HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa...

29
HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO NA KESHO Titus Mpemba Ikisiri Umuhimu wa ukalimani katika mawasiliano umeongezeka kutokana na utandawazi. Utandawazi umerahisisha kukutanika na kuwasiliana kwa watu wazungumzao lugha tofauti kupitia wakalimani. Kutokana na ongezeko hilo la umuhimu wa ukalimani, kumekuwa na jitihada mbalimbali katika nchi mbalimbali kuhakikisha wanaandaliwa wataalamu wa kutosha kuendana na ongezeko hilo. Hivyo, kumekuwa na ongezeko la tafiti katika uwanja huu na taasisi mbalimbali zimeanzishwa ili kuandaa wataalamu wa fani hiyo na baadhi ya asasi zilizokuwapo zimepanua mafunzo yake na kujumuisha programu za uzamili. Mathalani, mpaka kufikia mwaka 2011, Barani Ulaya peke yake kulikuwa na takribani programu za mafunzo ya ukali mani kwa “ngazi ya umahiri zipatazo 135” (Munday, 2008: 6). Mapinduzi haya, pamoja na kuendeshwa kwa makongamano mbalimbali na kuchapishwa kwa machapisho mbalimbali kutokana na juhudi hizi, yameuwezesha ukalimani kujichomoza na kusimama kama taaluma mahususi inayojitegemea (Garzone & Viezzi, 2002: 11). Kwa kutumia mkabala wa kihistoria, makala haya yanachunguza jinsi nchi ya Tanzania ilivyoitikia jitihada hizi za kukuza ukalimani na kufanya hivyo yatatathmini mafanikio, mbinu na changamoto za jana na leo na kutoa mapendekezo ya jinsi ya kufanikisha harakati hizi hapo kesho. Makala yanalenga kujibu maswali makuu matatu: (1) Ukalimani kama somo, ulianza kufunzwa lini nchini Tanzania? (2) Hivi sasa taaluma ya ukalimani ina hali gani? na (3) Nini mustakabali wa taaluma ya ukalimani nchini Tanzania? 1.0 Utangulizi Umuhimu wa ukalimani katika mawasiliano ya siku za hivi karibuni umeongezeka kutokana na utandawazi na kuongezeka kwa mwingiliano wa tamaduni mbalimbali duniani. Katika zama hizi za utandawazi, kumekuwa na ongezeko la makutano ya watu na tamaduni mbalimbali na haja ya watu haowazungumzao lugha tofautikuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii. Hali hii imesababisha mwitiko wa namna mbalimbali kutoka kwa watu wa nyanja mbalimbali duniani. Mathalani, watafiti wameongeza zaidi juhudi za kuutafiti uwanja wa ukalimani kama anavyothibitisha Riccardi (2002:15): Tangu miaka ya 1950, wakati machapisho kuhusu ukalimani mikutanoni yalipotokea, utafiti kuhusu ukalimani umefuata mikondo tofauti... (Herbert 1952; Rozan 1956; Paneth 1957). Kwa mujibu wa uchambuzi wa data za kibibliografia uliofanywa na Pöchhacker (1995a), idadi ya machapisho kuhusu ukalimani katika kipindi cha miaka 6 kuanzia 1989 hadi 1994 ilikuwa ni mara mbili ya yale ya miaka 36 iliyopita (1952 hadi 1988), hali inayoonesha ushahidi bayana wa kuongezeka kwa raghba katika utafiti kuhusu ukalimani (Tafsiri ni yangu).

Transcript of HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa...

Page 1: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA,

LEO NA KESHO

Titus Mpemba

Ikisiri

Umuhimu wa ukalimani katika mawasiliano umeongezeka kutokana na utandawazi. Utandawazi

umerahisisha kukutanika na kuwasiliana kwa watu wazungumzao lugha tofauti kupitia wakalimani.

Kutokana na ongezeko hilo la umuhimu wa ukalimani, kumekuwa na jitihada mbalimbali katika

nchi mbalimbali kuhakikisha wanaandaliwa wataalamu wa kutosha kuendana na ongezeko hilo.

Hivyo, kumekuwa na ongezeko la tafiti katika uwanja huu na taasisi mbalimbali zimeanzishwa ili

kuandaa wataalamu wa fani hiyo na baadhi ya asasi zilizokuwapo zimepanua mafunzo yake na

kujumuisha programu za uzamili. Mathalani, mpaka kufikia mwaka 2011, Barani Ulaya peke yake

kulikuwa na takribani programu za mafunzo ya ukalimani kwa “ngazi ya umahiri zipatazo 135”

(Munday, 2008: 6). Mapinduzi haya, pamoja na kuendeshwa kwa makongamano mbalimbali na

kuchapishwa kwa machapisho mbalimbali kutokana na juhudi hizi, yameuwezesha ukalimani

kujichomoza na kusimama kama taaluma mahususi inayojitegemea (Garzone & Viezzi, 2002: 11).

Kwa kutumia mkabala wa kihistoria, makala haya yanachunguza jinsi nchi ya Tanzania ilivyoitikia

jitihada hizi za kukuza ukalimani na kufanya hivyo yatatathmini mafanikio, mbinu na changamoto

za jana na leo na kutoa mapendekezo ya jinsi ya kufanikisha harakati hizi hapo kesho. Makala

yanalenga kujibu maswali makuu matatu: (1) Ukalimani kama somo, ulianza kufunzwa lini nchini

Tanzania? (2) Hivi sasa taaluma ya ukalimani ina hali gani? na (3) Nini mustakabali wa taaluma

ya ukalimani nchini Tanzania?

1.0 Utangulizi

Umuhimu wa ukalimani katika mawasiliano ya siku za hivi karibuni umeongezeka

kutokana na utandawazi na kuongezeka kwa mwingiliano wa tamaduni mbalimbali

duniani. Katika zama hizi za utandawazi, kumekuwa na ongezeko la makutano ya

watu na tamaduni mbalimbali na haja ya watu hao—wazungumzao lugha tofauti—

kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na

masuala mengine ya kijamii. Hali hii imesababisha mwitiko wa namna mbalimbali

kutoka kwa watu wa nyanja mbalimbali duniani. Mathalani, watafiti wameongeza

zaidi juhudi za kuutafiti uwanja wa ukalimani kama anavyothibitisha Riccardi

(2002:15):

Tangu miaka ya 1950, wakati machapisho kuhusu ukalimani mikutanoni yalipotokea, utafiti

kuhusu ukalimani umefuata mikondo tofauti... (Herbert 1952; Rozan 1956; Paneth 1957).

Kwa mujibu wa uchambuzi wa data za kibibliografia uliofanywa na Pöchhacker (1995a),

idadi ya machapisho kuhusu ukalimani katika kipindi cha miaka 6 kuanzia 1989 hadi 1994

ilikuwa ni mara mbili ya yale ya miaka 36 iliyopita (1952 hadi 1988), hali inayoonesha

ushahidi bayana wa kuongezeka kwa raghba katika utafiti kuhusu ukalimani (Tafsiri ni

yangu).

Page 2: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

Hali ya Taaluma ya Ukalimani Tanzania: Jana, Leo na Kesho

113

Akimuunga mkono Riccardi huku akitilia mkazo kuhusu mwaka mmoja tu wa

2004, Pöchhacker (2011: 7) anaongezea kwa kusema:

Mwaka 2004 ni mwaka muhimu katika uchambuzi wowote wa maandiko

yanayohusu taaluma ya ukalimani. Mbali na ukweli kwamba ni mwaka wa

kuchapishwa kwa kitabu changu kitangulizi cha kiada ambamo mnapatikana

maelezo ya kina kuhusu chimbuko na maendeleo ya uwanja huu, na ambamo mna

mada nyingi kuhusu uga huu, kwa kuangalia idadi kubwa ya vitabu

vinavyoshughulikia ukalimani tu ambavyo vilichapishwa mwaka huo, mwaka 2004

unajichomoza kama mwaka wa miujiza ya utafiti kuhusu ukalimani (Tafsiri ni

yangu).

Licha ya ongezeko la tafiti, vilevile kumeanzishwa asasi na kozi mbalimbali kwa

ajili ya kufunza wakalimani katika ngazi mbalimbali (tazama Moser-Mercer, 2011:

49; Munday, 2012: 6).

Kwa jumla, wadau wa ukalimani katika nchi mbalimbali wameitikia kwa namna

tofautitofauti katika kukabiliana na ongezeko la umuhimu na mahitaji ya

ukalimani na wakalimani. Kwa kutumia mkabala wa kihistoria, makala haya

yanachunguza jinsi wadau mbalimbali wa ukalimani nchini Tanzania walivyoitikia

jitihada hizi za kukuza ukalimani ili kutathmini mafanikio, changamoto na mbinu

zilizotumika jana na zinazotumika leo na kutoa mapendekezo ya jinsi ya

kufanikisha harakati hizi hapo kesho. Kwa kuwa dhana yoyote kuhusu somo lolote

la taaluma mara nyingi hutegemea udhahanishi wa mtu anayejihusisha nalo

(Pöchhacker, 2004: 13), kabla ya kujitoma katika kujibu maswali tunayojiuliza

kuhusu ukalimani, makala yanaifasili kwanza dhana ya ukalimani; kisha, yanatoa

kwa ufupi historia ya ukalimani kuanzia kuibuka kwake hadi sasa. Hatimaye

makala yanatoa mapendekezo ya kuiendeleza taaluma ya ukalimani kwa manufaa

ya sasa na ya baadaye na mwisho ni hitimisho.

2.0 Fasili ya Ukalimani

Maandiko mengi yanayoifasili dhana ya ukalimani yanaonyesha kuwakilisha

mitazamo mitano na hivyo yanaweza “kugawanywa katika makundi matano”

(Pöchhacker, 2009: 133-134). Mtazamo wa kwanza unautazama ukalimani kama

aina mojawapo ya tafsiri. Mtazamo huu unawakilishwa na wanazuoni kama vile

Kade (1968), Setton (2002), Pöchhacker (2004 & 2009), Hale (2007), Bakize

(2013), miongoni mwa wengineo, na taasisi kama Longhorn (2011a) na TUKI

(2013), tukitaja kwa uchache. Mtazamo wa pili unauona ukalimani kama

mchakato wa kuzalisha vilongo au matini. Wanaosimamia mawazo haya ni pamoja

na Roy (2000) na Hale (2004), miongoni mwa wengineo. Mtazamo wa tatu

unauona ukalimani kama shughuli inayohusisha mchakato wa kiakili wa kuchakata

na kutoa taarifa. Wawakilishi wa mtazamo huu ni pamoja na Mshindo (2010).

Page 3: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

KISWAHILI JUZ. 76 (2013) 114

Kundi la nne linautazama ukalimani kama upatanishi au uwezeshaji wa

mawasiliano baina ya pande mbili zinazotumia lugha tofauti. Katika kundi hili

kuna akina Nolan (2005) na Hatim (2009). Kundi la tano linauona ukalimani kama

jitihada za kutambua maana ya ujumbe na kuihawilisha kama ilivyo. Wawakilishi

wake ni pamoja na Seleskovitch (1968), Seleskovitch na Lederer (1989), Lederer

(1994), Seleskovitch na Lederer (1984/2001), na Israël na Lederer (2005), kwa

kutaja wachache tu.

Akiwakilisha mtazamo wa kwanza, Kade (1968), kama alivyorejelewa na

Pöchhacker (2004 & 2009), anaufasili ukalimani kuwa ni namna ya tafsiri ambapo

matini ya lugha chanzi huwasilishwa mara moja tu na hivyo haiwezi kupitiwa au

kurudiwa tena na ambapo matini ya lugha lengwa hutolewa katika mazingira

yenye shinikizo la ufinyu wa muda huku kukiwa na fursa finyu ya kufanya

masahihisho na udurusu. Akimuunga mkono Kade, Pöchhacker (2004: 11 & 2009:

133) anasema kuwa ukalimani ni “namna ya Tafsiri ambapo ufafanuzi wa

kwanza na wa mwisho kwa lugha nyingine hutolewa kwa kuzingatia

uwasilishaji wa mara moja wa usemi wa lugha chanzi” (tafsiri ni yangu lakini

msisitizo ni wake). Pöchhacker anafafanua kwamba anatumia neno “tafsiri”

linaloanza na herufi kubwa kwa maana yake pana. Anasema pia kwamba fasili

yake inachomoza kipengele cha upapo kwa papo.

