    umwagiko wa Roho Mtakatifu. Tunamshukuru Mungu kwamba anaendelea

    kumwaga Roho Wake juu ya kanisa la Afrika. Lakini, huu uamsho wa

    KiPentekoste lazima upanuke na kushika kasi. Wakati Yesu alipokuwa

    analihamasisha kanisa Lake pale Yerusalemu, aliwaagiza waende duniani

    kote na kuhubiri habari njema kwa kila mtu. Ila, aliwaagiza wakae

    Yerusalemu kwanza mpaka wawe wamevikwa nguvu au uweza wa Roho

    (Luka 24:49). Mwisho, muda mfupi kabla hajapaa mbinguni, aliwaacha kwa

    kutoa ahadi ya mwisho, hivi:

    1 Kwa mujibu wa takwimu za 2015.

  • 16

    “Lakini mtapokea nguvu, Roho Mtakatifu akiisha kuwajia, nanyi mtakuwa

    mashahidi wangu…mpaka miisho ya dunia” (Matendo 1:8, TLR). Ili

    kutimiza hatima yao ya umishenari, Assemblies of God Afrika lazima

    iongeze maombi yake kwa Bwana wa Mavuno. Ni lazima waombe hivi: “Ee

    Bwana! Kwa neema yako, mimina juu yetu Roho wako, na ututie nguvu

    kutimiza Utume Wako hapa duniani.”

    Kingine ambacho lazima kitokee katika Assemblies of God ya Afrika

    ni kwamba wachungaji lazima waanze kuhubiri mara kwa mara na kwa

    ufanisi sana juu ya umisheni. Hapo ndipo shauku kwa ajili ya mataifa

    ambayo hayajafikiwa itakapopandwa ndani ya mioyo ya watu wa Mungu.

    Lakini, kwa bahati mbaya sana kanisa la Assemblies of God Afrika

    halina kawaida ya karne nyingi ya kuhubiri juu ya umisheni, tofauti na

    Kanisa la Magharibi. Utamaduni huu wa Kanisa la Magharibi ulianza

    zamani – siku za William Carey, mwishoni mwa karne ya kumi na nane.

    Wakati kanisa la Afrika limekuwa likifukuzia kwa mafanikio sana swala la

    uinjilisti na kupanda makanisa, katika mipaka yao kitaifa, kihistoria ni

    kwamba hawajawahi kutafuta kujihamasisha kwa ajili ya umisheni wa

    kuifikia dunia. Matokeo yake ni kwamba hawajaendeleza desturi ya muda

    mrefu ya kuhubiri juu ya umisheni.

    Hiki kitabu kimetayarishwa kushughulikia swala hilo. Kimeandaliwa

    kama kitabu rejea kwa ajili ya wachungaji wa Kiafrika wanaotaka

    kuhamasisha makanisa yao kwa ajili ya umisheni. Wachungaji na viongozi

    wa kanisa wanaweza kutumia mahubiri haya kuwaamsha na kuwafundisha

    watu wao kanuni za umisheni, na hata utendaji wake. Kitabu hiki kinafuata

    kitabu cha kwanza cha mihutasari ya jumbe kilichochapishwa na Acts in

    Africa Initiative (AIA) mwaka wa 2011. Kitabu cha kwanza kiliitwa,

    Kuitangaza Pentekoste: Jumbe 100 Kuhusu Nguvu ya Roho Mtakatifu.2

    Mafanikio makubwa ya kitabu kile cha kwanza yamekuwa mazuri sana.

    Kufikia sasa, kimetafsiriwa kutoka lugha ya Kiingereza hadi lugha zingine

    sita za Kiafrika, ikiwa ni pamoja na Kifaransa, Kireno, Kiswahili, KiMoor

    na KiAmharik. Kimegawanywa kwa zaidi ya wachungaji elfu 35,000 katika

    nchi 31 za Afrika. Kinatumiwa katika nchi za Marekani Kati na Kusini, na

    hata Ufilipino. Ofisi za AIA zimepokea shuhuda nyingi jinsi kitabu hivyo

    kinavyotumiwa, na jinsi maelfu ya Wakristo Waafrika wanabatizwa kwa

    Roho Mtakatifu kama matokeo ya kitabu hicho. Mchungaji mmoja

    2 Hivi vitabu viwili na vingine vingi vinaweza kupakuliwa bure katika mfumo

    wa barua pepe kwenye tovuti hii: www.DecadeofPentecost.org. Vinaweza

    kununuliwa kama vitabu kupitia blogu yangu binafsi, hii ifuatayo:

    www.DenzilRMiller.com.

    http://www.decadeofpentecost.org/http://www.denzilrmiller.com/

  • 17

    Mwafrika alisema, kwa furaha sanad, “Kitabu hiki cha Kuitangaza Pentekoste kimeleta uamsho kwa kanisa letu la nchi.” Tunaomba kitabu hiki

    nacho kiwe na mguso na mafanikio kama hayo.

    Wachangiaji

    Mihutasari hii 100 katika hiki kitabu imechangiwa na kutolewa na

    wahubiri arobaini na tano wa KiPentekoste. Wahubiri hao ni pamoja na

    wamishenari wa Kiafrika na viongozi wa umisheni, wamishenari wa

    KiMarekani, na wachungaji wanaohusika na mambo ya umisheni. Mimi

    binafsi nimechangia moja ya nne ya mihutasari hiyo. Utaweza kumtambua

    kila mchangiaji kwa herufi mbili za jina lake zitakazokuwa mwisho wa kila

    muhtasari. Halafu ulinganishe hizo herufi mbili kwa orodha inayotolewa

    katika ukurasa wa 9 hadi 12 inayoitwa “Orodha ya Wachangiaji”. Vile vile,

    baada ya jina la kila mchangiaji na maelezo yake, utakuta katika mabano

    orodha ya mahubiri aliyochangia.

    Ninataka kutoa shukrani zangu za dhati kwa kila mmoja katika hao

    waliochangia kwa kuturuhusu kutumia mihutasari yao bila gharama yoyote.

    Jinsi Ya Kutumia Hiki Kitabu

    Niruhusu nikushauri jinsi unavyoweza kutumia hiki kitabu. Mchakato

    huanza kwa kuchagua ujumbe. Kwa mfano: Kama unataka kuhubiri kutoka

    andiko Fulani, unaanza msako wako kwa kuangalia “Orodha Ya Maandiko

    Yaliyotumika” iliyoko mwishoni mwa kitabu hiki. Msako huo utakuongoza

    ufikie mahubiri yoyote ambayo yamekwisha andaliwa kutegemeana na

    ujumbe ulioandaliwa kutokana na andiko lako ulilochagua.

    Pengine unataka kuhubiri ujumbe wa umisheni, lakini huna uhakika wa

    kile unachotaka kuhubiri. Kama ni hivyo, unaweza kuchambua katika kitabu

    uone ujumbe unaofaa. Pengien uanzie kwenye “Orodha Ya Yaliyomo”

    mwanzoni mwa kitabu. Kwa kufanya hivyo, utaona kwamba kitabu

    kimegawanywa katika sehemu kuu saba, ambazo ni pamoja na hizi

    zifuatazo:

    Kuitangaza Injili

    Agizo Kuu

    Ari Na Shauku Kwa Waliopotea

    Roho Mtakatifu Na Umisheni

    Wito Wa Mungu

    Kuhamasisha Kwa Ajili Ya Umisheni

    Maombi Na Vita Ya Kiroho

  • 18

    Kipengele kimoja katika hivi kinaweza kukuvutia. Hapo utaanza kutafuta

    ujumbe katika sehemu hiyo husika katika kitabu, na kwa njia hiyo

    kurahisisha msako au utafutaji wako.

    “Mahubiri Katika Sentensi Moja” ni sehemu inayoweza kukusaidia pia.

    Kwa kusoma hiyo sentensi moja ambayo ni kama majumuisho ya ujumbe,

    inakuwa rahisi kwako kupata wazo upesi kama ungependa kutafiti zaidi au

    hapana. Kama mada inakuvutia, basi unaweza kutazama muhtasari husika

    kwa ukaribu zaidi.

    Pengine ungetaka kufikia lengo Fulani katika mahubiri yako. Kwa

    mfano: Unataka kuwahamasisha wasikilizaji wako kuombea umisheni, au

    unataka wao wamfungulie Mungu mioyo yao ili wasikie sauti Yake

    anapowaita kwa umisheni. Kama ndivyo, itakubidi upitie ile sehemu

    inayoitwa “Kusudi La Mahubiri” ambayo ndiyo huanza kila muhtasari. Kwa

    namna hiyo, unaweza kuchagua ujumbe ambao utakusaidia kufikia lengo

    lako.

    Zidi kuona kwamba kila muhtasari kwenye kitabu hiki umeandaliwa

    kutosha kwenye kurasa mbili Kwa kufanya hivyo nimejaribu kuweka

    maudhui ya kutosha kwenye kila muhtasari ili kumpa mtumiaji mwelekeo

    ulio dhahiri juu ya kilichomo na jinsi ujumbe unavyotiririka. Hapo hapo,

    nimejaribu kufanya mambo kwa kifupi kiasi cha kuwapa wahubiri na

    waalimu nafasi ya kutosha kukuza na kutengeneza jumbe hizo kulingana na

    mahitaji pekee ya wasikilizaji wao. Unapojiandaa na kuombea ujumbe

    husika, na kuhubiri muhtasari wowote katika hizi, ninaamini kwamba Roho

    Mtakatifu atakuvuvia kwa mawazo mapya ya jinsi ya kuandaa na kupanua

    jumbe zako mwenyewe za umisheni.

    Zipo njia nyingi mbalimbali za wewe kutumia ule muhtasari

    utakaokuwa umechagua. Njia ya kwanza na iliyo dhahiri ni kuhubiri ujumbe

    huo kama ulivyoandikwa. Lakini ni kitu halisi kwamba kutataka

    kutengeneza ujumbe wako uendane na mazingira yako binafsi ambayo yana

    upekee wake, na kulenga mahitaji mahsusi ya wasikilizaji wako. Pia,

    utapenda kuongeza vitu vyako vya zaidi ulivyopata vya kuongezea kwenye

    ujumbe husika. Pamoja na hayo, unapo-omba na kutafakari mahubiri hayo,

    Roho Mtakatifu atazungumza na wewe. Kwa hakika utahitaji kuingiza hayo

    mambo uliyopata na kuyaongeza kwenye ujumbe wako. Na ni hakika

    kwamba utataka kuongezea mifano yako na hata vichekesho kidogo kwenye

    huo ujumbe. Kwa maneno mengine ni kwamba, ninakutia moyo ufanye

    mahubiri hayo kuwa ya kwako.

  • 19

    Jinsi Ya Kuhubiri Ujumbe Mkuu Wa Umisheni

    Namalizia kwa mawaidha machache juu ya jinsi unavyoweza kuchukua

    hii mihutasari ya mahubiri ili uweze kuhubiri jumbe kuu za kimisheni.

