ANNUUR 1106 JANUARI3
-
Upload
annurtanzania -
Category
Documents
-
view
695 -
download
0
Transcript of ANNUUR 1106 JANUARI3
-
8/13/2019 ANNUUR 1106 JANUARI3
1/12
ISSN 0856 - 3861 Na. 1106 RABIUL AWWAL 1435, IJUMAA , JANUARI 3-9, 2014 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=
Sauti ya Waislamu
www.annuurpapers.co.tz
Habari Uk. 3
PICHA juu: Wanajeshi wa Al Shabaab wakiwa katika mstari tayarkwa mapambano dhidi ya kikundi cha Ahlu Sunna wal Jamaa(wanaonekana katika picha chini). Wote hawa bendera zao zinaLaailha ilallah, lakini wanapigana, wanauwana. Soma uk. 6, 7.
Somalia wamekwamawanahitaji kusaidiwa
Wameshika bendera ya UislamuLakini wapo vitani wanauwanaSwali la msingi: Wanasaidiwaje?
Habari Uk. 6
Serikali yakiri kutambuachangamoto wanafunzi Waislamu
Habari Uk. 3
Habari kamili Uk. 12
Maoni ya Waislamuyatupwa rasimuKatiba Mpya
Jussa, Eddy wataka
Masheikh waachiweNa Alghaithiyyah
Zanzibar
M W A K I L I S H I w aJimbo la Mji MkongweZanzibar (CUF), IsmailJussa Landu amesemaikiwa kweli serikaliya umoja ya kitaifainataka kuonekanakuwa inaheshimuutawala bora nahaki za binaadamu,i tende haki kwakuwapa dhamana nakuwaachia Masheikh
w a J u m u i y a y aUamsho na Mihadharaya Kiislamu Zanzibar(JUMIKI) waliowekwandani zaidi mwakasasa.
ISMAIL Jussa Landu.
-
8/13/2019 ANNUUR 1106 JANUARI3
2/12
2 AN-NUU
RABIUL AWWAL 1435, IJUMAA JAN. 3-9, 201
AN-NUURS.L.P. 55105, Simu: +022 2400786
Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM.www.annuurpapers.co.t E-mail: [email protected]
Ofsi zetu zipo: Manzese Tip TopUsangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam
Tahariri/Habari
KATIKA miaka ya1980s/90s ilipokuwaimeshamiri minakashaya Ansaar Sunna nawatu walioitwa waMaulid, baadhi yaMashe ikh bada l aya kusema hawawanakataa Maulid,wanasema hawaAnsaar wanapingakuswal iwa MtumeMuhammad (s.a.w).
Katika kukoleza hojazao wanasema, Quraninasema kuwa MwenyeziMungu mwenyewena Ma l a i k a w ak ewanamswalia Mtume,kisha wanasoma ile ayainayosema:
I n n a l l a h awamalaaika tahuswalunala n nabii, yaa ayuhalladhiina aamanu sswalu alaihi wasalimtasliimaa..
Ta f s i r i na p i chawaliyokuwa wakitakak u i f i k i s h a k w aWaislamu ni kuwahawa Ansaar wanapingaQuran, wanapinga amri
ya Mungu. Yote hii iliWaislamu wawachukiena w as i w ak ub a l i .Wawaone kuwa ni
wapotoshaji. Wamekujana dini mpya inayopingakuswaliwa Mtume!!!
Lakini yupo AnsaarSunna anayekataakumswalia Mtume?
Jayupo. Ubishi haukuwak a t i k a k u m s w a l iMtume, bali namna yakumswalia.
Kwa matoleo kadhaaya gazeti hili, tumekuwatukitoa makala kutoatahadhari kuwa watuwawe makini, wasijewakaliparamia jambona kulishabikia, kumbelina madhara. Na kubwaikazungumziwa haliinayoendelea Jamhuri
ya Afrika ya Kati, Syriana Somalia. Swali likawaje, hali ya machafukona vita inayoendeleahuko inaweza kuitwa ni
Jihad?Kwa Afrika ya Kati
j a w a b u l i n a w e z akuwa jepesi sana kwaanayetaka kujua ukweli.Ukifungua mitandaombalimbali ya habariutaona picha za askariwa Seleka wanaodaiwakuwa ni wapiganaji waKiislamu-utaona baadhi
ya wapiganaj i haowakiwa ni wasichanawaliovaa bukuta/pensi
Tunachopinga ni kutumiwa
kujiangamiza sisi wenyewena T-Shirt, matiti nje.Sasa huwezi kusemampiganaji wa namnah i y o a n a p i g a n i akusimamisha Uislamu.A n a w e z a k u w aM u i s l a m u , l a k i n ihapiganii Uislamu. Ndiopale ikasemwa kuwakinachoendelea Afrika
ya Kati ni Civil War, ilaimetumbukizwa chuki zakidini, sasa yamekuwani mauwaji ya Waislamuna Wakristo.
Kwa upande wa Syriana Somalia, hili gumukidogo kuwa na jibu lawazi kwa tulio wengi.Linahitaji uchambuzi wakina na akili ya kutizamamambo kwa undani nakwa mapana. Sio kwauoni nyu.
Muhimu tunachosemahapa ni kuwa kamwehoja haijawa Jihad-kwa maana ya kukubaliau kukataa. Hoja nitahadhari. Ukisemanakwenda Jihad, iwekweli unachofanya ni
Jihad.Kama mtu anaamini
kuwa Syria/Somaliakuna Jihad na yeye kamaMuislamu anawajibika
kwenda, na mazingiray a n a m r u h u s ukwenda, basi afanyesafari aende. Asiachekwenda kwa kutoakisingizio kuwa kunawatu wanapinga Jihadndio wamemkwaza. Aukama anaona hawezikwenda, lakini anawezakutoa msaada wowotekwa namna yoyote, basiafanye hivyo.
Qur an inasema:Watasema: Mola wetu!Hakika tumewafuatamabwana wetu nawakubwa wetu, basiwao wametupoteza njia.
Mola wetu! Wape
hawa adhabu maradufu( k u b w a z a i d i ) n auwalaani laana kubwa.(33:67-68)
N a k a t i k a a y anyingine tunasoma: ( W a k u m b u s h ewakati) waliofuatwaw a t a k a p o w a k a t a awale waliowafuata,n a h a l i y a k u w awamekwisha kuionaadhabu, na yatakatikamafungamano yao.
N a w a t a s e m aw a l e w a l i o f u a t a , L a i t i t u n g e w e z ak u r u d i ( d u n i a n i )tukawakataa kama
wanavyotukataa. Hivindivyo Mwenyezi Munguatakavyowaonyeshavitendo vyao kuwam a j u t o y a o , w a l ahawatakuwa wenyekutoka Motoni. (2:166-167)
Hoja ya msingi hapani kuwa hapatakuwana utetezi kwambamimi sikufanya jambo
la kheri kwa sababu yakupotoshwa na fulani.We ukiridhika kuwa
jambo hili linafaa, fanyawala usitafute visingiziona kuleta malumbanokama yale ya kusemaAnsaara wanapingakuswal iwa Mtume,wakati wanachosema ninamna ya kumswalia.
Ila sisi tutaendeleakutahadharisha kuwahizi harakati za kuwatoavijana katika shughuliz ao z a k i m a i sha ,mashuleni na katikavyuo, et i wakaishimaisha ya kambi kwaaj i l i ya kuj iandaakusimamisha Uislamu,si sahihi na ni hadaa
ya kuja kuwaangamizaWaislamu na kuivuruganch i . Na harakat ikama hizi haziwezikuwa zimetokana naWaislamu, bali maaduiwa Uislamu.
Tumewahi kuj iul izav i j a n a k a m a h a owakiibuka watakuja naagenda gani? Je, wakijana yale yanayotajwakufanywa na BokoHaram, itakuwa ndiosalama kwa Waislamuna Uislamu? Kutakuwakunakalika? Je, yale
yanayodaiwa kufanywan a B o k o H a r a m ,tunadhani kuwa kwanamna yoyote yanasaidiaUislamu?
Basi tujue kuwa kilaatakayekuja na agenda
ya kuwakusanya vijanawa Kiislamu kuwapamafunzo ya mwelekeowa k imapambano ,anacholenga ni kuzalishawatu ki-Boko Haram. Nahuyu hawezi kuwa mtumwema si kwa nchi walaUislamu. Ni mamluki nawakala wa kuangamizaWaislamu na nchi.
Ubaya wa jambo hilini kuwa mawakala hawani watu wanaochezana saikolojia ya Watu.
Wanajua kuwa Waislamuwana malalamiko kinchina k i l imwengu nawanajua kuwa Waislamuu k i w a a m i n i s h akuwa wanapigania
Jihad, utawapelekaunavyotaka, hawarudinyuma wala kuogopachochote. Hapo ndipowanapotupata Waislamukwa wepesi mno nakututumia kwa masilahi
yao.Tu na we za ku sema
kwa uhakika kuwahawa ni mawakalawanaotumiwa katikakufanikisha ile agenda
ya kuleta ghasia katikanchi ili hatimaye yatokee
yale ya Congo (DRC),Afrika ya Kati, Pakistan,Yemen na Somalia.
Kwa Rwanda, ilikuwaWahutu na Watutsi.Kwa Tanzania itakuwakama Seleka na anti-balaka.
Hii ndiyo tahadharitunayoendelea kuitoa
na hatutachoka kwasababu ni wajibu wetuwa Kidini na kamawazalendo wa nchi hii.
Hii ni Jihad yetutuliyoipa kipaumbelekwa sasa na tunaombana kutaraji Tawfiiq yaAllah katika kulifanya
jambo hili.Quran inatuuliza
hamfkiri, hamuoni?Katika semina moja
wiki iliyopita, lilielezwatukio moja ambapowalifika watu Bukobawakajitambulisha kuwawao ni Al Shabab nawanatafuta vijana waKiislamu wa kuwapamafunzo ili wakashiriki
Jihad Somalia.Baadhi ya Waislamu
walishtuka wakawaripotiPolisi wakakamatwa.Hata hivyo, inasemekanak u w a w a t u h a owa l i ach iwa k imyakimya na hakuna kesiiliyofunguliwa dhidi yao.
Katika hali hii, ambayonchi yetu ipo katikaAMISOM na katika halihii ambayo kila maravyombo vyetu vya dolavinatoa tahadhari juu
ya Al Sh aba b ka mamagaidi:
Swal i ni je, niniunatara j ia kusik iakutoka vyombo vya dola
wakikamatwa watukama hawa. Lakini kwamujibu wa msimulizi,waliachiwa kimya kimyana akasikia wameibukiaMbeya katika Tabligh!
K i l i e l e z w a p i akisa cha mtu mmojaaliyeingia Singida nakudai kuwa yeye niasa wa jeshi mstaafumwenye uchungu namadhila wanayofanyiwaWaislamu Tanzaniana duniani. Akasema,anataka kukusanyav i j a n a k u w a p amafunzo ya kijeshi ilikuja kupigania hakiza Waislamu. Kweli
akapata vijana akaanzakazi ya kupeleka vijanaporini kufanya mazoezi.