Wakati Kade (1968) na Pöchhacker (2004) hawabainishi hali ya lugha

zinazohusika katika ukalimani kuwa ni ama mazungumzo, ishara au maandishi

kwa sababu wanachomoza kipengele cha upapo kwa papo, Longhorn (2011a) na

TUKI (2013), wakichomoza pia kipengele cha upapo kwa papo, wanazingatia

zaidi kipengele cha mazungumzo. Kwa mujibu wa Longhorn (2011a), ukalimani

ni “kazi ya kutafsiri maongezi au mazungumzo,” na kwa mujibu wa TUKI (2013),

ukalimani ni “kazi ya kufasiri papo kwa papo mazungumzo kutoka lugha moja

kwenda nyingine.” Maelezo ya Longhorn na TUKI kuwa kukalimani ni kutafsiri

mazungumzo yanashindwa moja kwa moja kutambua kuwa kuna ukalimani

unaotumia lugha za alama. Vilevile yanazibagua aina nyingine za ukalimani kama

ule wa soga za mtandaoni, upitishaji wa maandishi kwenye kiwambo cha runinga,

na ukalimani wa kutazamia ambapo mkalimani hutakiwa kuifafanua matini ya

kimaandishi inayokuwa mbele yake kwa lugha nyingine kwa njia ya uneni wa

papo kwa papo kadiri inavyosomwa katika lugha chanzi (Hale, 2007).

Ingawa kwa hakika wanazungumzia ukalimani, kwa kudai kuwa ukalimani ni aina

fulani ya tafsiri na kwamba ni kazi ya kutafsiri, Kade (1968), Pöchhacker (2004;

2009), Longhorn (2011a) na TUKI (2013) wanazitumia dhana za ‘ukalimani’ na

‘tafsiri’ kimtoano. Jambo hili tunadhani ni muhali kwa kuwa linazikanganya dhana

hizo na kuibebesha mzigo mzito dhana ya tafsiri. Pöchhacker (2004, 11)

Page 4: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

Hali ya Taaluma ya Ukalimani Tanzania: Jana, Leo na Kesho

115

mwenyewe anaelekea kukubaliana na madai haya anapoonesha wasiwasi fasili

yake kwa kusema, “Hata hivyo, kuiegemeza dhana yetu ya ukalimani katika

mawanda mapana ya Tafsiri kunatuweka katika mashaka makubwa ya jinsi ya

kuifasili dhana hii [ya Tafsiri].” Tunasema dhana hizi zinakanganywa kwa sababu

ukalimani na tafsiri, ingawa zina uhusiano wa karibu, ni taaluma mbili tofauti

zinazojitegemea. Garzone na Viezzi (2002: 11) wanathibitisha kuwa ukalimani ni

taaluma inayojitegemea wanaposema kuwa:

Ingawa utafiti wa ukalimani bado unatumia mikabala anuwai, wanazuoni

wanaojihusisha na utafiti huo sasa wanajitambua kwa kiasi kikubwa kuwa wako

katika jumuiya ya kiutafiti ambayo inajitegemea ... na inayoendelea kutambuliwa

kwa kiasi kikubwa na jumuiya ya kisayansi duniani (Tafsiri ni yangu).

Kukanganywa kwa istilahi za “ukalimani” na “tafsiri” kunaashiria kuwa licha ya

ukalimani na tafsiri kuwa sehemu ya maisha ya kawaida ya binadamu (Schäfner,

2004: 1), watu wengi bado hawajui umahususi wa shughuli za mkalimani na za

mfasiri, jambo ambalo tunadhani litaswihi kudokezwa hapa kidogo. Nolan (2005:

2-3) anatutofautishia pande hizi mbili kwa kueleza tofauti tatu za msingi baina ya

shughuli za mkalimani na shughuli za mfasiri:

1. Mfasiri huchunguza taarifa iliyoandikwa kwa lugha moja (“lugha chanzi”)

na kuiwasilisha kimaandishi kwa lugha nyingine (“lugha lengwa”).

Mkalimani husikiliza ujumbe wa mazungumzo ulio katika lugha chanzi na

kuuwasilisha kwa mdomo katika lugha lengwa kwa njia ama ya ukalimani

andamizi au ukalimani sawia.

2. Mfasiri hutegemea utafiti wa kina, huku akiwa na nyenzo mbalimbali kama

maandiko kadha wa kadha na kamusi mbalimbali ili aweze kutoa tafsiri ya

kimaandishi iliyo sahihi na inayosomeka kwa usahihi kadiri

inavyowezekana. Mkalimani hutegemea uwezo wake wa kupata kiini cha

ujumbe na kukiwasilisha papo kwa papo kwa hadhira lengwa.

3. Shughuli ya mfasiri ni kama ile ya mwandishi, ilhali utendaji kazi wa

mkalimani ni kama ule wa mchezaji. Mfasiri mzuri anatumia muda wake

mwingi kutafuta istilahi sahihi ya kiufundi au uteuzi sahihi wa neno, lakini

mkalimani mzuri lazima aibuke papo hapo na ufafanuzi wa kuridhisha au

angalau kisawe kinachofaa iwapo neno sahihi halitamjia kichwani, ili

asisababishe hadhira yake kumsubiri kwa muda mrefu (Tafsiri yangu)

Hata hivyo, Schäfner (2004: 1), akiungwa mkono pia na Pöchhacker (2004: 10),

anaona kwamba kutofautisha ukalimani na tafsiri kwa kigezo cha maandishi, yaani

kwa kuona kuwa tafsiri huhusika na matini andishi na ukalimani huhusika na

Page 5: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

KISWAHILI JUZ. 76 (2013) 116

usemi wa mazungumzo, ni mtazamo wa watu walei (wasio weledi) kwa kuwa

katika uwanja wa taaluma za tafsiri na mafunzo ya wafasiri na/au wakalimani

tayari kumeshafanyika jitihada za kueleza vigezo mahususi zaidi

vinavyozipambanua shughuli za pande hizo mbili. Akimrejelea Kade, Schäfner

(2004: 1-2) anachukua kigezo cha wakati kama msingi wa kuzitofautisha

shughuli za mkalimani na za mfasiri huku akikihusisha kigezo hicho na

upatikanaji wa matini chanzi. Anasema:

Kwa mfasiri, matini chanzi hupatikana katika muundo funge (kwa mfano, ikiwa

imechapwa katika karatasi au imerekodiwa katika kanda) mpaka pale matini lengwa

itakapokuwa imetolewa. Hali hii humruhusu mfasiri kuirejelea matini chanzi mara nyingi

kadiri inavyombidi ili kusahihisha na kudurusu matini lengwa, huku akitumia nyenzo

anuwai. Kwa hiyo, matini lengwa ya mwisho inaweza kuwa ni matokeo ya ‘majaribio’

kadhaa, ikiwa imetolewa ikipitia hatua kadhaa kuanzia rasimu ya kwanza hadi zao la

mwisho. Kinyume chake, mkalimani hupata jaribio moja tu la kutoa matini lengwa kama

zao la mwisho kwani matini lengwa huwasilishwa kwa mkalimani kwa mdomo na kwa

mara moja tu na matini lengwa haina budi kutolewa papo hapo. Hakuna uwezekano wa

kurejelea nyenzo na kuna fursa finyu ya kulifanyia masahihisho zao la mwisho.

Uwezekano wa kuhakiki uelewekaji wa matini chanzi na kusahihisha matini lengwa

hutegemea aina ya ukalimani: kwa mfano, inawezekana kuhakiki uelewekaji wa matini

chanzi kwenye ukalimani kiungo lakini si kwa ukalimani sawia ambapo mkalimani

hufanyia kazi kibandani. Hata kama matini chanzi itapatikana kwa mkalimani ikiwa katika

namna fulani ya mfumo funge (yaani nakala ya hotuba), matini halisi itakuwa ni hotuba

inayotolewa kwa mdomo (ambayo inaweza kutofautiana na ile iliyoandaliwa kimaandishi)

(Tafsiri yangu).

Kwa kuzingatia madai tuliyoyatoa hapo awali kwamba kitendo cha kutangaza

kuwa kukalimani ni kutafsiri mazungumzo kinazibagua aina kadhaa za ukalimani

kama ule wa kutumia lugha za alama na ule wa soga za mtandaoni, tunakubaliana

na Schäfner kuwa ni kweli kutumia kigezo cha maandishi na mazungumzo

kutofautisha ukalimani na tafsiri kina upungufu. Hata hivyo, tunaona kwamba

Nolan na Schäfner wanakamilishana zaidi kuliko wanavyotofautiana kama

tutakavyoonesha mwishoni mwa sehemu hii.

Tukiendelea na mtazamo wa pili, mwakilishi wa mtazamo huu, Roy (2000: 3-4),

anaufasili ukalimani kuwa ni mchakato wa kubadilishana mazungumzo kwa zamu

baina ya pande mbili zinazotumia lugha tofauti kwa njia ya mkalimani.

Wafuasi wa mtazamo wa tatu wanaufasili ukalimani kuwa ni shughuli

inayohusisha mchakato wa kiakili ambapo mkalimani huwa na jukumu la

kutambua, kuchakata na kutoa ujumbe wa kunenwa (Pöchhacker, 2009: 134).

Akiwakilisha mtazamo huu, Mshindo (2010: 30) anasema, “Ukalimani ni shughuli

ya kiakili inayowezesha kuwasiliana kwa maneno yanayosemwa au ishara

Page 6: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

Hali ya Taaluma ya Ukalimani Tanzania: Jana, Leo na Kesho

117

zinazooneshwa baina ya watu ambao hawasemi lugha moja, au ambao hawatumii

ishara za aina moja.”

Kwa mujibu wa mtazamo wa nne, ukalimani ni upatanishi au uwezeshaji wa

mawasiliano baina ya pande mbili au zaidi zinazotumia lugha tofauti na zenye

usuli wa tamaduni tofauti (Pöchhacker, 2008: 9-13; 2009: 134). Nolan (2005: 2)

anasema kwamba ukalimani unaweza kufasiliwa kwa ufupi kama uwasilishaji wa

uelewa kwa kuzingatia ukweli kwamba maana ya msemaji huelezeka vizuri zaidi

kwa lugha yake mama lakini hueleweka vizuri zaidi kwa lugha za wasikilizaji na,

kwa kuziba pengo la kimawasiliano baina ya lugha mbili au zaidi, wakalimani

huwasaidia wasemaji kutekeleza majukumu yao kwa kuwafanya waeleweke na

huwasaidia wasikilizaji kukidhi haja yao ya kuelewa yale yanayosemwa.

Wawakilishi wa kundi la tano, wanaufasili ukalimani kuwa ni jitihada za

kutambua maana ya ujumbe ambapo mkalimani hutakiwa kutoa ujumbe uliokitwa

kwenye uhawilishaji wa maana ya kauli nzima na si uhawilishaji wa maana ya

neno kwa neno ili kukidhi haja ya kimawasiliano ya pande zinazohusika katika

mawasiliano hayo (tazama Seleskovitch, 1968; Seleskovitch & Lederer, 1989;

Lederer, 1994; Seleskovitch & Lederer, 1984/2001; Israël & Lederer, 2005).

Mitazamo yote mitano hapo juu, tunaichukulia kuwa inakamilishana zaidi kuliko

inavyogongana. Kutokana na michango ya makundi yote matano, tunaweza

kubainisha vigezo mtambuka vinavyoweza kutusaidia kufasili dhana ya ukalimani

bila kuegemea mtazamo wowote mahususi. Vigezo hivyo ni pamoja na

upatikanaji wa matini chanzi, uchakataji wa ujumbe wa matini chanzi,

uzingatiaji wa utamaduni na muktadha, upapo kwa papo katika kutoa matini

lengwa, ufinyu wa fursa ya kuufanyia marekebisho ujumbe katika lugha

lengwa ukishatolewa, na lengo la mwisho ambalo ni kuwezesha mawasiliano

baina ya pande mbili zinazoshindwa kuwasiliana kwa sababu ya tofauti za lugha.

Kwa hiyo, kutokana na vigezo hivi, dhana ya ukalimani inaweza kufasiliwa kwa

upana kuwa ni “uwezeshaji wa mawasiliano baina ya pande mbili zinazotumia

lugha1 tofauti na zenye usuli wa tamaduni tofauti ambapo mwezeshaji hupokea

ujumbe wa matini ya lugha chanzi mara moja tu, huuchakata (huutafakari na

kuuelewa) na kisha kuuwasilisha kwa lugha nyingine papo kwa papo akizingatia

muktadha, sarufi na utamaduni wa lugha hiyo huku akiwa hana fursa ya kuufanyia

marekebisho.”

1 Tunalitumia neno lugha kwa maana yake pana inayojumuisha pia ishara zitumiwazo na watu

wasiosikia, yaani lugha ya alama.