    Jazwa na Roho Mtakatifu. Kwanza: Ili uweze kuhubiri ujumbe wa

    umisheni wenye ufanisi – au ujumbe wowote ule – ni lazima uwe umejaa

    Roho Mtakatifu. Mara nyingi sana katika Kitabu cha Matendo ya Mitume,

    mitume walianza mahubiri yao kwa kujazwaa na Roho Mtakatifu (Matendo

    2:4 na 14; 4:8; 4:31). Hakuna mbadala wa mahubiri yanayotolewa kwa

    nguvu za kujazwa na Roho. Hakuna kiwango chochote cha haiba binafsi ya

    mtu au mbinu za maonyesho kinachoweza kuchukua mahali pa kukosekana

    kwa Roho juu ya mhubiri. Acha Yesu awe mfano wako. Yeye alipoanza

    huduma, alitamka hivi: “Roho wa Bwana yuko juu yangu, kwa sababu

    amenitia mafuta ili kuhubiri habari njema…” (Luka 4:18).

    Mahubiri yawe ya kwako. Kama ilivyopendekezwa hapo nyuma, ufanye ujumbe husika uwe wa kwako. Yaani kwa maneno mengine, ukisha chagua

    muhtasari wa ujumbe utakaohubiri, anza “kuuingiza” ndani yako. Ingiza

    ujumbe huo ndani ya moyo wako na akili zako kwa kutafakari na hali ya

    maombi, ukiusoma mara kadhaa. Katika akili zako, jihubirie ujumbe huo

    mara kadhaa. Unapofanya hivyo, itikia ujumbe wenyewe. Jali unasema nini.

    Kama unahitaji kusimama kidogo na kuomba, basi fanya hivyo. Kama

    unahitaji kutubu, fanya hivyo pia.

    Vile vile, ni muhimu sana kukariri andiko la ujumbe husika pamoja na

    maandiko mengine muhimu yatakayotumika katika ujumbe. Hiyo itasaidia

    pia kuweka ujumbe huo katika moyo wako. Hiyo pia itakusaidia wakati wa

    mahubiri. Kwa kuwa mistari ya Maandiko iko moyoni mwako na katika

    akili yako, mahubiri yako yatatiririka kwa ubora na kwa urahisi sana.

    Wasikilizaji wako watasikia jinsi unavyoguswa na kile unachokisema, na

    jinsi unavyojua na kutawala mada yako, na wataitikia vizuri zaidi yale

    unayosema. Itakuwa msaada sana kwako kukariri yale mambo makuu ya

    mahubiri yako. Kwa kufanya hivyo, utawekwa huru kutoka kuangalia kitini

    ulichoandika, na utaweza kusema na watu wako moja kwa moja na kwa

    ushawishi mkubwa.

    Toa ujumbe wako. Unapohubiri ujumbe wako wa umisheni, zingatia

    mambo mawili. Kwanza, usiwe na maneno mengi. Maana yake ni kwamba

    usijaze ujumbe wako kwa maneno mengi yasiyo ya lazima, au hata mawazo

    yasiyofaa. Bakia kwenye mada yako. Kumbuka lengo lako, na usiseme

    chochote ambacho hakitakusaidia kufikia lengo hilo. Pili, unapohubiri, lenga madhabahu. Yaani, kila utakachosema lazima kiwe kimeandaliwa

    kuwafanya watu kujitoa, au kufanya maamuzi. Kisha, unapohitimisha

    ujumbe wako, “tupa nyavu”. Kama mvuvi anavyotupa wavu wake ndani ya

    maji na kuvuta samaki walionaswa kuingia kwenye mtumbwi wake, wewe

  • 20

    pia unapaswa “kutupa nyavu” kwa kuwaalika watu wafike madhabahuni.

    Waie wajiweke tayari kwa ajili ya utume wa Mungu na wawezeshwe na

    Roho ili kufanikisha jambo hilo.

    Kwa mawazo hayo, ninakupa kitabu hiki. Ni maombi yangu ya dhati

    kabisa kwamba utakitumia mara kwa mara kama kifaa kwa ajili ya

    kuhamasisha kanisa la Kristo kuwafikia mataifa kwa ngvu za Roho

    Mtakatifu.

    Ningependa kusikia kutoka kwako jinsi mihutasari hii ilivyokuwaidia.

    Tafadhali tuma shuhuda na mahitaji ya kuombewa kwa anwani hii ya barua

    pepe: [email protected].

    Ni mimi,

    Dkt. Denzil R. Miller

    Mhariri

  • 21

  • 22

    1 Kumtangaza Kristo Kwa Mataifa

    Ujumbe Wenyewe Katika Sentensi Moja: Ni lazima tuyatangazie

    mataifa habari za Kristo katika nguvu za Roho Mtakatifu.

    Kusudi La Ujumbe: Watu wajazwe na Roho na kujitolea na kujikabidhi

    kumtangaza Kristo kwa mataifa.

    Maandiko Ya Ujumbe: Marko 16:15-18

    Utangulizi 1. Kama watu ambao ni wamishenari wa Mungu, wote tumeitwa

    kumtangaza Kristo kwa mataifa.

    2. Agizo Kuu la Marko linaweka jambo hilo wazi zaidi: “Enendeni

    duniani kote mkahubiri habari njema kwa uumbaji wote.”

    3. Ujumbe huu utazungumzia mambo manne muhimu kuhusu wajibu

    wetu wa kumtangaza Kristo kwa mataifa: Utume wetu, Mbinu

    yetu, Namna tunayofanya hivyo, na Itikio linalotakiwa kutoka

    kwetu.

    I. UTUME WETU—DUNIA NZIMA A. Yesu alisema, “Nendeni duniani kote…” (Mk 16:15).

    1. Wakati mwingine alisema, “Hii injili ya ufalme itahubiriwa

    duniani kote [oikoumeme, dunia yenye watu], kuwa kama ushuhuda kwa mataifa yote [ethne, kundi la watu]; ndipo mwisho

    utakuja” (Mt 24:14).

    B. “Duniani kote” ni pamoja na…

    1. Kila mahali: “Mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu,

    na Uyahudi wote…mpaka mwisho wa dunia” (Mdo 1:8).

    2. Kila mtu: “mkahubiri…kwa kila kiumbe” (ms.15).

    3. Kila watu: “Enendeni basi, na kufanya wanafunzi katika

    mataifa yote (Kiyunani: ethne au makundi ya watu, makabila)” (Mt 28:19).

    B. Kitakachohitajika: Wengine watakwenda; wengine watatuma.

    (Soma Rum 10:13-15a).

    1. Kristo anawaita wengine waende.

    a. Waondoke nyumbani na kuacha familia na kwenda nchi

    za mbali na katika tamaduni ambazo hawajazizoea, na

    kutangaza habari njema.

    2. Yeye anatuita sisi wengine wote tuhusike kutuma.

    a. Kutoa fedha ili kuwategemeza wale wanaokwenda.

    b. Kuwaombea wamishenari, na waliopotea. 3. Hakuna asiyehusika.

    II. UJUMBE WETU—HABARI NJEMA

    A. Yesu alisema, “Nendeni duniani kote mkaihubiri injili…”

  • 23

    1. Habari njema (Injili) ni ujumbe wa kufa kwa Yesu msalabani, na

    kufufuka Kwake toka kwa wafu kwa utukufu mwingi.

    2. Inahusisha wito kwa watu kutubu dhambi zao na kumwamini

    Kristo peke Yake ili waokoke (Mk 1:15; Mdo 20:21).

    B. Kutenda kwetu (au kutokutenda) kuna matokeo ya milele.

    1. Yesu alisema, “Kila atakayeamini na kubatizwa ataokoka, lakini

    kila asiyeamini atahukumiwa” (ms. 16).

    2. Vile vile kuna matokeo ya kutokwenda na kutotangaza au

    kuhubiri:

    a. Soma na kujadili: Ezekieli 3:17-19

    C. Tusiruhusu jumbe za hali ya chini kutuelekeza pembeni.

    1. Onyo la Paulo kwa Timotheo (2Ti 4:3-5).

    2. Ujumbe wa Kristo tu ndiyo utakaoleta uzima wa milele

    (Yn 17:3).

    III. MBINU YETU—NGUVU YA ROHO MTAKATIFU A. Yesu aliahidi hivi: “Na hizi ishara zitawafuata…” (ms.17-18)

    1. Haya yote ni kazi ya Roho Mtakatifu (Mdo 4:30-33).

    2. Katika Matendo: “Kisha wanafunzi walitoka na kwenda

    kuhubiri kila mahali, na Bwana alifanya kazi pamoja nao na

    kulithibitisha neno lake kwa ishara zilizofuatana nalo” (Mdo

    16:20).

    3. Huduma yenye kuwezeshwa na Roho na kutiwa nguvu,

    inaonekana katika kitabu cha Matendo.

    B. Yesu ameahidi nguvu hiyo hiyo kupatikana kwetu sisi siku za leo.

    1. Ahadi Yake ya mwisho: (Mdo 1:8) “Mtapokea nguvu…”

    2. Amri Yake ya mwisho: (Mdo 1:4-5) “Msiondoke

    Yerusalemu, bali ingojeeni ile zawadi ambayo Baba yangu

    aliahidi…”

    IV. ITIKIO LETU LINALOTAKIWA—UTII A. Andiko letu linasema, “Ndipo wanafunzi walitoka na kuhubiri kila

    mahali…”

    1. Yaani, walitii amri ya Bwana Yesu.

    B. Mungu anataka itikio hilo hilo kutoka kwetu siku ya leo.

    1. Yesu alisema: “Mkinipenda, mtatii ninayoagiza” (Yn 14:15).

    2. Ni lazima tutii kwa kwenda, kutoa, na kuomba.

    Kumalizia, Na Wito Kwa Watu Kuja Mbele

    1. Njoo sasa ujitolee kwa ajili ya utume wa Kristo.

    2. Njoo utiwe nguvu na Roho Mtakatifu.

    [ DRM ]

  • 24

    2 Machozi Ya Mavuno

    Ujumbe Wenyewe Katika Sentensi Moja: Hata katika nyakati ngumu, ni

    lazima tupande mbegu ya Injili, tukimwamini Mungu kwa mavuno.

    Kusudi La Ujumbe: Kuwatia watu moyo wahubiri Injili hata katikati ya

    majaribu makubwa, na ugumu.

    Maandiko Ya Ujumbe: Zaburi 126:4-6

    Utangulizi 1. Katika hii “Zaburi Ya Kupanda,” wale waliokuwa utumwani

    walirudi Sayuni—wanachokuta ni magofu tu.

    a. Wakati wanapofurahia uhuru wao, hapo hapo wanalia

    wanapokumbuka utukufu wa kwanza wa mji huo.

    b. Wanapojenga upya mji wao ulioharibika, na kupanda mbegu

    zao za thamani katika mashamba yao makavu, wanalia.

    c. Lakini kwa imani wanamtazama Mungu kwa ajili ya mavuno

    yaliyoahidiwa.

    2. Leo tunalia kwa ajili ya Afrika.

    a. Katika Afrika, Shetani anao mateka wegi sana.

    b. Afrika kwa namna nyingi, ni magofu, kama Sayuni ilivyokuwa.

    1) Inasumbuliwa na vita, njaa na ukame, magonjwa, na ufisadi.

    c. Lakini, wakati tunapoililia Afrika, ni lazima tupande mbegu pia.