Lakini wakapatikanawatu wenye busarawakajiuliza maswalimeng i b i la kupatamajibu. Afsa wa jeshisi mjinga. Anajua nchiz inavyo fanya kaz i ,anajua vyombo vyadola vinavyofanya kazi.Lakini anajua pia hatari
ya jambo analofanyakwa nchi kama hii nakwa nchi yoyote duniani-kwamba hiyo ni sawa nakuunda kundi la waasina hivyo anajua fika
hatari yake na matokeyake.
Sasa inakuwaje huyasiwe na wasiwaskabisa? Wakastukawakaingilia kati mt
yule akatoweka, lakinalishakumba vijana.
Watu kama hawaw a k a t i m w i n g i nkup i t i a kwa watutunaowafahamu kuw
ni maustadh wetuwanaharakati, ndio hisasa wanafanya harakakubwa na michakat
ya kukusanya vi jankuwatia katika mfumwa maisha wa kuishkambini kujiandaa nagenda ambayo haipwazi hadi sasa. Lakinwanapokamatiwa, nkujiandaa kwa Jihad.
Labda tuseme kwlugha ya wazi kabisa
Jamani tuk ikubakufany ika mambkama haya, ndio baadautasikia kuna watwamelipua mahali, iwe nMsikiti, Kanisa, kituo ch
Polisi, halafu inadaiwkuwa waliofanya nmagaidi wa Kiislamu. Nutapatikana ushahidw a v i j a n a k a mhawa waliokusanywwakapewa mafunzo nhawa leo wanaojiitk uw a n i Maa f i s
jeshi wastaafu wenyuchungu na Uislamu!
H a t u n a a k i l iHatufikiri? Hatufammambo? Hatusik i
yanayotokea NigeriaYemen na Pakistan?
K am a t um e f i k imahali pa kutokuwna akili kiasi hichotukaona kuwa tuungmkono mtindo wa vijankutoweka shuleni, vyuonna katika shughuli zaza kimaisha wakapewmafunzo na watukama hawa walioibukBukoba na Singidab a s i t u m e s t a h i kkuingizwa katika lilkundi linalotajwa katikQuran pale iliposema:
N a b i l a s h a kTumewaumbia Moto wJahanamu wengi katikmajini na wanadam(kwa s a ba bu h i i )Nyoyo wanazo, lakinhawafahamu kwazo, nmacho wanayo, lakinhawaoni kwayo, nmasikio wanayo, lakinhawasikii kwayo. Hani kama wanyama; bawao ni wapotofu zaidHao ndio walioghaflika(7:179)
Sasa kama pamoja nneema ya akili na milang
ya fahamu al iyotupAllah, tumeshindwkuyatizama mambo hayna kuyapa tafsiri sahihtukachukua tahadharbasi tutakapojitia katik
jahanamu ya hapa hapduniani, tusijemlaummtu wala kutafutmchawi.
Mchawi ni ujinga wetwenyewe.
-
8/13/2019 ANNUUR 1106 JANUARI3
3/12
3 AN-NUU
RABIUL AWWAL 1435, IJUMAA JAN. 3-9, 201Habari/Tangazo
Rasimu ya Katiba isipokidhi kukataliwaKatibu Mkuu wa Chamacha Wananchi-CUF,Maalim Seif Sharif Hamad,amesema chama chakekitaendelea kusimamia
misingi ya haki na usawa,ili kuhakikisha kuwa kilaMzanzibari anapata hakiyake inayostahiki. Maalim Seif ambaye niMakamu wa Kwanza waRais wa Zanzibar, ameelezahayo wakati akihutubiamkutano wa hadhara yachama hicho uliofanyikaviwanja vya Kinyasini,
jimbo la Chaani.Amesema Chama hicho
kitaendelea kuwa mstariwa mbele kudai mamlakakamili ya Zanzibar, kwalengo la kuhakikisha kuwaZanzibar inaongozwa kwamisingi ya haki na usawaili wazanzibari waweze
kuamua mambo yaowenyewe bila ya kuingiwana mamlaka nyengine.
Hata hivyo amesifiaumakini wa Kamati yaM a r i d h i a n o , y e n y ewajumbe sita wakiwemowatatu kutoka ChamaCha Mapinduzi (CCM) nawatatu kutoka ChamaCha Wananchi-CUF, nakwamba wajumbe waKamati hiyo wameonyeshauzalendo wa hal i ya
ju u ka ti ka ku te ke le zamajukumu yao.
Kwa upande wake,Mwenyekiti wa Kamati yaMaridhiano, Mzee HassanNassor Moyo, amebainishakuwa mambo yanayodaiwakutolewa katika orodha
ya Muungano sio mageni,kwani yalikuwemo kwenyemamlaka ya Zanzibarkabla ya kuungana na
Tanganyika mwaka 1964. Ameyataja baadhi ya
mambo hayo kuwa nipamoja na sarafu, mambo
ya nje na rasi limali zamafuta na gesi asilia.
A idha Mzee Moyoamewanasihi Wazanzibarikuepuka chuki, tna naubaguzi na badala yakewaungane kupiganiamaslahi ya nchi yao.
A l i pongeza hatuailiyochukuliwa na RaisMstaafu wa Zanzibar Dkt.Amani Abeid Karume
na mwenzake KatibuMkuu wa CUF MaalimSeif Sharif Hamad, yak u f i k i a m a r i d h i a n oambayo yamewaunganishaWazanzibari.
N a y e M j u m b e w aKamati hiyo ya MaridhianoMansoor Yussuf Himid(CCM), amesema Zanzibarni ya Wazanzibari wote nakwamba kila Mzanzibarianastahili kupata hakisawa na mwengine.
A m e s e m a k u w aataendelea kuungana naWazanzibari kupiganiahaki ya Zanzibar ndani
ya Muungano, ili iwezekuendesha mambo yake
yenyewe na kuwashajiishavijana kutorudi nyumakatika kupigania haki hiyo.
Akizungumzia kuhusurasimu ya pili ya katibailiyotarajiwa kuwasilishwaDesemba 30, 2013 katika
viwanja vya Karimjeej i j ini Da r es Salaam,Himid al isema ik iwarasimu hiyo haitokidhianga lau was tan i wamatakwa ya Wazanzibari,h a w a t o i k u b a l i n awataikataa kabisa.
Watu wa mjini huwatuna wimbo tunasemasupu tayari lakinitunasema ikiwa supu hii
ya Jaji Warioba itapunguachumvi au pilipili mangatutaiongeza, lakini kamambaya hailiki tutamuachiamwenyewe supu yakealidokeza Bw. Himid.
W a j u m b e w en g i n ewanaounda Kamati hiyo
ambao wote walikuwepo
mkutanoni na kuzungumzani Abubakar Khamis Bakar(CUF), Ismail Jussa Ladhu(CUF), Eddy Riyami (CCM)na Salim Bimani (CUF).
Katika Mkutano huoMhe. Maalim Seif alikabidhi
kadi 459 kwa wanachamawapya walioamua kujiungac h a c h a m a h i c h o ,sambamba na kuwekamawe ya msingi katikamatawi matatu mapya yaCUF ndani ya jimbo la
Chaani na kufungua barz
ya vijana, iliyoyopewa jin
la barza ya Maalim Se
Sharif Hamad, katika kij
cha Bandamaji Chaani.
Serikali yakiri kutambua changamoto wanafunzi Waislamu
SERIKALI imebainishakuachana na utaratibu waawali wa kupanga alamaza ufaulu kwa wanafunzikatika mitihani ya Taifazilizo kuwa zikitumiwana Baraza la MitihaniTaifa (NECTA).
Hayo yamebainishwana Waziri wa Elimu naMafunzo ya Ufundi StadiDkt. Shukuru Kawambwa,wakati akizungumza nawanafunzi wa Kiislamukatika Mkutano wao Mkuuwa Jumuiya ya Wanafunziwa Kiislamu (TAMSYA),mjini Bagamoyo.
Dkt. Kawambwa, alisemaSerikali imeshughulikiana kurekebisha taratibuza Baraza la Mitihanizilizokuwa zinasababishamashaka mengi kwawadau.
Kuhusu Baraza laMtihani (NECTA) Waislamuwamekuwa na malalamikokwa muda mrefu kuhusuBaraza hi lo , naombanitumie fursa hii kwaniaba ya serikali, kwambataratibu za utunzi nausahihishaji wa mitihanina kupanga matokeasasa umebadilishwa, iledhana ya ubaguzi wakidini au ukabila nadhanihaitakuwepo. AlibainishaWaziri Kawambwa.
Alifafanua kuwa moja yamasuala yaliyolalamikiwasana na wadau wa elimu,ni utaratibu wa kupangamadara ja ya u fau luunaobadilika mara kwamara, yaani exible graderange.
A l i s e m a k a t i k ak u sh u gh u l i k i a h i l o ,kuanzia mwaka 2012serikali iliamua kutumia
Na Bakari Mwakangwale mfumo wa ufaulu wamitihani usiobadilika aukutofautiana baina yasomo na somo.
Aidha Waziri Kawambwa,alisema Serikali imesisitizam atu m i z i y a a l am aendelevu Cont inuousasasment, katika matokeo
ya mwisho ya mtihani wamwanafunzi.
Alibainisha kuwa sualahilo lilikuwa halitendeki nakusababisha mkaganyikomwingi, hata hivyo alidai
tat i zo h i lo hal ikuwabayana na halikuwekwawazi, yaani katika somomoja alama za kufikiadaraja B zinakuwa tofautina alama za daraja B zasomo jingine na kwamba,hilo ndilo jambo lililokuwalikileta mfarakano.
Kweli mambo hayay a l i k u w a h a y a i n g i iakilini, yaani yalikuwa si
ya kitaalamu, palikuwahakuna mlinganisho wasomo moja na jingine nasidhani kama kuna mahaladuniani utaratibu kamahuo unatumika, la muhimuzaidi ni uwazi katikatathimini ya mwanafunzi.
Alisema Dkt. Kawambwa.A l i o n g e z a k u w a
m w a n a f u n z i k a m aamesoma miaka minne,ukatumika ule mtihaniwake wa mwisho tu, bilakutumia alama zakeendelevu sio sahihi, kwanini vigumu kujua sikuhiyo ya kufanya mtihaniwa mwisho mwanafunzialiamka vipi, kwa kuwainawezekana kijana akawani mzuri sana lakiniasifanye vizuri katikamtihani wa mwisho.
D k t . k a w a m b w aalisema kuwa tathimini yamwanafunzi kwa miaka
minne nyuma kulinganana taratibu zilizopangwa,zitamwezeshe mwanafunzihuyo kuchangia katikamtihani wake wa mwisho.
A l i s em a h u o n d i outaratibu ambao Barazala Mitihani limeuchukuana ndivyo ilivyotangazwa.A l i s em a p am o j a n akwamba kuna changamotokatika utekelezaji wake nabaadhi hawajapendezwana utaratibu huo, lakiniS e r i k a l i i n aen d e l e a
kushughulikia suala hilokatika namna ambayom u a f a k a u n a w e z akupatikana.