Page 7: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

KISWAHILI JUZ. 76 (2013) 118

3.0 Hali ya Taaluma ya Ukalimani Nchini Tanzania: Jana, Leo na Kesho

Ukalimani unaelezwa kuwa ni desturi kongwe ambayo imekuwapo tangu kale

(Pöchhacker, 2004 & 2009; Giambruno, 2008; Baker & Saldanha, 2009) hata

kabla ya ugunduzi wa maandishi. Hata hivyo, ukalimani kama taaluma – elimu na

maarifa yanayopatikana kwa kusoma (Longhorn, 2011b) na kama mitalaa ya

utafiti – umeanza katika karne ya ishirini tu (Munday, 2008: 7; Pöchhacker, 2009:

129). Pöchhacker (2004) anaeleza kuwa shughuli hii imekua na kuendelea katika

vipindi mbalimbali vya kihistoria katika mazingira mbalimbali, tangu mazingira ya

kukutana kwa mara ya kwanza kwa makabila yanayotumia lugha tofauti hadi

kufikia hatua ya kuunganisha mataifa mbalimbali. Kwa kutumia mkabala wa

kihistoria, sehemu hii inayachunguza maendeleo hayo ya ukalimani, ikijihususisha

zaidi na nchi ya Tanzania. Tunaigawa historia ya maendeleo ya ukalimani nchini

Tanzania katika vipindi vikuu vitatu: jana (kabla ya na wakati wa ukoloni), leo

(baada ya ukoloni mpaka sasa) na kesho (siku zijazo). Katika kipindi cha jana,

tunaangalia hatua za mwanzo za ukalimani, yaani jinsi ulivyoibuka na kuendelea

nchini Tanzania. Tunaangalia pia jinsi ulivyostawi hadi kufikia hatua ya

kufundishwa kwenye mifumo rasmi ya elimu. Katika kipindi cha leo, tunaangalia

hali ya taaluma ya ukalimani ilivyo sasa na changamoto zinazoikabili. Na katika

kipindi cha kesho, tunaangalia mustakabali wa taaluma ya ukalimani nchini

Tanzania.

3.1 Jana

Kwa kuwa nyenzo kuu ya ukalimani ni lugha, kuibuka kwa ukalimani hakuna budi

kuhusishwa na kuzuka, kuanza kutumika na kuendelea kwa lugha. Ingawa

maandiko ya kidini yanaeleza kuwa Adamu alipoumbwa tu alipewa uwezo wa

kusema na kutoa majina kwa viumbe vyote vilivyokuwapo katika Bustani ya

Edeni (Mwanzo 2: 19-20), uhalisia unaonyesha kuwa binadamu anachukua muda

kujifunza lugha hadi kuwa na umilisi unaomwezesha kuitumia barabara. Utafiti pia

umeonesha kuwa ni takriban miaka kati ya 300,000 na 50,000 tu iliyopita ndipo

mwanadamu alianza kuwasiliana kwa kutumia lugha (Cobley, 2001; Holden na

wenzake, 2004; Yule, 2010). Ingawa mwanadamu alianza kutumia lugha miaka

mingi iliyopita, ni katika miaka ya karibuni tu ndipo ameanza kutumia huduma ya

ukalimani. Kwa mujibu wa Giambruno (2008: 27), “Kuna ushahidi wa kutumika

kwa wakalimani tangu miaka ya 3000KK huko Misri...” Ushahidi huo ni hiroglifu

na maandishi ya kwenye makaburi pamoja na marejeo ya kimaandishi

yanayoelezea majukumu muhimu ambayo wakalimani waliyatekeleza katika

Ugiriki ya Kale na Himaya ya Rumi. “Maandishi ya akina Caesar, Cicero, Horace,

Pliny na Valerius Maximus,” yote yanadokeza uhawilishaji wa ujumbe kutoka

lugha moja kwenda nyingine (Giambruno, 2008: 27).

Page 8: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

Hali ya Taaluma ya Ukalimani Tanzania: Jana, Leo na Kesho

119

Tukiacha nchi ya Misri inayotajwa kuwa ndipo ushahidi wa kale kuhusiana na

shughuli za ukalimani uliopatikana, utafiti wa wanazuoni wengi wa Kimagharibi

wanaochunguza maendeleo ya ukalimani unaelekea kuelemea upande wa nchi za

Magharibi na Asia peke yake (tazama, kwa mfano, Seleskovitch, 1968;

Seleskovitch & Lederer, 1989; Lederer, 1994; Seleskovitch & Lederer, 1984/2001;

Israël & Lederer, 2005; Pöchhacker, 2004 & 2009; Giambruno, 2008; Hatim,

2009). Hata hivyo, upo ushahidi kwamba ukalimani umekuwa pia ukiendelea

Barani Afrika kwa muda mrefu. Mathalani, Baker na Saldanha (2009: 313)

wanaeleza kuwa “tafsiri2 barani Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara ina umri

takriban sawa na mawasiliano kwa njia ya mdomo.”

Utafiti wake ukiwa umejielekeza katika jamii ya Wahaya, Mutembei (2013)

anafafanua kuwa ukalimani ambao ulikuwa ukiendelea Barani Afrika kwa muda

mrefu, na ambao ungali ukiendelea, ni ule wa lugha za wahenga, au mizimu,

ambazo hunenwa na viti3 wao wanapokuwa wamepagawa. Barani Afrika, kabla ya

ujio wa dini za kigeni na ukoloni, wahenga walikuwa sehemu muhimu ya maisha

ya kila siku ya Waafrika. Kwa mujibu wa Mutembei (2013), kulipotokea matatizo

mbalimbali ya kijamii, kidini au kisiasa, Waafrika walitafuta ufumbuzi wa

matatizo hayo kwa wahenga. Wahenga hawa walikuwa wakiwasiliana nao kupitia

viti. Viti walipopagawa walizungumza lugha ambayo haieleweki bila msaada wa

mkalimani. Hivyo, ili lugha ya wahenga iweze kueleweka kwa watu wote

waliohudhuria tukio lililohusika, ilikuwa ni lazima isimbuliwe na mkalimani.

Ukalimani huu ungali ukiendelea katika jamii mbalimbali za Tanzania na Afrika

kwa jumla (tazama Beattie & Middleton, 1969; Wisjen & Tanner, 2002). Kwa hiyo,

mbali na eneo la jumla la Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara linalotajwa na

Baker na Saldanha (2009), kuna ushahidi pia kwamba nchini Tanzania – ambayo

haikuwa na jina hili wakati huo – wakalimani walikuwapo hata kabla ya majilio ya

wakoloni.

Mbali na ukalimani wa lugha ya mizimu katika jamiilugha moja moja nchini

Tanzania, kulikuwapo pia na ukalimani baina ya watu waliozungumza lugha

tofauti katika biashara hasa ya kubadilishana vitu na mazao kabla ya ukoloni

(Pöchhacker, 2004; Hadjivayanis, 2011). Ingawa Pöchhacker (2004: 14) anadai

kuwa ukalimani wa kibiashara ndio wa kale zaidi, ukalimani wa lugha ya

mizimu unaelekea kuwa ndio ukalimani mkongwe kabisa kwani ulianza kabla

2 Baker na Saldanha wanatumia neno tafsiri kama istilahi ya jumla inayojumuisha pia ukalimani.

3 Wateule wanaopagawa na kutumiwa na wahenga kuzungumza ujumbe wao. Lugha wanenazo

wahenga hazieleweki kwa urahisi kwa watu wa kawaida. Hivyo, hukalimaniwa na watu maalumu

wanaoijua lugha ya kihenga.

Page 9: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

KISWAHILI JUZ. 76 (2013) 120

jamii hazijaanza kujihusisha na masuala ya biashara kati ya jamii moja na

nyingine.

Baadaye jamii zilistawi zaidi na kukazuka na kuimarika mifumo mbalimbali ya

kisiasa. Baadhi ya viongozi wa kisiasa wakaanza kubuni na kutumia lugha

maalumu ambayo haikueleweka kirahisi kwa watu wa kawaida. Hivyo, ilihitaji

kufafanuliwa na wakalimani ili watu wa kawaida waweze kuelewa. Wakimnukuu

Danquah (1928: 42), Baker na Saldanha (2009) wanafafanua kuwa wakalimani

hao hawakuwa na jukumu la kurudia tu maneno ya wakuu wao wakishasema kwa

lengo la kuyafanya yaeleweke kwa hadhira yote ya chifu au mfalme. Pia,

waliyadhihirisha kwa uwazi mamlaka ya mfalme yaliyokuwa katika kauli zake.

Aidha, wakalimani hao pia, walitarajiwa kuitia nakshi hotuba ya mfalme na

kufafanua dhamira yake kwa niaba yake. Baker na Saldanha (2009: 313-314)

wanaendelea kusema kwamba mkalimani hakutarajiwa kuongezea mada yoyote

mpya lakini alikuwa na ruksa ya kutanua semi za mfalme na kuzifuma upya

sentensi zake na kuichombeza hotuba kwa tafakuri za kicheshi na kifalsafa ambazo

zingempamba zaidi mfalme na mkalimani mwenyewe. Aidha, wanafafanua kuwa

jambo hili linathibitishwa na ukweli kwamba jamii za Kiafrika, Kusini mwa

Jangwa la Sahara kabla ya ukoloni, kama ilivyothibitishwa na utafiti wa

wanahistoria simulizi kama “Vansina, Bascom, Finnegan na Okpewho” na “baadhi

ya wamisionari na wapelelezi wa Kizungu”, zilikuwa zikihifadhi historia kichwani

na kuirithisha kutoka kizazi hadi kizazi kwa njia ya mdomo. Zilikuwa na watu

wenye vipaji vya kuhifadhi na kusimulia historia na utamaduni wa watu wao.

Hawa ndio walikuwa wakalimani na wafasiri wa wafalme, machifu na watemi

ambao walikuwa wakifanya kazi katika ikulu na mahakama ya himaya za kale za

Kiafrika. Hivyo, katika kipindi hiki ulizaliwa ukalimani wa kisiasa na ukalimani

wa mahakama. Hata hivyo, inafaa kudokeza hapa kwamba dhana ya mahakama

inayotajwa hapa ni tofauti na tunayoijua hivi leo.

Aidha, kufuatia kustawi kwa jamii na mifumo ya kisiasa kuzuka na kuimarika,

mbali na makutano ya wanajamii katika biashara, kuliibuka haja ya ushirikiano.

Viongozi wa kisiasa wa jamii zenye lugha tofauti waliweza kukutana na

kujadiliana kuhusu masuala mbalimbali ya kisiasa. Wakati mwingine viongozi

hawa walianzisha ushirikiano wa kisiasa baina yao. Jambo hili liliwezekana kwa

msaada wa wakalimani. Hata hivyo, wakati mwingine yalizuka mapigano baina

yao. Pöchhacker (2004: 14) anasema:

Pale wawakilishi wa jamii zenye lugha na tamaduni tofauti walipokutana kwa lengo

la kuanzisha na kuendeleza mahusiano ya kisiasa, ... walitegemea wawezeshaji wa

mawasiliano waliokuwa wakifanya ... ukalimani wa kidiplomasia. Pale mahusiano

yalipochacha, au pengine hata kabla hayajaanzishwa, migogoro ya kivita huenda

ililazimisha kuwapo kwa mawasiliano yaliyowezeshwa na wakalimani kwenye

Page 10: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

Hali ya Taaluma ya Ukalimani Tanzania: Jana, Leo na Kesho

121

mazingira ya kijeshi. Ukalimani wa kijeshi, kama unavyofanyika katika

mazungumzo na washirika, majadiliano ya kusitisha vita au usaili wa mateka, una

uhusiano wa kihistoria na ule wa kidiplomasia (Msisitizo ni wake lakini tafsiri

yangu)

Jamii zilivyoendelea kustawi, ziliendelea kujiimarisha na kupanua himaya zao,

huku jamii kadhaa zenye nguvu zikiziweka jamii dhaifu katika ukoloni na kuanza

kuwatawala. Kwa kufanya hivyo, ziliweka makundi ya watu mbalimbali

wanaosema lugha tofauti katika himaya moja. Katika hali kama hii, ili wakoloni

waweze kuwasiliana na watu waliowatawala na ili watu watawaliwa waweze

kupata huduma mbalimbali za kijamii, ilibidi ama watawala wajue lugha za

watawaliwa au watawaliwa wajue lugha ya watawala wao au pande zote zitegemee

huduma za wakalimani. Giambruno (2008: 29) anaeleza kuwa uvamizi mwingi na

mashambulio mengi katika mabara ya Asia, Afrika na Amerika ambayo

yalifanyika wakati wa ukoloni yalileta makutano ya lugha na kuhitaji ukalimani.

Aidha, kufuatia kuanzishwa kwa taasisi za kutekeleza sheria na kusimamia haki

katika maeneo mapya yaliyotekwa au yaliyowekwa chini ya ukoloni, wakalimani

waliandaliwa ili kuhakikisha kwamba hata watu wasiozungumza lugha ya

watawala wangeweza kuhudumiwa na kuwajibishwa pia. Hapo ukazaliwa

ukalimani mahakamani kwa dhana ya mahakama tunayoijua hii leo.