    3. Katika andiko letu, tunajifunza masomo muhimu sana kuhusu

    kupanda na kuvuna, kama ifuatavyo:

    I. SHAUKU YA KITUME: KUTAMANI KUPANDA

    Soma ms. wa 6 “Yeye aendaye kupanda akilia machozi…” A. Wakati wa ukame, mara nyingi tunajaribiwa tusifanye chochote.

    1. Kwa sababu ya maumivu, tunajaribiwa kuweka mbegu. B.

    Hata hivyo, shauku ya kitume inatuhamasisha kwenda

    shambani kupanda, kwa gharama yoyote.

    1. Ukame na njaa havipaswi kumzuia mkulima kupanda mbegu.

    2. Wakulima wa KiAfrika wanaelewa maana uya kupanda kwa

    machozi. Katika nyakati za ukame, wanajaribiwa kula hata

    mbegu iliyohifadhiwa kwa majira yajayo. Wanalia, lakini

    bado wanapanda mbegu shambani, wakiamini kwamba

    Mungu atawapa mavuno.

    C. Shauku ya kitume hutusukuma sisi kupanda hata katika nyakati ngumu.

    1. Tunasukumwa na Imani katika Bwana wa Mavuno (Mt 9:38),

    na mavuno ya roho za watu yaliyoahidiwa (Gal. 6:9), na kwa nguvu za Roho Mtakatifu (Mdo 11:12).

    2. Mara nyingi, machozi ndiyo bei itolewayo na Ufalme kwa

    ajili ya maendeleo.

  • 25

    II. RASILMALI ZA KITUME: MPANDAJI NA MBEGU ms. 6: “…akiwa amebeba mbegu za kupanda…”

    A. Injili ni kama mbegu nzuri (Lk 11:8; 1Pet 1:23).

    1. Kamwe usiwe na mashaka juu ya nguvu yake ya -

    kuwakomboa watu (Rum 1:16).

    2. Ni habari njema kwa ajili ya watu wote, haidhuru ni wagumu

    kiasi gani, wamepotea kiasi gani, au wanaonekana kuwa

    mbali kiasi gani kutoka kwenye neema ya Mungu.

    B Injili inaendelea kubadilisha maisha ya watu mamilioni kwa

    mamilioni.

    1. Imebadilisha jamii ambazo hapo kwanza zilikuwa zinajificha

    kwa hofu ya mizimu yao ya kiasili na kuzifanya kuishi maisha

    ya ushindi.

    2. Imebadilisha makundi ya watu ambao mwanzo walikuwa

    wanawanyanyasa, kuwauza na kuwaumiza wanawake wao,

    mpaka kuwa watu ambao sasa wanawasimika wanawake

    kuwa watumishi wa Injili.

    3. Imewabadilisha watu waliokuwa wamejaa choyo na ubinafsi

    kuwa watu wanaoweza kutoa kwa sehemu kubwa sana ili

    kutegemeza shughuli ya Kristo.

    C. Maisha yaliyobadilishwa ni mbegu nyingine nzuri (Mt 12:23; Lk

    8:15).

    1. Mungu huwasambaza watu Wake duniani kama mbegu.

    III. UHAKIKA WA KITUME: IMANI KATIKA MUNGU WA

    MAVUNO (ms.6 “…atarudi kwa nyimbo za furaha, akiwa amebeba

    miganda yake.”) A. Uhakika wetu uko katika Mungu wa mavuno.

    1. Tunajua atakuwa mwaminifu kwa ahadi katika Neno Lake.

    2. Anayo mamlaka na nguvu za kusababisha mavuno yatokee.

    3. Atatengeneza mazingira ya kawaida na ya kiroho kwa ajili ya

    mavuno.

    B. Tuna uhakika kwamba mfumo wa mavuno wa Mungu unafanya kazi.

    1. Tunaamini kwamba kupanda mbegu kuta leta mavuno.

    2. Mbegu zinapopandwa na mvua zinyeshe, hakuna

    kinachoweza kuzuia mbegu isichipuke na kuzaa.

    Kumalizia, Na Wito Kwa Watu Kuja Mbele: 1. Basi, tutafanya nini wakati tutakapoikuta Sayuni (yaaniAfrika) ikiwa

    magofu? Je, tutakimbia kwa sababu ya hofu? Hapana! Kwa machozi

    tutapanda mbegu na kumwamini Mungu kwa ajili ya mavuno.

    2. Njoo sasa, na ujitoe kwa ajili ya kupanda mbegu ya Injili.

    [ GB ]

  • 26

    3 Mtangaze Kristo Kwa Viumbe Vyote

    Ujumbe Wenyewe Katika Sentensi Moja: Ni lazima tumtangaze Kristo

    kwa viumbe vyote.

    Kusudi La Ujumbe: Watu wajitoena kuwa tayari kutii amri ya Kristo

    kuhubiri habari njema kwa viumbe vyote.

    Maandiko Ya Ujumbe: Marko 16:15-20

    Utangulizi 1. Katika maandiko yetu, Yesu anatoa Agizo Lake Kuu.

    2. Anatuamuru sisi kwenda “duniani kote na kuhubiri habari njema

    kwa viumbe vyote.”

    3. Katika andiko hili, tunajifunza kanuni tatu zenye nguvu sana juu

    ya wajibu wetu wa kumtangaza Kristo kwa viumbe vyote:

    I. KUMTANGAZA KRISTO KWA VIUMBE VYOTE NI AMRI

    YA BWANA A. Yesu ametuamuru sisi kwenda “duniani kote na kuihubiri habari

    njema kwa kila kiumbe” (Mk 16:15).

    B. Amri hii ilitoka chumba cha utawala wa mbinguni, yaani, kutoka

    mamlaka iliyo juu zaidi ya zote (Mt 28:18).

    C. Yesu ameamuru, hivyo sisi ni lazima tutii.

    1. Utii ni lazima (Yn 14:15, 31).

    2. Utii ni fursa kwa ajili ya wana na binti wote wa Mungu.

    II. KUMTANGAZA KRISTO KWA VIUMBE VYOTE NDIYO

    MSINGI KWA AJILI YA WATU KUAMINI NA KUOKOKA A. Yesu aliendelea na kusema hivi: “Yeyote atakayeamini na

    kubatizwa ataokoka, na yeyote asiyeamini atahukumiwa” (ms.16).

    1. Kazi yetu si kuhukumu, bali kuwaita watu wamwamini Kristo

    (Yn 3:16-17).

    B. Ni lazima tuambie viumbe vyote kwamba Yesu anaokoa.

    1. Yesu alitangaza Injili (Mk 1:15).

    2. Paulo alitangaza Injili (Mdo 16:31).

    3. Sisi pia ni lazima tuitangaze Injili.

    C. Kama wakiamini, wataokoka.

    1. “Yeyote aaminiye na kubatizwa, ataokoka” (ms.16).

    2. Je, umemwamini Kristo ili upate wokovu?

    a. Ikiwa bado, fanya hivyo sasa hivi!

    b. Yeye “ana nguvu za kuokoa” wote waliitao jina Lake (Is 63:1; Rum 10:13).

    III. KUMTANGAZA KRISTO KWA VIUMBE VYOTE NDILO

    KUSUDI LA ISHARA NA MAAJABU

  • 27

    A. Yesu alizidi kuahidi kwamba, “Na ishara hizi zitawafuata wale

    waaminio: Katika jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha

    mpya; watashika nyoka kwa mikono yao; na watakapokunywa

    sumu kali, haitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya

    wagonjwa, nao watapona” (Mk 16:17-18).

    B. Ni lazima twende katika nguvu za Roho Mtakatifu, tukimtazamia

    Mungu kuithibitisha Injili kwa ishara na maajabu.

    1. Yesu alihudumu katika nguvu ya Roho (Lk 4:18; Mdo 10:38).

    2. Kama tutakuwa waaminifu kuitangaza Injili, Mungu

    atathibitisha maneno yetu kwa ishara za kimuujiza, na

    maajabu.

    a. Alithibitisha mahubiri ya wanafunzi (Mk 16:20).

    b. Alithibitisha mahubiri ya Paulo (Rum 15:18-19).

    c. Atathibitisha mahubiri yetu.

    C. Lakini, tusisahau kamwe kwamba kusudi la ishara ni kuithibitisha

    Injili na kuwaelekeza watu kwa Kristo.

    1. Filipo huko Samaria (Mdo 8:5).

    2. Wakati Mungu anapotoa miujiza, hatupaswi kamwe kusahau

    kusudi la hiyo miujiza—kuwaelekeza watu kwa Kristo.

    Kumalizia, Na Wito Kwa Watu Kuja Mbele

    1. Njoo sasa, na ujitoe kwa ajili ya kumtangaza Kristo kwa viumbe

    vyote.

    2. Njoo utiwe nguvu na Roho Mtakatifu.

    [ EC ]

  • 28

    4 Tangaza Kwa Mataifa

    Ujumbe Wenyewe Katika Sentensi Moja: Ni lazima tuwatangazie

    mataifa kwamba Yesu Kristo ni Mwokozi na Mfalme.

    Kusudi La Ujumbe: Kuwaita watu wajitoe ili kutangaza ujumbe wa

    wokovu wa Mungu kwa mataifa.

    Maandiko Ya Ujumbe: Zaburi ya 96:1-13

    Utangulizi 1. Daudi aliandika hii Zaburi ya 96 wakati aliporudisha Sanduku La

    Agano katika mji wa Yerusalemu (Linganisha 1Ny 16:7, 23-33 na

    Zab 96:1-13).

    2. Ni wimbo wa kimishenari wenye kusherehekea jinsi Yahwe

    alivyo mfalme juu ya dunia yote.

    3. Katika hii Zaburi, Mungu anatuita sisi kutoa matangazo ya aina

    tatu kwa mataifa, kama ifuatavyo:

    I. TUNATAKIWA KUYATANGAZIA MATAIFA KWAMBA

    MUNGU NI MWOKOZI A. Daudi anaita dunia nzima imwabudu Yahwe (ms.1-2).

    1. Hii ni sawa kwa sababu mataifa yote kwa kweli ni mali ya

    Mungu.

    2. Kama itikio la ukuu Wake, mataifa yote na watu wote

    wanapaswa kumwimbia Mungu “wimbo mpya” (ms.1).

    3. Siku moja, hilo litafanyika na kutimia (Uf 5:9-10).

    B. Kama watu wa Mungu ambao ni wamishenari, kuabudu kwetu

    lazima kugeuke kuwa ushuhuda, kama ifuatavyo:

    1. Hatutakiwi tu kuabudu utukufu wa Mungu, bali tunatakiwa

    “kuutangaza utukufu wake katikati ya mataifa…” (Zab 96:3).

    2. Tunapaswa “kuzitangaza habari njema za wokovu Wake siku

    hata siku” (ms.2).

    C. Yesu ndiye ujumbe tunaotangaza kwa mataifa.

    1. Tunapaswa kutangaza kwamba Yesu ndiye Mwokozi wa

    binadamu wote.

    2. Yeye ndiye aliyetupa sisi wokovu na kuawshinda maadui wa

    roho zetu (Ef 1:19-23; Kol 2:13-15).