A l i s e m a k u w a n imikakati ya serikal i ,ikiwezekana utaratibu huoutaanza kutumika NECTAmwaka huu.
Utaratibu huo mpyandio uliokuwapo tanguzamani na mabadiliko hayo
yalifanyoka hapo katikati.Waziri alidai hata wakatiwanasoma, utaratibuulikuwa huo uliowekwasasa.
Aidha Dkt. Kawambwaa l i s em a an a tam b u amchango wa Jumiya za
Kidini ikiwemo TAMSYA,k a t i k a j u h u d i z a omashuleni, hususanikatika suala la maadili,hasa katika kipindi hikicha utandawazi.
Alisema Utandawazi nichamgamoto ni kubwakatika mmomonyoko wamaadili kupitia mipangombalimbali, lakini asasiza dini za wanafunzizimesaidia kuwafanyavijana kuendelea kulelewana kubaki katika maadili
yanayohitajiwa.Alisema Wizara yake
imeshiriki mara kadhaakatika kuhakikisha madai
ya wanafunzi wa Kiislammashuleni yanasikilizwna kupatiwa ufumbuzunaotakiwa.
Alibainisha kwambaWizara yake imetoa nyarakmbalimbali zikielekezm a m b o m u h i m
yakiwemo, vipindi vya Dimashuleni, uendeshawake, utaratibu wa mavakwa mabinti wa Kiislamshuleni na nyakati za swasambamba na mambmengine yanayohusu Din
Nikiri tu kama risali l ivyosomwa kwambanyaraka nyingine ni zmuda mrefu, ni jambo kibinadamu inawezekansehemu nyingine zimeanzkusaulika na hazijulikanzipo wapi.
Nikiri kwamba wakawa kuhuisha nyarakhizo umeka, ili ijuliakankwamba serikali msimamwake ni ule ule katika yamambo ambayo ilikuwimeelekeza. Alisisitiza.
W az i r i Kaw am b walisema nyaraka hizo n
juhudi za Serikali katikkuhakikisha wanafunzi wKiislamu wakiwa ni sehem
ya jamii ya Kitanzaniawanapata fursa na stahsawa kat ika kupatelimu, huku wakiendelekuabudu kwa imani zawakiwa masomoni.
Hata hivyo, alisemWizara yake inatambukuwepo changamotkadhaa kwa wanafunwa Kiislamu nchini katikvituo vya elimu, ambapalidai uzoefu unaonyeshmigogoro mingi inatokann a k u k o s e k a nmawasiliano ya kutoshkati ya walimu au viongona Taasisi za dini nwanafunzi mashuleni.
Maoni ya Waislamu yatupwa rasimu Katiba MpyaLICHA ya Waislamu,Jumuia na Taasisi zaokujitokeza kwa wingikushiriki kutoa maoniyao mbele ya Tume yaKuratibu na Kukusanyamaoni ya wananchijuu ya rasimu ya Katibampya, hakuna mahaliambapo maoni ya jamiihiyo yamezingatiwana kuingizwa katika
rasimu ya katiba hiyo.
Na Shaban RajabHili l imefahamika
baada ya mwenyekiti waTume hiyo, Jaji JosephWarioba, kuwasilisharasimu ya pili ya Katibana kuikabidhi kwa Rais
Jakaya Kikwete, katikaviwanja vya Karimjee
ji ji ni Dar es Sa laamJumanne wiki hii.
H a l i h i y oimewas ik i t i sha nakuwahuzunisha baadhi
ya viongozi wa Waislamunchini, jambo ambalo
limeendeleza tafsiri ykuendelezwa utamadunwa kupuuzwa Waislamkatika mambo ya msinna ya kisera nchini.
Tumesikitika sankuona kwamba maon
ye tu hayapo . Maanya Waislamu kushirikkutoa maoni yao, ilikuwni pamoja na kusukumwna f i k ra k w am bsasa mwarobaini wmatitizo yao ya kiiman
Inaendelea Uk.
Na Mwandishi Wetu
-
8/13/2019 ANNUUR 1106 JANUARI3
4/12
4 AN-NUU
RABIUL AWWAL 1435, IJUMAA JAN. 3-9, 201Makala
AHLU Sunna Waljama'ani kundi la wapiganajiw a K i i s l a m ulinaloundwa na watuwa Twarika (Sufis)ambao wanalipingakundi la Al-Shabaab.Hawa wameshikasilaha wakipigana naAl Shabab kwa madai
kuwa hawa Al Shababwakifanikiwa kushikanchi , wata i f anyaSomalia kuwa nchi yaWahhabi.
Wakati ule Somaliaikiwa imeshikiliwa namakundi ya wababew a k i v i t a , h a w aA S W J w a l i k u w awakishi r ik iana nam b ab e w a k i v i t aMohamed Farrah Aidid.
Hata hivyo wakatih u o A h l u S u n n aWaljama'a hawakuwani wenye kusikika sanampaka mwaka 2008wal iposhika si laha
kupambana na al-Shabaab. Inaelezwakuwa k i l i cho l ipuauhasama na vita kati yaAhlu Sunna Waljamaa,ni kitendo cha Al Shababkubomoa makaburi
y a M a s h e i k h n aMakhalifah wakubwawa-Kisu katika maeneowanayoshikilia.
Katika mapambanoy a o , A S W J ,w a m e f a n i k i w akuwatimua Al Shababkatika maeneo mengi yakatikati ya Somalia nakusini hasa kule Mudug,
Gedo, Galgaduud,baadhi ya sehemu zaHiiraan, Shebelle yakati na Bakool.
Machi 15, 2010,Ahlu Sunna Waljama'awalifanya makubalianona serikali ya Somaliaambapo wa l i pewawizara tano wachaguewatu kutoka kundilao wawe Mawaziri.Walipewa pia nafasi zakidiplomasia na ndani
ya vyombo vya usalama.Kwa upande wake
wapiganaji wa ASWJwalikubali kuendeleakushirikiana na jeshila serikali dhidi ya al-Shabab.
Kat ika jumla yam a p a m b a n o y amakundi haya mawili
ya Kiislamu yaliyoachamamia kwa makumi
ya askari wa pandezote mbili wakiuwanahalikadhalika raia wasiona hatia, ni pamojana lile lililopelekeaAhlu Sunna Waljama'akutwaa Dhuusamareebkule Galguduud kutokamikononi mwa AlShabab. Hiyo ilikuwa
Ahlu Sunna Waljamaa
Aprili 24, 2011.Mapambano mengine
ni ya Aprili 28, 2011,ambapo Ahlu SunnaWaljama'a wakiwapamoja na askari wa
TFG, walipambana naAl Shabab katika mjiwa Luuqin mkoa waGedo. Askari wengi wapande zote waliuwawa.
Mt u u t a j i u l i z a ,
katika askari hawaw a l i o u w a w a a uwaliouwana (Waislamukwa Waislamu), niwa kutoka kundi lipiwatakuwa wamekufamashahidi? Wote hawawanadai kupiganiaDini isiharibiwe!
H a w a A S W Jwanawaona Al Shababw a n a o w a v u n j i aheshma Masheikhwao wa Twariqa, niwatu waliopotea njia.Wanapotosha Uislamu.Al Shabab nao hivyohivyo. Je, mgogoro wanamna hii, mgogoro wakiitikadi na mtizamowa kidini, utatuzi wakeutapatikana kwa njia
ya risasi?Mwaka 1846 Sheikh
Ali alisema watu waQadiria katika utawalaGeledi waliokufa vitaniwakipigana dhidi yake,wanakwenda motoni.Ila maiti wake katikakund i l a Sunna ,wanakwenda Peponi.
H a t u o n i k u w amkanganyiko ule ndio
huo unaoendelea mpakaleo?
Labda tuanga l i ematukio meng ine.Mei 3, 2011, yalitokeamapigano makali kwamasaa kadhaa katikamji wa Garbaharey,Gedo. Katika mapiganohaya Ah lu SunnaWaljama'a walifanikiwak u t ek a eneo h i l o
lililokuwa chini ya AlShabab. Inaelezwa kuwakatika mapambanohayo askari 3 wa ASWJna askari 23 wa Al
Shabab, waliuwawa.Sheikh (Mwenyekiti)wa ASWJ wa mkoa waGedo, Sheikh HassanSheikh Ahmed (akaQoryoley) alijeruhiwana kukimbizwa Nairobikwa matibabu ambapoalifariki siku mbilibaadae.
M a p a m b a n o y anamna hii yamekuwa
ya kawa id a ambapoWaislamu wa makundihaya mawili, wamekuwawakiendesha darsa za
kujielimisha juu ydini yao halikadhalikmapambano wakiuwanna kutiana vi lemW a i s l a m u a m b awote katika uwanjw a m a p a m b a n awanapepea bender
yenye Kalima ya Laa ilhailallah Muhamma
Rasuulullah!Kabla ya kuanz
mapambano na AShabab, Masheikh w
Twarika (Sufis)--AhlSunna wal Jamaawalifanya mkutanNa i rob i , Novemb2009, ambapo ndiplilipopitishwa azimio lkushika silaha.
Chini ya Uenyekiti wSheikh Sheikh SharSheikh Muhieddinmakundi mbalimbali y
Twarika yaliwakilishwkatika mkutano huowote wakiwa na mtizammmoja wakidai kuwa AShabab wanapotoshUislamu.
Sheikh Sharif SheikMuhieddin anasemAl Shabaab ni watwaliopotoka ambawamefahamu vibaymaadili ya Kiislamu.
Alisema hayo wakaakiongea na vyombo vyhabari mara baada ymkutano huo.
Kat ika jumla ymadai yanayoletw
dhidi ya Al Shababni kuwa na msimamunaoweza kusema n
Inaendelea Uk.
Maoni ya Waislamu yatupwa rasimu Katiba MpyInatoka Uk. 3
umepatikana. Sasahatuna fursa tenaalisema kwa masikitikoSheikh Musa Kundecha,Amir wa Baraza Kuu la
Jumuia na Taasisi zaKiislamu nchini.
Alisema dhana nzimaya Waislamu kushirikikikamilifu katika kutoamaon i yao ka t ikamchakato huo, pamojana mambo mengineilikuwa ni kujaribukutafuta suluhu yakudumu kikatiba juu yamatatizo yao ya kiimani,lakini sasa fursa hiyoimepotea kufuat iamaoni yao kuwekwakando licha ya ushirikiwao.
Tulitoa maoni yetukatika rasimu ya kwanzahaiyakujumuishwa,
tuka jar ibu ka t ikarasimu hii ya pili, nakopia hayakujumuishwa,hakuna fursa tenailiyobaki , alifafanuaSheikh Kundecha.
Kufuatia hali hiyo,A m i r K u n d e c h a
alisema viongozi wa
Kiislamu wamejitahidikutoa maoni yao kamataasisi na kuhamasishaumma wa Kiislamukushiriki ipasavyokatika kutoa maoni yao,lakini rasimu ya piliimethibitisha kwambamaoni ya Waislamuhayapo.