Wakati wa majilio ya ukoloni, wakalimani Tanzania walitumika kuwezesha

mawasiliano baina ya machifu na watangulizi wa ukoloni kama wamisionari na

wapelelezi waliofanya mikataba ya udanganyifu na katika daawa mbalimbali

mahakamani. Mathalani, mkataba uliotiwa saini baina ya mpelelezi wa

Kijerumani, Dkt. Karl Peters, na Sultani Mangungo wa Msowero huko Usagara

mnamo tarehe 29 Novemba 1884 unaeleza kuwa, “Mkataba huu umefafanuliwa

kwa Sultani Mangungo na Mkalimani Ramazan kwa uwazi na uangavu”

(Hollingsworth, 1929: 139). Akithibitisha kutumika kwa wakalimani katika

biashara kabla ya ukoloni na katika daawa mbalimbali mahakamani wakati wa

ukoloni, Hadjivayanis (2011: 2) anaeleza kuwa “lugha ya Kiswahili ilitekeleza

jukumu la ufasiri wa mdomo uliofanywa na wakalimani ambao walijulikana kwa

jina la mtapta4 wakati wa vipindi vya biashara za awali na halikadhalika katika

mahakama za kikoloni”. Whiteley (1969: 64) naye anaeleza kwamba “Hatimaye

hatua muhimu ilichukuliwa mnamo mwaka 1955 ya kuanzisha ukalimani sawia wa

Kiingereza/Kiswahili katika vikao vya Baraza la Kutunga Sheria.” Wakalimani wa

mwanzo wanaotajwa katika historia ya ukalimani Tanzania ni Ramazan ambaye

4Ingawa Hadjivayanis analitumia neno mtapta kuwakilisha dhana za mkalimani na mfasiri na

analitumia hivyohivyo hata anapozungumzia wingi, ufafanuzi wa neno hilo kwenye kamusi za

Kiswahili (tazama BAKIZA, 2010: 278; Longhorn, 2011a: 355; TUKI, 2013: 388) unaonyesha

kuwa lina maana ya mkalimani tu na kwamba wingi wake ni watapta.

Page 11: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

KISWAHILI JUZ. 76 (2013) 122

alikuwa mkalimani wa mpelelezi wa Kijerumani Karl Peters (Hollingsworth,

1929: 139), Selemani bin Mwenye Chande ambaye alikuwa mkalimani rasmi wa

Gavana wa Kijerumani wa Afrika Mashariki enzi za ukoloni wa Wajerumani

(Hadjivayanis, 2011: 22, akimrejelea Rollins, 1983: 50) na Kadhi wa Kilwa,

Mohamed bin Abdulrahman Hamdani ambaye alikuwa mkalimani wa

mahakamani aliyezungumza kwa ufasaha lugha za Kijerumani, Kiingereza,

Kiarabu na Kigujerati, pamoja na Brenn ambaye alikuwa mfasiri na mkalimani wa

kujitegemea (Hadjivayanis, 2011: 22-23).

Ushiriki wa Tanzania katika ustawi wa ukalimani ulioelezwa hapo juu,

unaonyesha kuwa baadhi ya wakalimani walioshiriki katika kuwezesha

mawasiliano wakati huo, walikuwa na maarifa mapana ya lugha, jambo ambalo ni

ishara kuwa huenda kulikuwa na mafunzo waliyoyapata kabla. Jambo hili linaibua

udadisi wetu na kutufanya tujiulize, “Ukalimani ulianza kufunzwa lini nchini

Tanzania?” Kwa mujibu wa Hadjivayanis (2011: 24), ukalimani ulianza

kufundishwa nchini Tanzania enzi za ukoloni wa Wajerumani. Wakati huo “Afrika

Mashariki ya enzi za ukoloni wa Wajerumani, ambayo ndiyo Tanzania ya sasa”

ilikuwa na shule zenye mfumo wa ngazi tatu. “Katika miaka mitatu ya kwanza,

wanafunzi walikuwa wakifundishwa kusoma, kuandika na kuhesabu.” Katika

ngazi ya pili, ambayo ilikuwa ni miaka miwili, “kulitolewa mafunzo ya ufundi” na

katika ngazi ya juu kulikuwa na shule moja iliyojengwa Tanga ambayo “ilitoa

mafunzo ya ukarani, kazi za viwandani na ualimu na halikadhalika baadhi ya kozi

za kitaaluma zilizolenga kuandaa ... wakusanya kodi, wakalimani, na mafundi...”

(tafsiri na msisitizo ni vyangu). Ingawa Hadjivayanis hataji mwaka mahususi,

historia inatuambia kwamba Shule ya Tanga ilijengwa mnamo miaka ya 18905.

Hivyo, kutokana na ukweli huu, tunaweza kuchukulia kwamba ukalimani ulianza

kufundishwa nchini Tanzania mnamo miaka ya 1890. Hata hivyo, tunadhani

wakati huo wakalimani walifundishwa tu kozi mbalimbali za lugha ambazo

ziliwapa stadi za kuwawezesha kukalimani lakini hakukuwa na programu

maalumu iliyokusudiwa kutoa wahitimu wenye utaalamu mahususi wa ukalimani

wenye astashahada, stashahada au shahada za ukalimani.

Ni vyema kukumbusha hapa kwamba mafunzo ya ukalimani ambayo tunasema

kuwa yalianza kutolewa miaka ya 1890 ni yale yanayofuata mfumo rasmi wa

elimu ya kuingia na kukaa darasani. Ukalimani uliofafanua lugha ya mizimu

tulioutaja hapo awali ulianza zamani kabla Tanzania haijaanzisha mahusiano na

watu wa mataifa ya nje kama Waarabu, Wajerumani na kadhalika. Wakati huo

5 Wilfred Whitely (1969) Swahili: the Rise of a National Language, ukurasa wa 59 anataja mwaka

1893 ilhali Abdi Mahboob na Ali Mahboob (2013) “Tanga Town: an Introduction” katika tanga-

line.tripod.com ( imseomwa tarehe 7 Novemba 2013) wanataja mwaka 1895.

Page 12: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

Hali ya Taaluma ya Ukalimani Tanzania: Jana, Leo na Kesho

123

elimu ilikuwa ikitolewa kwa njia ya mdomo, kuangalia na kwa kutenda na ilikuwa

ikirithishwa kutoka kizazi kimoja kwenda kingine. Wakalimani wa lugha ya

mizimu walipata elimu yao, kama wanavyoipata leo, kwa kurithishwa. Na elimu

hii haikuwa kwa kila mtu, bali watu wachache, mathalani, ukoo fulani tu.

Waingereza walipochukua nchi kutoka kwa Wajerumani, waliendeleza juhudi

zilizoanzishwa na Wajerumani. Wakoloni wa Kiingereza walitumia sera ya

utawala wa machifu ambayo ilikuwa “udongo wenye rutuba kwa ustawi wa

wakalimani” (Hadjivayanis, 2011: 23).

Pamoja na ukweli kwamba wakoloni walistawisha ukalimani Barani Afrika,

wakoloni wengine waliuviza kutokana na sera za tawala zao. Mathalani, wakati

ambapo wakoloni wa Kiingereza walitumia sera ya utawala wa machifu ambayo

iliruhusu kustawi kwa wakalimani, kama tulivyokwishaona, Wareno na Wafaransa

walipendelea sera ya usilimisho ambayo haikutoa fursa kwa lugha za kienyeji

kustawi (Baker & Saldanha, 2009: 316) na hivyo ilififisha ustawi wa ukalimani na

wakalimani.

3.2 Leo

Kuondolewa kwa wakoloni na kupatikana kwa uhuru katika nchi zilizokuwa

zikitawaliwa kulikuwa na athari kuhusiana na suala la ukalimani. Makundi ya

watu mbalimbali wanaosema lugha tofauti yaliendelea kuwekwa chini ya utawala

mmoja wa kisiasa kufuatia mipaka iliyowekwa na serikali za kikoloni na baadaye

kurithiwa na mataifa huru. Kwa sababu hii, huduma za ukalimani zimeendelea

kuwa tegemeo la watu wengi katika nchi zisizokuwa na lugha moja

inayowaunganisha wananchi wote, Tanzania ikiwamo. Leo hii, ukichochewa na

mahitaji ya utandawazi na utangamano wa kikanda, ukalimani umekuwa ni jambo

muhimu sana katika mawasiliano kwani watu wanaozungumza lugha tofauti sasa

wanaweza kufanya mikutano wakaelewana bila matatizo kwa msaada wa

wakalimani (Nolan, 2005). Hali hii, kama tulivyoeleza hapo awali, imesababisha

mwitiko wa namna mbalimbali duniani, kuanzia kupanuka kwa utafiti wa

ukalimani hadi kuanzishwa na kupanuliwa kwa mafunzo ya wakalimani katika

ngazi mbalimbali. Je, Tanzania imeitikiaje mapinduzi haya? Imekuwa na

mafanikio gani na inakabiliwa na changamoto zipi?

Baada ya kupata uhuru mnamo mwaka 1961, miongoni mwa mambo mengineyo,

Tanzania ilikipandisha hadhi Kiswahili. Ilikifanya kuwa lugha ya taifa mnamo

mwaka 1962. Na baada ya miaka miwili, kwa sheria ya Bunge ya mwaka 1964,

Serikali ya Tanzania iliipandisha hadhi iliyokuwa Tume ya Lugha (ya Kiswahili)

ya Afrika Mashariki na kuwa Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili. Miongoni mwa

majukumu ya taasisi hii ni pamoja na kuandaa wakalimani na kutoa huduma za

Page 13: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

KISWAHILI JUZ. 76 (2013) 124

ukalimani. Ingawa haijaanza rasmi kuandaa wakalimani, Taasisi hii tayari

imekwishaanzisha Kituo cha Istilahi, Tafsiri, Ukalimani na Teknolojia ya Lugha

kama namna ya kuitikia mahitaji ya huduma hii.

Aidha baada ya uhuru, Serikali ya Tanzania ilibadili mfumo wa elimu iliourithi

kutoka kwa wakoloni wa Kiingereza. Mnamo mwaka 1967, Azimio la Arusha

lilitangazwa, Sera ya Elimu ya Ujamaa na Kujitegemea ikatungwa na Kiswahili

kikatangazwa kuwa lugha ya kufundishia elimu yote ya msingi. Elimu ya msingi

ilitengewa miaka saba mfululizo. Wahitimu wengi walitazamiwa kwenda kuishi

vijijini na kutekeleza sera ya ujamaa na kujitegemea. Kwa hiyo, lugha ya

Kiswahili ndiyo iliwafaa zaidi. Kwa kuwa wahitimu wengi walitazamiwa kwenda

kuishi vijijini na kutekeleza sera ya ujamaa na kujitegemea, suala la ukalimani

halikutiliwa maanani katika mfumo huu mpya wa elimu. Elimu ya sekondari

iligawanywa katika ngazi mbili – ngazi ya kawaida na ngazi ya juu na ni

wanafunzi wachache tu ndio walitarajiwa kuendelea na masomo ya sekondari hadi

elimu ya juu. Ukalimani pia haukupewa nafasi katika elimu ya sekondari.

Hata hivyo, kwa kutambua umuhimu wa ukalimani na masuala ya tafsiri, Serikali

ya Tanzania iliunda vyombo ambavyo, miongoni mwa mambo mengine, vilipewa

jukumu la kuratibu na kutoa huduma za ukalimani na tafsiri. Mathalani, mnamo

mwaka huohuo wa 1967 Bunge liliunda Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA).

Miongoni mwa majukumu ya Baraza hili ni kuratibu na kutoa huduma za

ukalimani ndani na nje ya nchi ya Tanzania.

Kufuatia kuongezeka zaidi kwa mahitaji ya ukalimani na wakalimani, na kwa

kutambua kwamba msingi mzuri hujengwa kuanzia ngazi za chini, mnamo mwaka

2005 Serikali iliamua kuingiza vipengele vya masomo ya ukalimani na tafsiri

katika mtalaa wa elimu ya kidato cha tano na sita. Hatua hii imewahamasisha

waandishi na wataalamu wa Kiswahili kuandika vitabu vya ukalimani na tafsiri.

Mathalani, mpaka kufikia mwaka 2005 kulikuwa na kitabu kimoja tu cha tafsiri

ambacho kilikuwa kinatumika kwa wanafunzi wa somo la tafsiri katika vyuo

vikuu (tazama Mwansoko, 1996). Kitabu hiki hakina mada yoyote kuhusu

ukalimani. Hata hivyo, katika kipindi cha miaka minne peke yake kuanzia mwaka

2010 mpaka kufikia mwaka 2013, vitabu vinne vinavyoligusa suala la ukalimani

(tazama Mshindo, 2010; Wanjala, 2011; Haule & Tatinka, 2012; Bakize, 2013)

vimechapishwa. Pamoja na ongezeko la nyenzo hizi za kuandalia wakalimani na

wafasiri, hata hivyo, kumekuwa na malalamiko kutoka kwa walimu wa somo la

Kiswahili kwamba vipengele hivyo vipya vya tafsiri na ukalimani vimeingizwa

bila ya wao kupatiwa mafunzo yoyote ya jinsi ya kufundisha maarifa hayo mapya

(tazama Bakize, 2013).