    3. Sawa na mitume, kamwe tusiache kutangaza kwamba Yesu

    ndiye Mwokozi (“Hatuwezi kuacha kusema!”—Mdo 4:20).

    II. TUNATAKIWA KUYATANGAZIA MATAIFA KWAMBA

    MUNGU NI MKUU

    A. Tunamtumikia Mungu aliye mkuu.

    1. Katika Zaburi ya 95 Daudi alizungumza juu ya ukuu wa

    Mungu (ms.4-6).

  • 29

    2. Yeye “asifiwe sana” (ms 4). (Tazama pia Kut 15:11.)

    3. Tunamtumikia Mwokozi aliye Mkuu:

    a. Yesu ni “Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana”

    (1Tim 6:15).

    b. Yeye ni Mwokozi wa dunia yote! (Yn 4:44; 1Yn 4:14).

    B. Ni lazima tutangaze ukuu Wake kwa mataifa.

    1. Daudi anatuambia nini tufanye: tumtangaze Yeye! (ms.3).

    2. Vile vile anatuambia kwa nini tufanye hivyo: Yeye ni mkuu!

    (ms.4).

    3. Yesu si “asifiwe sana” tu, bali pia anatakiwa atangazwwe

    sana – kwa njia kubwa (Mk.15:15-16).

    III. TUNATAKIWA KUYATANGAZIA MATAIFA KWAMBA

    MUNGU NI MTAKATIFU A. Daudi anayaita mataifa “kumwabudu Bwana katika uzuri wa

    utakatifu” (ms.9).

    1. Hii ni mara ya pili anatuita tuabudu.

    2. Hapa panafunua mapigo ya moyo wa kimishenari wa hii

    Zaburi―makundi yote ya watu siku moja yatamwabudu

    Mfalme (ms.10).

    B. Je, Bwana anataka “sadaka” gani kutoka kwetu?

    1. Anataka tumpe Yeye vyetu vyote (Mk 8:34-38).

    2. Ni lazima tuishi mbele Yake katika “uzuri wa utakatifu” (ms. 9).

    3. Yeye anakuja kwa ajili ya “kanisa tukufu, lisilo na doa wala

    kunyanzi wala chochote cha namna hiyo,” kanisa ambalo ni

    “takatifu, lisilo na mawaa” (Ef 5:27).

    C. Ni lazima tutangaze utakatifu Wake katikati ya mataifa.

    1. Ni lazima “tuseme katikati ya mataifa kwamba Bwana

    anatawala.”

    2. Kwa mara nyingine tena, kuabudu kunabadilika a kuwa

    ushuhudiaji (ms.10).

    a. “Jamaa za watu” sasa wanaitwa kumtangaza katikati ya

    mataifa (ms.7).

    b. Ukiri huu unatoa changamoto kwa miungu ile yote, na

    watawala wengine wote pamoja na mamlaka zote – kuna

    Mfalme mmoja tu.

    Kumalizia, Na Wito Kwa Watu Kuja Mbele 1. Kristo ametuagiza tujiunge Naye kutangaza utawala wa Mungu

    kwa mataifa (Mt 23:14; 28:19-20).

    2. Njoo! Jitoe mwenyewe kwenda, kutoa na kuomba ili mataifa

    yaweze kusikia juu ya wokovu wa Mungu ulio katika Yesu Kristo.

    [ SE ]

  • 30

    5 Ihubiri Injili

    Ujumbe Wenyewe Katika Sentensi Moja: Ni lazima tuihubiri Injili kwa

    uaminifu, katika nguvu za Roho Mtakatifu.

    Kusudi La Ujumbe: Ili waamini wajitoe wenyewe kuihubiri Injili na

    ishara zikifuatana nao.

    Maandiko Ya Ujumbe: Marko 16:15–20

    Utangulizi 1. tumesoma Agizo Kuu la Yesu katika Marko 16.

    2. Hapo, Yesu anatuambia sisi “kuhubiri habari njema,” yaani, ni lazima

    tutangaze ujumbe wa Kristo kwa mkazo na kwa ushawishi mkubwa.

    3. Kutokana na maandiko haya, tunaweza kujifunza masomo

    muhimu matatu, kama ifuatavyo:

    I. YESU AMETUAMURU TUHUBIRI A. Yesu ametuamuru sisi, “Nendeni…na kuhubiri.”

    1. Soma tena Marko 16:15

    2. Tunatakiwa kwenda kila mahali—na kwa kila mtu. 3. Tunatakiwa tupeleke na kutoa ujumbe wa Injili…

    a. …kwamba Yesu alilipa gharama ya dhambi zetu na sasa

    anatoa uzima wa milele kwa wote watakaomwamini Yeye.

    b. Ni lazima hao watubu na kuziamini hizo habari njema (Mk

    1:15).

    B. Ni lazima tuhubiri Injili kwa sababu hatima ya milele ya watu

    inahusika.

    1. Yesu alisema hivi: “Kila aaminiye na kubatizwa, ataokoka, lakini

    kila asiyeamini atahukumiwa” (ms.16).

    2. Hatupaswi kupuuza hii kazi ambayo ni ya maana sana.

    C. Basi, kila mwamini lazima aihubiri Injili.

    1. Je, utatii amri ya Kristo kuihubiri Injili?

    2. Lakini, Yesu hajatuamuru kuhubiri tu…

    II. YESU AMETUTUMA NA KUTUPA NGUVU

    A. Pamoja na amri ya Yesu kwamba tukahubiri, ipo ahadi ya nguvu.

    1. Hebu soma ms. 17-18: “Na ishara hizi zitafuata…”

    2. Ahadi hii ni kwa “yeyote aaminiye.”

    3. Yaani, ni pamoja na wachungaji, wamishenari, waalimu wa

    Shule ya Jumapili ya watoto na waalimu wa Uanafunzi na

    Maandiko, washirika wote na kila kijana anayeamini. B. Ikiwa tutakwenda na kuamini, Kristo atalithibitisha Neno kwa

    ishara zisizokuwa za kawaida.

    1. Lakini kumbuka, ni lazima twende “katika Jina Lake,”yaani,

    chini ya mamlaka Yake na kwa ajili ya utukufu Wake.

  • 31

    2. Hizo ishara za kimuujiza zitahusisha…

    a. Ukombozi wa kiungu (“watatoa pepo”)

    b. Usemaji wa kiungu (“watanena kwa lugha mpya”)

    c. Uponyaji wa kiungu (“watu wagonjwa…. watapona”)

    d. Ulinzi wa kiungu (“sumu ya nyoka…haitawadhuru”).

    C. Hii nguvu isiyo ya kawaida, ya kuhubiri Injili, huja wakati

    tumebatizwa na Roho Mtakatifu.

    1. Amri ya mwisho ya Yesu, na ahadi (Soma Mdo 1:4-5, 8)

    2. Wanafunzi waliipokea hiyo ahadi siku ile ya Pentekoste (2:4).

    3. Walianza kuhubiri Injili huku ishara zikifuatana nao.

    III. YESU ANATUTAZAMIA SISI KULIKUBALI NENO LA

    MUNGU

    A. Baada ya kupokea hiyo amri wanafunzi walikubali neno la Kristo

    na kutii amri Yake.

    1. Baada ya kutoa amri hiyo, Yesu alichukuliwa kwenda

    mbinguni.

    2. Mara ile ile wanafunzi wakatii. “Walitoka na kwenda kila

    mahali, wakihubiri kote kote” (ms.20).

    B. Mara wakagundua kwamba hawakuwa peke yao.

    1. “Bwana alifanya kazi pamoja nao, akithibitisha Neno Lake

    kwa ishara zilizoambatana nalo” (ms.20).

    2. Yesu kwa Roho Wake alikuwa hapo pembeni yao.

    3. Kwa sababu hiyo waliona matokeo ya kushangaza sana.

    C. Leo hii, Yesu anataka kufanya hivyo hivyo kupitia kwa kila

    mmoja wetu.

    1. Yesu aliweka hilo wazi katika Yohana 14:12, kwamba:

    “Yeyote anayeniamini mimi atafanya hayo ambayo nimekuwa

    nikifanya. Tena atafanya hata makubwa zaidi ya haya, kwa

    sababu mimi nakwenda kwa Baba.”

    2. Si makubwa kwa ubora, bali makubwa ki-idadi.

    D. Tunahitaji nini leo ili kufanya huduma kwa njia hii?

    1. Ni lazima tu-uamini ujumbe.

    2. Ni lazima tutiwe nguvu na Roho.

    3. Ni lazima twende katika Jina la Yesu. 4. Ni lazima tuhubiri habari njema kwa ujasiri.

    5. Ni lazima tumtazamie Mungu kulithibitisha Neno kwa ishara za kimuujiza zitakazofuata.

    Kumalizia, Na Wito Kwa Watu Kuja Mbele 1. Njoo sasa, ujitoe kwa ajili ya kuhubiri Injili.

    2. Njoo sasa, utiwe nguvu na Roho Mtakatifu.

    [ JF ]

  • 32

    6 Yesu: Wa Kuigwa Katika Kuvuna Roho

    Ujumbe Wenyewe Katika Sentensi Moja: Yesu ametupa sisi mfano wa

    uvunaji roho tunaoweza kuufuata.

    Kusudi La Ujumbe: Kuwatia moyo watu na kuwahamasisha wawe

    wanaovuna roho kama Yesu.

    Maandiko Ya Ujumbe: Yohana 4:4-42

    Utangulizi 1. Yesu alikuwa mvuna roho wa kwanza, na aliye mkuu sana.

    2. Katiki habari hii ya Mwanamke Kisimani, Yesu ametupa mfano

    tunaoweza kufuata.

    3. Ona mambo matatu jinsi Yesu alivyomvuta huyo mwanamke

    kwake Yeye Mwenyewe:

    I. ONA JINSI YESU ALIVYOMPA INJILI YULE MWANAMKE

    A. Yesu alianza kwa ombi rahisi kwa yule mwanamke.

    1. Alimwambia hivi: “Naomba unipe maji ninywe” (ms.7).

    2. Hii ilikuwa ndoano, kitu cha kuanzishia mazungumzo.

    3. Yule mwanamke alishangaa, kwa sababu Yesu alikuwa

    mwanamume Myahudi, huku yeye akiwa mwanamke

    Msamaria (ms.9).

    4. Ni lazima tuanzishe kwa makusudi mazungumzo na watu

    waliopotea.

    B. Yesu alimshirikisha yule mwanamke habari njema.

    1. Alimfunulia kwamba Yeye ndiye Masiya (ms.25-26).

    2. Alimpa maji yaliyo hai (ms.13-14).

    3. Kama Yesu, sisi nasi ni lazima tuwashirikishe Injili watu

    waliopotea.

    II. ONA JINSI MWANAMKE YULE ALIVYOMWITIKIA YESU A. Yule mwanamke Msamaria alikuwa na kiu, lakini si cha maji ya

    kawaida tu.

    1. Yesu alimwambia juu ya maji ya kiroho (ms.13-14).

    2. Mwanamke alimwomba Yesu ampe hayo maji yaliyo hai

    (ms.15).

    B. Mwanamke alikuwa tayari kukubali kwamba alikuwa anaishi maisha

    ya dhambi.