Nachukua fursa hiikuufahamisha ummawa Kiislamu kwamba,wasi f ik i r i v iongoz iwao wamewaangushana hawakuwajibikaipasavyo, wamejitahidi
k w a k a d i rwalivyoweza, lakinkama ilivyozoelekawamepuuzwa AlisemAmir Kundecha.
A i d h a a l i s e mkwamba pamoja nkwamba Taasisi yaimeshapeleka majin
ya wa jumbe wakw a l i o p e n d e k e z wkuingia katika Bungla Katiba, lakini hakunfursa ya kutoshiliyobaki ya kuwasilishna kuingizwa maoni yWaislamu katika rasimkatika chombo hicho.
Hata hivyo SheikKundecha, aliahidkwamba watakutanna viongozi wenginkulizungumzia sualhilo kwa kina zaidi nkulitolea ufafanuzi kwWaislamu baadae.
WAPIGANAJI wa Ahlu Sunna Waljamaa ambao wanapigana na AlShabab.
-
8/13/2019 ANNUUR 1106 JANUARI3
5/12
5 AN-NUU
RABIUL AWWAL 1435, IJUMAA JAN. 3-9, 201Habari za Kimataifa/Tangazo
K W A u c h a c h eW a i s l a m u 2 3wameuawa Ijumaamjini Bangui, mjimkuu wa Jamhuri yaAfrika ya Kati baadaya kushambuliwawakiwa ndani yamsikiti.
M a u a j i h a y oyamefanywa na kundil a wanamgambowa Kikristo la AntiBalaka.
Sheikh MuhammadWasi l , Imam waMasjidul Noor mjiniBangui amesemakuwa, Waislamu hao
wameuawa baada yakukimbilia Msikitih u m o k u j i p a t i ahifadhi.
Sheikh MuhammadWasil, ameongezakuwa wanamgambowa Ant i Ba laka,w a l i w a u w aWaislamu hao kwakuwakatakata na
Waislamu 23 wauawa
Msikitini Banguiwengine kuwachinjakama kuku kwakutumia mundu.
Imam wa MasjidulNoor ameongeza kuwa,wanamgambo hao waKikristo hawakuwana huruma hata kwawanawake na watoto,kwani wote waliokuwawamejicha Msikitinih u m o w a l i u a w akinyama na miil i
y a o i l i t e l e k e z w ap e m b e zo n i m w aMsikiti huo.
Imeelezwa kuwam a r e h e m u h a owatazikwa pembenimwa mwa Msikitih u o , b a a d a y amajesh i ya nch ihiyo kukataa kutoaruhusa ya kuzikwakwenye makaburi yaWaislamu yaliyoko nje
ya Bangui.
GAZETI la The Hill,l ina lochapishwanchini Marekanilimeandika habariza kuanza vita vyakiuchumi baina yanchi hiyo na China.
G a z e t i h i l olimeandika kuwa,Washington inapangamikakati ya kutilianasaini na nchi zaUmoja wa Ulaya nazile zilizopo pambizonimwa bahari ya Pasiki
kwa ajili ya kuzuianguvu za kiuchumi zaChina.
Msemaji wa Ofisiya mwakilishi waMarekan i kat ikaShirika la BiasharaDuniani, ameliambiagazeti hilo kwambamakubaliano hayo
ya pamo ja ka ti yaMarekani na Umojawa Ulaya ni hatua yapamoja ya kukabilianana wasiwasi wa nchihizo kuhusiana na
Vita vya kiuchumi Marekani
na China kuanzamasuala ya biasharaulimwenguni.
Imeelezwa kuwa,Marekani imeamuakuchukua uamuzi huokwa hofu kwamba,nguvu na hatuazake za kiuchumiz i n a z o p u n g u as i k u h a d i s i k uzitachukuliwa naChina.
Wakati huo huo,China nayo imeelezakuwa mikakati ya
Marekani ya kuletamabadiliko kwenyesheria za ndani nchinih u m o i m e g o n g amwamba. Hii ni katikahali ambay, Congressna Ikulu ya Marekanikwa pamoja, zinafanya
juhudi za kufa nyamiamala mikubwa
ya kiuchumi ambayoinahofiwa kuzushavita vya kiuchumi kati
ya nchi hiyo na Chinakatika miaka ijayo.
WANAWAKE Waislamuwa kabila la Rohingyanchini Myanmar ,wanakab i l iwa navitendo vya ukatili wakijinsia vinavyofanywana maafisa usalamakatika vituo vya polisinchini humo.
Kwa mujibu wa ripoti,maafisa wa usalaman c h i n i M y a n m a rwamekuwa wakiwatekanyara wanawake nawasichana Waislamu wakabila hilo na kuwapigana kuwatukana.
Polisi wabaka wanawake
Waislamu MyanmarHabari z inasemak u w a , b a a d a y amaasa hao kuwatekahuwalazimisha kutumiamadawa ya kulevya,huwapeleka kat ikavituo vya usalama nakuwabaka bila ya waokujielewa.
Hii ni katika haliambayo jamii ndogo yaWaislamu nchini humoimekuwa ikinyimwahaki zake za kimsingikutokana na serikali
ya Naypyidaw, kupingakuwapa Waislamu wa
jamii hiyo haki yoyotkwa madai kuwa siraia wa nchi hiyo.
Aidha mara kadhaMashirika ya Umojwa Mataifa ya kutetehaki za binaadamu
yamekuwa yakiituhumserikali ya nchi hiykwa kufumbia machvitendo vya ukatili wkijinsia vimavyofanywna maasa wa usalamna jeshi , dhidi ywanawake Waislamwa kabila la Rohingynchini humo.
Inawatangazia Waislamu wote kuwa kuimeandaa safari ya Hijja mwaka 2014 sawa namwaka 1435 Hijria kwa USD 3,600.Kutakuwa na punguzo la asilimia 18 kuanzia muda huu mpaka Machi 22, 2014 Itakuwadola 952 tu.Kuanzia 23 Machi 2014 kuna punguzo la asilimia 8 mpaka Juni 2014 itakuwa dola 3,312 tu
Mambo yatakayogharamiwa ni semina za Hijja, huduma za afya na kuchanja, airport chargena tiketi za ndege, nyumba Makka na Madina, Ihram na kuchinja kwa ajili ya Tama-Tuuchakula wakati wote, usari na ziara Makka na Madina, Mahema Mina na Arafa.
Umra mwezi wa Ramadhani itakuwa ni dola US 1975.Fomu zinapatikana Osi ya AHLUL DAAWA Dar es Salaam Mtaa wa Dosi na Mkadini-nyumba namba 26 mkabala na Showroom ya magari Tel: 0713 730444au 0773 804101au 0785 930444au 0773 930444.
Osi ya Ahlul Daawa Zanzibar Rahaleo Tel: 0777 484 982au 0777 413 987.
Abubakar Maulana wa Markaz Kiwalani Dar es Salaam Tel: 0784453838.Abdalla Saleh Mazrui (Hoko) Dar es Salaam Tel: 0715 724 444.Dukani kwa Abdalla HadhMazrui Wete Pemba Tel: 0777 482 665. Dukani kwa Mohammed Hadh Mazrui MkoanPemba Tel: 0777 456 911, Sheikh Daud Khamis Sheha Tel: 0777 679 692, Maalim SeiHumoud Hamed Kijichi Zanzibar Tel: 0777 417 736.
Wahi kulipa osi ya Ahlul Daawa Dar es Salaam Tel: 0713 730 444 au 0773 804 101au0785 930 444.
Osi ya Ahlul Daawa Zanzibar Rahaleo Tel: 0777 484 982au 0777 413 987.Maalim SeiHumoud Salim Tel: 0777 417 736.Sheikh Salim Mohamed Salim Tel: 0774 412 974au
Account No 048101000030NBC Kariakoo.Atakayemaliza taratibu zote mwanzo ndiye atakayeshughulikiwa mwanzo. Ukilipa kwa njiaya Account kwanza piga simu 0774 412 975.Kumbuka kikundi cha AhlulDaawa kwa bei nafuu kuliko wote na huduma bora kuliko weng
Wabillah Tawq
AHLUL DAAWA HAJJ AND TRAVEL AGENCY
-
8/13/2019 ANNUUR 1106 JANUARI3
6/12
6 AN-NUU
RABIUL AWWAL 1435, IJUMAA JAN. 3-9, 201Makala
Na Omar Msangi
KUWA Msomali, nikuwa Muislamu. Huoni msemo mashuhuriwa Wasomali.
Wanachomaanisha nikuwa Wasomali wote niWaislamu. Wanasemak uw a k am a y up o
Msomali anayedai kuwayeye sio Muislamu,basi atakuwa mamlukitu anayepewa pesa iliakanushe Usomali naUislamu wake.
Msomal i anawezaakawa asi, mlevi, haswali,hatoi zakka, lakinihamtaelewana ukimgusakatika Uislamu wakeau kumtaka aritadi.Ndio walivyo kwa asili.Kama ni kubadilika,labda wabadilike hawaw anao ham i a nch inyingine wakakuliakatika mazingira ambayosi ya Kisomali.
I w a p o U i s l a m uumekuwa kama ndiomila na utambulishowa Msomali, swali ni
je : mbona Uislamuhuu tunaoamb iwani d in i ya amani ,neno lenyewe Islamni amani; haujawezakuwasaidia Wasomalina kuwaepusha namapigano na mauwaji
ya wao kwa wao? Je,hii hali ya kupigana nakuuwana wenyewe kwawenyewe miaka nendamiaka rudi, haiwi sababu
ya kuupaka Uislamu
matope na kuoneshakuwa hauna msaadawowote kwa jamii?
Why has Islam notkept us from kill ingeach other? (Kwa niniUislamu haujatusaidiau k a t u e p u s h a n akuuwana wenyewe kwawenyewe?).
Wanajiuliza Wasomalina wanauliza baadhi yawatati na waandishi wavitabu.
Hivi sasa Somaliaipo katika vita. Jeshila serikali-TransitionalFederal Government
(TFG), linapambana namakundi ya Kiislamuambayo yanapingaserikali yakidai kuwani kibaraka wa nchi zakikari. TFG inaongozwana Sharif Sheikh Ahmed.Huyu alikuwa ndiyekiongozi wa Umojaw a Mahak am a z aKiislamu ambao uliwezakusimamisha vurugu,mauwaji na uhalifuikaanza kujenga serikali
ya Kiislamu. Serikalihiyo ya Kiislamu ambayondio kwanza ilikuwaikijengwa, ilivurugwa
Somalia wamekwamawanahitaji kusaidiwa
Wameshika bendera ya UislamuLakini wapo vitani wanauwanaSwali la msingi: Wanasaidiwaje?
na kungolewa baadaya uvamizi uliofanywana Ethiopia ikisaidiwana Marekani. Marekaniilidai kuwa Umoja waMahakama za Kiislamuni magaid i wenye
uhusiano na Al Qaidah.Baada ya kungolewa
utawala wa Mahkamaza Ki islamu, hawaw a l i o k u w a n d i ow a a n z i l i s h i n awapiganaji walioweza
kusimamisha mamlakailiyoleta amani ya mudaSomalia, wakagawika.Baadhi wakaingia katikaserikali mpya (TFG),wengine wakapinga nawale vijana waliokuwa
n d i o k i k o s i c hmapambano katikUmoja wa Mahkamza Kiislamu, wengi wawakaibuka na kund
jipya la Al Shabab.Kwa hiyo, kimsing
Al Shabab sio kundl a k i g a i d i k a minavyoda iwa , ba llimeibuka kupamban
na uvamizi wa Ethiopina baada ya hapkupambana na serikawanayodai ni kibarakpamoja na askarkutoka nje walioingiSomalia kuilinda TFG
Muhimu la kutajhapa ni kuwa, ukiachmuda mfupi usiozidmiezi si ta ambapMahkama za Kiislamzilileta amani, Somaliimekuwa haina amankwa miaka 18.