Page 14: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

Hali ya Taaluma ya Ukalimani Tanzania: Jana, Leo na Kesho

125

Katika kutekeleza majukumu yake, BAKITA limekuwa pia likiunga mkono juhudi

hizi za kuitikia mahitaji ya ukalimani na wakalimani. Mnamo mwaka 2007, kwa

mfano, BAKITA liliandaa warsha ya siku nne ili kutoa mafunzo kwa wakalimani.

Warsha hiyo ilihudhuriwa na wakalimani wasiopungua kumi, mwandishi wa

makala haya akiwa mmojawapo.

Aidha, viongozi wakubwa wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pia

wanatambua umuhimu wa fani ya ukalimani hivi sasa na wanafanya jitihada

mbalimbali kuhimiza vyombo vinavyohusika kuanzisha mafunzo ya ukalimani.

Kwa mfano, mnamo tarehe 27 Juni 2009, akizindua Taasisi ya Taaluma za

Kiswahili (TATAKI) – iliyokuwa Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (TUKI),

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Mizengo

Pinda, alilithibitisha jambo hili aliposema: “Fani ya ukalimani ni muhimu hasa

wakati huu ambapo Kiswahili kinatumika sana katika mawasiliano ya viongozi wa

Serikali, katika mikutano na warsha mbalimbali zinazofanyika ndani na nje ya

Nchi.” Kwa kauli hii ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, hatuhitaji kusisitiza utambuzi

wa serikali kuhusu kuongezeka kwa umuhimu wa ukalimani na mahitaji ya

wakalimani. Hata hivyo, ni vyema tujiulize, “Je, ni hatua gani zaidi zimechukuliwa

kukabiliana na kuongezeka huko kwa mahitaji ya wakalimani na ukalimani?”

Kutokana na mabadiliko kadha wa kadha yaliyofanyika katika mataifa huru, mbali

na aina za ukalimani zilizokuwa zinatumika enzi za biashara ya kale na enzi za

ukoloni, aina nyingine za ukalimani ambazo hazikuwapo hapo awali zimeendelea

kujitokeza. Mathalani, suala la usawa wa binadamu limewashughulisha viongozi

wengi katika kuhakikisha kwamba wananchi wao wote wanapata ustawi na fursa

sawa katika huduma mbalimbali za kijamii, hali ambayo imesababisha aina

mbalimbali za ukalimani ziendelee kujitokeza na kustawi. Kwa mfano, sheria na

sera zinazotungwa ili kutoa fursa kwa viziwi kuwa na ushindani sawa na watu

wengine katika soko la ajira zimetoa msukumo mkubwa katika maendeleo ya

huduma za ukalimani kwa watumiaji wa lugha za alama (Pöchhacker, 2004: 14).

Kwa jitihada kama hizi, viziwi wamejikuta wakiingia katika mafunzo ya

kuwaandaa kuingia katika ajira na katika elimu kwa ujumla wake. Katika

mazingira kama haya, kumezaliwa ukalimani wa lugha ya alama katika elimu

(unaojulikana pia kama ukalimani wa kielimu). Tanzania imehakikisha watu

wenye matatizo ya kusikia hawaachwi nyuma. Kwa mujibu wa WASLI (2005)

kuna chuo kimoja cha walimu kinachoandaa walimu kwa ajili ya shule za watu

wenye mahitaji maalumu zipatazo nane na vitengo kwa ajili hiyo katika shule

nyingine za kawaida zipatazo 28 (tazama pia WFD & SNAD, 2008). Aidha,

kupitia vyombo kama Chama cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) mafunzo kwa

wakalimani wa lugha ya alama yamekuwa yakitolewa. Kwa mujibu wa WASLI

(2005: 31), “Mafunzo ya majuma sita” hutolewa na CHAVITA kwa watu

Page 15: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

KISWAHILI JUZ. 76 (2013) 126

wanaotaka kuwa wakalimani wa lugha ya alama ya Tanzania ambao hufanya

ukalimani katika shule mbalimbali.

Suala la ukimbizi na uhamiaji nalo limeibua mahitaji mapya ya kimawasiliano.

Watu wamekuwa wakizikimbia nchi zao kutokana na vita au majanga mengineyo

na kuhamia katika nchi zingine zinazozungumza lugha tofauti na za kwao. Hivyo,

ili wahamiaji hawa waweze kuishi vizuri katika nchi walimokimbilia na wapate

huduma za kijamii, kwa kuzingatia misingi ya upatikanaji wa fursa sawa kama

ilivyokuwa kwa viziwi katika soko la ajira, hakuna budi kuwe na huduma za

ukalimani katika taasisi anuwai za umma na huduma mbalimbali za kijamii. Kwa

hiyo, suala la uhamiaji limesababisha kuibuka kwa ukalimani wa kijamii,

“ambao pia unajulikana kama ukalimani katika huduma za umma (hasa nchini

Uingereza) na ukalimani wa kiutamaduni (nchini Kanada)” (Pöchhacker, 2004:

15). Ukalimani wa kijamii, kwa mujibu wa Pöchhacker (2004: 15) “umeibuka

kama uwanja mpya mpana wa shughuli za ukalimani, huku ukiwa na ukalimani

katika huduma za afya (ukalimani katika matibabu, ukalimani hospitalini) na

ukalimani wa kisheria kama nyanja muhimu zaidi za asasi.” Kwa mujibu wa

Chama cha Kimataifa cha Wakalimani Mikutanoni (maarufu kama AIIC (2013))6,

nchini Tanzania kuna wakalimani weledi wanachama wa chama hicho wapatao

kumi na sita walioko jijini Arusha wakifanya kazi ya ukalimani katika Mahakama

ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita Rwanda. Aidha, kutokana na uchache7 wa

wakalimani wa lugha ya alama, mbali na kutoa huduma shuleni, hufanya pia kazi

katika maeneo mengine ambapo huduma hiyo inahitajika. Nayo ni pamoja na

mikutanoni, hospitalini, mahakamani na runingani, kwa kutaja maeneo

machache tu. Akidokeza suala la wakalimani wa lugha ya alama Tanzania kufanya

kazi katika mazingira mbalimbali, Falconer (2003: 1 & 2) ana haya ya kusema:

… Hatimaye alikuwa mkalimani wa lugha ya alama Tanzania. Ndugu Singo amekuwa

mkalimani kwa miaka 6 sasa na amesafiri kwenda Uganda, Kenya, Uswidi … Msumbiji,

Zambia na Australia kukalimani mikutanoni ambako hufanya kazi kutoka Kiingereza

kwenda lugha ya alama ya Tanzania. Yeye [ndugu Singo] anawasiliana kwa ufasaha kwa

Kiswahili, Kiingereza na lugha ya alama ya Tanzania.

[Ndugu Singo] hupata pesa nyingi zaidi anapofanya kazi ya ukalimani kuliko

anapofundisha. Katika mazingira mengine, hata hivyo, ndugu Singo hukalimani bila

malipo kwa sababu anajua kwamba viziwi hawawezi kumudu [kulipia huduma hiyo kwa]

masuala ya binafsi kama harusi, mahakamani …, hospitalini, au katika chumba cha

6 http://aiic.net/directories/interpreters/city/1208/arusha

7 Idadi inayotajwa ni kati ya wakalimani 34 (tazama WASLI, 2011) na 45 (tazama WFD, 2008).

Hata hivyo, mkalimani mzoefu wa lugha ya alama Tanzania, Ndugu Geden Baulen Singo,

anasisitiza kuwa kuna wakalimani wa lugha ya alama Tanzania “watano tu” (tazama WASLI,

2007: 31).

Page 16: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

Hali ya Taaluma ya Ukalimani Tanzania: Jana, Leo na Kesho

127

kuhifadhia maiti – amewahi kwenda na ndugu kiziwi ili kutambua mwili wa

mwanafamilia. Kazi mbaya kuliko zote alizowahi kufanya ilikuwa kukalimani kwa

mwanamke kiziwi ambaye alikuwa anajifungua. Alifadhaishwa sana na hali hiyo (Tafsiri,

msisitizo na mabano mraba vyangu).

Aina nyingine ya ukalimani iliyoibuka katika kipindi hiki ni ukalimani katika

vyombo vya habari, au ukalimani matangazo. Ukalimani wa aina hii

unajidhihirisha zaidi kwenye runinga, na hivyo mara nyingi hutajwa kama

ukalimani runingani (Pöchhacker, 2004: 15). Nina hakika baadhi yetu

tumeshaona wakalimani wa lugha ya alama wakitoa huduma hii kwenye viwambo

vya runinga Tanzania. Aina hii kimsingi imebuniwa ili kuwawezesha watumiaji

wa vyombo vya habari ndani ya jamii kupata maudhui ya matangazo ambayo

vinginevyo hawawezi kuyapata kwa kuwa yanatolewa kwa lugha wasizozielewa.

Kwa mfano, lugha za kigeni, au lugha za kusemwa kama wanaotazama ni

watumiaji wa lugha za alama. Kwa upande wa lugha za kigeni, ukalimani huu

unaweza kufanywa kwa kupitisha maandishi kwenye kiwambo cha runinga; au

kwa lugha ya alama ili kuwawezesha watumiaji wa lugha za alama kupata habari.

Mambo mengine yaliyoibua aina mpya ya ukalimani ni utandawazi, utangamano

wa kikanda na maendeleo ya teknolojia. Tumekwishaeleza kuwa umuhimu wa

ukalimani katika mawasiliano ya binadamu kutokana na kuchochewa na mahitaji

ya utandawazi na utangamano wa kikanda, umeongezeka sana. Hii leo, kutokana

na mahitaji hayo na kufuatia maendeleo ya kiteknolojia, watu wanaozungumza

lugha tofauti kutoka pande mbalimbali za dunia wanafanya mikutano na

kuelewana bila matatizo kwa msaada wa wakalimani. Hivyo, mazingira haya

yameibua aina nyingine ya ukalimani inayojulikana kama ukalimani mikutanoni.

Kuna kampuni zisizopungua tano nchini Tanzania ambazo hutoa huduma ya

ukalimani mikutanoni. Idiomatic International Company Limited, Pinnacle

Interpretation Services, JHN Services Limited, Symposium International Limited

na Proficient Language Interpretation and Translation Services ni baadhi ya

kampuni yanayomilikiwa na Watanzania ambayo hutoa huduma ya ukalimani

mikutanoni.

Tunaona kwamba huduma za ukalimani kwa aina zote zilizoelezwa hapo juu

hupatikana katika nchi ya Tanzania. Ingawa huduma za ukalimani zinatolewa

nchini Tanzania, hali ya ukalimani kama taaluma bado hairidhishi nchini humo.

Akizindua TATAKI mnamo tarehe 27 Juni 2009, Waziri Mkuu wa Tanzania,

Mheshimiwa Mizengo Pinda alisema, kauli ambayo aliirudia tena katika hotuba

yake ya kufunga mkutano wa tisa wa Bunge la Kumi uliofanyika mwezi Novemba

mwaka 2012, kwamba nchini Tanzania. “Hakuna chuo kikuu kinachotoa mafunzo

ya ukalimani. Watu wanaohitaji stadi hii ya ukalimani wanalazimika kwenda

Page 17: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

KISWAHILI JUZ. 76 (2013) 128

kusomea katika vyuo vikuu vya nje ya Afrika Mashariki.” Maelezo haya ya Waziri

Mkuu ni ya kweli. Si tu kwamba hakuna chuo kikuu kinachotoa mafunzo ya

ukalimani bali hakuna chuo chochote kinachotoa mafunzo ya ukalimani.

Mathalani, kulingana na tovuti ya chama cha wakalimani mikutanoni

(www.aiic.net), kati ya asasi zaidi ya 508 duniani zinazohusika na mafunzo ya

wakalimani na kutoa programu za astashahada, stashahada na shahada zaidi ya 100

(tazama pia Munday, 2008: 6), ni taasisi tatu tu ndizo ziko Barani Afrika (mbili

zikiwa nchini Kameruni na moja ikiwa nchini Msumbiji). Tukiacha kozi mojamoja

ambazo mara nyingi huunganishwa kama tafsiri na ukalimani zikiwa ndani ya

programu za shahada za sanaa, lugha na ualimu, hakuna programu maalumu nchini

Tanzania inayotoa ama astashahada, stashahada au shahada ya ukalimani. Hata

hizo kozi zinazotolewa hazikidhi mahitaji kwani ni fupi na hazimpi mwanafunzi

fursa ya kubobea na kupata stadi stahiki zinazomwezesha kuwa mkalimani au

mfasiri mweledi. Kwa sababu taasisi za ukalimani ni chache, na idara nyingi za

serikali na vyombo vya habari havijaweka vitengo au idara za ukalimani,

wanafunzi hawapati fursa ya kufanya mafunzo kwa vitendo katika mazingira halisi

ya shughuli hizo. Aidha, walimu wengi wanaozifundisha kozi hizo si weledi wa

taaluma za ukalimani.