    1. Yesu alifunua mtindo wake wa maisha ya dhambi (ms.16-18).

    2. Mwanamke alikiri dhambi yake na kutubu (ms.17, 19). C. Yule mwanamke alitubu na kumwamini Yesu (ms.25-29).

    1. Alikiri dhambi yake.

    2. Aliweka Imani yake katika Kristo.

  • 33

    D. Yule mwanamke alipeleka ujumbe wa Yesu kwa wengine (ms.28-

    30).

    1. Wasamaria kutoka ule mji walimwamini Yesu kwa sababu ya

    ushuhuda wa yule mwanamke (ms.30).

    2. Sisi ni lazima tufanye kama yule mwanamke Msamaria.

    III. ONA JINSI YESU ALIVYOWAFUNDISHA WANAFUNZI

    WAKE

    A. Yesu aliwafundisha juu ya umuhimu wa kuzivuna roho.

    1. Kufanya mapenzi ya Baba na kuzivuna roho vilikuwa

    “chakula” Chake―yaani, kitu kilichompa Yeye kuishi

    (ms.31-34).

    2. Ndivyo inavyotakiwa kuwa hata kwetu siku za leo.

    3. Yesu ameagiza kwamba sisi twende na kufanya mataifa yote

    kuwa wanafunzi (Mt 28:18-20).

    4. Waliopotea hawawezi kuokoka kama hakuna atakayekwenda

    na kuwaambia kuhusu Yesu (Rum 10:13-15).

    B. Yesu aliwafundisha kuhusu uharaka katika kuzivuna roho.

    1. Mavuno ni sasa—sio miezi minne kutoka sasa (ms.35).

    2. Ni lazima tuvune roho sasa, kabla hatujachelewa milele (Yn

    9:4).

    C. Yesu aliwafundisha juu ya thawabu ya kuvuna roho.

    1. Anayevuna roho hupata “malipo ya milele” (ms.36).

    2. Apandaye na avunaye hufurahi kwa pamoja (ms.36-37).

    3. Na mbingu hufurahi pamoja nao (Lk 15:10).

    Kumalizia, Na Wito Kwa Watu Kuja Mbele: 1. Yesu ndiye mvuna roho tunayepaswa kumwiga. Ni lazima tufuate

    hatua Zake.

    2. Njoo sasa ujitoe kuwa mtu anayevuna roho.

    [ CK ]

  • 34

    7 Mambo Manne Ya Lazima Kwa

    Ajili Ya Mavuno

    Ujumbe Wenyewe Katika Sentensi Moja: Ikiwa tunataka kukamilisha

    uvunaji, ni lazima kwa ujasiri mkubwa tukubaliane na “Mambo

    Manne Ya Lazima Kwa Ajili Ya Mavuno”, ya Kristo.

    Kusudi La Ujumbe: Watu wapate kujitoa wenyewe kumtangaza Kristo

    kwa mataifa katika nguvu za Roho Mtakatifu.

    Maandiko Ya Ujumbe: Luka 24:33-49

    Utangulizi 1. Kuna vitu ambavyo ni lazima... na vingine ambavyo ni lazima

    kidogo ... na vitu vingine ni vya lazima kabisa!

    2. Yesu anazungumzia mambo manne ya lazima yanayohusiana na

    mavuno.

    3. Ona maneno katika mstari wa 46 "basi, ikawa lazima" 4. Neno la Kiyunani linalotafsiriwa “lazima” (edei) linamaanisha

    “ulazima ulio dhahiri” au “ulazima unaofunga” (kwa mujibu wa

    Kamusi ya Kiyunani ya Vine).

    5. Basi, Yesu anadhihirisha lazima nne, zenye kufunga wahusika,

    kuhusiana na mavuno—yaani vitu vine ambavyo ni lazima kwa

    ajili ya wokovu wa mwanadamu:

    I. ILIKUWA NI LAZIMA KABISA KWA YESU KUFA MSALABANI “Ilimpasa Kristo kuteswa…”

    (ms.46).

    A. Kanuni ya milele: “Pasipo damu kumwagika…hakuna ondoleo [la

    dhambi]” (Ebr 9:22).

    B. Pale msalabani, Kristo alilipa gharama kwa ajili ya watu wote.

    1. “Bwana ameweka juu yake maovu yetu wote” (Isa 53:6).

    C. Bila msalaba = Hakuna ukombozi = Hakuna mavuno.

    II. ILIKUWA NI LAZIMA KABISA KWA YESU KUFUFUKA

    KUTOKA KWA WAFU “Ilimpasa Kristo…afufuke toka kwa

    wafu…” (ms.46)

    A. Kristo alijenga huduma Yake yote kwenye tukio la ufufuo.

    1. Mfano: Wakati waliokuwa wanamshutumu walipomwuliza,

    “Tuonyeshe ishara”, Yeye aliwaambia juu ya kufufuka

    Kwake (Mt 9:38-40). 2. Alijenga yote aliyosema na kudai kwenye kufufuka Kwake.

    B. Angalia Paulo anavyosema kuhusu ufufuo wa Kristo:

    1. “Ikiwa Kristo hajafufuliwa…. Kuhubiri kwetu hakuna faida;

    Imani yetu ni bure; sisi ni mashahidi wa uongo; na bado tumo

    katika dhambi zetu” (1Kor 15:14-17).

  • 35

    2. Mtu ni lazima aamini kuhusu ufufuo ili aweze kuokoka

    (Rum 10:9-10).

    C. Pasipo ufufuo: Hakuna ukombozi, hakuna mavuno.

    III. NI LAZIMA KABISA INJILI IHUBIRIWE KWA MATAIFA

    YOTE. “Ilikuwa lazima…toba na ondoleo la dhambi vihubiriwe kwa Jina Lake kwa mataifa yote…” (ms.46-47).

    A. Matokeo ya zile lazima mbili za kwanza husimama au kuanguka

    kwenye lazima ya tatu.

    1. Ondoa yoyote moja, na mpango wa Mungu wa ukombozi

    unaharibika.

    2. Ilikuwa ni lazima kabisa kwa Yesu kuteseka, lakini hiyo

    haikutosha…Alipaswa afufuke toka kwa wafu. Lakini cha

    kushangaza, hata hiyo haitoshi…

    3. Ni lazima vile vile kwamba watu wasikie juu ya hayo na

    kuamini juu ya kifo Chake na kufufuka Kwake (Rum 10:9-

    10).

    4. Hebu soma na kueleza kidogo Warumi 10:13-14.

    B. Tumepata fursa ya kuwa na sehemu katika mpango wa Mungu wa

    ukombozi:

    1. Yeye tu ndiye angeweza kuteseka msalabani, na ni Mungu tu

    ndiye angeweza kumfufua toka kwa wafu; lakini, kazi ya

    kumtangaza kwa mataifa tumepewa sisi kanisa Lake.

    2. Kwa hiyo, Kristo ametupa sisi Agizo: Mk16:15-16.

    IV. NI LAZIMA KABISA KWA KANISA KUTIWA NGUVU NA

    KUWEZESHWA KWA ROHO MTAKATIFU KUIFANIKISHA ILE KAZI “…nanyi ni mashahidi…lakini kaeni humu mjini, hata

    mvikwe uwezo utokao juu” (ms.48-49). A. Ili kanisa liweze kufanikisha hii kazi ya kuhubiri Injili kwa

    mataifa, ni lazima kutiwa nguvu na Roho Mtakatifu.

    1. Hii ndiyo lazima ya nne kwa ajili ya mavuno.

    B. Kabla ya Yesu kupaa mbinguni, aliliachia kanisa kazi, amri na

    hadi (Mdo 1:4-8).

    1. Kazi: “Mtakuwa mashahidi wangu…” (ms.8b)

    2. Amri: “Mngojeni…Roho Mtakatifu” (ms.4-5)

    3. Ahadi: “Mtapokea nguvu…” (ms.8a)

    C. Ni lazima tutiwe nguvu na Roho.

    Kumalizia, Na Wito Kwa Watu Kuja Mbele 1. Ni lazima tukubali na kushika yale mambo manne ambayo ni

    “lazima kwa ajili ya mavuno.”

    2. Njoo sasa ili utiwe nguvu na Roho na ujitolee kwa

    upya kwa ajili ya mavuno. [ DRM ]

  • 36

    8 Injili Hii Itahubiriwa

    Ujumbe Wenyewe Katika Sentensi Moja: Kazi ya msingi ya kanisa ni

    kuhubiri Injili kwa mataifa yote kabla Yesu hajarudi mara ya pili.

    Kusudi La Ujumbe: Watu waweze kujitoa kwa ajili ya kupeleka Injili

    kwa mataifa yote.

    Maandiko Ya Ujumbe: Mathayo 24:3-14 (mkazo ni kwenye ms.14)

    Utangulizi

    1. Angalia kwa makini swali la wanafunzi kwa Yesu:

    a. “Nini itakuwa ishara [katika umoja] ya kuja kwako, na ya mwisho wa dunia?” (Mt 24:3).

    b. Yesu anaanza jibu Lake kwa kueleza sifa za mwenendo wa

    kipindi cha wakati huu.

    1) Vitu ambavyo kimsingi si ishara za wakati wa mwisho. 2) Stanley Horton, akitoa mchango wake kuhusu jibu la

    Yesu katika mstari wa 3, aliandika hivi, “Basi Yesu

    alichukua muda kuwaonya wanafunzi Wake kuhusu vikwazo

    ambavyo vingeweza kuwaondoa kwenye shughuli yao

    kubwa ya kueneza Injili.” (Katika kitabu chake kiitwacho

    The Promise of His Coming, uk.33) 2. Mwisho, katika mstari wa 14, Yesu anajibu swali lao kama

    ifuatavyo: “Injili hii ya ufalme itahubiriwa duniani kote…”

    a. George Eldon Ladd anasema juu ya mstari huu, kama

    ifuatavyo: “pengine ndiyo mstari mmoja wa muhimu sana

    katika Neno la Mungu.”

    b. Ndiyo kiini cha kuelewa historia.

    c. Katika Mt 24:14 Yesu anazungumzia dhana tatu muhimu sana

    kuhusu ufalme wa Mungu:

    I. UJUMBE WA UFALME

    A. Yesu anaanza ahadi hii hivi: “Hii Injili ya ufalme…”

    1. Ona maneno haya: “Hii Injili…” 2. Yaani, ni Injili ile ile ambayo ilihubiriwa na Yeye na mitume.

    3. Hakuna Injili nyingine. (Soma Gal. 1:6-9.)

    B. Hii Injili aliyosema Yesu ni ipi? 1. Hii Injili ya ufalme ni ujumbe kwamba Yesu alikuja kujenga

    ufalme wa Mungu duniani.

    2. Ni ujumbe wa kifo cha Yesu na kufufuka Kwake.

    a. Soma 1Kor 15:1-4; 1Kor 2:1-2: “Yesu Kristo…amesulubiwa” 3. Injili ya ufalme inahusisha onyesho la mamlaka ya ufalme na nguvu.

    a. Mt 12:28: "Kama mimi kwa Roho wa Mungu ninatoa ..."

    b. Lk 9:1-2 “Aliwapa nguvu…aliwatuma…”

    c. 1Kor 2:4: Kwa maneno na katika maonyesho.