Lingine la kutajhapa ni kuwa hawwalio katika serikal
ndio waliokuwa katikMahkama za Kiislamwakidai kusimamishUislamu, lakini sasndio wanaopambanna Al Shabab. Kwhiyo hapa ni Waislamambao awali walikuwpamoja wakidai kuwwana lengo moja, lakinsasa ni maadui walikatika majeshi mawitofauti yakipambana.
Jingine ni kuwa haymakundi ya Kiislamsio moja, sio Al Shabapekee. Wapo Al-Ah
Takr Wal-Hijra, JamaIslamiyah, WahdatuIslamiayat, ambayimekuja kuwa Al-Ittihaal-Islami (AIAI).
Mengine yaliyoibukkatika siku za karibunni pamoja na AhlSunnah Wal-jamaa.
Hata hivyo, pamoja nkuwa na makundi yothayo, lakini muhimzaidi katika vita ykupinga serikali ySharif Sheikh Ahmedni al Shabaab. Japwapo pia na Hezb aIs lamiya. V i ta h iiliyoanza toka Desemb2006 inakisiwa kuw
imesababisha kuuliwwatu kwa maelfu. Nkatika kukoleza vitzaidi, nchi za Kiafrikz imekuja na ThAfrican Union Missioin Somalia (AMISOMhupeleka maelfu yaskari kupambana nmakundi ya Kiislam
yanayopinga serikali.Lakini pengine l
kusikitisha zaidi, hawHizb al Islamiya na AShabab, wamekuwnao ni maadui wa
Inaendelea Uk.
WAFUASI wa Ahlu Sunna wakidhikiri, wakimaliza kudhikiri wanashikabunduki kwenda kupambana na Al Shabab.
-
8/13/2019 ANNUUR 1106 JANUARI3
7/12
7 AN-NUU
RABIUL AWWAL 1435, IJUMAA JAN. 3-9, 201Makala
Inatoka Uk. 6
Inaendelea Uk.
Somalia wamekwamawanahitaji kusaidiwa
kwa wao. Badala yakupambana na askariwa AMISOM na wale waserikali, hutokea naowakashikiana silahawakauwana na kuuwaraia katika mapigano
yao.
I n a s e m e k a n akumekuwa na harakatikatika nchi mbalimbalikuhamasisha vijanaw a j i t o l e e k w end aSomal ia kupiganaupande wa Al Shabab.
Jaal iya hilo ni kwel ina w anap a t i k anaWaislamu wa kwendahuko. Kwa upandemwingine, Sharif Sheikhnaye anazidi kupewamsaada wa askari nasilaha kupitia AMISOMna sasa jeshi la Kenyalipo ndani ya Somalia
likipigana.Picha ya kwanza
t u n a y o t a k i w atuitizame ni hii: Hawani Waislamu ambaowote walikuwa katikaUmoja wa Mahakamaza K i i s l amu. H i v isasa wamegawanyikani makundi mawili
y anay o ha s i m i ana .Moja linapata misaadakutoka nchi unawezakuzi i ta za kikaf ir i(AMISOM na UN) pamojana za Waislamu. Kundi
jingine linatangaziwa
ugaidi. Hakuna nchiinayoweza kujitokezawaziwazi kuwasaidia AlShabab. Ndio unakutahii inayoitwa kampeni yachini kwa chini ya watubinafsi, sio katika ngazi
ya kiserikali au nchi,kutafuta vijana kwendakupigana Somalia.
V y o v y o t eutakavyoitafsiri pichahii, kwamba ni Jihad ausio, lakini wanaouwanana kuangamizana niWasomali. Ni Waislamuwenyewe kwa wenyewe!
Pengine labda turejeenyuma tutizame historia
ya Somalia tukitaraj ikuwa huenda tukapata
ji bu la li le swa li lams ing i : Kwa n in iUislamu haujasaidiakuondoa mauwaji yaWasomali wenyewe kwawenyewe?
U k i f a n y a r e j e ambalimbali za vitabu,zitakuonesha kuwamakundi ya mwanzo
yaliyoingia na kuingiza
U i s l a m u S o m a l i akatika karne ya 17,18 na 19, yalikuwa yaMasu-Twarika (watuwa dhikri). Na hawawalikuwa Qadiriyah,Ahmadiyah na Salihiyah.Masheikh mashuhurina viongozi wa Twarikahizi wakitajwa kuwan i She ikh Madar ,Sheikh Abdirahman Al-Zayli, Sheikh Aweysal-Baraawi, SheikhMohamed Guleed ,Sayid MohamedAbdulle
Hassan, Sheikh Ali Maye,Sheikh Su na wengineowalioheshimiwa sana nawatu wa Somalia.
Inaelezwa kuwa awaliMasheikh hawa, Muridhawa, walihubiri kwaamani , hawakuwawagumu kwa watuna wakati mwinginewaliwaacha kufanyamambo waliyozoeya hatakama hayapo katikaUislamu. Kwa namnamoja au nyingine,hawakushiriki kabisa
katika migogoro au haliiliyoleata umwagikajidamu, bali walikuwawasuluhishi wakubwa.
Hata hivyo inaelezwakuwa yapo matukiom ak ub w a m a t a t ua m b a y o , p e n g i n e
yanaonyesha kuwatoka mwanzo Uislamuhaukuwa umepokewakatika ufahamu uliosahihi na ndio ikawasababu ya kuanzauhasama miongoni mwamakundi ya Kiislamu na
kuibua na kuimarishk i l e k i n a c h o i t whivi sasa Msimammkali wa Kiislamu(Islamicmilitancy.)
Tukio la kwanzlimetajwa na watafiwengi kuwa lilitokek a t i k a m j i wBaardheere, kusini mwSomalia. Na hili lilikuwna ugomvi kat i ywanadini wa Bardheer(Jamaaca) na watu wsultani wa Geledi katikAfgoye.
Bardheere kamm ak az i y a w a t uinarejea mwaka 181mwanzi l ishi akiwS h e i k h I b r a h i mY ab a ro w , am b ayaliweka taratibu nShariah za Kiislamu kwbaadhi ya vipengele vymaisha. Kwanza alipigmarufuku matumiz
ya tumbaku (s igarana kucheza muzik
Alipiga pia marufukbiashara ya pembe zndovu. Kwa upandwa mavazi, ilikuwa nlazima kwa wanawakkuvaa hijabu.
Kufikia miaka y1 8 3 0 s , J a m a a cwakaamua kujipanuna kusambaa katikmikoa na miji minginhuo ukiwa ni wakawa Sharif Abdirahmana Shari f Ibrahimwaliotokea SarmaanBakool. 1840 wapiganawa Jamaaca walifikBaidoa eneo liitwal
Luuq na hat imaykuondoa uongozi wQadiriyah katika mji wBaraawe. Hii ilipelekemasheikh wakubwwaliolelewa chini yQadiriyah kama SultaAhmed Yusuf wa Geledna Sheikh Maadow wkoo ya Hintire, kupangnamna ya kukabilianna upanuzi huu wUislamu usio katik
Twarika zao. Watwa mji wa Baraawwalilazimika kukubakufuata kanuni zKiislamu zilizoletwa npia kulipa kodi ya Pess500 kwa mwaka.
Hata hivyo, hii ilizumanunguniko kutokkwa baadhi ya koambazo chini ya uongowa Geledi Sultan YusuMohamed, walipatikanwapiganaji kiasi 40,00am b ao w a l i v am imiji hii ya Kiislamkama Bardheere nkuiangamzia kabisa.
Baadhi ya waandishwa historia ya Somalik a m a P r o f e s s oCassanelli, wanalieleze
WAPIGANAJI wa jeshi la Al Shabaab.
WAPIGANAJI wa kikundi cha Hizbu Islamiyah.
-
8/13/2019 ANNUUR 1106 JANUARI3
8/12
8 AN-NUU
RABIUL AWWAL 1435, IJUMAA JAN. 3-9, 201Makala
Ahlu Sunna WaljamaaInatoka Uk. 4
wa Ki-Ansaar Sunnakwa upande mmoja, nakwa upande mwingineni kukosa uvumilivu nakuwastahamilia wengineambapo katika hali hiyowanadaiwa kupingana kuwashambuliawatu wa Su kwambani makari pamoja nakubomoa makaburi yaMasheikh wao pamojana sehemu wanazoaminikuwa ni takatifu katikaKismayo kutokana nahistoria ya Usu katikaSomalia.
Usu, ndio mtizamomkubwa na ulioeneasehemu kubwa yaSomalia ambapo maranyingi na mahali pengi,wakuu wa Twarikakatika miji ndio hao haowakuu wa koo.
Hofu iliyoingia kwama-Su hawa ni kuwai w ap o A l Shab abwataachwa washikenchi, basi wataangamizaaqida ya ki-Sufi nabadala yake kuwekawalichodai kuwa niUwahabi (kwa mtizamowao, sio mtizamo wamwandishi).
Katika historia yaKiislamu tunasoma
j u u y a K h a w a r i j(Kharijite) waliouwaWaislamu waliokuwana mitazamo tofauti na
ya kwao. Hawa ASWJ,wanaamini kuwa AlShabab nao wamekujakuuwa Wasomali wasiowafuata. Ni Khawarijwa leo.
Ni katika kikao chaNairobi, As Ahlu Sunnawal Jamaa waliundaBaraza la Vita (warcouncil), na kuanzak uw ek a m i k ak a t i
ya kupata si laha nawapiganaji.
K w a u p a n d emwingine, Ahlu Sunnawal Jamaa (ASWJ),
wamepiga marufukubaadhi ya vitabu vya
dini vinavyochapishwa
na kusambazwa na Al
Shabab wakidai kuwa
vinafundisha vijana
kuj i l ipua kwa niaya ku ji toa muhanga(suicide bombers).Madaimengine ni kuwa AlShaba wanawachukuliaWaislamu wasiofuatamsimamo wao kuwa nimakari. Humkufurishakila asiyekuwa Sala
Katika zoezi hilo,ASWJ, wamefanikiwak u o n d o a V i t a b uh i vyo ka t ika m i j i
y a D h u s a m a r e b ,A d a d o , G u r i e l ,Harardhere, Hobyo namaeneo mbalimbaliwanayomiliki katikaSomalia ya kati.