Kwa kuwa ukanda mzima wa Afrika Mashariki hauna chuo kinachotoa mafunzo

ya ukalimani, tukiacha vyuo vilivyoanzisha kozi za ukalimani kama sehemu ya

programu za shahada nyingine, hatua zaidi zinahitajika kuchukuliwa. Mathalani,

kunahitajika kuanzishwa taasisi mahususi inayohusika na masomo ya ukalimani tu

ili wanafunzi wapikwe na kuiva barabara na wataalamu waliobobea katika uwanja

huu wapatikane.

Kama nchini Tanzania, na hata Afrika Mashariki yote, hakuna chuo kinachotoa

mafunzo ya ukalimani, je, wakalimani weledi basi tunao nchini Tanzania? Kama

tunao, je, hadi kufikia hivi leo wakalimani weledi waliopo ni wangapi na

wamefunzwa wapi? Pengine kabla ya kujitoma katika kuyajibu maswali haya,

ingeswihi kueleza tuna maana gani tunaposema “wakalimani weledi”. Weledi ni

hali ya kuwa na uelewa, ufahamu au ujuzi wa kina kuhusu kitu au jambo fulani

(Longhorn, 2011a & b; TUKI, 2013) unaotokana na kupata “mafunzo rasmi katika

uga” husika (Baker, 2012: 1). Kwa hiyo, wakalimani weledi ni wakalimani wenye

ujuzi wa kina kuhusu uga wa ukalimani ambao wameupata kutokana na

kuhudhuria mafunzo rasmi ya uga huo.

8 Idadi hii inahusu tu zile asasi zinazokidhi vigezo vya chama cha kimataifa cha wakalimani

mikutanoni (AIIC).

Page 18: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

Hali ya Taaluma ya Ukalimani Tanzania: Jana, Leo na Kesho

129

Tukirejea katika maswali yetu, si rahisi kupata vyanzo tunavyoweza kuvitegemea

na kusema kwa yakini kwamba wakalimani weledi tunao na idadi yao ni kadhaa.

Michuzi (2011), ingawa hatumii neno weledi, anadai kwamba wataalamu pekee

wa ukalimani wa kulipwa waliopo nchini Tanzania ni watatu. Nao ni David

Loserian, Gossaji Iddi Massoud, na Louis Taguaba ambao hutoa huduma katika

mikutano mbalimbali ya kimataifa kwa lugha za Kiingereza, Kifaransa, Kireno na

Kihispaniola. Ingawa yeye hatumii neno weledi, kwa kuzingatia fasili ya neno

utalaamu kuwa ni elimu au ujuzi wa kiwango cha hali ya juu (Longhorn, 2011b)

katika jambo au fani maalumu (BAKIZA, 2010), tunaweza kudai kuwa hawa

wanaotajwa na Michuzi ni wakalimani weledi, na hivyo kuhitimisha kuwa

wakalimani weledi nchini Tanzania wapo.

Hata hivyo, kauli ya Michuzi kuwa hao wakalimani watatu aliowataja ndio

wataalamu pekee wa ukalimani wa kulipwa nchini Tanzania inatia shaka.

Kuna wakalimani wengine kama vile Ahmed Idarous, Donathila Mwaituka, Paul

Mwaituka, Valentine Karugaba, Imani Swilla na Mujawiri Mujawandu9, miongoni

mwa wengineo, watoao huduma ya ukalimani kwa malipo ambao Michuzi

hakuwataja. Shaka hii pia inathibitishwa na Chama cha Kimataifa cha Wakalimani

Mikutanoni (AIIC (2013)) ambacho kinasema kwamba nchini Tanzania kuna

wakalimani weledi wanachama wa chama hicho wapatao kumi na sita, wote

wakiwa jijini Arusha wakifanya kazi katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu

wa Kivita Rwanda (ICTR). Hawa hutoa huduma kwa lugha za Kiingereza na

Kifaransa tu. Majina yao yanatajwa kuwa ni Eli K. AMEMAVOR, Livinus

ATANGA, Aatsa ATOGHO, Emmanuel AYUK, Arlette BIKOK, Cheikh DIA,

Charles Diéne FAYE, Damian Atanga FONCHA, Kofi Elolo Sylvester

KUMODZI, Solange Balbine KENGUÉ TIOGO, Léontine MABIKA, Daniel

MBOUA YOGO, Emmanuel NDEH AVWONTOM, Justine Anastasie

NDONGO-KELLER, Edwin OCLOO-SEWOR na Oscar TANIFUM. Hata hivyo,

ingawa orodha hii ya AIIC ya wakalimani weledi nchini Tanzania ni ndefu,

inaonekana haihusishi Watanzania kwa kuwa wakalimani wote wanaotajwa

kwenye orodha hiyo wanaonekana kuwa ni raia wa Kameruni waliosomea fani ya

ukalimani katika Chuo Kikuu cha Buea nchini humo.

BAKITA, ambalo ni chombo cha Serikali chenye dhamana ya kuratibu na kutoa

huduma za ukalimani ndani na nje ya nchi, pia linakubali kwamba wakalimani

weledi wapo. Hata hivyo, lina shaka kuhusu idadi yao kamili. Mkuu wa Idara ya

Ukalimani na Tafsiri katika Baraza hilo anathibitisha jambo hili anaposema:

9 Mwandishi wa makala haya anawafahamu wakalimani hawa.

Page 19: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

KISWAHILI JUZ. 76 (2013) 130

Nimetakiwa … niijibu baruapepe … kuhusu kupatiwa inventory ya wakalimani

wanaotambuliwa na BAKITA na viwango vyao vya elimu. Kwa ujumla, nikuambie

tu kwamba hapa nchini kwetu wakalimani wanatoa huduma hiyo kwa uzoefu tu na

kwamba waliosomea hasa ukalimani na kupata vyeti ni wawili au watatu tu.

Nadhani hali hiyo unaielewa maana data hiyo tuliitoa wakati wa warsha yetu

(BAKITA) ambayo tuliifanya Kibaha wewe ukiwa mmojawapo wa washiriki. Idadi

ya wakalimani hao wanaofanya kazi kwa uzoefu inaweza kufikia 15. Hawa ni wa

lugha za Kiswahili, Kiingereza, Kifaransa na Kireno (Bi. D. Mwaituka, 3 Desemba,

2013, mawasiliano binafsi, msisitizo ni wangu).

Katibu Mtendaji wa BAKITA naye anaunga mkono madai ya Mkuu wa Idara ya

Tafsiri na Ukalimani anaposema:

Ukalimani, tofauti na tafsiri, hauna wataalamu hapa kwetu. Wataalamu

wanaoaminika ni Prof. Swilla (ambaye hakusomea fani hiyo) na Mzee Karugaba

(huyu sina uhakika kama kasomea au la). Mkalimani ambaye alikuwa amesomea

kabisa alikuwa hayati Prof. Magoti. Wengine ni wakalimani wa ridhaa ambao

kimsingi hawana diploma za fani hiyo. Donatila Mwaituka amesomea ukalimani

huko Msumbiji na ni mmoja wa wakalimani wachache wanaotumiwa na Umoja wa

Afrika katika mikutano na bunge lake … Kwa msingi huo sidhani kama kuna data

kubwa itakayopatikana katika eneo hilo (Dkt. S. Sewangi, 3 Desemba, 2013,

mawasiliano binafsi, msisitizo ni wangu).

Madondoo haya ni ithibati kwamba, kama tulivyodokeza hapo awali, si rahisi

kupata vyanzo tunavyoweza kuvitegemea kwa yakini kutupatia idadi kamili na

majina kamili ya wakalimani. Pengine kwa kuangalia majina ya wakalimani

weledi na wanaofanya kazi kwa uzoefu wanaotajwa katika madondoo hayo hapo

juu, pamoja na kumbukumbu za mwandishi alipohudhuria warsha inayotajwa hapo

juu na utafiti wake wa awali, tutaje kama kianzio cha mjadala majina machache

tunayoyakumbuka ya wakalimani Watanzania wanaofanyia kazi nchini Tanzania

(tazama jedwali la 1 hapa chini).

Jedwali la 1: Wakalimani wa Tanzania na Viwango Vyao vya Elimu ya Ukalimani

Na. Jina la

mkalimani

Kiwango

cha juu

cha elimu

Kiwango cha

elimu ya

ukalimani

Taasisi/Chuo

alikopatia

mafunzoya

ukalimani

Lugha

anazofanyia

kazi

1. Prof. Imani

Nitike Swilla

shahada ya

uzamivu

uzoefu - Kifaransa/

Kiingereza/

Kiswahili

2. Bw.

Valentino

Karugaba

shahada ya

umahiri

uzoefu - Kifaransa/

Kiswahili

Page 20: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

Hali ya Taaluma ya Ukalimani Tanzania: Jana, Leo na Kesho

131

3. Bw. Daniel

Mwaituka

shahada ya

awali

cheti cha tafsiri

na ukalimai

Chuo Kikuu

cha Eduardo

Mondlane,

Msumbiji

Kireno/Kiswahili

4. Bw. Titus

Mpemba

shahada ya

umahiri

uzoefu/mafunzo

ya siku nne

BAKITA Kiingereza/

Kiswahili

5. Dkt. Shani

Omari

shahada ya

uzamivu

uzoefu/mafunzo

ya siku nne

BAKITA Kifaransa/

Kiswahili

6. Bi. Donathila

Paul

Mwaituka

shahada ya

umahiri

cheti10

cha tafsiri

na ukalimani

Chuo Kikuu

cha Eduardo

Mondlane,

Msumbiji

Kiingereza/

Kireno/

Kifaransa/

Kiswahili

7. Bw. Ahmed

Idarous

shahada ya

umahiri

shahada ya

umahiri

Chuo Kikuu

cha Paris,

Ufaransa

Kifaransa/Kiinge

reza/Kiswahili

8. Bw. David

Loserian

shahada ya

umahiri

shahada ya awali Chuo Kikuu

cha Geneva,

Uswisi

Kifaransa/Kiinge

reza/Kiswahili

9. Daudi Sudi

Makabwe

shahada ya

awali

shahada ya awali Chuo Kikuu

cha Besançon,

Ufaransa

Kiingereza/

Kifaransa/

Kiswahili

10. Matthew

Kamba

stashahada uzoefu - Kiingereza/

Kiswahili

11. Bi. Judith

Prince

shahada ya

awali

cheti cha tafsiri

na ukalimai

Chuo Kikuu

cha Mtakatifu

Bonifasi,

Kanada

Kiswahili/

Kiingereza/

Kifaransa

12. Bw. Louis

Lwema

Taguaba

shahada ya

awali

uzoefu - Kifaransa/

Kiingereza/

Kiswahili

13. Bw. Mujawiri

Mujawandu

shahada ya

awali

uzoefu/mafunzo

ya siku nne

BAKITA Kiingereza/

Kiswahili

14. Bi. Hadija

Chipa

shahada ya

awali

uzoefu/mafunzo

ya siku nne

BAKITA Kiingereza/

Kiswahili

15. Bw. Geden

Baulen Singo

shahada ya

awali

uzoefu/mafunzo

ya majuma 6

CHAVITA Kiingereza/

Kiswahili/Lugha

ya Alama ya

Tanzania

16. Bw. Ibrahim

Mlosi

shahada ya

awali

uzoefu/shahada

ya

awali/mafunzo

ya majuma 6

Chuo cha

Imam Ali,

Syria/

CHAVITA

Kiingereza/

Kiarabu/

Kiswahili/Lugha

ya Alama ya

Tanzania

10

Vilevile amefanya utafiti juu ya ukalimani na kuwasilisha matokeo yake kwa kuandika tasnifu

iliyowasilishwa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa minajili ya kukidhi matakwa ya

kutunukiwa Shahada ya Umahiri wa Kiswahili.

Page 21: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

KISWAHILI JUZ. 76 (2013) 132

17. Bw. Gossaji

Iddi Massoud

hatukufani

kiwa

kupata

taarifa

zake.

hatukufanikiwa

kupata taarifa

zake.

hatukufanikiwa

kupata taarifa

zake.

hatukufanikiwa

kupata taarifa

zake.

Chanzo: Data za awali kutokana na utafiti wa mwandishi

Kuna wakalimani wengine wanaotajwa katika tovuti mbalimbali ambao

hawakutajwa katika jedwali hili kutokana na kutokuwa na uhakika wa taarifa zao.

Mathalani, kuna wakalimani wapatao 13 wanaofanya kazi kwa uzoefu na

wakalimani 5 wenye vyeti wanaokalimani kwa lugha za Kiswahili, Kiingereza,

Kifaransa, Kireno, Kigiriki na Kikorea wanaorodheshwa katika

www.translatorstown/freelance-interpreters/tanzania. Tukiacha wakalimani

wanoonekana katika jedwali la 1 na wanaotajwa katika

www.translatorstown/freelance-interpreters/tanzania na tovuti nyinginezo, pia

kuna wakalimani wanaotoa huduma katika majukwaa ya kidini. Hawa pia hufanya

kazi kwa uzoefu tu na si rahisi kupata idadi yao kamili.