  • 37

    4. Hii Injili ya ufalme inawaita watu “kutubu na kuamini habari njema” (Mk 1:5).

    C. Tunapaswa kuanzisha mfumo huu katika shughuli zetu zote za umisheni.

    II. UTUME WA UFALME

    A. Katika Mt 24:14 Yesu anaendelea kusema hivi: “…itahubiriwa

    duniani kote kuwa ushuhuda kwa mataifa yote…”

    1. Utume wa kanisa ni kushuhudia ulimwengu.

    2. Linganisha Mt 24:14 na Mt 28:18-20.

    B. Katika Mt 24:14, Yesu anadhihirisha upana wa utume: 1. Sisi tunatakiwa kwenda “duniani kote.” a. Neno “Dunia” kwa Kiyunani oikoumeme, maana yake ni

    dunia inayokaliwa na watu.

    b. Matendo 1:8 inataja “mwisho wa nchi.”

    2. Sisi tunatakiwa kuwa “mashahidi kwa mataifa yote.” a. “Mataifa” kwa Kiyunani ethne, yaani makabila, au

    makundi ya watu.

    C. Yesu anatuhakikishia mafanikio ya hakika. 1. "Hii Injili...ita hubiriwa. Itatokea! 2. Swali, basi, siyo “Je, itatimia?” bali ni “Je, sisi tutakuwa na

    sehemu katika hili?”

    3. Biblia inatupa picha kuhusu wakati ujao, yaani mpaka

    mbinguni, kama ifuatavyo:

    a. Hapo tunawaona watu kutoka “kila kabila na lugha na

    jamaa na taifa” (Ufu 5:9, pia ona Ufu 7:9).

    4. Sisi tunaweza kuwa na sehemu katika huu ukusanyaji mkuu wa

    mavuno makubwa sana ya roho za watu.

    III. KUKAMILIKA KWA UFALME

    A. Yesu anamalizia Mt 24:14 kwa kusema, “…ndipo mwisho

    utakapokuja.”

    1. Je, mwisho ni lini?

    2. Baada ya hii Injili ya ufalme kuhubiriwa duniani kote kuwa

    kama ushahidi kwa kila taifa.

    3. MANENO YA Stanley Horton, “Mungu atakuwa na watu

    waliokombolewa kwa damu ya Yesu ‘kutoka kila…taifa…’

    Mpaka atakapowapata, mwisho hautakuja. Basi, tunachohitaji,

    si kujali zaidi juu ya kitakachotokea, bali kujali juu ya

    kuenezwa kwa Injili.” (Katika kitabu kiitwacho Promise, uk.33) B. Tunaweza kusaidia kuharakisha “kasi” ya kurudi kwa Bwana kwa

    kuihubiri Injili katika dunia yote. (Soma 2Pet 3:12.)

    Kumalizia, Na Wito Kwa Watu Kuja Mbele

    Njoo sasa ujitoe mwenyewe kwa Kristo na utume Wake. [ DRM ]

  • 38

    9 Sisi Hatutaacha Kutangaza

    Ujumbe Wenyewe Katika Sentensi Moja: Ni lazima tuamue kutangaza

    kwa uaminifu ujumbe wa Kristo katika nguvu ya Roho Mtakatifu.

    Kusudi La Ujumbe: Kwamba, watu wajikabidhi na kujitoa wenyewe kwa

    Kristo na kutangaza Injili Yake.

    Maandiko Ya Ujumbe: Matendo 4:1-20 (angalia mstari wa 8 na 20)

    Utangulizi 1. Wakati mwingine wachungaji hujaribiwa kuhubiri jumbe

    zinazopendwa, lakini za hali ya chini, zisizo na uzito.

    a. Matokeo yake ni kwamba wanaacha ujumbe wa kweli wa Injili.

    b. Leo tunajifunza somo muhimu sana kutoka kwa Petro na

    Yohana.

    2. Simulia hadithi ya kukamatwa na ukiri wa akina Petro na Yohana

    katika Matendo sura ya 4. (Wakati walipoagizwa kuacha kuhubiri

    katika jina la Yesu, walijawa na Roho Mtakatifu na kujibu hivi:

    “Hatuwezi kuacha kusema juu ya Kristo!”)

    3. Tutafanya vizuri sana kujitoa kwa namna nne:

    I. Kujitoa Namba 1: “HATUTAACHA KUMTANGAZA KRISTO

    KWA WALIOPOTEA” A. Cha kusikitisha ni kwamba, makanisa mengi yanayojiita “ya

    KiPentekoste” yameachwa ujumbe wa Kristo kwa kuhubiri “Injili

    zingine” (angalia Gal 1:6-9).

    B. Lakini, wakati walipoamriwa kuacha kumhubiri Kristo, mitume

    walijibu hivi: “Hatuwezi kuacha kusema juu ya Kristo!”

    C. Kristo alikuwa ndiyo ujumbe mmoja wa kanisa katika kitabu cha

    Matendo.

    1. Filipo alikwenda Samaria na kumhubiri Kristo (Mdo 8:5).

    2. Paulo alimhubiri Kristo kwa askari jela wa Filipi (Mdo 16:30+).

    3. Petro: “Wala hakuna wokovu katika mwingine yeyote…”

    (Mdo 4:12).

    D. Kamwe tusiache kuhubiri ujumbe wa Kristo.

    II. Kujitoa Namba 2: “HATUTAACHA KUHUBIRI KATIKA

    NGUVU YA ROHO MTAKATIFU” A. Mitume na wahubiri katika kitabu cha Matendo walimtangaza

    Kristo katika nguvu ya Roho.

    1. Petro Siku ya Pentekoste (Mdo 2:4, 14, 22-24). 2. Petro tena (Mdo 4:8-12).

    B. Sisi pia ni lazima tumtangaze Kristo katika nguvu za Roho Mtakatifu.

    1. Amri ya Yesu ya mwisho ni hii: Mdo 1:4-5: “Msiondoke Yerusa-

    lemu, bali ingojeeni ile zawadi iliyoahidiwa na Baba yangu…”

  • 39

    2. Ahadi ya mwisho ya Yesu ni hii: Mdo 1:8: “Ninyi mtapokea

    nguvu…”

    3. Mwombe Roho aje juu yako na akujaze sasa hivi.

    III. Kujitoa Namba 3: “HATUTAACHA KUPANDA MAKANISA YA

    KIMISHENARI, YALIYOTIWA NGUVU NA ROHO

    MTAKATIFU” A. Katika kitabu cha Matendo, mitume walipanda makanisa ya

    kimishenari yaliyotiwa nguvu na Roho.

    1. Yaani, makanisa ambayo kwa haraka yangepanda makanisa

    mengine ya kimishenari, yaliyotiwa nguvu na Roho

    Mtakatifu.

    2. Kama kanisa la Antiokia (Mdo 11:19-21).

    3. Matokeo ya hilo ni kwamba makanisa yaliongezeka sana

    katika Dola ya Rumi.

    B. Sisi pia ni lazima tupande makanisa ya kimishenari yaliyotiwa

    nguvu na Roho Mtakatifu.

    1. Yaani, makanisa yaiyotiwa nguvu na Roho Mtakatifu…

    a. …na karibuni yatapanda makanisa mengine ya aina hiyo hiyo.

    b. …na yatajihusisha katika kutuma wamishenari.

    2 Makanisa aina hii hayatawezekana pasipo mpango wa

    makusudi, uliochambuliwa vizuri sana wa kuyapanda.

    IV. Kujitoa Namba 4: “SISI HATUTAACHA KUHAMASISHA

    MAKANISA YETU KWA AJILI YA UMISHENI”

    A. Mitume walipowahamasisha makanisa ya kimisheni

    yaliyowezeshwa na Roho Mtakatifu, walifanya hivyo kwa kusudi

    la kuieneza Injili “katika Yerusalemu, na Uyahudi yote, mpaka

    miisho ya dunia” (Mdo 1:8).

    1. Kila kanisa la mahali pamoja lazima lihamasishwe kushiriki

    katika kazi ya umisheni.

    2. Kila aaminiye ni lazima afundishwe juu ya wajibu wake

    binafsi wa kushiriki katika umisheni.

    B. Wote ni lazima tushiriki katika umisheni kwa njia tatu:

    1. Ni lazima wote twende kwa waliopotea na kuwashirikisha Injili. 2. Ni lazima wote tuombe kwa ajili ya mavuno nyumbani na

    nchi za ng’ambo.

    3. Ni lazima wote tutoe kwa ajili ya kazi ya umisheni.

    Kumalizia, Na Wito Kwa Watu Kuja Mbele 1. Njoo ujitoe mwenyewe kwa Kristo na kwenye kutangaza Injili

    Yake kwa waliopotea.

    2. Njoo utuwe nguvu na Roho ili uweze kuitangaza Injili.

    [ DRM ]

  • 40

    10 Kuitangaza Kikamilifu Injili Ya Kristo

    Ujumbe Wenyewe Katika Sentensi Moja: Tunawajibika “kuitangaza

    kikamilifu Injili ya Kristo” kwa wote.

    Kusudi La Ujumbe: Kwamba Wakristo waweze kujitoa wenywe kikami-

    lifu kabisa kuitangaza kikamilifu Injili nyumbani na duniani kote.

    Maandiko Ya Ujumbe: Warumi 15:15-21

    Utangulizi 1. Katika mstari wa 19 Paulo anatamka hivi: “Mimi nimeitangaza

    kikamilifu kabisa Injili ya Kristo.”

    2. Basi, nini maana ya “kutangaza kwa ukamilifu” Injili?

    3. Kutokana na mstari wetu, tunajifunza kwamba sisi tunakuwa

    tumeitangaza Injili kikamilifu wakati tu tunapokuwa tumefanya mambo matatu:

    Kwanza, tunakuwa tumeitangaza Injili kikamilifu…

    I. WAKATI TUMEKWISHA KUTANGAZA KWA UWAZI NA

    USAHIHI KABISA UJUMBE WA YESU KRISTO

    A. Sisi kama watu wa Mungu ambao ni wamishenari, wajibu wetu

    wa msingi ni kuutangaza ujumbe wa kufa kwa Kristo msalabani,

    na ufufuo Wake wa ushindi kutoka kaburini.

    1. Paulo alielewa huu wajibu mkubwa wa kipekee.

    a. Aliwaambia Warumi (ms.19): “Mimi nimehubiri

    kikamilifu kabisa…”

    b. Akaendelea hivi (ktk ms.20): “Siku zote imekuwa shauku

    yangu kuihubiri Injili…”

    2. Alifafanua Injili kuwa ni ujumbe wa Kristo kufa, kuzikwa, na

    kufufuka. (Soma 1Kor 15:1-4.)

    3. Ni “nguvu ya Mungu iletayo wokovu.” (Soma War 1:16-17.)

    B. Kutangaza kikamilifu Injili pia ni pamoja na kuwaita watu

    wapokee Imani na toba (Mk 1:15; Mdo 20:21).

    C. Kwa ujasiri kabisa, ni lazima tuitangaze “injili kamili”…

    1. Yesu anaokoa! Yesu anaponya! Yesu anabatiza watu kwa

    Roho Mtakatifu! Yesu anakuja tena!