Katika zoezi hil i ,A S W J , w a m e p a t au u n g w a j i m k o n omkubwa na wananchiambao wamekuwa
w a k i d a i k u w awanahoa kuona watotowao wakipotoshwana kupambana naWaislamu wenzao.
I am happy thatAhlu Sunna wal Jamaaclerics, who have a deepunderstanding of thereligion, are prohibitingour children from beingtaught al-Shabaabswrong ideology aboutsuicide bombing. All
praise is due to God forguiding our clerics to
prevent such dangers.Alinukuliwa Mama
S a d i a M o h a m e d ,akisema akimaanishakuwa anawashukuruMasheikh wa ASWJ,kwa kuondoa hatarihiyo.
A child is not bornbelieving in suicidebombing and viewingo th e r Mu s l ims a sinfdels. This is an ideathat is indoctrinatedand it will cause manysocietal problems if it isnot combated.
Aliongeza Mama huyo,hali inayoonyesha kuwahata kama Al Shabab
watafanikiwa kushindavita ya silaha na kushikamadaraka ya kuongozanchi, bado kutakuwa navita ya kiitikadi ambayoitaendelea kusumbuana kuibua vita ya silahamara kwa mara.
Sio ASWJ pekee wapo
pia na Hizbul Islam
Hizbul Islam iliundwaJanuari 2009, SheikhOmar Iman, akiwamwenyekiti wake wa
kwanza. Msimamo waHizbul Islami kamawalivyoutangaza hapotarehe 7 Februari ,2009, ni kupambana naserikali ya Sharif SheikhAhmed na majeshi yaAfrican Union (AMISON)
yaliyo Mogadishu.Kundi hili limekuwa
dhaifu ikilinganishwana Al Shabab kutokanan a m i g o g o r o n augomvi wa kugombeamadaraka. Hali hiyoimepelekea kwamba kilawanapopigana na Al
Shabab, hupigwa.Baadhi ya wakatimigogoro hiyo hupelekeakugawika makundimawili moja likajiungana Al Shabab kupiganana jingine. Katika kuzidikusambaratika, penginena kutafuta namna
ya ku jihami , il if ik iakundi zima likatangazakujiunga na Al Shabab.
Hata hivyo mwakajana (2012) lili jitengat e n a k u t o k a a l -Shabaab na kuanzamapambano. Walifanya
hivyo Septemba 2012,baada ya al-Shababkup igwa sana namajeshi ya serikali/AMISON na kutimuliwak a t i k a m a e n e ombalimbali waliyokuwawakishikilia.
Ndugu waliokuwawakipigana katika safumoja kupambana naadui, sasa wakashikabunduki kuuwanawenyewe kwa wenyewe
wakiacha pembeni aduiwaliyekuwa wakimpigakwa pamoja.
Ukichukua ugomvihuu wa Al Shabab naHizbul Islami, unakutakuwa mgogoro waSomal i a unakuwakatika hali ya utata zaidimaana unazaa Vita yawenyewe kwa wenyewendani ya vita ya wenyewekwa wenyewe (Civil-war-within-a-civil-war.)
Civil war ya kwanzani kati ya Majeshi ya
Serikali yakiwa pamojana Ahlu Sunna WalJamaa yakipambanana Al Shabab/HizbulIslam (Islamists vs. TFG)na Civil war ya pili ni alShabab wakipambanana Hizbul Islam (AlShabab vs. HizbulIslam).
Swa l i l a ms ing ihapa ni je, Waislamuhawa, Wasomali hawa,wanasaidiwaje?
Ukirejea mkanganyikowa itikadi za Kisufi
Vs unaodaiwa kuwUwahabi/misimammikali, na hali hii ykivita iliyodumu kwmuda mrefu sasaunaloliona kwa harakn i k uw a So m a l ikuna tatizo kubwa lel imu na ufahamu
Sasa uk i chukul ikuwa hali ya kivitimedumu kwa mudmrefu, ni kuwa ujingna kuchanganyikiw(confusion) , i tazidk u o n g e z e k a k wsababu watoto waliwengi hawapati mudwa kwenda kusoma, shule wala madarsaKatika hali hii ya kivitwatu watasomaje?
B ina f s i nadhank i t a k a c h o w e zkuwasaidia Wasomana kikaleta matunda y
kudumu, sio kulisaidkundi moja kulishindjingine kwa mtutu wbunduki.
Kama kutapatikanu w e z e k a n o wkuwafanya Wasomawaweke silaha chini nkuwa chini ya serika
yoyote madhubutilimuradi wanabaki nuhuru wao wa kufanyibada, iwe kwa mtizamwa ki-Sufi, AnsaaSunna, Salaf i n.kkisha katika hali hiy
ya amani na utulivu
kazi kubwa ikafanyikkutoa elimu kwa watuWatu wakapata furs
ya kwenda shul e
wakaz i soma s i as
za ulimwengu zilivy
hivi sasa, wakaisom
dini vizuri na mbin
sahihi za kukisha n
kusimamisha Uislamuhuenda hilo baadalikaleta hata hiyo Dola yKiislamu itakayoungwmkono na Waislamwote wa Somalia nitakayojengwa katik
misingi ambayo si rahikubomolewa na maaduwa nje.
Al Shabab kwa vilndio wanaonekank u w a n a n g u vkuliko makundi yotewanaweza kushindvita. Lakini katika hahii ya kuwa katikmgogoro wa kiitikadna Sufi ambao wanidadi kubwa ya wafuakatika nchi, na saswamejifunza kutumisilaha, wataka wapi?
MPIGANAJI wa kikundi cha Hizbu Islamiyah.
-
8/13/2019 ANNUUR 1106 JANUARI3
9/12
9 AN-NUU
RABIUL AWWAL 1435, IJUMAA JAN. 3-9, 201Makala
Somalia wamekwamawanahitaji kusaidiwa
Inatoka Uk. 7
t u k i o h i l i k a m amapambano kati yanguvu inayoibuka yakuhuisha Uislamu naWaislamu wahadhinakatika Geledi.
Baadhi ya waandishiwanataja kuwa sultaniwa Geled i (Geled iSultanate), alikuwa namahusiano mazuri naSultan wa Zanzibarwakati huo, Sultan SayidBarghash, na hivyoalipata msaada kutokakwake. Hilo ni tukio lakwanza linalooneshahistoria ya mapambano
ya Waislamu wenyewekwa wenyewe katikaSomalia.
T u k i o l a p i l ilinahusishwa na kuingiaSheikh Ali Abdurahman(1787-1952) katikamji wa Merca mwaka1946 ambapo alizuamapambano na uongozi
katika usultani waGeledi. Huyu SheikhAli anatajwa kuzaliwakatika mkoa wa Nugalulio kati ya Growe naLaas-Aanood katikaPuntland ya leo. Kabla
ya kuka hapo alikuwaMakka, Saudi Arabiakisha Baghdad, Iraqkwa ajili ya masomo.Akiwa huko anadaiwakukutana na wafuasiwa Sheikh MohamedA b d u l w a h a b n aal iporejea Somal iaakaja na misimamo ya
wafuasi hao katika dinina akataka kuilazimishakwa watu wa Somalia,wengi wakiwa Sufi/
Twarika.Alianza kujenga chuo
cha Kiislamu. Hata hivyoakalazimika kuhamabaada ya kukataliwana watu wa mji/koo
yake. Alihamia mjimwingine, lakini napoakakataliwa kabla yakwenda kwa Sultan NurOsman. Hata hivyo napoaliona hapamfai kwa
kuona kuwa Shariahza Kiislamu zinapingwawaziwazi na Sultan Ali.Hapo akaungana na HajiFarah Hirsi, ambayealiasi familia akitakakusimamisha usulutaniwake. Wakakubalianakuwa wakishinda, HajiFarah atakuwa kiongoziwa k is iasa wakat iSheikh Ali akisimamiamambo ya dini.
Ilikufanikisha lengohili, Sheikh Ali alitafutamsaada kutoka kwa
mtawala wa Sharja,
Sheikh Saqar al-Qasimi,lakini hakufanikiwa.Baada ya kukosamsaada huo, SheikhAli alikwenda Zanzibarakitaka msaada waSultan Said al-Bu-Saidi.
Akiwa na wazo lakusimamisha Falme
ya Kiislamu, Sheikh Alialifika Merca mwaka1946, miaka mitatubaada ya kushindwautawala mwingine waKiislamu Baardheere nabadala yake Usultani wa
Geledi Sultanate kuwa
ndio nguvu iliyotawalasehemu kubwa yakusini mwa Somalia.
Hata hivyo, koo yaBiimal, ambayo ndiyokoo kubwa kabisa katikaMerca, iliasi kipindihicho na Sheikh Aliakaona kuwa hao ndiowatu wa kuwatumiakatika mipango yake.
Mwanzo alijifanyampatanishi baina yaSultan Yusuf na watuwa koo ya Biimal. Hatahivyo Sultan Yusuf
akakataa upatanishi
wake. Hapo Sheikh Aliakatumia fursa hiyokutangaza vita dhidi yaSultan Yusuf akitarajikuwa watu wa Biimalwatamsaidi. Lakinihawakufanya hivyo.Akaingia vitani na watuwachache aliohama naona ikawa rahisi sanakwake kushindwa. Hiyoilikuwa mwaka 1846.
K w a u p a n d emwingine, matarajio
yake ya kupata msaadakutoka kwa Sultan wa
Zanzibar yalikwama kwsababu Sultan alionkuwa kumsaidia nkuupa nguvu Uwahabkatika eneo hilo. Kwhiyo Sultan wa Zanzibaakaamua kumsaidiSultan Geledi kamnamna ya kukabilianna Uwahabi.
Waandishi wengwaliochambua historihi i wanakubal iankuwa msimamo mkawa Sheikh Al i wkuwaona wengine siWaislamu, ni makarndio uliosababishakose wafuasi wkutosha kukisha elimaliyokuja nayo. Ilikuwkila asiye katika mtizamwake, ni kari. Ikawuhasama mkubwa ka
yake na Waislamu walwengi wa Twariqa nwasoma Maulid. Na h
inadhihirishwa katikvita hii baina yake Sultawa Geledi ambapalisema kuwa Waislamwaliokufa wakipiganupande wa Sultan nwatu wa motoni, ilwaliokufa wa upandwake ni Mashaheedwanakwenda Peponi.
H a l i h i y o yk u t o w a v u m i l iWaislamu wengine nkutafuta namna nzu
ya kuwafikia kuwapelimu, bali kupeannembo ya ukaf i r iiliendelea kushikiliwna wafuasi wa Sheikhuyu. Hi l i l ikawmbegu iliyozaa ha
ya ku tokuvumi li aniliyoendelea mpaka leo
T u k i o l a t a tl i n a m h u s u S a y iMohamed Abdul lHassan. Huyu aliingiBerbera mwaka 189na anatajwa katikvitabu vya historia kuwpamoja na kuwa mbekatika mapambano ysilaha ya kupamban
na mkoloni, lakini pialikuwa chanzo chmapambano ya wenyewkwa wenyewe kati ymakundi tofauti ya Su(Somali Suf Orders).