3.3 Kesho

Taaluma ya ukalimani inakua kwa kasi na wadau mbalimbali, kama

tulivyokwishaona, wanaitikia kwa namna mbalimbali ili kuendana na kasi ya

ongezeko hilo. Hata hivyo, ukalimani kama taaluma nchini Tanzania bado

unalegalega. Katika hali kama hii, tunajiuliza, “Nini mustakabali wa taaluma ya

ukalimani nchini Tanzania?” Ili kuweza kujibu swali hili hatuna budi kwanza

kubainisha ni changamoto gani zinazoikabili taaluma ya ukalimani nchini

Tanzania. Tunatakiwa pia kubainisha ni mambo gani yanayofanya taaluma

iendelee na istawi.

Hapo awali tulisema kuwa katika hotuba yake ya kufunga mkutano wa tisa wa

Bunge la Kumi uliofanyika mwezi Novemba 2012, Waziri Mkuu wa Tanzania,

Mheshimiwa Mizengo Pinda alisema kuwa nchini Tanzania hakuna chuo kikuu

kinachotoa mafunzo ya ukalimani na kwamba watu wanaohitaji stadi ya ukalimani

wanalazimika kwenda kuisomea katika vyuo vya nje ya Afrika Mashariki. Kwa

hiyo, changamoto ya kwanza ni ukosefu wa vyuo vinavyofundisha taaluma ya

ukalimani. Mbali na changamoto hii, Waziri Mkuu pia alibainisha kuwa:

Hata kama kukiwepo na wakalimani, bado hakuna kumbi za kisasa zenye vifaa vya

kusikilizia tafsiri za lugha mbalimbali. Kumbi nyingi tunazofanyia mikutano, tukiacha

Ukumbi wa Kimataifa wa Arusha (AICC), hazina vifaa hivyo. Changamoto tuliyo nayo

kama Nchi na hasa wawekezaji wa kumbi za mikutano ni kuhakikisha kumbi zinazojengwa

na zilizopo zinakuwa na vifaa vya kutoa huduma ya ukalimani. Lengo ni kutumia fursa

hiyo katika kukuza lugha yetu ya Kiswahili.

Page 22: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

Hali ya Taaluma ya Ukalimani Tanzania: Jana, Leo na Kesho

133

Kwa hiyo, changamoto kubwa zinazoikabili taaluma ya ukalimani nchini Tanzania

ni pamoja na ukosefu wa vyuo vinavyotoa mafunzo ya stadi hiyo na ukosefu wa

miundombinu inayowezesha kazi ya ukalimani kufanyika kwa ufanisi.

Kukosekana kwa vyuo vya ukalimani nchini, kumeikosesha Tanzania upendeleo

adhimu iliopewa na Umoja wa Afrika mwaka 2004 wa kupeleka wakalimani wa

Kiswahili wenye sifa ili waajiriwe na Umoja huo. Fursa hii imeharibika kutokana

na ukosefu wa vyuo vinavyohusika; na matokeo yake nchi imeendelea kupeleka

wabangaizaji wasio na sifa kielimu na kiumri11

.

Ili taaluma ya ukalimani iweze kuendelea na kustawi vizuri, kuna mambo kadhaa

yanayotakiwa kufanyika. Kwanza, kama tulivyoona hapo juu hakuna chuo cha

mafunzo ya fani hii, inabidi kuwe na taasisi zinazotoa mafunzo maalumu ya stadi

ya ukalimani. Akisisitiza umuhimu wa jambo hili katika ustawi wa taaluma

yoyote, Munday (2008: 6) anasema kuwa taaluma za tafsiri na ukalimani katika

nchi za Ulaya zimestawi na kuwa taaluma zinazojitegemea kwa sababu, miongoni

mwa mambo mengineyo, “kumekuwa na ongezeko kubwa la kozi zinazohusika

na tafsiri na ukalimani katika ngazi zote za shahada za awali na umahiri” ambazo

“zinaweka mkazo mahususi katika kutoa mafunzo ya wafasiri na wakalimani

weledi … na zinatumika kama kigezo aali cha kuwapokea wahitimu katika

ulimwengu wa wafasiri na wakalimani weledi”. Hata hivyo, ni vyema tukadokeza

hapa kwamba kuwapo kwa taasisi peke yake hakutoshi. Kunatakiwa pia kuwe na

miundombinu mbalimbali inayotakiwa na inayokidhi mahitaji ya kiwakati pamoja

na rasilimali muhimu zinazohitajika. Kwa mfano, mbali na miundombinu ya

kwenye kumbi za mikutano iliyotajwa na Waziri Mkuu hapo juu, katika uandaaji

wa wakalimani vyuoni kunahitajika pia madarasa mazuri, maabara bora, vitabu na

walimu wenye ujuzi. Kisha kunatakiwa kuwe na mazingira ya kuwapokea

wahitimu katika soko la ajira. Kwa mfano, vyombo vya habari, wizara za serikali,

na ofisi nyingine za serikali kama ikulu zinapaswa kuwa na vitengo vya ukalimani.

Kwa juhudi za vyuo kuanzisha kozi ya ukalimani katika mitalaa yao, tunaamini

kuwa mustakabali wa taaluma ya ukalimani utakuwa wa kutia matumaini kwa

kuwa ni kama umeanza kufunguliwa njia ya kusonga mbele. Jambo lililobaki ni

kuandaliwa kwa miundombinu ya kisasa na kuandaliwa kwa mazingira ya

kuwapokea wahitimu.

Jambo la pili linaloweza kusaidia ustawi wa taaluma ya ukalimani ni sera

zinazounga mkono juhudi ambazo zimeanza kuonekana katika taaluma hiyo.

Jambo hili linawezekana kama watunga sera watashawishika kuunga mkono

taaluma hii. Serikali ya Tanzania bila shaka inaunga mkono taaluma ya ukalimani

11

Taarifa hii ilitolewa na mtumishi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Zimbabwe nilipozungumza

naye mwezi Mei mwaka 2013.

Page 23: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

KISWAHILI JUZ. 76 (2013) 134

kama Waziri Mkuu, akizungumzia ukosefu wa taasisi zinazotoa mafunzo ya

ukalimani, anavyothibitisha anaposema, “Mimi najiuliza, hivi hili nalo tunalikubali

wakati lugha ni yetu? Ninaamini tunao uwezo wa kutumia vyuo vikuu na vyuo

vingine tulivyonavyo kufanya kazi hii ya kufundisha wakalimani. Ni vizuri vyuo

vyetu Nchini vianzishe Idara za Mafunzo ya Ukalimani ili kupunguza tatizo hilo.”

Kwa kauli hii ya Waziri Mkuu, inaweza kudaiwa kuwa milango iko wazi kwa

ustawi wa taaluma ya ukalimani kwani mazingira ya kisera yanaweza kuipa fursa

hiyo. Hata hivyo, tunadhani ingekuwa vizuri zaidi kama serikali ingeweka sera ya

kuvitaka vyombo vya habari, wizara za serikali na ofisi zingine za serikali kama

ikulu ziwe na vitengo vya ukalimani.

Jambo la tatu, ambalo limesaidia taaluma nyingi kustawi na kusimama kidete, ni

utafiti na uwasilishaji wa matokeo ya utafiti huo katika makongamano mbalimbali

na uchapishaji wake katika majarida na vitabu. Munday (2008: 6) anashadidia

suala hili kwa kusema kwamba ustawi wa taaluma za ukalimani na tafsiri katika

nchi za Magaharibi umechangiwa na utafiti na “kuongezeka kwa makongamano,

vitabu na majarida kuhusu tafsiri kwa lugha mbalimbali” katika miongo miwili

iliyopita. Anataja, kwa mfano, majarida ya Babel na Target (ya nchini Uholanzi),

Meta na TTR (ya nchini Kanada), The Translator, Translation and Literature na

Translation Studies (ya nchini Uingereza), Across Languages and Cultures (la

nchini Hungaria), Cadernos de Tradução (la nchini Brazili), Perspectives (la

nchini Denmaki), Rivista Internazionale di Tecnica della Traduzione (la nchini

Italia), na Hermeneus, Livius na Sendebar (ya nchini Hispania). Kwa nchi ya

Tanzania, jambo hili bado ni changamoto. Hakuna hata jarida moja la ukalimani!

Hata majarida yaliyopo ya taaluma zinazohusiana na ukalimani kama vile isimu na

lugha, si rahisi kukuta makala ya ukalimani. Kwa upande wa vitabu, mpaka sasa

vitabu vinavyohusu ukalimani au vinavyogusia suala la ukalimani

vilivyochapishwa, kama ilivyokwishadokezwa, ni vinne tu. Utafiti uliojibainisha

kuhusu uwanja wa ukalimani ni tasnifu moja tu ya umahiri; ya kwanza kutokea

katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (tazama Mwaituka, 2013). Kwa hiyo, ili

ukalimani ustawi nchini Tanzania siku zijazo, eneo la utafiti na uchapishaji wa

matokeo linahitaji kufanyiwa kazi zaidi.

Jambo la mwisho ni jumuiya za kitaaluma. Wataalamu wa ukalimani wanapaswa

kuwa na majukwaa ya kubadilishana mawazo katika ngazi ya kitaifa, kikanda na

kimataifa. Hivyo, wanapaswa kuanzisha vyama vya kitaifa na/au kujiunga na

vyama vya kikanda au kimataifa vya taaluma yao. Jambo hili litawaleta pamoja na

kuwaweka katika mtandao wa jumuiya nyingine zinazofanya kazi inayofanana na

yao. Akineneleza umuhimu wa jambo hili, Munday (2008: 6) anasema:

Page 24: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

Hali ya Taaluma ya Ukalimani Tanzania: Jana, Leo na Kesho

135

Jumuiya za kimataifa pia zimestawi. Jumuiya ya Fédération Internationale des

Traducteurs, iliyoanzishwa mnamo mwaka 1953 na Chama cha Wafasiri wa Kifaransa …

ilivileta pamoja vyama vya kitaifa vya wafasiri. Katika siku za karibuni zaidi, wanazuoni

wa taaluma za ukalimani wamejiunga pamoja kitaifa na kimataifa katika vyama kama

Association canadienne de traductologie (kilichoanzishwa huko Ottawa mnamo mwaka

1987), the European Society for Translation Studies (Vienna, 1992), the European

Association for Studies in Screen Translation (Cardiff, 1995) na the International

Association of Translation and Intercultural Studies (Korea, 2004) (Tafsiri yangu).

Nchini Tanzania kuna jumuiya moja tu ya wakalimani, nayo ni Chama cha

Wakalimani wa Lugha ya Alama Tanzania, ambayo inajulikana zaidi kwa jina lake

la Kiingereza la Tanzania Association of Sign Language Interpreters (TASLI)

iliyoanzishwa mwaka 2006 (WASLI, 2005). Kwa hiyo, ili kuistawisha taaluma ya

ukalimani nchini Tanzania, wanazuoni wa ukalimani wanahimizwa kuanzisha

jumuiya za kitaifa na kikanda na kujiunga katika jumuiya za kimataifa. Kwa

kufanya hivyo, tutaweza kuujenga mustakabali mzuri wa taaluma hii kwa miaka,

miongo au hata karne kadhaa zijazo.

4.0 Hitimisho

Makala haya yameabiri hali ya taaluma ya ukalimani nchini Tanzania.

Yameonesha kuwa umuhimu wa ukalimani katika mawasiliano siku za hivi

karibuni umeongezeka kutokana na utandawazi na kuongezeka kwa mwingiliano

wa tamaduni mbalimbali duniani, jambo ambalo limesababisha kuongezeka kwa

utafiti wa ukalimani, kuanzishwa kwa asasi na kozi mbalimbali kwa ajili ya

kufunza wakalimani na miitiko mingine ya namna tofautitofauti. Kwa kuzingatia

mazingira hayo na kwa kutumia mkabala wa kihistoria, makala yametilia mkazo

jinsi wadau wa ukalimani nchini Tanzania walivyoitikia. Yamejaribu kujibu

maswali makuu matatu: (1) Ukalimani ulianza kufunzwa lini nchini Tanzania? (2)

Hivi sasa taaluma ya ukalimani ina hali gani? na (3) Nini mustakabali wa taaluma

ya ukalimani nchini Tanzania?