    Halafu, tunakuwa tumeitangaza Injili kikamilifu…

    II. WAKATI TUNAPOKUWA TUMEONYESHA NGUVU YA

    INJILI KWA “ISHARA NA MIUJIZA KWA NJIA YA NGUVU

    ZA ROHO MTAKATIFU” A. Kuitangaza Injili kikamilifu ni zaidi ya kuzungumza tu: ni pamoja na

    kuonyesha nguvu za ufalme. (Soma 1Kor 4:20.)

    1. Paulo aliwaambia Warumi kwamba aliweza kuwavuta watu

    wa Mataifa “kwa nguvu za ishara na miujiza, kupitia nguvu za

    Roho” (ms.18-19).

  • 41

    2. Mahali pengine, aliwakumbusha Wathesalonike jinsi

    ambavyo Injili iliwafikia. (Soma 1The 1:5.)

    3. Aliendelea kuwakumbusha Wakorintho…(Soma 1Kor 2:4.)

    4. Sisi pia tutazamie Mungu kuthibitisha kutangazwa kwa Injili

    na “ishara zinazofuatana” (Mk 16:15-20).

    B. Mfano wa Agano Jipya unahusisha kutangazwa kwa Injili na

    maonyesho:

    1. Yesu alionyesha mfano (Mt 4:23).

    2. Filipo alifuata mfano wa Yesu (Mdo 8:5-7).

    3. Paulo alitumia mbinu hiyo hiyo huko Listra (Mdo 14:7-10).

    C. Kama na sisi tutafuata mfano huo wa Agano Jipya, inabidi tufanye

    mambo mawili:

    1. Ni lazima tutiwe nguvu kwa Roho Mtakatifu (Lk 24:49; Mdo 1:8).

    2. Ni lazima tufanye mambo kwa Imani jasiri, kama Paulo huko

    Listra (Mdo 14:9-10).

    Mwisho, tunakuwa tumeitangaza Injili kikamilifu tu…

    III. WAKATI TUMEPELEKA INJILI HADI MAHALI AMBAPO

    KRISTO HAJULIKANI

    A. Ona jinsi ambavyo Paulo anaunganisha “kutangaza Injili

    kikamilifu” na kuhubiriwa kwa Injili “mahali ambapo Kristo

    hajawahi kujulikana”:

    1. “Kwa hiyo, kutoka Yerusalemu mpaka maeneo yote

    kuzunguka Iliriko, nimeitangaza Injili ya Kristo kikamilifu.

    Imekuwa shauku yangu kila mara kuihubiri Injili mahali

    ambapo Kristo hakuwa anajulikana…” (ms.19-20).

    2. Halafu ananukuu maneno ya nabii Isaya : “Wale ambao

    hawakuambiwa juu yake wataona, na wale ambao

    hawajasikia, wataelewa” (ms.21; rejea Isa 52:15).

    B. Yesu anatutazamia kwenda “duniani kote na kuhubiri habari

    njema kwa viumbe vyote” (Mk 16:15).

    1. Sisi wote tunashiriki katika wajibu wa kumtangaza Kristo

    kwa mataifa.

    2. Wengine lazima waende, wengine lazima watume, lakini wote

    lazima washiriki (Rum 10:13-15).

    3. Sisi hatuja“tangaza kikamilifu Injili ya Kristo” mpaka

    tutakapokuwa tumeshirikisha habari za Kristo kwa wale

    ambao hawajawahi kusikia hizo habari.

    Kumalizia, Na Wito Kwa Watu Kuja Mbele

    Njoo, jitoe kikamilifu wewe mwenyewe ili kuhubiri Injili kwa

    ukamilifu kabisa. Njoo utiwe nguvu na kuwezeshwa na

    Roho Mtakatifu [ DRM ]

  • 42

    11 Tumaini Moja Kwa Ajili Ya Dunia

    Ujumbe Wenyewe Katika Sentensi Moja: Ni lazima tutangaze ujumbe

    wa matumaini yaliyomo katika Kristo kwa dunia, kwa nguvu za Roho

    Mtakatifu.

    Kusudi La Ujumbe: Ni ili wasikilizaji wajazwe na Roho Mtakatifu, na

    kujitoa kutangaza ujumbe wa msalaba kwa watu wote.

    Maandiko Ya Ujumbe: 1 Wakorintho 1:17-25

    Utangulizi 1. Njia pekee ya dunia kumjua Mungu ni kwa kanisa lililojaa nguvu

    za Roho linapotangaza Injili ya Kristo.

    2. Katika 1Kor 1-2, Paulo anatoa hoja yenye nguvu na kufafanua

    zaidi kweli hii.

    I. PAULO ANATOA HOJA KWAMBA UJUMBE WA MSALABA

    NDIYO TUMAINI MOJA KWA AJILI YA DUNIA (1Kor 1:17-

    25)

    A. Kuhubiri ujumbe wa msalaba huonekana upumbavu kwa dunia.

    1. Ni “upumbavu,” tena ni “kikwazo” (1Kor 1:23).

    B. Watu wa kimwili hujitazama wenyewe na uwezo wao ili kupata

    majibu kwa matatizo yao mazito na ya ndani sana.

    1. Tangu mwanzo wa wakati, watu wamejaribu kutafuta viongozi

    sahihi, na mipango mizuri ya kiuchumi, kijamii na kielimu.

    2. Hiyo mipango yote (hata ile iliyo bora kabisa) hatimaye

    hushindwa.

    a. Watu wasiokuwa wa kiroho hujaribu kutibu dalili huku

    wakipuuzia mzizi unaosababisha matatizo yao.

    b. Ugonjwa halisi ni dhambi, na dawa pekee ya dhambi ni

    Kristo.

    c. Mwanadamu hataweza kamwe kupata majibu yeye peke

    yake (1Kor 1:20).

    C. Kinacho-onekana kwa dunia kuwa upumbavu na udhaifu kwa

    kweli ndiyo hekima ya Mungu na nguvu Yake kuokoa (ms. 24-25).

    1. Sisi hupatanishwa na Mungu kupitia toba na kumwamini Kristo.

    2. Kristo kweli ndiyo Tumaini Moja Tu kwa dunia.

    II. PAULO ANAENDELEA KUTOA HOJA KWAMBA NI LAZIMA

    TUTANGAZE UJUMBE WA MATUMAINI KATIKA KRISTO

    KWA UAMINIFU A. Huko Korintho, Paulo kwa makusudi kabisa analenga kwenye

    kutangazwa kwa ujumbe wa Yesu Kristo aliyesulubiwa.

    1. Soma 1Kor 2:1-2.)

    2. Alichagua kutotangaza ujumbe mwingine wowote.

  • 43

    3. Aliandika 1Wakorintho kwa sababu kanisa lilikuwa

    linapoteza mwelekeo wa ujumbe wa Injili.

    4. Kanisa hilo Lilikuwa linapoteza uwezo wake wa kuwa shahidi

    wenye nguvu sana kwa ajili ya Kristo.

    B. Kanisa la Korintho – kama kanisa linguine lolote – lilikuwa

    limeitwa kuendeleza utume wa Mungu kupitia ushuhuda uliotiwa

    nguvu na kuwezeshwa na Roho Mtakatifu.

    1. Kila kanisa la mahali pamoja limeitwa kuwa jeshi la

    kimisheni.

    5. Paulo akuwa anajali juu ya kanisa pamoja na uwezo wake wa

    kutekeleza utume wa Mungu.

    C. Kwa hiyo Paulo aliwasihi waweke kando tofauti ndogo ndogo na

    kuungana kwenye ujumbe wa Injili (1Kor 1:10).

    III. MWISHO, PAULO ANATOA HOJA KWAMBA, ILI KUWEZA

    KUTANGAZA KWA UFANISI UJUMBE WA MATUMAINI, NI

    LAZIMA TUTEGEMEE NGUVU YA ROHO MTAKATIFU

    (1Kor 2:3-5, 10-14)

    A. Nguvu za Roho Mtakatifu zilimwezesha Paulo kufikisha kwa ngu-

    vu sana ujumbe wa Kristo kwa Wakorintho. (Soma 1Kor 2:3-5.)

    B. Kama Paulo, sisi pia tunahitaji nguvu za Roho ili kuweza

    kutangaza ujumbe wa Kristo katika mazingira yetu.

    1. Tunamhitaji Roho ili kuelewa ujumbe husika (1Kor 2:10, 12).

    2. Tunamhitaji Roho ili kufundisha ujumbe husika (ms.13).

    3. Tunamhitaji Roho kuonyesha uhalisi wa ujumbe husika (ms.4-5).

    4. Tunamhitaji Roho kuaminisha na kufungua mioyo ili kupokea

    ujumbe husika.

    C. Korintho ilianzishwa kwa uamsho mkubwa, wenye madhihirisho

    ya nguvu za Roho Mtakatifu.

    1. Lakini wakaanza kujikwaa na kuangalia mambo yao ya

    binafsi.

    2. Paulo anashughulikia baadhi ya vitu vilivyowaondoa kwenye

    kujali mambo muhimu baadaye katika 1Kor.

    D. Katika Matendo 1:8, Yesu alieleza nguvu inayohitajika kumtangaza

    Kristo.

    Kumalizia, Na Wito Kwa Watu Kuja Mbele Njoo uwezeshwe na Roho Wake ili usaidie katika kutimiza huo utume.

    [ MRT ]

  • 44

  • 45

  • 46

    12 Amri Ya Kwanza Ya Agizo Kuu: “Ombeni!” ~ Amri Za Agizo Kuu ~

    Ujumbe Wenyewe Katika Sentensi Moja: Ili kushiriki kwa ufanisi

    mkubwa katika Agizo Kuu, ni lazima tutimize amri ya maombi.

    Kusudi La Ujumbe: Watu wajitoe kuomba kwa ajili ya mavuno.

    Maandiko Ya Ujumbe: Mathayo 9:35-38

    Utangulizi

    1. Katika andiko letu la ujumbe, Yesu alisema kuhusu shamba

    laenye mavuno. (Soma ms. 35-37.)

    a. Watu walikuwa “wananyanyasika, na wasio na msaada.”

    b. Kwa sababu hiyo, Yesu anawaagiza wanafunzi Wake hivi:

    “Ombeni!” (v.38).

    2. Ujumbe huu ni kuhusu Njia Tano za sisi kuombea mavuno:

    I. OMBENI KWA AJILI YA NGUVU ZA MAVUNO (Mt 9:35-38)

    A. Yesu aliwapa wanafunzi Wake maagizo dhahiri kuhusu maombi,

    hivi:

    1. Walitakiwa waombe kwa “Bwana wa Mavuno.” 2. Walitakiwa kuomba kwa ajili ya “watenda kazi wengine waingie

    katika shamba Lake la mavuno.”

    3. Kwa maneno mengine, walitakiwa waombe kwa ajili ya

    Nguvu Ya Mavuno.

    B. Kuvuna mavuno kunahitaji rasilmali.

    1. Inahitajika rasilmali watu—Kwa hiyo, ni lazima tuombe.

    2. Inahitajika rasilmali fedha —Kwa hiyo, ni lazima tuombe.

    C. Nguvu ya Mavuno pia inahitaji upangaji kimkakati.

    1. Ni lazima tushirikiane na Roho Mtakatifu ili kuwapanga

    watenda kazi wa mavuno mahali anapotaka waende.