Alipoingia BerberaSayid Mohamed alipingmamlaka na ufuasi wQadiriyah akaja ntwarika yake iliyoitwaSalihiyah (SalihiyaOrder). Aliwashambulihadharani Masheikwa Qadiriyah, na kuto
Inaendelea Uk. 1
BENDERA ya chini ni ya Al Shabab na ya juu ni ya Ahlu SunnaWaljamaa. Wote wanapepea bendera ya Laailha ila llahu Muhammadarrasuulullah, lakini wanapigana, wanauwana.
-
8/13/2019 ANNUUR 1106 JANUARI3
10/12
10 AN-NUU
RABIUL AWWAL 1435, IJUMAA JAN. 3-9, 201Makala
Somalia wamekwamawanahitaji kusaidiwa
Inatoka Uk. 9
fat wah mbalimbalik u p i n g a m a m b o
yaliyokuwa yakifanyika.H a t a h i v y o ,
Masheikh wa Qadiriyahwalishinda changamotohii kupitia midahalo namihadhara iliyoelimishana k uw a i m ar i shawafuasi wao. Na kazihii haikufanywa naMasheikh wa eneo hilopekee, bali walialikwaMashe i k h k u t o k asehemu mbalimbaliwak iwemo She ikhMadar kutoka Hargeysa,aliyekuwa mkuu waQ ad i r i y ah k a t i k amkoa/Jimbo hilo. Hiyoilikuwa mwaka 1897na haukupita muda,Waislamu Qadiriyah waBerbera wakamtimuaSayid Mohamed.
Lakini la kufahamikahapa ni kuwa kabla
ya Sayid Mohamedkulazimika kukimbiakutoka Berbera, ilibidiserikali ya kikolonikuingilia kati kutulizaghasia baina ya makundimawili ya Kiislamu,Qadiriyah na wafuasiwa Sayid Mohamed.
Ugomvi huu waQadiriyah na SayidMuhamad , ukawachanzo cha chuki nauhasama wa mudamrefu kati ya Waislamu
Qadiriyah na Salihiyah.Na unatajwa kuwawa kisiasa upandemmoja na kwa upandemwingine dini. Kisiasakwa sababu SayidMohamed alikuwa nalengo la kusimamishautawala wa Kiislamukwa mtizamo wa Twariqa
yake, lakini hakuchukuamuda kuwaelimishana kupata kuungwamkono na Masheikhwengine waliokuwa nasauti. Hiyo ikamjengeachuki na kutengwa
na Masheikh wenzakepamoja na viongozi wakoo.
K w a u p a n d ewa dini , Sal ihiyahw a l i w a k u f u r i s h aQadiriyah, wakidai kuwaUislamu sahihi ni ule tuwa Salihiyah. Ugomviulikuwa mkubwa kiasicha Mashe ikh wapande mbili kutungianamashairi ya kutukananana kukufurishana nakuingizana motoni(Angalia B. G. Martin,
aluyetafsiri baadhi yamashairi hayo).
Hali hii ilipelekeamapambano ya silahabaina ya Waislamu wamakundi haya mawiliambapo Aprili 14, 1909,wafuasi wa Salihiyahwal imuuwa Sheikh
Aweys al-Baraawi waBiyooley. Kwa bahatim b ay a au k a t i k akilele cha kuoneshachuki na uhasamaul iokuwepo, Say idMohamed alipopatahabari za kuul iwaSheikh Aweys, alisikikaaki imba kibwagizocha kujipongeza kwaushindi.
Akasema tizameni,hatimaye, tulipomuuwamjusi kikongwe, mvuaimeanza kunyesha.( C a n d h a g o d o b l e
goortaan dilaa roobkinoo daaye).
Hakuishia hapo nawafuasi wake, lakiniwanatajwa pia kuchomamoto madrasa nyingi zamakundi yasiyokuwa
yaki fuata mt izamowao. Hii ilileta chuki,uhasama, mapambanona mauwaji baina yaWaislamu.
U k i a n g a l i a n akuchambua historiana matuk io hayamatatu, utaona kuwa
yal ikuwepo mambomatatu ambayo ni tatizo.Moja, ni kushindwakutambua, kukubalina kuvumilia uwepo wawatu wenye mtizamotofauti. Pili, kundi mojakujipa Hati Miliki ya Dini(monopoly of religious
legitimacy). Kwa maanakuwa wao ndio pekeehalali kuwepo. Tatu,utumiaji wa nguvu,vurugu, mapambano(violence) dhidi yamakundi ya Kiislamu
yanayotofautiana. Nanne, ni utumiaji waShariah, hovyo hovyo(kwa kuchagua).
H a l i h i i y akimapambano ya sasa,inaanzia kwa kuibukaAl- i t ihad al- Islamikatika miaka ya 1980sambapo harakati zake
za vita vya silaha dhidiya Wa is lamu wa siokatika mtizamo wakundi hilo, kuliwaleteamaafa makubwa katikamapambano ya Kismayo(1991), Puntland (1992)na Gedo (1996).
Pamoja na kuwepomakundi mengi yaKiislamu kama Al-Ahl,
Takir Wal-Hijra, JamaIslamiyah, WahdatulIslamiyat na Al-Ittihadal-Islami (AIAI), lakinimakundi makubwa
ambayo h i v i sasayameshika si laha niAl-Shabab na Hizb al-Islami.
Pamoja na kuwawote hawa wanapiganad h i d i y a s e r i k a l i
y a Sh a r i f Sh e i k hAhmed, lakini nao pia
ni maadui. Hutokeawakapigana wao kwawao na kusababishamaafa baina yao nakwa Waislamu wasio nahatia.
Wapo pia Ahlu SunnahWal-jamaa, ambao naopia hutwangana na AlShabab.
Swali ni hili: kamakundi moja wapo katikahaya yaliyoshika silahakupigana na serikalil i t a s h i n d a , k u n auwezekano wa makundimengine kutambua
ushindi huo na kuwekasilaha chini kuachakundi hilo litawale?Au baada ya kushindana kuondoka askariwa AMISOM, wataanzakupigana wenyewe kwawenyewe?
Kama wameshindwakuwa wamoja katikalengo la kupiganana adui, watakuwawamoja baada ya aduikuondoka?
H a p a n a s h a k ak i nacho k w am i sha
m a k u n d i h a ykuungana na kuwchini ya uongozi mmojwenye lengo moja nmambo mawili. Kwanzni msimamo mkali wmakundi haya. Kila mojlinamwona mwenzaksio sahihi.
Je, hatuoni hii ni sawna ile misimamo ySalihiyah na Qadiriyahna hivyo si rahisi kuletamani na kusimamishUislamu, zaidi ya kuletmaafa kwa raia na kwWasomali wote?
J a m b o j i n g i nlinalojitokeza ni tama
ya kila kundi kutakndio lishike madarak
ya utawala.Je, ha tu oni ku w
msimamo huu mkana kushikiana huksilaha miongoni mwAl-Shabab, Hizb aIslamiyah, Ahli SunnaWal-Jamaa, dhidi yserikali, itazidi kuongezmaafa na kuteseka kwWasomali?
H a t u o n i k u wpanahitajika wasomwatafiti, wachambuzw a n a s o s h o l o j i awanasiasa na wasomw a K i i s l am u ; wkuchambua hali hna kutafuta namn
ya kuwaweka kwanzW a s o m a l i k a t i khali ya maridhianokuvumiliana na amanndio baadae wakakaw anaha rak a t i wKiislamu kwa kusomhali halisi ya mazingir
y a d un i a y a l e owakizingatia mifan
ya Taliban, FIS na jukwa Morsi; watatumi
Da wah na mbinu
gani hadi kufanikiw
kusimamisha IlamiState katika Somalia?
B ina f s i naaminkutafuta wanaharakat
ama wa kusimam
upande wa Al Shabaau Hizb al-Islamiyahh u k u A M I S O MMarekani na UN nawakiongeza majeshsilaha na msaada wkifedha n.k, kwa upandwa ser ika l i (TFG)matokeo yatakuwa nkuzidi kuwaangamizWasomali na kuzidkuivuruga nchi.
HAWA ni wapiganaji wa kikundi cha Hezb al-Islamiya
-
8/13/2019 ANNUUR 1106 JANUARI3
11/12
11AN-NUU
RABIUL AWWAL 1435, IJUMAA JAN. 3-9, 201Habari/Matangazo
Na Mahitaji Size Idadi @ Tshs
1 Nondo 12 MM Pcs 120 18,000 2,160,000.00
2 Nondo 8 MM Pcs 60 8000 480,000.00
3 Binding Wire 20 Kg 1 52000 52,000.00
4 MAWE 200 CM Lori 20 250000 5,000,000.00
5 KOKOTO 70 CM Lori 7 750000 5,250,000.00
6 Mchanga 40 CM Lori 4 220,000 880,000.00
7 Cement Mifuko 350 13500 4,725,000.00
8 Mbao Cypruss 1 6 120 9000 1,080,000.00
9 Misumari Kg 10 3000 30,000.00
JUMLA NDOGO 19,657,000.00
Deni la Mkandarasi(mjenzi)
JUMLA KUU 35,657,000.00
Msaada ujenzi wa MsikitiMahitaji ya Vifaa yanayohitajika kukiahatua ya Zege la Jamvi PLOT No. 152
Block A, Masjid Jumuiyatil Islamia UbungoDarajani.
Nb: haya ni Mahitaji kwa ajili ya Zege la JamviKwa mawasiliano zaidi Tupigie Mwenyekiti 0754 462 050 Katibu 0719 760
777 Mwenyekiti Kamati ndogo ya ujenzi ( Goha) 0787 318 116.International Commercial Bank No A/c 00001/01/601059/01 au A/c 0000/01/
0009/94/02.Au tutembelee katika Msikiti wetu uliopo Ubungo Darajani.
Wabillah Taufq
Masheikh waachiweInatoka Uk. 12peke yao, lakini tutizamewale akina mama waliopomajumbani mwao ambayowana watoto wadogowatakuwa wameathirikakiasi gani kwa waume zaokuwekwa ndani siku zote
tokea mwezi wa 10 mwakajana (juzi) mpaka leo kesiinakwenda na kurudishwanakuna linalokuwa sasamimi natoa wito kwaWaziri wa Sheria, Makamowa kwanza wa Rais ambaompo hapa katika mkutanonyinyi ni miongoni mwaserikali tunasema sualahili tunaomba mlizingatiesu a l a l a k u en d e l e akuwaweka ndani Masheikhwananchi wamechoka,alisema Eddy.
Kaul i za kutetewaMasheikh hao zimeonekanakuvuta hisia za wananchiwengi ambapo baadhi
yao walikuwa wakisemani wakati mwafaka sasaSerikali kushughulikiakama ni kuwatia hatianiau kuwapa dhamana lakinikuendelea kuwaweka
rumande kunawanyimahaki zao kikatiba nahakuwatendei haki waona familia zao.