Tumeona kwamba ukalimani ulianza kufundishwa nchini Tanzania miaka ya 1890

wakati wakoloni wa Kijerumani walipojenga Shule ya Tanga ambayo “ilitoa

mafunzo ya ukarani, kazi za viwandani na ualimu na baadhi ya kozi za kitaaluma

zilizolenga kuandaa ... wakusanya kodi, wakalimani, na mafundi...” Kuhusu hali

ya taaluma ya ukalimani hivi sasa, imebainika kwamba aina mbalimbali za

ukalimani zimeendelea kuibuka na Tanzania haijabaki nyuma kuenda na wakati

kwani imeamua kuingiza vipengele vya masomo ya ukalimani na tafsiri katika

mtalaa wa elimu ya ngazi ya sekondari ya juu, hatua ambayo imewahamasisha

waandishi na wataalamu wa Kiswahili kama Mshindo (2010), Wanjala (2011),

Haule na Tatinka (2012) na Bakize (2013) kuandika na kuchapisha vitabu vya

ukalimani na tafsiri. Sanjari na juhudi hizi, vyombo vya Serikali kama BAKITA

Page 25: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

KISWAHILI JUZ. 76 (2013) 136

vimekuwa vikiandaa warsha kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wakalimani na

viongozi wa Serikali wanahimiza vyombo vinavyohusika kuanzisha mafunzo ya

ukalimani. Imeelezwa pia kwamba asasi zisizo za kiserikali kama vile CHAVITA

zimekuwa zikitoa mafunzo kwa wakalimani wa lugha ya alama ili kuhakikisha

watu wenye matatizo ya kusikia hawaachwi nyuma. Pamoja na juhudi zote hizi,

imebainika kuwa taaluma ya ukalimani bado inalegalega kwa kuwa hakuna chuo

chochote kinachotoa mafunzo ya ukalimani Tanzania na ukanda mzima wa Afrika

Mashariki, hali ambayo imesababisha hata idadi ya wakalimani weledi na

wanaofanya kazi kwa uzoefu nchini isijulikane kwa yakini.

Ili taaluma ya ukalimani iendelee na kustawi Tanzania, unatolewa wito

kuanzishwe taasisi zinazotoa mafunzo maalumu ya taaluma ya ukalimani;

kuwekwe miundombinu mbalimbali inayotakiwa na inayokidhi mahitaji ya

kiwakati pamoja na rasilimali muhimu zinazohitajika; yaandaliwe mazingira ya

kuwapokea wahitimu wa ukalimani katika soko la ajira; zitungwe sera zinazounga

mkono ukalimani; ufanyike utafiti wa ukalimani, matokeo yawasilishwe katika

makongamano na yachapishwe katika majarida na vitabu; na wanazuoni wa

ukalimani waanzishe vyama vya kitaifa na/au wajiunge na jumuiya za kimataifa za

taaluma yao ili wawe na majukwaa ya kubadilishana mawazo.

Marejeo

AIIC. (2013). “Professional Interpreters by Language Pairs” kutoka

http://aiic.net/directories/interpreters/city/1208/arusha, imesomwa tarehe 5 Mei,

2014. Baker, Mona. (2012). In Other Words: a Coursebook on Translation, London na

New York: Routledge.

Baker, Mona na Saldanha, Gabriela (wah.) (2008) Routledge Encyclopedia of

Translation Studies 2nd Edition, Abingdon/New York/Canada: Routledge.

BAKIZA (2010). Kamusi la Kiswahili Fasaha, Nairobi: Oxford University Press

East Africa Ltd

Bakize, Leonard H. (2013). Tafsiri na Ukalimani kwa Shule za Sekondari, Dar

es Salaam: Leonard Herman Bakize.

Beattie, John na Middleton, John (wah.) (1969). Spirit Mediumship and Society in

Africa, London: Routledge & Kegan Paul.

Cobley, Paul. (2001). “Introduction” katika Cobley, Paul (mh.) The Routledge

Companion to Semiotics and Linguistics, London/New York: Routledge,

kur. 3-13.

Page 26: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

Hali ya Taaluma ya Ukalimani Tanzania: Jana, Leo na Kesho

137

Falconer, Kristi. (2003). “Profile of a Sign Language Interpreter from Tanzania,

East Africa” katika The AVLIC NEWS Juz. XIX No. 3 Julai 2003, Alberta:

the Association of Visual Language Interpreters of Canada, kur. 1-2.

Garzone, Giuliana na Viezzi, Maurizio. (2002). “Introduction” katika Garzone,

Giuliana na Viezzi, Maurizio (wah.) Interpreting in the 21st Century:

Challenges and Opportunities, Amsterdam/Philadelphia: John Benjamins

Publishing Company.

Giambruno, Cynthia. (2008). “The Role of the Interpreter in the Governance of

Sixteenth-and Seventeenth-century Spanish Colonies in the “New World”:

Lessons from the Past for the Present” katika Valero-Garces, Carmen na

Martin, Anne (wah.) Crossing Borders in Community Interpreting:

Definitions and Dilemmas, Amsterdam/Philadelphia: John Benjamins

Publishing Company, kur. 27-50.

Hadjivayanis, Ida. (2011). Norms of Swahili Translations in Tanzania: An

Analysis of Selected Translated Prose. Tasnifu ya Uzamivu, SOAS

http://eprints.soas.ac.uk/13602 imesomwa tarehe 31 Oktoba 2013.

Hale, Sandra B. (2007). Community Interpreting: Research and Practice in

Applied Linguistics, New York: Palgrave Macmillan.

Hale, Sandra B. (2004). The Discourse of Court Interpreting: Discourse Practices

of the Law, the Witness and the Interpreter, Amsterdam/Philadelphia: John

Benjamins Publishing Company.

Hatim, Basil. (2009). “Translating Text in Context” katika Munday, Jeremy (mh.)

The Routledge Companion to Translation Studies, London and New York:

Routledge-Taylor & Francis Group, kur. 36-53.

Haule, Festo C. na Tatinka, Feslas K. (2012). Nadharia ya Ukalimani: Sekondari

na Vyuo, Dar es Salaam: F. C. Haule.

Holden, Constance na wenzake. (2004). “The Origin of Speech” katika Science,

Washington DC: American Association for the Advancement of Science,

kur 1316-1319, www.science.org, imesomwa tarehe 27 Mei 2014.

Hollingsworth, Lawrence W. (1929). A Short History of the East Coast of Africa,

London: Macmillan and Co. Ltd.

Israël, F na Lederer, Marriane (wah.) (2005). La théorie interprétative de la

traduction, majuz. 3,Paris/Caen: Minard Lettres Modernes.

Lederer, Marriane. (1994/2003). La traduction aujourd’hui: Le modèle

interprétatif, Paris.

Hachette, kimefasiliwa na N. Larche kama Translation: The interpretive model

(2003), Manchester: St Jerome.

Longhorn. (2011a). Kamusi ya Karne ya 21, Dar es Salaam/Kampala/Nairobi:

Longhorn Publishers.

Longhorn. (2011b). Kamusi Kibindo ya Kiswahili, Dar es

Salaam/Kampala/Nairobi: Longhorn Publishers.

Page 27: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

KISWAHILI JUZ. 76 (2013) 138

Michuzi, Muhidin I. (2011). “Mabingwa wa Fani ya Ukalimani Tanzania” katika

issamichuzi.blogspot.com/2011/10/mabingwa-wa-fani-ya-ukalimani-

nchini.html?=1, imesomwa tarehe 3 Novemba 2013.

Mohamed, Mohamed A. (2011). Comprehensive Swahili-English Dictionary,

Nairobi/Kampala/Dar es Salaam/Kigali: East African Educational Publishers.

Mshindo, Hamad B. (2010). Kufasiri na Tafsiri, Zanzibar: Kiwanda cha Uchapaji

Chuo Kikuu cha Chukwani.

Munday, Jeremy. (2008) (toleo la 2). Introducing Translation Studies: Theories

and Applications, London na New York: Routledge-Taylor & Francis

Group.

Munday, Jeremy. (2012) (toleo la 2). Introducing Translation Studies: Theories

and Applications, London na New York: Routledge-Taylor & Francis

Group.

Mutembei, Aldin K. (2013). “Transcendental Language of the Bantu: the Case of

the Diviner-Mediums of the Haya People (Bahaya)” katika Legère, Karsten

(mh.) Bantu Languages and Linguistics: Papers in Memory of Dr. Rugatiri

D. K.Mekacha (Bayreuth African Studies Vol. 91), kur. 269-282, Bayreuth:

BASS.

Mwaituka, D. P. (2012). “Matatizo ya Kiutendaji katika Ukalimani wa Mikutano”

Dar es Salaam: Tasnifu ya Shahada ya Umahiri, Dar es Salaam

(Haijachapishwa).

Mwansoko, Hermus J. M. (1996). Kitangulizi cha Tafsiri: Nadharia na Mbinu,

Dar es Salaam: TUKI.

Nolan, James. (2005). Interpretation: Techniques and Exercises,

Clevedon/Buffalo/Toronto:Multilingual Matters Ltd.

Pöchhacker, Franz. (2004). Introducing Interpreting Studies, New York/Canada:

Routledge.

Pöchhacker, Franz. (2008). “Interpreting as Mediation” katika Valero-Garces,

Carmen na Martin, Anne (wah.) Crossing Borders in Community

Interpreting: Definitions and Dilemmas, Amsterdam/Philadelphia: John

Benjamins Publishing Company, kur. 9 – 26.

Pöchhacker, Franz. (2009). “Issues in Interpreting Studies” katika Munday, Jeremy

(mh.) The Routledge Companion to Translation Studies, London & New

York: Routledge-Taylor & Francis Group, kur. 128-140.

Pöchhacker, Franz. (2011). “Researching Interpreting: Approaches to Inquiry”

katika Nicodemus, Brenda na Swabey, Laurie (wah.) Advances in

Interpreting Research: Inquiry in Action, Amsterdam/Philadelphia: John

Benjamins Publishing Company, kur. 5 – 26.

Riccardi, Alessandra. (2002). “Interpreting Research: Descriptive Aspects and

Methodological Proposals” katika Garzone, Giuliana na Viezzi, Maurizio

(wah.) Interpreting in the 21st Century: Challenges and Opportunities,

Page 28: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

Hali ya Taaluma ya Ukalimani Tanzania: Jana, Leo na Kesho

139

Amsterdam/Philadelphia: John Benjamins Publishing Company, kur. 15 –

27.

Roy, Cynthia B. (2000). Interpreting as a Discourse Process, New York/Oxford:

Oxford University Press.

Schäffner, Christina. (2004). “Researching Translation and Interpreting” katika

Schäffner, Christina (mh.) Translation Research and Interpreting Research:

Traditions, Gaps and Synergies, Clevedon/Buffalo/Toronto: Multilingual

Matters Ltd, kur. 1 – 9.

Seleskovitch, Danica. (1968/1978). L’interprète dans les conférences

internationales: problèmes de langage et de communication, Paris: Minard,

kimefasiriwa (1978) kama Interpreting for International Conferences,

Washington, DC: Pen and Booth

Seleskovitch, Danica na Lederer, Marrianne. (1989). Pédagogie raisonnée de

l’interprétation, Paris: Didier Erudition.

Seleskovitch, Danica na Lederer, Marriane. (1984/2001). Interpréter pour

traduire, Paris: Didier Erudition.

Setton, Robin. (2002). “A Methodology for the Analysis of Interpretation

Corpora” katika Garzone, Giuliana na Viezzi, Maurizio (wah.) Interpreting

in the 21st Century: Challenges and Opportunities,

Amsterdam/Philadelphia: John Benjamins Publishing Company, kur. 29 –

45.

TUKI. (2013). Kamusi ya Kiswahili Sanifu, Dar es Salaam/Nairobi: Oxford

University Press.

Wanjala, Fred S. (2002). Misingi ya Ukalimani na Tafsiri: kwa Shule, Vyuo na

Ndaki, Mwanza: Serengeti Educational Publishers.

WASLI (World Association of Sign Language Interpreters) (2005) “Tanzania”

katika WASLI Country Reports 2005, Kampala: WASLI, uk. 31

WASLI (World Association of Sign Language Interpreters) (2011) “Tanzania

Country Report.” katika WASLI Country Reports 2011,

http://efsli.blogspot.com/2011/07/tanzania-country-report.html, imesomwa

tarehe 24 Mei 2014.

Whitely, Wilfred. (1969). Swahili: The Rise of a National Language. London.

Methuen and Co. Ltd.

Wisjen, Frans na Tanner, Ralph. (2002). ‘I am Just a Sukuma’: Globalization and

Identity Construction in Northwest Tanzania, New York: Editions Rodopi.

WFD (World Federation of the Deaf) na SNAD (Swedish National Association of

the Deaf). (2008) Global Survey Report. WFD Regional Secretariat for

Southern and Eastern Africa (WFD RSESA). Global Education Pre-

Planning Project on the Human Rights of Deaf People. Finland: World

Federation of the Deaf.

Page 29: HALI YA TAALUMA YA UKALIMANI TANZANIA: JANA, LEO ... - Mwalimu Wa …€¦ · kuwasiliana kwa sababu za kibiashara, kisiasa, kidiplomasia, kielimu, kidini na masuala mengine ya kijamii.

KISWAHILI JUZ. 76 (2013) 140

Yule, G. (2010). The Study of Language Fourth Edition, New York: Cambridge

University Press.