    2. Basi, ni lazima tuombe hekima na maongozi.

    II. OMBENI KWA AJILI YA MASHAMBA YA MAVUNO (Soma Yn 4:35-36.)

    A. Yesu aliwaambia wanafunzi Wake, “Yatazameni mashamba.”

    1. Aliwaambia kwamba mavuno “ni mengi” (Mt 9:37) na

    “yameiva” (Yn 4:35)

    2. Maneno Ni mengi ni maelezo kuhusu ukubwa wake—na neno

    yameiva ni maelezo juu ya “utayari” wake. B. Kwa sababu mavuno yameiva, muda ni kitu muhimu cha

    kuzingatia, yaani, kuna uharaka.

    1. Ni lazima tuvune mavuno kabla hatujachelewa sana.

    C. Kwa hiyo, ni lazima kuomba kwa ajili ya shamba la mavuno.

  • 47

    III. OMBENI KWA AJILI YA KITAKACHOPATIKANA ( Ufu 5:9.)

    A. Yohana aliona wakati ujao na kuona kitakachokuwa kimepatikana

    katika mavuno makuu ya Mungu siku za mwisho.

    1. Aliona kundi kubwa la watu “kutoka kila kabila na lugha na

    jamaa na taifa” (Ufu 5:9).

    B. Watafiti wanakadiria kwamba kuna makundi ya watu kiasi cha

    16,000 na zaidi duniani.

    1. Kila kikundi kimoja katika hivi ni lazima kiwakilishwe

    miongoni mwa hao waliokombolewa.

    2. Mpaka sasa, kiasi cha makundi ya watu 6,600 na zaidi

    hayajafikiwa.

    3. Ni lazima tupige hatua ya kuwafikia wale wote ambao bado

    hawajafikiwa.

    C. Ni lazima tuombe kwamba kanisa lijizatiti kufikia makundi ya

    watu ambao hawajafikiwa.

    IV. OMBENI DHIDI YA ADUI WA MAVUNO (Soma Mt 13:19; 28; 2Kor 4:4)

    A. Adui wa mavuno ni Shetani. (Soma Mt 13:19, 28.)

    1. Sisi tuko katika vita ya kiroho (Efe 6:12).

    B. Adui hupinga mavuno kwa njia tatu:

    1. Yeye “huondolea mbali” nguvu za ile mbegu ya Injili (ms.19).

    2. Hupanda magugu (watenda maovu) kati ya ngano (Mt 13:25).

    3. Hupofusha akili za wasioamini (2Kor 4:4).

    C. Ni lazima tupigane vita za kiroho kwa silaha za kiroho (2Kor 10:4).

    1. Silaha mojawapo ni maombi (Efe 6:18).

    V. OMBENI UWEZO WA KUVUNA MAVUNO (Soma Mdo 1:8.)

    A. Ni lazima tuwe na nguvu ya Mungu ili kuweza kufanya na

    kufanikisha kazi ya Mungu.

    1. Yesu aliahidi nguvu kwa ajili ya kushuhudia (Mdo 1:8).

    2. Tunapokea nguvu ya Roho wakati tunapobatizwa katika Roho

    Mtakatifu (Mdo 2:4).

    3. Mavuno ya Agano Jipya yalianza siku ile ya Pentekoste (Mdo

    2:41).

    B. Ili shughuli ya kimisheni ya kanisa ifanikiwe, ni lazima itiwe

    nguvu na kuwezeshwa na Roho Mtakatifu.

    C. Nguvu ya Roho inapatikana kwa maombi.

    1. Yesu alisema, “Ombeni nanyi mtapewa” (Lk 11:9). 2. Nguvu ya Roho pia hudumishwa kwa maombi.

    Kumalizia, Na Wito Kwa Watu Kuja Mbele

    1. Kuombea umisheni si jambo la hiari. Ni amri! [ UA ]

  • 48

    13 Amri Ya Pili Ya Agizo Kuu: “Nendeni!” ~ Amri Za Agizo Kuu ~

    Ujumbe Wenyewe Katika Sentensi Moja: Ni lazima twende na

    kumtangaza Kristo kwa mataifa katika nguvu za Roho Mtakatifu.

    Kusudi La Ujumbe: Watu waweze kujitoa wenyewe kutii amri ya Kristo

    ya kwenda kwa mataifa.

    Maandiko Ya Ujumbe: Mathayo 28:18-19; na Mathayo 21:28-31

    Utangulizi 1. Mistari yetu inazungumzia wajibu wetu kama wanafunzi wa

    Kristo kwenda kwa mataifa.

    2. Andiko la kwanza linajulikana kama “Agizo Kuu.”

    3. Andiko la pili ni ule mfano (hekaya) wa watoto wawili. (Simulia

    hadithi yenyewe)

    a. Mtoto wa kwanza alisema hatakwenda, halafu akatubu, na

    akaenda.

    b. Mtoto wa pili alisema atakwenda—lakini hakwenda.

    c. Mtoto wa kwanza ndiye aliyetenda mapenzi ya baba yake.

    d. Somo hapa: Utii ni zaidi ya ukiri – ni kutenda.

    4. Kiwango cha utii wetu ndicho kiwango tunachofanya mapenzi ya

    Mungu.

    5. Ujumbe huu unahusu sisi kutii Agizo Kuu.

    a. Matamko matano kuhusu ni kwa nini twende, na jinsi

    tunavyopaswa kwenda:

    I. KWA NINI NI LAZIMA TWENDE (Mt 28:19)

    A. Ni lazima twende kwa sababu Yesu ametuagiza sisi twende.

    1. Yeye ndiye Bwana wa Mavuno mwenye “mamlaka yote

    mbinguni na duniani” (ms.18).

    2. …kwa sababu kwenda ni alama ya uaminifu na upendo wetu

    Kwake.

    a. Maneno ya Yesu: “Mkinipenda mimi, mtatii…

    (Yn 14:15).

    3. …kwa sababu ni lazima tuwe na huruma kwa ajili ya

    waliopotea (2Kor 5:14).

    B. Itikio letu lisiwe kusema , “Tutakwenda,” halafu tusiende.

    Badala yake, liwe hivi: “Ndiyo, tutakwenda,”na kweli twende.

    II. MAHALI AMBAPO NI LAZIMA TWENDE (Mdo 1:8)

    A. Yesu kwanza aliwatuma wanafunzi Wake kwa “kondoo waliopotea wa Israeli” (Mt. 10:5; 15:24).

    1. Lakini, wakati “walio Wake” walipomkataa, Injili ilikwenda kwa

    kila mmoja ambaye ange “liamini jina Lake (Yn 1:11-12).

  • 49

    B. Hatimaye Yesu akaagiza kwamba Injili ipelekwe kwa kila kundi

    la watu, kila mtu binafsi, na kila mahali duniani (Mt 28:19; Mk

    16:15; Mdo 1:8).

    1. Kwa “dunia yote…kwa kila taifa” (Mt 24:14).

    2. Kwa “wenye hekima na wapumbavu” (Rum 1:14).

    3. Mpaka “mwisho wa nchi” (Mdo 1:8).

    4. Kila mahali ambapo “Kristo hatajwi” (Rum 15:20).

    C. Kwa hiyo basi, hebu twende kila mahali na kuzitangaza habari

    njema!

    III. WAKATI TUNAOTAKIWA KWENDA (Yn 4:35)

    A. Ni lazima twende sasa! 1. Maneno ya Yesu: “Yatazameni mashamba. Yamekwisha kuwa

    tayari kuvunwa” (ms. 35)

    2. Alikuwa anazungumzia uharaka wa uvunaji. 3. Maneno ya Yesu: “Maadamu bado ni mchana, ni lazima kuifanya

    kazi Yake Yeye aliyenituma. Usiku unakuja, ambapo hakuna

    anayeweza kufanya kazi” (Yn 9:4).

    B. Je, kwa sasa uko tayari, kwenda, kuomba na kutuma?

    IV. JINSI TUNAVYOTAKIWA KWENDA (Mdo 26:16)

    A. Ni lazima twende kama “watumishi na mashahidi” (Mdo 26:16)

    B Ni lazima tuwe na mtazamo wa mtumishi (siyo bwana).

    1. Sisi tunapaswa kuhudumu kama “kondoo katikati ya mbwa

    mwivu” (Mt 10:16).

    2. Ni lazima twende kama watumishi, wenye kutegemea moja kwa

    moja uwepo wa Kristo na nguvu za Roho (Mt 28:20; Mdo 1:8).

    C. Kusudi la kwenda ni kuwa shahidi kwa ajili ya Kristo (Lk 24:46-48).

    V. NINI CHA LAZIMA KWENDA NACHO (Mk 3:14; Mdo 1:8)

    A. Kwanza: Ni lazima twende na ujumbe.

    1. Yesu alisema, “…mtakuwa mashahidi wangu…” (Mdo 1:8). 2. Tunashuhudia kwa ajili ya Kristo na kuhusu Kristo.

    B. Pili: Ni lazima twende na nguvu ya Roho Mtakatifu.

    1. Maneno ya Yesu: “Mtapokea nguvu, wakati Roho Mtakatifu

    atakapokuja juu yenu…” (Mdo 1:8).

    2. Pasipo nguvu ya Roho, sisi tutashindwa hakika.

    3. Lakini katika nguvu za Roho, hakika tutafanikiwa.

    Kumalizia, Na Wito Kwa Watu Kuja Mbele 1. Njoo sasa, ujitoe kwa ajili ya utume wa Kristo.

    2. Njoo utiwe nguvu na Roho Mtakatifu. [ UA ]

  • 50

    14 Amri Ya Tatu Ya Agizo Kuu: “Hubirini!” ~ Amri Za Agizo Kuu ~

    Ujumbe Wenyewe Katika Sentensi Moja: Ni lazima tuhubiri Injili kwa

    uaminifu kila mahali na kwa kila mmoja.

    Kusudi La Ujumbe: Kwamba watu wa Mungu wajitoe wenyewe kuhubiri

    Injili kwa waliopotea.

    Maandiko Ya Ujumbe: 1 Wakorintho 1:21; Mathayo 24:14

    Utangulizi 1. Nini kinachotofautisha mahubiri na hotuba za wanasiasa na

    wasanii?

    a. Maudhui ya ujumbe na nia au kusudi la msemaji.

    b. Ujumbe wa wanasiasa na wasanii ni ahadi zisizo na kitu – na

    nia yao ni kujipigia debe.

    c. Ujumbe wa mhubiri ni Kristo – na nia au kusudi lake ni

    wokovu kwa waliopotea.

    2. Ujumbe huu utakazia wajibu wetu wa kuhubiri Injili kwa watu

    wote kila mahali kabla Yesu hajarudi.

    a. Paulo alisema, “Mungu, kupitia upumbavu wa kile kilichokuwa

    kinahubiriwa, alipendezwa kuwaokoa wale wote walioamini”

    (1Kor 1:21).

    b. Yesu alitamka hivi: “Injili hii ya ufalme ita