Katika mkutano huowajumbe wa Kamati yaMaridhiano wakiongozwana Mzee Moyo waliungana
na Makamo wa Kwanza waRais Maalim Seif SharifHamad kwa kuwatakaWazanzibari kuunganana kuacha kusiki l izamaneno ya chokochokoambazo mwisho wake nikuumizana na kujengahasama miongoni mwao.
Maalim Seif alisemani wakati mwafaka sasaWazanzibari kukataakufitinishwa kwani nimuda mrefu wamekuwak a t i k a m i f a r a k a n oisiyokuwa na maanana sasa wameunganakwa maslahi ya nchina wananchi wote bilaubaguzi hivyo alitoa witokuendelea kushikamanaili kukia lengo la kuitetea
Zanzibar na Mamlakayake.
Bismillahir Rahmanir Rahiim
TANGAZO LA NAFASI ZA MASOMORIDHWAA SEMINARI-KINONDONI
MKWAJUNI KIDATO CHA KWANZA NACHEKECHEA-2014
UONGOZI WA RIDHWAA SEMINARI UNAPENDA KUWATANGAZIA WAISLAMU WOTENAFASI ZA MASOMO KWA KIDATO CHA KWANZA NA CHEKECHEA-2014
MASOMO YANAYOFUNDISHWA NI HAYA YAFUATAYO:KOMPYUTA, ARABIC ,ENGLISH ,KISWAHILI , MATHEMATICS, GEOGRAPHY
HISTORY, CHEMISTRY, PHYSICS, BIOLOGY, CIVICS, COMMERCE, BOOKKEEPINGNA ELIMU YA DINI YA KIISLAMU.
SIFA ZA SHULE:-SHULE IMESAJILIWA KWA NAMBA S.537 NA S.738-SHULE INA WAALIMU MAHIRI, WENYE UZOEFU NA NIDHAMU YA HALI YA JUU KAMA
VILE SHEIKHRUSAGANYA, ABU BILALI, SOVU N.K-SHULE INA MAKTABA,UKUMBI NA MAABARA ZA KISASA KWA MASOMO YA SAYANS-SHULE NI YA KUMI BORA KATIKA JIJI LA DAR ES SALAAM MATOKEO YA KIDATO
CHA SITA-2013-SOMO LA QURAAN HUSOMESHWA KILA SIKU ASUBUHI KABLA YA KUANZA VIPINDIWAHI SASA NAFASI NI CHACHE NA IKUMBUKWE KATIKA KUJALI HALI YA KIPATO
CHA WAZAZI WETU ADA NI NAFUU MNO NA INALIPWA KWA AWAMU MBILI TU.KAULI MBIU YETU NI:MLETE MWANAO APATE ELIMU BORA ILIYOSHEHENI MAADILI NA MALEZI MEMA
YA KIISLAMU KWA MAENDELEO YA KIROHO NA YA KIDUNIA.USAILI HUFANYIKA KILA SIKU YA JUMAMOSI KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA SIMU
YA MEZANI- 022-2762144AU SIMU YA MKONONI 0713-215918 AU 0713-400079.WAHI SANA NAFASI NI CHACHE MNO!
-
8/13/2019 ANNUUR 1106 JANUARI3
12/12
12 AN-NUU
RABIUL AWWAL 1435, IJUMAA JAN. 3-9, 20112MAKALA
AN-NUUR12 RABIUL AWWAL 1435, IJUMAA JAN. 3-9, 2014
SomaGazeti la AN-NUUR
kila Ijumaa
Nahodha sasa nayealilia mamlaka kamiliNa Mwandishi Wetu
A L I Y E K U W AWaziri wa Ulinzi naMwakilishi wa jimbola Mwanakwerekwe,Shamsi Vuai Nahodha,amesema anaungana
na kundi la Wazanzibarwanaotaka Zanzibarkuwa na mamlakakamili ndani ya katibaijayo ya Jamhuri yaMuungano Tanzania.
Akizungumza nawanachama na viongozikatika ofisi za CCMmkoa wa Mjini, Nahodhaalisema kuwa katikabaadhi ya maeneo yakuendesha nchi, sualala mamlaka kamili nimuhimu ili kuimarishauchumi wa Zanzibar.
Aidha Bw. Nahodha,
ambaye aliwahi kuwaWaziri wa Mambo yaNdani wa Serikali ya
Jamhuri ya Muunganona baadae kuhamishwana kuwa Waziri waUlinzi na Jeshi laKujenga Taifa kabla
ya kujiuzulu kufuatia
sakata la kashfa yaOperesheni TokomezaUjangili, alidai kuwa
yeye ni mtetezi wa hojaya kuondolewe suala lamafuta na gesi kwenyemuungano.
Hata hivyo alisemakuwa anashangazwana baadhi ya viongoziwa vyama vya siasa,wanaodai sarafu yaZanzibar, Kit i chaZanzibar katika Umojawa Mataifa na Wizara
y a U l i nz i , ak i d a i
kuwa masuala hayoyanahit aj i ghara makubwa za uendeshaji.
Aidha Bw. Nahodhaa m e s e m a w a k a t iZanzibar ikiendeleakuadhimisha miaka50 ya Mapinduz i ,muungano utaendeleakubaki kuwa uti wamgongo wa maendeleo
ya ulinzi na usalama waZanzibar.
Al isema kwambalicha ya mfumo wamuungano wa serikalimbili kujaa matatizo,lakini njia ya kuyapatiaufumbuzi matatizohayo ziko huru badala
y a k u ng an g a n i amuungano wa mkatabaau serikali tatu ambaoa l i d a i ha i t ak uw asalama na Zanzibar.
ALIYEKUWA Waziri wa Ulinzi na Mwakilishiwa jimbo la Mwanakwerekwe, Shamsi VuaiNahodha.
M W A K I L I S H I w aJimbo la Mji MkongweZanzibar (CUF), IsmailJussa Landu amesemaikiwa kweli serikaliya umoja ya kitaifainataka kuonekanakuwa inahesh imuutawala bora na haki zabinaadamu, itende hakikwa kuwapa dhamana nakuwaachia Masheikh waJumuiya ya Uamsho naMihadhara ya KiislamuZanz ibar (JUMIKI )waliowekwa ndani zaidimwaka sasa.
M a s h e i k h h a owaliwekwa ndani tokeamwezi wa 10 mwaka juzi2012 bila ya kupewadhamana kwa madai yakuhatarisha usalama wataifa ambapo Mkurugenziwa Mashitaka Zanzibar(DPP) alitumia kifungucha sheria ya usalama wataifa katika kujenga hoja
ya kuwanyima dhamanawatuhumiwa hayo 10.
Akizungumza katikamkutano wa hadhara waChama Cha Wananchi
Jussa, Eddy wataka Masheikh waachiweNa Alghaithiyyah
Zanzibar( C U F ) u l i o f a n y i k ahuko Chaani , Mkoawa Kaskazini Unguja,
Jussa alisema Tanzaniani miongoni mwa nchia m b a z o z i m e s a i n imkataba wa kimataifawa kuheshimu haki zabinaadamu na hivyoinapaswa kuheshimuhaki hizo bila ya kubagua.
Alisema, katika katibazote mbili ya Tanzaniana ile ya Zanzibar katikakifungu cha 18 cha katibahizo kinampa mtu uhuruwa kutoa maoni yake na
kupokea kwa mujibu washeria bila ya kuadhibiwa.J u s sa am b a ye n i
Mjumbe wa Baraza KuuTaifa alisema Masheikhwa Uamsho wamewekwandani zaidi ya mwakasasa bila ya kupewadhamana wakati sheriainaipa mahakama uwezowa kutoa dhamana kwawatuhumiwa wa makosa
yote isipokuwa mauaji nauhaini.
Ikiwa Zanzibar inatakai o n e k a n e k w a m b ainaheshimu haki zabinaadamu, basi iwapedhamana Mashe ikhh a w a m a a n a h a t ahuko kuwaweka ndani
bila kuwapa dhamanani kinyume na hakiza binaadamu mudaumeshakuwa mwingiwamewekwa ndani bila
ya kuzingatia athari zakekatika jamii, alisisitiza
J u ssa n a k u u n gw amkono wa wananchiwaliohudhuria katikamkutano huo.
Katika kitu ambachokinaonekana kuitia doaSerikali ya Umoja waKitaifa, Jussa alisema nihuko kuendelea kuwawekandani Masheikh hao nakuwanyima dhamanawakati sheria inasemahuwezi kutiwa hatianim p a k a k u w e p o n aushahidi uliokamilikah i v y o k u e n d e l e akuwaweka ni kwendakinyume na sheria ambazoZanzibar wamezipitishawenyewe.
Mjumbe wa BarazaK u u h u y o a l i s e m aMasheikh hao wanapaswakupewa dhamana kwaniikiwa wamefanya kosawahukumiwe kihaki nahaki itendeke kila mmojaaweze kuona na kuridhikana isiwe kwa Masheikh tubali sheria hiyo iwakamatepia wale wenye kufanya
ubadhirifu wa mali yaumma na kujirimbikiziamali ambapo kamati zazilizoundwa na Baraza laWawakilishi zimeoneshakumekuwepo na wizimkubwa lakini hakunaaliyetiwa hatiani walakuwekwa ndani licha
ya u shah i d i kami l ikupatikana.
T u n a s e m a w a p owatu ambao wanaibana ushahidi upo, lakinih aw ak am atw i w a l ahawawekwi ndani na walahakuna sheria iliyowagusa
wapo nje wanatembea bilaya kuchukuliwa hatuayoyote.
S a s a t u n a s e m a ,mahakimu wa mwishoni Wazanzibari wenyewewakiona hakuna hakii n a y o t e n d e k a k w aMashe ikh wao bas iWazanzibari wataamuaifikapo 2015, alisemana kushangir iwa nawananchi wengi kwakupigiwa mako.
Kauli hiyo ya Jussaimeungwa mkono naaliyekuwa Mkereketwawa Chama Cha MapinduziM o h a m m e d A h m e dSultan (Eddy Riamy)
ambaye ametoa wito kwserikali ya Umoja wKitaifa kuwapa dhamanMasheikh kwani imekuwkero kubwa kwa wananckila unapopita mitaani.
Eddy alisema kuendelekuwekwa ndan i nkunyimwa dhamanMasheikh hao kunaletkero kwa wananchi walwengi ambao wamekuwwakifuatilia habari zMasheikh hao ambawana mchango mkubwkwa jamii hasa ukizingatMasheikh hao ni walim
wa vyuoni na wengine nMaimamu wa Misikiti.Mkereke twa huy
ambaye alifuatana nKamati ya watu sita yMaridhiano iliyoongozwna Mzee Hassan NassoMoyo, alisema kwambmbali ya kukosekandarsa na kusalisha kwMasheikh hao lakini pfamilia zao zimeathirikkiuchumi na kisaikolojk u tok an a n a k u wwaume ndio waliokuwwakitizama familia nsasa kuwekwa ndankumeathiri familia hizo.
Tusiwatizame wa
Inaendelea Uk. 1